Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

Embed Size (px)

Citation preview

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    1/21

    | Zanzibar Daima Online | Toleo Nambari 07 | Novemba 2013 - Disemba 2013 | Toleo la bure

    ONLINE

    ZANZIBAR DAIMAUMOJA

    WAKITA

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    2/21

    A

    2 Zanzibar Daima OnlineTAHARIRI

    Ahmed Rajab

    Ni Uungwana kumpa mtu haki

    yake. Katika toleo hili tuna maka-la yenye kumpa haki yake Rais Ali Mo-

    hamed Shein kwa msimamo wake wa

    kuitetea Serikali ya Umoja wa Kitaifa

    (SUK) na kumkinga Makamu wake wa

    Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif

    Hamadi, ambaye pia ni Katibu Mkuu

    wa Chama cha Wananchi (CUF).

    Si siri kwamba kuna baadhi ya Wa-

    zanzibari ambao kila siku, usiku na

    mchana, wanakula njama za kuihu-

    jumu SUK. Wanaitwa wahafidhina

    kwa sababu hawana siasa za kileo, za

    kimaendeleo. Hawataki Serikali hiyo

    ifanikiwe. Kwa hakika, hawataki Se-rikali hiyo iendelee kuishi. Wanataka

    ife, leo kesho.

    Wanaiombea Serikali hiyo mauti kwa

    sababu wanaelewa vilivyo nini kina-

    choweza kutokea Serikali hiyo ikifa au

    hata ikisambaratika tu.

    Wanachotaka wahafidhina hao, am-

    bao ni wachache sana katika jamii

    yetu, ni kuirejesha Zanzibar kule ili-

    kotoka na tusikotaka kurudi. Wa-

    nachotaka wao ni kuiona Zanzibar

    ina machafuko, michirizi ya damu na

    uhasama utaovifanya visiwa vyetuvisikalike. Hali hiyo ndiyo wanayoililia,

    ndiyo wanayoitilia ubani irudi, tena

    kwa haraka sana.

    Hawataki kuiona Zanzibar yenye utu-

    livu na amani hali ambazo ni mu-

    himu kwa maendeleo. Hakuna taifa

    linaloweza kuendelea ikiwa halina

    utengamano, utulivu na hali ya amani.

    Wahafidhina hao wachache, ambao

    hatuchoki kuwaombea dua Mungu

    awahidi, wana silaha kadhaa wana-

    zozitumia ili kulifanikisha lengo lao.Silaha yao kubwa ni fitna. Kwanza

    wanataka kuwafitinisha wabia kati-

    ka SUK. Na wanaanza hukohuko juu

    kuwagonganisha vichwa wakubwa

    wa Serikali hiyo. Mishale yao ya fitna

    wamekuwa wakiilenga kwa Maalim

    Seif. Wanav yo ona wao ni kwamba ni

    wao waliomweka Maalim Seif katika

    kiti cha umakamu wa Rais.

    Wanachosahau au wasichokijua ni

    kwamba hii si Serikali iliyo mali yao.

    Ni Serikali ya Wazanzibari wote.

    Wala hii si Serikali inayoundwa nachama kimoja. Ni Serikali iliyoundwa

    na vyama vyote viwili vikuu vilivy-

    ochuana katika uchaguzi mkuu uliopi-

    ta. Hivyo ndivyo Katiba ya Zanzibar

    isemavyo baada ya kura ya maoni ya

    2010 iliyoidhinisha kwa asilimia ku-

    bwa uundwaji wa Serikali aina hiyo.

    Mchezo walioupanga ni kumpaka

    matope Maalim Seif na kumfitinisha

    na Rais wake.

    Matamshi ya Rais Shein alipozun-

    gumza na waandishi wa habari hivi

    majuzi yalikuwa na lengo la kuukatahuo mzizi wa fitna. Kwa hilo hatuna

    budi ila kumpa heko Rais Shein. Tu-

    nampa heko huku tukimsihi aendelee

    kuwa na ujasiri wa kuushika uzi hu-

    ohuo.

    Wanaitumia pia fitna kujaribu kutu-

    fitinisha sisi Wazanzibari wa kawa-

    ida na kujaribu kutugawa baina ya

    Wapemba na Waunguja. Watafurahi

    wakituona tunapofoana macho na

    kuchinjana.

    Silaha nyingine inayotumiwa na hao

    wanaojikakamua kutuletea balaani kuzipanda na kuzipalili mbegu za

    chuki. Hawakuanza jana. Walianza

    na chuki za kikabila. Sasa wameka-

    mia kupalilia chuki kati ya Pemba na

    Unguja ikiwa ni sehemu ya mkakati

    wao niliokwishautaja wa kutugawa.

    Bahati nzuri hakuna Mzanzibari mwe-

    nye akili yake timamu anayewasikili-

    za na kuwatia maanani wanapozun-

    gumzia juu ya kuzitenganisha Pemba

    na Unguja. Wengi wa Wazanzibari

    wanawaona hawa wahafidhina kuwa

    ni muflis wa kisiasa. Hawana lao jam-

    bo. Na wenyewe wanajijuwa na ndiomaana wanatapatapa.

    Silaha yao ya tatu ni kutumia vitisho.

    Wanajaribu kumtisha kila mtu waki-

    sahau kwamba enzi za kutishana zi-

    mekwisha zamani Zanzibar. Hii tuliyo

    nayo ni enzi ya siasa mpya na mwele-

    keo mpya.

    Hatusemi kwamba siasa zetu ni safi

    safina wala hatusemi kwamba Se-

    rikali tuliyo nayo imekamilika. La-

    kini tunachosema na kukitambua ni

    kwamba Wazanzibari kwa wingi wetu

    tumeamua kuwa wamoja, kuziachasiasa za kutugawa na za kuturudisha

    nyuma. Tunachotaka ni maendeleo na

    ufanisi wetu sote bila ya kujali, kabila,

    dini, itikadi za kisiasa au kisiwa gani

    au kijiji gani tumetoka.

    Inavyoonyesha ni kwamba Rais She-

    in naye pia anayatambua haya na

    ndio maana aliyasema aliyoyasema

    alipokutana majuzi na waandishi wa

    habari

    Shein anatambua

    tulikotoka na tuendako4

    9

    12

    14

    18

    22

    26

    30

    34

    HABARI KUUShein awaangusha Wahafidhina.

    NIONAVYO

    Uroho wa Wanasiasa kujitajirisha.

    NGURUMO LA MKAMA NDUMEDonge na Pemba ni moja na zitabaki hivyo.

    MKEKA WA MWANA WA MWANAKama Zanzibar haiwezi kuchangia serikali Tatu,

    Bara inachangiaje kwenye Serikali Mbili.

    KAULI YA MWINYI MKUU

    Shein astahili kuitwa Rais wa busara.

    TUFUNGUE KITABUVuta nkuvute, kielelezo cha uandishi wa Kizanzibari

    WARAKA KUTOKA BONNWazanzibari tujipange, mafuta yasije yakawa nuksi

    kwetu.

    BARZA YA JUMBA MARO

    Dk. Mvungi ameikosa treni ya mwisho, ila tuko nae.

    HEKAYA ZA ZANZIBARHadithi fupi ya meza fupa ya Ally Hilal.

    Zanzibar DaimaOnline

    YaliyomoMHARIRI MKUU

    Ahmed RajabEmail: [email protected]

    MHARIRI MSAIDIZIMohammed Ghassani

    Email: [email protected]

    MHARIRI MSANIFUHassan M Khamis

    Email: [email protected]

    MSIMAMIZI WA MAWASILIANOHassan M Khamis

    WAANDISHIJabir Idrissa

    Email: [email protected]

    Othman MirajiEmail: [email protected]

    Hamza RijalEmail: [email protected]

    Mohamed AbdulrahmanEmail: [email protected]

    Ally SalehEmail: a [email protected]

    WASAMBAZAJImzalendo.net

    zanzibardaima.netzanzibardaima/facebook

    MATANGAZOHassan M Khamis

    Simu: +44 7588550153Email: [email protected]

    WASIALIANA [email protected]

    JARIDA HILI HUCHAPISHWA NAZanzibar Daima Collective

    233 Convent WaySouthallUB2 5UH

    Nonnstr. 2553119 Bonn

    Germany

    www.zanzibardaima.net

    Timu Yetu

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    3/21

    PAGINATION 15

    Zanzibar Daima Online4 Zanzibar Daima Online 5Zanzibar Daima Online

    Zanzibar Daima Online

    HABARI KUU

    SHEIN AWAANGUSHA

    WAHAFIDHINA

    Wahafidhina ndani ya Chama

    Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar

    wameangushwa puuu.

    Haya yalitokea pale Rais wa Zanzibar naMwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.

    Ali Mohamed Shein, alipofanikiwa kuihami

    serikali anayoongoza ya Umoja wa Kitaifa

    dhidi ya njama zenye lengo la kuisambara-

    tisha.

    Dk. Shein katika hali iliyoonesha kuwa

    anajua mitego ya siasa, alijibu kwa ufasa-

    ha alipoulizwa anamchukulia vipi Makamu

    wake wa Kwanza Maalim Seif Shariff Ham-

    ad ambaye amekuwa akitoa kauli nzito

    zilizoashiria kama ndio msimamo wa Seri-

    kali kuhusu upatikanaji wa Katiba ya Muun-

    gano Tanzania.

    Suala hili limekuwa likitajwa mara kwa

    mara na wahafidhina wakiwemo viongozi

    wa Umoja wa Vijana wa CCM, kama uth-

    ibitisho wa Maalim Seif kukiuka utaratibu

    na walimtaka Rais amchukulie hatua kali za

    kinidhamu.

    Lakini Dk. Shein, mzaliwa wa Mkanyageni,Mkoa wa Kusini Pemba, alimhami Maalim

    Seif kwa kusema kuwa kiongozi huyo ame-

    kuwa akieleza msimamo wake binafsi kati-

    ka suala hilo wala si msimamo wa Serikali

    anayoiongoza.

    Dk. Shein ambaye aliingia madarakani No-

    vemba 3, 2010, alisema yeye na mawa-

    ziri wake wanafanya kazi kwa pamoja na

    kwa kuvumiliana ambapo kila linalofany-

    wa na Serikali wanaliamua kwa pamoja na

    wanafanya kazi kwa mshikamano mkub-

    wa tofauti na ilivyotokea katika nchi nyingi

    zilizounda Serikali kwa mfumo wa Serikali

    ya Umoja wa Kitaifa.

    Nchi zilizounda serikali ya mfumo huo kwa

    Afrika ni pamoja na Zimbabwe ambako

    ZANU-PF cha Robert Mugabe kimeunda

    Serikali pamoja na Chama cha Movement

    for Democratic Change (MDC) cha Morgan

    Tsvangirai na Kenya ambako serikali hiyo il-

    iundwa kama njia ya kuleta amani baada ya

    machafuko ya uchaguzi mkuu wa Desemba

    2007. Rais Mwai Kibaki ambaye amestaafu,aliunda Serikali ya ubia pamoja na Muunga-

    no wa Upinzani chini ya Raila Odinga.

    Dk. Shein anaongoza Serikali ya ushirikiano

    yenye mawaziri kutoka chama chake cha

    CCM na Chama cha Wananchi (CUF) vilivyo-

    pata kura za wananchi siku ya uchaguzi Ok-

    toba 31, 2010.

    Alisema Serikali hiyo inafanya kazi vizuri li-

    cha ya changamoto nyingi zinazoisibu; laki-

    ni amesema kuwa mambo yanakuwa rahisi

    kwa vile wanashauriana kwa pamoja bila ya

    kujali itikadi za vyama vyao vya siasa vilivy-

    owaingiza uongozini.

    Dk. Shein alionesha ujasiri kiuongozi kwa

    kumkingia kifua Maalim Seif Sharif Ham-

    ad hata pale alipoulizwa atachukua hatua

    gani dhidi ya kilichoelezwa kama kauli za

    Makamu wake wa kwanza zinazoashiria

    kuisemea serikali kuhusu msimamo wake

    Na Jabir Idrissa Zanzibar

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    4/21

    DONATE FOR PEMBA

    A brief reminder about the Pemba Foundations crowdfunding campaign to introduce new cash

    crops to the impoverished Zanzibar island of Pemba. We had a good start but are stuck at $1,225

    -- only 11% of the goal, with 55 days left.

    For those who have already contributed -- thanks again, and please pass along the link to friends

    who might be interested.

    For those who would like to contribute but havent got to it yet, please click on the link to the Indie-

    gogo campaign page and then click on Contribute Now. Donations are by credit card in dollars, but

    UK or other cards work. Your donation will be matched one-for one, so it will be worth double.

    Donations are tax deductible in the US. You will be able to give anonymously if you wish.

    Here is the link to the campaign page:

    http://www.indiegogo.com/projects/a-passion-for-fruit

    Many thanks.

    John Angier

    6

    6 Zanzibar Daima Online 7

    HABARI KUUZanzibar Daima Online

    katika suala la upatikanaji wa katiba mpya

    ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Alisema ni yeye tu mwenye wajibu wa

    kikatiba kuisemea Serikali katika suala hilo;

    wengine watachofanya ni kutoa misimamo

    yao binafsi.Hakuna kiongozi yeyote wa kutoa msima-

    mo wa Serikali isipokuwa mimi mwenyewe

    Rais. Makamu wangu wote watatoa mi-

    simamo yao kama viongozi binafsi katika

    vyama vyao. Sina tatizo la kauli za Maalim

    Seif; najua yeye ana haki ya kutoa msimamo

    wake binafsi. Na mimi pia ninayo haki kama

    hiyo. Lakini mimi ni Rais ndiye nitakayetoa

    msimamo, sijafanya hivyo, alisema akijibu

    swali lililoulizwa na mwandishi wa habari wa

    gazeti la Zanzibar Leo, Mwantanga Ame.

    Kumekuwa na shinikizo ndani ya CCM kum-

    taka Rais Shein amchukulie hatua kali Maal-

    im Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF,

    kutokana na kile wanachodai wahafidhina

    kuwa kutoa kauli za kuisemea Serikali huku

    akimzidi mamlaka Makamu wa Pili, Balozi

    Seif Ali Iddi, ambaye ndiye kiongozi wa Seri-

    kali katika Baraza la Wawakilishi.

    Wahafidhina wakiwemo viongozi waandam-

    izi ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM (UV-

    CCM) wamekuwa wakimsukuma Rais wa

    Zanzibar amfukuze kazi Maalim Seif kwa

    kumtuhumu kuwa amekuwa akimtii zaidi

    Rais Mstaafu Amani Abeid Karume kuliko

    Rais aliyemteua.

    Maalim Seif aliteuliwa na Dk. Shein kwa

    mujibu wa Katiba ya Zanzibar iliyofanyiwa

    marekebisho makubwa mwaka 2010, kabla

    ya uchaguzi mkuu, kwa kujumuishwa ibara

    zinazoweka wadhifa wa Makamu wawili wa

    Rais kama wasaidizi wakuu wa Rais.

    Mabadiliko hayo yaliidhinishwa katika mpan-

    go mpana wa kuruhusu kuundwa kwa Seri-

    kali ya Umoja wa Kitaifa baada ya uchagu-

    zi, mpango uliowezeshwa na maafikiano ya

    kujenga siasa za Maridhiano Zanzibar yal-

    iyofikiwa na Maalim Seif na Amani Karume

    alipokuwa rais.

    Hatua hiyo ya Maridhiano waliifikia baada ya

    kufanya majadiliano ya faragha tangu mwa-

    ka 2009 kutokana na mpango ulioasisiwa na

    Mzee Hassan Nassor Moyo akisaidiwa na

    ile inayoitwa Kamati ya Maridhiano inayoju-

    muisha makada watatu wa CCM na viongozi

    waandamizi watatu wa CUF.

    Serikali ya Umoja wa Kitaifa ambayo ni pigo

    kubwa kwa wana-CCM wasiopenda mabadi-

    liko, imekuwa ikikabiliana na majaribio mengi

    ya kuisambaratisha.

    Wahafidhina wamekuwa wakichochea vuru-

    gu kwa kuzuia demokrasia kuenea huku

    wakimtukana Maalim Seif hadharani kupi-

    tia maandishi kwenye mbao za maskani

    ya Muembekisonge na Kachorora. Matusi

    mengine hutolewa kwenye majukwaa ya

    mikutano ya hadhara ya chama hicho

    http://http//www.indiegogo.com/projects/a-passion-for-fruithttp://http//www.indiegogo.com/projects/a-passion-for-fruit
  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    5/21

    9Zanzibar Daima Online

    NIONAVYO

    Na Mohamed Abdulrahman Nionavyo

    Uroho wa wanasiasa kujitajirisha

    Rais Jose Albarto Mujica

    Cardano wa Uruguay

    Ukisema kama kuna nchi yenye Rais maskini duniani kuna watakaoangalia kwa jicho la

    sadiki ukipenda, kuwa ni porojo tu na si wengi watakaokuamini. Sidhani kutokuamini

    kwao kunatokana na dhana ya kuwa haiwezekani , lakini si katika wakati huu tulionao

    ,kwani uongozi umegeuka na kuwa jukwaa la kujitajirisha badala ya utumishi kwa umma. Hata

    hivyo kweli ni kwamba kiongozi wa aina hiyo yupo. Naye ni Jose Alberto Mujica Cordano (ana-

    tamkwa kihispania - Khose Mukhika), Rais wa Uruguay.

    Mujica mwenye umri wa miaka 78 ,alishinda uchaguzi 2009 na akaingia madarakani Machi 1,

    2010. Bwana huyo mpiganaji wa zamani wakati wa vita vya chini kwa chini dhidi ya utawala wa

    kidikteta ,aliyejeruhiwa kwa risasi, kufungwa , kuteswa na polisi na kuwekwa gerezani kwa mia-

    ka 14 , kabla ya kuteuliwa waziri katika serikali ya muungano wa vyama vya mrengo wa kushoto

    (2005-2008), hutoa asilimia 90 ya mshahara wa urais , dola za Marekani 12,000, kila mwezi kwa

    jumuiya za misaada kuwasaidia masikini na wajasiri amali.

    Anaishi katika nyumba yake mwenyewe kwenye kiunga kimoja cha mji mkuu Montevideo. Gari

    anayoendesha ni aina ya Volkswagen Beatle ya miaka ya 1960 na wala hana walinzi. Nivmtu wa

    ajabu anayewashangaza wengi katika ulimwengu wa Leo. Nasema katika ulimwengu wa leo kwa

    sababu, kuna viongozi wal-

    iotekeleza alau sehemu ya

    walichohubiri na hasa kuhu-

    siana na hili la kujitajirisha

    wakitarajia watakaowafuata

    baadaye wataendelea kuwa

    ni dira kwa jamii. (Mfano

    mmoja Mwalimu JuliusNyerere aliyeondoka madar-

    akani baada ya miaka 27 bila

    ya yeyote kuthubutu kum-

    nyooshea kidole kwamba al-

    itumia madaraka yake kuji-

    tajirisha).

    Leo hii mambo ni mengine.

    Mbunge anaweza kuwa ta-

    jiri katika kipindi cha miakamitano tu. Hugombea ubu-

    nge kwa malengo ya ku-

    jinufaisha binafsi na badala

    ya bunge kuwa chombo ki-

    kuu cha uwakilishi wa umma

    limegeuka kuwa mahala pa

    kula.

    Ubinafsi Umetawala

    Kinachokirihisha ni pale

    wabunge na wawakilishi

    wanapokuwa na moyo wa

    kulalamika hadharani kuwa

    mishahara yao haitoshi na

    wanataka waongezewe. La

    kukirihisha zaidi ni pale vi-

    ongozi wa juu wanapokaa

    kimya na kushindwa ku-

    wakemea mabwana wakub-

    wa.

    Hivi karibuni kumeibuka ma-

    dai ya wabunge kuwa msha-

    hara hautoshi. Sambamba na

    madai hayo ni zumari lililop-ulizwa na Spika wa bunge

    la Muungano Anna Makinda

    kuyaunga mkono madai hayo

    . Akitoa mfano alisema yeye

    binafsi amewahi kuende-

    wa na wabunge watatu wa

    zamani wakiomba msaada

    kwa vile hali zao ni mbaya.

    Ingawa hakutaja kiwangocha mishahara ya wabunge,

    Makinda amegusia posho ya

    vikao Shilingi 330,000 kwa

    siku, Shilingi 30,000,000 za

    shughuli za jimbo na Shilingi

    72,000,000/= zikiwa kiinua

    mgogo mbunge anapomal-

    iza miaka 5.

    Makinda amedai wabunge

    wengi wanashindwa kukidhi

    mahitaji yao katika mazingira

    yaliopo sasa .

    Spika amesema wabunge

    wengi wanajuta kuwan-

    ia ubunge na wangetam-

    ani kurejea katika taaluma

    zao. Sijui kama taaluma

    hizo zingewapa marupuru-

    pu na fedha wanazojikingia.

    Kiroja cha mambo madak-

    tari wamekuwa wakivutana

    na serikali kuhusu misha-

    hara na mazingira yao ka-

    zini. Matatizo yao mpaka leo

    hayajapatiwa suluhuhisho lakudumu.

    Spika Makinda hajanis-

    hangaza, Waswahili wanase-

    ma .Mwamba ngoma hu-

    vutia pande wake, kwani

    marupurupu anayopata yeye

    mwenyewe hayasemeki.

    Wazanzibari hawana tafauti

    Hoja hii inawagusa pia

    wabunge wa Zanzibar ka-

    tika bunge la Muungano na

    hata wajumbe wa Baraza

    la Wawakilishi (BLW) . Hivi

    tunapozingatia na kujiuliza

    kuhusu kiwango cha fed-

    ha anazojikingia mbunge

    wa Zanzibar na mshahara

    wa mfanyakazi wa kawaida

    tunakuwa na majibu gani ?

    Ni wafanyakazi wangapi wa

    serikali wanaoweza kupa-

    ta kiinua mgongo cha kiasi

    hicho baada ya miaka 30 ya

    utumishi, ukilinganisha na

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    6/21

    10 Zanzibar Daima Online

    10

    tija za miaka mitano ya ubu-

    nge ? Wabunge wangapi wal-

    iotumia posho wanaolipwa

    kushughulikia kweli matatizo

    majimboni mwao ?

    Kwa bahati mbaya ugonj-

    wa huu hauko tu miongonimwa wabunge wa chama kin-

    achotawala cha CCM bali hata

    kwa wale wa vyama vya up-

    inzani.

    Sikio la kufa halisikii dawa

    Zanzibar ina serikali ya ubia

    na waliokuwa wapinzani sasa

    nao wamo serikalini. Kwa ba-

    hati mbaya lakini baadhi ya

    waliokuwa wakiyalalamikia

    sasa hayazungumzwi tena.

    Ukihoji unaambiwa Waziri

    anapaswa kuishi kulingana na

    hadhi yake. Je, daktari hap-

    aswi kuishi kulingana na hadhi

    ya taaluma yake ?

    Kwa kumbukumbu zangu ni

    mwakilishi wa Mji mkongwe

    Ismail Jussa peke yake ali-

    yepinga kuongezwa masila-

    hi ya wawakilishi,alipokuwa

    akichangia katika kikao cha

    bajeti ya Serikali ya Mapinduzi

    Zanzibar Juni 18 mwaka huu .

    Lakini sikio la kufa halisikii

    dawa. Mwanzoni mwa mwe-

    zi wa Novemba, ilitangazwa

    kwamba BLW limepandis-

    ha posho ya vikao kutoka

    Sh. 100,000 hadi Sh.150,000

    kuanzia mwaka huu .

    Wananchi wameanza kukata

    tamaa na kutokuwa na ima-

    ni na wanasiasa. Hata hivyo,wao pia wana wajibu mkub-

    wa wa kujiletea mabadiliko.

    Kwanza wanapaswa wata-

    fakari ni kina nani wanaofaa

    kuwawakilisha, kuwapigan-

    ia na kuwaletea maendeleo.

    Kuna matumaini Katiba mpya

    huenda ikawa na kifungu ki-

    takachoruhusu wagombea

    binafsi. Hiyo itakuwa nafasi

    muruwa ya kuwapima wanao-

    faa kuwa viongozi bora.

    Kiongozi anayewajibika kwa

    umma

    Rais Jose Mujica alipoamua

    kugombea urais alishawishi-

    wa na hali ngumu aliyoiona

    wakikabiliana nayo walala

    hoi. Alisahau umimi akawe-ka mbele utaifa. Hakukimbilia

    utajiri bali uwajibikaji. Uamuzi

    wake wa kutoa asilimia 90 ya

    mshahara wake kila mwezi

    kwa jumuiya za kiraia kwa ajili

    ya miradi mbalimbali ya ku-

    wasaidia masikini ni kielelezo

    cha uadilifu anaopaswa kuwa

    nao kiongozi . Uadilifu huo ni

    wa kuwatetea, kuwasimamia

    na kuwapigania waliomcha-

    gua. Nikimnukuu, amesema

    hivi: Mshahara wa mke wan-

    gu ambaye tumejuana katika

    siasa na ni Seneta unatutos-

    ha, kwanini cha ziada tusitoekwa wengine.

    Mujica anasema anashaji-

    ishwa na falsafa ya utu, ya

    kumheshimu na kumfikiria

    binadamu mwengine na hasa

    masikini.

    Hadi miaka ya 1970 wakati

    Mujica Rais wa 40 wa Uru-

    guay akiwa gerezani sisi pia

    tulikuwa nao viongozi wa aina

    hiyo waliowajali na kujitolea

    kuwatumikia raia , waliobakia

    wakati wote kuwa sawa na

    wengine.... gari na vazi la ka-

    waida, viatu vya kanda tu na

    hata nyumba ya kawaida na

    waliokuwa karibu na umma

    kuanzia majimboni hadi kitai-

    fa, viongozi ambao umma naoulijivunia. Kama usemavyo

    usemi wa kihispania Un

    gobierno honrado, un pas de

    primera Serikali yenye hes-

    hima ni ile inayoliweka taifa

    mbele. Je, wengi wa viongozi

    na wanasiasa wa kwetu ni wa

    aina gani ?

    Barua za Wasomaji

    Ni fakhari ya kila Mzanzibari wa kweli kuwa na watu we-nye upeo, misimamo na kauli thabit kama wewe auntRiziki. Hapana shaka wewe ni moja katika rizki kubwa kwa

    taifa la ZANZIBAR. Jazaaka llah l kheir.

    [email protected]

    Mshirazi

    [email protected]

    Ahsante kwa makala yako murwa kabisa. Umenifurahishasana Sheikh Othman. Mungu akujaze kheir kwa hilo. LakiniAli Mrandazi, kwa uhakika, hatujui kama alikuwa walii wala la,

    lakini kwa ulengo wangu ana alama na dalili za uwalii.

    Tatizo Bwana Ali Saleh unalijua. Hapa petu wewe si mgeni wa siasa.Unajua kitu kinachopiganiwa hapa si utaifa bali ni matumbo kujaa. Sasahawa wahadimu wa pande hizi mbili, CUF na CCM, hawana mtafarukuisipokuwa wanatafuta mtu wamtie kati wamtoe kafara. Unawaona,Muamsho, waliwatumia CCM na CUF, baadaye, wamewatafutia gunia

    wamewavisha. Usione wewe umebahatika na umepata hicho kijifupa, sihaba. Hawa CUF, walikupigisha vigongo hata nakukutilisha ndani wakatiwanyamunyamu hawa kukumbuka. Sasa wache wapige ngoma watacheza wenyewe, kubomoa rahisi kujenga kazi.

    Nawe Bwana Ahmed Rajab una maoni mazuri na michango ndani yamajarida na mitandao mbalimbali ya k idunia, lakini wewe mchangowako wa kivitendo hatuuoni. Umekuwa kama Zanzibar. Wengine,wako ughaibuni, wana tuchochea, sisi wahadimu wanatuua, waowanakula raha ughaibuni. Tunasikia, wewe baada ya kustaafu umeonahapakaliki Zanzibar, umeomba uraia Kenya. Unajua hapa hapafai, sasakwa kuwa mwenzetu umealimka, ugemuiga mzee wetu almaruhum AliNabwa, aliyewaelimisha na kuwafunza mengi. Mungu amlipe mema naamughufiriye dhambi zake na amuondoshee adhabu ya kaburi. Na wewenjoo uwaelimishe, utarajie mema kwa Mungu. Muda huu wa mapumziko,

    ya utu uzima, ikumbuke jamii yako iliyo dhulumika miaka 50. Na weweunajua mengi kuhusu Zanzibar, makomredi mana deni kwa Wazanzibari.

    Ali Azani [email protected]

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    7/21

    12 13

    NGURUMO LA MKAMA NDUMEZanzibar Daima Online Zanzibar Daima Online

    Wengine tutauchuku-lia mwezi huu waNovemba kuwa wa

    aina yake visiwani Zanzi-bar kwa sababu ya matukiomawili, tunayoyaona ni mu-himu kwa maendeleo yakidemokrasia na kiutawalavisiwani humo.

    Moja ni kujizoazoa kwaSerikali ya Mapinduzi (SMZ)na kuja juu dhidi ya vyombovya habari vitakavyotumiavibaya uhuru wa habari na

    kuchapisha au kutangazahabari zenye lengo la ku-vuruga amani.

    Hayo yalisemwa na wazirianayeshughulikia habari,Said Ali Mbarouk, katika kilekilichotajwa na vyombo vyahabari vya Tanzania kuwa nimkutano wa waziri huyo nawakuu wa vituo vya rediovya Zenj FM na Coconut FM,

    vyote vya Zanzibar.Ujuu iliokuja nao SMZ katikahili ni kutoa onyo kwambaama vyombo hivyo viachekupandikiza mgawanyikowa Pemba na Unguja auvichukuliwe hatua kali. Hatu-

    jui ukali wa hatua hizo kali,lakini mazoea ya serikalizetu yanatupa mwelekeowa makisio - vitapigwa faini,vitafungiwa, lakini havitape-lekwa mahakamani. Vikipe-lekwa mahakamani itakuwa

    ni hatua nyengine kubwa yakupongezwa katika ukuajiwa demokrasia na utawalawa sheria nchini mwetu.

    Isifahamike kwamba makalahaya yanapingana na onyohilo la Waziri Said. La hasha.Kwa hakika, yanakubaliananalo kabisa na yangelipendahata liongezwe nguvu zaidi,yaani sio tu vyombo hivyo

    vikabiliane na adhabu iwapovikiendelea, bali viwajibikesasa kwa yale ambayo tayarivimeshayatangaza.

    Ikiwa msingi wa kuchukuliwakwao hatua hapo baadayeni athari za matangazo yaodhidi ya Umoja wa Kitaifawa Wazanzibari, basi ta-yari umoja huo umeanzakuathiriwa. Sikiliza kauli zaviongozi wajiitao wa shehia,wazee na vijana wa Ungujakutoka Chama cha Mapin-

    duzi (CCM) wakifoka hadimapovu kuwatoka dhidi yawatu wenye asili ya kisiwacha Pemba. Hapa nimewaitawajiitao na namaanishahivyo hivyo wajiitao waUnguja.

    Hao niwaitao wajiitao waUnguja wanasikika wakita-mka kwamba Wapembahawapaswi kuendelea kuba-

    kia kisiwani Unguja kamawanapingana na mfumo waMuungano wa Serikali Mbi-li uliopo sasa. Wasikie haowajiitao Waunguja waki-kumbusha mauaji yaliyofany-ika wakati wa Mapinduzi nawakiapa kwamba wako ta-yari kwa mapinduzi menginekama hayo ili kuweka heshi-

    ma na adabu.Chuki, hasira na kisasikinaonekana wazi kwenyemaneno yao kama zioneka-navyo kwenye nyuso nadhamira zao. Kauli ya vita,damu, mauaji, majeruhi,unaweza kuihisi kwa mba-li. Makala haya yanadhanikwamba hatua zilipaswa ku-chukuliwa leo, mfano wa vileviongozi wa Uamsho walivyo-chukuliwa hatua na Serikali hiihii, ikiwa kweli Serikali ilikuwa

    na haki ya kufanya vile wakatiule.

    Ila kama panangojewa hadiwatu washikiane mapanga,kama ilivyotokea Rwandabaada ya Redio Intarahamwekutumika kuchochea mauajidhidi ya kabila la Watutsi naWahutu wenye msimamo wawastani, basi natusubiri uleuitwao kwetu pwani ushahi-di wa Kinyamwezi.

    Nimeiita hatua hii ya sasa

    ya Serikali kwamba imekujabaada ya kujizoazoa. Nakus-udia kwamba ni hatua nzuriiliyokuja baada ya Serikalikuchelewa sana na kuwa-chelea wakubwa. Paliku-wa pamezoeleka kwa walewanaojinasibisha na Mapin-duzi na Chama cha Mapindu-zi, hata kama ni mijitu mijahili,mijinga na mikatili, kuogope-wa na SMZ. Ni kituko, lakini

    ndio ukweli kwamba Serikaliya Mapinduzi inawaogopawajinasibishao na Mapinduzi,hata kama hawana uwezowala njia za kupindua tena.

    Si haba kwamba angalau kwamara ya kwanza hao wajina-sibishao na Mapinduzi nakwa hakika ukichungua his-

    toria utawakuta wengi waohata hawakuhusika nayo sasa wanaambiwa kwambaZanzibar si yao mali yao, walayao peke yao.

    Novemba hii pia itaingia tenakwenye historia ya mae-ndeleo ya kisiasa visiwaniZanzibar, kwani kwa maraya kwanza tangu kurudikwa mfumo wa vyama vingi,Serikali iliamua kusimamiahaki ya kisiasa ya kila raiakwa kukiruhusu Chama cha

    Wananchi (CUF) kufanyasiasa za wazi k wenye jimbola Donge, ambalo kwa miakayote 20 na ushei ya siasa zavyama vingi wanasiasa wa-hafidhina wa chama tawalawamejenga mazingira ya ku-litenga na sehemu nyengineza Zanzibar kama kwambaDonge ni nchi pekee.

    Nakumbuka mwaka 2005,kundi letu la wanahabarililipojikuta likilazimika kuripotirisasi na mabomu pale Ma-

    honda baada ya polisi kuwa-zuia wana-CUF kwa maranyengine. Matokeo yake,yalikuwa majeruhi na mauaji.Uvunjwaji wa haki za binada-mu ukaendelea hata baada yahapo.

    Lakini ukweli ni kwam-ba mambo yana zama nazamu. Ndivyo alivyosemaRais Mstaafu wa Zanzibar,

    Dk. Salmin Amour Juma, sikuakitoa hotuba ya kusisimua

    juu ya umoja wa Wazanzi-bari, Ikulu ya Mnazimmojakwenye mkesha wa Mwafakawa kwanza wa kisiasa kati yaCCM na CUF mwaka 1999.

    Sasa zama zimebadili-ka na mabadiliko haya

    yanawaumiza wanasiasa am-bao walivuta pumzi, walikulana walikunywa uhasama wakisiasa. Donge imefungukana kujiunga tena na sehemunyengine za Zanzibar.

    Wala kujiunga huko si lazimakumaanishe kuiacha mkonoCCM na kuikumbatia CUF. Lahasha. Kunamaanisha kwam-ba sehemu hiyo nayo sasa ikotayari kusikiliza hoja na kuzip-ima ndani ya ardhi yake kishaikafanya uamuzi baada ya

    kuzipokea hoja hizo. Wanao-taka kujiunga na CUF waka-fanya hivyo kwa mujibu wawalichoelewa na wanaotakakusalia CCM wakafanya hivyokwa mujibu huo huo. Lakini sikinyume chake.

    Mantiki muhimu hapa nikwamba kubwa kuliko yoteDonge nayo ni Zanzibar, ime-kuwa hivyo na itakuwa hivyomilele. Kama ilivyo Pemba,kwa ujumla wake, ndivyo il-ivyo Donge kwa udhati wake.

    Zote ni sehemu za Zanzibar,zimekuwa hivyo na zitabakihivyo milele.

    Wale wanasiasa waliopiganiakuitenga Donge na Zanzibarna ambao sasa wanahubiriutengano wa Pemba na Un-guja, imekula kwao kwakutumia lugha ya vijana wakileo

    Na Mohammed Ghassani Ngurumo la Mkama Ndume

    Donge na Pemba nimoja na zitabaki hivyo

    Ali Shamhuna Mwakilishi wa Donge

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    8/21

    1514

    MKEKA WA MWANA WA MWANA

    Zanzibar Daima Online Zanzibar Daima Online

    Kama Zanzibar haiwezi kuchangia Serikali Tatu,Tanzania Bara inachangiaje kwenye Serikali Mbili?

    Hoja ya Mheshimiwa Awadhi

    ina mapungufu mengi. Mo-

    jawapo ni ikiwa kama hicho

    anachokisema ni cha kweli,

    basi kwa nini asipendekeze

    serikali moja tu kabisa, maana

    kwa vyovyote vile Zanzibar

    inatakiwa ichangie kwenye

    mfumo huu wa sasa uliopo na

    kama haitaweza kuchangia

    wakati huo, haiwezi kuchan-

    gia sasa pia. Hii ni kuuambia

    upande wa pili wa Muungano

    kwamba umekuwa ukiibeba

    Zanzibar sikuzote na sasa ...

    Na Riziki Omar Mkeka wa Mwana wa Mwana

    Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Fedha

    na Uchumi ya Baraza la Wawakilishi la Zanzi-

    bar, Salmin Awadh Salmin, alisema hivi karibuni

    kwamba Zanzibar haitakuwa na uwezo wa ku-

    changia uendeshaji wa Serikali ya Jamhuri ya

    Muungano kama muundo wake utakuwa wa

    Serikali Tatu.

    Kwa mujibu wa mwakilishi huyo wa jimbo la

    Magomeni (CCM), Zanzibar haiwezi kuchang-

    ia hata kwa asilimia 10. Hayo aliyazungumza

    kwenye semina ya Wabunge wa Muungano

    na Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi la

    Zanzibar mjini Dodoma Jumatatu ya tarehe 11

    Novemba, 2013. Hoja yake kubwa ni kwam-

    ba Zanzibar ina uchumi mdogo na, kwa hivyo,

    mfumo wa sasa wa serikali mbili ndio unaofaa

    katika kuudumisha Muungano.

    Nimekuwa mbunge kwa mwaka wa nane huu,

    nikiwakilisha maslahi ya Zanzibar kwenye

    bunge la Muungano, na lazima niseme kauli ya

    mtunga sheria mwenzangu huyu, Mzanzibari

    mwenzangu, ilinikirihisha. Wakati mwengine

    anasimama mtu kutokea upande wako wa

    nchi, analisema neno, unatamani uingie chini ya

    meza kukimbia aibu na fedheha. Huu ulikuwa ni

    wakati mmojawapo kwangu.

    Hoja ya Mheshimiwa Awadhi ina mapungufu

    mengi. Mojawapo ni ikiwa kama hicho ana-

    chokisema ni cha kweli, basi kwa nini asipende-

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    9/21

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    10/21

    Dk. Shein astahili kuitwa

    Rais wa Busara

    KUMBE Rais wa Zanzibar, Dk. AliMohamed Shein, ana busara nyin-gi.

    Daktari huyu wa binadamu, ninayem-fahamu kwa miaka 20 hivi tangu akiwaofisa mdogo katika k ilichokuwa Kiten-go cha Kudhibiti Ugonjwa wa Ukimwianashangaza.

    Najua anapoamua kusema au kutenda,anaweza. Akatenda kwa kiwango usi-choweza kuamini. Tatizo kwa asili yake,hatabiriki. Labda upole wake unachan-gia. Nini maana yake?Pale unapomtarajia afikirie suala fulaninamna unavyoliona, usishangae aka-wa anafikiria tafauti. Anaweza kufikiriavingine kabisa na bado mkaendeleakujadiliana. Hana papara. Mtulivu kwe-likweli.

    Wanasaikolojia wanasema tabia hii nimoja ya sifa za watu wenye akili nyingi.Sijiingizi kusema naye ana akili nyingi.Kwa muda mrefu sijakaa naye kujadili-ana lolote, nikapata kumpima.

    Wiki iliyopita, alikutana na waandishiwa habari, wengine wakitoka Dar esSalaam kwa kugharimiwa na ofisi yake.

    Sikubahatika kualikwa. Nin-geupata mwaliko, ningeu-daka kwa moyo mkunjufu.Ningehudhuria maana ninamaslaha makubwa na Zan-zibar. Kwa hivyo, ningepatamawili matatu ya kujifunza.Tunapojadili Zanzibar na sia-sa zake, ingenisaidia.Hata mwaka jana, ingawanilitarajia, baada ya ku-wasiliana na Mkurugenzi waMawasiliano Ikulu, HassanKhatib, sikualikwa. Ofisahuyu anajua zaidi kilichot-okea. Hilo ni historia leo,mkutano umepita. Kinacho-

    endelea sasa ni watu kuta-fakari maelezo aliyoyatoaRais, maswali aliyoulizwa,na majibu aliyoyatoa. Kuto-kuwepo kwangu, walakini,hakuninyimi haki yangu yakuchambua aliyoyasema.Ndo ninachokifanya.

    Dk. Shein amenikoshaalivyoihifadhi Serikali an-

    ayoiongoza. Amefanikiwakuifichia matatizo yake kiu-tendaji. Aibu zake kitaswira.Ameifichia Serikali ya Umoja

    wa Kitaifa (SUK) madhambiyake. Ameitetea vya kutoshaakisema inafanya kazi vizuri,kwa mshikamano imara nauvumilivu.Haya yanawasuta waha-fidhina wanaohangaikakuisambaratisha. Walitarajiaatashambulia. Wao waliami-ni atamsema na kumbomoaMaalim Seif Sharif Hamad,

    mmoja wa wasaidizi wakewawili wakuu.

    Maalim ni Makamu waKwanza wa Rais. Makamuwa pili, ni Balozi Seif Ali Iddiambaye pia ni kiongozi washughuli za Serikali katikaBaraza la Wawakilishi chombo cha kutunga sheriana chenye kuisimamia Seri-kali katika utendaji.Moja ya maswali aliyoulizwaDk. Shein lilihusu eneo hilila mwenendo wa Makamuwa Kwanza wa Rais, kuhusuKatiba mpya ya Jamhuri ya

    Muungano.Wahafidhina wanamchukuliavingine Maalim Seif. Wa-nambeza na kudhani sistahili yake kupewa wadhifahuu. Wanamwona kuwa nishawishi tu asiye na lolote.Kwao, Maalim Seif, hanamchango. Amejiingiza Seri-kalini. Wanadhani ile nafasi

    NASEMA HIVI, DK. SHEIN ANABUSARA SANA. ANAJUA SIKUATAKAYOMBOMOA MA ALIMSEIF HADHARANI, NA HATAKWENYE BARAZA LA MAPIN-DUZI, ITAKUWA JAMBO KUB-WA.

    18 19

    Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar,

    Maalim Seif Shariff Hamad

    Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein

    Na Jabir Idrissa Kauli ya Mwinyi Mkuu

    KAULI YA MWINYI MKUU

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    11/21

    21HABARI KUUZanzibar Daima Online Zanzibar Daima Online20

    si kumfukuza Maalim Seif.Hawa hawasomi Katiba yaZanzibar, hasa lile fungulililoweka nafasi yenyewe yaMakamu wa Kwanza. Si kati-ka asili zao kusoma. Maranyingi hukurupuka. Ndiomaana kila wanapofanyashambulio dhidi yake, hujik-uta wakiishia kupiga ngumibaharini. Hakuna mtikisikoila yale maji yanamwagikianyusoni mwao.

    Mabao ya maskani yaMwembekisonge naKachorora yanaandikamaandishi ya kuthibitishamashambulizi dhidi ya Maa-lim Seif. Kazi yao kila wakatini hiyo tu ya kumsukumaakasirike. Wanakosea sana;hata mara moja kiongo-zi huyu hajababaishwa namashambulizi yao.

    Na kule kubaki kwake imaraofisini, kubaki imara katikakumsaidia na kumshauriRais wanachukia. Kubakiimara katika kufanya kaziyake kwa ushujaa mkubwakunawatesa. Kwa upandemwingine, wanapomwonaanafanikiwa huku akizidikukijenga Chama cha Wa-nanchi (CUF) kilichomfikishahapo, wanaumia wahafidhi-na.

    Ni pigo kubwa kwao kwanimashambulizi wanayomlen-gea yanawarudia. Hayam-pati na wanamkuta ametuliakama maji mtungini. Hatamara moja Maalim Seif haja-toa kauli ya kuwalenga wa-hafidhina. Yeye sanasana nikuelekeza wananchi kutuliawasichafue amani. Husematu Ndugu wananchi nawasi-

    hi bakini watulivu, mt ayaonamengi makubwa yatatokeachini ya Serikali hii.

    Dk. Shein anasema Serikaliinatekeleza majukumu yakekwa ufanisi na mshikama-no mkubwa. Ninamnukuu:Serikali yangu imefanikiwakudumu kwa miaka mitatusasa kutokana na kuvumil-iana na kufanya kazi kwapamoja bila ya kutangulizaitikadi za kisiasa.

    Nchi nyingine zime-jaribu hili (mfumo huu waSerikali ya Umoja wa Ki-taifa) zimeshindwa, laki-ni sisi tumefanikiwa kwasababu tunavumiliana. Hililinahitaji stahamala kub-wa vinginevyo tutagawanambao na sitaki hili litokeekwenye uongozi wangu.

    Aliyasema haya aliposukum-wa kusema anachukuliajekauli za Maalim Seif wakatihuu wa maandalizi ya kuan-dikwa Katiba mpya. Ni kweliMaalim Seif analizungum-zia kila wakati suala hili.Wao wahafidhina wanaonaanaisemea Serikali ilhali yeyesi rais. Walishasema am-fukuze.

    Dk. Shein amesema yeyendo wa kutoa msimamo waSerikali. Hajafanya hivyona hawezi kufanya hivyokiongozi mwingine yeyotekatika Serikali anayoiongo-za. Si Makamu wa Kwanzawala wa Pili. Wao wanawe-za kutoa misimamo binafsiinayozingatia mielekeo yavyama vyao. Anasema hatanaye aweza kutoa maonikulingana na mtizamo wa

    Chama Cha Mapinduzi (CCM).

    Maalim Seif amesema sanakuhusu suala la Katiba. Am-etoa msimamo binafsi, mbalikabisa na wa CUF. AnatakaMuungano wa Mkataba naZanzibar yenye mamlaka ka-mili. Sera ya CUF ni ya kuwana muundo wa Muunganowenye Serikali tatu. Aliyase-ma hayo mbele ya Tume yaMabadiliko ya Katiba ya JajiJoseph Warioba. Maalim Seifanajiamini kwa kile ana-chokiamini.

    Ona alivyomkingia kifuaMakamu mwenzake, BaloziSeif, alipojikuta ak ishambuli-wa na umma unaopendeleamabadiliko ya Muunganokwa kutaka Muungano waMkataba chini ya Serikali yaZanzibar yenye mamlakakamili.

    Balozi Seif alitegwa naSerikali ya Muungano kwakuombwa kueleza ushirikiwa Zanzibar katika kujadilimapendekezo ya marekebi-sho ya Sheria ya Mabadilikoya Katiba. Alipoinuka aka-liambia Bunge kuwa Zan-zibar ilishirikishwa. Kumbe,Zanzibar ilipewa vifunguvinne tu vya mapendekezokati ya 12 vilivyopitishwaSeptemba 6 na Wabunge waCCM pekee pamoja na Au-gustine Mrema wa TanzaniaLabour Party (TLP).

    Maalim Seif alimtetea Balozikuwa alijibu kwa kuangaliavifungu walivyovijadili Ser-ikalini. Hakujua wataalamuwa Wizara ya Sheria naKatiba na Ofisi ya Mwa-nasheria Mkuu wa Serikali

    waliweka vifungu vingi zaidikatika Mswada, vikiwemo vileambavyo vina maslaha makub-wa na Zanzibar.

    Nasema hivi, Dk. Shein anabusara sana. Anajua sikuatakayombomoa Maalim Seifhadharani, na hata kwenye

    Baraza la Mapinduzi, itakuwajambo kubwa. Atakuwa ameji-umiza na kujimaliza. Atakuwaameondoka kwenye mstari.Atakuwa amejichongea. AnajuaSerikali ina deni kubwa kwawananchi. Anajua Serikali hai-

    jatimiza ahadi zake.Dk. Shein anajua Maalim al-isema nini Bwawani siku ma-tokeo yalipotangazwa. Anajuaametimiza au hajatimiza yale.

    Anajua Maalim Seif anasaidiakuwepo amani na utulivu nchi-ni. Anajua akimbeza ni hatarikwake. Wahafidhina wanasubi-ri hali hiyo itokee.

    Watu hawa wamekuwa waki-taka Serikali ivunjike ili pazukebalaa. Siku zote imekuwa

    ni imani yao kwamba kui-shi kwao kunategemea sanasiasa chafu, zilizojaa chuki,hasama na ubaguzi dhidi yawatu wa wasioipenda CCM nahasa Wazanzibari wenye asiliya Pemba ambao wanawa-ona kama wasiostahili kuwaWazanzibari.Wanapata shida leo kwa saba-bu vile viapo vyao kuwa Ikuluhataigusa kiongozi kutoka

    Pemba vimefika mwisho kwakuwa Dk. Shein amezaliwaMkanyageni, Kusini Pemba.Hata Maalim Seif, Makamuwake wa Kwanza, ni mzaliwawa Mtambwe, Kaskazini Pem-ba. Wanatokea wapi?

    Viapo hivi ni kama vile

    walivyoapa wahafidhina waDonge kuwa kamwe MaalimSeif na CUF yake hawataingiaDonge kufanya mkutano wahadhara. Maalim ameingia naCUF yake ikafanya mkutanomkubwa Novemba 10, hukumzaliwa wa Donge na muasisiwa CUF, Machano Khamis Ali,ambaye ni Makamu Mwenyeki-ti, akihutubia

    Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi

    KAULI YA MWINYI MKUU

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    12/21

    2322

    TUFUNGUE KITABUZanzibar Daima Online Zanzibar Daima Online

    Shafi Adam Shafi

    TANBIHI: Uhakiki huu uliandikwa kwa

    lugha ya Kiingereza naFLAVIA AIELLOTRAOREkwa jina la INVESTIGATING

    TOPICS AND STYLE IN VUTA NKUVUTE BY

    SHAFI ADAM SHAFI. Hapa tumeutafsiri

    kwa minajili ya kuwapa wasomaji wetu

    mtazamo wa wengine kwa fasihi ya

    Kizanzibari.

    Kwa miongo mingi

    sasa, wahakiki wa

    kazi za fasihi wame-

    zisifu kazi za waandishi waKizanzibari kwa sifa tele.

    Kwa mfano, akirejea riwaya

    za Mohamed Suleiman Mo-

    hamed, Said Ahmed Mo-

    hamed na Shafi Adam Shafi,

    M. M. Mulokozi aliandika

    mwaka 1985: Maendeleo

    muhimu kabisa, na pengine

    ya kufurahisha sana, katika

    kazi za fasihi za K iswahili ka-

    tika miaka ya 1970 na 1980,ni kuibuka kwa Zanzibar

    kama mtoaji bora kabisa wa

    kazi za Kiswahili kuwahi ku-

    tokea hadi sasa, na kiongozi

    wa wazi wa riwaya za Kiswa-

    hili katika siku zijazo.

    Hisia kama hizi zinaelezewa

    pia na R. Ohly ambaye, baa-

    da ya kukumbana na riwaya

    zilizoandikwa na waandishi

    wa Kizanzibari na wale wa

    Kitanzania na Kikenya bai-

    na ya mwaka 1975 na 1981,amezielezea riwaya za Ki-

    zanzibari kama changamoto

    kubwa kwa uwezo wa kisa-

    naa kwa waandishi wengine

    wa Kiswahili.

    Ingawa mnasaba uliotumi-

    wa na Ohly unaweza kujadi-

    lika kwa kujikita kwake na

    kazi zilizotolewa Bara hasahadithi fupi fupi na kuwaa-

    cha waandishi wenye vipaji

    kama vile Eupluase Kezila-

    habi au Claude Mungongo,

    uhakiki wake bado umezu-

    ngumzia sifa kuu za riwaya

    za Kizanzibari, yaani kujikita

    sana kwenye masuala ya ki-

    historia na kijamii, pamoja na

    utajiri wa lugha mwanana na

    kutokufanya mzaha kwenyemasuala ya fani.

    Sifa hizi za fani zinashabihi-

    ana sana na riwaya ya Vuta

    Nkuvute iliyoandikwa na

    Shafi Adam Shafi na kuchap-

    ishwa mwaka 1999, ambayo

    ndiyo shughuliko la uhakiki

    huu.

    Waandishi wa Kizanzibari

    mara kadhaa wamean-dika riwaya za kihistoria,

    wakizikita simulizi zao kati-

    ka zama za ukoloni ama za

    kabla ya Mapinduzi visiwani

    humo. Kufuatia hali hiyo,

    matukio kwenye Vuta Nku-

    vute nayo yanazungumzia

    siku za mwisho mwisho za

    ukoloni visiwani Zanzibar.

    Mandhari ya riwaya hii ni

    changamano sana, maisha

    ya dhiki ya wahusika wakuu

    yanachorwa kupitia matukio

    kadhaa, wahusika wadogo,

    matendo ya kuchangam-

    sha, yote yanaunganishwa

    na mapenzi ya uhuru na ku-

    jutawala (KUJUTAWALA NI

    NINI?), katika viwango taf-

    auti vya maisha ya kibinafsi,kijamii na kisiasa, na hivyo

    kuusafirisha ule moyo wa

    Ujamaa katika muonekano

    wa kilimwengu zaidi.

    Hadithi yenyewe inaanza

    kwa kumtambulisha mso-

    maji kwa msichana wa Ki-

    hindi, Yasmin, ambaye ku-

    tokana na mila ya ndoa za

    kupangwa na wazazi, anak-

    wenda Mombasa na mume

    wake, mfanyabiasharamzee, Bwana Raza. Lakini

    Yasmin anaoneshwa kuwa

    mtu asiye na furaha na mp-

    weke na hatimaye anaasi na

    kurudi nyumbani, Zanzibar.

    Kutabiri matokeo ya makuzi

    mabaya ni jambo maarufu

    kwenye riwaya za Kiswahili,

    ambapo kawaida waandishihuchora mashaka yale yale

    yanayoathiri maisha ya vija-

    na, hasa wa kike, ama kus-

    hindwa hadi kufikia mauti

    yao au mateso ya kiakili na

    kimwili kama vile Rosa Mis-

    tika au Asumini, au kukimbia

    mazingira kandamizi kama

    vile Maimuna na Yasmin,

    ambapo mote hupelekea

    maisha mapya kabisa.

    Mara tu baada ya kurudi Zan-

    zibar, Yasmin anakataliwa na

    mjomba wake na anaomba

    msaada wa shoga yake wa

    pekee, Mwajumba, msicha-

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    13/21

    2524 Zanzibar Daima OnlineTUFUNGUE KITABU

    WATUHUMIWA MENO YA

    TEMBO WAONGEZEKA

    JESHI la Polisi Zanzibar li-mewakamata watuhumi-wa wengine watatu, waki-

    wamo maofisa wawili wa

    Mamlaka ya Mapato nchini

    (TRA) kituo cha Bandari Zan-

    zibar kwa kuhusika na kash-

    fa ya kupatikana kwa menoya tembo yenye thamani ya

    mabilioni ya shilingi.

    Kamishna wa Polisi Zanzi-

    bar (CP) Mussa Ali Mussa,

    amewataja maofisa hao wa

    TRA waliokamatwa kuwa

    ni Omari Hamad Ali (50) na

    Mohammed Hija (48) ambao

    wote wanafanya kazi katika

    Bandari ya Zanzibar. Mtu-

    humiwa mwingine ni kiba-

    rua wa Mamlaka ya Bandari

    Zanzibar, Haidar Ahmad Ab-

    dallah (54).

    Kukamatwa kwa watuhumi-wa hao kunaifanya idadi ya

    watuhumiwa waliokamatwa

    hadi sasa kwa kuhusika na

    sakata hilo kufikia watano.

    Kamishna Mussa amesema

    watuhumiwa wengine wa-

    wili ambao ni wafanyakazi

    TANBIHI:

    Habari hiiiliandikwana gazeti laTanzania Daimala tarehe 17

    Inaendelea Uk. 40

    na wa Kiswahili anayeishi

    kwenye mitaa ya masikini

    ya Ngambo, ambaye anam-

    pokea kwa moyo wote.

    Licha ya ukarimu wa Mwa-

    juma, mama yake Yasmin

    anakataa kumsamehe bin-

    tiye sio tu kwa kuiabisha fa-

    milia kwa kumuasi mumewe,

    bali pia kwa kujichanganya

    na Waswahili na hivyo ku-

    vunja khulka ya jamii yake na

    tafauti za kijamii na kitama-

    duni zilizojikita sana kwenye

    unyanyapaa wa sera za

    kikoloni linapohusika suala la

    mahusiano kati ya makabilayanayounda jamii kubwa ya

    Kizanzibari.

    Baada ya kukandamiz-

    wa kwenye misuguano na

    ubaguzi wa kijamii huko

    alikokulia, Yasmin anapa-

    ta ladha ya maisha mapya

    wakati akiishi kwa Mwa-

    juma, ambako anagunduamaisha yenye wasaa zaidi,

    mukiwemo ulevi, klabu za

    usiku na, zaidi ya yote, an-

    apendana na kijana aitwaye

    Denge.

    Denge ni kijana msomi ali-

    yerejea nyumbani akitokea

    Ulaya akiwa hana chochote

    zaidi ya digrii yake ya Kiru-

    si na dhamira madhubuti ya

    kuikomboa nchi yake kutoka

    kwenye Himaya ya Mwing-

    ereza. Yeye na marafiki zake

    wanaandamwa na polisi kwa

    kufanya propaganda ya ki-

    siasa na kuingiza kwenye

    nchi vitabu na magazeti

    yaliyopigwa marufuku na

    wakoloni.

    Yasmin anajikuta akihusi-

    ka moja kwa moja katika

    mapambano kati ya kundi

    la Denge na polisi, ambaowanajaribu kumlazimisha

    amsaliti mpenzi wake mko-

    munisti na kafiri, lakini

    anaamua kuwasaidia wan-

    aharakati hao, akiamini wa-

    naandamwa kwa sababu tu

    wanapigania uhuru.

    Kama inavyoelezwa na

    Denge katika ukurasa wa68 wa riwaya hii, serikali ya

    Kiingereza ilijaribu kuwaten-

    ganisha wapigania uhuru na

    wafuasi wao kwa kutumia

    sera ya wagawe uwatawale:

    Sikiliza Sista, hawa wakolo-

    ni na vijibwa vyao ni watu

    wapumbavu kabisa, kwao

    kila mtu ni koministi Ukid-

    ai haki yako wewe koministi

    Ukisema kweli wewe komin-

    isti Ukipinga kutawaliwa

    wewe koministi. Kila anaye-

    dai haki kwao ni koministi,na sumu yao kubwa wanay-

    oitumia ya kutaka kuten-

    ganisha watu kama hao

    na wananchi wenziwao ni

    kusema kwamba watu hao

    wanaowaita makoministl

    hawaamini Mungu.

    Mapambano ya daima kati ya

    maafisa wa kikoloni na wap-

    igania uhuru yanaipeleka ri-waya hii kwenye upeo wa ha-

    dithi ya kusisimua, kurusha

    roho na hekaya za kijasusi,

    mtindo ambao uliletwa kwa

    mara ya kwanza kwenye

    riwaya za Kiswahili na Mo-

    hamed Said Abdulla (Bwana

    MSA), ingawa kwenye riwaya

    hii polisi wamekuwa wahusi-

    ka wabaya, wanaotumikiamaslahi ya kikoloni kibubusa.

    Kama inavyoelezewa na Pazi

    katika ukurasa wa 113, kati-

    ka mapambano ya kuwania

    uhuru, ni muhimu kutumia

    hata njia zisizo za halali

    kisheria

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    14/21

    2726Zanzibar Daima Online

    WARAKA KUTOKA BONNZanzibar Daima Online

    Kutafuta mafuta Zanzibarkumeanza mwaka 1957, ilitarajiwakisima cha Chuwini peke yakekitachimbwa kufikia futi 12,000 ....

    K

    atika wiki mbili za mwanzo za mwe-

    zi huu wa Novemba nilitembelea

    Umoja wa Falme za Kiarabu. Lichaya kuizuru nchi hiyo mara kadhaa hapo ka-

    bla, safari yangu ya mwishoni ilikuwa ndefu

    kabisa kuwahi kuifanya na ya kwanza kukaa

    na wenyeji walio Waimarati wa kindakinda-

    ki, kama wanavojiita watu wa asili wa nchi

    hiyo ilio ya muungano wa falme saba ndo-

    gondogo.

    Imarati, nchi yenye wahamiaji wengi wa Ki-

    zanzibari, pia ni nchi yenye historia ya main-

    giliano ya miaka na dahari na Zanzibar, ime-piga maendeleo makubwa katika miongo ya

    miaka ya karibuni, hasa ya miundo mbinu.

    Hivyo imekuwa ni kivutio kwa Wazanzibari

    wengi kwenda kutafuta ajira. Wananchi we-

    ngi katika miji ya Dubai, Abu Dhabi, al-Ain

    na Ras al-Khaimah wanaishi katika neema

    ambayo hata watu wa Ulaya wanawaonea

    gere. Wafanya kazi hawatozwi kodi ya ma-

    Syd.Khalifa akiikagua mitambo yakuchimba mafuta, Zanzibar. Pamojanaye ni M.M.Pennel Mkuu wa Kampuniya Shell.

    Waziri Ramadhan AbdallahShaaban akibadilishana hatiiya makubaliano na Mwenyekitiwa Kampuni ya Shell

    Wazanzibari tujipange, mafuta yasije yakawa nuksi kwetu

    Na Othman Miraji Waraka kutoka Bonn

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    15/21

    29Zanzibar Daima Online

    28 Zanzibar Daima Online

    pato, na serikali inatoa nafuu nyingi kwa

    wananchi .

    Familia nilikofikia ya watu watano, ukiwacha

    watoto wanne, kila mmoja ana gari mbili za

    fahari. Tulipoketi kula chakula, meza ilijaa

    vyakula vinavoweza kuwashibisha watu 40.

    Nilijiuzulu moyoni: kuna harusi? Kadiri asi-limia 60 ya vyakula vinabakia na hutupwa

    mapipani. Sebuleni mazungumzo ya weny-

    eji wangu yalikuwa tu juu ya likizo zao wa-

    lipokuwa Marekani na Ulaya. Mikahawa ya

    Kimarekani ya Macdonald na Kentucky ime-

    furika katika miji ya Imarati. Vipindi vya te-

    levisheni wanavoangalia wenyeji wangu ni

    vya kutoka Marekani na Ulaya, ni nadra wao

    kuangalia vya Kiarabu.

    Nilivuta fikra hadi udogoni mwangu nika-

    iona sura ya maduka ya tende, nguru, papa

    na chumvi yaliosheheni wakati huo katika

    mtaa wa Mchangani, Unguja mjini, pamoja

    na suwela na hanide waliokuwa wanauzwa

    Malindi. Vitu hivyo vilikuwa vinaletwa Zan-

    zibar na mababu wa hawa Waimarati wa

    sasa waliokuja katika majahazi yao ya Mu-

    sim. Waliporejea makwao pale pepo za Mu-

    sim zilipogeuka, watu hao walichukua bori-

    ti kutoka Bara na bidhaa nyingine kutokeaZanzibar.

    Mnamo muda wa kizazi kimoja tu, maisha

    ya Waimarati yamebadilika kwa mshangao

    mkubwa, na yote imetokana na utajiri wao

    mkubwa wa mafuta ya petroli, k wa jina len-

    gine dhahabu nyeusi. Watu hao hadi katika

    miaka ya 1950 walikuwa wanaishi katika hali

    ngumu, wengi majangwani katika mahema

    na katika miji midogo pembezoni mwa Ghu-

    ba, wakivua samaki na kula tende, maziwa

    na nyama ya ngamia. Sasa wanakula kwa

    wingi vyakula vya kutoka ngambo, nyama

    kutoka Marekani na Australia inayowaonge-

    zea uzito mwilini. Matokeo yake wanapatwana magonjwa ambayo hapo zamani yaliku-

    wa nadra kusikika Arabuni.

    Niliwauliza wenyeji wangu: Je, mmefikiria

    vipi nchi yenu itakavyokuwa bila ya mafuta?

    Walinijibu kwamba akiba yao ya mafuta ita-

    bakia kwa zaidi ya miaka 100 ijayo. Hata wa-

    najizuia kuchimba mafuta mingi hivi sasa ili

    bei isiporomoke. Niliwaambia kwamba hata

    kama mafuta yatabakia daima, lakini Wa-zungu na Wamarekani, wanaonunua mafu-

    ta hayo kwa wingi, itafika wakati watafaulu

    kujitosheleza na nishati mbadala ilio safi,

    kama vile ile ya kutoka nguvu za jua, upepo

    au maji ya moto chini ya ardhi. Walinijibu: Al-

    lahu Qadeer -Mwenyezi Mungu ni mwenye

    nguvu ya kufanya kila kitu. Kama alivowa-

    pa utajiri wa mafuta hivi sasa , basi atawapa

    utajiri mwingine pale mafuta yatakapokua

    hayahitajiki. Hilo ni jibu la kujipa moyo tu. In-

    asikitisha.

    Mafuta, licha ya kurahisisha maisha ya watu

    wa Uarabuni, neema hiyo nimeona ina ma-

    tatizo na hasara zake pia. Raia wengi wa-

    naupoteza utambulisho wao na utamaduni

    wao, baadhi wameingiwa na kiburi cha kuwa

    matajiri sana. Ukiwaona wanatoka kwe-

    nye maduka makubwa ya Supermarkets,

    wamebeba mifuko mikubwa iliojaa vyakula

    chungu nzima vya aina mbalimbali, vitu vya

    anasa - vingi ambavyo hata hawatavitumia

    - ukiwaona kila mwezi wanabadilisha simu

    za mikononi na kuchukua mpya zilizoingia

    masokoni unajiuliza: wazimu huu wa ku-

    tumbua na kutumbua fedha bila ya mipaka

    mwisho wake ni nini?

    Ni nchi za Ulaya, Marekani na sasa China zi-

    naziuzia nchi za Kiarabu zilizo tajiri kwa ma-

    futa bidhaa hizo. Cha kushangaza ni kwam-

    ba ni raia wa nchi hizo za Ulaya na Marekani

    wanaotambua sasa hasara ya kutumia na

    kutumbua mali bila ya mipaka. Ulaya na Ma-

    rekani sasa zinajifunza kupunguza matumi-zi, zinajizuia kutumia ovyo rasilmali na utajiri

    wao, zikishikilia kwamba binadamu inabidi

    aachane na mtindo wa kuishi kwa raha sana

    ya kupita kiasi kwa gharama ya vizazi vija-

    vyo. Serikali zinawahimiza raia wao wayahi-

    fadhi mazingira kwa ajili ya uhai wa sayari

    yetu hii ya dunia.

    Nchi za Kiarabu zina akiba kubwa ya mafu-

    ta, lakini hiyo haina maana kwamba mafutahayo yatumiwe ovyoovyo. Ukiona taa nyingi

    zinazowaka ovyo usiku mzima mabarabara-

    ni na maji ya chumvi mengi yanayogeuzwa

    kuweza kunyunyuzia bustani unasikitishwa

    na uchafuzi mkubwa wa ma zingira unaosa-

    babishwa na moshi mchafu hewani. Bei ya

    lita moja ya mafuta Abu Dhabi ni asilimia 14

    tu ya bei mtu anayolipia akiwa Berlin,Ujeru-

    mani.

    Mwanadamu alitoka kutoka enzi ya ustaara-

    bu wa kutumia mawe na kuingia katika enzi

    ya ustarabu wa kutumia chuma, na hiyo si

    kwa sababu mawe yalikwisha. Hasha. Ila tu

    binadamu alitanabahi kwamba chuma ndio

    njia ya kuboresha maisha yake. Na hivyo

    ndivyo itakavokuwa pale mwanadamu ata-

    kapoachana na mafuta, si kwamba mafuta

    hayatakuweko, lakini kutakuwako mbadala

    ulio bora.

    Kuna habari nzuri kwamba si miaka mingi

    kutoka sasa, Inshaallah, nchi yetu ya Zan-

    zibar itakuwa mtoaji wa mafuta ya petroli.

    Nahisi ni wakati sasa kwa Wazanzibari kuji-

    tayarisha, kisaikolojia, juu ya ujio wa neemahiyo. Mafuta yameleta maendeleo kwa nchi

    kadhaa, lakini utajiri huo kwa baadhi ya nchi

    umeziletea madhara. Si tu tujifunze namna

    ya kuyachimbua mafuta hayo na kutowa-

    achia kila kitu wageni watufanyie, lakini pia

    tupange tangu sasa namna ya kujiepusha

    na hasara zilizopata nchi nyingine kutokana

    na mafuta, kisaikolojia, kwa wananchi wao,

    kimazingira, na kupanuka mizozo ya kijamii.

    Tujue kutakuweko uchochezi wa kutoka njewa waroho watakaonyemelea kuupora uta-

    jiri huo kwa kutugonganisha vichwa weny-

    ewe kwa wenyewe Wazanzibari. Pia tuchu-

    kue tahadhari juu ya kumomonyoka maadili

    na tunu zetu, kwa kisingizio cha utandawazi

    unaotokana na utajiri huo. Mafuta yawe ba-

    raka na si nakama na balaa k wetu

    WARAKA KUTOKA BONN

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    16/21

    30 31Zanzibar Daima OnlineZanzibar Daima Online

    Dk Mvungi ameikosatreni ya mwisho ilatuko naye

    Watu wengi wamekuwa wakisikia

    sifa nyingi mno za Dk Adri-

    an Sengondo Hamis Mwarabu

    Mvungi katika kipindi alichokuwa amejeru-

    hiwa na wanaodhaniwa kuwa ni majambazilakini wamesikia zaidi baada ya kufa kwake.

    Si ajabu watu wengi wanadhani hizo ni sifa

    anazopewa tu kwa sababu ameshakufa

    hasa kwa kuwa Waafrika na watu wenye

    imani ya dini wanaamini kuwa maiti hasem-

    wi vibaya. Lakini hiyo sio kweli hata kidogo.

    Kwa hakika Dk Mvungi, aliyetimiza umri wa

    miaka 61 siku moja kabla hajashambuli-

    wa, alikuwa ni mtu mwema, mstahamilivu,

    msikivu na hodari sana kwa watu.

    Kama kuna njia ya kumwombea binadamu

    wa kawaida apite njia nyepesi kuelekea kwa

    Muumba wake, sisi wajumbe wa Tume am-

    bao tumemjua Dr Mvungi tusingesita kufa-

    nya hivyo. Kila mmoja wetu anaijua sifa ya

    ukarimu wake pamoja na umbo kubwa am-

    balo lingemfanya awe na kiburi cha maguvu.

    Daktari huyu wa sheria aliyasabilia maisha

    yake kwa watu. Alianza kwa ndugu zake na

    jamaa zake. Si hasha moja ya matunda yake

    ni padre anayesimamia kanisa la St Joseph

    mjini Dar es salaam na utitiri wa nduguzeambao wengi wao wamehitimu hata elimu

    ya juu.

    Akajitolea kusimamia wachochole na wala-

    lahoi kwa nguvu na elimu yake. Alianzia kwa

    kuanzisha kituo cha kisheria cha kuwasaidia

    wanyonge na baadaye alisukuma kuund-

    wa Kituo cha Haki za Binadamu na Sheria

    (LHRC) na kushirikiana nacho katika mambo

    kadhaa pamoja na kubuni njia kadhaa za ku-

    wasaidia watu wa tabaka hilo.

    Ndipo mwombolezaji mmoja aliposema, Ni

    kinyume cha mambo kwamba waliomuua ni

    katika kundi la wanyonge ambao angeweza

    kwenda Mahakamani kuwatetea. Lake ali-

    jualo Mungu ni la shani zaidi.

    Ratiba ya Dlk Mvungi ilikuwa ya ajabu sana.

    Dk. Adrian SengondoHamis Mwarabu Mvungi

    Daktari huyu wa sheriaaliyasabilia maisha yakekwa watu. Alianza kwandugu zake na jamaazake. Si hasha moja yamatunda yake ni padreanayesimamia kanisala St Joseph mjini Dar

    es salaam na utitiri wanduguze ambao wengiwao wamehitimu hataelimu ya juu.

    Barza ya Jumba MaroNa Ally Saleh

    BARAZA YA JUMBA MARO

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    17/21

    32 33Zanzibar Daima OnlineZanzibar Daima Online

    Nayo hiyo ilitokana na muda mrefu wa ku-

    jizoesha ambapo kila siku ya Mungu alikuwa

    akifanya mchakamchaka, au saa 12 asubuhi

    alikuwa ameshaanza kazi kama alivyoshu-

    hudia mfanyakazi mwenzake wa South Law

    Chambers aliyekutana naye siku hiyo ya ku-

    zaliwa kwake tarehe 2 Novemba.

    Kwenye taaluma Dk Mvungi, ambaye ali-

    kuwa mwalimu wangu wa somo la Katiba

    katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam, haku-

    wahi kufanikiwa kufikia uprofessa na miye

    naamini ni kwa sababu alikosa muda kwa

    vile kipindi kikubwa alikitumia akijitolea ku-

    wasaidia watu.

    Aliandika sana kuhusu haki za binadaamu na

    mambo ya katiba na alitoa matamko mengi

    ambayo ungeyasikia kama yalivyonukuli-

    wa na LHRC ungetokwa na machozi. Alijaa

    tamaa ya usawa, uchu wake, kiu ya mabadi-

    liko lakini hasa alikuwa na ashiki ya usawa.

    Alikuwa Mjamaa ndani ya moyo wake lak-

    ini pia alikuwa yu tayari kwa mabadiliko ya

    zama mpya. Na ndio maana akaona njia pe-

    kee ni kuingia ndani ya mfumo na akajaribu

    kugombea Urais mwaka 2000, lakini mfu-

    mo ulimjibu vilivyo maana hata kura yake

    mwenyewe katika k ituo alichopiga kura hai-kuonekana na kuhesabika.

    Alikiri kushindwa katika ugombezi huo bila

    ya kinyongo na akaona kunakomfaa katika

    harakati hizi ni kuwa upande wa wananchi

    na ndipo nguvu zake za kudai Katiba Mpya

    zikawa za kasi, kina na nguvu zaidi.

    Si katika waliochelewa hata huko nyuma.

    Maana alianza pale mwaka 1992 NCCR-Ma-

    geuzi ilipoanza kutokana na Watanzania

    kuona haja ya mabadiliko ya Kikatiba.

    Niliwahi binafsi kukutana naye katika Kama-

    ti ya Katiba iliyoundwa na vyama mbalim-

    bali vya siasa. Mimi nikaonekana nafaa ku-wemo humo tutengeneze Katiba ambayo

    ingepelekwa Serikalini, lakini Serikali ilisema

    wakati bado.

    Rais Jakaya Kikwete wakati wa kuzindua

    Tume ya Katiba mwaka jana alimdhiha-

    ki Dk Mvungi kwa kumwambia alimkuta

    amejifungia katika hoteli moja Bagamoyo

    akitengeza Katiba. Akamwambia kwamba

    sasa kuwamo katika Tume ya Katiba ni fur-

    sa ya kutumia nguvu zake zote katika kazi

    hii mpya.

    Na kwa kweli sisi tulio ndani ya Tume tuna-

    kiri alitumia nguvu zake zote. Alikuwa tayari

    kufanya utafiti, kusoma makala ya ziada na

    hata kujitolea kwa lolote lile. Alitoa sulu-

    hu palipokwama, alitoa ushauri penye fun-

    do alimradi alichotaka ni kwamba mwisho

    Katiba ipatikane.

    Nilibahatika kufanya naye kazi kwenye

    Kamati iliyoaminiwa kuwa ngumu kuliko

    zote katika Tume. Humo ndiko nilikomjua

    zaidi na kustaladhi kufanya naye kazi. Kub-

    wa ni kuwa alikuwa mtu wa maridhiano. Ali-

    kuwa muda wote tayari kuuacha msimamo

    wake pindi akishawishiwa na alitafuta sulu-

    hu ili kuuridhia upande ulojisogeza.

    Tulimtania sana na yeye alikuwa na utani

    mwingi. Mimi sijawahi kufanya kazi katika

    Tume ya Kitaifa yoyote ile, lakini nimeona

    kazi katika Tume ya Katiba ilikuwa nyepesi

    kwa sababu ndani yake pamekuwa na nafa-si ya ubinadamu na zaidi watu wote wame-

    jifanya ni wa daraja moja na kwa hivyo

    wamejenga ukuruba. Mmoja aliyekurubiwa

    na kila mtu ni yeye Dk. Mvungi.

    Aliwahi kusema kwamba angetamani kus-

    hona suti ili aende katika Bunge la Katiba

    kutetea andiko la Tume ambalo alifanya kila

    njia liaminike na likubalike kwa sababu al-

    ijua huo ni mchango wake muhimu na ali-

    fanya kazi kana kwamba ndio kazi yake ya

    mwisho.

    Lakini hakuwahi kuivaa suti yake kama al-

    ivyokosa kuendelea kuwemo katika Treni yaKatiba ambayo inaelekea kituo chake cha

    mwisho. Ila wengi tunaamini japo hatutam-

    wona tena atakuwa akitusubiri kusherehek-

    ea na sisi Katiba Mpya katika zama mpya

    za Tanzania ambazo wanawe na wanetu

    wataishi nazo

    Wanachama wa NCCR - Mageuzi wakiwa wamebebajeneza lilohifadhi mwili wa Kiongozi wao Marehemu

    Mvungi, ambae pia alikuwa ni Mjumbe wa Tume yaMadiliko ya Katiba Mpya.

    BARAZA YA JUMBA MARO

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    18/21

    34 35

    HEKAYA ZA Z ANZIBAR

    Zanzibar Daima OnlineZanzibar Daima Online

    MEZA FUPABila ya kubaini, chembe

    ndogo ya wema

    uipandayo ardhini, huenda

    ikachipua na kutoa mti

    mkubwa utakaoweza

    kukupatia kivuli aukuwapatia wengine

    wakati wa jua kali la

    kiangazi.

    Bila ya kubaini, chem-

    be ndogo ya wema

    uipandayo ardhini,

    huenda ikachipua na kutoa

    mti mkubwa utakaoweza

    kukupatia kivuli au kuwap-atia wengine wakati wa jua

    kali la kiangazi.

    Ilikuwa ni safari ya mwendo

    mkubwa, walikuwa ni vijana

    watatu walioongozana kati-

    ka kukitafuta kijiji ambacho

    walipata kusikia kuwa aliishi

    bibi mwenye historia nzima

    ya nchi yao. Bibi aliyeishi mi-

    aka mia mbili, ndiye pekeye

    aliyeweza kutambua hali hal-

    isi ya nchi yao. Sio kama hai-kuwepo historia, lakini histo-

    ria iliyokuwepo ilipotoshwa

    na kuwaziba macho vijana

    waitwao kizazi kipya.

    Walilkuwa ni vijana watatu

    wenye umri kati ya miaka

    ishirini hadi thelathini. Aliyekuwa mstari

    wa mbele katika kuiandaa safari hii ali-

    kuwa ni Miftaha, kijana jasiri asiyeogopa

    kitu katika kuitafuta haki. Mwili wake ul-

    ionekana dhaifu kutokana na wembamba

    wake, alikuwa ni mweusi kidogo, hakuwamrefu sana ila wembamba wa umbile lake

    ulimfanya aonekane mrefu wa kimo.

    Wengine walikuwa ni Suheli na Maimuna.

    Wanaume wawili na mwanamke mmoja.

    Maimuna alikuwa ni ndugu yake Miftaha.

    Bi. Msiri alifanana na jina lake. Moyo wake

    uliyabeba mengi tena makubwa mithili ya

    dunia au sawa na umri wake. Miaka mia

    mbili kwa ulimwengu wa sasa utatolewa

    kwenye vyombo vya habari na kuingiz-

    wa katika kundi la watu wa maajabu. Huundio ulikuwa umri wa bibi huyu aliyeishi

    katika kiijiji cha Maukio. Pamoja na umri

    wake mkubwa, bibi huyu alikuwa na meno

    yote thelathni na mbili, macho yake yali-

    kuwa hayaoni tena vizuri lakini alikuwa na

    uwezo wa kusikia kama mtoto mdogo, si

    Hekaya za ZanzibarNa Ally Hilal

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    19/21

    36 37Zanzibar Daima OnlineZanzibar Daima Online

    rahisi kumsengenya ukiwa karibu yake.

    Alikuwa anatembea kwa tabu sana, alitem-

    bea kwa mkongojo wake uliochongwa vi-

    zuri, ulichorwa nakshi nzuri za msumeno na

    ulikuwa umeandikwa TUTAFIKAJE?

    Bi Msiri aliishi kando na mto mkubwa ul-

    iokuwepo katika bonde kubwa kijijini pale.

    Maisha yake yalikuwa ya upweke tangu al-

    ipokuwa na miaka ishirini baada ya kuipo-

    teza familia yake yote katika hali tata hadi

    leo hakuweza kuwaona tena.

    Alikuwa mtu wa mwanzo kuhamia kijiji

    hiki baada ya kukimbia mjini kwao na kuji-

    tokomeza katika bonde hili. Aliishi kwa tabu

    sana akiwa mafichoni huku ambako kuliku-wa mbali na mji aliotoka.

    Miaka ilivyozidi kusonga mbele, nyumba zili-

    sogea hadi kufika sehemu aliyoishi Bi Msiri.

    Ni historia ndefu ambayo hakuna aliyeijua,

    walioishi naye walikuwa hawajui chochote

    kuhusu bibi huyu, walimuona kuwa ni bibi

    wa kawaida tu asiyepungua umri wa miaka

    themanini kutokana na muonekano wake

    lakini hawakuujua umri halisi wa bibi huyu.Hakuwahi kuwa na rafiki wa karibu ambaye

    aliweza kubadilishana naye mawazo zaidi

    ya Bi Tausi aliyekuwa mkulima katika bonde

    hili, alikuwa na shamba lake mwenyewe.

    Linaweza likajengeka suali katika akili ya mtu

    kuhusu bibi huyu aliyejitenga na watu kwa

    miaka mingi na aliyebeba siri nzito moyoni

    mwake, suali jengine ni kuwa vipi Miftaha

    na wenzake waliujuwa uwepo wa bibi huyu

    na kwa ajili gani waliamua kumtafuta.

    Miftaha ni miongoni mwa vijana waliopata

    elimu, alisoma hadi chuo kikuu nje ya nchi,

    alibahatika kusomeshwa na serikali yake il-

    iyokuwa madarakani kutokana na nafasi ya

    baba yake, baba yake alikuwa mfuasi mkub-

    wa wa chama kilichokuwepo madarakani,

    hapakuwa na chama cha upinzani kwa sa-

    babu serikali iliogopa kupingwa na kukosa

    wafuasi iwapo wataendesha serikali yao

    kinyume na wanavyotaka wananchi. Pamo-

    ja na hayo wananchi wengi hawakukiunga

    mkono chama hiki, walikipinga chini kwa

    chini kwa kuhofia kukamatwa na kuishia

    gerezani. Pamoja na kwamba Miftaha al-iishi kwa baba yake, baba yake alikuwa ni

    mshauri wa raisi wa nchi, aliyajua mengi yal-

    iyokuwa yakitendeka nchini, lakini watoto

    wake wote wawili hawakukubaliana naye,

    kila siku waligombana na baba yao. Licha ya

    elimu yake, Miftaha hakuweza kupata na-

    fasi za juu serikalini kama ilivyokusudiwa na

    baba yake hapo awali, kusoma kwake nje

    ilikuwa ni kuandaliwa ili aweze kuingizwa

    katika mfumo wa serikali lakini alionekanana msimamo tofauti, kutokana na sababu

    hiyo alibaki kuwa mwalimu wa skuli.

    Siku moja alirudi mapema skuli kwa sababu

    kichwa kilikuwa kinamuuma, ilikuwa ni jioni

    saa kumi na moja kamili, alikutana na Bibi

    mmoja aliyechoka sana, mguu wake uliku-

    wa unavuja damu, alikuwa ametafunwa na

    nyoka, ilikuwepo gari moja tu inayokuja ku-

    toka kijiji alichoishi bibi huyu, ilikuja asubuhi

    na kuondoka jioni, alikuwa ni Bi Tausi, rafiki

    yake bi Msiri.

    Miftaha alisimama na kusogea pembeni al-

    ipokuwepo bibi huyu, alimuweka kwenye

    kibao cha baiskeli yake na kumpeleka hos-

    pitali.

    Hakuna aliyemjali mgonjwa, kila mmoja ali-

    jishuhulisha na kazi zake, baadhi ya waugu-

    zi walimtazama mgonjwa wa Miftaha kwa

    dharau bila ya kujali kuwa alikuwa katika hali

    mbaya kwani sumu ya nyoka ilikuwa inazidi

    kumuenea mwilini. Daktari wa zamu aliku-

    wa amekaa nje anasoma kitabu cha riwaya.Miftaha alitoka hadi nje baada ya kuambi-

    wa kuwa daktari wa zamu alikuwepo nje,

    alimkuta daktari amewacha kitabu na sasa

    anacheza karata na vijana wa mtaa. Ilimuu-

    ma sana kumuona daktari anacheza karata

    huku wagonjwa wakiumia bila ya matibabu,

    alimsogelea daktari na kumwambia kuwa

    kuna mgonjwa yuko hali mbaya.

    Alipata majibu ya kukatisha tamaa.

    Kijana mimi mwenyewe ni mgonjwa hapa,

    au hujui kama na sisi madaktari ni wagonj-

    wa na tiba yetu hatujaiona, vilio vyetu hav-

    isikilikani maana tuna sauti ndogo, ila nyinyi

    munataka tuvisikilize vilio vyenu, je vyetu

    avisikilize nani?

    Maneno haya alikuwa anayazungumza da-

    ktari kumwambia Miftaha bila ya kumtaza-

    ma aliyekuwa akizungumza naye.

    Kwa hiyo unataka kunambia kuwa wagon-

    jwa wetu tuwaache wafe?

    Yule daktari aliendelea kucheza karata na

    kumjibu Miftaha bila ya kumtazama usoni.

    Kufa! Mh! Sasa wewe unafikiri mimi unay-

    eniita daktari niko hai! Kwa lipi la kusema ni

    uhai, mimi ni maiti k wenenda!

    Muda ulizidi kupotea, Miftaha aliamua kuz-

    itawanya karata na kuuharibu mchezo, vi-

    jana waliokuwepo pale walipanda hasira na

    karibia kumrukia Miftaha, muda wote huo

    Daktari alikuwa hajamjua anayelumbananaye, alipoinua uso wake alimuona Maal-

    im Miftaha ambaye alikuwa ni mwalimu

    msaidizi wa skuli ya Mwendapole, alikuwa

    ni mwalimu wa watoto wa daktari, alipojua

    kuwa alikuwa ni mwalimu wa watoto wake

    aliomba radhi kwa kudai kuwa alikuwa ha-

    jamjua. Aliwatuliza vijana waliokuwa na ha-

    sira na kutaka wamuache mwalimu.

    Miftaha alitikisa kichwa na kuongozana nadaktari bila ya kumjibu kitu ingawa daktari

    alijifanya mchangamfu kwa lengo la ku-

    jizimuwa kwa maneno yake yaliyomkera

    Miftaha.

    Itaendelea.

    HEKAYA ZA Z ANZIBAR

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    20/21

    38 39Zanzibar Daima OnlineZanzibar Daima Online38

    KALAMU YA BIN RAJAB

    HOTELI MPYA YA NYOTA SABAKUFUNGULIWA MJI MKONGWE

    Na Ahmed Rajab Kalamu ya Bin Rajab

    Mapema mwakani hoteli mpya ita-

    funguliwa Mji Mkongwe. Inase-

    mekana kwamba hoteli hiyo ita-

    kuwa na hadhi ya nyota saba. Ikiwa ni kweli

    basi tunastahiki kujipigia makofi kwani niju-

    avyo ni kwamba duniani kuna hoteli moja tu

    yenye nyota saba; nayo imejibandika yeny-

    ewe hadhi hiyo ya kuwa ya nyota saba.

    Hiyo hoteli inayojigamba kwamba ni yenye

    nyota saba ni hoteli ya Burj al Arab iliyo Du-

    bai. Nijuavyo ni kuwa hata ya nyota sita iko

    moja tu duniani, nayo ni Hoteli ya Fullerton

    iliyoko Singapore.

    Bila ya kujiingiza katika mabishano ya iwapo

    ni kweli hoteli hiyo mpya ya Mji Mkongwe

    itakuwa ya nyota saba ni sahihi nadhani tu-

    kisema tu kwamba hoteli hiyo itakuwa ku-

    bwa na ya kisasa. Mapambo na nakshi za

    ndani ya hoteli ni za hali ya juu kabisa.

    Hoteli hiyo itayofunguliwa mwakani Mji

    Mkongwe itaendeshwa na Kundi la Ma-

    Burj Al Arab

  • 8/13/2019 Zanzibar Daima Online: Toleo la Saba

    21/21

    40 41KALAMU YA BIN RAJAB

    Zanzibar Daima Online Zanzibar Daima Online

    kampuni ya Melia yenye makao yake makuu

    Uhispania. Kweli sio sisi tuliotoa fedha za

    kuijenga kwa hivyo hatuwezi kusema kuwa

    ni yetu lakini iko kwetu.

    Hilo si fanikio dogo kwa sababu kampuni

    hiyo ya Uhispania kuamua kujenga hoteli

    aina hiyo Mji Mkongwe kunaashiria mengi

    kuhusu Zanzibar.

    Muhimu ni kwamba kampuni hiyo baada ya

    kuipima na kuitathmini hali ya mambo ilivyo

    Zanzibar imeona kwamba kuna usalama na

    utulivu wa kutosha kisiwani humu wa kuha-

    kikisha kwamba rasilmali yao wanayoileta

    Zanzibar haitokuwa hatarini.

    Walioijenga hoteli hiyo wanasema k wambaujenzi wake umefuata kanuni za kuuhifadhi

    Mji Mkongwe ambao umetangazwa na Shi-

    rika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi

    na Utamaduni (Unesco) kuwa ni moja ya Tu-

    rathi za Dunia.

    Hayo yote ni sawa. Lakini kuna mingine

    yaliyo mazito pia yanayostahili kuzingatiwa

    na waendeshaji wa hoteli hiyo ili isije ikawa

    chanzo cha mfarakano baina ya wakazi wa

    Unguja mjini, hasa wa Mji Mkongwe, na ho-

    teli yenyewe.

    Tunafahamu kwamba hoteli ya babu kubwa

    kama hiyo itahitaji iwe na wafanyakazi we-

    nye ujuzi mkubwa na uzoefu wa shughuli za

    utalii. Tunatambua kwamba huenda tusiwe

    na watu wa aina hiyo walio tayari kupatiwa

    ajira hotelini humo.

    Hata hivyo, tuna haki ya kuwauliza wakuu

    wa hoteli hiyo iwapo wameandaa mkakati

    wowote wa kuwafunza vijana wenyeji wa

    Mji Mkongwe shughuli za utalii ili wawezenao kupatiwa ajira humo badala ya kuajiri-

    wa watu kutoka nje ya Zanzibar.

    Ikifanya hivyo basi hoteli hiyo itasaidia ku-

    wapatia ajira vijana na hivyo kuwaingiza ka-

    tika jamii badala ya kuwatenga na itasaidia

    pia kuupiga vita umaskini na unyonyaji.

    Mwaka 1999, Jumuiya ya Umoja wa Mataifa

    ya Utalii Duniani (UNWTO) ilitunga kanuni za

    maadili kuhusu utalii ambazo zinatakiwa zi-

    fuatwe kote duniani. Kanuni hizo zina lengo

    la kupunguza athari mbaya zinazopata nchi

    na wana wa nchi, kutokana na shughuli za

    utalii.

    Kwa hakika, inatia moyo kuona kwamba

    mahoteli duniani siku hizi yanajihusisha na

    masala ya haki za binadamu na maadili ya

    kufanyia biashara. Katika muda wa miaka

    kumi iliyopita makampuni makubwa ya ho-

    teli yamechukua hatua muhimu za kuziun-

    ganisha sera za haki za binadamu na ku-ziingiza katika sera zao kuhusu maadili na

    namna ya kufanya biashara.

    Suala la maadili lina umuhimu mkubwa

    katika nchi kama ya kwetu yenye kufuata

    maadili ya Kiislamu. Utalii tunautaka lakini

    hatuutaki ikiwa utakuwa unazikanyaga mila

    zetu, dini yetu na ut amaduni wetu.

    Hapo ndipo penye hatari. Na hatari inaweza

    ikazuka mara moja iwapo hatuhakikishi ya

    kwamba wageni wenye kuendesha shughuli

    za utalii nchini mwetu hawendi kinyume na

    maadili yetu. Miongoni mwa wanayopaswa

    kuyafanya ni kuhakikisha kwamba haki za

    binadamu zinaheshimiwa na kwamba wa-

    toto wadogo wanapewa hifadhi na hawa-

    tumiwi kwa shughuli za kifisadi, kama kwa

    mfano za ngono, na wateja wa hoteli.

    Wakuu wa hoteli hiyo, pamoja na nyingine-

    zo zilizo Mji Mkongwe, wana wajibu wa ku-

    angalia namna gani wanaweza kuwasaidiawenyeji wa Mji Mkongwe sio tu katika ku-

    wapatia ajira lakini pia katika mambo min-

    gine ili wahisi kwamba hizo hoteli kweli ni

    sehemu ya jamii yao

    wa Kampuni ya Uwakala wa Mizigo ya Is-

    land Sea Food Limited, Mohammed Sule-

    iman Mussa (45) na Juma Ali Makame (34),

    walikamatwa siku ya tukio la kukamatwa

    kwa meno hayo ya tembo kwenye Bandari

    ya Zanzibar.

    Tayari watuhumiwa hao wamesafirishwa

    kwenda Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es

    Salaam kwa ajili ya mahojiano zaidi. Pamoja

    na mambo mengine, kusafirishwa kwa wa-

    tuhumiwa hao kwenda jijini Dar es Salaam,

    kunatokana na Zanzibar kutokuwa na sheria

    maalumu inayohusu wanyamapori.

    Maofisa wa Idara ya Wanyamapori nchini

    leo wamekamilisha kazi ya kuhesabu na ku-

    linganisha vipande 1,023 vya meno ya tem-

    bo vilivyokamatwa juzi kwenye Bandari ya

    Zanzibar na kubaini idadi ya tembo walio-

    uawa kuwa ni 305.

    Meno hao yenye uzito wa kilo 2,915 yenye

    thamani ya dola 4,775,000 sawa na Sh

    7,480,125,000 za Tanzania, yalikamatwa

    Inatoka Uk. 25 WATUHUMIWA MENO YA TEMBO WAONGEZEKAjuzi yakiwa yamehifadhiwa katika magu-

    nia 98 na kuwekwa kwenye kontena moja

    la futi 40 lenye namba PCIU 857619/0 li-lilokuwa tayari kupakiwa kwenye meli ya

    MV Kota Henning kupelekwa nchini Ufili-

    pino kwa magendo.

    Hadi sasa bado makachero wa Polisi wa

    Kimataifa (Interpol) nchini kwa kushirikia-

    na na makachero wa Polisi Zanzibar, Idara

    ya Wanyamapori makao makuu wanaen-

    delea na upelelezi kuwabaini waliohusika

    na kashfa hiyo.

    Jana Kamishna wa Polisi Zanzibar (CP)

    Mussa Ali Mussa, alisema kuwa kazi ku-bwa iliyobaki ni kuhakikisha upelelezi wa

    kina unafanyika ili kuwakamata wahusika

    wa mtandao huo.

    Alisema hadi sasa Jeshi la Polisi bado li-

    namsaka tajiri aliyewezesha mipango ya

    kukusanywa na kusafirisha shehena hiyo

    kutoka Tanzania Bara hadi Zanzibar ili ku-

    safirishwa nje ya nchi