31
Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa 1 SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 MPANGILIO WA VIFUNGU Kifungu Kichwa cha habari 1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika. 2. Matumizi. 3. Tafsiri. SEHEMU YA PILI WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA 4. Uanzishwaji wa Wakala. 5. Kazi za Wakala. 6. Mamlaka ya Wakala. 7. Baraza la usimamizi wa maafa. 8. Kazi za Baraza. SEHEMU YA TATU USIMAMIZI WA WAKALA 9. Mkurugenzi Mkuu. 10. Mamlaka ya Mkurugenzi Mkuu. 11. Kurugenzi na watumishi wa Wakala. 12. Kitabu cha orodha ya vitu. 13. Kamati ya usimamizi ya Mkoa. 14. Kazi za Kamati ya Mkoa. 15. Kamati za Wilaya. 16. Kazi za Kamati za Wilaya. 17. Uwezo wa kamati za Mikoa na Wilaya. 18. Kamati za kata. 19. Kazi za Kamati za Kata. 20. Kamati za vijiji. 21. Kazi za Kamati za vijiji. 22. Miongozo ya Kamati za usimamizi. 23. Kanuni za shughuli za kamati ya maafa.

SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

1

SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014

MPANGILIO WA VIFUNGU

Kifungu Kichwa cha habari

1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika.

2. Matumizi.

3. Tafsiri.

SEHEMU YA PILI

WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA

4. Uanzishwaji wa Wakala.

5. Kazi za Wakala.

6. Mamlaka ya Wakala.

7. Baraza la usimamizi wa maafa.

8. Kazi za Baraza.

SEHEMU YA TATU

USIMAMIZI WA WAKALA

9. Mkurugenzi Mkuu.

10. Mamlaka ya Mkurugenzi Mkuu.

11. Kurugenzi na watumishi wa Wakala.

12. Kitabu cha orodha ya vitu.

13. Kamati ya usimamizi ya Mkoa.

14. Kazi za Kamati ya Mkoa.

15. Kamati za Wilaya.

16. Kazi za Kamati za Wilaya.

17. Uwezo wa kamati za Mikoa na Wilaya.

18. Kamati za kata.

19. Kazi za Kamati za Kata.

20. Kamati za vijiji.

21. Kazi za Kamati za vijiji.

22. Miongozo ya Kamati za usimamizi.

23. Kanuni za shughuli za kamati ya maafa.

Page 2: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

2

SEHEMU YA NNE

HATUA ZA KULINDA RAIA

24. Hatua za kulinda raia.

25. Wajibu wa jumla.

SEHEMU YA TANO

SHUGHULI WAKATI WA MAAFA NA HALI YA HATARI

26. Kutangaza maafa.

27. Hali ya hatari inayojikusanya kwenye maeneo.

SEHEMU YA SITA

MPANGO WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAAFA

28. Mpango wa Taifa wa Usimamizi.

SEHEMU YA SABA

MFUKO WA USIMAMIZI WA MAAFA

29. Mfuko wa Taifa wa usimamizi wa maafa.

30. Usimamizi wa makusanyo na misaada.

SEHEMU YA NANE

MASHARTI YA FEDHA

31. Vyanzo vya fedha

32. Taarifa ya mwaka ya mahesabu.

33. Uwasilishaji wa taarifa ya mwaka.

34. Usimamizi na udhibitisho wa fedha.

35. Bajeti ya mwaka na ya nyongeza.

SEHEMU YA TISA

MAKOSA NA ADHABU

36. Kanuni za uendeshaji.

37. Uwezo wa kuwekeza.

38. Makosa na adhabu.

39. Makosa na bodi shirikishi.

Page 3: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

3

SEHEMU YA KUMI

MASHARTI YA MCHANGANYIKO

40. Jukwaa la Usimamizi wa maafa.

41. Kinga dhidi ya mashtaka.

42. Kanuni.

43. Kufuta na kubakiza Sura 242.

____

JEDWALI

______

Page 4: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

4

TAARIFA

________

Muswada huu utakaowasilishwa Bungeni umechapishwa pamoja na

Madhumuni na Sababu zake wa ajili ya kutoa taarifa kwa umma.

Dar es Salaam, OMBENI Y. SEFUE

15 Oktoba, 2014 Katibu wa Baraza la Mawaziri

MUSWADA

wa

Sheria kwa ajili ya kuanzishwa kwa Sheria ya Wakala wa Usimamizi

wa Maafa; usimamizi wa athari zitokanazo na maafa; uratibu

wa hatua za kuzuia, kukabiliana, kupunguza maafa, kujiandaa

na kurejesha hali ya awali na kuanzisha na kusimamia Mfuko

wa Usimamzi wa Maafa na kuhusiana na mambo

yanayohusiana nayo.

IMETUNGWA na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Page 5: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

5

SEHEMU YA KWANZA

MASHARTI YA AWALI

Jina na tarehe

ya kuanza

kutumia

1. Sheria hii itaitwa Sheria ya Uasimamizi wa Maafa

ya mwaka, 2014 na itaanza kutumika katika tarehe ambayo

itateuliwa na Waziri kupitia Tanganzo la Serikali

litakalochapishwa kwenye Gazeti.

Matumizi 2. Sheria hii itatumika Tanzania Bara Tafsiri 3. Katika sheria hii, isipokuwa kama muktadha

utahitaji vinginevyo: “Wakala” maana yake ni Wakala wa Usimamizi wa Majanga

Tanzania inayoanzishwa chini ya kifungu cha 4; “afisa muidhiniwa” maana yake ni mtu yeyote aliyeidhinishwa

kutekeleza shughuli yeyote kama atakavyoelekezwa na

Wakala; “Baraza” maana yake ni Baraza la Usimamizi wa Majanga

Tanzania linaloanzishwa chini ya kifungu cha 7; “Mkurugenzi Mkuu” maana yake ni Mkurugenzi Mkuu wa

Wakala anayeteuliwa chini ya kifungu cha 9 cha

Sheria hii; “maafa” maana yake ni tukio au mfululizo wa matukio, ama

ya asili au yanayosababishwa na binadamu,

yanayosababisha au kutishia kutokea vurugu au tishio

kwenye shughuli za jamii, yanayosababisha kuenea

kwa majanga yanayosababishwa na binadamu au ya

asili katika uchumi au mazingira yanayozidi uwezo

wa jamii hiyo kupambana nayo kwa kutumia

rasilimali zake; “eneo la maafa” maana yake ni eneo lililotangazwa kuwa

eneo la maafa chini ya Sheria hii; “usimamizi wa maafa” maana yake ni juhudi endelevu za

mipango ya utekelezaji unaolenga- (a) kuzuia hatari au tishio la maafa; (b) kupunguza ukali au matokeo ya maafa; (c) kujizatiti dhidi ya na maafa; (d) kuanzisha au kuimarisha juhudi za kujiandaa dhidi

ya maafa;

Page 6: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

6

(e) kuanzisha njia za haraka za kukabiliana na maafa; (f) kuanzisha au kuimarisha njia za kurudisha hali ya

kawaida baada ya maafa na kurekebisha athari

zitokanazo na maafa. “kujiandaa na maafa” maana yake ni hali ya kuwa tayari

kukabiliana na tishio la hali ya maafa, maafa na athari

zake; “uzuiaji wa maafa” maana yake ni hatua zinazochukuliwa

kuondoa au kuzuia matukio ya kibinadamu au ya asili

yasisababishe kutokea kwa maafa; “urekebishaji wa athari za maafa” maana yake ni hatua

zinazosaidia kurejesha hali ya maisha, mali na

kiwango cha uzalishaji cha jamii zilizoathirika

kurejesha miundombinu muhimu, uwezo wa

uzalishaji, taasisi na huduma zilizoharibiwa au

kuonekana kutokufanya kazi kutokana na maafa na

kusaidia kuleta maendeleo endelevu kwa kufanya

marekebisho muhimu kwa mabadiliko

yaliyosababishwa na maafa au kuboresha na kurudisha

katika hali ya kawaida; “kukabiliana na maafa” maana yake ni hatua yoyote

inayochukuliwa kabla na mara baada ya athari za

maafa inayochukuliwa kuokoa maisha, kulinda mali na

mazingira au kushughulikia uharibifu uliotokea na

madhara mengine yaliyosababishwa na maafa; “upunguzaji wa hatari za maafa” maana yake ni hatua

zinazochukuliwa kupunguza uwezekano wa matokeo

yenye athari ya maafa kama vile vifo, majeruhi,

matarajio ya upotevu wa mali, maisha, kuathirika kwa

shughuli za uchumi au uharibifu wa mazingira

unaotokana na mwingiliano wa athari za asili

zinazotokana na mazingira magumu na shughuli za

binadamu; “Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya

usimamzi wa maafa; “kupunguza” maana yake ni hatua zinazoelekezwa

kupunguza athari, matokeo au athari za maafa;

Page 7: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

7

“Mpango wa Taifa wa Usimamizi wa Maafa” maana yake ni

mpango ambao unelezea hatua zitakazochukuliwa

katika kushughulikia, kupunguza hatari za usimamizi

wa maafa; “maafa ya asilia” maana yake ni maafa yanayotokana na

mwingiliano wa matukio ya asili bila kusababishwa na

binadamu na inajumuisha matukio kama vile,

tetemeko, kimbunga, mafuriko, ukame, moto au

magonjwa ya mlipuko; “Jukwaa” maana yake ni Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa

Maafa lililoanzishwa chini ya Sheria hii; “Kamati ya Kata” maana yake ni Kamati ya Usimamizi wa

Maafa ya Kata iliyoanzishwa chini ya Sheria hii; “Kamati ya Kijiji” maana yake Kamati ya Kijiji ya Usimamzi

wa Maafa iliyoanzishwa chini ya Sheria hii; “Kamati ya Mkoa” maana yake ni Kamati ya Mkoa ya

Usimamizi wa Maafa iliyoanzishwa chini ya Sheria

hii; “udhaifu” maana yake ni kiwango cha uwezekano wa watu

kupatwa au kuathirika na maafa.

SEHEMU YA PILI

WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA

Uanzishwaji

wa Wakala 4.-(1) Inaanzishwa wakala ambayo itajulikana kama

Wakala wa Usimamizi wa Maafa Tanzania. (2) Wakala itakuwa ni Bodi hodhi na kwa jina lake

hodhi litakuwa na uwezo wa- (a) kushtaki na kushtakiwa; (b) kuingia katika mikataba, makubaliano, waraka wa

maelewano, hati na kutekeleza mipangilio

mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika;

na (d) kuwa na muhuri wake.

Page 8: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

8

(3) Mwanasheria Mkuu atakuwa na haki ya

kuunganishwa katika shauri lolote au jambo lolote

lililofunguliwa na au dhidi ya Wakala. (4) Endapo, Mwanasheria Mkuu ataunganishwa katika

shauri lolote, masharti ya Sheria ya Mwenendo wa Mashauri

ya Serikali yatatumika, katika shauri au jambo hilo kama

kwamba yamefunguliwa na au dhidi ya Serikali. (5) Kwa madhumuni ya vifungu (3) na (4), Wakala

itakuwa na wajibu wa kumfahamisha Mwanasheria Mkuu

kuhusu shauri lolote ambalo liko mahakamani au kusudio la

kufungua shauri au kupeleka suala au suala kwa au dhidi ya

Wakala.

Kazi za

Wakala 5.-(1) Wakala itakuwa ni kitovu cha taifa cha kuratibu

upunguzaji wa hatari ya maafa na usimamizi wake. (2) Katika utekelezaji wa kazi zake kufuatana na

masharti ya kifungu kidogo cha (1), Wakala- (a) itatayarisha sera na mipango kwenye shughuli zote

zinazohusiana na usimamizi wa maafa Tanzania

Bara; (b) itakuwa kituo cha mipango, asasi ya uratibu na

usimamizi wa uzuiaji, upunguzaji, utayarishaji,

kukabiliana, utekelezaji na uokoaji baada ya maafa

kwa kuzingatia uwezekano wa kuwepo kwa hatari

ya maafa; (c) itaratibu na kusimamia taasisi za wizara, sekta

mbalimbali na kamati za kitaalam zenye dhamana

ya usimamzi wa maafa katika ngazi zote; (d) itaunda Kituo cha Dharura cha Kusimamia Maafa; (e) itaunda mfumo wa tahadhari ya awali

utakaohusisha sekta zote na kuwa kiungo kati ya

asasi mbalimbali zinatoa huduma ya tahadhari; (f) itaendeleza elimu, uelewa na utumiaji wa taarifa,

teknolojia ya mawasiliano ya usimamizi wa maafa

kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma; (g) kutafuta rasilimali kwa ajili ya usimamizi wa

shughuli za maafa; na

Page 9: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

9

(h) kuhitaji kutoka taasisi yoyote, idara, mamlaka, mtu

au watu, kupeleka taarifa inayotakiwa kwa ajili ya

shughuli za usimamzi wa maafa kama Mkurugenzi

atakavyoelekeza.

Mamlaka ya

wakala 6.-(1) Kwa madhumuni ya kutekeleza kazi zake,

Wakala itakuwa na mamlaka ya- (a) kuamuru watu kuondoka katika meneo ya maafa

au maeneo yanayopatwa na maafa mara kwa mara; (b) kusimamisha au kuzuia mauzo kutoa au

kushirikisha vileo, vinywaji, silaha, milipuko, au

mazao mengine ambayo hayapaswi kuwa kwenye

maeneo ya maafa; na (c) kuchukua na kutumia rasilimali za Serikali

itajumuisha maghala, vifaa na nyenzo nyingine

kama itakavyonekana ni lazima kwa shughuli za

dharura.

(2) Wakala itatumia mamlaka iliyopewa katika

utekekezaji wa maelekezo yoyote yaliyotolewa chini ya

mamlaka yake na kuchukua na kusababisha kuchukuliwa kwa

hatua hizo ikijumuisha kupeleka shauri mahakamani au

kwenye baraza.

(3) Wakala anaweza, baada ya kutoa taarifa ya

kuridhisha ya kusudio lake la kuchukua hatua hizo, kuelekeza

taasisi, idara, mamlaka, mtu au chombo cha watu, kutekeleza,

ndani ya muda utakaopangwa na kwanamna kama

itakavyoelekeza, kazi yoyote au nyingine iliyowekwa na au

chini ya Sheria hii au Sheria nyingine yoyote kuhusiana na

usimamizi na utekelezaji wa Sheria.

(4) Endapo itatokea kushindwa kutekelea maelekezo

hayo, Wakala inaweza kufanya au kusababisha kufanyika kazi

zinazotakiwa na gharama zitakazotumika zitarudishwa na

Wakala kutoka kwenye taasisi, idara, mamlaka, mtu au

chombo cha watu shirikishi kwa njia ya madai.

Page 10: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

10

Baraza la

usimamizi

wa maafa

7.-(1) Kutakuwa na Baraza la Usimamizi wa Maafa

Tanzania.

(2) Baraza litaundwa na wajumbe wafuatao- (a) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana ya

Usimamizi wa maafa ambaye atakuwa

Mwenyekiti; (b) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana ya ulinzi na

Jeshi la Kujenga Taifa ambaye atakuwa Makamu

wa Mwenyekiti; (c) Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali; (d) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana ya mamlaka

na tawala za mikoa na serikali za mitaa; (e) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana na fedha; (f) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana na afya na

ustawi wa jamii; (g) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana na

mawasiliano; (h) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana na

mazingira;

(i) Katibu Mkuu Wizara yenye dhamana na Kilimo; na

(j) Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Hali ya Hewa Tanzania.

(3) Mkurugenzi Mkuu wa Wakala atakuwa Katibu wa

Baraza.

(4) Baraza linaweza kumualika mtu yeyote wakati wa

Mkutano wake kama Baraza litakavyoona lazima.

(5) Masharti ya Jedwali la Sheria hii yatahusu

shughuli za Baraza na mambo mengine yanayohusiana nayo.

Kazi za

Baraza 8.-(1) Baraza litasimamia shughuli za Wakala.

(2) Katika kutekeleza kazi zake, Baraza litakuwa na

Page 11: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

11

jukumu la- (a) kuhakikisha kwamba juhudi za kupunguza athari

za maafa zinajumuisha taasisi muhimu za Serikali,

sera za maendeleo, mikakati na program za kitaifa,

kimkoa na kimtaa; (b) kutoa msaada katika utafutaji wa rasilimali kwa

azma ya kupata njia bora ya kupunguza na

kusimamia athari za maafa; (c) kuhamasisha maendeleo ya taarifa za Taifa na

uelewa wa mikakati ya usimamizi na uanzishaji wa

mtandao wa wadau wa athari za usimamizi wa

maafa; (d) kupitia na kuboresha sera za usimamizi wa athari

za maafa; na (e) kumshauri Waziri kuhusiana na usimamizi wa

maafa na mambo yote yanayohusiana nayo.

SEHEMU YA TATU

USIMAMIZI WA WAKALA

Mkurugnezi

Mkuu 9.-(1) Kutakuwa na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala

ambaye atateuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watumishi

wa umma wenye sifa husika.

(2) Mkurugenzi Mkuu atakaa madarakani kwa kipindi

cha miaka mitano na anaweza kuchaguliwa kwa mara

nyingine.

(3) Mkurugenzi Mkuu atakuwa Mtendaji Mkuu na

Afisa Masuhuli wa Wakala na atawajibika kwenye Baraza. Mamlaka ya

Mkurugenzi

Mkuu

10.-(1) Mkurugenzi Mkuu anaweza wakati wa hali ya

hatari na baada ya kushauriana na Mwenyekiti wa Baraza

kutoa maelekezo au amri ambayo ni muhimu katika

kushughulikia jambo husika.

(2) Mkurugenzi Mkuu baada ya kushauriana na

Mwenyekiti-

Page 12: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

12

(a) atamfahamisha Waziri kuhusu hatua za dharura

zilizochukuliwa ili kukabili hali iliyotokea; (b) kuelekeza kuwepo kwa mkutano wa dharura wa

Baraza ili kutoa maamuzi kuhusu hali iliyotokea. Kurugenzi

nawatumishi

wa Wakala

11.-(1) Wakala kwa idhini ya Mamlaka husika,

anaweza kuanzisha kurugenzi, vitengo kama itakavyoonekana

lazima kwa ajili ya utekelezaji wa kazi za Wakala.

(2) Wakala, kwa idhini ya Baraza itateua au kuajiri

idadi ya maofisa wa umma kama itakavyoonekana ni lazima

kwa ajili ya utekelezaji mzuri wa kazi chini ya sheria hii.

Kitabu cha

orodha ya

vitu

12.-(1) Mkurugenzi Mkuu ataanzisha na kutunza

Ktabu cha orodha ya vitu kwa ajili ya misaada ya kimaisha na

uhakiki wa muundo mbinu kwa ajili ya shughuli za usimamizi

wa majanga.

(2) Kitabu au orodha iliyoandaliwa na Wakala

itakuwa ni mali ya kiofisi kwa matumizi ya Wakala, na

Wakala anaweza akawashirikisha taarifa zilizomo katika

kitabu au orodha na mtu mwingine yeyote, idara au taasisi

kama atakavyoona inafaa.

(3) Uhakiki wa miundombinu kama, ilivyotumika

katika kifungu kidogo cha (1), ina maana yake, mchakato wa

mfumo, nyenzo, teknolojia, mtandao, mali na huduma

maalum za afya, usalama, au uchumi mzuri na utekelezaji wa

kazi za Serikali na jamii. Kamati ya

usimamizi ya

Mkoa

13.-(1) Sekretarieti ya Mkoa ilianishwa chini ya

Sheria ya Tawala za Mikoa, itakuwa Kamati ya usimamizi ya

Maafa ya Mkoa katika mamlaka ya mipaka yake.

(2) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1)

na kifungu cha (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa, Kamati ya

Mkoa pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa

ikiwajumuisha wajumbe wafuatao waliochaguliwa na Katibu

Tawala wa Mkoa-

Page 13: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

13

(a) mratibu wa usimamizi wa maafa wa mkoa, (b) mwakilishi kutoka jumuiya asasi zisizo za serikali

za mkoa; (c) wawakilishi wawili kutoka sekta binafsi ndani ya

mkoa; (d) mwakilishi wa Mkoa wa Chama cha Msalaba

Mwekundu na asasi nyingine za kibinadamu na za

kujitolela; (e) wawakilishi watatu kutoka taasisi za dini; na (f) watu wawili mashuhuri.

(3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (2),

kamati ya Mkoa inaweza, kumwita mtu yeyote ambaye si

mjumbe wa kamati kuhudhuri na kutoa maamuzi ya kamati.

(4) Mratibu wa kamati ya usimamizi wa maafa ya

mkoa kwa madhumuni ya kifungu hiki atakuwa Katibu wa

Kamati ya Mkoa.

Kazi za

Kamati ya

Mkoa

14. Kazi za Kamati za Mkoa zitakuwa-

(a) kumshauri Mkuu wa Mkoa kwenye masuala ya

usimamizi wa maafa na shughuli zinazofanywa

mkoani na mambo mengine yoyote yatakayoletwa

na Kamati ya Mkoa; (b) kuangalia na kuratibu upungazaji wa athar za

usimamzi wa maafa na shughli za dhamila

miongoni mwa taasisi za kisekta za Serikali,

Serikali za mitaa, jamii na wahenga wengine

wanaojihusisha katika upunguzaji wa athari za

usimamiziw a maafa; (c) kuhamasisha rasilimali kwa ajili ya usimamizi wa

maafa na kushughulika na maafa yanayotokea

katika mikoa yao;

(d) kulinganisha mfumo wa awali wa tahadhari wa

Mkoa na kuwezesha uanzishaji wa kuwa na data za

taarifa ya athari za maafa kimkoa kwa kushirikiana

Page 14: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

14

na Wakala; na (e) kuratibu mipango ya Wilaya katika kuzuia maafa

na namna ya kuyapunguza iliyowasilishwa na

Kamati ya Wilaya.

Kamati za

Wilaya 15.-(1) Kamati ya Baraza la Usimamizi lililoanzishwa

chiniya Sheria ya Serikali ya Mtaa (Mamlaka ya Mji) na

Sheria ya Serikali ya Mtaa (Mamlaka ya Wiaya) kwa ajili ya

Sheria hii, zitakuwa Kamati za usimamizi za maafa za Wilaya

katika maeneo ya mamlaka ya Wilaya husika.

(2) Bila kuathiri kifungu akidogo cha (1) na masharti

ya sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka ya Wilaya) kuhusu

uundwaji wa Baraza la usimamizi, Kamati za Wilaya

zitajumuisha pamoja na wajumbe wa Kamati ya Usimamizi

wa Baraza ikiwajumuisha wajumbe walioteuliwa na

Mkurugenzi Mtendaji wafuatao- (a) mratibu wa Wilaya wa usimamzi wa maafa; (b) wawakilishi wawili wa sekta binafsi ndani ya

Wilaya; (c) wawakilishi katoka jumuiya ya Mkoa ya Asasi

zisizo za Serikali; (d) watu wawili mashuhuri; (e) mwakilishi wa Wilaya wa chama cha Msalaba

Mwekundu na taasisi za hiari na za kujitolea; (f) wawakilishi watatu wa taasisi za dini;

(3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (2),

Mkurugenzi wa Halmashauri ikiwa ataonekana lazima,

kumwita mtu yeyote ambaye si mjumbe wa kamati

kuhudhuria maazimio ya kamati.

(4) Mratibu na msimamizi wa maafa wa Wilaya kwa

madhumuni ya kifungu hiki atakuwa katibu wa kamati wa

Wilaya;

Kazi za

Kamati za

Wilaya

16. Kazi za Kamati ya Wilaya zitakuwa-

Page 15: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

15

(a) kumshauri Kamishna kuhusu masuala ya

usimamizi wa maafa na kufanya shughuli za

wilaya na mambo mengine yaliyoletwa na Mkuu

wa Wilaya; (b) kuangalia na kuratbu athari za usimamizi wa maafa

na shughuli za dharura katika ngazi ya wilaya; (c) kuhamasisha rasilimali zinazohusiana na

usimamizi wa maafa.

Uwezo wa

kamati za

Mikoa na

Wilaya

17. Kamati za Usimamizi maafa na mkoa na wilaya

zitashirikiana na Wakala, zitakuwa na uwezo wa-

(a) kuelekeza taasisi zote katika Mkoa na Wiaya

kutayarisha, kuzuia au kupunguza maafa; (b) kuamuru watu kuondoka katika maeneo ambayo

yameathirika au kufikiwa na maafa na kuwapangia

maeneo mengine; (c) kumuomba mtu yeyote au asasi ndani ya mkoa au

wilaya kutoa usafiri, jingo oote, vifaa, bidhaa muhimu

na usambazaji mwingine kwa ajili ya kusaidia juhudi

za usimamizi katika wilaya; (d) kuanzisha kamatiai ndogo kwa ajili ya kuhakikisha

utekelezaji mzuri wa kazi zake; (e) kufanya jambo lolote ambalo ni la lazima kufanywa au

kulingana na utekelezaji wa kazi zake chini ya sheria

hii kutegemeana na sera iliyoanzishwa, mipango na

taratibu; Kamati za

kata 18.-(1) Vikundi vya usimamizi vya Kata

vinavyoundwa chini ya sheria ya Serikali za mitaa (Mamlaka

ya Wilaya) kwa madhumuni ya sheria hii, zitakuwa kamati za

usimamizi wa maafa za Kata kutoka maeneo ya mamlaka zao.

(2) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1), na masharti

ya Sheria ya Seriakli za Mitaa (Mamlaka ya Wilaya)

kuhusiana na uundaji wa vikundi vya usimamizi vya kata,

kamati za Kata kwa kujumuisha wajumbe wa vikundi vya

usimamizi za kata, ikijumuisha wajumbe wafuatao ambao

wameteuliwa na Mkurugenzi wa Baraza kwa kushauriana na

Page 16: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

16

Afisa Kaa Mtendaji. (a) wawakilishi wawili kutoka sekta binafsi ndani ya

Kata; (b) wawakilishi wa taasisi za kijamii ndani ya Kata; (c) watu wawili mashuhuri; (d) mwakilishi kutoka chama cha msalaba mwekundu

na taasisi nyingine za kibinadamu na hiari; na

(2) wawakilishi watatu kutoka taasisi za dini.

(3) Afisa mtendaji wa kata aweza, iwapo ataona kuna

ulazima, kumjumuisha mtu yeyote ndani ya kata husika

ambaye si mjumbe wa Kamati kuhudhuria kikao cha kamati.

(4) Mkurugenzi wa Halmashauri wa Kata, atamfanya

afisa yeyote wa kata kuwa Katibu wa kamati ya Kata kwa

madhumuni ya kifungu hiki.

Kazi za

Kamati za

Kata

19. Kazi za Kmati ya Kata zitakuwa ni:

(a) kuangalia na kuratibu athari za usimamizi wa

maafa na shughli za dhamira katika ngazi ya Kata; (b) kuhamasisha rasilimali klingana na usimamizi wa

maafa; (c) kusaidia utekelezaji wa mipango ya usimamizi wa

mafaa ya kata; (d) kutoka katika utaratibu ulioratibiwa,hali yoyote ya

dharura katika ngazi ya kata.

Kamati za

Kata 20.-(1) Kikundi cha usimamizi wa kijiji

kinachoanzishwa chini ya sheria ya serikali (mamlaka ya

wilaya) kwa madhumuni ya sheria hii, Kamati ya usimamizi

ya maafa ya vijiji katika maeeo ya mamlaka yake.

(2) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1) na masharti

ya sheria ya Serikari (Mamlaka za Wilaya) kuhusu aina na

uundaji wa kikundi cha wilya kwa kujumuisha wajumbe wa

kikundi cha utawala wa kijiji. Ikijumuisha wajumbe wafuatao

walioteuliwa na Mkurugezi wa Halmashauri kwa kushauriana

Page 17: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

17

na Afisa Mtendaji wa Kijiji: (a) wawakilishi wa sekta binafsi zilizopo katika kijiji; (b) mwakilishi wa jumuiya za asasi zisizo za Serikali

zilizopo katika kijiji; (c) watu wawili mashuhuri; (e) mwakilishi kutoka chama cha msalaba mwekundu

na taasisi dini.

(3) Bila kujali masharti ya kufungu kidogo (2), Afisa

Mtendaji wa kijiji aweza, pale anapoona ni lazima kumwita

mtu yeyote kutoka ndani ya kijiji husika ambaye si mjumbe

wa kamati kuhudhuria kikao cha maamuzi cha Kamati.

(4) Mkurugenzi wa Baraza kwa kushuriana na Afisa

Mtendaji wa Kijiji atamfanya afisa yeyote wa kijiji kuwa

Katibu wa Kamati ya Kijiji kwa madhumuni ya kifungu hiki.

Kazi za

Kamati za

vijiji

21.-(1) Kazi za Kamati za Kijiji zitakuwa-

(a) kuangalia na kuratibu athari za usimamizi wa

maafa na shughuli za dharura katika ngazi ya

kijiji; (b) kuwa kama chombo cha taarifa kuhusiana na

utoaji taarifa za athari mapema; (c) kuhamasisha rasilimali kuhusu usimamizi wa

maafa; (d) kutekeleza mipango ya utoaji taarifa na

uwelewa katika vijiji; na (e) kuitikia katika utaratibu ulioratibiwa hali

yoyote ya dharura katika ngazi ya kijiji.

(2) Katika utekelezaji wa kazi zake, Kamati ya kijiji

kama itakavyowekana itatumia sheria za kimira, taratibu za

kimila na mbinu za wazawa ya tahadhari na mawasiliano.

Miongozo ya

Kamati za

usimamizi

22.-(1) Waziri anaweza kutengeneza mwongozo kwa

ajili ya usimamizi mzuri kamati za wilaya, Kata na vijiji.

Page 18: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

18

(2) Miongozo iliyotengenezwa chini ya kifungu hiki

zitaelezea- (a) utayarishaji wa mipango kwa ngazi mbalimbali ya

Kamati; (b) njia za mawasiliano na usambazaji wa taarifa

kuhusiana na kupunguza athari za maafa na

usimamizi; (c) usambazaji wa taarifa mapema kuhusiana na

tahadhari; (d) uendeshaji wa shughuli za Kamati.

(3) Waziri anaweza kutunga miongozo ambavyo

itatumwa na Kamati zilizoainishwa. Kanun za

shughuli za

kamati ya

maafa

23. Kamati za Mkoa, Wilaya, Kata na vijiji zitaweka

kanuni za kujiongoza katika mamlaka zao husika.

SEHEMU YA NNE

HATUA ZA KULINDA RAIA

Hatua za

kulinda raia 24.-(1) Wakala itaweka hatua za kulinda raia kwa asasi

za Serikali za mitaa na asasi za Sekta mbalimbali

zinazojihusisha na usimamizi wa maafa.

(2) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (1) wakala

atachukua watu kama itakavyoweza kuona ni lazima

kuendeleza mipango kwa kupanga uwezao kwa Kamati za

Mikoa na Wilaya, taasisi za serikali na taasisi mbalimbali za

kisekta mufuata na masharti ya huduma za lazima na taratibu

zitakazofuatwa katika kutekeleza shughuli za uokoaji wa

maafa. (3) “Kulinda raia mali” ilivyotumika katika kifungu

hiki, ina maana ya juhudi za pamoja za vitengo tofauti za

dharura katika kuandaa jamii kujilinda na hatari ya

kuongezeka ka maafa.

Wajibu wa

jumla 25. Kila mtu ana wajibu wa -

(a) kuweka mpangilio wa ustawi wa jamii na kutunza

Page 19: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

19

amani na mapatano; (b) kutunza tatbia ambazo zinapunguza athari za

maafa; na (c) kuwa tayari kuonyesha na kuridhia kushiriki katika

shguhuli za usimamizi wa maafa.

SEHEMU YA TANO

SHUGHULI WAKATI WA MAAFA NA HALI YA HATARI

Kutangaza

maafa 26.-(1) Pale wakala atakaporidhika kwamba hali ya

Hatari inajikusanya kwenye eneo la maafa, itahuisha mpango

wa dhamira wa kujiandaa na kutekelezaji wa Taifa kwa

kutumika katika eneo hilo kwa kipindi cha miezi mitatu.

(2) Pale ambapo mpango wa dharura wa Taifa wa

kujiandaa na utekelezaji una huishwa katika eneo, Waziri

atatoa amri kwenye Gazeti, kuweka utaratibu wa shughuli

ambazo zitatumika katika eneo hilo.

(c) Hali ya Hatari

Hali ya hatari

inayojikusan

ya kwenye

maeneo

27.-(1) Pale hali ya hatari inapojikusanya kwenye

maafa ni ya aina ambayo kwamba inahitaji hatua za kipekee,

Baraza litapendekeza kwa Waziri kwamba hali ya hatari

itatangazwa katika eneo lolote au kwa Tanzania Bara pale,

baada ya waziri kuridhika kwamba hali ya hatari ya maafa

inaruhusu kutangazwa kwa hali ya hatari, Waziri atamuomba

Rais kutumia uwezo wake alipopewa na Katibu kutangaza hai

ya htari kwa eneo husika au Tanzania Bara yote.-

(2) Tangazo la hali ya Hatari litajumuisha na kueleza

hatua za haraka ambazo zitakazochukuliwa ikijumuisha- (a) kuwahamisha au kuwaondoa watu na mali zao; (b) kutumia msaada wa Jeshi; (c) kupata msaada wa kimataifa; (d) hatua nyingine kama itakavyokuwa lazima

kulingana na hali halisi ya mazingira.

Page 20: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

20

SEHEMU YA SITA

MPANGO WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAAFA

Mpango wa

Taifa wa

Usimamizi

28-(1) Wakala kwa kibali cha Waziri, atatayarisha na

kutunza mpango wa Taifa wa usimamizi wa maafa.

(2) Mpango wa Taifa wa usimamizi wa maafa

utaunganishwa katika mpango wa maendeleo wa Taifa wa

mwaka na utakuwa unahuishwa na kutengenezwa kama ni

lazima. (3) Mpango wa Taifa na usimamizi wa maafa

itawezesha mwelekeo wa upunguzaji wa athari za maafa na

usimamizi katika maendeleo na kisekta na itatumiwa na

Wakala, Kamati za Mkoa na Wilaya na Serikali na asasi

mbalimbali.

(4) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (3) Kila

Wakala, Kamati za Mikoa na Wolaya, Serikali na asasi

mbalimbali za kisekta zitakayarisha na kuwasilisha taarifa ya

mwaka kwenye Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa kwa

majadiliano na kupeana uzoefu.

(5) Waziri, kwa kanuni atatoa tamko kwa mambo

ambayo atayajumuisha katika mpango wa Taifa wa usimamizi

wa maafa.

SEHEMU YA SABA

MFUKO WA USIMAMIZI WA MAAFA

Mfuko wa

Taifa wa

usimamizi

wa maafa

29.-(1) Kutakuwa na Mfuko wa Taifa wa Usimamizi

wa maafa.

(2) Vyanzo vya fedha vya Mfuko vitakuwa- (a) kiasi cha fedha ambacho kitakachoainihswa na

Bunge kwa madhumuni ya usimamizi wa maafa; (b) mchango wa hiari kwa Mfuko kutoka kwa mtu

yeyote au taasisi; (c) fedha yoyote ambayo imetolewa kwa njia kya

msaada au mkopo kutoka ndani na nje ya Jamhuri

Page 21: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

21

ya Muungano. (d) fedha yoyote iliyopatikana kwa njaa mauzo ya vitu

vilivyotolewa kama msaada; na (e) kutokana na harambee;

(3) Mfuko utasimamiwa na kuongozwa na wakala na

Mkurugenzi Mkuu atakuwa ndiye afisa masuhuli.

(4) Mfuko utatumika kwa- (a) masharti ya bidhaa muhimu na misaada mingine

kwa waathirika wa maafa yoyote, hatari au

dharura; na (b) kuzuia, kupunguza, kutayarisha katika maafa na

shughuli nyingine zinazohusu usimamizi wa

maafa.

Usimamizi

wa

makusanyo

na misaada

30.-(1) Wakala unaweza kuendesha mchango maalum

au wa jumla kwa jamii kuchangia vitu au fedha kwa

madhumuni ya kuokoa maisha, vitu, kupunguza uharibifu au

kuhifadhi maisha ya jamii iliyoathirika na maafa.

(2) Pale ambapo kuna mantiki kwa ombi la wakala,

mtu yeyote au taasisi inayokusanya vitu au fedha

zilizochangwa, itatakiwa kuwasilisha taarifa kwa wakala,

kuelezea vitu vilivyokusanywa na fedha ambayo vitu hivyo

au fehda ziligawiwa kwa jamii iliyoathirika na maafa.

(3) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (2),

misaada kwa jamii iliyoathirika na maafa itapelekwa moja

kwa moja kwa jamii husika au kupitia kamati za Mkoa au

Wilaya, Wakala au viongozi wa Kitaifa.

SEHEMU YA NANE

MASHARTI YA FEDHA

Vyanzo vya

fedha 31.-(1) Vyanzo vya fedha za Wakala vitajumuisha-

(a) fidia kama zitakavyoainishwa na Bunge ; (b) fedha zozote au rasilimali ambayo inaweza

kuwekwa au kupatikana kutoka kwenye vyanzo

Page 22: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

22

vingine; (c) ada zinazowekewa na gharama nyingine

zilizokusanywa kutoka katika huduma

zilizotolewa. (d) zawadi, mikopo na michango; (e) fedha inayopatikana kutokana na mauzo ya

rasilimali za wakala; na (f) fedha nyingine yoyote, iliyokopwa, kupokelewa

na, au iliyopatikana kwa ajili ya Wakala kwa

madhumuni ya kazi zake.

(2) Ada na malipo yanalipwa chini ya Sheria hii

yataelezewa na kanuni.

Taarifa ya

mwaka ya

mahesabu

32.-(1) Katika sheria “mwaka wa fedha” ina maana ya

mwaka wa fedha wa Serikali.

(2) Mkurugenzi Mkuu, katika kila “mwaka wa fedha”

atatayarisha taarifa ya utekelezaji wa mwaka wa shughuli

zinazochukuliwa na wakala na kuwasilishwa kwa Waziri

baada ya kuidhinishwa na Bodi.

(3) Mkurugenzi Mkuu, atahakikisha kwamba taarifa ya fedha

ya mwisho wa mwaka inaandaliwa na kukaguliwa ndani ya

miezi mitatu baada ya mwaka wa fedha.

(4) Taarifa ya fedha itajumuisha- (a) taarifa ya utendaji wa fedha; (b) taarifa ya hali ya fedha; (c) taarifa ya mtiririko wa fedha; (d) taarifa ya mabadiliko ya hisa; na (e) tangazo la taarifa ya fedha.

Uwasilishaji

wa tarifa ya

mwaka

33.-(1) Mkurugenzi Mkuu atawasilisha kwa Waziri

taarifa ya fedha iliyokaguliwa pamoja na taarifa ya Mkaguzi

wa Mahesabu hayo miezi mitatu baada ya mwisho wa mwaka

wa fedha wa kila mwaka.

(2) Mkurugenzi Mkuu atatayarisha na kuwasilisha

Page 23: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

23

kwenye bodi makadirio ya mapato na matumizi ya wakala

miezi mitatu kabla ya mwisho wa mwaka unaoisha.

(3) Hakuna matumizi yatakayofanywa ndani ya

makadirio ya mwaka wa fedha kutoka katika fedha za Wakala

isipokuwa kama itaidhinishwa na Mkurugenzi .

Usimamizi

na

uthibitisho

wa fedha

34.-(1) Wakala itatunza vitabu vya mahesabu na

kuweka kumbukumbu za shughuli zake kulingana na viwango

vya mahesabu ya Kitaifa.

(2) Wakala atasababisha kutayarisha na kutunza vizuri

vitabu vya mahesabu na kumbukumbu kufuata na- (a) rasilimali na madeni; (b) mapato na matumizi ya fedha na Ankara nyingine

za fedha; (c) taarifa ya hali ya fedha na taarifa inayoonyesha

maelezo ya utendaji wa fedha utakaotayarishwa

kila mwaka wa fedha;

(3) Feha na rasilimali za Wakala zitatumika kwa ajili

ya utekelezaji mzuri wa malengo ya sheria hii.

(4) Matumizi ya Wakala yatakuwa kwa mujibu wa

usimamizi wa kupitiwa. Bajeti ya

mwaka na ya

nyongeza

35.-(1) Bodi itaidhinisha bajeti ya mwaka ya kiasi

kinachotarajiwa kupokelewa na kulipwa kwa kipindi cha

mwaka huo wa fedha, si chini ya mwezi mmoja kabla ya

kuanza kwa mwaka wa fedha wowote.

(2) Pale ambapo katika mwaka wowote wa fedha,

Wakala inataka kufanya malipo yoyote ambayo

hayakutolewa au kiasi chochote kinachozidi kiasi ambacho

kiliwekwa katika bajeti ya mwaka huo, Bodi itaidhinisha

bajeti ya nyongeza inayoelezea malipo hayo.

(3) Bajeti ya Mwaka na kila bajeti ya nyongeza

itakuwa katika fomu na itajumuisha maelezo kama

Page 24: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

24

yatakavyotakiwa na sheria.

Kauni za

uendeshaji 36. Wakala-

(a) itafungua na kuendesha vitabu vyote vya

mahesabu, leja, jarada na vitabu vingine vya

mahesabu kufuatana na kitabu cha mwongozo wa

mahesabu; (b) itapitia na kubadili hati kwa ajili ya kurejesha

uwekaji mzuri wa vitabu vya mahesabu kama

itakavyoelekezwa na mamlaka husika.

Uwezo wa

kuwekeza 37. Wakala inaweza kwa idhini ya Waziri mwenye

dhamana ya mambo ya fedha, kuwekeza fedha yoyote katika

namna ambayo itaona inafaa.

SEHEMU YA TISA

MAKOSA NA ADHABU

Makosa na

adhabu 38. Mtu ambaye-

(a) anachelewesha au kumzuia afisa yeyote

kutekeleza kazi zake chini ya Sheria hii. (b) anakataa kumpa afisa yeyote msaada unaofaa

kama atakavyoombwa na afisa kwa

madhumuni ya kutekeleza kazi zake chini ya

sheria hii. (c) anatoa taarifa za uongo na huku anajua

kwamba si za kweli, anatenda kosa na akitiwa

htiani atalipa adhabu ya fehda zisizopungua

shilingi milioni moja au kifungo kwa kipindi

kisichozidi miaka miwili au vyote viwili.

Makosa na

bodi

shirikishi

39. Pale kosa linapokuwa linatendeka na bodi

shirikishi au shirika, mtu yeyote ambaye wakati kosa hilo

linatendwa alihusika na usimamizi wa bodi shirikishi hiyo au

shirika atachukuliwa kuwa amefanya kosa hilo yeye.

Page 25: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

25

SEHEMU YA KUMI

MASHARTI YA MCHANGANYIKO

Jukwaa la

Usimamizi

wa maafa

40.-(1) Kutokana na Jukwaa la Taifa la usimamizi wa

maafa ambalo litatoa nafasi ya wadau kukutana na kujadili

mambo yanayohusu usimamizi wa maafa na kuishauri Serikali

kikamilifu.

(2) Jukwaa litaundwa na- (a) Mkurugenzi Mkuu ambaye atakuwa ni

mwenyekiti; (b) Wakuu wa Idara yenye dhamana na usimamizi wa

maafa kutoka: (i) Wizara yenye dhamana ya Kilimo na

Chakula; (ii) Wizara yenye dhamana ya Mambo ya

Ndani ; (iii) Wizara yenye dhamana ya Fedha; (iv) Wizara yenye dhamana ya Serikali za

Mitaa; (v) Wizara yenye dhamana ya Afya na Ustawi

wa Jamii; (vi) Wizara yenye dhamana ya Mazingira (vii) Wizara yenye dhamana ya Madini; (viii) Wizara yenye dhamana ya Mawasiliano; (ix) Wizara yenye dhamana ya Ardhi na

Nyumba; (x) Wizara yenye dhamana ya Usafiri; na (xi) `Wizara yenye dhamana ya nguvu za

atomu. (c) Wakuu wa taasisi zifuatazo: (i) Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano

Tanzania; (ii) Kikosi cha zimamoto; (iii) wakala wa taifa wa akiba ya chakula;

(iv) kituo cha chakula na Lishe Tanzania; (v) upimaji wa jeologia Tanzania; (vi) mamlaka ya chakula na dawa.

Page 26: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

26

(d) mwakilishi wa wakala wa Hali ya hewa; (e) watu wanne wanaowakilisha Vyuo vya Elimu ya

Juu; (f) mwakilishi wa Jeshi la Wananchi; (g) mwakilishi wa taasisi ya dhamana na mipango ya

Taifa; (h) wawakilishi watatu kutoka Jumuiya ya Taasisi ya

Vyama vya kiraia; (i) wawakilishi watatu kutoka taasisi za dini;

(2) Jukwaa linaweza kumualika mtu mwingine

yeyote kama itakuwa ni lazima.

(3) Jukwaa litakutana mara mbili kwa mwaka lakini

linaweza kukutana wakati mwingine wowote kama kutakuwa

na suala ambalo linahitaji kujadiliwa haraka.

(4) Jukwaa litaweka taratibu zake lenyewe.

(5) Jukwaa laweza kuunda kamati ambazo wajumbe

wake watateuliwa kutoka miongoni mwao.

Kinga dhidi

ya mashtaka 41.-(1) Mwajiriwa yeyote wa Wakala hatashtakiwa

binafsi kwa jambo lolote alilolitenda au kuacha kutenda kwa

nia njema akitekeleza au kuchukuliwa kutotekeleza kazi

yoyote akiwa kama mwajiriwa wa wakala.

(2) Wakala itamlipa na kumrudishia kwa kiwango

cha namna kama itakavyoelezwa mtu anayejitolea na mtu

mwingine aliyeshughulika na usimamizi wa maafa gharama

za msingi alizoingia ikiwa ni matokeo ya- (a) kutekeleza mwitikio wa kutoa huduma za maafa

kwa mujibu wa sheria hii; (b) kupatikana kwa ajali ya maafa, ardhi , yoyote au

vituo.

Kanuni 42. Waziri atatunga Kanuni kuhusu jambo lolote

ambalo ni la lazima kwa madhumuni ya utekelezaji au wa

kuipa nguvu ya utekelezaji wa sheria hii.

Page 27: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

27

Kufuta na

kubakiza

Sura 242

43.-(1) Sheria ya Uratibu wa Maafa inafutwa.

(2) Bila kujali kufutwa kwa sheria ya maafa, kanuni

zozote, amri, mashtaka au matangazo ya serikali yaliyofanywa

chini ya Sheria ya Maafa na ambayo bado yatakuwa na nguvu

kabla ya sheria hii kuanza kutumika yatabakia kuwa na nguvu

kama yametengenezwa chini ya sheria hii.

______

JEDWALI

______

(Imetengenezwa chini ya kifungu cha 7(4))

_________

UTARATIBU WA MIKUTANO YA BARAZA NA MAMBO

MENGINE

Mikutano 1.-(1) Baraza litakutana kwa kufanya shughuli zake

katika muda na sehemu itakayoamuliwa na Baraza.

(2) Mikutano ya kawaida ya Baraza itafanyika mara

moja kwa kila miezi mitatu.

(3) Mwenyekiti au ikiwa kama hauyupo Makamu

Mwenyekiti anaweza katika wakati wowote kuitisha kikao cha

dharura cha Baraza, baada ya kupokea ombi la kimaandishi

kutoka kwa wajumbe wengi wa Baraza.

(4) Mwenyekiti au kama hayupo, Makamu

mwenyekiti ataongoza mikutano ya Baraza.

(5) Mwenyekiti au kama hayupo, Makamu

Mwenyekiti anaweza kumwalika mtu mwingine ambaye si

mjumbe kuhudhuria mkutano wowote wa kamati isipokuwa

kupiga kura.

Akidi 2. Akidi ya mkutano wowote wa Baraza itakuwa ni

nusu ya wajumbe wa Baraza.

Page 28: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

28

Uamuzi wa

Baraza 3.-(1) Swali linaloletwa katika Baraza litaamuliwa kwa

wingi wa kura za wajumbe waliohudhuria wakati wa upigaji

kura na kama kura zitakuwa sawa, mtu anayeongoza kikao

atakuwa na kura ya uamuzi.

(2) Bila kujali kifungu kidogo cha (1), uamuzi wa

Baraza unaweza kufanywa bila ya Mkutano kwa njia ya

mzunguko wa hati husika miongoni mwa wajumbe na

mwelekeo wa maandishi wa maoni ya wengi ya wajumbe ndio

utakaokuwa uamuzi wa wengi.

Kumbukumb

u za kikao 4.-(1) Baraza litasababisha kumbukumbu za mkutano

kuwekwa na kutunzwa na kumbukumbu zitatumiwa au

kurekebishwa na kuidhinishwa katika mkutano wa Baraza na

kusainiwa na mtu anayeongoza kikao.

(2) Kumbukumbu zilizosainiwa na mtu aliyeongoza

kikao cha Baraza kwa uthibitisho wa kutokuwepo kwa

makosa, zitachukulliwa kuwa kumbukumbu sahihi za kikao.

Kutokuhudh

uria

hakutaharami

sha kikao

5. Uhalali wa kikao au jambo lolote la Baraza

halitaathiriwa kwa sababu ya kutokuwepo kwa mmoja kati ya

wajumbe au kosa lolote la uteuzi wa mmoja wao.

Amri,

maelekezo,

matangazo

au hati

6. Amri, maelekezo, matangazo au hati

zilizotengenezwa au kutolewa kwa niaba ya Baraza

zitasainiwa na-

(a) Mwenyekiti au Mkurugenzi Mkuu au Ofisa

mwingine yeyote wa Wakala aliyeidhihishwa kwa

niaba ya Mkurugenzi Mkuu.

Lakili ya

Baraza 7. Lakili ya Baraza na itawekwa kwenye hati yoyote

isipokuwa mbele ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti au

Mkurugenzi Mkuu. Baraza

kuweka

taratibu zake

8. Kulingana na masharti ya Jedwali hili, Baraza

linaweza kuweka namna ya kuendesha taratibu zake.

Page 29: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

29

MADHUMUNI NA SABABU

______________

Muswada huu unapendekezwa kutungwa kwa Sheria ya Usimamizi

wa Maafa ya Mwaka, 2014.

Madhumuni ya Muswada huu ni kuzuia, Kujiandaa na kukabiliana

na maafa kwa madhumuni ya kuanzisha Wakala inayojitegemea ya

Menejimenti ya Maafa itakayokuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Ofisi

ya Waziri Mkuu itakuwa ni kituo cha kuratibu menejimenti na usimamizi

wa maafa kati ya wadau na asasi mbalimbali zinazuhusiana na maafa.

Muswada unakusudia kuwaweka pamoja wadau wote wanaohusika na

masuala ya kuratibu,kuzuia, kujiandaa, kusimamia na kukabili maafa.

Muswada umegawanyika katika sehemu kuu Tisa. Sehemu ya

Kwanza ya Muswada inahusu mambo ya utangulizi, kama vile jina fupi la

Sheria, matumizi na tafsiri ya maneno mbalimbali yaliyotumika katika

Muswada.

Sehemu ya Pili ya Muswada inahusu uanzishwaji wa Wakala

inayojitegemea ya Menejimenti ya Maafa. Ofisi ya Waziri Mkuu

itasimamia Wakala, na itakuwa ni kituo cha kuratibu, kuzuia na

kusimamia masuala yatokanayo na maafa. Wakala utakuwa na Baraza

litakaloratibu na kumeneji kazi na masuala yote yatokanayo na maafa.

Sehemu ya Tatu ya Muswada inahusu mambo ya kiutawala ya

Wakala,inapendekezwa chini ya Sehemu hii kuteuliwa kwa Mkurugenzi

Mkuu atakayateuliwa na Mheshimiwa Rais. Ndani ya Sehemu hii

inapendekezwa kuanzishwa kwa Kamati za Kuratibu Masuala ya Maafa ya

Mikoa, Wilaya, Kata na Vijiji. Muudo na kazi za Kamati pia zimeainishwa

chini ya Sehemu hii. Miogozo ya Kamati, jinsi ya kuratibu shughuli za

kamati zimeainishwa na namna Kamati zitakavyotoa taarifa zake pia

zimeaanishwa.

Sehemu ya Nne ya Muswada inaainisha masuala ya usimamizi wa

haki za watu watakao athirika na maafa. Inapendekezwa ndani ya Muswada

kuwa Serikali ihusike au Wakala uhusishwe kwa ajili ya kutoa misaada

kwa wananchi mara yatokeapo maafa. Zaidi ya Serikali kutoa misaada pia

Page 30: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

30

wananchi wawe na jukumu la kuzuia, kujiandaa kumeneji na kukabili

maafa.

Sehemu ya Tano ya Muswada inapendekeza kuwepo na namna ya

kutoa tamko na ufafanuzi wa kazi zitakazohusika ama kufuatwa wakati

yatakapotokea maafa. Muswada pia unapendekezwa kuwepo na tamko la

kuteua au kutangaza sehemu iliyoadhirika na maafa, sababu ya kuitangaza

sehemu hiyo na mambo ya muhimu yatakayobidi yafanyike katika sehemu

yalipotokea maafa.

Sehemu pia inapendekeza kuwa Wakala waweze kutoa Tangazo

katika vyombo vya habari na katika Gazeti la Serikali iwapo Wakala

utaridhika kuwa kumetokea maafa ambayo yanapaswa yapewe kipaumbele.

Sehemu ya Sita inapendekaza kuwepo na utaratibu wa kuratibu,

kusimamia na kuandaa Mwongozo wa Taifa wa Kumeneji Maafa chini ya

usimamizi wa Wakala na hatimaye kupitishwa na Waziri.

Sehemu hii pia inapendekeza kuwa Serikali za Mitaa ziwe na

jukumu la kusaidia kutekeleza Mpango wa Taifa wa kuzuia, kujiandaa na

kukabili maafa. Muswada pia unapendekeza asasi za kiserikali na zisizo za

kiserikali kuandaa Mipango yao ya kukabiliana na masuala ya maafa ili

kuweza kutekeleza majukumu yao kama ilivyoainishwa ndani ya Mpango

wa isimamizi,uzuiaji na kukabili maafa.

Sehemu ya Saba ya Muswada inapendekeza kuanzishwa kwa Mfuko

wa Kumeneji na kusimamia Maafa. Mfuko huu utakuwa chini ya

usimammizi wa Wakala; pia Sehemu hii imeainisha matumizi ya fedha,

usimamizi na ukaguzi wa matumizi ya fedha.

Sehemu ya Nane inaainisha makosa na adhabu mbalimbali ambayo

pia yanahusu makosa yanayofanywa na mashirika.

Sehemu ya Tisa inahusu mambo ama masharti ya ujumla ambayo

yanahusu kuwepo kwa Jukwaa la Taifa la Kumeneji na Kusimamnia Maafa,

inazuia ama kusimamia iwapo kutatokea kitu chochote kitakachofanyika,

tendwa ama kutotendwa kwa nia njema ama kutodhamiriwa , kuondoa

masuala ya kodi wakati wa maafa. Sehemu hii inaongelea jinsi ya

kusimamia wataalamu wa kimataifa wanaokuja kusaidia wakati wa maafa,

majukumu ya Tawala za Mikoa na Wilaya na mambo yanayohusu fidia.

Page 31: SHERIA YA WAKALA WA USIMAMIZI WA MAAFA, 2014 … · maelewano, hati na kutekeleza mipangilio mingine; (c) kumiliki mali inayohamishika na isiyohamishika; na (d) kuwa na muhuri wake

Sheria ya Wakala wa Usimamizi wa Maafa

31

Muswada, pia katika Sehemu hii unapendekeza masharti ya

kufuatwa wakati wa kutoa fidia iwapo kutatokea hasara au kuharibika kwa

vitu,utoajii wa fidia, kisasi na malipo. Muswada pia unapendekeza uwezo

wa Waziri wa kutengeneza Sheria ndogo kuhusiana na mambo ya Sheria

hii. Mwisho, Muswada unapendekeza kufutwa kwa Sheria ya Maafa na

Uratibu wa Misaada Sura 242 (Disaster Relief Coordination Act (Cap. 242).

Dar es Salaam, MIZENGO P. PINDA

10 Oktoba, 2014 Waziri Mkuu