4
Volume 1, Issue 1 Business Name WARSHA YA WADAU WA KILIMO NA MKUTANO MKUU WA MWAKA 1. Dkt Sinare Sinare - Mwenyekiti 7. Bibi. Jackline Mkindi– Mjumbe 2. Professa Andrew Temu - M/ Mwenyekiti 8. Bibi. Helen Ainea Usiri– Mjumbe 3. Dr. Salum Diwani - Mwekahazina 9. Bw. Sebastian Sambuo– Mjumbe 4. Bw. Salum Shamte– Mjumbe 10. Bw. Felix Mosha– Mjumbe 5. Bw. Abdul Mwilima– Mjumbe 11. Mhe. Jitu Soni– Mjumbe 6. Bw. Willigis Mbogoro– Mjumbe YALIYOMO Jarida la Agricultural Council of Tanzania Jarida la Agricultural Council of Tanzania We unite, we dialogue, we advocate Toleo Na. 16. Oktoba – Disemba 2013 KILIMO KWANZA– AGRICULTURE FIRST WARSHA YA WADAU WA KILIMO NA MKUTANO MKUU WA MWAKA WAJUMBE WA BODI WA ACT KUPEANA TAARIFA NA KUZITUMIA KUENDELEZA VYAMA MAFUNZO YA KILIMO– BIASHARA KWA WARATIBU WA TAP KUBADILISHANA UZOEFU KUHUSU UTUNGAJI WA SERA ZA KILIMO KUFUFUA ZAO LA KOROSHO Tarehe 2 na 3 Desemba 2013, ACT ilifanikisha matukio muhimu mawili. Siku ya kwanza ilikutanisha wataalamu wa nyanja mbalimbali wapatao 80 kujadili masuala matatu: Ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji, Upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kilimo na ufugaji, Athari za kodi kwenye sekta ya kilimo. Siku ya pili ulifanyika Mkutano Mkuu wa Mwaka. Wanachama walipokea na kujadili mada ambazo ni za kawaida katika tukio la aina hii. Miongoni mwake ni: Kupokea na kujadili Taarifa ya Mwenyekiti na Hesabu za ACT, na kuchagua Wakaguzi wa Hesabu. Wakati huohuo, ACT inaandaa mkutano wa wadau utakaofanyika Januari 2014, ambao utajadili suala la Kilimo cha Kibiashara katika nchi za Afrika Mashariki. Pia, Bodi ya ACT ilipata viongozi wapya. Viongozi hao ni; Dkt. Sinare Y. Sinare kama Mwenyekiti, Profesa Andrew Temu, kutoka SUA, Morogoro kama Makamu Mwenyekiti, na Bw. Abdul Mwilima, kutoka Agricomat, Kigoma, kama Mjumbe. WAJUMBE WA BODI YA ACT

Jarida la Agricultural Council of Tanzania Toleo Na. …actanzania.or.tz/wp-content/uploads/2016/08/ACT...yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya Kilimo. 2

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Jarida la Agricultural Council of Tanzania Toleo Na. …actanzania.or.tz/wp-content/uploads/2016/08/ACT...yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya Kilimo. 2

Newsletter Date

Volume 1, Issue 1

Business Name

WARSHA YA WADAU

WA KILIMO NA MKUTANO MKUU WA MWAKA

1. Dkt Sinare Sinare - Mwenyekiti 7. Bibi. Jackline Mkindi– Mjumbe

2. Professa Andrew Temu - M/ Mwenyekiti 8. Bibi. Helen Ainea Usiri– Mjumbe

3. Dr. Salum Diwani - Mwekahazina 9. Bw. Sebastian Sambuo– Mjumbe

4. Bw. Salum Shamte– Mjumbe 10. Bw. Felix Mosha– Mjumbe

5. Bw. Abdul Mwilima– Mjumbe 11. Mhe. Jitu Soni– Mjumbe

6. Bw. Willigis Mbogoro– Mjumbe

YALIYOMO

Jarida la Agricultural Council of Tanzania

Jarida la Agricultural Council of Tanzania

We unite, we dialogue, we advocate

Toleo Na. 16. Oktoba – Disemba 2013

KILIMO KWANZA– AGRICULTURE FIRST

WARSHA YA

WADAU WA

KILIMO NA

MKUTANO MKUU

WA MWAKA

WAJUMBE WA

BODI WA ACT

KUPEANA

TAARIFA NA

KUZITUMIA

KUENDELEZA

VYAMA

MAFUNZO YA

KILIMO–

BIASHARA KWA

WARATIBU WA

TAP

KUBADILISHANA

UZOEFU KUHUSU

UTUNGAJI WA

SERA ZA KILIMO

KUFUFUA ZAO LA

KOROSHO

Tarehe 2 na 3 Desemba 2013, ACT ilifanikisha

matukio muhimu mawili. Siku ya kwanza

ilikutanisha wataalamu wa nyanja mbalimbali

wapatao 80 kujadili masuala matatu:

Ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji,

Upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kilimo na

ufugaji,

Athari za kodi kwenye sekta ya kilimo.

Siku ya pili ulifanyika Mkutano Mkuu wa

Mwaka. Wanachama walipokea na kujadili

mada ambazo ni za kawaida katika tukio la

aina hii.

Miongoni mwake ni: Kupokea na kujadili

Taarifa ya Mwenyekiti na Hesabu za ACT, na

kuchagua Wakaguzi wa Hesabu. Wakati

huohuo, ACT inaandaa mkutano wa wadau

utakaofanyika Januari 2014, ambao utajadili

suala la Kilimo cha Kibiashara katika nchi za

Afrika Mashariki.

Pia, Bodi ya ACT ilipata viongozi wapya.

Viongozi hao ni; Dkt. Sinare Y. Sinare kama

Mwenyekiti, Profesa Andrew Temu, kutoka

SUA, Morogoro kama Makamu Mwenyekiti,

na Bw. Abdul Mwilima, kutoka Agricomat,

Kigoma, kama Mjumbe.

WAJUMBE WA BODI YA ACT

Page 2: Jarida la Agricultural Council of Tanzania Toleo Na. …actanzania.or.tz/wp-content/uploads/2016/08/ACT...yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya Kilimo. 2

KUPEANA TAARIFA NA KUZITUMIA KUENDELEZA VYAMA

Tarehe 22 hadi 25 Oktoba 2013, watumishi

wawili wa ACT, Bw. Cleophas Rwechungura na

Khalid Ngassa, walikuwa Bujumbura, Burundi,

ambako walishiriki katika mafunzo kuhusu

utaalamu wa kupeana habari / taarifa kwa lengo

la kuendeleza vyama vya wakulima. Mafunzo

hayo yalifadhiliwa na IFAD na kusimamiwa na

Muungano wa Vyama vya Wakulima Afrika

Mashariki– EAFF.

Mafunzo hayo yalishirikisha baadhi ya vyama vya

wakulima kutoka Kenya, Burundi na Tanzania.

Washiriki walifundishwa jinsi ya kuimarisha

vyama vya wakulima kwa kuelimisha watendaji

pamoja na wanachama, na mbinu za kupeana

taarifa na kwa lengo la kujiendeleza. Hii ni

pamoja na: “Kuimarisha upashanaij wa habari

na utamaduni wa kubadilishana maarifa na

ujuzi”.

MAFUNZO YA KILIMO– BIASHARA KWA WARATIBU WA TAP

Ubia wa Kilimo Tanzania - TAP kwa sasa unao waratibu

wa shughuli zake katika wilaya 25. Katika jitihada za

kufanya kilimo kiendeshwe kibiashara, TAP iliomba msaada

wa kifedha na kitaalamu ili kuelimisha Waratibu wake

ustadi wa kilimo cha kibiashara na kanuni za kilimo cha

mkataba.

Mafunzo haya yamekuwa yakifanyika kwa awamu. Zoezi

la karibuni lilifanyika katikati ya Novemba 2013, jijini Dar

es Salaam. FAO kupitia Programu ya Kuendeleza

Mifumo ya Uzalishaji wa Chakula, Nyanda za Juu- SHFSP,

ilifanikisha mafunzo kwa Waratibu wa TAP, ambao

baadae watatoa elimu hiyo kwa wakulima, na kwa wadau

wengine kwenye mlolongo wa thamani.

Utaalamu huu ni muhimu sana, hasa tukizingatia

kwamba TAP II itaanza karibuni, ambayo mkazo wake ni:

“Kukuza kilimo kwakuchochea uwekezaji na

kukiendesha kibiashara”.

Page 2 Jarida la Agricultural Council of Tanzania ACT NEWS

2 Jarida la ACT– Toleo Na. 16

Awamu ya kwanza ilikuwa ya miaka mitatu

2008– 2011 na ilihusisha wilaya 25. Matarajio ni

kwamba awamu ya pili itapanuka kwa

kujumuisha wilaya nyingine 25.

Baadhi ya washiriki kwenye mafunzo wakisikiliza kwa makini mtoa mada.

ACT hufanya shughuli zake kwa kushirikiana na sekta binafsi na ya umma. Huduma zake zinalenga wadau wote, wa ngazi zote kulingana na mahitaji yao halisi.

Page 3: Jarida la Agricultural Council of Tanzania Toleo Na. …actanzania.or.tz/wp-content/uploads/2016/08/ACT...yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya Kilimo. 2

KUFUFUA ZAO LA KOROSHO

Mwanzoni mwa Oktoba 2013, Bw. Renatus

Mbamilo kutoka ACT alikuwa miongoni mwa

washiriki kwenye warsha iliyojadili uzoefu wa

Vyama vya Wakulima katika michakato ya

kuimarisha hali ya chakula katika ngazi ya taifa na

kanda. Warsha hiyo ilifanyika jijini Nairobi.

Madhumuni ya jumla, ni kuimarisha ushiriki wa

Shirikisho la Vyama vya Wakulima, Afrika

Mashariki - EAFF kwenye mchakato huu.

Washiriki walipanuliwa ufahamu wao kuhusu

utaratibu wa mchakato. Kumewekwa mfumo

wa kupima, kufuatilia na kutathmini athari za sera

za kilimo kwa wazalishaji.

Mfumo huu unatekelezwa na FAO kwa

kushirikiana na wabia wengine kwa lengo kukuza

utendaji katika vyama, na hivyo kuimarisha

ukuaji wa kilimo.

Page 3 Volume 1, Issue 1 ACT NEWS

3 Jarida la ACT– Toleo Na. 16

Tarehe 4 na 5 Novemba 2013, ANSAF na ACT kwa

pamoja waliandaa warsha ya kujadili changamoto

zinazokabili zao la korosho nchini Tanzania.

Wabia wengine kwenye shughuli hii ni; Bodi ya

Korosho Tanzania, Kituo cha Uwekezaji Tanzania,

Taasisi za Kifedha, Wahisani, na wawakilishi wa

wakulima wa korosho. Lengo la warsha lilikuwa

kutafakari jinsi ya kufufua zao la korosho ili tunufaika

nalo.

Hali ya korosho siyo nzuri, kiwango cha uzalishaji wa

korosho na ubora wake, uko chini sana, isitoshe, ni

asilimia 20 tu ndiyo inayosindikwa hapa Tanzania, kiasi

kinachobakia husafirishwa hadi India kubanguliwa.

Katika hali hii, washiriki wa warsha walikubaliana:

Kusaidia wakulima katika jitihada zao za kupata

mazao makubwa yenye ubora wa juu.

Kuhakikisha kwamba korosho zote zinabanguliwa

hapahapa Tanzania, kusudi bei yake iongezeke, pia

wananchi wapate ajira.

KUBADILISHANA UZOEFU KUHUSU UTUNGAJI WA SERA ZA KILIMO

Baadhi ya wawakilisha wa taasisi

zilizoandaa warsha hii.

Zabibu ni zao linaloweza kutajirisha Wakulima.

Soko lake ni kubwa.

Page 4: Jarida la Agricultural Council of Tanzania Toleo Na. …actanzania.or.tz/wp-content/uploads/2016/08/ACT...yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya Kilimo. 2

ACT NEWS

Ubia wa Kilimo Tanzania (Tanzania Agricultural Partnership– TAP. Ni muungano wa hiari

baina ya taasisi za umma na binafsi zinazofanya kazi kwa pamoja katika masuala ya kilimo.

Wabia wanochangia katika ushirikiano huu ni pamoja na CNFA/TAGMARK, AGRA, FIPS,

RUDI. Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, NMB na MS-Tanzania. Pamoja na makampuni

ya mbolea na mbegu na mbegu kama Yara, minjingu Mines & Fertilizer Co. Bytrade, Pannar,

Mosanto, Seedco na Kibo Seed. Hadi sasa shughuli za TAP zimeenea kwenye wilaya 25.

Malengo ya TAP

Lengo kuu la Ubia wa Kilimo Tanzania ni kuchangia kupunguza umasikini vijijini. Na lengo

mahususi ni kutoa pembejeo sahihi za kilimo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji na kuboresha

masoko ya mazao kwa kutumia mlolongo wa thamani wenye tija ukisaidiwa na sekta ya

umma na binafsi.

Programu inalenga katika:

Upatikanaji nafuu wa pembejeo

Masoko bora ya bidhaa za wazalishaji

Ongezeko la uzalishaji katika kilimo

Uwekezaji kwenye sekta binafsi ya Kilimo

Mbinu za kufanikisha shughuli za maendeleo na biashara

Wasiliana na: Mratibu Kitaifa,

Tanzania Agricultural Partnership,

S. L. P 14130,

Dar es Salaam.

Simu: +255-22-2128032

Barua pepe: [email protected]

1. Ms. Janet Bitegeko—Mwenyekiti

2. Mr. Mark Magila—Mjumbe

3. Mr. Cleophas Rwechungura—Mjumbe

4. Ms. Milly Sanga-Mjumbe

Bodi ya Wahariri

Je, unataka kufahamu zaidi kuhusu ACT?Je, unataka kufahamu zaidi kuhusu ACT?

Wasiiliana na:Wasiiliana na:

Mkurugenzi Mtendaji:Mkurugenzi Mtendaji:

Agricultural Council of Tanzania Agricultural Council of Tanzania

S.L.P 14130,Dar es Salaam S.L.P 14130,Dar es Salaam

Simu:+255 22 2124851, Simu:+255 22 2124851,

Nukushi: +255 22 2128032, Nukushi: +255 22 2128032,

Barua pepe: act@actanzania .or.tzBarua pepe: act@actanzania .or.tz

Tovuti: www.act.anzania. or.tzTovuti: www.act.anzania. or.tz

DIRA YA ACT

DHAMIRA YA ACT

MALENGO YA ACT

1. Kuimarisha uwezo wa ACT wa kushawishi na kutetea masuala

yaliyofanyiwa utafiti na kuhakikiwa, ambavyo yanaathiri sekya ya

Kilimo.

2. Kuimarisha uwezo wa ACT wa kubuni na kutoa huduma katika

maeneo ya kimuundo, kiufundi, kiuongozi na programu za kutoa

huduma, kwa wanachama wake.

3. Kuongeza uelewa kwa wanachama wa ACT kuhusu programu zake,

huduma za kuwaongezea uwezo na kupata mitaji; ili kubaki na

angalau asilimia 85 ya wanachama wake, pamoja na kurudufu idadi

ya wanachama ifikapo 2018.

4. Kupanua uwanja wa kupata rasilimali –fedha, ili ACT iwe na uwezo

wa kujitegemea kwa asilimia 20 ifikapo 2018.

4 Jarida la ACT– Toleo Na. 16

FAHAMU SHUGHULI ZA TAP

Kuwa chombo kilele na kiongozi,

chenye jukumu la kuinua ustawi wa

wadau katika sekta ya Kilimo

nchini Tanzania

Kutetea kuwepo kwa mazingira

muafaka kwa Biashara ya Kilimo,

na kutoa huduma stahiki ili

kuongeza tija na faida kwa jamnii

ya Wakulima