Upload
dangdat
View
653
Download
17
Embed Size (px)
Citation preview
Joining Instructions Kiss 2017 Email: [email protected] Page 1
بسم هللا لرحمن الرحيم
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
Maelekezo ya Kujiunga na Kidato cha Kwanza
Mwaka 2017.
Soma kwa makini taarifa na maelekezo juu ya shule kisha uthibitishe
kukubali nafasi hii kwa kulipa mkupuo wa kwanza wa ada kabla ya
tarehe 22/12/2016. Ada isipolipwa katika muda uliotajwa, nafasi
itatolewa kwa mwanafunzi mwingine. Shule itafunguliwa tarehe
31/12/2016.
Utangulizi
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni Shule ya Kiislamu
inayotazama elimu kuwa ni jambo la kwanza na muhimu kwa
mwanadamu. Tunajifunza katika Qur’an kuwa Nabii Adam (a.s) kabla
hajaletwa hapa ulimwenguni kwa kazi yake ya ukhalifa (uongozi),
alielimishwa kwanza kuhusu mazingira yake (Rejea Qur’an, (2:31). Vile
vile tunajifunza kuwa Mtume wa mwisho Muhammad (s.a.w) kabla
hajaanza kazi yake kubwa ya kuhuisha uislamu alipewa kwanza amri
ya kusoma (rejea Qur’an 96:1-5).
Mtume (s.a.w) akasisitiza kuwa ni faradhi (lazima) kwa kila muislamu
mwanamume na kila muislamu mwanamke kutafuta elimu. Pia Mtume
(s.a.w) amesisitiza kuwa elimu itafutwe hata ikibidi ifungiwe safari ya
mbali (Uchina).
Tunalojifunza kutoka katika Qur’an na hadithi sahihi za Mtume (s.a.w)
ni Kuwa, kwanza elimu ni zana ya kwanza ya msingi ambayo muislamu
hana budi kuwa nayo ili aweze kuishi maisha ya kiislamu na awe
Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa duniani.
Pili, tunajifunza kuwa katika uislamu hapana ubaguzi wa elimu ya
dunia na elimu ya akhera.Kila fani ya elimu inayomwezesha
mwanadamu kufikia lengo la kuwa Khalifa wa Allah (s.w) hapa duniani
ni faradhi (wajibu/lazima) kwa waislamu wote.
Joining Instructions Kiss 2017 Email: [email protected] Page 2
1. LENGO LA SHULE:
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ina malengo ya jumla
yafuatayo:
(i) Kuwaelimisha na kuwalea vijana wa kiislamu kuanzia kidato
cha kwanza hadi kidato cha sita.
(ii) Kuwaandaa vijana kuwa viongozi (Makhalifa) wa kutegemewa
na jamii ya Kiislamu na Taifa kwa ujumla. Ili kufikia malengo
haya shule hii inatoa mafunzo katika kiwango cha kawaida
(O’Level) na kiwango cha juu (A’ Level).
Masomo yanayofundishwa kwa (O’level) ni:
(1)
(2) Qur’an
(3) Lugha ya kiarabu.
(4) English Language
(5) Kiswahili
(6) History
(7) Geography
(8) Basic Mathematics
(9) Pysics
(10)Chemistry
(11)Biology
(12)Commerce
(13)Book Keeping
(14)Civics
(15) Computer Applications
2. MAHALI SHULE ILIPO:
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ipo wilaya ya SAME, Mkoani
Kilimanjaro. Ukitokea Dar es Salaam au Tanga shule ipo kati ya
Makanya na SAME mjini umbali wa kilometa kumi (10 km) kabla ya
kufika Same Mjini. Ukitokea Moshi shule ipo kilometa kumi baada ya
kupita SAME mjini. Kutokea Kilipo kibao cha shule hadi shuleni ni
umbali wa kilometa 1.4.
Kwa maelezo zaidi fika Juhudi Studio SAME Mjini mkabala na benki
ya NMB.
Elimu ya Dini ya kiislamu.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
4. USAFIRI:
Wanafunzi watajitegemea kwa usafiri wa kuja shuleni na kurudi
nyumbani wakati wa likizo. Uongozi wa shule utahusika kuwafanyia
mpango wa usafiri wa pamoja ili kutafuta nafuu ya gharama na usalama
wa watoto na hasa wakati wa kufunga shule kwenda likizo
5. ADA YA SHULE :
Ada ya shule kwa mwaka 2017 ni Tshs 1,850,000/=(milioni moja na
laki nane na elfu hamsini tu.)
Ada italipwa kwa mikupuo miwili;
a) Mkupuo wa kwanza Tshs 1,000,000 kabla ya tarehe
24/12/2016.
b) Mkupuo wa pili Tshs 850,000/= kabla ya tarehe za mwanzo
za muhula wa pili 2017.
Ada ya shule, na pesa za matumizi (Pocket money) zitalipwa kupitia
benki.
Majina ya benki, namba za A/c na jina la A/c ni kama ifuatavyo:
(i) Benki ya AMANA A/C No: 005120109690001 kwa jina la
Kirinjiko Islamic Secondary School.
(ii) Benki ya NMB A/C No: 40503500042. kwa jina la Kirinjiko
Islamic Secondary School.
Mambo muhimu ya kuzingatia juu ya malipo:
(a) Wazazi/Walezi wanaoishi au wanaosafiri katika miji yenye
matawi ya Amana Bank, yaani Dar Es salaam, Arusha, Mwanza
n.k wanatakiwa kufanya malipo kupitia Benki ya Amana.
(b) Stakabadhi(receipt) za malipo yote zitaandikiwa shuleni
Kirinjiko Islamic tu.
(c) Nakala kivuli (Photocopy) ya Pay-in-slip haitapokelewa kwa
sababu zozote zile.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(d) Malipo yakishafanyika hayatarudishwa kwa sababu yoyote ile.
(e) Malipo ya ada lazima yapitie Benki.Fedha taslim
hazitapokelewa shuleni kwa sababu yoyote ile.
(f) Mwisho wa kulipa mkupuo wa kwanza wa ada ni tarehe
24/12/2016. Kulipa mkupuo wa kwanza wa ada ndio
kuthibitisha kukubali nafasi. Kwa hiyo baada ya tarehe tajwa,
kwa mzazi ambaye atakuwa hajafanya malipo haya nafasi ya
mtoto wake itatolewa kwa mhitaji mwingine.
(g) Pay-in-slip ya ada na pocket money ziwe tofauti. Pay-in-slip
iandikwe/ziandikwe jina la mwanafunzi anayelipiwa na
kidato anachosoma ili kuondoa usumbufu unaoweza kujitokeza
(Mfano: 1.Ada ya Ahmed Ally- Form ID. 2.Pocket money ya
Amina Juma -Form IA).
(h) Baada ya kulipa, Tafadhali wasilisha nakala halisi (original)
Pay-in-slips kwa Mhasibu wa shule ili kupatiwa stakabadhi ya
malipo (receipt).
(i) Wanafunzi watakaokuja na pesa za matumizi wanatakiwa
kuziwasilisha kwa Mhasibu na kupatiwa stakabadhi. Upo
utaratibu maalum uliowekwa na shule wa kuwapatia fedha
hizi pale watakapozihitaji kwa matumizi.
(j) Mwanafunzi haruhusiwi kukaa na zaidi ya shs 5,000/-
bwenini.
(k) Shule haitahusika na upotevu wa aina yoyote wa fedha za
mwanafunzi.
6. SARE ZA SHULE
(A) Sare ya Darasani
i) Wavulana
1) Suruali 2 rangi ya “light blue”
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
2) Nusu kanzu nyeupe; urefu wa kufika magotini, mikono mirefu,
Isiyopasuliwa na isiyo na kola.
3) Kofia mbili nyeupe zisizokuwa na urembo wa aina yoyote na ziwe za
kitambaa sio za kufuma kwa nyuzi.
4) Viatu vyeusi vya ngozi vya kufunga kamba, unene wa soli
ya viatu usizidi nchi mmoja (1 inch), soksi nyeusi au dark blue.
ii) Wasichana
1) Nusu kanzu mbili (light blue), ndefu zenye mikono mirefu isiyo
na mifuko.
2) Suruali (pajama) 2 za rangi ya light blue.
3) Shungi (juba) 2 nyeupe kubwa ya duara yenye urefu wa
Kufika magotini.
4) Baibui 2 (pana na ndefu) zenye rangi ya zambarau. Aina ya
zambarau inayokusudiwa ni ile tu inayotambulika na kushonwa
shuleni. Ili kuepusha kuharibu vigezo vya sare yetu wanafunzi wote
watashonea sare zao shuleni.
5) Viatu vyeusi vya ngozi vya kufungwa kwa kamba, unene wa soli
ya viatu usizidi nchi moja (1 inch) vifunike miguu,na soksi za dark
blue au nyeusi.
Angalizo:
Mwanafunzi hataruhusiwa kuingia darasani na ikibidi anaweza
kurudishwa nyumbani iwapo atakiuka utaratibu wa sare ya shule hata
kwa kipengele kimoja.
(B) Sare za Nje ya Darasa
(a) Wavulana
i). Suruali 2 nyeusi (siyo Jeans, Lee, wala Corduroy) zilizoshonwa kwa
mshono wa suruali za kawaida na isiyobana.
ii). Fulana 2 za rangi ya dark blue, zenye nembo ya shule
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
iii) Kanzu nyeupe
iv) Track-suit nyeusi au Dark bluu na raba kwa ajili ya
michezo/mazoezi.
v) Jacket/sweta lenye rangi ya dark blue au nyeusi lisilo na picha wala
maandishi yoyote kwa ajili ya matumjzi ya kipindi cha baridi.
vi) Gun boot za kawaida.
(b)Wasichana
i). Gauni refu la mikono mirefu la rangi ya damu ya mzee lisilopasuliwa,
lisiloungwa na lisilokuwa na mikunjo kiunoni.
ii). Pajama ya rangi ya damu ya mzee.
iii). Ushungi mkubwa wa mviringo (juba), urefu wa kufika magotini wa
rangi ya damu ya mzee.
iv). Kitenge jozi moja. Kanga hairuhusiwi shuleni.
v). Nguo za michezo: Track suit dark blue au nyeusi na pana kiasi na
fulana isiyobana (dark blue au nyeusi) ya mikono mirefu.
vi). Nguo za kulalia (night dress) – shumizi ndefu 2.
vii) Gun boot za kawaida.
Zingatia:
i) Zaidi ya sare, mwanafunzi hataruhusiwa kuwa na nguo nyingine
yoyote.
ii) Nguo yoyote inayobana au inayoonesha ndani (transparent) au
iliyoshonwa kinyume na maagizo haitakubaliwa kama sare ya shule.
iii) Hairuhusiwi kwa wanafunzi kuvaa mapambo ya aina yoyote wakiwa
shuleni au nje ya shule (likizo) wakati bado ni mwanafunzi wa shule
hii.
iv) Mwanafunzi atakayekiuka utaratibu huu na kuthibitishwa na
uongozi wa Shule, atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni
pamoja na Kunyang’anywa mapambo hayo na hatarudishiwa.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Muhimu:
Ili kuondoa tatizo la kutofautiana kwa rangi za vitambaa na muundo
wa Sare za shule; sare zote za shule zitashonwa hapa shuleni kwa
gharama zilizotajwa kwenye kifungu namba saba (7) (Gharama za
mashono).
7. GHARAMA ZA MASHONO YA SARE ZA SHULE
(A)Sare za Darasani
(i) Wavulana
1. Suruali 1
2. Nusu kanzu 1 Jumla = 30,000.
3. Kofia 1
(ii)Wasichana
1. Baibui 1
2. Pajama 1 Jumla = 30,000/=
3. Nusu kanzu 1
4. Ushungi (Juba) 1
Sare za Nje
(i)Wavulana
1. Suruali nyeusi @ 13,000/= Jumla = 25,000/=
2. Fulana @ 12,000/=
(ii)Wasichana
1. Gauni damu ya mzee 1
2. Pajama 1 Jumla = 27,000/=
3. Ushungi 1
Muhimu:
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(i) Vipimo vya sare vitafanyika hapa shuleni.
(ii)Malipo ya sare za shule yatafanyika hapa shuleni kwa Mhasibu wa
shule.
8. VIFAA VYA MASOMO
Mwanafunzi atalazimika kununua vifaa vyote vya masomo
vinavyohitajika kama vile :
(a) Madaftari makubwa (counter books) ya kila somo. Madaftari ya saizi
ya kati (3Quires) yenye nembo ya shule yanapatikana kwa Tshs 2,5000.
(b) Kalamu na mkebe wa vifaa vya hisabati (Mathematical set).
(c)Licha ya uwepo wa maktaba ya shule, kila mwanafunzi anashauriwa
kujinunulia vitabu vinavyohusiana na masomo yake ili aweze
kujisomea kikamilifu akiwa ndani na nje ya shule.
(d)Kila mwanafunzi aripoti shuleni akiwa na Jalada(Box file) la
kutunzia mitihani na majaribio.
( e) Graph paper pad.
9. VIFAA VYA BWENI:
(i) Godoro la upana wa futi mbili na nusu ( ft x3 lnch). Ili kuondoa
tatizo la kusafiri na magodoro,magodoro yanapatikána hapa shuleni
kwa Tshs 30,000/=.
(ii) Shuka mbili za rangi ya pink pia zinapatikana shuleni kwa Tsh
12,000/= @ Ths 6,000/=.
(iii) Mto na foronya mbili.
(iv) Taulo na blanketi.
(v) Chandarua chá pembe nne. Vyandarua vinapátikana shuleni kwa
Tsh 9,000/=.
(vi) Sabuni za kutosha za kufulia (za unga) na za kuogea.
(vii) Vyombo vya chakula; sahani, bakuli, kikombe, na kijiko. Sahani
na bakuli visiwe vya udongo (nunua stainless steel au pembe).
(viii) Begi kwa ajili ya kuhifadhia vitabu na vitu vingine.
212
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(ix) Ndoo ya kuhifadhia maji.
Zingatia:
Sanduku la chuma (tranker) HALIRUHUSIWI shuleni.
Muhimu:
Mwanafunzi atakapoacha, kufukuzwa au kuhama shule vifaa vyake
kama vile godoro, begi n.k ataondoka navyo. Pindi atakapoviacha, shule
haitakuwa na dhamana ya vifaa hivyo.
10. UANDIKISHWAJI
Siku ya kuripoti shuleni, mwanafunzi awe na vifaa vifuatavyo:
(i) Fomu za Utambulisho wa mwanafunzi na wazazi/walezi wa
mwanafunzi zikiwa zimejazwa na kubandikwa picha.
(ii) Fomu ya daktari (Medical Examination form). Kama mwanafunzi
ana matatizo maalum ya kiafya maelezo ya daktari
yaeleze tahadhari anazotakiwa kuchukua akiwa shuleni.(kiambatis
ho B).
(iii) Fomu ya wajibu wa mzazi/mlezi (kiambatisho C)
(iv) Fedha za kitambulisho TSh. 5,000/=
(v) Pay-in-slip ya malipo ya ada.
(viii) Kitabu-Mwongozo wa mafanikio katika Elimu(Supu ya Elimu)
Shilingi 12,000.
(ix) Msahafu wa tafsiri ya Kiswahili wenye tangulizi za sura wa
(Abdullah Saleh Al
Farsy).Kwa shuleni unapatikana kwa Tshs. 15,000/=.
(x) Kitabu cha kwanza Elimu ya Dini ya Kiislam.Tshs.9,000/=
(xi) Kitabu cha Riyadh Swalihina (Tafsiri ya Kiswahili) Tsh 20,000/=
(xii) Kitabu cha dua na adhkar (HisnulMuslim) cha kiarabu-
Kiswahili.Tsh.2,000.
(xiii) Kitabu cha Lugha ya Kiarabu kidato cha 1 sh.5,000/=
MUHIMU;
• Mwanafunzi atakayeshindwa kukamilisha mahitaji
hatapokelewa.
11. MAENDELEO YA DARASANI.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Kila mwanafunzi anatakiwa kufanya bidii katika masomo yake kwa
kuhudhuria vipindi vyote, kufanya kazi za darasani katika kila
kipindi, kufanya majaribio na mitihani yote inayotolewa shuleni,
kutumia maktaba ya shule kujisomea vitabu na majarida mbalimbali
ya kielimu ili kujiongezea maarifa zaidi.
Ili kufaulu kuingia kidato kingine, mwanafunzi anatakiwa afikishe
wastani wa angalau alama 50 (daraja C) au zaidi na crediti 7 au zaidi
katika masomo yake yote anayosoma. Crediti ni madaraja C, B na A.
12. KAZI ZA NJE YA DARASA.
Kujibidiisha katika kazi ni katika nidhamu ya kiislamu. Hivyo, kila
mwanafunzi atawajibika kushiriki kikamilifu katika kutenda kazi za
usafi wa mazingira, ujenzi na kazi nyinginezo kama atakavyoelekezwa
na walimu au viongozi wa wanafunzi. Kutegea kazi, iwe ya darasani au
nje ya darasa ni kukiuka maadili anayotarajiwa awe nayo mwanafunzi
wa shule hii na haitavumilika.
13. NIDHAMU
Shule hii ni ya Kiislamu. Hivyo mwenendo wa wanafunzi na
wafanyakazi wake unatarajiwa uwe wa kiislamu. Kukiuka maadili ya
kiislamu kwa mujibu wa Qur’ani tukufu na Sunnah sahihi za Mtume
(S.A.W) ni sawa na kukiuka maadili ya shule. Mwanafunzi yeyote
atakayekiuka kwa makusudi kanuni na mwenendo bora wa shule,
atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
14. KANUNI NA MWENENDO BORA WA SHULE
(i) Kila mwanafunzi wa shule hii anapaswa kutambua kuwa yupo hapa
kwa ajili ya Uislamu. Kwa sababu hiyo chochote kilichopo nje ya
Uislamu hakina nafasi katika shule hii, kiwe kwa maneno au kwa
vitendo.
(ii) Kila mwanafunzi atakuza pendo lake kwa Allah (s.w) na mtume
wake(s.a.w), dini yake na waumini wenzake.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Pamoja na haki za muumba zilizo juu ya kila Muislam, yamwajibikia
kila mwanafunzi achunge haki na nafasi yake na atumie vipaji vyake
katika uchamungu ndani na nje ya shule.
(iii) Kila mwanafunzi atatumia muda wake vizuri katika
kujielimisha kwa ajili ya Allah (s.w) ikizingatiwa kuwa
kujielimisha kwa ajili ya Alla(s.w) ni amri ya kwanza kwa
kila muislamu.
(iv) Kila mwanafunzi atalazimika kuhudhuria kila kipindi cha
somo, kufanya mazoezi, majaribio ya kila somo na mitihani
yote itakayotolewa shuleni. Mwanafunzi atakayeshindwa
kuhudhuria darasani mfululizo kwa siku tatu au zaidi bila
sababu yoyote ya msingi, atakuwa amejifukuzisha shule.
(v) Kila mwanafunzi anapaswa kuzingatia na kufuata ratiba na
utaratibu wa shule kikamilifu. Ni kosa kubwa kutoonekana
katika eneo husika kwa mujibu wa ratiba kama vile;
kuonekana bwenini wakati wa masomo. Wanafunzi wagonjwa
wanapaswa kuripoti kwa mwalimu wa zamu na darasa ili
wapewe kibali cha kwenda zahanati.
(vi) Wakati wote wa kuja shule au wakati wa kurudi nyumbani,
vazi rasmi ni sare ya shule ya darasani. Kutokuwa na sare
katika wakati huo ni kosa lisilovumilika.
(vii) Wanafunzi wote wanatakiwa wavae nguo za Kiislamu wakiwa
ndani na nje ya shule. Wasichana wavae nguo za kuenea mwili
mzima isipokuwa uso na vitanga vya mikono rejea Qur-an
{24:31}.
(viii) Ni marufuku kwa mwanafunzi wa jinsia yoyote kuvaa
mapambo wakati akiwa shuleni na nje ya shule.
a. Wavulana wavae nguo za heshima na zisizo na maandishi au
picha ya aina yoyote. Hairuhusiwi kuvaa kaptura, jeans, msuli
au carwash katika maeneo ya shule.
b. Hairuhusiwi kwa wasichana kuvaa nguo za kubana, fupi au
zinazoonesha ndani (Transparent) akiwa shuleni au nje ya
shule.
(ix) Ni marufuku kwa mwanafunzi yeyote kufuga kucha, kujipaka
rangi za kucha, rangi za midomo, kupaka hina, kunyoa nyusi,
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
kupaka wanja, kutumia manukato kwa wasichana, kuvaa viatu
vya kuchuchumia au vinavyotoa sauti, kukali nywele, kutia
rangi, kusuka rasta au kubadilisha nywele, kucha,kope au
ngozi kwa namna yoyote ile na kufuga nywele kwa wavulana.
Angalizo:
Kwa wasichana itakapobidi kutumia manukato watatumia Nivea ya kupaka kwapani tu (Rolling)ambayo harufu yake ataihisi mpakaji mwenyewe.Ama body spray na manukato ya aina zote ni makosa kukutwa nayo.
(x) Ni marufuku mwanafunzi kuchochea, kushawishi,
kuhamasisha,au kushiriki mgomo kwa namna moja au nyingine
hata kama kuna sababu za msingi. Ni kosa kubwa kugomea amri
au maelekezo ya viongozi wa serikali ya wanafunzi, walimu na
uongozi wa shule kwa ujumla.
(xii) Mwanafunzi asionekane katika vilabu vya pombe, nyumba za
Kupangisha wageni (Guest house), kumbi za dansi na sinema.
(xiii) Kila mwanafunzi ni mlinzi wa mali ya shule, mali yake binafsi
na ya wenzake. Mwanafunzi atakayeharibu,
kusababisha mali ya shule kuharibika, kuibiwa au kupotea
atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kulipa.
Hivyo mwanafunzi atakapogundua wizi au uharibifu wowote dhidi
ya mali ya shule au ya mwanafunzi mwingine atoe taarifa kwa walimu
au viongozi wanaohusika mara moja.
(xiv) Kuiba ni kosa kubwa, mwanafunzi atakayethibitika kuiba mali
ya shule au mwanafunzi mwenzake au nje ya shule atachukuliwa
hatua kali za
kinidhamu ikiwa ni pamoja na kufukuzwa shule.
(xv) Mwanafunzi anapokuwa na shida yoyote hapa shuleni, kwanza
aanze kwa viongozi wanafunzi na ndipo aende kumuona mwalimu wa
zamu au wa Darasa lake, au walimu wengine wanaohusika. Kama
mwanafunzi baada ya kufuata ngazi hizo shida yake haijatatuliwa,
aende kwa Makamu Mkuu wa shule, kisha kwa Mkuu wa shule
itakapobidi kufanya hivyo Mwanafunzi asishitakie shida zake nje ya
shule kabla hajamuona Mkuu wa shule.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(xvi) Kila mwanafunzi anatakiwa awe msafi wakati wote, ashiriki
vyema katika usafi wa mwili wake binafsi; kitanda, nguo, nywele,
kucha, na usafi wa madarasa, bweni,bwalo la chakula na mazingira ya
shule kwa jumla.
(xvii) Kelele za aina yoyote hazitaruhusiwa, ziwe darasani, kwenye
baraza za madarasa, ndani ya bweni, au popote iwe kwa mwanafunzi
mmoja au wengi (kundi). Tunalazimika kuonesha maadili ya Kiislalmu
katika mazungumzo yetu yote.(Rejea Qur’ani 31:19)
(xviii) Shule haimruhusu mwanafunzi kutoka ndani ya shule na
kulala nje ya eneo la shule bila ya kibali maalum cha maandishi
kilichoidhinishwa na Mkuu wa shule.
Wakati wa mapumziko mafupi (mid-term break) wanafunzi
watabakia katika eneo la shule.Hawataruhusiwa kwenda
nyumbani.
(xix) Mwanafunzi hatakiwi kulala au kwenda katika nyumba za
watumishi isipokuwa kwa dharura maalum itakayoidhinishwa na
Mkuu wa shule.
(xx) Wanafunzi wa jinsia tofauti hawaruhusiwi kuchanganyika katika
jambo lolote bila ya uangalizi wa mwalimu iwe faragha au bayana,
kufanya hivyo ni kosa la kukaribia zinaa ambalo adhabu yake ni
kufukuzwa shule.
(xxi) Kupigana ni kosa kubwa. Mwanafunzi atakayepigana au kumpiga
mwenzake atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
(xxii) Mwanafunzi anapaswa kuripoti shuleni katika tarehe na muda
uliopangwa baada ya likizo, atakapochelewa kwa dharura, taarifa
itolewe kwa Mkuu wa Shule kabla ya kufunguliwa shule, na baada ya
hapo aje na mzazi/mlezi wake anaetambulika kiofisi ndani ya siku
saba (7) baada ya shule kufunguliwa, atakayechelewa zaidi ya hapo
bila taarifa shule haitakuwa na dhamana naye.
(xxiii) Wazazi wa wanafunzi wanaruhusiwa kuwatembelea wanafunzi
(watoto wao)
shuleni siku za Jumapili tu ya kila mwisho wa mwezi. Hata hivyo
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
kutokana na uhaba wa makazi shuleni, shule haitahusika
kumpatia mzazi/mlezi malazi atakapomtembelea mwanae.
(xxiv) Wakati wa kuwatembelea wanafunzi, mzazi/mlezi haruhusiwi
kuleta vyakula au vinywaji vya aina yoyote kwa mwanafunzi. Vifaa
vitakavyoletwa kwa wanafunzi vikabidhiwe kwanza kwa mwalimu wa
zamu/darasa ili vikaguliwe.
(xxv) Zaidi ya mashine ya kufanyia hesabu (calculator), vifaa vyote
vya electronics kama vile simu, camera, radio, radio cassette n.k
haviruhusiwi mwanafunzi kuwa navyo katika mazingira ya shule.
Mwanafunzi atakayekutwa navyo vitu hivyo hapa shuleni, atapewa
adhabu kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa shule na havitarudishwa.
(xxvi Ni kosa kwa mwanafunzi kukaa na pesa taslimu bwenini
zinazozidi Tsh 5,000/=. Pesa zote zihifadhiwe kwa Mhasibu wa
shule. Kutakuwa na utaratibu wa kuchukua pesa kiasi kidogo kwa
ajili ya matumizi.
(xxvii) Shule imetenga maeneo maalum kwa ajili ya michezo.Hivyo ni
marufuku mwanafunzi kukutwa anacheza mpira na michezo mingine
ya kutimua vumbi na kushawishi kelele za kishabiki na mfano wake
katika maeneo yanayozunguka bweni,darasa na maeneo mengine mfano
wa hayo nje ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya michezo.
(xxviii) Swala ni nguzo kuu ya kumtambulisha mtu kuwa ni muislamu
na ufunguo wa milango ya mafanikio. Hivyo shule haitamvumilia
mwanafunzi yeyote atakayeonekana kupuuza swala kwa makusudi hata
kama ni kwa tabia ya kuchelewachelewa na kukosa jamaa msikitini.
(xxix) Mbali na mzazi kuruhusiwa kumtembelea mtoto wake na kujua
maendeleo yake kitaaluma na kitabia kila Jumamosi na Jumapili
ya mwisho wa mwezi, pia anakaribishwa shuleni au kuwasiliana
na uongozi wa shule wakati wowote kwa lengo la kuleta ufanisi kwa
mwanae na jamii ya waislamu kwa
ujumla.
15. MAKOSA YANAYOWEZA KUSABABISHA KUFUKUZWA SHULE.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Pamoja na maelezo yote hayo, mwanafunzi atakayechupa kwa makusudi
mipaka ya Uislamu na kuvunja maadili na kanuni za shule kwa
kutenda makosa makubwa kama yalivyoainishwa atafukuzwa shule;
(1) Kunywa pombe.
(2) Kwenda nyumba za starehe kama vile kwenye kumbi za
madansi, disko n.k
(3) Uzinzi au kukaribia zinaa kwa kuwa na rafiki wa jinsia
tofauti (boy Friend/girl friend).
(4) Kuvuta bangi, sigara, madawa ya kulevya, n.k
(5) Kutosimamisha swala
(6) Kumiliki vitu vya electronics kama simu au line, redio,
kamera n.k
(7) Kukaa nje ya shule kwa muda wa siku 3 bila kibali maalum
kilichoidhinishwa na Mkuu wa shule.
(8) Kuanzisha, kuchochea, kushiriki au kuongoza mgomo.
(9) Kuhatarisha amani ya shule kwa kupigana au kuchochea
watu wapigane.
(10) Wizi, uporaji na uharibifu wa mali ya shule na ya
wanafunzi au wakazi wa kituo.
(11) Kukosa mitihani/jaribio bila ya sababu za msingi.
(12) Kutohudhuria masomo/darasani bila sababu maalumu za
msingi.
(13) Kujirudiarudia katika makosa ya uvunjifu wa kanuni na
mwenendo bora wa shule.
16. HITIMISHO
Ni matumaini yetu kuwa Mzazi/ Mlezi na mwanafunzi mtarajiwa
mmeyasoma maelekezo haya vizuri na kwa makini na kuyaelewa
vilivyo.
Mwanafunzi unatakiwa kuzingatia na kutekeleza maelekezo yote ili
kuepusha usumbufu.
Mzazi/Mlezi anashauriwa kujitahidi kushirikiana na shule kwa
kutekeleza wajibu wake kikamilifu ikiwa ni pamoja na kulipa ada kwa
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
wakati na kumsimamia mwanae katika maadili ya Kiislamu hasa
wakati wa likizo.
Kirinjiko Islamic Secondary School ni shule yenye mazingira mazuri
sana ya kusoma na malezi ya maadili mema ya kiislamu.
TUNAKUTAKIA MAANDALIZI MEMA NA KARIBU
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL, KAMA
MWANAFAMILIA MPYA WA KIRINJIKO.
Kauli mbiu: “Soma kwa jina la Mola wako Aliyeumba”(96:1).
MKUU WA SHULE.
2017.
Wabillah Tawfiiq.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
الرحيمبسم هللا لرحمن
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
Maelekezo ya Kujiunga na Kidato cha Kwanza
Mwaka 2017.
Soma kwa makini taarifa na maelekezo juu ya shule kisha uthibitishe kukubali nafasi hii kwa kulipa mkupuo wa kwanza wa ada kabla ya tarehe 22/12/2017. Ada isipolipwa katika muda uliotajwa, nafasi itatolewa kwa mwanafunzi mwingine. Shule itafunguliwa tarehe 30/12/2018.
1.Utangulizi.
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni Shule ya Kiislamu inayotazama elimu kuwa ni jambo la kwanza na muhimu kwa mwanadamu. Tunajifunza katika Qur’an kuwa Nabii Adam (a.s) kabla
hajaletwa hapa ulimwenguni kwa kazi yake ya ukhalifa (uongozi), alielimishwa kwanza kuhusu mazingira yake (Rejea Qur’an, (2:31). Vile vile tunajifunza kuwa Mtume wa mwisho Muhammad
(s.a.w) kabla hajaanza kazi yake kubwa ya kuhuisha uislamu alipewa kwanza amri ya kusoma (rejea Qur’an 96:1-5).
Mtume (s.a.w) akasisitiza kuwa ni faradhi (lazima) kwa kila muislamu mwanamume na kila muislamu mwanamke kutafuta elimu. Pia Mtume (s.a.w) amesisitiza kuwa elimu itafutwe hata ikibidi ifungiwe safari ya mbali (Uchina).
Tunalojifunza kutoka katika Qur’an na hadithi sahihi za Mtume (s.a.w) ni Kuwa, kwanza elimu ni zana ya kwanza ya msingi ambayo muislamu hana budi kuwa nayo ili aweze kuishi maisha ya kiislamu na
awe Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa duniani. Pili, tunajifunza kuwa katika uislamu hapana ubaguzi wa elimu ya dunia na elimu ya akhera. Kila fani
ya elimu inayomwezesha mwanadamu kufikia lengo la kuwa Khalifa wa Allah (s.w) hapa duniani ni faradhi (wajibu/lazima) kwa waislamu wote.
2. LENGO LA SHULE: KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ina malengo ya jumla yafuatayo:
(i) Kuwaelimisha na kuwalea vijana wa kiislamu kuanzia kidato cha kwanza hadi kidato cha sita. (ii) Kuwaandaa vijana kuwa viongozi (Makhalifa) wa kutegemewa na jamii ya Kiislamu na Taifa
kwa ujumla. Ili kufikia malengo haya shule hii inatoa mafunzo ya elimu ya sekondari ngazi ya
awali (O’Level) na elimu ya sekondari ngazi ya juu (A’ Level).
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Masomo yanayofundishwa kwa (O’level) ni: 1. Elimu ya diniya kiislam 2. Qur’an 3. Lugha ya kiarabu. 4. English Language 5. Kiswahili 6. History
7. Geography 8. Basic Mathematics
9. Pysics 10. Chemistry 11. Biology 12. Commerce 13. Book Keeping 14. Civics 15. Computer Applications
S/N TITLE PUBLISHER/AUTHOR FORM I
1 History for Secondary Schools Longhorn 8500
2 Kiswahili Shule za Sekondari Oxford 9000
3 Secondary English Oxford 10000
4 Geography For Secondary Schools Azika Juma 9000 5 Civics for Secondary Schools Longhorn 6500
6 Basic Mathematics TIE 10000
7 Fundamental Biology Form One longhorn/mwaniki Gofrey 9,000
8 Physics Oxford 10,500
9 Chemistry Oxford 10,500
10 Oxford Student Dictionary Oxford 21,000
11 Mabala The Farmer Ben and Company Ltd 4000
12 Hawa The Bus Driver Ben and Company Ltd 4000
13 Kalulu the Hare 4500
14 Magic Garden 4000
15 Commerce for sec schools forms 1&2 Nyambani Nyangwine publishers 9000
16 Book for sec schools forms 1&2 Nyambani Nyangwine publishers 9000
TOTAL 138500
ORODHA YA VITABU NA BEI ZAKE KIDATO CHA KWANZA 2017/218
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
3. MAHALI SHULE ILIPO:
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ipo wilaya ya SAME, Mkoani Kilimanjaro. Ukitokea Dar es Salaam au Tanga shule ipo kati ya Makanya na SAME mjini umbali wa kilometa kumi (10 km) kabla
ya kufika Same Mjini. Ukitokea Moshi shule ipo kilometa kumi baada ya kupita SAME mjini. Kutokea Kilipo kibao cha shule hadi shuleni ni umbali wa kilometa 1.4.
Kwa maelezo zaidi fika Juhudi Studio SAME Mjini mkabala na benki ya NMB.
4. USAFIRI: Wanafunzi watajitegemea kwa usafiri wa kuja shuleni na kurudi nyumbani wakati wa likizo. Uongozi wa shule utahusika kuwafanyia mpango wa usafiri wa pamoja ili kutafuta usalama wa watoto na hasa wakati wa kufunga shule kwenda likizo.
5. ADA YA SHULE : Ada ya shule kwa mwaka 2018 ni Tshs 2,000,000/= (milioni mbili tu.)
Ada italipwa kwa mikupuo miwili; a. Mkupuo wa kwanza Tshs 1,100,000 kabla ya tarehe 22/12/2017.
b. Mkupuo wa pili Tshs 900,000/= kabla ya tarehe 30/06/ 2018. Ada ya shule, na pesa za matumizi (Pocket money) zitalipwa kupitia benki. Majina ya benki, namba za A/c na jina la A/c ni kama ifuatavyo:
i. Benki ya AMANA A/C No: 005120109690001 kwa j ina la Kirinjiko Islamic Secondary School.
ii. Benki ya NMB A/C No: 40503500042. kwa jina la Kirinjiko Islamic Secondary School. Mambo muhimu ya kuzingatia juu ya malipo:
(l) Stakabadhi(receipt) za malipo yote zitaandikiwa shuleni Kirinjiko Islamic tu.
(m) Nakala kivuli (Photocopy) ya Pay-in-slip haitapokelewa kwa sababu zozote zile.
(n) Malipo yakishafanyika hayatarudishwa kwa sababu yoyote ile.
(o) Malipo ya ada lazima yapitie Benki. Fedha taslim hazitapokelewa shuleni kwa sababu yoyote ile.
(p) Mwisho wa kulipa mkupuo wa kwanza wa ada ni tarehe 20/12/2017. Kulipa mkupuo wa kwanza wa ada ndio kuthibitisha kukubali nafasi. Kwa hiyo baada ya tarehe tajwa, kwa mzazi ambaye atakuwa hajafanya malipo haya nafasi ya mtoto wake itatolewa kwa
mhitaji mwingine.
(q) Pay-in-slip ya ada na pocket money ziwe tofauti. Pay-in-slip iandikwe/ziandikwe jina la
mwanafunzi anayelipiwa na kidato anachosoma ili kuondoa usumbufu unaoweza
kujitokeza (Mfano: 1.Ada ya Ahmed Ally- Form ID. 2.Pocket money ya Amina Juma -Form IA). 3. Gharama za Vifaa na vitabu vya Najat Hudhaifa Form 1, n.k.
(r) Baada ya kulipa, Tafadhali wasilisha nakala halisi (original) Pay-in-slips kwa Mhasibu wa shule ili kupatiwa stakabadhi ya malipo (receipt). Hakikisha unatunza stkabadhi ya shule
kipindi chote mpaka mtoto kuhitimu masomo katika ngazi husika.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(s) Wanafunzi watakaokuja na pesa za matumizi wanatakiwa kuziwasilisha kwa Mhasibu na kupatiwa stakabadhi. Upo utaratibu maalum uliowekwa na shule wa kuwapatia
fedha hizi pale watakapozihitaji kwa matumizi. (t) Mwanafunzi haruhusiwi kukaa na zaidi ya shs 5,000/- bwenini.
(u) Shule haitahusika na upotevu wa aina yoyote wa fedha za mwanafunzi. (v) MWANAFUNZI ASIYEKAMILISHA ADA YA MUHULA HUSIKA HATAPOKELEWA KWA
SABABU YOYOTE NA HATARUHUSIWA KUFANYA MITIHANI YA SHULE.
6. SARE ZA SHULE (A) Sare ya Darasani i ) Wavulana 1. Suruali 2 rangi ya “l ight blue” 2. Nusu kanzu nyeupe; urefu wa kufika magotini, mikono mirefu, Isiyopasuliwa na isiyo na kola. 3. Kofia mbili nyeupe zisizokuwa na urembo wa aina yoyote na ziwe za kitambaa sio za kufuma
kwa nyuzi. 4. Viatu vyeusi vya ngozi vya kufunga kamba, unene wa soli ya viatu usizidi nchi moja (1 inch),
soksi nyeusi au dark blue. i i ) Wasichana
1. Nusu kanzu mbili (l ight blue), ndefu zenye mikono mirefu isiyo na mifuko. 2. Suruali (pajama) 2 za rangi ya light blue.
3. Shungi (juba) 2 nyeupe kubwa ya duara yenye urefu wa Kufika magotini. 4. Baibui 2 (pana na ndefu) zenye rangi ya zambarau. Aina ya zambarau inayokusudiwa ni ile tu
inayotambulika na kushonwa shuleni. Ili kuepusha kuharibu vigezo vya sare yetu wanafunzi wote watashonea sare zao shuleni.
5. Viatu vyeusi vya ngozi vya kufungwa kwa kamba, unene wa soli ya viatu usizidi nchi moja (1 inch) vifunike miguu, na soksi za dark blue au nyeusi.
Angalizo: Mwanafunzi hataruhusiwa kuingia darasani na ikibidi anaweza kurudishwa nyumbani iwapo atakiuka
utaratibu wa sare ya shule hata kwa kipengele kimoja.
(B) Sare za Nje ya Darasa
(a) Wavulana
1. Suruali 2 nyeusi (siyo Jeans, Lee, wala Corduroy) zilizoshonwa kwa mshono wa suruali za kawaida na isiyobana.
2. Fulana 2 za rangi ya dark blue, zenye nembo ya shule
3. Kanzu nyeupe 4. Track-suit nyeusi au Dark bluu na raba kwa ajili ya michezo/mazoezi.
5. Jacket/sweta lenye rangi ya dark blue au nyeusi lisilo na picha wala maandishi yoyote kwa ajili ya matumjzi ya kipindi cha baridi.
6. Gun boot za kawaida.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(b)Wasichana
1. Gauni refu la mikono mirefu la rangi ya damu ya mzee lisilopasuliwa, lisiloungwa na lisilokuwa
na mikunjo kiunoni. 2. Pajama ya rangi ya damu ya mzee.
3. Ushungi mkubwa wa mviringo (juba), urefu wa kufika magotini wa rangi ya damu ya mzee. 4. Kitenge jozi moja. Kanga hairuhusiwi shuleni.
5. Nguo za michezo: Track suit dark blue au nyeusi na pana kiasi na fulana isiyobana (dark blue
au nyeusi) ya mikono mirefu. 6. Nguo za kulalia (night dress) – shumizi ndefu 2.
7. Gun boot za kawaida.
Zingatia:
i. Zaidi ya sare, mwanafunzi hataruhusiwa kuwa na nguo nyingine yoyote.
ii. Nguo yoyote inayobana au inayoonesha ndani (transparent) au iliyoshonwa kinyume na maagizo haitakubaliwa kama sare ya shule.
iii. Hairuhusiwi kwa wanafunzi kuvaa mapambo ya aina yoyote wakiwa shuleni au nje ya shule
(likizo) wakati bado ni mwanafunzi wa shule hii. iv. Mwanafunzi atakayekiuka utaratibu huu na kuthibitishwa na uongozi wa Shule,
atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na Kunyang’anywa mapambo hayo na hatarudishiwa.
MUHIMU:
Ili kuondoa tatizo la kutofautiana kwa rangi za vitambaa na muundo wa Sare za shule; sare zote za shule zitashonwa hapa shuleni kwa gharama zilizotajwa kwenye kifungu namba saba (7) (Gharama za mashono).
7. GHARAMA ZA MASHONO YA SARE ZA SHULE (A)Sare za Darasani
( i ) Wavulana 1. Suruali 1 2. Nusu kanzu 1 Jumla = 30,000.
3. Kofia 1
( i i)Wasichana
1. Baibui 1 2. Pajama 1 Jumla = 30,000/= 3. Nusu kanzu 1 4. Ushungi (Juba) 1
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
Sare za Nje (i )Wavulana
1. Suruali nyeusi @ 13,000/= Jumla = 25,000/= 2. Fulana (dark blue) @ 12,000/=
( i i)Wasichana
1. Gauni damu ya mzee 1
2. Pajama 1 Jumla = 27,000/= 3. Ushungi 1 Muhimu: (i) Vipimo vya sare vitafanyika hapa shuleni. (ii)Malipo ya sare za shule yatafanyika hapa shuleni kwa Mhasibu wa shule.
8. VIFAA VYA MASOMO Mwanafunzi atalazimika kununua vifaa vyote vya masomo vinavyohitajika kama vile :
(a) Madaftari makubwa (counter books) ya kila somo. Madaftari ya saizi ya kati (3Quires) yenye nembo ya shule yanapatikana kwa Tshs 2,5000.
(b) Kalamu na mkebe wa vifaa vya hisabati (Mathematical set). (c) Licha ya uwepo wa maktaba ya shule, kila mwanafunzi anashauriwa kujinunulia vitabu
vinavyohusiana na masomo yake ili aweze kujisomea kikamilifu akiwa ndani na nje ya shule. (d) Kila mwanafunzi aripoti shuleni akiwa na Jalada(Box file) la kutunzia mitihani na majaribio. (e) Graph paper pad.
9. VIFAA VYA BWENI:
i. Godoro la upana wa futi mbili na nusu ( ft x3 lnch). Ili kuondoa tatizo la kusafiri na
magodoro, magodoro yanapatikána hapa shuleni kwa Tshs 38,000/= ii. Shuka mbili za rangi ya pink pia zinapatikana shuleni kwa Tsh 13,000/= @ Ths 6,500/=.
iii. Mto na foronya mbili. Tsh. 12,000. iv. Blanketi Tsh. 15,000.
v. Chandarua chá pembe nne. Vyandarua vinapátikana shuleni kwa Tsh 9,000/=. vi. Sabuni za kutosha za kufulia (za unga) na za kuogea.
vii. Vyombo vya chakula; sahani, bakuli, kikombe, na kijiko. Sahani na bakuli visiwe vya udongo (nunua stainless steel au pembe).
viii. Begi kwa ajili ya kuhifadhia vitabu na vitu vingine. ix. Ndoo ya LITA 10 kwa ajili ya kuhifadhia maji.
Zingatia: Sanduku la chuma (tranker) HALIRUHUSIWI shuleni.
Muhimu: Mwanafunzi atakapoacha, kufukuzwa au kuhama shule vifaa vyake kama vile godoro, begi n.k
ataondoka navyo. Pindi atakapoviacha, shule haitakuwa na dhamana ya vifaa hivyo.
212
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
10. UANDIKISHWAJI Siku ya kuripoti shuleni, mwanafunzi awe na vifaa vifuatavyo:
i) Fomu za Utambulisho wa mwanafunzi na wazazi/walezi wa mwanafunzi zikiwa zimejazwa na kubandikwa picha.
ii) Fomu ya daktari (Medical Examination form). Kama mwanafunzi ana matatizo maalum ya kiafya maelezo ya daktari
yaeleze tahadhari anazotakiwa kuchukua akiwa shuleni.(kiambatisho B). iii) Fomu ya wajibu wa mzazi/mlezi (kiambatisho C)
iv) Fedha za kitambulisho TSh. 5,000/= v) Pay-in-slip ya malipo ya ada. vi) Kitabu-Mwongozo wa mafanikio katika Elimu (Supu ya Elimu) Shilingi 12,000. vii) Msahafu wa tafsiri ya Kiswahili wenye tangulizi za sura wa (Abdullah Saleh Al Farsy).Kwa
shuleni unapatikana kwa Tshs. 15,000/=. viii) Kitabu cha kwanza Elimu ya Dini ya Kiislam.Tshs.9,000/= ix) Kitabu cha Riyadh Swalihina (Tafsiri ya Kiswahili) Tsh 20,000/=
x) Kitabu cha Lugha ya Kiarabu kidato cha 1 sh.5,000/= xi) Qur-an na sunna Juzuu ya tatu DWW. Tsh.9000/=
xii) Jalada la kuhifadhia nyaraka za taaluma. 5000/= MUHIMU
• Mwanafunzi atakayeshindwa kukamilisha mahitaji haya hatapokelewa. 11. MAENDELEO YA DARASANI. Kila mwanafunzi anatakiwa kufanya bidii katika masomo yake kwa kuhudhuria vipindi vyote,
kufanya kazi za darasani katika kila kipindi, kufanya majaribio na mitihani yote inayotolewa shuleni, kutumia maktaba ya shule kujisomea vitabu na majarida mbalimbali ya kielimu ili kujiongezea maarifa zaidi. Ili kufaulu kuingia kidato kingine, mwanafunzi anatakiwa afikishe wastani wa angalau alama 50 (daraja C) au zaidi na crediti 7 au zaidi katika masomo yake yote anayosoma. Crediti ni madaraja C, B na A. 12. KAZI ZA NJE YA DARASA.
Kujibidiisha katika kazi ni katika nidhamu ya kiislamu. Hivyo, kila mwanafunzi atawajibika kushiriki kikamilifu katika kutenda kazi za usafi wa mazingira, ujenzi na kazi nyinginezo kama
atakavyoelekezwa na walimu au viongozi wa wanafunzi. Kutegea kazi, iwe ya darasani au nje ya
darasa ni kukiuka maadili anayotarajiwa awe nayo mwanafunzi wa shule hii na haitavumilika. 13. NIDHAMU
Shule hii ni ya Kiislamu. Hivyo mwenendo wa wanafunzi na wafanyakazi wake unatarajiwa uwe wa kiislamu. Kukiuka maadili ya kiislamu kwa mujibu wa Qur’ani tukufu na Sunnah sahihi za Mtume (S.A.W) ni sawa na kukiuka maadili ya shule. Mwanafunzi yeyote atakayekiuka kwa makusudi kanuni na mwenendo bora wa shule, atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
14. KANUNI NA MWENENDO BORA WA SHULE
(i) Kila mwanafunzi wa shule hii anapaswa kutambua kuwa yupo hapa kwa ajili ya Uislamu. Kwa sababu hiyo chochote kilichopo nje ya Uislamu hakina nafasi katika shule hii, kiwe kwa maneno au kwa vitendo.
(ii) Kila mwanafunzi atakuza pendo lake kwa Allah (s.w) na mtume wake (s.a.w), dini yake na
waumini wenzake. Pamoja na haki za muumba zilizo juu ya kila Muislam, yamwajibikia kila mwanafunzi
achunge haki na nafasi yake na atumie vipaji vyake katika uchamungu ndani na nje ya shule.
(iii) Kila mwanafunzi atatumia muda wake vizuri katika kujielimisha kwa ajili ya Allah (s.w) ikizingatiwa kuwa kujielimisha kwa ajili ya Alla(s.w) ni amri ya kwanza kwa kila muislamu.
(iv) Kila mwanafunzi atalazimika kuhudhuria kila kipindi cha somo, kufanya mazoezi, majaribio ya kila somo na mitihani yote itakayotolewa shuleni. Mwanafunzi atakayeshindwa
kuhudhuria darasani mfululizo kwa siku tatu au zaidi bila sababu yoyote ya msingi, atakuwa amejifukuzisha shule.
(v) Kila mwanafunzi anapaswa kuzingatia na kufuata ratiba na utaratibu wa shule kikamilifu.
Ni kosa kubwa kutoonekana katika eneo husika kwa mujibu wa ratiba kama vile; kuonekana bwenini wakati wa masomo. Wanafunzi wagonjwa wanapaswa kuripoti kwa mwalimu wa
zamu na darasa ili wapewe kibali cha kwenda zahanati. (vi) Wakati wote wa kuja shule au wakati wa kurudi nyumbani, vazi rasmi ni sare ya shule ya
darasani. Kutokuwa na sare katika wakati huo ni kosa lisilovumilika. (vii) Wanafunzi wote wanatakiwa wavae nguo za Kiislamu wakiwa ndani na nje ya shule.
Wasichana wavae nguo za kuenea mwili mzima isipokuwa uso na vitanga vya mikono rejea Qur-an {24:31}.
(viii) Ni marufuku kwa mwanafunzi wa jinsia yoyote kuvaa mapambo wakati akiwa shuleni na nje ya shule.
a. Wavulana wavae nguo za heshima na zisizo na maandishi au picha ya aina yoyote. Hairuhusiwi kuvaa kaptura, jeans, msuli au carwash katika maeneo ya shule.
b. Hairuhusiwi kwa wasichana kuvaa nguo za kubana, fupi au zinazoonesha ndani (Transparent) akiwa shuleni au nje ya shule.
(ix) Ni marufuku kwa mwanafunzi yeyote kufuga kucha, kujipaka rangi za kucha , rangi za
midomo, kupaka hina, kunyoa nyusi, kupaka wanja, kutumia manukato kwa wasichana, kuvaa viatu vya kuchuchumia au vinavyotoa sauti, kukali nywele, kutia rangi, kusuka rasta
au kubadilisha nywele, kucha,kope au ngozi kwa namna yoyote ile na kufuga nywele kwa wavulana.
Angalizo: Kwa wasichana itakapobidi kutumia manukato watatumia Nivea ya kupaka kwapani tu
(Rolling)ambayo harufu yake ataihisi mpakaji mwenyewe. Ama body spray na manukato
ya aina zote ni makosa kukutwa nayo. (x) Ni marufuku mwanafunzi kuchochea, kushawishi, kuhamasisha, au kushiriki mgomo kwa
namna moja au nyingine hata kama kuna sababu za msingi. Ni kosa kubwa kugomea amri au maelekezo ya viongozi wa serikali ya wanafunzi, walimu na uongozi wa shule kwa
ujumla.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
(xi) Mwanafunzi asionekane katika vilabu vya pombe, nyumba za Kupangisha wageni (Guest house), kumbi za dansi na sinema.
(xii) Kila mwanafunzi ni mlinzi wa mali ya shule, mali yake binafsi na ya wenzake. Mwanafunzi atakayeharibu, kusababisha mali ya shule kuharibika, kuibiwa au kupotea atachukuliwa
hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kulipa. Hivyo mwanafunzi atakapogundua wizi au uharibifu wowote dhidi ya mali ya shule au ya mwanafunzi mwingine atoe taarifa kwa
walimu au viongozi wanaohusika mara moja. (xiii) Kuiba ni kosa kubwa, mwanafunzi atakayethibitika kuiba mali ya shule au ya mwanafunzi
mwenzake au nje ya shule atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kufukuzwa shule.
(xiv) Mwanafunzi anapokuwa na shida yoyote hapa shuleni, kwanza aanze kwa viongozi wanafunzi na ndipo aende kumuona mwalimu wa zamu au wa Darasa lake, au walimu wengine wanaohusika. Kama mwanafunzi baada ya kufuata ngazi hizo shida yake haijatatuliwa, aende kwa Makamu Mkuu wa shule, kisha kwa Mkuu wa shule itakapobidi kufanya hivyo Mwanafunzi asishitakie shida zake nje ya shule kabla hajamuona Mkuu wa
shule. (xv) Kila mwanafunzi anatakiwa awe msafi wakati wote, ashiriki vyema katika usafi wa mwili
wake binafsi; kitanda, nguo, nywele, kucha, na usafi wa madarasa, bweni,bwalo la chakula na mazingira ya shule kwa jumla.
(xvi) Kelele za aina yoyote hazitaruhusiwa, ziwe darasani, kwenye baraza za madarasa, ndani ya bweni, au popote iwe kwa mwanafunzi mmoja au wengi (kundi). Tunalazimika kuonesha maadili ya Kiislalmu katika mazungumzo yetu yote.(Rejea Qur’ani 31:19)
(xvii) Shule haimruhusu mwanafunzi kutoka ndani ya shule na kulala nje ya eneo la shule bila ya kibali maalum cha maandishi kilichoidhinishwa na Mkuu wa shule. Wakati wa mapumziko mafupi (mid-term break) wanafunzi watabakia katika eneo la shule. Hawataruhusiwa kwenda nyumbani.
(xviii) Mwanafunzi hatakiwi kulala au kwenda katika nyumba za watumishi isipokuwa kwa
dharura maalum itakayoidhinishwa na Mkuu wa shule. (xix) Wanafunzi wa jinsia tofauti hawaruhusiwi kuchanganyika katika jambo lolote bila ya
uangalizi wa mwalimu iwe faragha au bayana, kufanya hivyo ni kosa la kukaribia zinaa ambalo adhabu yake ni kufukuzwa shule.
(xx) Kupigana ni kosa kubwa. Mwanafunzi atakayepigana au kumpiga mwenzake atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
(xxi) Mwanafunzi anapaswa kuripoti shuleni katika tarehe na muda uliopangwa baada ya likizo, atakapochelewa kwa dharura, taarifa itolewe kwa Mkuu wa Shule kabla ya kufunguliwa shule, na baada ya hapo aje na mzazi/mlezi wake anaetambulika kiofisi ndani ya siku saba
(7) baada ya shule kufunguliwa, atakayechelewa zaidi ya hapo bila taarifa shule haitakuwa na dhamana naye.
(xxii) Wazazi wa wanafunzi wanaruhusiwa kuwatembelea wanafunzi (watoto wao) shuleni kulingana na ratiba iliyoainishwa na uongozi wa shule hapo chini na si vinginevyo. Hata
hivyo kutokana na uhaba wa makazi shuleni, shule haitahusika kumpatia mzazi/mlezi malazi atakapomtembelea mwanae.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
RATIBA YA KUWATEMBELEA WANAFUNZI KWA MUHULA HUU NI KAMA INAVYOONEKANA HAPA
CHINI.
1. TAREHE: 28/01/2018.
2. TAREHE : 25/02/2018.
3. TEREHE : 01/04/2018. 4. TAREHE: 29/04/2018. ANGALIZO: Tunapenda kuwakumbusha wazazi kuwa mtu pekee anayeruhusiwa kumtembelea mwanafunzi ni mzazi au mlezi anayetambulika katika nyaraka muhimu za utambulisho wa wazazi/walezi za shule tu, na si vinginevyo. Haturuhusu vyakula wala vinywaji vya aina yoyote wakati wa kumtembelea mwanafunzi.
(xxiii) Wakati wa kuwatembelea wanafunzi, mzazi/mlezi haruhusiwi kuleta vyakula au vinywaji vya aina yoyote kwa mwanafunzi. Vifaa vitakavyoletwa kwa wanafunzi vikabidhiwe kwanza
kwa mwalimu wa zamu/darasa ili vikaguliwe. (xxiv) Zaidi ya mashine ya kufanyia hesabu (calculator), vifaa vyote vya electronics kama vile simu,
camera, radio, radio cassette n.k haviruhusiwi mwanafunzi kuwa navyo katika mazingira ya shule. Mwanafunzi atakayekutwa navyo vitu hivyo hapa shuleni, atapewa adhabu kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa shule na havitarudishwa.
(xxv) Ni kosa kwa mwanafunzi kukaa na pesa taslimu bwenini zinazozidi Tsh 5,000/=. Pesa zote zihifadhiwe kwa Mhasibu wa shule. Kutakuwa na utaratibu wa kuchukua pesa kiasi kidogo
kwa ajili ya matumizi. (xxvi) Shule imetenga maeneo maalum kwa ajili ya michezo.Hivyo ni marufuku mwanafunzi
kukutwa anacheza mpira na michezo mingine ya kutimua vumbi na kushawishi kelele za kishabiki na mfano wake katika maeneo yanayozunguka bweni,darasa na maeneo mengine
mfano wa hayo nje ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya michezo. (xxvii) Swala ni nguzo kuu ya kumtambulisha mtu kuwa ni muislamu na ufunguo wa milango ya
mafanikio. Hivyo shule haitamvumilia mwanafunzi yeyote atakayeonekana kupuuza swala kwa makusudi hata kama ni kwa tabia ya kuchelewachelewa na kukosa jamaa msikitini.
(xxviii) Mbali na mzazi kuruhusiwa kumtembelea mtoto wake na kujua maendeleo yake kitaaluma na kitabia kila Jumapili ya mwisho wa mwezi, pia anakaribishwa shuleni au kuwasiliana na uongozi wa shule wakati wowote kwa lengo la kuleta ufanisi kwa mwanae na jamii ya waislamu kwa ujumla.
Joining Instructions Kiss 2018 Email: [email protected]
15. MAKOSA YANAYOWEZA KUSABABISHA KUFUKUZWA SHULE.
Pamoja na maelezo yote hayo, mwanafunzi atakayechupa kwa makusudi mipaka ya Uislamu na kuvunja maadili na kanuni za shule kwa kutenda makosa makubwa kama yalivyoainishwa
atafukuzwa shule; i. Kunywa pombe.
ii. Kwenda nyumba za starehe kama vile kwenye kumbi za madansi, disko n.k iii. Uzinzi au kukaribia zinaa kwa kuwa na rafiki wa jinsia tofauti (boy Friend/girl friend).
iv. Kuvuta bangi, sigara, madawa ya kulevya, n.k v. Kutosimamisha swala vi. Kumiliki vitu vya electronics kama simu au line, redio, kamera n.k
vii. Kukaa nje ya shule kwa muda wa siku 3 bila kibali maalum kilichoidhinishwa na Mkuu wa shule.
viii. Kuanzisha, kuchochea, kushiriki au kuongoza mgomo. ix. Kuhatarisha amani ya shule kwa kupigana au kuchochea watu wapigane.
x. Wizi, uporaji na uharibifu wa mali ya shule na ya wanafunzi au wakazi wa kituo. xi. Kukosa mitihani/jaribio bila ya sababu za msingi.
xii. Kutohudhuria masomo/darasani bila sababu maalumu za msingi . xiii. Kujirudiarudia katika makosa ya uvunjifu wa kanuni na mwenendo bora wa shule.
16. HITIMISHO Ni matumaini yetu kuwa Mzazi/ Mlezi na mwanafunzi mtarajiwa mmeyasoma maelekezo haya vizuri na kwa makini na kuyaelewa vilivyo. Mwanafunzi unatakiwa kuzingatia na kutekeleza maelekezo yote ili kuepusha usumbufu. Mzazi/Mlezi anashauriwa kujitahidi kushirikiana na shule kwa kutekeleza wajibu wake kikamilifu ikiwa ni pamoja na kulipa ada kwa wakati na kumsimamia mwanae katika maadili ya Kiislamu hasa wakati wa likizo.
Kirinjiko Islamic Secondary School ni shule yenye mazingira mazuri sana ya kusoma na malezi ya maadili mema ya kiislamu.
TUNAKUTAKIA MAANDALIZI MEMA NA KARIBU
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL, KAMA MWANAFAMILIA MPYA WA
KIRINJIKO.
Kauli mbiu: “Soma kwa jina la Mola wako Aliyeumba”(96:1). MKUU WA SHULE.
2017. Wabillah Tawfiiq.