5

Click here to load reader

Mkristo na uchumi part 1

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Mkristo na uchumi   part 1

 

 MKIRSTO  NA  UCHUMI. 

 

Utangulizi

Mkristo ni nani? 

Mkristo ni mtu aliyemwamini Yesu Kristo na kumpokea au kumfanya Bwana na Mwokozi wa maisha  yake  (Warumi  10:9‐10).  Haitoshi  tu  kusema,  ‘Mkristo  ni  mtu  aliyemwamini  Yesu’, kwasababu  Biblia  inasema  ‘hata  shetani  naye  anaamini  na  kutetemeka  pia’  lakini  si  mkristo (Yakobo 2:19) 

Uchumi ni nini? 

Uchumi  ni Maarifa  ya  namna  ya  kutumia  rasilimali  (resources)  zilizopo  au  chache  (scarce)  ili kukutana na mahitaji na matakwa mengi (needs and wants) katika maisha ya mtu/watu. 

Ni mapenzi ya Mungu tuyafurahie maisha yetu aliyotupa yeyé hapa duniani kama anavyosema

katika kiyabu cha Isaya 1:19 ‘mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi.’ Na kila kitu unachohitaji

kwa ajili ya maisha mazuri ya utoshelevu, kipo hapa hapa ulipo.

Rasilimali zote tunazozihitaji kwa ajili ya Maisha mazuri ya Baraka, tunazo hapa hapa. Lakini

wewe kama Mkristo, hautaweza kuyafurahia maisha aliyokuandikia Mungu, uyaishi hapa duniani,

kama hutajua namna/jinsi/mbinu/kanuni za ki-Mungu za kufanikiwa kimaisha ili kukutana na

mahitaji yako na matakwa yako ya kimaisha.

Tujifunza siri na kanuni za kufanikiwa kiuchumi kwa maisha ya tajiri mmoja, aliyeandikwa katika

Biblia, na jinsi alivyofanikiwa sana kimaisha na kiuchumi, japo alianza maisha kwa shida na taabu.

Mtu huyu tajiri anaitwa Yakobo. Habari hii utaipata katika kitabu cha Mwanzo 28:1-5; 29: 13-30; 30:25-43; 31:1-3; 32:1-18

Kwa ufupi ni kwamba:

Yakobo alipomkimbia ndugu yake Esau, alifika kwa mjomba Labani akiwa na fimbo tu, lakini baada 

ya  kukaa  huko  kwa  muda,  alirudi  katika  nchi  ya  Baba  zake  akiwa  tajiri  mkubwa  mwenye 

wafanyakazi 1,200 (Matuo mawili = Makundi mawili ya watu 600)   Soma Mwanzo 32:9‐12. Fikiri 

mwenyewe,   mtu mwenye wafanyakazi 1,200 alikuwa ana wanyama wangapi? Thamanisha mali 

zake kwa fedha ya sasa.  

Page 2: Mkristo na uchumi   part 1

 

Utakapokwenda kuisoma habari hii, utaona  jinsi Yakobo alivyokuwa tajiri, kwa maana alikuwa na 

uwezo wa  kutoa  zawadi  kwa mtu,  kiasi  cha  punda  200,  farasi  200,  ngamia  200,  ng’ombe  200, 

kondoo 200 na mbuzi 200. Utajiri huu kwa  lugha ya  sasa; Punda 200  (kiuchumi, hii  inakadiriwa 

kuwa ni sawa na magari madogo ya mizigo (pickup) 16; yaani punda 12 wanaweza kubeba mzigo 

wa pickup 1). Kondoo 200 ni sawa na maduka 4 ya nguo, ngamia 200 ni sawa na malori madogo ya 

mizigo 16, farasi 200 ni sawa na pikipiki 50. 

Unaweza kuona jinsi Yakobo wa Isaka alivyokuwa tajiri. Mtu anayeweza kukupa zawadi ya pikipiki 

50,  maduka  4  ya  nguo,  malori  madogo  16  na  magari  madogo  ya  mizigo  (pickup)  16;  yeyé 

anabakiwa  na  kiasi  gani  cha  utajiri? Na  kama  alianza  akiwa mikono mitupu,  alitumia  njia  gani 

kufikia katika mafanikio hayo ya kiuchumi? Hata mimi nataka kujua. Utashangaa kwamba, Biblia 

inafundisha uchumi kiasi hiki. 

KANUNI ZA KIBIBLIA ZA UCHUMI MZURI 

1. Maono ‐ Kuona Fursa za kiuchumi 

Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya au nzuri, bali yanapangwa. Ukiona mtu amefanikiwa 

kiuchumi,  ujue  aliona  kwanza  fursa  hiyo  na  akaichuchumilia  na  kuifuatilia  mpaka 

akafanikiwa. Hivyo muombe Mungu  akupe  kuziona  fursa  zilizopo.  Tafuta  kuona mahitaji 

mbalimbali ya jamii, huwezi kukosa kuona fursa kadhaa za kiuchumi.  

 

Utakapokwenda  kusoma  habari  hizi,  utagundua  kwamba, mjomba  Labani  alikuwa  tajiri 

mwenye shughuli mbalimbali na wafanyakazi wengi sana. Kwa muda mfupi ambao Yakobo 

alikaa kwa mjomba wake, aligundua kwamba, ataweza kufanikiwa kwa kujishughulisha na 

kazi mojawapo  za mjomba,  hivyo  akachagua  kujikita  katika mifugo  ya mjomba  Labani. 

Mwanzo 29: 15‐20.  

 

Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya au nzuri, bali yanapangwa. Lazima uwe na uwezo wa 

kuona  fursa  za  kiuchumi na  kujitosa humo baada  ya  kufanya upembuzi  yakinifu. Ukiona 

mtu amefanikiwa kiuchumi, ujue aliona kwanza fursa hiyo na akaichuchumilia na kuifuatilia 

mpaka  akafanikiwa.  Soma Mwanzo  21:14‐19  na Waefeso  1:15‐19  utaona  umuhimu wa 

kuwa  na  macho  yanayoweza  kuona  vitu  vilivyojificha.  Hivyo  muombe  Mungu  akupe 

kuziona  fursa  zilizopo.  Tafuta  kuona mahitaji mbalimbali  ya  jamii,  huwezi  kukosa  kuona 

fursa kadhaa za kiuchumi.  

Page 3: Mkristo na uchumi   part 1

 

2. Malengo mahususi – Kujua kwa hakika unataka kufika wapi 

Alijua alichokuwa anataka na alikaza uso kutoyumbishwa mapaka apate anachotaka. Hii ni 

tabia ya kila mjasiliamali aliyefanikiwa. Lazima uwe ‘focused’ usiyumbishwe. Utaiona tabia 

hii ya Yakobo kwa jinsi alivyojaribiwa katika swala la kupata mke aliyemtaka. Alijua anataka 

mke, na sio bora mke. 

 

Mjomba Labani alikuwa na mabinti wawili, Lea na Raheli. Aliambiwa kama anataka kumuoa 

Raheli, atoe mahari ya kufanya kazi kwa miaka 7. Baada ya maiaka 7 akapewa Lea badala 

ya Raheli. Kwa  lugha rahisi, alitapeliwa au alizulumiwa. Akaambiwa, kama vado anamtaka 

Raheli, afanye kazi tena kwa miaka 7 ndipo atapewa Raheli.  

 

Kama Yakobo  angekuwa  anataka bora mke,  angeridhika na  Lea,  lakini  kwakuwa  alikuwa 

anamtaka  Rachel,  akalenga  ‘kutokupumzika’  mpaka  ampate  Raheli,  bila  kuyumbishwa. 

Akaapinda mgongo  tena  kwa miaka  7  ili  tu  kuyafikia malengo  yake,  na  akampata mke 

aliyemtaaka, Raheli !!!    Mwa 29:16‐18. 

 

Ni muhimu sana kwa mtu kuwa na makusudio ya moyo (Malengo). 

• Malengo hufungulia nguvu za Mungu (Msaada wa Mungu)  

‘Nawe  utakusudia  neno,  nalo  litathibitika  kwako;  na mwanga  utaziangazia  njia 

zako’ (Ayubu 22:28) 

• Malengo hukupa nidhamu ya kimaisha (Descipline)  

‘Pasipo maono,  watu  huacha  kujizuia  (yaani  hukosa  nidhamu,  au  msimamo  ‐ 

huyumba‐yumba)   (Mith 29:18). 

 

Yeremia 1:5‐10; Mungu alimtenga Yeremia kuwa Nabii  tangu  tumboni mwa mamaye,  Je 

wewe ulitengwa uwe nani? Tafuta kujua mpango wa Mungu kwako. Usipopatia wito wako, 

kuna  hatari  ya  kutofanikiwa  katika  baadhi  ya  vitu  unavyohangaika  kuvifaya.  Mungu 

anabariki  kazi  zake,  si  kila  kazi. Ni muhimu uutafuta uso wa Mungu  ili ujue mpango wa 

Mungu juu ya maisha yako.  Yeremia 29:11‐13,  Zaburi 32:8 

 

 

 

Page 4: Mkristo na uchumi   part 1

 

3. Mipango Mizuri – Kuwa na njia za kukufikisha katika malengo yako 

Mwanzo 30:25‐36;  Ili kufikia mafanikio na maisha mazuri, mtu wa Mungu  si  tu kwamba 

anahitaji  kuwa  na maono  na malengo  tu,  bali  pia  anahitaji  kuwa  na mipango mizuri  ya 

kumfikisha katika maono na malengo yake.  Jiulize, ni kwa njia gani nitaweza kufikia kule 

ninakotamani kufika? Hizo njia utakazopata, ndio tunaita mipango.  

 

Katika  habari  hii  ya  Yakobo,  unaona  anapanga  kuwachukua  wanyama  wa  mjomba  na 

kwenda nao umbali wa siku tatu (3) na kukita kambi ya mifugo huko. Na utaona anapanga 

kukaa huko kwa miaka mitatu (3). Hizi namba unazoziona hapa, ni mipango madhubuti. N 

mawazo  ya mtu  aliyefanya  uchunguzi  wa  eneo  zuri  la  kuweka  kambi  ya mifugo  na  ni 

mawazo  ya mtu  aliyepiga mahesabu  kuona,  ni  baada  ya muda  gani  atakuwa  ameweza 

kutengeneza faida. 

 

Mipango  mizuri  itazaa  matokeo  mazuri.  Mipango  mibaya  itazaa  matokeo  mabaya. 

Kwahiyo,  tafuta  namna  ya  kutengeneza  mipango  mizuri,  ikibidi  tumia  wataalam  wa 

mipango.  Fanya  Fisibility  study    na  tengeneza  a  good  Business  Plan.  Yakobo  alijitenga 

mwendo wa siku 3 na akakaa nyikani muda wa miaka mitatu. Huu ni Mpango wa Shughuli 

(This  is  a    business  plan  au  activity  plan). Baada  ya miaka  kadhaa,  Yakobo  alikuwa mtu 

mwenye  mafanikio  na  utajiri  mkubwa,  leo  tungemuita  ‘Milionea’  mkubwa.  Kumbuka; 

Mipango mizuri itazaa matokeo mazuri. Mipango mibaya itazaa matokeo mabaya. 

 

Itaendelea toleo líjalo 

 

Mafundisho mengine ya mwalimu, yanapatikana katika duka la vitabu la Kanisa Kuu, Azania 

Front. Pia vipindi vya mafundisho ya mwalimu Mgisa, vinarushwa katka Radio ya Kanisa, 

Upendo FM Radio, 107.7 kila siku ya Jumanne, saa 3:00 – saa 4:00 usiku. Ukiwa na maswali 

juu ya somo hili au shuhuda  jinsi somo hili  lilivyokusaidia, unaweza kuwasiliana na mwali 

kwa njia zifuatazo; 

Mwl. Mgisa Mtebe, 

P. O. Box 837, Dar es Salaam. 

Simu: (+255) 0713497654. 

Barua pepe (Email): [email protected]

Page 5: Mkristo na uchumi   part 1

 

Tovuti (Website): www.mgisamtebe.org