4
Jarida la Sikika Toleo 19: Septemba, 2015 Namba ya Usajili - 00005809 Huduma bora za afya kwa watanzania wote Utangulizi T oleo hili la 19 linaelezea kwa ufupi baadhi ya shughuli zilizotekelezwa na Sikika katika robo ya tatu ya mwaka 2015. Sikika ilishiriki katika mafunzo yaliyotolewa na Ofisi ya Mdihibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka katika mikoa ya Dodoma, Morogoro na Iringa. Mafunzo hayo yalilenga kuongeza uelewa wa ripoti ya ukaguzi ya CAG na jinsi ya kuitafsiri. Shirika pia limeendela kuitaka serikali ijayo kutatua changamoto za dawa na vifaa tiba nchini ili kuokoa maisha ya watanzania. Ukosefu wa dawa na vifaa tiba muhimu umeendela kuwa tatizo sugu nchini na suluhu ya kudumu bado haijapatikana. NDANI CAG atoa mafunzo kwa AZAKI ........................................................................................................................2 Viongozi wajao watatue changamoto za dawa na vifaa tiba .............................................................................3 Mabadiliko ya mara kwa mara ARVs yawa kero ................................................................................................3 Afya: Kipaumbele muhimu kabla, baada ya Uchaguzi Mkuu .............................................................................4 Ziara ya shirika katika baadhi ya vituo pia ilibaini kuwa baadhi ya watumia huduma za VVU na UKIMWI wamekuwa wakibadilishiwa dawa za ARVs mara kwa mara. Hali hiyo imejitokeza katika vituo mbalimbali vya afya jijini Dar es Salaam. Sikika pia ilifanya tathmini ya ilani za baadhi ya vyama vya siasa na kuvishauri kujumuisha masuala ya afya, hususan kwenye maeneo manne ambayo shirika linayafanyia utetezi. Kwa taarifa zaidi kuhusu kazi za Sikika, tafadhali peruzi tovuti yetu; www.sikika.or.tz, twitter - @ sikika1, facebook - Sikika Tanzania na blogspot - www.sikika-tz.blogspot.com. Kwa maoni tafadhali wasiliana nasi kupitia [email protected] au sms 0688- 493-882. Mkuu wa Idara ya Dawa na Vifaa tiba, Sikika Bi. Alice Monyo akitoa ufafanuzi juu ya changamoto za mfumo wa usambazaji dawa na vifaa tiba katika mkutano uliojumuisha wadau mbalimbali nchini. Kushoto kwake ni Afisa Program wa Idara hiyo, Scholastica Lucas na washiriki wengine. Sikika Newsletter Q3, 2015 - Toleo 19.indd 1 11/9/15 8:33 AM

Jarida la Sikika Namba ya Usajili - 00005809 Toleo 19 ... · ambazo zitatekelezeka baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2015. Ni takriban miaka 23 sasa tangu Tanzania

  • Upload
    lamlien

  • View
    232

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Jarida la SikikaToleo 19: Septemba, 2015Namba ya Usajili - 00005809

Huduma bora za afya kwa watanzania wote

Utangulizi

Toleo hili la 19 linaelezea kwa ufupi baadhi ya

shughuli zilizotekelezwa na Sikika katika robo ya

tatu ya mwaka 2015.

Sikika ilishiriki katika mafunzo yaliyotolewa na Ofisi

ya Mdihibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

(CAG) kwa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka katika

mikoa ya Dodoma, Morogoro na Iringa. Mafunzo

hayo yalilenga kuongeza uelewa wa ripoti ya ukaguzi

ya CAG na jinsi ya kuitafsiri.

Shirika pia limeendela kuitaka serikali ijayo kutatua

changamoto za dawa na vifaa tiba nchini ili kuokoa

maisha ya watanzania. Ukosefu wa dawa na vifaa

tiba muhimu umeendela kuwa tatizo sugu nchini na

suluhu ya kudumu bado haijapatikana.

NDANICAG atoa mafunzo kwa AZAKI ........................................................................................................................2

Viongozi wajao watatue changamoto za dawa na vifaa tiba .............................................................................3

Mabadiliko ya mara kwa mara ARVs yawa kero ................................................................................................3

Afya: Kipaumbele muhimu kabla, baada ya Uchaguzi Mkuu .............................................................................4

Ziara ya shirika katika baadhi ya vituo pia ilibaini

kuwa baadhi ya watumia huduma za VVU na

UKIMWI wamekuwa wakibadilishiwa dawa za ARVs

mara kwa mara. Hali hiyo imejitokeza katika vituo

mbalimbali vya afya jijini Dar es Salaam.

Sikika pia ilifanya tathmini ya ilani za baadhi ya vyama

vya siasa na kuvishauri kujumuisha masuala ya afya,

hususan kwenye maeneo manne ambayo shirika

linayafanyia utetezi.

Kwa taarifa zaidi kuhusu kazi za Sikika, tafadhali

peruzi tovuti yetu; www.sikika.or.tz, twitter - @

sikika1, facebook - Sikika Tanzania na blogspot -

www.sikika-tz.blogspot.com. Kwa maoni tafadhali

wasiliana nasi kupitia [email protected] au sms 0688-

493-882.

Mkuu wa Idara ya Dawa na Vifaa tiba, Sikika Bi. Alice Monyo akitoa ufafanuzi juu ya changamoto za mfumo wa

usambazaji dawa na vifaa tiba katika mkutano uliojumuisha wadau mbalimbali nchini. Kushoto kwake ni Afisa

Program wa Idara hiyo, Scholastica Lucas na washiriki wengine.

Sikika Newsletter Q3, 2015 - Toleo 19.indd 1 11/9/15 8:33 AM

Jarida la Sikika - Toleo 19: Septemba, 2015

2

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za

Serikali (CAG) ilitoa mafunzo kwa wawakilishi wa

Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka katika mikoa ya Dodoma,

Morogoro na Iringa. Sikika ilikuwa ni miongoni mwa

washiriki wa mafunzo hayo yaliyolenga kuongeza

uelewa wa ripoti ya ukaguzi ya CAG na jinsi ya kuitafsiri.

Mafunzo yalifanyika mkoani Morogoro kuanzia Juni 15

hadi 16, 2015.

Sambamba na mafunzo hayo, wawakilishi wa AZAKI

walijadiliana na kuuliza maswali mbalimbali, kupata

ufafanuzi na kutoa michango yao ili ofisi ya CAG iweze

kuifanyia kazi. Baada ya mafunzo na majadiliano AZAKI

na ofisi ya CAG walifikia makubaliano na kuazimia

mambo kadhaa.

Mosi, iliazimiwa kuwa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (CAG)

iishauri serikali kutunga sheria inayowalazimisha

wakaguliwa (mfano Wizara, Idara na Mashirika ya

Umma) kutekeleza mapendekezo ndani ya muda utakao

ainishwa na sheria. Pia kuwepo kitengo maalumu cha

kufuatilia mapendekezo ya CAG na kutoa taarifa ya

hatua gani zichukuliwe endapo hakuna utekelezaji.

Pili, washiriki pia walipendekeza kuimarisha kitengo

cha sheria ili kuisaidia ofisi ya Mdhibiti katika masuala

mbalimbali ya kisheria hasa ukaguzi na katika

kushughulikia masuala mbalimbali yatokanayo na ripoti

za ukaguzi.

Tatu, ofisi ya CAG iimarishe ushirikiano na AZAKI

katika kupanga shughuli za ukaguzi na katika kufuatilia

utekelezaji wa mapendekezo ya ukaguzi. Mfano,

ofisi iangalie namna ya kutumia tafiti mbalimbali

zinazofanywa na asasi za kiraia wakati wa ukaguzi. Pia

ilipendekezwa kuwa ofisi ya Mdhibiti iangalie uwezekano

wa kuwaelimisha wawakilishi zaidi wa AZAKI juu ya

mamlaka ya CAG na masuala ya ripoti. Pia wawakilishi

hao wafuatiliwe na kuwezeshwa kuelimisha watu wengi

zaidi.

Wawakilishi hao wa AZAKI walipendekeza kwamba

ofisi ya CAG iongeze uwanda wa ukaguzi wa masuala

ya mapato ya serikali na madeni ya Taifa ili kutunza

rasilimali za nchi kwa maendeleo ya Wananchi.

Mwisho, washiriki walipendekeza Ofisi ya Taifa ya

Ukaguzi iishauri serikali kuendelea na utaratibu wa

kuwaelimisha wananchi na watumishi wake juu ya

maadili na uwajibikaji kwa ujumla. Wawakilishi hao

wa AZAKI walihitimisha kwa kupendekeza uwepo wa

mikutano ya tathmini ya kufuatilia mapendekezo ya

ripoti za ukaguzi.

CAG atoa mafunzo kwa AZAKI Na Wilson Kitinya, Morogoro

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad akiendesha moja ya mafunzo kwa taasisi na

wadau wa usimamizi wa sheria. Picha kwa hisani ya mtandao: http://www.nao.go.tz

Sikika Newsletter Q3, 2015 - Toleo 19.indd 2 11/9/15 8:33 AM

Jarida la Sikika - Toleo 19: Septemba, 2015

3

Mabadiliko ya mara kwa mara ARVs yawa kero Na Maria Kalavo

Baadhi ya watumia huduma za VVU na UKIMWI

katika vituo mbalimbali vya afya jijini Dar es Salaam

wamelalamikia ubadilishwaji wa mara kwa mara wa

chapa (brand) ya dawa wanazotumia kukabiliana na

makali ya VVU na UKIMWI. Haya ni malalamiko ambao

yamekuwa yakijitokeza na kujirudia katika mikutano ya

watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi (WAVIU) ambayo

Sikika imehudhuria kwa nyakati tofauti jijini Dar es

Salaam.

Baadhi ya WAVIU wameeleza kuwa dawa kutoka katika

baadhi ya makampuni zimekuwa zikiwasababishia

madhara kama vile kuishiwa nguvu, kulegea viungo na

kuhisi kizunguzungu jambo linalowafanya washindwe

kuendelea na shughuli zao. Kwa maelezo yao, watumia

huduma hawa wamekua wakiomba kupewa dawa

za aina moja au chapa moja lakini imeshindikana.

Maelezo wanayopata ni kwamba vituo havina uwezo

wa kuwabadilishia kwa kuwa hupokea dawa hizo kama

zilivyo kutoka Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

Tatizo la kubadilishiwa dawa na kupewa za aina

nyingine ambazo zimeonekana kuwaathiri watumiaji

linasababisha baadhi ya WAVIU kutotumia dawa siku

zote (adherence) au kuacha kunywa siku ambazo mtu

atakuwa amejipangia safari au shughuli zinazohitaji awe

na nguvu. Kitendo cha kuacha kunywa dawa kina athari

kubwa kwa WAVIU kwani huweza kusababisha mwili

kujijengea usugu wa dawa.

Katuni kwa hisani ya Gazeti la Mtanzania Agosti 20, 2015

Changamoto za dawa na vifaa tiba zitatuliwe Na Siri Mtware

Ukosefu wa dawa na vifaa tiba umeendela kuwa

tatizo sugu ambalo suluhu yake bado haijapatikana.

Taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

kwa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) 2014, imebainisha

uwepo wa dawa kwa asilimia 24 tu kwa vituo vya

serikali na 47% kwa vituo binafsi.

Sababu kuu zinazotajwa ni pamoja na kutoshiriki kwa

wananchi katika kusimamia rasilimali na mipango

iliyowekwa katika vituo vyao vya kutolea huduma za

afya, ufinyu wa bajeti zinazopangwa na serikali na

matumizi mabaya ya rasilimali kwa baadhi ya watendaji

katika sekta ya afya.

Wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa

madiwani, wabunge na Rais, ni wakati sasa wa

wananchi kuhakikisha kuwa viongozi wanaowachagua

wanafanyia kazi changamoto hizo. Tuwahoji wagombea;

watafanya nini ili kuhakikisha tatizo la dawa linakuwa

historia nchini? Je, ni jinsi gani watahakikisha bajeti za

dawa muhimu na vifaa tiba zinaongezeka?

Zaidi, wanaoomba kuongoza waeleze; wataweka

mikakati ipi kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu

katika mipango ikiwa ni pamoja na kupatiwa taarifa

muhimu ili waweze kufanya ufuatiliaji wa huduma

zinazotolewa katika vituo vya kutolea huduma za

afya? Wananchi wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha

changamoto hizi zinatatuliwa ili kuboresha upatikanaji

wa dawa na vifaa tiba nchini.

Mwisho, pamoja na changamoto zinazoendelea

kujitokeza, suala la upatikanaji wa dawa na vifaa tiba

lipewe kipaumbele kwa kusimamiwa na kufuatiliwa

kwa karibu ili kuondoa mianya ya ubadhilifu wa

watendaji wasio waaminifu. Kiasi kidogo cha fedha

kinachopatikana kikitumika ipasavyo kitapunguza

pengo la upungufu wa dawa na vifaa tiba katika vituo

vya kutolea huduma za afya vya umma nchini.

WAVIU hao wanaiomba serikali iweke utaratibu wa kupata

mrejesho kutoka kwa watumiaji wa dawa na huduma za

UKIMWI. Kwa sasa hakuna sehemu ambapo WAVIU

wanaweza kupeleka maoni/malalamiko yao moja kwa

moja kwa watunga sera au viongozi wanaohusika na

shughuli za UKIMWI.

Utaratibu wa kubadilishiwa dawa mara kwa mara

umeendelea kuwepo kwa muda sasa lakini watumia

huduma hawajaona serikali ikichukua hatua zozote.

Ushauri kwa serikali ni kushirikiana na wafadhili ili

kuhakikisha kwamba dawa zinazoagizwa ni zile

zinazotoka kwenye makampuni ambayo dawa zake

hazijalalamikiwa na watumiaji kuwa zina madhara.

Sikika Newsletter Q3, 2015 - Toleo 19.indd 3 11/9/15 8:33 AM

Nyumba Na. 69Ada Estate, KinondoniBarabara ya TunisiaMtaa wa WaverleyS.L.P 12183Dar es Salaam, TanzaniaSimu: +255 22 26 663 55/57

Ujumbe mfupi: 0688493882Faksi: +255 22 26 680 15Barua pepe: [email protected]

Blog: www.sikika-tz.blogspot.com

Facebook: Sikika Tanzania

Nyumba Na. 340Mtaa wa KilimaniS.L.P 1970Dodoma, TanzaniaSimu: 026 23 21307Faksi: 026 23 21316

Zaidi, ilipendekezwa kuongeza rasilimali watu katika

afya, kuhakikisha uwepo na upatikanaji wa dawa na

vifaa tiba wa uhakika pamoja na kuboresha huduma za

VVU na UKIMWI.

Shirika limeendela kutoa elimu kwa jamii kuhusu tathmini

hiyo kwa kutumia njia mbalimbali za mawasiliano.

Tunaamini tathmini hiyo itachangia kuboresha Ilani za

vyama mbalimbali vya siasa nchini. Vilevile itakuza uelewa

na ushiriki wa wananchi katika kufuatilia utekelezaji wa

vipaumbele vya afya, kwa wagombea na vyama vyao.

Sikika inatoa rai kwa wananchi wasiishie kuwa

watazamaji katika kipindi cha uchaguzi bali kushiriki kwa

kipindi chote cha miaka 5 kwa kudai utekelezaji wa Ilani

na vipaumbele hata baada ya uchaguzi. Hii itatoa fursa

kwa jamii kuwawajibisha wanaowapa kura kwa lengo la

kupata huduma bora za jamii.

Ilani ya chama ni mkataba au hati ya chama cha

siasa inayotoa muhtasari wa mambo ambayo chama

kinapanga kuyatekeleza endapo wapiga kura watakipa

fursa ya kuunda serikali.

VYAMA vya Siasa nchini vimeshauriwa kutunga ilani

ambazo zitatekelezeka baada ya uchaguzi mkuu

unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2015.

Ni takriban miaka 23 sasa tangu Tanzania ilipoingia rasmi

katika mfumo wa vyama vingi. Vyama mbalimbali vya

siasa nchini vimekuwa vikiandaa Ilani zao na kunadi sera

na vipaumbele kwa wananchi lakini baadhi zimekuwa

hazifahamiki kwa wananchi na hazitekelezwi, mathalan

kwa upande wa afya.

Kwa kutambua hivyo, Sikika ilitathmini ilani za vyama

4 vya siasa kwa miaka mitano iliyopita na hatimaye

kuandaa mapendekezo na matarajio ya wananchi kwa

miaka 5 ijayo, kwa upande wa afya. Shirika lilipata fursa

ya kutoa maoni juu ya vipaumbele vya afya kwa vyama

vya siasa kupitia kituo cha Demokrasia na Maendeleo

(TCD).

Tathmini ya Sikika iliyojikita katika upande wa afya

ilipendekeza kuimarisha utawala bora, uwazi na ushiriki

wa wananchi katika kupanga bajeti za afya na utekelezaji.

Afya: Kipaumbele muhimu kabla, baada ya Uchaguzi MkuuNa Richard Msittu, Dodoma

Baadhi ya akinamama wakisubiri huduma katika kituo cha cha afya Ndago wilayani Iramba.

Sikika Newsletter Q3, 2015 - Toleo 19.indd 4 11/9/15 8:33 AM