Upload
others
View
30
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
1Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI 2020 NA MPANGO WA MAENDELEO 2020/21
KITABU CHA PILI
TUME YA MIPANGO ZANZIBARJUNI, 2020
iMwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
YALIYOMO
YALIYOMO
Mada Ukurasa
YALIYOMO .....................................................................................................i
Orodha ya Viambatisho .....................................................................................iv
VIFUPISHO ......................................................................................................v
1.0 UTANGULIZI ............................................................................................1
2.0 MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2020 ..................3
2.1 Mwelekeo wa Uchumi wa Dunia ................................................................3
2.2 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ..............................................................3
2.3 Mwelekeo wa Ukuaji wa Uchumi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ................................................................................................................4
2.4Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ya Mashariki ..........................................4
2.5 Mwelekeo wa Mfumko wa Bei wa Dunia ................................................5
3.0 MWELEKEO WA UCHUMI WA ZANZIBAR 2020 ................................6
3.1. Uchumi wa Buluu ......................................................................................6
3.2.Sera ya Viwanda ya Zanzibar ......................................................................7
3.3Sekta ya Utalii ..............................................................................................8
3.4.Viwanda Vidogo Vidogo .............................................................................9
4.0 MATARAJIO YA UKUAJI WA UCHUMI .................................................9
5.0 MFUMKO WA BEI WA ZANZIBAR ........................................................10
6.0 SHABAHA NA MALENGO YA UCHUMI KWA 2020-2022. .................10
7.0 MWELEKEO WA BAJETI, 2020/21 .........................................................11
iiMwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
7.1 Mwelekeo wa Mapato na Matumizi: ..........................................................11
7.1.1 Mapato ya Ndani ......................................................................................11
7.1.2 Mapato ya Nje ..........................................................................................12
7.2 Makadirio ya Matumizi kwa Mwaka 2020/21 ............................................12
8.0 MAPENDEKEZO YA HATUA ZA KUIMARISHA MAPATO .................12
9.0 MWELEKEO WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2020/21 ..........................................................................................................................13
10.0 MAENEO YA VIPAUMBELE KWA MWAKA 2020/21 .........................13
11.0 RASILIMALI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2020/21 .........................................................15
12.0 MWELEKEO WA PROGRAMU NA MIRADI YA MAENDELEO KWA MAENEO MAKUU YA MATOKEO ...............................................................18
13.0 MWELEKEO WA PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO NA SHUGHULI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA 2020/21 KIWIZARA .......................................................................................................21
13.1 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi .............................21
13.2 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais .............................................................22
13.2.1 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Madawa ya Kulevya .......24
13.3 Wizara ya Fedha na Mipango ...................................................................25
13.3.1 Tume ya Mipango Zanzibar ...................................................................30
13.4 Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ........................................34
13.5 Wizara ya Biashara na Viwanda ................................................................40
13.6 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ....................................................44
13.7 Wizara ya Afya ..........................................................................................46
13.8 Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati ..............................................52
13.9 Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ........................................55
iiiMwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.10 Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto ..................58
13.11 Wizara ya Katiba na Sheria .....................................................................61
13.11.1 Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ......................................................61
13.12 Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora ............................62
13.12.1 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi .......................62
13.13 Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale ..........................................63
13.13.1 Kamisheni ya Utalii .............................................................................64
13.14 Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo ..................................65
13.15 Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ..................................................................................................................66
13.15.1 Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar ...........................68
13.15.2 Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) .................................69
13.15.3 Kikosi cha Valantia ..............................................................................69
13.15.4 Chuo cha Mafunzo ...............................................................................70
13.15.5 Jeshi la Kujenga Uchumi .....................................................................71
13.15.6 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi .........................................................72
14.0 PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO CHINI YA MFUKO WA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE FUND) ..........................................72
15.0 UFUATILIAJI NA TATHMINI ................................................................74
16.0 WASHIRIKA WA MAENDELEO ............................................................74
17.0 HITIMISHO ..............................................................................................75
ivMwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Orodha ya Viambatisho
Kiambatisho 1: Mgao wa Fedha za Programu/Miradi ya Maendeleo 2020/21 Kiwizara.
Kiambatisho 2: Mgao wa Fedha za Programu/Miradi ya Maendeleo 2020/21 kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs).
Kiambatisho 3: Programu/Miradi ya Maendeleo Chini ya Mfuko wa Miundombinu (Infrastructure Fund)
vMwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
VIFUPISHOBF Busket Funds (Mfuko wa Wafadhili)
BoT Bank of Tanzania (Benki Kuu ya Tanzania)
CCM Chama cha Mapinduzi
GBS General Budget Support (Msaada wa Kibajeti)
KRAs Key Result Areas (Maeneo Makuu ya Matokeo)
M&E Monitoring and Evaluation (Ufuatiliaji na Tathmini)
MKUZA III Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar Awamu ya Tatu
SDGs Sustainable Development Goals (Malengo ya Maendeleo Endelevu)
SMIDA Small and Medium Industry Development Agency (Wakala wa Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati)
SMT Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
SMZ Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
TRA Tanzania Revenue Authority (Mamlaka ya Mapato Tanzania)
TZS Tanzania Shilings (Shilingi ya Tanzania)
UKIMWI Upungufu wa Kinga Mwilini
UNDP United Nations Development Programme (Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa)
VAT Value Added Tax (Kodi ya Ongezeko la Thamani)
ZECO Zanzibar Electricity Corporation (Shirika la Umeme Zanzibar)
ZRB Zanzibar Revenue Board (Bodi ya Mapato Zanzibar)
ZURA Zanzibar Utilities Regulatory Authority (Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati)
1Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
1.0 UTANGULIZI
Juhudi kubwa zinaendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wake ili kukuza uchumi, kupunguza umasikini na kuleta maendeleo endelevu kwa wote. Katika kuendeleza juhudi hizo Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2020/21itaendelea kutekeleza mikakati mikuu ya Kitaifa inayomaliza muda wake wa utekelezaji 2020 ambayo ni Dira ya Maendeleo ya 2020, Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar – Awamu ya Tatu (MKUZA III) na Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/20. Aidha, Mpango huu wa maendeleo utaendeleza utekelezaji wa Mipango na makubaliano ya Kimataifa iwemo utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu.
Juhudi za Kukuza Uchumi jumuisho unaozingatia masikini zitaendelezwa kwa kasi ambapo kwa mwaka 2020 jambo kuu na la msingi litakuwa ni kuhuisha sekta za kiuchumi na kijamii ambazo zimeathiriwa na maradhi ya COVID 19, sambamba na kuendeleza hatua za kujenga uchumi imara na mpana zaidi (diversified). Aidha, huduma za msingi za jamii kama vile afya, elimu, nyumba na maji zitapewa kipaumbele.
Kutokana na athari za maradhi hayo, kasi ya ukuaji wa uchumi wa Zanzibar inatarajiwa kupungua na kufikia kati ya wastani wa asilimia 3 hadi 5. Hii ni kutokana na kushuka kwa kasi ya uwekezaji nchini, kupungua kwa shughuli za kibiashara kati ya Zanzibar na washirika wa kibiashara, kupungua kwa uagiziaji wa bidhaa na huduma na kusimama kwa biashara na huduma zinazoambatana na sekta ya utalii. Aidha, kupungua kwa ajira katika sekta binafsi na biashara za wajasiriamali wadogo wadogo navyo pia vinaonekana kuathiri ukuaji wa uchumi. Hata hivyo, Serikali inatarajia kuhuisha ukuaji wa uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi kwa kuendelea kuyafanyia kazi maeneo ambayo yatakuwa ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.
2Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mwaka 2020/21 ni kipindi cha mwisho cha utekelezaji wa mipango na mikakati inayomalizika muda wake ambayo ni Dira ya mwaka 2020 na MKUZA Awamu ya Tatu unaoishia mwaka 2020/21. Kwa mnasaba huo vipaumbele vya Mpango wa Maendeleo vimejikita katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 – 2020 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020. Sekta kuu za kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi zikiwemo kilimo, utalii, miundombinu, elimu na afya zitaendelea kupewa msukumo unaostahiki kupitia utekelezaji wa program na miradi mbali mbali ya maendeleo. Aidha, Serikali pia itazidi kuendeleza mageuzi ya kiuchumi na kijamii kwa kuimarisha uchumi endelevu, kujenga miundombinu imara, kukuza uzalishaji kwenye sekta ya kilimo, kuimarisha utalii na viwanda vidogo vidogo, kuimarisha rasilimali watu, kukuza ubora wa huduma za kijamii ikiwemo afya, elimu na kuimarisha mazingira endelevu na misingi ya utawala bora.
Kwa mwaka 2020/21 programu na miradi mikuu ya maendeleo itakayotekelezwa ni pamoja na Mpango wa Kuhuisha Uchumi (Economic Recovery Plan) ambao lengo kuu ni kuhuisha na kuziendeleza sekta za kiuchumi na kijamii baada ya mtikisiko wa uchumi kutokana na COVID-19; Ukamilishaji wa jengo la abiria la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar (Terminal III); Kuimarisha Uchumi Buluu; kuanza ujenzi wa hospitali mpya ya rufaa ya Binguni; ujenzi wa bandari ya Mpigaduri; ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu; ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji maji; ujenzi wa mji wa kisasa Kwahani; ujenzi wa barabara ya Chake Chake – Wete; ujenzi wa miundombinu na matangi ya kuhifadhia mafuta katika eneo la bandari ya Mangapwani sambamba na kuimarisha ulinzi na usalama nchini.
Kitabu hiki kinatoa Mwelekeo wa Hali ya Uchumi kwa mwaka 2020 na Mwelekeo wa Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2020/21.
3Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
2.0 MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2020
2.1 Mwelekeo wa Uchumi wa Dunia
Mwelekeo wa Uchumi wa dunia kwa mujibu wa Mtazamo (World Economic Outlook), ukuaji wa uchumi wa Dunia unatarajiwa kupungua na kufikia asilimia -3.0 kwa mwaka 2020 kutoka ukuaji wa wastani wa asilimia 2.9 kwa mwaka 2019, kinyume na matarajio ya awali ya ukuaji wa wastani wa asilimia 3.5 mwaka 2020. Kasi ya ukuaji wa Uchumi wa nchi Zilizoendelea inatarajiwa kupungua na kufikia wastani wa asilimia -6.1 mwaka 2020 kutoka wastani wa asilimia 1.8 mwaka 2019, kinyume cha matarajio ya awali ya ukuaji wa asilimia 1.7 kwa mwaka 2020. Hali hii imetokana na janga la ugonjwa wa corona (COVID-19) ambalo limeenea duniani kote na kupelekea kusimama kwa shughuli nyingi za kiuchumi ikiwemo Utalii, Usafiri wa anga, usafirishaji na biashara, sekta za fedha na sekta nyengine za kijamii. Nchi zote duniani zimejikita kuwekeza na kusaidia mifumo ya kiafya ili kuokoa maisha ya watu.
Aidha, kasi ya ukuaji wa uchumi kwa nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia kiuchumi inatarajiwa kupungua na kufikia wastani wa asilimia -1.0 mwaka 2020, ikilinganishwa na ukuaji wa wastani wa asilimia 4.5 kwa mwaka 2019, kinyume cha matarajio ya awali ya kasi ya ukuaji wa uchumi wa wastani wa asilimia 4.8. Athari za ugonjwa wa COVID-19 umesababisha khofu na mshtuko na kupeleke kusimama kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kwa nchi hizi. Vile vile, kupelekea ugumu wa utafutaji wa mitaji na kufunga maswala ya dhamana katika masoko ya kimataifa ambayo huleta mtikisiko kwa dola ya Marekani.
2.2 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika
Katika Bara la Afrika kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2020 zilizotolewa na Benki ya Dunia, kuna watu zaidi ya 640 milioni Afrika wanaishi bila ya umeme, 210 milioni kati ya hao wanaishi katika maeneo ya migogoro ya vita na zaidi ya watu 416 milioni wanaishi katika umasikini. Zaidi ya matatizo hayo yanayoikumba Bara la Afrika, kazi nyingi zinapotea, madeni kuongezeka, sambamba na kupungua uwezekano wa kulipa madeni hayo.
4Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Kasi ya ukuaji wa uchumi wa Bara la Afrika inatarajiwa kupungua na kufikia wastani wa asilimia -1.7 mwaka 2020 kutoka wastani wa asilimia 3.5 mwaka 2019, kinyume cha matarajio ya awali ya ukuaji wa uchumi wa asilimia 3.9. Hii ni kutokana na mategemeo ya kuzorota kwa uchumi kwa nchi zinazokuwa kwa kasi kubwa zaidi Bara la Afrika na Kanda ya Afrika Mashariki na Uchumi wa Kanda ya Jumuiya ya Afrika Magharibi na Muungano wa Kifedha wa kanda hiyo (West Afrika Economy na Monetary Union). Hali hiyo ni pamoja na athari za kushuka kwa zaidi ya asilimia 7 kwa uchumi wa nchi zinazosafirisha mafuta na kwa asilimia 8 ya uchumi wa nchi zinazosafirisha bidhaa za chuma (Metals). Muelekeo wa uchumi wa Afrika umeathiriwa zaidi na matokeo ya maradhi ya COVID-19 ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiri uchumi wa dunia nzima kupitia kupungua kwa uzalishaji, shughuli za kitalii na mzunguko wa fedha.
2.3 Mwelekeo wa Ukuaji wa Uchumi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara
Mwelekeo wa hali ya uchumi wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo zinaunganisha zaidi ya watu 1.2 bilioni kibiashara na ndio kwa sasa ni sehemu kubwa inayo tekeleza biashara huria duniani unatarajiwa kupungua kwa kasi ya baina ya asilimia -2.5 na asilimia -5.1 kwa mwaka 2020 kutoka asilimia 4.3 ya mwaka 2019, kinyume cha matarajio ya awali ya ukuaji wa uchumi wa asilimia 3.5. Kushuka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi kunatarajiwa kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa bidhaa za kilimo, kupungua kwa mnyororo wa usambazaji, mivutano ya kibiashara pamoja na kuzorota kwa upatikanaji wa ajira na mategemeo ya kupungua kwa misaada ya kibajeti ambayo imesababishwa na kuwepo kwa janga la maradhi ya mripuko ya COVID-19 ambayo yameathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wa Kanda ya Jangwa la Sahara kwa zaidi ya dola za kimarekani kati ya 37- 79 bilioni.
2.4 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ya Mashariki
Kwa mwaka 2020 kasi ya ukuaji wa uchumi kwa nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki inatarajiwa kupungua kutokana na matarajio ya kushuka kwa uchumi
5Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
wa dunia na nchi za Afrika kutosababishwa na kusimama kwa shughuli na uzalishaji viwandani, kuzorota kwa sekta ya huduma kutokana na kupungua soko la utalii. Hali hii imetokana na ugonjwa wa COVID-19 uliopelekea kusimama kwa shughuli za kiuchumi ikiwemo kuyumba kwa sekta ya utalii kwa kusitishwa kwa safari za ndege na kufungwa kwa mipaka. Hata hivyo, sekta ya kilimo hususani katika nchi ya Tanzania inategemewa kupanda kutokana na juhudi za Serikali za kuhakikisha uwepo wa chakula cha kutosha pamoja na kupunguza utegemezi wa kuagiza bidhaa za chakula kutoka nje. Kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika Mashariki inatarajiwa kufikia wastani wa asilimia 2.0 mwaka 2020 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 6.2 ya mwaka 2019, kinyume cha matarajio ya awali ya ukuaji wa uchumi wa asilimia 6.9.
Uchumi wa nchi ya Uganda unatarajiwa kukua kwa kasi ya wastani wa asilimia 3.5 mwaka 2020 kutoka asilimia 6.3 mwaka 2019, Kenya uchumi wake unatarajiwa kukua kwa kasi ya asilimia 1.0 kwa mwaka 2020 kutoka asilimia 5.9 mwaka 2019. Tanzania asilimia 4.0 kwa mwaka 2020 kutoka asilimia 6.8 mwaka 2019. Rwanda uchumi wake unatarajiwa kukua hadi kufikia asilimia 3.5 kwa mwaka 2020 kutoka asilimia 8.7 mwaka 2019 na nchi ya Burundi uchumi unatarajiwa kushuka na kufikia asilimia -5.5 kwa mwaka 2020 kutoka asilimia 3.3 mwaka 2019. Kupungua kwa kasi ya ukuaji wa uchumi kwa nchi zote za Jumuia ya Afrika Mashariki kutokana na kusimama kwa shughuli za uchumi ikiwemo usafirishaji, uzalishaji viwandani na utalii
2.5 Mwelekeo wa Mfumko wa Bei wa Dunia
Kasi ya mfumko wa bei wa Dunia inatarajiwa kupanda hadi kufikia wastani wa asilimia 3.6 kwa mwaka 2020 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.4 mwaka 2019. Matarajio ya kupanda kwa mfumko wa bei duniani yanachangiwa zaidi na kupanda kwa baadhi ya bidhaa kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa bidhaa za kilimo na viwandani uliosababishwa na marufuku ya kutoka nje kutokana na mripuko wa maradhi ya COVID-19. Kwa nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia kiuchumi mfumko wa bei unatarajiwa kufikia asilimia 4.8 kwa mwaka 2020
6Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
kutoka wastani wa asilimia 4.7 mwaka 2019. Hata hivyo, kasi ya mfumko wa bei kwa nchi Zilizoendelea unatarajiwa kubaki wastani wa asilimia 1.7 kwa mwaka 2020 ikilinganishwa na asilimia 1.7 mwaka 2019. Hali ya mfumko wa bei inatarajiwa kuwa tulivu kutokana na hatua za benki zinazoendelea kuchukuliwa za kupunguza viwango vya riba, Serikali kusaidia sekta za uzalishaji pamoja na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia.
3.0 MWELEKEO WA UCHUMI WA ZANZIBAR 2020Mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2020 unategemea kwenda sambamba na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2020, MKUZA III pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020. Kwa mwaka 2020 jambo kuu na la msingi litakuwa ni kuhuisha sekta za kiuchumi na kijamii ambazo zimeathiriwa na COVID-19, sambamba na kuendeleza hatua za kujenga uchumi imara na mpana zaidi (diversified). Aidha, huduma za msingi za jamii kama vile afya na elimu zitapewa kipaumbele.
Kutokana na athari za maradhi hayo, kasi ya ukuaji wa uchumi wa Zanzibar ambayo awali ilitarajiwa kufikia kasi ya ukuaji wa asilimia 7-8 haitoweza kufikiwa. Kasi ya ukuaji wa uchumi inatarajiwa kupungua na kufikia kati ya wastani wa asilimia 3 hadi 5. Hii ni kutokana na kushuka kwa kasi ya uwekezaji nchini, kupungua kwa shughuli za kibiashara kati ya Zanzibar na washirika wa kibiashara, kupungua kwa uagiziaji wa bidhaa na huduma kutokana na kufungwa kwa viwanda vya uzalishaji duniani na kupunguza mnyororo wa usambazaji wa bidhaa (supply chain) na kusimama kwa biashara na huduma zinazoambatana na sekta ya utalii. Sababu nyengine ni kusimama kwa ajira katika sekta binafsi na biashara za wajasiriamali wadogo wadogo. Hata hivyo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajia kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi kwa kuendelea kuyafanyia kazi maeneo yafuatayo ambayo yatakuwa ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa Zanzibar:
3.1. Uchumi wa Buluu
Uchumi wa Buluu unajumuisha shughuli zote zinazoambatana na maeneo
7Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ya bahari na fukwe kama vile uvuvi, utalii, usafiri wa bahari, mafuta na gesi, ufugaji wa mazao ya bahari pamoja na shughuli za kijamii za baharini. Kuwepo kwa uchumi endelevu unaotokana na Uchumi wa Buluu tunatarajia kutekeleza mambo yafuatayo:
i. Kuwa na mpango mahsusi wa matumizi ya bahari na fukwe (Marine Spatial Planning);
ii. Kuanzishwa kwa Idara inayohusiana na masuala ya Uchumi Buluu;iii. Kuwekeza zaidi katika rasilimali watu ili kupata wataalamu wa
kutosha katika eneo hili;iv. Kufanya tathmini ya kuzitambua rasilimali zetu za bahari;v. Kuhakikisha kuwa shughuli za baharini zinajumuishwa katika Sera na
Sheria pamoja na miongozo katika kupunguza umasikini.
3.2. Sera ya Viwanda ya Zanzibar
Sera ya Viwanda Zanzibar imetoa muongozo katika kuwezesha wajasiriamali katika kujiongezea vipato vyao kupitia wawekezaji wa nje na ndani, kwa kutumia mchango wa Serikali na msaada kutoka kwa washirika wa maendeleo. Baadhi ya shabaha ambazo Serikali imejiwekea kwa kusaidia Maendeleo ya viwanda vya Zanzibar ni pamoja na:
i. Kutenga ardhi na kuendeleza miundombinu ya shughuli za viwanda katika maeneo tofauti ya Zanzibar katika kuvutia wawekezaji wa ndani na nje;
ii. Kuongeza mashirikiano baina ya Vyuo vya Ufundi vya Serikali na wadau wote katika shughuli za uzalishaji viwandani.
iii. Kuongeza usimamizi wa vyuo kwa ajili ya kutoa taaluma kwa wawekezaji wadogo wadogo na wa kati ili kuongeza vipato vya wajasiriamali;
iv. Kuongeza mashirikiano baina ya taasisi, idara ambazo zinazoshughulika na biashara katika kuzuia biashara haramu na ushindani usio sawa;
v. Kushajihisha matumizi ya rasilimali inayorejesheka.
8Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
3.3 Sekta ya Utalii
Ni dhahiri kuwa Sera za Serikali zimelenga katika kuunganisha baina ya sekta ya utalii na sekta nyengine za uzalishaji ili utalii uweze kuwa na faida zaidi. Sekta ya utalii inatoa mchango mkubwa katika ukuaji wa Uchumi wa Zanzibar. Hii ni pamoja na kuunganisha sekta ya kilimo na utalii kwa kuanzisha ‘agri-tourism’. Mambo yafuatayo yataendelea kufanyiwa kazi:
i. Kushirikisha jamii katika maendeleo ya programu ya mahoteli.Wana vijiji wanaozunguka maeneo ya hoteli waweze kuuza
bidhaa za chakula na kazi za mkono;Kuwawezesha wajasiriamali ili baadhi ya bidhaa ziweze
kuzalishwa ndani. ii. Sekta mjumuisho ya program ya maendeleo ya utalii
Kuitangaza zaidi Zanzibar; Kuimarisha maeneo ya vivutio vya utalii vilivyopo kama
vile, shamba za viungo, urithi wa utamaduni wa mzanzibari na biashara;
Kukiwezesha Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kutoa wataalamu katika fani ya utalii;
Kuongeza uhusiano baina ya sekta ya utalii na sekta ya kilimo ikiwemo kupata bidhaa za chakula kutoka kwa wakulima wa ndani;
Kuhakikisha Zanzibar ni kituo cha utalii kinachozingatia kwa umakini zaidi afya ya wageni kutokana na mripuko wa maradhi ya COVID19.
iii. Kuwaunganisha wananchi na sekta ya utalii.Kuongeza usarifu wa bidhaa za chakula na kushajihisha
viwanda vya usambazaji wa vyakula kwa mahoteli na ndege za kimataifa;
Kuitumia Miongozo ya Tafsiri ya Biashara ya mwaka 2016 (Trade Transaction Regulations of 2016) ambayo inawataka wauzaji wa bidhaa na huduma kwa mkopo kuingia katika
9Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
makubaliano baina ya pande mbili);Kuwashajihisha wananchi kununua bidhaa zilizozalishwa
ndani kwa kuwapa wazalishaji unafuu wa kodi.
3.4. Viwanda Vidogo Vidogo
Viwanda vidogo vidogo vinajumuisha takribani viwanda vya usarifu na uhifadhi wa bidhaa ya chakula na zisizo za chakula. Zanzibar inayo nafasi kubwa kuongeza uzalishaji na kuleta mafanikio zaidi katika kukuza uchumi, mambo yafuatayo yataendelea kufanyiwa kazi:-
i. Kuvutia wawekezaji binafsi katika sekta mbalimbali, zikiwemo sekta ya uvuvi wa bahari kuu, ufugaji wa samaki, kuongeza thamani zao la mwani na ushajihishaji wa kilimo cha asili;
ii. Kufanya tafiti katika maeneo ya kilimo, mifugo, uvuvi na afya na hatimae kufanyiwa kazi mapendekezo yatokanayo na tafiti hizo.
4.0 MATARAJIO YA UKUAJI WA UCHUMI
Matarajio ya ukuaji wa uchumi yatatokana na kuendelea kuyafanyia kazi maeneo manne yaliyotajwa hapo juu pamoja na:-
i. Kuhuisha sekta za kiuchumi na kijamii baada ya mtikisiko wa uchumi kutokana na COVID-19;
ii. Kuimarisha sekta ndogo ya usafirishaji. Serikali pamoja na wawekezaji binafsi wanatarajiwa kuongeza meli za mizigo pamoja na abiria;
iii. Kuendelea na juhudi za kuongeza uzalishaji wa vifaranga na ufugaji wa samaki;
iv. Kuendelea kwa uvuvi wa bahari kuu baada ya kupatikana boti mbili za uvuvi;
v. Kuimarisha vituo vya utafiti vilivyopo nchini (Vituo vya utafiti wa uvuvi, kilimo, mifugo na afya);
vi. Kuongezeka kwa usafirishaji wa zao la karafuu, mwani na kuongeza mnyororo wa thamani wa zao hilo;
10Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
vii. Kuongezeka kwa uhamasishaji wa uwekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa kutekelezwa miradi mipya;
viii. Kutumika ipasavyo kwa dhana ya Sekta Mjumuisho kwa sekta za uzalishaji (Twin Engine approach)
ix. Kupunguza vikwazo vya kufanya biashara Zanzibar.
5.0 MFUMKO WA BEI WA ZANZIBAR
Kasi ya mfumko wa bei kwa mwaka 2020 inatarajiwa kuendelea kubakia katika tarakimu moja kutokana na sababu zifuatazo: -
i) Kuongezeka kwa uzalishaji wa ndani na wa nchi jirani, yakiwemo mazao ya kilimo zikiwemo mboga mboga na uzalishaji viwandani;
ii) Kuimarika kwa sekta ya Uvuvi kwa kuanza kwa shughuli za uvuvi wa bahari kuu;
iii) Serikali kuendelea kutoa punguzo maalumu la ushuru kwa bidhaa muhimu za chakula;
iv) Kuendelea kufanya ufuatiliaji wa mwenendo wa bei za bidhaa ili kudhibiti upandaji wa bei usio wa lazima;
v) Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuendelea kudhibiti kushuka kwa Shilingi ya Tanzania dhidi ya sarafu nyengine duniani;
vi) Kushajihisha na kuimarisha shughuli za uzalishaji viwandani;
6.0 SHABAHA NA MALENGO YA UCHUMI KWA 2020-2022.
Shabaha na malengo ya uchumi kwa kipindi cha miaka mitatu ni kama ifuatavyo:-
i. Kasi ya ukuaji wa Pato halisi la Taifa inategemewa kuwa baina ya asilimia 3 hadi 7;
ii. Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumko wa bei kuwa wastani wa chini ya asilimia 5;
iii. Mapato ya ndani yanakadiriwa kufikia wastani wa asilimia 26.4 ya Pato la Taifa mwaka 2020/21 kutoka asilimia 24.2 kwa mwaka 2019/20;
iv. Matumizi ya Serikali yanakadiriwa kufikia wastani wa asilimia 39.4
11Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ya Pato la Taifa mwaka 2020/21 kutoka wastani wa asilimia 38 mwaka 2019/20;
v. Kwa kipindi cha miaka mitatu nakisi ya bajeti inakadiriwa kupungua kutoka wastani wa asilimia 3.9 mwaka 2019/20 na kufikia wastani wa asilimia 2.8 mwaka 2020/21 na;
vi. Kuendelea kuwepo kwa amani na utulivu.
7.0 MWELEKEO WA BAJETI, 2020/21
Serikali itaendelea na dhamira ya kujenga jamii iliyoelimika, yenye siha kwa kuwepo uhakika wa chakula, uwezo wa kiuchumi na inayothamini na kufuata misingi ya utawala bora. Bajeti ya mwaka 2020/2021 itaendelea kuimarisha na kuendeleza maeneo yaliyozingatiwa katika Bajeti iliyopita yakiwemo (i) Huduma za Elimu (ii) Huduma za Afya na Ustawi wa jamii (iii) Miundombinu ya msingi; na (iv) Utawala bora.
7.1 Mwelekeo wa Mapato na Matumizi:
Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Serikali inatatarajia kukusanya jumla ya TZS 1,579.2 bilioni zikiwemo TZS 1,050.0 bilioni zitokanazo na vianzio vya ndani na TZS 412.7 bilioni kutoka kwa washirika wa maendeleo, TZS 45.0 bilioni ni mikopo ya ndani na TZS 61.0 billioni ni marejesho ya mkopo. Aidha, mwelekeo wa Serikali ni kukadiria kutumia jumla ya TZS 1,579.2 bilioni katika mwaka wa fedha 2020/21 bilioni ikiwemo matumizi ya Kazi za Kawaida ya TZS 969.2 bilioni na matumizi ya Kazi za Maendeleo ya TZS 609.9 bilioni.
7.1.1 Mapato ya Ndani
Jumla ya TZS 1,050.0 bilioni zinatarajiwa kukusanywa kwa mwaka 2020/21 kutoka katika vianzio vya ndani kwa mchanganuo ufuatao:
a) ZRB: inatarajiwa kukusanya TZS 516.7 bilioni b) TRA: inatarajiwa kukusanya TZS 383.5 bilioni c) Mapato ya mawizara: TZS 128.7 bilionid) Kodi ya Mapato kwa wafanyakazi wa SMT: TZS 21.0 bilioni
12Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
7.1.2 Mapato ya Nje
Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Serikali inatarajia kupokea jumla ya TZS 412.7 bilioni kutoka kwa washirika wa maendeleo; hii inajumuisha ruzuku ya TZS 72.2 bilioni na mikopo ya TZS 340.5 bilioni.
7.2 Makadirio ya Matumizi kwa Mwaka 2020/21
Kwa mwaka 2020/21 jumla ya TZS 1,579.2 bilioni zimekadiriwa kutumika kwa Kazi za Kawaida na Maendeleo sawa na ongezeko la asilimia 11.5 ya makadirio ya TZS 1,419.4 bilioni mwaka 2019/20. Kati ya fedha hizo Matumizi ya Kawaida ni TZS 969.2 bilioni na Matumizi ya Kazi za Maendeleo ni TZS 609.9 bilioni. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2020/21 utegemezi wa Bajeti unatarajiwa kupungua kutoka asilimia 6.2 kwa mwaka 2019/20 hadi kufikia asilimia 4.6. Hali hii imechangiwa na kuimarika kwa mapato ya ndani na kupungua kwa misaada ya kibajeti (GBS).
8.0 MAPENDEKEZO YA HATUA ZA KUIMARISHA MAPATO
Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Serikali inakusudia kurekebisha Sheria mbali mbali kwa lengo la kuongeza ufanisi na kuimarisha usimamizi na ukusanyaji wa mapato ya Serikali katika mwaka 2020/21 hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato. Marekebisho haya yamezingatiwa kwa umakini sana bila kuleta athari katika biashara, uwekezaji na wananchi kwa ujumla. Serikali bado itaendelea na Sera ya kutopandisha viwango vya kodi katika vyanzo vya ndani ili kuhakikisha kuwa mfumo wa kodi unaendelea kuwa tulivu kwa lengo la kuvutia uwekezaji zaidi hapa nchini. Hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa katika kuimarisha ukusanyaji wa Mapato ni pamoja na:
i. Kufanya Marekebisho katika Sheria za Kodi ili kuwawekea mazingira bora na kuwapunguzia gharama za uwajibikaji wafanyabiashara.
ii. Kufanya mapitio ya Ada na Tozo zinazosimamiwa na Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwa lengo la kuondosha mgongano wa kimajukumu
13Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
na kupunguza utitiri wa utozaji wa tozo na ada katika Sekta za kiuchumi na kijamii.
iii. Kufatilia na kudhibiti utoaji wa misamaha ya kodi kwa lengo la kupunguza mianya ya upotevu wa mapato.
iv. Kutoa elimu zaidi kwa walipakodi na kuwajengea uwezo watendaji katika nyanja mbalimbali kwa lengo la kuongeza ufanisi katika usimamizi na ukusanyaji wa mapato.
9.0 MWELEKEO WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2020/21
Mpango wa Maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2020/21, utaendelea kuzingatia utekelezaji wa MKUZA III kupitia programu na miradi ya kimkakati (Flagship projects), Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 na Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein aliyoitoa katika uzinduzi wa Baraza la Tisa la Baraza la Wawakilishi. Mpango huu ni wa awamu ya mwisho ya utekelezaji wa mikakati mikuu ya taifa ikiwemo Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020. Aidha, mwelekeo wa mwaka 2020/21 utazingatia shabaha na malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) ili kuweza Kukuza Uchumi wa Zanzibar.
Mpango huu wa mwaka 2020/21, utaendelea kuendeleza mageuzi ya kiuchumi na kijamii kwa kuimarisha uchumi endelevu, kujenga miundombinu imara, kukuza uzalishaji kwenye sekta ya kilimo, kuimarisha utalii na viwanda vidogo vidogo, kuimarisha rasilimali watu, kukuza ubora wa huduma za kijamii ikiwemo afya, elimu na kuimarisha mazingira endelevu na misingi ya utawala bora.
10.0 MAENEO YA VIPAUMBELE KWA MWAKA 2020/21
Mwaka 2020/21 ni kipindi cha mwisho cha utekelezaji wa mipango na mikakati inayomalizika muda wake ambayo ni Dira ya mwaka 2020 na MKUZA Awamu
14Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ya Tatu unaoishia mwaka 2020/21. Kwa mnasaba huo vipaumbele vya Mpango wa Maendeleo vimejikita katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 – 2020 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020. Sekta kuu za kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi zikiwemo kilimo, utalii, miundombinu, elimu na afya zitaendelea kupewa msukumo unaostahiki kupitia utekelezaji wa program na miradi mbali mbali ya maendeleo. Kwa kuzingatia umuhimu na faida zinazopatikana, vipaumbele vya mwaka 2020/21 vimepangwa katika maeneo mawili kama ifuatavyo:-
Vipaumbele vya Kwanzai. Kuhuisha uchumi baada ya athari ya maradhi ya Corona kwa kutekeleza
Mpango wa Kuhuisha Uchumi (Economic Recovery Plan – ERP)ii. Ukamilishaji wa jengo la abiria la uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Zanzibar (Terminal III);iii. Kuimarisha uchumi buluu kwa kuandaa Mpango wa Matumizi ya Bahari
na maeneo yake (Marine Spatial Plan) na kuanza utekelezaji;iv. Ujenzi wa hospital mpya ya rufaa ya Binguni;v. Ujenzi wa hospital ya Wete kuwa ya Mkoa;
vi. Kukamilisha ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu;vii. Kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji maji katika
mabonde ya Chaani, Kinyasini na Kibokwa kwa Unguja na Makwararani na Mlemele kwa Pemba;
viii. Ujenzi wa Bandari ya Mpigaduri;ix. Kuendeleza ujenzi wa mji wa kisasa Kwahani;x. Kuimarisha sekta ya mafuta na gesi kwa kuendelea na ujenzi wa
miundombinu ya matangi ya kuhifadhia mafuta katika eneo la bandari ya Mangapwani;
xi. Kuimarisha ulinzi na usalama;xii. Ujenzi wa barabara ya Chake Chake – Wete; na xiii. Ujenzi wa kituo cha maonesho ya biashara na mikutano ya kimataifa
(Convention Centre) kwa mfumo wa mashirikiano ya sekta ya umma na sekta binafsi.
15Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Vipaumbele vya Pilii. Kuendelea na kuimarisha ajira kwa vijana;
ii. Kuimarisha utalii kwa kuendeleza maeneo ya kihistoria na utalii kwa wote;
iii. Kuendeleza maeneo ya uwekezaji (Industrial Park);iv. Ujenzi wa skuli ya sheria (Law school);v. Kuanza maandalizi ya ujenzi wa mji wa kisasa kwa Pemba;
vi. Kuanza ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Fedha na Mipango Unguja;vii. Kuendelea na shughuli za utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi;viii. Kuimarisha elimu kwa ujenzi wa skuli tatu za ghorofa katika maeneo ya
Mfenesini na Gamba kwa Unguja na Kifundi kwa Pemba;ix. Ujenzi wa daraja la Uzi – Ng’ambwa;x. Ujenzi wa chelezo kwa matengenezo ya vyombo vya baharini; na
xi. Ujenzi wa barabara ya Kisauni – Fumba.
11.0 RASILIMALI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2020/21
Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2020/21 unalenga kutekeleza jumla ya programu 24 (program tatu ni mpya), na miradi 53 (miradi saba ni mipya) ya maendeleo. Jumla ya TZS 609.99 bilioni zitatumika kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo ikiwa ni ongezeko la TZS 32.97 bilioni sawa na asilimia 5.7 ikilinganishwa na Bajeti ya Maendeleo ya mwaka 2019/20 ya TZS 577.02 bilioni.
Serikali imepanga kutumia TZS 197.33 bilioni sawa na asilimia 32.35 ya Bajeti ya Maendeleo ikiwa ni ongezeko la TZS 14.93 bilioni sawa na asilimia 8.2 ya Bajeti ya Maendeleo ya mwaka 2019/20 ya TZS 182.4 bilioni. Kati ya fedha za Serikali (TZS 197.33 bilioni), TZS 110.76 bilioni ni kwa programu na miradi ya kimkakati, yenye mikataba au dhima ‘Commitment’ na TZS 86.57 bilioni kwa miradi mengine. Aidha, jumla ya TZS 412.66 bilioni sawa na asilimia 67.65 ya bajeti ya maendeleo zimepangwa kutoka kwa Washirika wa Maendeleo ikiwa
16Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
TZS 72.16 bilioni ni ruzuku na TZS 340.50 bilioni ni mikopo. Fedha hizo ni ongezeko la TZS 18.06 bilioni sawa na asilimia 4.6 ikilinganishwa na fedha zilizotengwa kwa mwaka 2019/20 zenye jumla ya TZS 394.6 bilioni.
Mgawanyo wa fedha za bajeti kiwizara na kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs) kwa programu na miradi ya maendeleo unaonekana kwenye kiambatisho namba 1 na 2. Aidha, jadweli namba 1 hapo chini linaonesha muhtasari wa mgawanyo wa fedha kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs).
17Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
16
Jadw
eli
nam
. 1:
Muh
tasa
ri w
a Fe
dha
Zili
zopa
ngw
a kw
a U
pand
e w
a Se
rika
li na
Was
hiri
ka w
a M
aend
eleo
kw
a
Prog
ram
u/M
irad
i ya
Mae
ndel
eo k
wa
Mae
neo
Mak
uu y
a M
atok
eo 2
020/
21.
EN
EO
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 (T
ZS.
"00
0")
SMZ
%
R
UZ
UK
U
MK
OPO
JUM
LA
YA
FED
HA
ZA
WA
SHIR
IKA
WA
MA
EN
DE
LE
O
%
JUM
LA
YA
BA
JET
I %
KR
A A
: K
uwez
esha
Uku
aji
wa
Uch
umi
Jum
uish
i na
Ende
levu
85
,950
,000
25
29
,323
,400
22
2,37
6,10
4 25
1,69
9,50
4 75
33
7,64
9,50
4 55
KR
A B
: Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Wat
u 3,
000,
000
82
650,
628
65
0,62
8 18
3,
650,
628
1.0
KR
A C
: Kut
oa H
udum
a B
ora
kwa
Wot
e 43
,362
,220
23
35
,068
,935
11
3,57
8,31
6 14
8,64
7,25
1 77
19
2,00
9,47
1 31
KR
A D
: K
uwep
o M
azin
gira
End
elev
u na
Uhi
mili
w
a M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i 30
0,00
0 24
96
5,71
2 0
965,
712
76
1,26
5,71
2 0.
1
KR
A
E:
Kus
hika
man
a na
M
isin
gi
ya
Uta
wal
a B
ora
64
,720
,000
86
6,
154,
702
4,54
1,00
0 10
,695
,702
14
75
,417
,702
12
JUM
LA
KU
U
197,
332,
220
32
72,1
63,3
78
340,
495,
420
412,
658,
798
68
609,
991,
018
100
18Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
12.0 MWELEKEO WA PROGRAMU NA MIRADI YA MAENDELEO KWA MAENEO MAKUU YA MATOKEO
Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar Awamu ya Tatu (MKUZA III) unatekelezwa kupitia maeneo makuu matano ya matokeo. Maeneo hayo yanatoa fursa kwa kila sekta kuweza kujua ni katika eneo lipi inaweza kujikita zaidi na kusaidia katika utekelezaji wa MKUZA III. Kwa kuzingatia hilo, mgawanyo wa programu na miradi ya maendeleo umejikita katika maeneo hayo kama ifuatavyo:
i. Kuwezesha Ukuaji wa Uchumi Jumuishi na Endelevu Hili ni eneo la kwanza katika MKUZA III ambalo linakusudia kuimarisha mazingira bora yatakayosaidia ukuaji wa uchumi endelevu ili kupambana na umasikini wa kipato. Matarajio ni kuwa na mazingira rafiki kwa ukuaji wa sekta binafsi na upatikanaji wa ajira, kuwa na uwekezaji wa umma unaotosheleza ili kusaidia miundombinu ikiwemo ya mawasiliano na vichocheo vyengine vya uchumi, kuwa na sekta yenye ushindani ya utalii yenye manufaa endelevu na jumuishi kwa wananchi, kuwepo na uzalishaji wa kisasa katika sekta za kilimo na viwanda kwa kuongeza thamani, kuwepo sekta binafsi iliyoshamiri na kuimarika kwa hifadhi ya jamii. Programu na miradi inayotekelezwa katika eneo hili ni yenye lengo la kuimarisha miundombinu ya usafirishaji ikiwemo barabara, viwanja vya ndege, bandari; kuimarisha miundombinu ya kilimo na uvuvi; kuweka mazingira bora ya biashara; na kuendeleza viwanda na utalii.
Jumla ya programu 11 (programu moja mpya) na miradi 16 (miradi mitatu mipya) ya maendeleo inatarajiwa kutekelezwa kupitia eneo hili kwa mwaka 2020/21, ambapo limetengewa TZS 337.6 bilioni sawa na asilimia 55.0 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 85.9 bilioni sawa na asilimia 25 ya bajeti ya eneo hili, Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 251.7 bilioni sawa na asilimia 75 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 29.3 bilioni na mkopo ni TZS 222.4 bilioni.
19Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ii. Kukuza Uwezo wa WatuEneo la pili linakusudia kuimarisha uwezo wa watu ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Eneo lina matarajio ya kuongeza ajira kwa watu wote (vijana, wanawake, watu wenye ulemavu) mijini na vijijini kwa kuendeleza maarifa yao na kuongeza uwezo wa wajasiriamali ili kuimarisha fursa za kuweza kujiajiri. Eneo hili linajumuisha programu na miradi inayojikita na shughuli za kukuza ajira kwa vijana, kuimarisha jinsia na kuwaendeleza wajasiriamali nchini.
Kwa mwaka 2020/21, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu mbili na mradi mmoja wa maendeleo ambapo limetengewa jumla ya TZS 3.6 bilioni sawa na asilimia 1.0 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 3.0 bilioni sawa na asilimia 82 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 650 milioni sawa na asilimia 18 ya bajeti ya eneo hili ambayo ni ruzuku.
iii. Kutoa Huduma Bora kwa WoteEneo la tatu linakusudia kuimarisha upatikanaji wa huduma bora na za kisasa kwa jamii. Matarajio ni kuwa na huduma bora za afya na usafi wa mazingira, maji safi na salama, na kupambana na maradhi yenye kuambukiza na yasiyoambukiza; kuwa na elimu bora kwa wote na jinsia zote; kuwa na makaazi bora, matumizi bora ya ardhi na upatikanaji wa nishati; kuwa na udhibiti wa unyanyasaji wa watoto na wanawake; kuwa na uwezo na utayari wa kupambana na majanga/dharura za aina zote; na kuwa na usalama wa upatikanaji wa chakula kwa jamii yote. Program na miradi inayotekelezwa kupitia eneo hili ni ile yenye azma ya kuimarisha miundombinu ya afya, elimu, maji na nishati kwa mijini na vijijini sambamba na uhifadhi wa haki za wananchi wakiwemo wazee na watoto.
Kwa mwaka 2020/21, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu saba na miradi 16 (mradi mmoja ni mpya) ambapo limetengewa jumla ya TZS 192.0 bilioni sawa na asilimia 31.0 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 43.4 bilioni sawa na asilimia 23 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo
20Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
wanatarajiwa kuchangia TZS 148.6 bilioni sawa na asilimia 77 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 35.1 bilioni na mkopo ni TZS 113.5 bilioni.
iv. Kuwepo Mazingira Endelevu na Uhimili wa Mabadiliko ya TabianchiEneo la nne linakusudia kuimarisha uwezo wetu wa kukabiliana na mabadiliko ya mazingira na tabia nchi. Matarajio ya eneo hili ni kuwa na uwezo wa kutosha wa kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi; kuwa na uhifadhi wa viumbe vya baharini na nchi kavu na kupunguza upotevu wake; kuzuia uharibifu wa mazingira na kupunguza athari za kijamii zinazotokana na shughuli za kiuchumi. Miradi inayotekelezwa katika eneo hili inalenga kuimarisha masuala ya usimamizi wa mazingira, maliasili na kuongeza uhimili wa mabadiliko ya tabianchi.
Eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya miradi miwili ambapo limetengewa jumla ya TZS 1.3 bilioni sawa na asilimia 0.1 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 300 milioni sawa na asilimia 24 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 965.7 milioni sawa na asilimia 76 ya bajeti ya eneo hili ambazo ni ruzuku.
v. Kushikamana na Misingi ya Utawala BoraEneo la tano la mkakati huu limejumuisha masuala yote ya kisheria na uongozi. Katika eneo hili inakusudiwa kuimarisha misingi ya utawala bora, haki na sheria katika ngazi zote. Matarajio ya eneo hili ni kuwa na mifumo ya kiutawala na kitaasisi yenye kuwajibika, ilio wazi na bila rushwa; kufikia usawa na uwiano wa kijinsia, jamii jumuishi, na uwezeshaji wa wanawake, watoto wa kike, vijana, walemavu, na watu walio katika mazingira hatarishi; kuwa na upatikanaji wa haki, kuheshimu utawala wa sheria, haki za msingi za binadamu na uimarishaji wa demokrasia; kuwa na uwajibikaji wa mashirika kwa jamii; na kuwa na mazingatio zaidi ya watu katika mipango. Program na miradi inayotekelezwa kupitia eneo hili ina lengo la uwekaji mazingira mazuri ya makaazi kwa wananchi na wafanyakazi, kuwepo na mageuzi ya kiutumishi, kuimarisha ulinzi na usalama nchini na kuimarisha rasilimali za ndani na usimamizi wa maliasili.
21Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Kwa mwaka 2020/21, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu nne (programu moja ni mpya) na miradi 18 (miradi mitatu mipya) ambapo limetengewa jumla ya TZS 75.4 bilioni sawa na asilimia 13 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 64.7 bilioni sawa na asilimia 82 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 10.7 bilioni sawa na asilimia 18 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 6.2 bilioni na mkopo ni TZS 4.5 bilioni.
13.0 MWELEKEO WA PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO NA SHUGHULI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA 2020/21 KIWIZARA
13.1 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ni taasisi yenye dhamana ya kusimamia kazi za Baraza la Mapinduzi (Baraza la Mawaziri), Ofisi ya Rais Ikulu na shughuli za Ushirikiano wa Kimataifa na Wazanzibari waliopo nje ya nchi (Diaspora). Aidha, ofisi hii ni kiungo muhimu cha maendeleo ya nchi katika kusimamia utekelezaji wa kazi za Baraza la Mapinduzi na kamati zake, kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza ahadi za Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na kuwapatia taarifa za shughuli za Serikali na maendeleo. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Ofisi hii imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 1.5 bilioni.
Mradi wa Uimarishaji wa Nyumba za Viongozi na Nyumba za SerikaliMradi umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha makaazi ya viongozi wakuu wa nchi kwa kuweka mazingira na mandhari nzuri ya makaazi yao pamoja na kuimarisha usalama wa nyumba hizo. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21 umepangiwa kiasi cha TZS 1.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
22Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa kutekelezwai. Kufanya ukarabati katika Ikulu ya Mnazi Mmoja;
ii. Kuendelea na ujenzi wa nyumba za makaazi katika Ikulu ya Micheweni;iii. Kujenga nyumba za viongozi wastaafu, Dodoma; iv. Kujenga ukuta katika nyumba ya makaazi ya Mheshimiwa Rais katika
Ikulu ya Dodoma;v. Ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na VIP katika Ikulu ya Dodoma;
vi. Kuzuia mmong’onyoko katika nyumba ya makaazi ya Mheshimiwa Rais katika Ikulu za Mkoani na Migombani.
13.2 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ina dhamira ya kuratibu na kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali katika sekta zote za SMZ, mambo ya Muungano kwa kufuata misingi ya Katiba, Sheria, taratibu pamoja na kupata misingi ya haki za binaadamu na ushirikishwaji. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Ofisi imepanga kutekeleza programu moja na miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 23.05 bilioni (TZS 350.0 milioni kutolewa na Serikali na TZS 22.69 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo).
Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini Awamu ya Tatu (TASAF III) Kipindi cha Pili Mpango wa Kitaifa unaotekelezwa baina ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa lengo la kuziwezesha kaya masikini sana kuongeza kipato, fursa na uwezo wa kugharamia mahitaji muhimu ya kibinadamu hasa chakula, afya na elimu pamoja na kuibua miradi ya kutoa ajira ili kuwawezesha kujikwamua na umasikini. Kwa mwaka 2020/21, programu hii awamu ya tatu katika kipindi cha pili imepangiwa jumla ya TZS 21.6 bilioni (TZS 50 milioni kutoka Serikalini na TZS 21.55 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuratibu shughuli za TASAF III kati ya Zanzibar na Dar es Salaam,
ikiwemo ufuatiliaji na tathmini ya shughuli za mradi kwa Unguja na Pemba;
23Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ii. Kufanya vikao vinne vya Kamati ya Wataalamu na viwili vya Kamati ya Uongozi wa mradi.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo i. Kufanya malipo kwa walengwa wa kaya masikini (Conditional Cash
Transfer (CCT)) kwa Shehia 388 za Unguja na Pemba;ii. Kuratibu na kuibua kaya mpya za walengwa wa Shehia za Unguja na
Pemba;iii. Kuwajengea uwezo wadau wa TASAF jinsi ya utekelezaji wa mpango
mpya; iv. Uibuaji na utekelezaji wa miradi ya ujenzi.
Mradi wa Kujenga Uwezo wa Kukabiliana na MaafaMradi huu unagharamiwa na Umoja wa Mataifa (UNDP) ukiwa na lengo la kujenga uwezo kwa jamii katika kukabiliana na maafa pamoja na kuratibu utekelezaji wa sera za kukabiliana na maafa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 186.0 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuandaa muongozo wa kusaidia kuratibu kituo cha huduma za
dharura;
ii. Kuanzisha mfumo shirikishi utakaosaidia kuhifadhi taarifa za majanga na maafa;
iii. Kufanya mapitio kwa Mpango wa Taifa wa Kukabiliana na Maafa;
iv. Kuratibu vikao vya Kamati Kiongozi na Kamati Tendaji juu ya Mpango wa Kutokomeza Kipindupindu Zanzibar.
Mradi wa Kuimarisha Usimamizi wa Mazingira, Maliasili na Mabadiliko ya Tabianchi - Zanzibar Mradi huu umeanza mwaka 2017, na una lengo la kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza za mazingira na kuongeza uhimili wa mabadiliko ya tabianchi Zanzibar, ili kufikia maendeleo endelevu. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano
24Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
baina ya Serikali na UNDP. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 589.8 milioni (TZS 300.0 milioni kutoka Serikalini na TZS 289.8 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuweka uzio wa mawe kwa ajili ya kulihami eneo lilioathirika na
mabadiliko ya tabianchi la Msuka Pemba;
ii. Ujenzi wa mtaro wa kupitishia maji ya mvua ili kuzuia mmong’onyoko wa fukwe ya Msuka.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo i. Kufanya mkutano wa Kamati ya Wataalamu na Kamati ya Uongozi ya
mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya kutathmini utekelezaji wa shughuli za mradi;
ii. Kufanya ununuzi wa kifaa cha kusomea hali ya hewa;
iii. Kutayarisha mfumo wa usimamizi na uhamasishaji wa fedha za mabadiliko ya tabianchi;
iv. Kufanya ukarabati wa Ofisi ya Idara ya Mazingira na ununuzi wa samani.
13.2.1 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Madawa ya KulevyaTume hii ina jukumu la kuratibu mapambano dhidi ya biashara, usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya, kutoa taaluma kwa jamii juu ya athari za dawa za kulevya, tiba pamoja na ushauri nasaha kwa waathirika wa dawa hizo. Kwa mwaka 2020/21, Tume imepanga kutekeleza mradi mmoja utakaogharimu jumla ya TZS 1.9 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Tiba na Marekebisho ya TabiaMradi umeanza mwaka 2018 kwa awamu ya pili (II) na una lengo la kuimarisha kituo cha matibabu na kurekebisha tabia kwa watumiaji wa dawa za kulevya. Mradi huu unatekelezwa na Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21 umepangiwa kiasi cha TZS 1.9 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
25Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa kituo cha Tiba na Marekebisho ya Tabia
-Kidimni.
13.3 Wizara ya Fedha na Mipango
Sekta ya Fedha na Mipango inajumuisha shughuli zote zinazohusiana na maendeleo ya kifedha, kiuchumi na mipango nchini ikiwemo usimamizi wa mapato na matumizi Serikalini, mwenendo na maendeleo ya mabenki na taasisi za fedha, usimamizi wa misaada, usimamizi wa mipango ya kitaifa na kimataifa, usimamizi wa uchumi mkuu pamoja na shughuli zote za taasisi nyengine zinazojihusisha na masuala ya fedha, mipango na uwekezaji nchini. Aidha, sekta hii inajukumu la kupanga na kusimamia mipango ya maendeleo ya nchi ya muda mfupi, wa kati na muda mrefu. Kwa mwaka 2020/21, Wizara hii imepanga kutekeleza programu nne na miradi minne ya maendeleo kwa gharama ya TZS 68.17 bilioni. Kati ya hizo Serikali imepanga kutoa TZS 41.92 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 26.25 bilioni.
Programu ya Ujenzi wa Ofisi za Serikali ZanzibarProgramu hii ina lengo la kugharamia ujenzi wa Ofisi za Serikali katika maeneo ambayo yamependekezwa na Serikali. Aidha, program imekusudia kuweka mazingira bora ya kazi kwa wafanyakazi wa Serikali. Kwa mwaka 2020/21, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 19.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha wa ujenzi wa jengo la Mahkama Kuu - Tunguu pamoja na
ununuzi wa samani;ii. Kuanza ujenzi wa jengo la Wizara ya Fedha na Mipango – Mazizini
Unguja; iii. Kuanza ujenzi wa Taasisi za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali (G5)
- Mazizini; iv. Kuendelea na ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya
26Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Kale;v. Kuanza matayarisho ya ujenzi wa Ofisi za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Dodoma.
Programu ya Ujenzi wa Miji MipyaProgramu hii imeanzishwa kwa lengo la kuweka miji ya Zanzibar katika muonekano mzuri pamoja na kuwapatia wananchi makaazi bora na ya kisasa. Maeneo mbali mbali yamechaguliwa na Serikali ikiwemo Kwahani ili kuweza kuyafanya miji mipya na ya kisasa kwa kujenga majengo ya kisasa na yaliyobora zaidi. Kwa mwaka 2020/21, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 20.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na ujenzi wa Mji Mpya wa nyumba za Kwahani;
ii. Kuanza matayarisho ya ujenzi wa mji mmoja Pemba.
Programu ya Ukuzaji Uchumi Jumuishi Zanzibar (BIG-Z)Programu ya Ukuzaji Uchumi Jumuishi Zanzibar ina lengo kuimarisha maeneo ya miji ya sasa na miji mengine inayoibukia ili kukabiliana na changamoto za tofauti za maendeleo na uhifadhi wa eneo la urithi wa Mji Mkongwe eneo ambalo ni kivutio kwa watalii na kulinda historia ya mji wa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, programu hii itatekelezwa kwa fedha wa Washirika wa Maendeleo pekee ambapo jumla ya TZS 19.96 bilioni zimepangwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa miundombinu ya huduma za kijamii ikiwemo maji, barabara
na maegesho ya magari;ii. Kuendeleza maeneo muhimu ya urithi wa kihistoria ya Mji Mkongwe;
iii. Kuendeleza eneo la Michenzani kwa uwekaji wa miundombinu ya kisasa (Green Corridor);
iv. Kujengea uwezo taasisi za usimamizi wa miji, kuongeza ubunifu pamoja na ununuzi wa vifaa.
27Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Programu ya Mageuzi Katika Usimamizi wa Fedha (PFMRP)Programu hii ina lengo la kuhakikisha mapato na matumizi yanasimamiwa na kudhibitiwa kwa ufanisi mkubwa. Katika kufanikisha lengo hilo, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo inatekeleza programu hii katika taasisi za Serikali, Wizara na Serikali za mitaa na kuratibiwa katika Wizara ya Fedha na Mipango. Kwa mwaka 2020/21, programu hii itatekelezwa kwa fedha za Washirika wa Maendeleo pekee ambapo jumla ya TZS 1.6 bilioni zimepangwa kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuimarisha sera za kodi na zisizo za kodi katika kuongeza mapato ya
ndani; ii. Kuimarisha mfumo wa mipango na uandaaji bajeti;
iii. Kuimarisha mfumo wa kuripoti matumizi na utekelezaji wa bajeti; iv. Kuandaa mfumo bora wa ukaguzi na udhibiti wa hesabu pamoja na
kuunganisha mifumo ya fedha za umma; v. Kuandaa ripoti ya ukaguzi na ununuzi na kufanya mafunzo kwa vitengo
vya ununuzi vya Wizara zote;vi. Kutoa mafunzo ya ukaguzi kwa watendaji 30 wa Ofisi ya Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu ukaguzi unaozingatia vihatarishi (Risk Based Audit).
Mradi wa Kujenga Uwezo Taasisi za SerikaliMradi huu una lengo la kusaidia uratibu wa ufuatiliaji na tathmini ya MKUZA III pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDG’s) na kutoa uelewa wa utekelezaji wa malengo yaliyopangwa ili kupata matokeo yake na kuhakikisha kwamba rasilimali zilizopo zinatumika kwa ufanisi unaohitajika kwa manufaa ya watu na taifa kiujumla. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Washirika wa Maendeleo (UNDP) ambapo kiasi cha TZS 126.8 milioni (TZS 20 milioni kutoka Serikalini na TZS 106.8 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zitatumika kutekeleza shughuli zifuatazo:
28Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuratibu vikao viwili vya Kamati Kiongozi na vikao vinne vya Kamati
ya Wataalamu;
ii. Kufanya ufuatiliaji wa shughuli za mradi.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kutoa uelewa kwa Serikali za Mitaa, Taasisi za Elimu ya Juu na makundi ya wanawake na vijana kuhusiana na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050;
ii. Kushiriki katika mikutano ya mashirikiano ya nchi zinazoendelea (South South Cooperation) juu ya utekelezaji wa lengo la 1 na 17 la SDGs;
iii. Kuandaa warsha juu ya utayarishaji wa Mpango wa Maendeleo wa muda wa kati katika kutekeleza Dira ya 2050;
iv. Kuwasilisha maeneo ya vipaumbele vya Dira 2050 kwa Washirika wa Maendeleo.
Mradi wa Uimarishaji wa Rasilimali za Ndani na Usimamizi wa MaliasiliMradi wa Uimarishaji wa Rasilimali za Ndani na Usimamizi wa Maliasili ni mradi unaotekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa lengo la uimarishaji wa rasilimali za ndani na usimamizi wa maliasili. Taasisi zinazonufaika na mradi ni Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tawi la Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 4.6 bilioni ambapo Serikali itatoa TZS 100.0 milioni na Washirika wa Maendeleo TZS 4.5 bilioni kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali i. Kuratibu vikao vya kamati;
ii. Kuandaa mikutano ya Washirika wa Maendeleo.
29Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Ununuzi wa vifaa vya Ofisi ya ZURA; ii. Kuandaa mifumo itakayoongeza uwezo wa ZRB kukusanya mapato
pamoja na ununuzi wa vifaa;iii. Kujenga uwezo kwa watendaji wa Mamlaka ya Ukusanyaji wa Mapato
Tanzania;iv. Kutoa mafunzo kwa wateja kuhusiana na ulipaji wa kodi.
Mradi wa Kuimarisha Maeneo Huru Mradi huu umeanza mwaka 2020, ukiwa na lengo la kuendeleza maeneo huru ya uchumi kwa kuweka miundombinu itakayovutia kwa lengo la kukuza uchumi wa viwanda nchini. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 1.8 bilioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwai. Ujenzi wa barabara na uwekaji wa miundombinu ya maji na umeme
katika eneo la Micheweni-Pemba.
Mradi wa Mtandao wa Uingizaji wa Taarifa za BajetiMradi huu umeanza mwaka 2020 ukiwa na lengo la kuimarisha utayarishaji na usimamizi wa utekelezaji wa bajeti. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 500 milioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya ununuzi wa vifaa vya mtandao na kompyuta kwa Serikali za
Mitaa na Serikali Kuu;ii. Kutoa mafunzo ya “system” kwa Serikali za Mitaa na Serikali Kuu;
iii. Kufanya uhakiki wa taarifa za kibajeti.
30Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.3.1 Tume ya Mipango Zanzibar
Tume ya Mipango ya Zanzibar ni chombo cha juu chenye dhamana ya kupanga, kuratibu na kusimamia mipango ya kiuchumi na kijamii. Aidha, chombo hiki kinashughulikia uratibu na upangaji wa vipaumbele vya Taifa, sambamba na kuelekeza, kutoa miongozo na kusimamia masuala ya kiuchumi na mipango ya maendeleo. Kwa mwaka 2020/21, Tume ya Mipango imepanga kutekeleza programu mbili na miradi mitano ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 12.8 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali itatoa TZS 8.3 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 4.5 bilioni.
Programu ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA)Programu hii imelenga kuwakwamua wananchi na umasikini kupitia urasimishaji wa biashara na ardhi ili ziweze kutumika katika juhudi za kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kwa mwaka 2020/21, programu imepanga kutumia kiasi cha TZS 650 milioni (TZS 550.0 milioni kutoka Serikalini na TZS 100.0 milioni kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
i. Kutayarisha na kuchapisha hati za usajili kwa maeneo yaliyotambuliwa;ii. Ununuzi wa vifaa vya upimaji;
iii. Kutoa mafunzo na kuwahakiki wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chake Chake;
iv. Urasimishaji wa ardhi maeneo ya Mbweni, Magomeni na Sogea.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
i. Kujenga uwezo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo juu ya usimamizi na uendeshaji wa biashara Wilaya ya Kusini -Unguja;
ii. Kuratibu vikao viwili vya Kamati Kiongozi na vikao vinne vya Kamati ya Wataalamu;
31Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
iii. Kufanya ufuatiliaji wa shughuli za mradi.
Mpango wa Kuhuisha Uchumi (ERP)Mpango wa Kufufua Uchumi ni mpango maalum ulioanzishwa na Serikali ili kuweza kuzihuisha sekta za kiuchumi na kijamii ambazo zitaathirika kutokana na maradhi ya Corona. Athari hizo zinatokana na kusitishwa kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi kama vile uingiaji wa watalii ili kupunguza usambazaji wa ugonjwa wa Corona ambako kupelekea baadhi ya sekta hususan za kiuchumi kuathirika. Hivyo, Serikali kupitia Tume ya Mipango Zanzibar imepanga kuhuisha uchumi katika mwaka wa fedha wa 2020/21 kupitia mpango wake wenye lengo la kuhuisha uchumi. Mpango huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa jumla ya TZS 7.0 bilioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuzihuisha na kuziendeleza sekta zilizoathirika kutokana na janga la
maradhi ya Corona.
Mradi wa Kupunguza Umasikini na Ufuatiliaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs)Mradi umeanzishwa kwa lengo la kusaidia Serikali katika jitihada zake za kupambana na umasikini Zanzibar. Mradi umejikita katika kuandaa mikakati mbali mbali itakayosaidia nchi na wananchi wake katika kuibua na kutekeleza mipango na miradi mbali mbali itakayowawezesha kujikwamua na umasikini. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa jumla ya TZS 150 milioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Utayarishaji wa Mkakati wa Maendeleo wa Zanzibar wa muda wa kati
2021 - 2025; ii. Kufanya utafiti wa shehia masikini zitakazotambuliwa katika ripoti ya
Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya (ZHBS) 2019/20;
32Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
iii. Kufanya uchambuzi wa bajeti kwa programu na miradi ya maendeleo.
Mradi wa Uratibu na Usimamizi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na MKUZA IIIMradi umeanzishwa kwa lengo la kujenga uwezo kwa taasisi za Serikali na zisizo za Kiserikali katika kusimamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, uratibu wa MKUZA III na namna ya kuandika na kutoa taarifa za programu na miradi ya maendeleo. Aidha, mradi huu umepanga kuimarisha mfumo wa takwimu Zanzibar kwa kuandaa mkakati, sera na kutoa mafunzo kwa wazalishaji na watumiaji wa takwimu. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 901.1 milioni (TZS 100.0 milioni kutoka Serikalini na TZS 801.1 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kufanya tathmini ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza
Umasikini Zanzibar – Awamu ya Tatu (MKUZA III).
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuandaa ripoti ya mwaka ya Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs);
ii. Kuandaa Mpango wa Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu;iii. Kuimarisha mashirikiano ya kisekta na midahalo kuhusu Malengo ya
Maendeleo Endelevu kwa taasisi za Serikali, binafsi na Asasi za Kiraia;iv. Kuandaa semina elekezi kwa viongozi wa dini, Masheha na Radio Jamii
na Asasi zisizokuwa za Serikali juu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu.
Mradi wa Kuimarisha Utafiti na UbunifuMradi wa Kuimarisha Utafiti na Ubunifu umeanzishwa kwa lengo la kukiimarisha kitengo cha utafiti katika Tume ya Mipango ili kuweza kusimamia tafiti mbali mbali za kiuchumi na kijamii hapa Zanzibar. Aidha, mradi huu una azma ya kushirikiana na taasisi mbali mbali katika kuibua na kusimamia tafiti kama
33Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
zilivyoainishwa katika agenda ya Utafiti Zanzibar. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa jumla ya TZS 500 milioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuratibu na kufanya tafiti kama zilivyoainishwa katika Agenda ya Utafiti
Zanzibar;ii. Kujenga uwezo kwa maafisa wa Serikali juu ya kuandika ripoti na kutumia
“software” za kompyuta kwa ajili ya kufanya uchambuzi wa taarifa za tafiti;
iii. Kufanya manunuzi ya vifaa vya ofisini;iv. Kuipitia na kubainisha maeneo mapya ya utafiti ambayo yatabainishwa
katika Agenda ya Utafiti Zanzibar.
Mradi wa Uzalishaji na Utumizi wa Taarifa za Idadi ya Watu
Lengo kuu la mradi huu ni kuona kwamba kuna takwimu sahihi na stahiki zilizochambuliwa katika makundi tofauti kutokana na vyanzo mbali mbali ikiwemo sensa, tafiti na kadhalika. Aidha, taasisi zote za Serikali, taasisi za elimu ya juu na vituo vya tafiti vinatumia vigezo vya masuala ya idadi ya watu wakati wa upangaji wa sera na mipango yao. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Washirika wa Maendeleo (UNFPA). Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 286 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuimarisha mfumo ya takwimu katika ngazi za chini za Serikali kupitia
daftari la shehia na kufanya ufuatiliaji;ii. Kuimarisha mfumo wa usajili wa vizazi na vifo katika ngazi za chini za
Serikali;iii. Kuimarisha mfumo wa takwimu za watu wenye ulemavu Zanzibar;iv. Kuandaa vikao vya kila robo mwaka vya masuala ya idadi ya watu;
34Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
v. Kuimarisha mfumo wa takwimu wa taarifa za Malengo Endelevu ya Dunia kupitia muundo wa uwasilishaji na ufuatiliaji.
Mradi wa Uendelezaji Takwimu Zanzibar (ZSDP)Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha uzalishaji na usimamiaji wa takwimu sahihi katika mfumo wa takwimu Zanzibar ambazo zitatumika kwa ajili ya kufuatilia na kutathmini mipango ya maendeleo ya kisekta, kitaifa, kikanda na kimataifa. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Washirika wa Maendeleo. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 3.3 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwai. Utekelezaji wa Mkakati wa Maendeleo ya Takwimu Zanzibar;ii. Kuendelea na kazi za utafiti wa kufuatilia kaya;iii. Kufanya utafiti wa Hali ya Afya ya Mama na Mtoto;iv. Kujenga uelewa wa utekelezaji wa SDGs;v. Kuimarisha takwimu za jinsia;vi. Kuendelea na kazi za Sensa ya Kilimo na Mifugo;vii. Kuanza kazi za matayarisho ya Sensa ya Watu na Makaazi ya mwaka
2022;viii. Kufanya Utafiti wa Watu Wenye Uwezo wa Kufanya Kazi.
13.4 Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi
Sekta ya kilimo ni miongoni mwa mihimili mikuu ya uchumi wa Zanzibar ambayo inatoa mchango wa moja kwa moja katika kujikwamua na umasikini. Sekta hii ina jukumu kubwa la kuimarisha huduma za kilimo kwa upatikanaji wa mbegu, utoaji wa mafunzo kwa wakulima, wavuvi na wafugaji, uhifadhi wa mazao, samaki na mifugo pamoja na upatikanaji wa teknolojia za kisasa za kilimo, mifugo na uvuvi. Kwa mwaka 2020/21, Wizara hii imepanga kutekeleza programu tatu na miradi saba ya maendeleo kwa gharama ya TZS 106.54 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 23.0 bilioni na Washirika wa
35Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 83.54 bilioni.
Programu ya Umwagiliaji Programu hii imekusudia kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji maji kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga kwa wakulima sambamba na kuwajengea uwezo wa kitaalamu wakulima juu ya uzalishaji bora kwa kutumia pembejeo za kilimo. Kwa mwaka 2020/21, programu hii imepangiwa jumla ya TZS 67.09 bilioni (TZS 19.9 bilioni kutoka Serikalini na TZS 47.19 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuendelea na ulipaji wa fidia ya mazao kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu
ya umwagiliaji katika mabonde ya Chaani na Kinyasini kwa Unguja, Makwararani na Mlemele kwa Pemba;
ii. Kufanya malipo ya mchango wa Serikali wa asilimia 12.5 kwa mwaka wa pili kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji.
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa fedha kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya Chaani, Kilombero, Kibokwa na Kinyasini kwa Unguja na Mlemele na Makwararani kwa Pemba.
Programu ya Kusaidia Kilimo na Uhakika wa Chakula (ERPP)Program hii ina lengo la kuongeza mbegu bora za mpunga kwa utumiaji wa teknolojia ya uzalishaji wa zao la mpunga. Kwa mwaka 2020/21, programu imepangiwa jumla ya TZS 2.21 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa i. Kutoa mafunzo kwa wakulima wa uzalishaji wa mbegu za mpunga katika
bonde la Kibonde Mzungu (wakulima 76) na Ole (wakulima 24);ii. Kutoa mafunzo ya mbinu bora za uzalishaji wa mpunga kwa maafisa
36Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ugani Unguja na Pemba;iii. Kutoa mafunzo ya kilimo shadidi (SRI) kwa wakulima kupitia mashamba
40 ya mfano; iv. Kutoa mafunzo kwa wakulima juu ya mbinu mchanganyiko za kudhibiti
wadudu na maradhi ya mimea (IPM);v. Kufanya ziara ya kujifunza Tanzania Bara;
vi. Kununua mbegu za mpunga tani 12 kwa ajili ya mpango wa ruzuku kwa wakulima.
Programu ya Kuimarisha UvuviProgramu hii ina dhamira ya kuendeleza uvuvi na kuongeza uzalishaji wa samaki na mazao ya baharini pamoja na kusimamia na kuhifadhi rasilimali za baharini kwa matumizi endelevu. Programu hii ina miradi miwili ifuatayo: Uimarishaji Uvuvi wa Bahari KuuLengo la mradi huu ni kuendeleza shughuli za uvuvi kwa ujenzi wa miundombinu ya uvuvi na kuwawezesha wavuvi kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 14.15 bilioni (TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini na TZS 12.15 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Mchango wa Serikali wa asilimia nane (8%) katika ujenzi wa jengo la
soko la Malindi.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kukamilisha ujenzi wa jengo la soko la samaki Malindi.
Kuimarisha Ufugaji wa Mazao ya BahariniMradi huu una lengo la kushajihisha ufugaji wa mazao yatokanayo na bahari ikiwemo samaki, majongoo ya bahari na kaa kwa lengo la kupata tija kwa haraka.
37Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 736.48 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ununuzi wa samaki wazazi kwa ajili ya upatikanaji wa vifaranga;
ii. Ununuzi wa vifaa kwa ajili ya utengenezaji wa chakula cha samaki;
iii. Kutoa mafunzo ya mbinu bora za ufugaji wa samaki, kaa na majongoo bahari kwa wafugaji wa mazao ya baharini;
iv. Kutoa mafunzo ya utengenezaji wa mashamba ya kufugia kaa, samaki na majongoo bahari kwa vikundi vya ufugaji wa mazao ya baharini.
Mradi wa Kuendeleza Utafiti wa MifugoLengo la mradi huu ni kuijengea uwezo Taasisi ya Utafiti wa Mifugo kuweza kufanya tafiti kwa ufanisi zaidi ili kuongeza uzalishaji bora wa mifugo na bidhaa zake. Mradi unakusudia kuimarisha miundombinu ya utafiti wa kilimo. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa maabara tano za utafiti wa mifugo;
ii. Ujenzi wa kiwanda cha kati cha chakula cha mifugo; iii. Ujenzi wa ukuta katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo.
Mradi wa Usimamizi wa Shughuli za Uvuvi wa Kanda ya Kusini Mashariki mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH)Lengo la mradi huu ni kushajihisha jamii juu ya kuendeleza uvuvi maalum uliopewa kipaumbele kwa dhamira ya kuongeza kipato kwa jamii. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 8.65 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na ujenzi wa Ofisi ya Maabara ya Taasisi ya Uvuvi Maruhubi;
38Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ii. Kuendelea na ujenzi wa chelezo Malindi; iii. Kutoa mafunzo kwa wavuvi juu ya uvuvi wa kipaumbele Unguja na
Pemba;iv. Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi 10 shahada ya uzamili (masters) na
watatu shahada ya uzamivu (PhD); v. Kuendelea kupitia Sheria ya Uvuvi;
vi. Kurekebisha mfumo wa takwimu za uvuvi.
Mradi wa Kudhibiti Sumu Kuvu Inayotokana na Ulaji wa Mahindi na NjuguLengo la mradi huu ni kupunguza athari zinazotokana na sumu kuvu kwenye mahindi na njugu kwa kuongeza taaluma na kuimarisha miundombinu na teknolojia kabla na baada ya mavuno. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 931.7 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kutoa mafunzo juu ya mbinu bora za kuzuia upotevu wa mazao kabla na
baada ya mavuno; ii. Kufanya tathmini ya athari ya sumukuvu Unguja na Pemba;
iii. Kutengeneza michoro (BoQ) kwa ujenzi wa ghala Unguja na Pemba;iv. Ujenzi wa ghala na ununuzi wa vifaa kwa ajili ya kuhifadhia mazao;v. Mafunzo kwa watendaji na wananchi juu ya kujikinga na kudhibiti athari
za sumukuvu; vi. Kujenga uwezo kwa wafanyakazi, wazalishaji wa mazao na wauzaji juu
ya kukinga na kudhibiti athari za sumukuvu; vii. Kufanya tathmini ya athari za kimazingira na kijamii juu ya uendelezaji
wa miundombinu ya mradi.
Mradi wa Uhifadhi wa Misitu kwa Faida za KiuchumiLengo la mradi huu ni kupunguza wimbi lisiloendelevu la bidhaa zinazotokana na misitu ili kuendeleza rasilimali za misitu. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 3.80 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
39Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwai. Kutoa mafunzo ya uhifadhi wa misitu kwa jumuiya za wakulima;
ii. Kufanya tafiti za kilimo;iii. Kufanya upembuzi wa awali wa mradi;iv. Ujenzi wa ofisi za misitu ya kihifadhi.
Mradi wa Kilimo cha Kushajihisha Ukulima wa Mboga na MatundaMradi huu una lengo la kusaidia mnyororo wa thamani wa mazao ya mboga mboga sambamba na upotevu wa mazao hayo baada ya mavuno. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 5.60 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ununuzi wa vifaa vya kulimia kilimo cha mboga ikiwemo vifaa vya
kuhifadhia maji, mbegu na mipira ya umwagiliaji maji;ii. Kutoa mafunzo kwa wakulima wa mboga na maafisa ugani;
iii. Ununuzi wa vifaa vya kuhifadhia mazao;iv. Kuandaa Mpango Mkakati na Mpango wa Utekelezaji wa Mradi. v. Kufanya uzinduzi wa mradi;
vi. Kufanya tathmini ya awali ya mradi; vii. Kufanya mikutano na wadau juu ya ulimaji wa kilimo cha mboga.
Mradi wa Mandeleo ya Kilimo na UvuviMradi huu ni mradi unaotekelezwa kwa mashirikiano baina ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa upande wa Zanzibar mradi huu umejikita zaidi katika kuimarisha shughuli za uvuvi kwa kuwawezesha wananchi kuweza kuvua katika kina kirefu cha maji. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 2.14 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwai. Kufanya upembuzi wa awali wa mradi;
ii. Kuanza na taratibu za ununuzi wa boti nne za kuvulia;
40Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
iii. Kujenga bwawa la kufugia samaki Pemba;iv. Kujenga bwawa la kupokelea vifaranga Pemba;v. Kutoa mafunzo kwa wafugaji wa mazao ya baharini ikiwemo kaa,
majongoo bahari na samaki.
Mradi wa Kudhibiti Nzi wa MatundaMradi huu una lengo la kupunguza upotevu wa matunda unaosababishwa na wadudu waharibifu. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 220.0 milioni (TZS 100.0 milioni kutoka Serikalini na TZS 120.0 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kutoa mafunzo kwa maafisa ugani;
ii. Kuratibu vikao vya kamati ya wataalamu.
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa Fedha kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Ununuzi wa vifaa vya kunasia nzi ikiwemo mitego na dawa za kunasia nzi;
ii. Kutoa mafunzo kwa maafisa wa kilimo jinsi ya kutambua aina ya wadudu;iii. Kutoa mafunzo juu ya uwekaji wa mitego ya kunasia nzi wa matunda.
13.5 Wizara ya Biashara na Viwanda
Malengo makuu ya Wizara ya Biashara na Viwanda ni kukuza biashara nchini na uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na kuleta maendeleo. Katika bajeti ya mwaka 2020/21, Wizara inaendelea kutekeleza shughuli za maendeleo kupitia programu na miradi ya maendeleo iliyojipangia ili kusaidia kupunguza uagiziaji wa bidhaa kutoka nje, kujenga mnyororo wa thamani, kuongeza ajira na kuongeza pato la taifa. Wizara hii imepanga kutekeleza programu mbili na miradi miwili ya maendeleo kwa gharama ya TZS 14.8 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 10.2 bilioni na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 4.6 bilioni.
41Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Programu ya Mazingira Bora ya BiasharaProgramu hii ina lengo la kutoa huduma za kuimarisha sekta ya biashara na kutoa msaada kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa nchini. Kwa mwaka 2020/21, programu hii inatarajia kutumia fedha za Serikali pekee na imepangiwa jumla ya TZS 300 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya ununuzi wa magazebo;
ii. Kuendeleza Uwanja wa Maonesho wa Kimataifa wa Zanzibar (Nyamanzi);iii. Kuendeleza Mkakati wa “Branding” Awamu ya Pili (Branding Phase II);iv. Kufanya utafiti wa kuainisha bidhaa zinazotengenezwa Zanzibar (Made
in Zanzibar);v. Kujenga uwezo kwa Wajumbe wa Mabaraza ya Biashara ya Mikoa;
vi. Kuandaa ziara ya kimafunzo kwa Wajumbe wa Baraza la Taifa la Biashara /Mikoa;
vii. Kufanya ununuzi wa vifaa vya Ofisi kwa Mabaraza ya Mikoa.
Programu ya Kuendeleza ViwandaKatika kutekeleza programu ya viwanda, Wakala wa Kusimamia na Kuendeleza Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati (SMIDA) ina jukumu la kuwalea wazalishaji kwa kuwapatia mafunzo na ushauri wa kitaalamu katika bidhaa zao. Programu hii kwa mwaka 2020/21 imepangiwa TZS 11.1 bilioni (TZS 6.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 4.6 kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) na itatekelezwa kupitia miradi mitatu kama ifuatavyo:
Mradi wa Kuimarisha Maeneo Tengefu ya Viwanda (Industrial Park)Mradi huu umeanzishwa mwaka 2020, ukiwa na lengo la kuanzisha maeneo tengefu ya viwanda ili kubadili muelekeo wa uchumi wa Zanzibar kwa kuhamasisha sekta ya kilimo ambayo ina mchango mkubwa wa kutoa malighafi kwa ajili ya kuendeleza viwanda vidogo na vya kati, sambamba na kupunguza umasikini na kutoa fursa mpya za ajira kwa vijana wa mijini na vijijini. Kwa
42Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya kazi za kusafisha eneo na uwekaji wa uzio Dunga na Nungwi;
ii. Kufanya upembuzi yakinifu katika eneo la viwanda Dunga na Nungwi;iii. Kuimarisha miundombinu katika maeneo ya Dunga na Nungwi.
Mradi wa Kuimarisha Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuongeza thamani ya bidhaa na ubora wa vifungashio ili kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kufanya shughuli zao kwa ufanisi. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Wakala wa Maendeleo ya Viwanda
Vidogo Vidogo na Vya Kati (SMIDA).
Mradi wa Kuwasaidia Wajasiriamali Wadogo Wadogo, Wakati na WakubwaMradi wa kuwasaidia wajasiriamali unakusudia kuwaunganisha pamoja na kuwapatia mafunzo ya vitendo wajasiriamali hao ili waweze kuendeleza biashara zao sambamba na kuwawezesha kwa kuwapatia mikopo. Mradi huu unatekelezwa kwa pamoja na Mfuko wa Maendeleo kutoka falme za Kiarabu katika kuwaendeleza wajasiriamali wadogo wadogo. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 9.1 bilioni (TZS 4.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 4.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo wadogo Unguja na Pemba
kwa kuwapatia elimu ya ujasiriamali;ii. Uratibu na usimamizi wa mradi;
iii. Kuimarisha miundombinu.
43Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo wadogo Unguja na Pemba kwa kuwapatia elimu ya ujasiriamali;
ii. Kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia mikopo.
Mradi wa Kuimarisha Taasisi ya Viwango ZanzibarViwango ni jambo muhimu katika kuongeza ubora na ushindani wa bidhaa zinazozalishwa nchini, Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) inasimamia ubora wa viwango vya bidhaa zote zinazoingizwa nchini na zile zinazotengenezwa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 3.0 bilioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na ujenzi wa ofisi na maabara ya Taasisi ya Viwango Zanzibar;ii. Ununuzi wa vifaa vya maabara.
Mradi wa Mfumo Mpya wa Utoaji Leseni kwa Maendeleo ya Sekta BinafsiMradi huu una lengo la kuweka taratibu na udhibiti wa utoaji leseni na kuimarisha usajili kwa njia ya kielektroniki ili kuwa na takwimu sahihi za wafanyabiashara waliosajiliwa. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 400 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kusimamia utekelezaji wa mfumo mpya wa utoaji leseni kwa njia ya
kielektroniki;ii. Kuunganisha mfumo baina ya Baraza la Kusimamia Mfumo wa Utoaji
Leseni (BLRC) na Mamlaka zinazotoa leseni kwa upande wa Serikali Kuu;
iii. Kuunganisha mfumo baina ya BLRC na Mamlaka za Serikali za Mitaa;iv. Kufanya utafiti wa urahisi wa ufanyaji biashara kwa kutumia vigezo vya
benki ya dunia;
44Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
v. Kufanya utafiti wa utaratibu wa utoaji leseni kwa kutumia tathmini ya usimamizi (Regulatory Impact Asessement).
13.6 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Sekta ya Elimu ni moja ya kichocheo muhimu cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Taifa lolote hapa duniani ambapo rasilimali muhimu zinapoekezwa katika elimu, hupelekea kukuwa kwa ubora na uwezo wa watu katika taifa hilo. Kwa mnasaba huo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikijitolea kuekeza katika sekta hii ili kuongeza ubora na usawa wa upatikanaji wa elimu bora, na kuhakikisha kuwa raia wote wana uwezo wa msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu. Kwa mwaka 2020/21, sekta ya elimu imepanga kutekeleza programu moja na miradi miwili ya maendeleo yenye jumla ya TZS 19.46 bilioni ambapo Serikali imepanga kutoa TZS 4.5 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 14.96 bilioni.
Programu ya Miundombinu ya ElimuProgramu hii imeanzishwa kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya sekta ya elimu kiujumla ili kuwawezesha wananchi kuweza kupata elimu bora na yenye kukidhi mahitaji yao. Programu inatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali ambapo jumla ya TZS 1.0 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa madarasa 50 yaliyoanzishwa na wananchi Unguja
na Pemba na kujenga nyumba 10 za walimu;
ii. Kuendelea na ujenzi wa Ofisi ya Mkaguzi Mkuu Wilaya ya Kaskazini B na ununuzi wa vifaa vya kufanyia kazi;
iii. Kujenga ghala mbili Unguja na Pemba.
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya MsingiLengo kuu la mradi wa uimarishaji elimu ya msingi ni kutoa elimu bora kwa watoto wote wa Zanzibar kwa ngazi ya msingi. Mradi huu unatekelezwa na
45Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Washirika wa Maendeleo ambapo jumla ya TZS 402.2 milioni zitatumika kwa utekelezaji wa shughuli za mwaka 2020/21 kama zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea kuwapatia chakula wanafunzi katika skuli 27 za msingi;
ii. Kuimarisha elimu ya msingi katika lugha ya Kiingereza darasa la kwanza hadi la nne;
iii. Kuzipatia zawadi skuli 100 zinazofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya darasa la sita.
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya LazimaLengo kuu la mradi wa uimarishaji elimu ya lazima ni kuhakikisha kwamba Wazanzibari wote wanapata haki yao ya kupatiwa elimu na kupunguza umasikini. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo ambapo jumla ya TZS 18.0 bilioni (TZS 3.5 bilioni za Serikali na TZS 11.3 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka 2020/21 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuanza ujenzi wa skuli tatu za ghorofa katika maeneo ya Mfenesini na
Gamba kwa Unguja na Kifundi kwa Pemba;
ii. Kuandaa Mtaala wa Elimu ya Maandalizi na Msingi;
iii. Kupitia na kuandaa vitabu pamoja na miongozo ya walimu kwa ajili ya Mitaala ya Maandalizi na Msingi;
iv. Ununuzi wa vitabu vya masomo ya Kemia, Fizikia, Baiolojia na Kiswahili kwa kidato cha kwanza, pili, tano na sita.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuanza ujenzi wa skuli tatu za ghorofa katika maeneo ya Mfenesini na Gamba kwa Unguja na Kifundi kwa Pemba;
46Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ii. Kujenga maabara katika skuli 15 za Unguja na Pemba;
iii. Kupitia na kuandaa vitabu pamoja na miongozo ya walimu kwa ajili ya Mitaala ya Maandalizi na Msingi;
iv. Kuandaa Mtaala wa Mafunzo ya walimu wa Maandalizi na Msingi;
v. Kuzipatia zawadi skuli 200 zinazofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kidato cha pili (100) na kidato cha nne (100);
vi. Kuzisaidia skuli gharama za kujiendesha kufuatia kufutwa kwa michango ya wazee;
vii. Kuupitia na kuandaa mfumo wa mitihani;
viii. Kutoa mafunzo kwa walimu wa msingi darasa la tano, sita na sekondari ya kuwasaidia watoto wenye ufahamu mdogo;
ix. Kuimarisha science, technolojia, engineering and maths (STEM).
13.7 Wizara ya Afya
Sekta ya Afya ina jukumu la kuhakikisha kuwa Wazanzibari wote wanapata huduma bora za afya. Sekta hii inalenga kutekeleza lengo la MKUZA III la kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya kwa kuzingatia makundi maalum ikiwa na shabaha ya kuimarisha uwezo wa sekta ya afya na taasisi zake juu ya upatikanaji wa huduma bora za afya. Kwa mwaka 2020/21, sekta ya afya imepanga kutekeleza programu nne za maendeleo zenye jumla ya TZS 42.65 bilioni ambapo Serikali imepanga kutoa TZS 21.00 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 21.65 bilioni.
Programu ya Kumaliza Maradhi ya Malaria ZanzibarProgramu hii ina lengo la kutokomeza maradhi ya malaria kwa kuhakikisha kwamba maradhi haya yanamalizika kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba. Aidha, programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo. Kwa mwaka 2020/21,
47Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
programu imepangiwa jumla ya TZS 5.8 bilioni (TZS 248.0 milioni kutoka Serikalini na TZS 5.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Ununuzi wa dawa za malaria (ASAQ dose 15,000 na Inj Antersunate
7,488);ii. Kufanya mafunzo na ugawaji wa dawa kwa maeneo yanayotoka wagonjwa
wa malaria na uchapishaji wa vitendea kazi;iii. Ununuzi wa vitendanishi na vifaa vya uchunguzi wa vimelea vya malaria
kwa njia ya darubini na vinasaba vya ugonjwa wa malaria; iv. Ununuzi wa ndege nyuki (drones) itakayosaidia utiaji dawa kwenye
madimbwi ambayo hayawezi kufikiwa; v. Uchukuaji wa hatua za haraka za udhibiti wa hali ya ugonjwa wa malaria
na miripuko itokanayo na mbu ikiwemo upigaji wa dawa na ununuzi wa vyandarua.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kufanya uchunguzi na utibabu wa ugonjwa wa malaria;ii. Kuendelea na udhibiti wa mbu waenezao ugonjwa wa malaria;
iii. Kufanya ufuatialiaji wa mwenendo wa ugonjwa wa malaria.
Programu ya Kuimarisha Miundombinu ya AfyaProgramu hii ina lengo la kuimarisha huduma za afya zitolewazo nchini na inajumuisha miradi saba yenye gharama ya TZS 21.4 bilioni kama ifuatavyo:-
Mradi wa Kuipandisha Hadhi Hospitali ya Mnazi MmojaMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja ili ifikie ngazi ya kutoa huduma za rufaa kwa kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma za afya zikiwemo huduma za afya ya mama na mtoto, huduma za matibabu ya ubongo na uti wa mgongo; na huduma za upasuaji wa
48Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
maradhi mbali mbali. Mradi huu, unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 1.5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na ukarabati wa jengo la upasuaji katika hospital ya Mnazi
Mmoja;ii. Kufanya ununuzi wa vifaa mbali mbali vya utoaji wa huduma za afya
ikiwemo vifaa vya matibabu ya mifupa na macho.
Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Binguni (Awamu ya Kwanza)Mradi huu una lengo la kujenga hospitali ya kisasa ya rufaa na kufundishia kwa Zanzibar, ambayo inatarajiwa kufundisha fani za madaktari bingwa, wauguzi na madaktari wetu ambao watakuwa mafunzoni. Mradi huu unatekelezwa kwa kutumika fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 6.0 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa
i. Kuendelea na ujenzi wa hospitali ya kisasa ya rufaa na kufundishia ya Binguni.
Kuimarisha Taasisi ya Utafiti wa AfyaMradi wa kuimarisha utafiti wa afya umeanzishwa mwaka 2020 kwa lengo la kupata taarifa zitakazopelekea kufanya maamuzi sahihi juu ya magonjwa mbali mbali. Mradi huu unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 2.0 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa maabara ya Taasisi ya Tafiti za Afya (ZAHRI);
ii. Ununuzi wa vifaa vya maabara kwa Taasisi ya Tafiti za Afya.
49Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Wagonjwa wa AkiliMradi huu umeanza mwaka 2017, ukiwa na lengo la kuimarisha huduma za afya ya akili nchini. Aidha, hospitali hii inatarajiwa kutumika katika kufundishia utoaji wa huduma za afya ya akili na kufanya tafiti za maradhi ya akili. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Chuo Kikuu cha Houkland - Uholanzi (Houkland University), ambapo jumla ya TZS 2.8 bilioni (TZS 1.4 bilioni za Serikali na TZS 1.4 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka 2020/21 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali na Washirika wa Maendeleo
i. Kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wagonjwa wa Akili - Kidongo Chekundu.
Mradi wa Kuzipandisha Hadhi Hospitali za Wilaya na Hospitali za VijijiMradi huu umeanza mwaka 2011, ukiwa na lengo la kuzipandisha hadhi hospitali za Makunduchi, Kivunge na Wete kuwa za Mkoa na hospitali ya Micheweni kuwa ya Wilaya kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya Unguja na Pemba. Kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 5.0 bilioni kutoka Serikalini zimepangwa kutumika kwa ajili ya kutekeza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya ununuzi wa vifaa tiba na samani kwa hospitali za Wilaya;
ii. Kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za mama na mtoto katika hospitali ya Chake Chake;
iii. Ujenzi wa nyumba za wafanyakazi katika hospitali ya Mkoa ya Abdalla Mzee na hospitali ya Wilaya ya Kivunge;
iv. Kuanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya - Mbuzini;v. Ununuzi wa CT - scan kwa hospitali ya Abdalla Mzee;
vi. Ujenzi wa maabara katika hospitali ya Wilaya - Makunduchi.
50Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mradi wa Ujenzi wa Bohari Kuu ya Dawa- PembaMradi huu umeanza mwaka 2018/19, ukiwa na lengo la kuondoa tatizo la uhaba wa dawa unaosababishwa na kuchelewa kupelekwa dawa na hali ya usafirishaji wa dawa Pemba. Mradi huu unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21 jumla ya TZS 2.0 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa bohari kuu ya dawa - Vitongoji;
ii. Kufanya ununuzi wa vifaa mbali mbali vya bohari kuu ya Vitongoji;iii. Kufanya utanuzi wa ghala ya kuhifadhia dawa na vifaa vya utibabu-
Maruhubi.
Mradi wa Ujenzi wa Maabara ya Kisasa ya Mamlaka ya Dawa na Vipodozi Zanzibar Mradi huu umeanzishwa ukiwa na lengo la kuimarisha uchunguzi, ubora na usalama wa bidhaa za dawa na vipodozi ili kuepuka kusambaa kwa dawa zisizo na ubora na bandia katika soko la Zanzibar. Mradi huu unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 2.1 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchunguzi wa dawa, chakula
na vipodozi Mombasa.
Programu ya Kudhibiti Maradhi ya UKIMWI, Homa ya Ini, Kifua Kikuu na UkomaProgramu hii inajumuisha miradi ya kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na ukoma. Lengo kuu ni kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kupunguza vifo vinavyotokana na maradhi ya kifua kikuu na kupunguza maambukizi ya ukoma. Programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo ambapo jumla ya TZS 5.3 bilioni (TZS 248.0 milioni za Serikali na TZS 5.09 bilioni za
51Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka 2020/21 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kusimamia utoaji wa huduma bora za UKIMWI, Homa ya Ini, Kifua
Kikuu na Ukoma;ii. Kufanya ukaguzi wa vituo vinavyotoa huduma za UKIMWI;
iii. Kuimarisha huduma za uchunguzi na tiba za Homa ya Ini.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuimarisha huduma za tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya (methadone);
ii. Kuimarisha utoaji wa huduma za maradhi ya Kifua Kikuu na Ukoma;iii. Kuimarisha huduma za UKIMWI kwa makundi maalum na makundi
hatarishi.
Programu Shirikishi ya Huduma za Afya ya Uzazi wa Mama na MtotoProgramu hii ina lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano. Programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo ambapo jumla ya TZS 10.07 bilioni (TZS 500.0 milioni za Serikali na TZS 9.57 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka 2020/21 kwa ajili ya kutekeza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuimarisha huduma za mama na watoto wachanga;
ii. Kuimarisha huduma za damu salama;iii. Kuimarisha huduma za chanjo.
52Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleoi. Kuimarisha mfumo wa taarifa za mama wajawazito, vijana na watoto;
ii. Kuimarisha huduma za chanjo kwa ununuzi wa chanjo pamoja na usambazaji;
iii. Kufanya ununuzi wa vifaa vya uchunguzi wa afya ya uzazi ikiwemo “mobile ultrasound”.
13.8 Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati
Wizara hii inajumuisha sekta ya ardhi, nyumba, maji na nishati ambazo ni sekta muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika taifa lolote. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Wizara hii imepanga kutekeleza jumla ya miradi mitano ya maendeleo itakayogharimu kiasi cha TZS 93.44 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 4.96 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 88.48 bilioni. Shughuli za miradi hiyo ya maendeleo zitakazotekelezwa kwa fedha za Serikali na za Washirika wa Maendeleo ni kama ifuatavyo:
Mradi wa Kuendeleza Visima vya Ras el KhaimahMradi huu umegharamiwa kwa msaada kutoka Ras el Khaimah na mchango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama Zanzibar hususan kwa maeneo ya vijijini. Kupitia mradi huu jumla ya visima 150 vimechimbwa katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba katika awamu tatu tofauti. Kwa sasa mradi huu unatekelezwa na Serikali pekee ambapo kazi zinazoendelea ni uwekaji wa miundombinu ya maji ili kuhakikisha wananchi wa maeneo yaliyochimbwa visima hivo wanapata maji safi na salama. Mwaka 2020/21 ni mwaka wa ukamilishaji wa kazi hizo ambapo mradi utaendelea na shughuli za kukamilisha visima kumi na tatu (13) vilivyobakia vinavyotarajiwa kugharimu jumla ya TZS 4.0 bilioni katika utekelezaji wa shughuli mbali mbali zikiwemo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya kazi za uvutaji na uwekaji wa pampu, ununuzi vifaa na ulazaji
53Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
wa mabomba kwa visima 13 vilivyochimbwa katika maeneo ya Muembe Mchomeke, Chuini, Kibonde Mzungu, Mzungu Punda, Selemu 1 na 2, Dimani, Bungi na Mbuzini kwa Unguja na Sharifu Ali 1 na 2 na Mahuduthi kwa Pemba
ii. Ujenzi wa vibanda vya kuendeshea pampu.
Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar (INDIA)Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa tatizo la maji katika maeneo ya Mjini linaondoka kabisa na wananchi wanaweza kupata maji safi na salama muda wote. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya India ambapo jumla ya TZS 67.59 bilioni (TZS 466.2 milioni kutoka Serikalini na TZS 67.13 bilioni kutoka India). Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa mwaka 2020/21 ni kama ifuatavyo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Ulipaji wa fidia katika maeneo yatakayoathirika na mradi;
ii. Kuratibu vikao vya Kamati Kiongozi na Kamati ya Wataalamu.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuanza kazi za uchimbaji wa visima;ii. Kuanza kazi ya ujenzi wa matangi;
iii. Kuanza kazi ya ujenzi wa vibanda vya kuendeshea pampu;iv. Kuanza ujenzi wa Ofisi ya ZAWA – Madema;v. Malipo ya Mshauri Elekezi.
Mradi wa Kujenga Uwezo na Matengenezo ya Miundombinu ya Umeme ZanzibarMradi huu una lengo la kujenga uwezo katika masuala ya kiufundi na kufanya matengenezo katika miundombinu ya umeme ili kuhakikisha upatikanaji na
54Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
usambazaji wa umeme endelevu. Mradi huu unatekelezwa kwa msaada wa Serikali ya Norway na kwa mwaka 2020/21 umepangiwa jumla ya TZS 3.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Upelekaji umeme katika kisiwa cha Kokota na Njau;
ii. Kuimarisha laini ya 11kv Unguja yenye kilomita 61;iii. Upelekaji wa umeme vijijini – Pemba.
Mradi wa Usambazaji Umeme VijijniMradi wa usambazaji umeme vijijini una lengo la kuvipatia huduma ya umeme vijiji mbalimbali vya Unguja na Pemba. Mradi huu unaendeleza juhudi za Serikali za kuvipatia huduma ya umeme vijiji na visiwa vidogo vidogo vyote viliopo Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, Serikali imepanga kutumia jumla ya TZS 500 milioni katika utekelezaji wa shughuli za mradi huu kama ifuatavyo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kusambaza umeme kutoka line kubwa kwenda kwenye transfoma ili
kuweza kupeleka kwa wananchi; ii. Uwekaji wa trasfoma kwa ajili ya upelekaji umeme katika visiwa vya
Kokoto na Njau.
Mradi wa Kuifanyia Mabadiliko Sekta ya Nishati (ZEST)Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha utekelezaji katika sekta ya nishati kwa kuzijengea uwezo taasisi zinazoshughulikia masuala ya nishati ikiwemo Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) ili kuweza kuendesha shughuli zake kwa ufanisi zaidi. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mshirika wa Maendeleo ambae ni Benki ya Dunia. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 17.85 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
55Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwai. Kutafuta mshauri elekezi kwa ajili ya usimamizi wa mradi;
ii. Kutafuta mshauri elekezi kwa ajili ya kusaidia katika masuala ya kiufundi;
iii. Kusaidia utekelezaji wa shughuli za mradi;iv. Kufanya malipo ya fidia kwa maeneo yatakayo athirika na mradi.
13.9 Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji
Wizara hii ina jukumu la kusimamia sekta ya ujenzi, mawasiliano na usafirishaji. Sekta hizi ni miongoni mwa sekta muhimu zinazochochea maendeleo ya sekta nyengine na ukuaji wa uchumi wa taifa. Kwa mwaka 2020/21, Wizara imepanga kutumia jumla ya TZS 177.41 bilioni (TZS 35.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 141.91 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa utekelezaji wa program mbili na miradi miwili ya maendeleo.
Programu ya Ujenzi wa BarabaraProgramu hii inahusisha ujenzi wa barabara mbalimbali Unguja na Pemba kwa kiwango cha lami. Programu hii inatekelezwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo. Jumla ya TZS 38.82 billioni (TZS 21.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 17.3 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka wa fedha 2020/21 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kufanya upimaji wa eneo na usafishaji kwa barabara ya Chake Chake –
Wete (km 21); ii. Kukamilisha ujenzi wa barabara ya Jozani-Charawe-Ukongoroni (km
23);
iii. Kuanza ujenzi wa daraja katika eneo la Unguja Ukuu-Uzi Ngambwa
iv. Kukamilisha ujenzi wa barabara ya Bububu-Mahonda Mkokotoni katika eneo la Kwanyanya hadi kufikia eneo la Bububu kituo cha Polisi;
56Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
v. Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kizimbani - Kiboje (7.2 km);
vi. Kuanza shughuli za ulipaji wa fidia wa nyumba na vipando vitakavyoathirika kwa ujenzi wa barabara ya Fumba –Kisauni (km 12) na Chake Chake – Wete (km 21);
vii. Kufanya upembuzi yakinifu kwa barabara za Kitogani-Paje, Mahonda-Donge-Mkokotoni, Dunga-Chwaka-Kiwengwa, Kizimkazi-Makunduchi na Muyuni-Nungwi;
viii. Kendelea kufanya tathmini na ulipaji fidia kwa barabara za Kizimbani - Kiboje (km 7.2);
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kuanza shughuli za ujenzi wa makalvati, uwekaji kifusi, uwekaji wa lami pamoja na uwekaji wa alama za barabarani kwa barabara ya Chake Chake – Wete (km 21);
ii. Kukamilisha kazi za uwekaji wa kifusi tabaka la tatu, uwekaji wa lami, alama za barabarani pamoja na ujenzi wa kituo katika barabara ya Bububu- Mahonda - Mkokotoni.
Programu ya Kuimarisha Viwanja vya Ndege Program hii ina lengo la kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa abiria na mizigo pamoja na huduma zinazotolewa katika viwanja vya ndege Unguja na Pemba ambapo inatekelezwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo. Kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 131.1 billioni (TZS 6.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 124.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Kuendelea na malipo ya msimamizi wa ujenzi wa jengo jipya la abiria
Terminal III;ii. Ujenzi wa ukuta katika Terminal III;
57Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
iii. Ulipaji wa fidia kwa maeneo yatakayoathirika na ujenzi wa uwanja wa ndege Pemba.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
i. Kukamilisha ujenzi wa jengo jipya la abiria (Terminal III) kwa uwekaji wa miundombinu ya maji, umeme, vipozahewa, ngazi, lift, pamoja na uwekaji wa madaraja ya kupanda na kushukia ndege.
Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya MpigaduriMradi huu una lengo la kujenga bandari kubwa kwa ajili ya kuhudumia meli kubwa za mizigo ili kupunguza msongamano uliopo katika bandari ya sasa inayotoa huduma kwa abiria pamoja na mizigo ambayo hupelekea usumbufu na uchelewaji wa huduma za upakiaji na upakuaji wa mizigo. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 5.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:- Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa
i. Kukamilisha upembuzi yakinifu wa ujenzi wa bandari ya Mpigaduri;ii. Kpeleka miundombinu ya maji na umeme pamoja na kuanza kazi za
ujenzi wa bandari.
Mradi wa Ununuzi wa Boti (Land Craft)Mradi huu una lengo la kurahisisha usafiri wa abiria na mizigo katika visiwa vidogo vidogo vya maeneo mbalimbali ya Zanzibar. Lengo hili linakwenda sambamba na malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar awamu ya III (MKUZA III) ambayo yamedhamiria kuimarisha usafirishaji baina ya visiwa vidogo vidogo. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TSZ 2.5 bilioni, kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
58Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha malipo ya ununuzi wa boti tano za kuvushia wananchi katika
visiwa vidogo vidogo Zanzibar (Fundo-Uvinje, Makoongwe, Kisiwa Panza, Kojani na Tumbatu).
13.10 Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto
Wizara hii imeundwa na Taasisi na Idara ambazo zinasaidia katika kutekeleza majukumu ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia Mfuko wa Uwezeshaji, kusimamia utekelezaji wa Sheria na Kanuni za Kazi pamoja na kusimamia haki za watoto, wazee na wanawake. Kwa mwaka 2020/21, jumla ya TZS 3.26 bilioni zimepangwa kutekeleza programu moja na miradi minne ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 2.1 bilioni na TZS 1.16 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.
Programu ya Kuimarisha JinsiaProgramu hii imeanzishwa kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake wa Zanzibar kiuchumi. Programu hii inatekelezwa kupitia miradi miwili ifuatayo:-
Usawa wa Kijinsia na Kuwawezesha WanawakeMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kukuza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake kiuchumi. Mradi unatekelezwa na Washirika wa Maendeleo (Shirika la Umoja wa Mataifa (UN-WOMEN)), ambapo kwa mwaka 2020/21 jumla ya TZS 180.0 milioni zimepangwa kutumika kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:- Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya vikao vya kamati juu ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa
Kupinga Vitendo vya Udhalilishaji;ii. Kuwajengea uwezo wanawake wanaojikita katika uzalishaji wa umeme
wa jua;iii. Kuandaa taarifa za utekelezaji wa mikataba ya kimataifa ya kupinga
vitendo vya udhalilishaji dhidi ya wanawake.
59Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mradi wa JinsiaMradi wa Jinsia umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa kitaifa katika kukuza uzingatiaji wa masuala ya kijinsia katika sera na mipango sambamba na kupambana na udhalilishaji wa kijinsia. Mradi unatekelezwa na Shirika la Kimataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA). Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 470.6 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kutoa misaada ya kijamii kwa wahanga wa matukio ya udhalilishaji;ii. Kutoa elimu kwa jamii katika kupinga ukatili na udhalilishaji;iii. Kufanya kampeni dhidi ya haki za wanawake na kupinga udhalilishaji.
Mradi wa Hifadhi ya WazeeMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha hali za wazee wanaoishi katika makaazi ya wazee yaliopo Unguja na Pemba yanaimarika pamoja na kuwapatia huduma zao za msingi kikamilifu. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwa mwaka 2020/21 umepangiwa jumla ya TZS 1.1 bilioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa
i. Ujenzi wa ukuta katika nyumba za wazee Welezo.
Mradi wa Uhifadhi wa Haki za WatotoMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha katika ngazi ya kitaifa kunajengeka uwezo wa kutoa huduma za hifadhi ya mtoto kwa ufanisi mzuri sambamba na kuondoa masuala ya udhalilishaji wa watoto visiwani. Mradi unatekelezwa na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF), ambapo kwa mwaka 2020/21 umepangiwa jumla ya TZS 387.5 milioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
60Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kufanya utafiti juu ya udhalilishaji wa watoto;ii. Kukamilisha muongozo juu ya mafunzo ya uhifadhi wa watoto;iii. Kuandaa muongozo juu ya familia bora na Taifa imara;iv. Kuimarisha mfumo wa hifadhi ya watoto;v. Kusaidia uendeshaji wa kituo cha kurekebisha watoto - Madema.
Mradi wa Hifadhi ya JamiiMradi wa Hifadhi ya Jamii umeanzishwa ukiwa na lengo la kuhakikisha utekelezaji wa Sera ya Hifadhi ya Jamii unafanikiwa ipasavyo. Mradi umeanzishwa mwaka 2014 ambapo ulikuwa unatekelezwa kwa fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, kwa sasa mradi huu unadhaminiwa na Mshirika wa Maendeleo ambae ni Shirika la Kuwahudumia Watoto Duniani (UNICEF), na kwa mwaka 2020/21 umepangiwa jumla ya TZS 121.0 milioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuimarisha kitengo cha hifadhi ya jamii kwa kuwajengea uwezo juu ya
uendeshaji, ufuatiliaji na usimamizi wa mfumo wa taarifa (database);ii. Kufanya ufuatiliaji na tathmini juu ya programu ya hifadhi ya jamii.
Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kulea na Kutotolea Wajasiriamali (Incubator)Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuwajengea uwezo wajasiriamali ili wanapomaliza mafunzo yao waweze kujiajiri wenyewe na kuweza kupunguza umasikini Zanzibar. Aidha, mradi huu unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali, ambapo kwa mwaka 2020/21 jumla ya TZS 1.0 bilioni zimepangwa kutumika kwa shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa kituo cha kulea na kutotolea wajasiriamali Mbuzini, Pemba.
61Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.11 Wizara ya Katiba na Sheria
Wizara hii ina jukumu la kuhakikisha jamii inapata huduma bora za kisheria zenye ufanisi kwa kuzingatia misingi ya katiba na sheria pamoja na haki za binadamu ili kuwa na mfumo madhubuti wa sheria nchini. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Wizara hii imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo wenye jumla ya TZS 1.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Usimamizi wa Upatikanaji wa Haki Mradi huu una lengo la kuimarisha upatikanaji wa haki na kukuza uwezo wa sheria Zanzibar. Mradi utatekelezwa kwa fedha za Serikali, ambapo kwa mwaka wa fedha 2020/21 umepangiwa jumla ya TZS 1.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa fedha za Serikali i. Kuanza ujenzi wa skuli ya Sheria –Tunguu.
13.11.1 Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka
Ofisi hii ina jukumu la kusimamia na kuendesha kesi za jinai kwa Mahkama za Zanzibar ili kuhakikisha uwepo wa haki kwa wananchi. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Ofisi imepanga kutekeleza mradi mmoja utakaogharimu kiasi cha TZS 600.0 milioni.
Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Mafunzo ya Sheria na Utafiti
Mradi huu umeanzishwa mwaka 2020 ukiwa na lengo la kuelimisha jamii juu ya masuala ya sheria za jinai ili kuweza kuzifahamu, kuzitumia na kupunguza uhalifu nchini. Kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 600.0 kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa i. Kuanza ujenzi wa kituo cha mafunzo ya sheria na utafiti - Tunguu.
62Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.12 Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Ofisi hii ina jukumu la kusimamia masuala yote yanayohusiana na utawala bora ikiwemo kuhakikisha kuwepo kwa uadilifu, uwazi pamoja na uwajibikaji katika utendaji wa shughuli za kiutumishi, pamoja na kuratibu na kuimarisha utendaji wa watumishi wa umma. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Ofisi imepanga kutekeleza programu moja ya maendeleo yenye jumla ya TZS 400.0 milioni.
Programu ya Mageuzi ya Utumishi wa Umma Zanzibar Awamu ya II (ZPSRP II)
Programu hii ina lengo la kuimarisha utendaji, uwajibikaji wa mtumishi wa umma ikiwemo miundo, mifumo na utoaji huduma bora kwa umma. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, programu imepangiwa jumla ya TZS 400.0 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kumalizia uandaaji wa Sera ya Mafunzo kwa watumishi wa Umma; ii. Kuandaa Mpango wa Utekelezaji wa Sera ya Mafunzo kwa Watumishi
wa Umma; iii. Kuandaa Sera ya Usimamizi wa Mfumo wa Rasilimali Watu; iv. Kuandaa mpango wa watumishi na kuwapima uwezo wa mahitaji yao; v. Kufanya upembuzi yakinifu na tathmini ya usimamizi wa mifumo ya
pamoja Serikalini; vi. Kuimarisha Mfumo wa kielektroniki wa usajili wa Taarifa za Mali na
Madeni ya Viongozi wa Umma.
13.12.1 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi
Ofisi hii ina wajibu wa kupambana na kuzuia vitendo vyote vya rushwa na uhujumu uchumi, ili kupata mafanikio endelevu ya kiuchumi na kijamii Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Ofisi imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo kwa gharama ya TZS 1.0 bilioni.
63Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa Na Uhujumu Uchumi
Mradi huu una lengo la kuimarisha Ofisi za Serikali kuwa na majengo mazuri yenye mazingira bora kwa wafanyakazi. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo-:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuanza ujenzi wa Ofisi ya Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu
Uchumi - Tunguu.
13.13 Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale
Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale ina jukumu la kusimamia mambo makuu matatu ambayo ni habari, utalii na mambo ya kale. Kwa mwaka 2020/21, Wizara inatarajia kutekeleza programu moja na mradi mmoja wa maendeleo itakayosaidia kutoa huduma bora katika sekta ya habari na kuongeza vivutio vya utalii katika sekta ya utalii na mambo ya kale. Wizara imepanga kutekeleza programu na mradi huo wa maendeleo kwa gharama ya TZS 4.1 bilioni kutoka Serikalini.
Programu Mjumuisho ya Kuendeleza UtaliiUtalii ni sekta muhimu ambayo inakua kwa kasi na kuweza kutoa fursa za ajira pamoja na kuongeza pato la taifa na kuitangaza nchi yetu katika mataifa tofauti nchi za nje. Kwa mwaka 2020/21, programu hii inatarajia kutumia kiasi cha TZS 2.7 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuimarisha na kuendeleza maeneo ya kihistoria ikiwemo Amani,
Mnazimmoja, Mwinyi Mkuu, Fukuchani na Kwa Bikhole kwa Unguja na Chwaka-Tumbe, Mvuleni, Makangale na Mkamandume kwa Pemba;
ii. Kufanya ukarabati wa jengo la Beit al Ajab.
64Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Ujenzi wa Jengo la Ofisi na Studio za Redio Mkanjuni - PembaLengo la mradi huu ni kuimarisha upatikanaji na usambazaji wa habari kwa kufanya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Ofisi na studio ya Mkanjuni Pemba ili kuimarisha mazingira ya kufanyia kazi. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.4 bilioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi na studio za redio Mkanjuni, Pemba;
ii. Ununuzi wa samani.
3.13.1 Kamisheni ya Utalii
Jukumu la msingi la Kamisheni ya Utalii ni kusimamia na kuratibu shughuli za utalii pamoja na kuwahamasisha wananchi juu ya dhana ya utalii kwa wote. Kwa mwaka 2020/21, Kamisheni ya Utalii inakusudia kutekeleza mradi wa kuimarisha utalii kwa wote utakaogharimu kiasi cha TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Kuimarisha Utalii kwa WoteLengo la mradi huu ni kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na matunda ya utalii na anashiriki katika kutunza na kuendeleza utalii huo sambamba na kuimarisha huduma na vivutio kwa watalii. Kwa mwaka 2020/21, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 2.0 bilioni, kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendeleza miundombinu ya utoaji wa huduma ikiwemo barabara, maji
na umeme katika eneo la kwa Bikhole - Bungi;ii. Kujenga maegesho ya boti (marina) kwa Bikhole - Bungi.
65Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.14 Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo ina jukumu la kuimarisha maendeleo ya vijana na ustawi wa jamii kwa kusimamia uendeshaji na uimarishaji wa sekta ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuendeleza na kuimarisha maisha ya vijana na jamii kwa kuzitumia sekta hizo kwa kujipatia ajira na kuweza kujikimu kimaisha. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Wizara hii inatarajia kutekeleza programu moja na mradi mmoja ambapo jumla ya TZS 4.5 bilioni zinatarajiwa kutumika kutoka Serikalini.
Programu ya Ajira kwa VijanaProgramu ya Ajira kwa Vijana imeaza mwaka 2018 kwa lengo la kuimarisha maisha ya vijana kwa kuwasaidia kuwa wabunifu na kuwawezesha kujiajiri ili waweze kujipatia kipato chenye tija kitakachowawezesha kujikimu na kuendesha maisha yao ya kila siku. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Programu ya ajira kwa vijana inatarajia kutumia jumla ya TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuviwezesha vikundi vya kilimo awamu ya pili kwa kuvipatia pembejeo za
kilimo, uwekaji wa mifumo ya maji, ujenzi wa “greenhouse”, kuimarisha maeneo yao ya ufugaji, ujenzi wa mabwawa ya kufugia samaki pamoja na kuwapatia vifaa na pembejeo za kilimo;
ii. Kuwapatia mafunzo kazi vijana na mabaraza ya vijana, wasanii katika fani za ushonaji, useremala, uwashi na uchomaji pamoja na kuwapatia vifaa (vitendea kazi) vikundi vya vijana vitakavyoundwa baada ya kumaliza masomo yao ya ufundi;
iii. Ujenzi wa nyumba ya sanaa Mwanakwerekwe;
iv. Kuendeleza Kituo cha Michezo (OTC) Dole kwa kuimarisha miundombinu ya barabara, ujenzi wa madarasa na vyoo;
v. Kusaidia wahitimu wa vyuo (graduate) katika kuwapatia mafunzo kazi na vitendea kazi.
66Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mradi wa Uimarishaji wa Viwanja vya MichezoMradi wa Uimarishaji wa Viwanja vya Michezo umeanza mwaka 2017 kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya michezo Zanzibar na kuifanya sekta ya michezo kuweza kuimarika na kutoa ajira kwa jamii. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, mradi unatarajiwa kutumia jumla ya TZS 2.5 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuimarisha kiwanja cha Gombani Pemba kwa kufanya matengenezo ya
mfumo wa taa na kuweka ubao wa matangazo (Scoreboard).
13.15 Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ
Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ina jukumu la kuratibu shughuli za mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ikiwemo Ugatuzi, Idara Maalum za SMZ na Usajili wa Vitambulisho kwa kutoa huduma bora kwa jamii, kudumisha amani na usalama, kusimamia shughuli za maendeleo kwa maeneo yao kwa kuzingatia misingi ya utawala bora. Kwa mwaka wa fedha 2020/21, Wizara hii imepanga kutekeleza programu moja na miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 14.39 bilioni (TZS 11.5 bilioni kutoka Serikalini na TZS 2.89 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo).
Programu ya Ugatuzi wa Masuala ya ElimuProgramu hii inatekeleza dhana ya ugatuzi katika masuala ya elimu ikiwa ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya kupeleka madaraka katika Serikali za Mitaa pamoja na ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi. Kwa mwaka 2020/21, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 3.89 bilioni (TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini na TZS 2.89 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikalii. Ujenzi wa skuli ya maandalizi ya Ng’ombeni Mkoani Pemba;
67Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
ii. Ujenzi wa madarasa 44 yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwemo skuli za Potoa, Kitope, Binguni, Welezo, Kombeni, Micheweni, Tumbe, Chanjaani, Uwandani, Chwaka, Ngwachani na Mtemani.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleoi. Kutoa ruzuku kwa skuli 825 za maandalizi (TuTu, Maandalizi na Jamii);
ii. Kuanzisha vituo 30 vya TUTU;
iii. Kujenga madarasa 10 mapya ya maandalizi kwa kutumia mafundi wadogo wadogo;
iv. Kufanya ukarabati katika skuli 5 na madarasa 170 ya maandalizi na ya vituo vya TuTu;
v. Kukamilisha madarasa 30 yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi;vi. Kuwaajiri na kulipa mishahara/posho walimu 800 wa vituo vya TUTU;
vii. Uhamasishaji wa jamii katika maendeleo ya elimu;
viii. Kuendelea kuwapatia chakula wanafunzi katika skuli 27 za msingi.
Mradi wa Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya UlinziMradi wa Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi awamu ya pili una lengo la kuimarisha ulinzi kwa kufikia viwango vya kimataifa ili kuweka mazingira salama kwa wananchi na wageni wakiwemo watalii katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa kiasi cha TZS 8.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na kazi za uwekaji wa vifaa vya ulinzi na usalama katika
maeneo mbali mbali ikiwemo miji ya Pemba.
Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Ushoni (ZQTL)Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa mavazi ya
68Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
askari kwa kushona sare za maaskari pamoja na nguo za kibiashara. Ili kuwa na ufanisi mzuri kiwanda kinahitaji kupatiwa vifaa bora ambavyo vitaendana na mfumo wa viwanda vya aina hii. Mradi unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa jumla ya TZS 2.5 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa kiwanda cha ushoni - Mtoni;
ii. Kufanya ziara ya kimafunzo juu ya uendelezaji na uendeshaji wa viwanda.
13.15.1 Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar
Ofisi ya Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar ina jukumu la kuimarisha mifumo ya usajili wa taarifa za vizazi, vifo, ndoa, talaka na vitambulisho hapa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, Ofisi imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu kiasi cha TZS 1.0 bilioni zinazotarajiwa kutolewa na Serikali.
Mradi wa Kuimarisha Mfumo wa UsajiliMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha taarifa na usalama wa mfumo wa usajili wa taarifa za matukio ya kijamii. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2020/21 umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa
i. Ujenzi wa vituo vya usajili vya Wilaya ya Chake Chake, Wete na Mkoani;ii. Ujenzi wa Ofisi Kuu Wete-Pemba;
iii. Ununuzi wa kamera;iv. Ujenzi wa uzio kwa vituo 11 vya usajili Unguja na Pemba.
69Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
13.15.2 Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM)
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia masuala yote ya ulinzi wa baharini na nchi kavu ili kudhibiti biashara haramu za magendo kwa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 5.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Kuimarisha Huduma za Uzamiaji na UokoziMradi huu umeanzishwa kwa lengo la kukabiliana na maafa ya baharini katika ukanda wa bahari ya hindi Unguja na Pemba yanayosababishwa na majanga ya kuzama kwa meli za abiria na mizigo na vyombo vyengine vya usafiri wa baharini. Mradi unatekelezwa kupitia fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, umepangiwa jumla ya TZS 4.8 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuanza ujenzi wa Chelezo cha kupandishia vyombo vya bahari kwa ajili
ya matengenezo.
Mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Kambi na Nyumba za KMKMMradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Kambi na Nyumba za KMKM ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, mradi umetengewa kiasi cha TZS 700.0 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa mahanga Micheweni na Wete;
ii. Kufanya utafiti wa hali ya kimazingira pamoja na michoro kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Uongozi -Kama.
13.15.3 Kikosi cha Valantia
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya
70Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Zanzibar kinachoshughulika kutoa huduma ya ulinzi na huduma nyenginezo wakati wa majanga. Kwa mwaka 2020/21, Kikosi kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 1.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya MaaskariMradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya Maaskari wa Kikosi cha Valantia, ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha kuwa Idara Maalum za SMZ zinapata majengo mazuri ili kuimarisha utendaji wa kazi kwa wafanyakazi wake. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee. Kwa mwaka 2020/21, mradi umetengewa kiasi cha TZS 1.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Ujenzi wa mahanga, nyumba za maofisa katika kambi za Kikungwi kwa
Unguja, Pujini na Micheweni kwa Pemba.
13.15.4 Chuo cha Mafunzo
Chuo cha Mafunzo kimeanzishwa kwa lengo la kuwapokea, kuwahifadhi, kuwalinda na kuwarekebisha wananchi wanaofanya makosa mbali mbali na kupatiwa vifungo hapa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, chuo kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 1.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makaazi na MahangaMradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makaazi na Mahanga kwa Chuo cha Mafunzo ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee, na umepanga kujenga majengo mapya na kukarabati majengo chakavu. Kwa mwaka 2020/21, mradi umetengewa kiasi cha TZS 1.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
71Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa kambi ya Kangagani - Pemba;
ii. Kuanza ujenzi wa mahanga katika kambi ya Wete;iii. Kufanya upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa gereza la kisasa- Hanyegwa
Mchana.
13.15.5 Jeshi la Kujenga Uchumi
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia masuala ya ulinzi na ujenzi wa uchumi kwa Zanzibar. Kwa mwaka 2020/21, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 4.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari na Ufundi ya JKU – MtoniMradi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari na Ufundi katika Kambi ya JKU Mtoni una lengo la kuwapatia vijana elimu katika fani mbali mbali. Mradi huu, unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, mradi umepangiwa jumla ya TZS 2.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kuendelea na ujenzi wa chuo cha ufundi JKU Mtoni.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya Kambi za JKU Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya Kambi za JKU umeanzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa kuanzia umepanga kutekeleza shughuli zake katika kambi za Pemba. Kwa mwaka 2020/21, mradi umetengewa kiasi cha TZS 2.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa majengo matatu, mahanga mawili na bwalo katika
72Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
kambi ya Msaani Pemba;ii. Kuanza ujenzi wa mahanga katika kambi za Pujini, Kwapweza na Wawi;
iii. Ujenzi wa Ofisi –Mtoni.
13.15.6 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ni miongoni mwa Idara maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia shughuli zote za uzimaji moto na uokozi wa mali za raia. Kwa mwaka 2020/21, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu kiasi cha TZS 2.5 bilioni.
Mradi wa Ujenzi wa Mahanga na Nyumba za MaaskariMradi wa Ujenzi wa Mahanga na Nyumba za Maaskari katika Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2020/21, umetengewa kiasi cha TZS 2.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa i. Kukamilisha ujenzi wa kituo cha Zimamoto Kijichame na kuanza ujenzi
wa kituo Wete;ii. Ununuzi wa magari mawili ya kuzimia moto;
iii. Kufanya upembuzi yakinifu juu ya uanzishwaji wa chuo cha mafunzo ya zimamoto.
14.0 PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO CHINI YA MFUKO WA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE FUND)
Katika mwaka 2015, Serikali ilianzisha Mfuko wa Miundombinu ikiwa ni mfuko maalum chini ya kifungu nambari 11 cha Sheria ya Fedha za Umma ya mwaka 2005 kwa ajili ya kusaidia uimarishaji wa miundombinu. Mfuko wa
73Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
miundombinu unalenga kukusanya rasimali kutoka katika kodi za miundombinu na katika vyanzo vyengine kwa lengo la kusaidia maendeleo ya Zanzibar. Aidha, rasilimali za mfuko huu zinatolewa kwa lengo kuu la kuwekeza katika miundombinu ya umma ili kusaidia kunyanyua uchumi na maendeleo ya jamii.
Mfuko huu ulianza kazi zake rasmi tarehe 1 Julai 2015, na tokea kuanzishwa kwake utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo unaendelea kupata fungu kutoka mfuko huo ambapo kwa mwaka 2020/21 jumla ya TZS 44.2 bilioni zimepangwa kutumika katika kugharamia utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo. Hii ni ongezeko la TZS 3.2 bilioni ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2019/20 ambapo jumla ya TZS 41.0 bilioni zilitengwa kugharamia miradi 17 ya maendeleo.
Kwa mwaka 2020/21, jumla ya miradi 15 ya maendeleo, imepangwa kutekelezwa kupitia Mfuko wa Miundombinu. Miradi yenyewe ni:-
i) Uimarishaji Uvuvi wa Bahari Kuu; ii) Ujenzi wa hospital ya rufaa ya Binguni; iii) Ujenzi wa daraja la Uzi Ng’ambwa; iv) Kuimarisha Taasisi ya Viwango Zanzibar; v) Kuendeleza Visima vya Ras el Khaimah;vi) Usambazaji Umeme Vijijini; vii) Ununuzi wa “Land Crafts”; viii) Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi; ix) Ujenzi wa Kiwanda cha Nguo (ZQTL) (Ununuzi wa vifaa na malighafi); x) Ujenzi wa Viwanja vya Michezo vya Wilaya; xi) Kuimarisha Huduma za Uzamiaji na Uokozi; xii) Ujenzi wa Skuli ya Ufundi - Mtonixiii) Kuimarisha Utalii kwa Wote; xiv) Ujenzi wa Mahanga na Nyumba za Maaskari (KZU) (Ununuzi wa Vifaa);
na xv) Ujenzi wa Ofisi za ZAECA.
74Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
Mchanganuo wa mgawanyo wa fedha zilizopangwa kwa utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo inayopatiwa fedha kupitia Mfuko wa Miundombinu kiwizara unaonekana katika kiambatisho nambari 3.
15.0 UFUATILIAJI NA TATHMINI
Kwa mwaka 2020/21, Serikali kupitia Tume ya Mipango Zanzibar imepanga kusimamia masuala ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Mpango wa Maendeleo kupitia maeneo yafuatayo:-
i. Kushirikiana na sekta katika kuandaa Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini (M & E System) kwa miradi ya maendeleo ikiwemo kutayarisha mpango unaozingatia matokeo, unaohusisha kuwepo malengo makuu (goals), matokeo ya muda wa kati (outcome), na muda mfupi (output), shabaha (targets) na viashiria vitakavyotumika kupima matokeo hayo;
ii. Kufanya ufuatiliaji na tathmini kwa programu na miradi mbali mbali ya maendeleo;
iii. Kuendeleza kazi na utaratibu wa kupima matokeo juu ya utekelezaji wa shughuli za programu na miradi ya maendeleo.
16.0 WASHIRIKA WA MAENDELEO
Washirika watakaochangia bajeti ya maendeleo kwa mwaka 2020/21 ni pamoja na ACRA, AfDB, BADEA, BASKET FUND, CHINA, DFID, EDF, EU, EXIM BANK, FAO, GEF, GLOBAL FUND, GPE, Hopeland University, INDIA, IFAD, IITA, IMF, JAPAN, JICA, KHALIFA FUND, KOICA, KOREA, MILELE FOUNDATION, NORAD, NORWAY, OPEC, PCD, PMI, SAUDI FUND, SIDA, THPS, UK, UNDP, UNFPA, UNESCO, UNICEF, URT, USDA-USAID, UN-WOMEN, WHO na WORLD BANK.
75Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
17.0 HITIMISHO
Kitabu hiki kinatoa mwelekeo wa Hali ya Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2020/21 ambao utekelezaji wake utaziwezesha Taasisi na Idara za Serikali kufikia malengo ya mipango na mikakati ya kitaifa na kimataifa. Maeneo ya utekelezaji ya kufikia matokeo kwa kipindi hiki yameainishwa na inatarajiwa kuwa wakuu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali watakitumia kitabu hiki kwa madhumuni ya kusimamia na kuratibu utekelezaji wa programu na miradi iliyoainishwa .
Ili kuweza kupima na kujua ufikiaji wa matokeo yaliyokusudiwa, Wizara, Idara na Taasisi za Serikali zinatakiwa kutoa taarifa za utekelezaji wa kazi zinazoainishwa katika kitabu hiki wiki ya pili ya kila robo mwaka (2020/21) na kuziwasilisha Tume ya Mipango bila ya kuchelewa. Aidha, taarifa za matumizi ya fedha ziwasilishwe kwa usahihi zikiwemo za Serikali na Washirika wa Maendeleo
Mashirikiano makubwa yanahitajika kwa Wizara na Taasisi za Serikali katika kufanikisha malengo yetu. Aidha sekta binafsi na asasi za kiraia zinahitaji kuwa na mikakati maalum ya kuungana na juhudi za Serikali kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kurasa zifuatazo zina viambatisho ambavyo vinaonesha mgawanyo wa fedha za Programu na Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2020/21. Mgawanyo wa fedha za SMZ na Washirika wa Maendeleo kwa Programu na Miradi ya Maendeleo Kiwizara unaonekana katika kiambatisho namba 1 na mgao wa fedha kwa Maeneo Makuu ya Matokeo unaonekana kwenye kiambatisho namba 2. Aidha, mgao wa fedha za SMZ kupitia Mfuko wa Miundombinu kwa miradi ya maendeleo iliyoteuliwa unaonekana katika kiambatisho namba 3.
76Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
PO
A01
Mira
dii)
Uim
aris
haji
Nyu
mba
za
Vio
ngoz
i na
Nyu
mba
za
Ser
ikal
i 2,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U2,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
C01
Mpa
ngo
wa
Kun
usur
u K
aya
Mas
ikin
i (TA
SAF
III)
40,0
00
50
,000
50,0
00
W
OR
LD
BA
NK
21,5
47,9
95
21
,597
,995
Mira
dii)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abilia
na n
a M
aafa
UN
DP
186,
000
18
6,00
0ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
350,
000
-
0iii)
Kui
mar
isha
Usi
mam
izi w
a M
azin
gira
, M
alia
sili
na
Mab
adilik
o ya
Tab
ianc
hi-Z
anzi
bar
300,
000
300,
000
300,
000
U
ND
P28
9,80
058
9,80
0iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adilik
o ya
Tab
ianc
hi (A
DB
-AC
CF)
50,0
00-
AfD
B67
5,91
267
5,91
2JU
MLA
YA
FU
NG
U74
0,00
0
350,
000
-
350,
000
1,
151,
712
21,5
47,9
95
23
,049
,707
C04
iii) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ti
ba n
a M
arek
ebis
ho y
a Ta
bia
680,
000
1,
900,
000
1,90
0,00
0
1,
900,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
680,
000
1,
900,
000
-
1,
900,
000
-
1,90
0,00
0
F01
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a O
fisi z
a Se
rikal
i Za
nzib
ar10
,002
,300
19,5
00,0
0019
,500
,000
19,5
00,0
00Pr
ogra
mu
ya U
kuza
ji U
chum
i Jum
uish
i Zan
ziba
r (B
IG -
Z)W
B19
,964
,000
19,9
64,0
00Pr
ogra
mu
ya U
patik
anaj
i Ras
ilim
ali F
edha
300,
000
-
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Miji
Mip
ya20
,000
,000
20,0
00,0
00
20
,000
,000
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
-
N
OR
WA
Y1,
639,
026
1,63
9,02
6M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u10
0,00
0-
AfD
Bii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilimal
i za
Nda
ni n
a U
sim
amiz
i wa
Mal
iasi
li50
,000
100,
000
100,
000
A
fDB
4,54
1,00
04,
641,
000
iii) M
radi
wa
Kuj
enga
Uw
ezo
Taas
isi z
a S
erik
ali
50,0
0020
,000
20,0
00
U
ND
P10
6,82
612
6,82
6iv
) Uim
aris
haji
wa
Mae
neo
Hur
u M
iche
wen
i Pem
ba1,
800,
000
1,80
0,00
0
1,
800,
000
v) M
tand
ao w
a U
ingi
zaji
wa
Taar
ifa z
a B
ajet
i50
0,00
050
0,00
0
500,
000
vi) M
radi
wa
Kue
ndel
eza
Ban
dari
ya M
anga
pwan
i4,
000,
000
-
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
14,5
02,3
002,
420,
000
39,5
00,0
0041
,920
,000
1,74
5,85
224
,505
,000
68,1
70,8
52F0
3TU
ME
YA
MIP
AN
GO
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
: M
GA
O W
A F
EDH
A P
RO
GR
AM
U/M
IRA
DI K
IWIZ
AR
A 2
020/
21 T
ZS "
000"
KIF
UN
GU
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
OFI
SI Y
A R
AIS
NA
MW
ENY
EKIT
I WA
BA
RA
ZA L
A M
API
ND
UZI
OFI
SI Y
A M
AK
AM
O W
A P
ILI W
A R
AIS
TUM
E Y
A K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Page
1 o
f 6
77Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Mpa
ngo
wa
Kur
asim
isha
Ras
ilim
ali
na B
iash
ara
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(MK
UR
AB
ITA
)50
0,00
055
0,00
055
0,00
0
UR
T10
0,00
0
650,
000
Mpa
ngo
wa
Kuh
uish
a U
chum
i (ER
P)7,
000,
000
7,00
0,00
0
7,
000,
000
Mira
di0
i) K
upun
guza
Um
asik
ini n
a U
fuat
iliaji
wa
SD
Gs
230,
000
150,
000
150,
000
15
0,00
0ii)
Ura
tibu
na U
sim
amiz
i wa
Mal
engo
na
Mae
ndel
eo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I20
,000
100,
000
100,
000
U
ND
P80
1,15
090
1,15
0iii)
Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya
Uza
zi, J
insi
a na
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i-
UN
FPA
286,
000
286,
000
iv) U
ende
leza
ji w
a Ta
kwim
u Za
nzib
ar (Z
SD
P)
UN
- W
OM
EN
/ A
DB
/EU
/ U
NIC
EF/
U
NFP
A3,
321,
700
3,32
1,70
0iv
) Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
500,
000
500,
000
50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U75
0,00
01,
300,
000
7,00
0,00
08,
300,
000
4,50
8,85
00
12,8
08,8
50L0
1Pr
ogra
mu
ya U
mw
agili
aji
1,00
0,00
019
,900
,000
19,9
00,0
00
K
OR
EA
47,1
93,4
6467
,093
,464
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a K
ilim
o na
Uha
kika
wa
Cha
kula
(ER
PP)
80,0
00-
WB
2,21
0,52
22,
210,
522
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Uvu
vii)
Uim
aris
haji
Uvu
vi w
a B
ahar
i Kuu
1,40
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
JI
CA
12,1
51,9
0714
,151
,907
ii) K
uim
aris
ha U
fuga
ji w
a M
azao
ya
Bah
arin
i20
0,00
0-
FAO
/ K
OR
EA
736,
479
736,
479
Mira
di
i) M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a S
hugh
uli z
a U
vuvi
wa
Kan
da
ya K
usin
i Mas
harik
i mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00-
WO
RLD
B
AN
K8,
651,
376
8,65
1,37
6
ii) M
radi
wa
Mae
ndel
eo y
a K
ilimo
na U
vuvi
IFA
D2,
141,
198
2,14
1,19
8iii.
Kue
ndel
eza
miu
ndom
binu
ya
Mifu
go n
a W
afug
aji
Wad
ogo
Wad
ogo
1,00
0,00
0-
0iv
. Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,20
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
v) M
radi
wa
Kud
hibi
ti N
zi w
a M
atun
da10
0,00
010
0,00
0
IITA
120,
000
220,
000
vi) K
udhi
biti
Sum
u K
uvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
guA
fDB
931,
698
931,
698
vii)
Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
iU
ND
P3,
801,
497
3,80
1,49
7vi
ii) K
ilimo
cha
Kus
hajih
isha
Uku
lima
wa
Mbo
ga M
boga
na
Mat
unda
ED
F-E
U5,
602,
995
5,60
2,99
5
JUM
LA Y
A F
UN
GU
4,93
0,00
010
0,00
022
,900
,000
23,0
00,0
00
24
,623
,400
58,9
17,7
3610
6,54
1,13
6R
01Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a20
0,00
030
0,00
0
300
,000
30
0,00
0
WIZ
AR
A Y
A K
ILIM
O,
MA
LIA
SILI
, MIF
UG
O N
A U
VUVI
WIZ
AR
A Y
A B
IASH
AR
A N
A V
IWA
ND
A
Page
2 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Mpa
ngo
wa
Kur
asim
isha
Ras
ilim
ali
na B
iash
ara
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(MK
UR
AB
ITA
)50
0,00
055
0,00
055
0,00
0
UR
T10
0,00
0
650,
000
Mpa
ngo
wa
Kuh
uish
a U
chum
i (ER
P)7,
000,
000
7,00
0,00
0
7,
000,
000
Mira
di0
i) K
upun
guza
Um
asik
ini n
a U
fuat
iliaji
wa
SD
Gs
230,
000
150,
000
150,
000
15
0,00
0ii)
Ura
tibu
na U
sim
amiz
i wa
Mal
engo
na
Mae
ndel
eo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I20
,000
100,
000
100,
000
U
ND
P80
1,15
090
1,15
0iii)
Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya
Uza
zi, J
insi
a na
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i-
UN
FPA
286,
000
286,
000
iv) U
ende
leza
ji w
a Ta
kwim
u Za
nzib
ar (Z
SD
P)
UN
- W
OM
EN
/ A
DB
/EU
/ U
NIC
EF/
U
NFP
A3,
321,
700
3,32
1,70
0iv
) Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
500,
000
500,
000
50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U75
0,00
01,
300,
000
7,00
0,00
08,
300,
000
4,50
8,85
00
12,8
08,8
50L0
1Pr
ogra
mu
ya U
mw
agili
aji
1,00
0,00
019
,900
,000
19,9
00,0
00
K
OR
EA
47,1
93,4
6467
,093
,464
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a K
ilim
o na
Uha
kika
wa
Cha
kula
(ER
PP)
80,0
00-
WB
2,21
0,52
22,
210,
522
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Uvu
vii)
Uim
aris
haji
Uvu
vi w
a B
ahar
i Kuu
1,40
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
JI
CA
12,1
51,9
0714
,151
,907
ii) K
uim
aris
ha U
fuga
ji w
a M
azao
ya
Bah
arin
i20
0,00
0-
FAO
/ K
OR
EA
736,
479
736,
479
Mira
di
i) M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a S
hugh
uli z
a U
vuvi
wa
Kan
da
ya K
usin
i Mas
harik
i mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00-
WO
RLD
B
AN
K8,
651,
376
8,65
1,37
6
ii) M
radi
wa
Mae
ndel
eo y
a K
ilimo
na U
vuvi
IFA
D2,
141,
198
2,14
1,19
8iii.
Kue
ndel
eza
miu
ndom
binu
ya
Mifu
go n
a W
afug
aji
Wad
ogo
Wad
ogo
1,00
0,00
0-
0iv
. Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,20
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
v) M
radi
wa
Kud
hibi
ti N
zi w
a M
atun
da10
0,00
010
0,00
0
IITA
120,
000
220,
000
vi) K
udhi
biti
Sum
u K
uvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
guA
fDB
931,
698
931,
698
vii)
Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
iU
ND
P3,
801,
497
3,80
1,49
7vi
ii) K
ilimo
cha
Kus
hajih
isha
Uku
lima
wa
Mbo
ga M
boga
na
Mat
unda
ED
F-E
U5,
602,
995
5,60
2,99
5
JUM
LA Y
A F
UN
GU
4,93
0,00
010
0,00
022
,900
,000
23,0
00,0
00
24
,623
,400
58,9
17,7
3610
6,54
1,13
6R
01Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a20
0,00
030
0,00
0
300
,000
30
0,00
0
WIZ
AR
A Y
A K
ILIM
O,
MA
LIA
SILI
, MIF
UG
O N
A U
VUVI
WIZ
AR
A Y
A B
IASH
AR
A N
A V
IWA
ND
A
Page
2 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
PO
A01
Mira
dii)
Uim
aris
haji
Nyu
mba
za
Vio
ngoz
i na
Nyu
mba
za
Ser
ikal
i 2,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U2,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
C01
Mpa
ngo
wa
Kun
usur
u K
aya
Mas
ikin
i (TA
SAF
III)
40,0
00
50
,000
50,0
00
W
OR
LD
BA
NK
21,5
47,9
95
21
,597
,995
Mira
dii)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abilia
na n
a M
aafa
UN
DP
186,
000
18
6,00
0ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
350,
000
-
0iii)
Kui
mar
isha
Usi
mam
izi w
a M
azin
gira
, M
alia
sili
na
Mab
adilik
o ya
Tab
ianc
hi-Z
anzi
bar
300,
000
300,
000
300,
000
U
ND
P28
9,80
058
9,80
0iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adilik
o ya
Tab
ianc
hi (A
DB
-AC
CF)
50,0
00-
AfD
B67
5,91
267
5,91
2JU
MLA
YA
FU
NG
U74
0,00
0
350,
000
-
350,
000
1,
151,
712
21,5
47,9
95
23
,049
,707
C04
iii) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ti
ba n
a M
arek
ebis
ho y
a Ta
bia
680,
000
1,
900,
000
1,90
0,00
0
1,
900,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
680,
000
1,
900,
000
-
1,
900,
000
-
1,90
0,00
0
F01
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a O
fisi z
a Se
rikal
i Za
nzib
ar10
,002
,300
19,5
00,0
0019
,500
,000
19,5
00,0
00Pr
ogra
mu
ya U
kuza
ji U
chum
i Jum
uish
i Zan
ziba
r (B
IG -
Z)W
B19
,964
,000
19,9
64,0
00Pr
ogra
mu
ya U
patik
anaj
i Ras
ilim
ali F
edha
300,
000
-
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Miji
Mip
ya20
,000
,000
20,0
00,0
00
20
,000
,000
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
-
N
OR
WA
Y1,
639,
026
1,63
9,02
6M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u10
0,00
0-
AfD
Bii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilimal
i za
Nda
ni n
a U
sim
amiz
i wa
Mal
iasi
li50
,000
100,
000
100,
000
A
fDB
4,54
1,00
04,
641,
000
iii) M
radi
wa
Kuj
enga
Uw
ezo
Taas
isi z
a S
erik
ali
50,0
0020
,000
20,0
00
U
ND
P10
6,82
612
6,82
6iv
) Uim
aris
haji
wa
Mae
neo
Hur
u M
iche
wen
i Pem
ba1,
800,
000
1,80
0,00
0
1,
800,
000
v) M
tand
ao w
a U
ingi
zaji
wa
Taar
ifa z
a B
ajet
i50
0,00
050
0,00
0
500,
000
vi) M
radi
wa
Kue
ndel
eza
Ban
dari
ya M
anga
pwan
i4,
000,
000
-
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
14,5
02,3
002,
420,
000
39,5
00,0
0041
,920
,000
1,74
5,85
224
,505
,000
68,1
70,8
52F0
3TU
ME
YA
MIP
AN
GO
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
: M
GA
O W
A F
EDH
A P
RO
GR
AM
U/M
IRA
DI K
IWIZ
AR
A 2
020/
21 T
ZS "
000"
KIF
UN
GU
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
OFI
SI Y
A R
AIS
NA
MW
ENY
EKIT
I WA
BA
RA
ZA L
A M
API
ND
UZI
OFI
SI Y
A M
AK
AM
O W
A P
ILI W
A R
AIS
TUM
E Y
A K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Page
1 o
f 6
78Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,00
0,00
0
-
0
i) U
imar
isha
ji w
a M
aene
o ya
Viw
anda
(Ind
urst
rial P
ark)
1,00
0,00
0
1
,000
,000
1,
000,
000
ii) K
uim
aris
ha v
iwan
da v
idog
o vi
dogo
na
vya
kati
(SM
IDA
)1,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0iii)
Mra
di w
a K
uwas
aidi
a W
ajas
iriam
ali W
adog
o W
adog
o,W
akat
i na
Wak
ubw
a4,
500,
000
4,5
00,0
00
KH
ALI
FA
FUN
D4,
600,
000
9,10
0,00
0M
iradi
i)Kui
mar
isha
Taa
sisi
ya
Viw
ango
Zan
ziba
r2,
000,
000
3,00
0,00
0
3
,000
,000
3,
000,
000
ii) M
fum
o m
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sek
ta B
inaf
si40
0,00
040
0,00
0
400
,000
40
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U4,
600,
000
7,20
0,00
03,
000,
000
10,2
00,0
004,
600,
000
014
,800
,000
K01
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
bnu
ya E
limu
1,50
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
aand
aliz
i
-
G
PE
/ M
ILE
LE3,
253,
333
3,25
3,33
3
ii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
-
PC
D/
UN
ICE
F/
MIL
ELE
/ WB
252,
230
150,
000
402,
230
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a3,
300,
000
3,50
0,00
0
3
,500
,000
BA
DE
A/
OP
EC
/ K
OIC
A/W
B2,
821,
521
8,48
5,00
014
,806
,521
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
Mba
dala
na
Am
ali -
Aw
amu
ya
Pili
1,00
0,00
0
-
A
fDB
0JU
MLA
YA
FU
NG
U5,
800,
000
1,00
0,00
03,
500,
000
4,50
0,00
06,
327,
084
8,63
5,00
019
,462
,084
H01
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
alar
ia Z
anzi
bar
248,
000
248,
000
248,
000
P
MI/G
F5,
586,
365
5,83
4,36
5Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a A
fya
i) K
uipa
ndis
ha h
adhi
Hos
pita
li ya
Mna
zi M
moj
a2,
650,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0ii)
Kuz
ipan
dish
a ha
dhi H
ospi
tali
za W
ilaya
na
hosp
itali
za V
ijiji
4,25
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
iii) A
wam
u ya
Kw
anza
ya
ujen
zi w
a H
ospi
tal y
a R
ufaa
B
ingu
ni6,
500,
000
6,00
0,00
06,
000,
000
6,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a B
ohar
i Kuu
ya
Daw
a-P
emba
1,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
v) U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mam
laka
ya
Daw
a na
Vip
odoz
i1,
000,
000
2,10
0,00
02,
100,
000
2,10
0,00
0
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
01,
400,
000
1,40
0,00
0
H
opel
and
Uni
vers
ity1,
400,
000
2,80
0,00
0vi
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a U
tafit
i wa
Afy
a2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
WIZ
AR
A Y
A E
LIM
U N
A M
AFU
NZO
YA
AM
ALI
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Page
3 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Mpa
ngo
wa
Kur
asim
isha
Ras
ilim
ali
na B
iash
ara
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(MK
UR
AB
ITA
)50
0,00
055
0,00
055
0,00
0
UR
T10
0,00
0
650,
000
Mpa
ngo
wa
Kuh
uish
a U
chum
i (ER
P)7,
000,
000
7,00
0,00
0
7,
000,
000
Mira
di0
i) K
upun
guza
Um
asik
ini n
a U
fuat
iliaji
wa
SD
Gs
230,
000
150,
000
150,
000
15
0,00
0ii)
Ura
tibu
na U
sim
amiz
i wa
Mal
engo
na
Mae
ndel
eo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I20
,000
100,
000
100,
000
U
ND
P80
1,15
090
1,15
0iii)
Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya
Uza
zi, J
insi
a na
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i-
UN
FPA
286,
000
286,
000
iv) U
ende
leza
ji w
a Ta
kwim
u Za
nzib
ar (Z
SD
P)
UN
- W
OM
EN
/ A
DB
/EU
/ U
NIC
EF/
U
NFP
A3,
321,
700
3,32
1,70
0iv
) Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
500,
000
500,
000
50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U75
0,00
01,
300,
000
7,00
0,00
08,
300,
000
4,50
8,85
00
12,8
08,8
50L0
1Pr
ogra
mu
ya U
mw
agili
aji
1,00
0,00
019
,900
,000
19,9
00,0
00
K
OR
EA
47,1
93,4
6467
,093
,464
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a K
ilim
o na
Uha
kika
wa
Cha
kula
(ER
PP)
80,0
00-
WB
2,21
0,52
22,
210,
522
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Uvu
vii)
Uim
aris
haji
Uvu
vi w
a B
ahar
i Kuu
1,40
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
JI
CA
12,1
51,9
0714
,151
,907
ii) K
uim
aris
ha U
fuga
ji w
a M
azao
ya
Bah
arin
i20
0,00
0-
FAO
/ K
OR
EA
736,
479
736,
479
Mira
di
i) M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a S
hugh
uli z
a U
vuvi
wa
Kan
da
ya K
usin
i Mas
harik
i mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00-
WO
RLD
B
AN
K8,
651,
376
8,65
1,37
6
ii) M
radi
wa
Mae
ndel
eo y
a K
ilimo
na U
vuvi
IFA
D2,
141,
198
2,14
1,19
8iii.
Kue
ndel
eza
miu
ndom
binu
ya
Mifu
go n
a W
afug
aji
Wad
ogo
Wad
ogo
1,00
0,00
0-
0iv
. Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,20
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
v) M
radi
wa
Kud
hibi
ti N
zi w
a M
atun
da10
0,00
010
0,00
0
IITA
120,
000
220,
000
vi) K
udhi
biti
Sum
u K
uvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
guA
fDB
931,
698
931,
698
vii)
Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
iU
ND
P3,
801,
497
3,80
1,49
7vi
ii) K
ilimo
cha
Kus
hajih
isha
Uku
lima
wa
Mbo
ga M
boga
na
Mat
unda
ED
F-E
U5,
602,
995
5,60
2,99
5
JUM
LA Y
A F
UN
GU
4,93
0,00
010
0,00
022
,900
,000
23,0
00,0
00
24
,623
,400
58,9
17,7
3610
6,54
1,13
6R
01Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a20
0,00
030
0,00
0
300
,000
30
0,00
0
WIZ
AR
A Y
A K
ILIM
O,
MA
LIA
SILI
, MIF
UG
O N
A U
VUVI
WIZ
AR
A Y
A B
IASH
AR
A N
A V
IWA
ND
A
Page
2 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,00
0,00
0
-
0
i) U
imar
isha
ji w
a M
aene
o ya
Viw
anda
(Ind
urst
rial P
ark)
1,00
0,00
0
1
,000
,000
1,
000,
000
ii) K
uim
aris
ha v
iwan
da v
idog
o vi
dogo
na
vya
kati
(SM
IDA
)1,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0iii)
Mra
di w
a K
uwas
aidi
a W
ajas
iriam
ali W
adog
o W
adog
o,W
akat
i na
Wak
ubw
a4,
500,
000
4,5
00,0
00
KH
ALI
FA
FUN
D4,
600,
000
9,10
0,00
0M
iradi
i)Kui
mar
isha
Taa
sisi
ya
Viw
ango
Zan
ziba
r2,
000,
000
3,00
0,00
0
3
,000
,000
3,
000,
000
ii) M
fum
o m
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sek
ta B
inaf
si40
0,00
040
0,00
0
400
,000
40
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U4,
600,
000
7,20
0,00
03,
000,
000
10,2
00,0
004,
600,
000
014
,800
,000
K01
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
bnu
ya E
limu
1,50
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
aand
aliz
i
-
G
PE
/ M
ILE
LE3,
253,
333
3,25
3,33
3
ii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
-
PC
D/
UN
ICE
F/
MIL
ELE
/ WB
252,
230
150,
000
402,
230
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a3,
300,
000
3,50
0,00
0
3
,500
,000
BA
DE
A/
OP
EC
/ K
OIC
A/W
B2,
821,
521
8,48
5,00
014
,806
,521
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
Mba
dala
na
Am
ali -
Aw
amu
ya
Pili
1,00
0,00
0
-
A
fDB
0JU
MLA
YA
FU
NG
U5,
800,
000
1,00
0,00
03,
500,
000
4,50
0,00
06,
327,
084
8,63
5,00
019
,462
,084
H01
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
alar
ia Z
anzi
bar
248,
000
248,
000
248,
000
P
MI/G
F5,
586,
365
5,83
4,36
5Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a A
fya
i) K
uipa
ndis
ha h
adhi
Hos
pita
li ya
Mna
zi M
moj
a2,
650,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0ii)
Kuz
ipan
dish
a ha
dhi H
ospi
tali
za W
ilaya
na
hosp
itali
za V
ijiji
4,25
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
iii) A
wam
u ya
Kw
anza
ya
ujen
zi w
a H
ospi
tal y
a R
ufaa
B
ingu
ni6,
500,
000
6,00
0,00
06,
000,
000
6,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a B
ohar
i Kuu
ya
Daw
a-P
emba
1,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
v) U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mam
laka
ya
Daw
a na
Vip
odoz
i1,
000,
000
2,10
0,00
02,
100,
000
2,10
0,00
0
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
01,
400,
000
1,40
0,00
0
H
opel
and
Uni
vers
ity1,
400,
000
2,80
0,00
0vi
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a U
tafit
i wa
Afy
a2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
WIZ
AR
A Y
A E
LIM
U N
A M
AFU
NZO
YA
AM
ALI
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Page
3 o
f 6
79Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u Sh
iriki
shi y
a A
fya
ya U
zazi
wa
Mam
a na
M
toto
700,
000
500,
000
500,
000
UN
FPA
/ W
HO
/ U
NIC
EF
9,57
4,37
210
,074
,372
Prog
ram
u ya
Kud
hibi
ti M
arad
hi y
a U
kim
wi,
Hom
a ya
Ini,
Kifu
a K
ikuu
na
Uko
ma
248,
000
248,
000
248,
000
G
F/TH
PS
/ U
NIC
EF
5,09
0,36
25,
338,
362
JUM
LA Y
A F
UN
GU
17,8
96,0
0011
,100
,000
9,89
6,00
020
,996
,000
21,6
51,0
980
42,6
47,0
98N
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a M
aji
Miji
ni2,
948,
000
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jini
3,86
3,00
0M
iradi
i) M
radi
wa
Uhu
isha
ji na
Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Usa
mba
zaji
Maj
i Zan
ziba
r (IN
DIA
)46
6,22
046
6,22
0
IND
IA67
,129
,316
67,5
95,5
36ii)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah4,
000,
000
4,00
0,00
0
4,
000,
000
iii) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 65
0,70
050
0,00
050
0,00
0
500,
000
iv) M
radi
wa
Kui
fany
ia M
abad
iliko
Sek
ta y
a N
isha
ti (Z
ES
T)-
WO
RLD
B
AN
K17
,850
,000
17,8
50,0
00v)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
arN
OR
AD
3,50
0,00
03,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
7,46
1,70
050
0,00
04,
466,
220
4,96
6,22
0
3,
500,
000
84,9
79,3
1693
,445
,536
P01
Prog
ram
u ya
uje
nzi w
a ba
raba
rai)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a Tu
nguu
-Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
ke C
hake
- M
koan
i (31
km)
2,80
0,00
0-
0ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
9,00
0,00
0-
0iii)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
(km
7.2)
na
Ju
mbi
-Koa
ni (k
m 6
.3)
2,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
B
AD
EA
2,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e1,
000,
000
8,00
0,00
08,
000,
000
BA
DE
A8,
990,
000
16,9
90,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(3
1 km
), M
kwaj
uni-K
ijini (
9.4
km),
Pal
e K
iong
ele
- M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni -
K
ombe
ni (k
m 8
.6) n
a B
ubub
u P
olis
i - C
huin
i (km
3)4,
000,
000
1,50
0,00
0
1,
500,
000
AfD
B8,
334,
300
9,83
4,30
0vi
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya J
ozan
i-Cha
raw
e-U
kong
oron
i (k
m 2
3)3,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, Kin
yasi
ni -
Kiw
engw
a na
Dun
ga -
Chw
aka
400,
000
2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
viii)
Uje
nzi w
a D
araj
a la
Uzi
- N
g'am
bwa
5,00
0,00
0
5,
000,
000
5,00
0,00
0ix
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya F
umba
- K
isau
ni (1
2 km
)1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
gei)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
61,0
30,0
005,
500,
000
5,50
0,00
0
12
4,58
6,07
313
0,08
6,07
3
WIZ
AR
A Y
A A
RD
HI,
NY
UM
BA
, MA
JI N
A N
ISH
ATI
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Page
4 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,00
0,00
0
-
0
i) U
imar
isha
ji w
a M
aene
o ya
Viw
anda
(Ind
urst
rial P
ark)
1,00
0,00
0
1
,000
,000
1,
000,
000
ii) K
uim
aris
ha v
iwan
da v
idog
o vi
dogo
na
vya
kati
(SM
IDA
)1,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0iii)
Mra
di w
a K
uwas
aidi
a W
ajas
iriam
ali W
adog
o W
adog
o,W
akat
i na
Wak
ubw
a4,
500,
000
4,5
00,0
00
KH
ALI
FA
FUN
D4,
600,
000
9,10
0,00
0M
iradi
i)Kui
mar
isha
Taa
sisi
ya
Viw
ango
Zan
ziba
r2,
000,
000
3,00
0,00
0
3
,000
,000
3,
000,
000
ii) M
fum
o m
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sek
ta B
inaf
si40
0,00
040
0,00
0
400
,000
40
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U4,
600,
000
7,20
0,00
03,
000,
000
10,2
00,0
004,
600,
000
014
,800
,000
K01
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
bnu
ya E
limu
1,50
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
aand
aliz
i
-
G
PE
/ M
ILE
LE3,
253,
333
3,25
3,33
3
ii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
-
PC
D/
UN
ICE
F/
MIL
ELE
/ WB
252,
230
150,
000
402,
230
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a3,
300,
000
3,50
0,00
0
3
,500
,000
BA
DE
A/
OP
EC
/ K
OIC
A/W
B2,
821,
521
8,48
5,00
014
,806
,521
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
Mba
dala
na
Am
ali -
Aw
amu
ya
Pili
1,00
0,00
0
-
A
fDB
0JU
MLA
YA
FU
NG
U5,
800,
000
1,00
0,00
03,
500,
000
4,50
0,00
06,
327,
084
8,63
5,00
019
,462
,084
H01
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
alar
ia Z
anzi
bar
248,
000
248,
000
248,
000
P
MI/G
F5,
586,
365
5,83
4,36
5Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a A
fya
i) K
uipa
ndis
ha h
adhi
Hos
pita
li ya
Mna
zi M
moj
a2,
650,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0ii)
Kuz
ipan
dish
a ha
dhi H
ospi
tali
za W
ilaya
na
hosp
itali
za V
ijiji
4,25
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
iii) A
wam
u ya
Kw
anza
ya
ujen
zi w
a H
ospi
tal y
a R
ufaa
B
ingu
ni6,
500,
000
6,00
0,00
06,
000,
000
6,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a B
ohar
i Kuu
ya
Daw
a-P
emba
1,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
v) U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mam
laka
ya
Daw
a na
Vip
odoz
i1,
000,
000
2,10
0,00
02,
100,
000
2,10
0,00
0
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
01,
400,
000
1,40
0,00
0
H
opel
and
Uni
vers
ity1,
400,
000
2,80
0,00
0vi
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a U
tafit
i wa
Afy
a2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
WIZ
AR
A Y
A E
LIM
U N
A M
AFU
NZO
YA
AM
ALI
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Page
3 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u Sh
iriki
shi y
a A
fya
ya U
zazi
wa
Mam
a na
M
toto
700,
000
500,
000
500,
000
UN
FPA
/ W
HO
/ U
NIC
EF
9,57
4,37
210
,074
,372
Prog
ram
u ya
Kud
hibi
ti M
arad
hi y
a U
kim
wi,
Hom
a ya
Ini,
Kifu
a K
ikuu
na
Uko
ma
248,
000
248,
000
248,
000
G
F/TH
PS
/ U
NIC
EF
5,09
0,36
25,
338,
362
JUM
LA Y
A F
UN
GU
17,8
96,0
0011
,100
,000
9,89
6,00
020
,996
,000
21,6
51,0
980
42,6
47,0
98N
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a M
aji
Miji
ni2,
948,
000
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jini
3,86
3,00
0M
iradi
i) M
radi
wa
Uhu
isha
ji na
Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Usa
mba
zaji
Maj
i Zan
ziba
r (IN
DIA
)46
6,22
046
6,22
0
IND
IA67
,129
,316
67,5
95,5
36ii)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah4,
000,
000
4,00
0,00
0
4,
000,
000
iii) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 65
0,70
050
0,00
050
0,00
0
500,
000
iv) M
radi
wa
Kui
fany
ia M
abad
iliko
Sek
ta y
a N
isha
ti (Z
ES
T)-
WO
RLD
B
AN
K17
,850
,000
17,8
50,0
00v)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
arN
OR
AD
3,50
0,00
03,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
7,46
1,70
050
0,00
04,
466,
220
4,96
6,22
0
3,
500,
000
84,9
79,3
1693
,445
,536
P01
Prog
ram
u ya
uje
nzi w
a ba
raba
rai)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a Tu
nguu
-Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
ke C
hake
- M
koan
i (31
km)
2,80
0,00
0-
0ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
9,00
0,00
0-
0iii)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
(km
7.2)
na
Ju
mbi
-Koa
ni (k
m 6
.3)
2,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
B
AD
EA
2,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e1,
000,
000
8,00
0,00
08,
000,
000
BA
DE
A8,
990,
000
16,9
90,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(3
1 km
), M
kwaj
uni-K
ijini (
9.4
km),
Pal
e K
iong
ele
- M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni -
K
ombe
ni (k
m 8
.6) n
a B
ubub
u P
olis
i - C
huin
i (km
3)4,
000,
000
1,50
0,00
0
1,
500,
000
AfD
B8,
334,
300
9,83
4,30
0vi
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya J
ozan
i-Cha
raw
e-U
kong
oron
i (k
m 2
3)3,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, Kin
yasi
ni -
Kiw
engw
a na
Dun
ga -
Chw
aka
400,
000
2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
viii)
Uje
nzi w
a D
araj
a la
Uzi
- N
g'am
bwa
5,00
0,00
0
5,
000,
000
5,00
0,00
0ix
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya F
umba
- K
isau
ni (1
2 km
)1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
gei)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
61,0
30,0
005,
500,
000
5,50
0,00
0
12
4,58
6,07
313
0,08
6,07
3
WIZ
AR
A Y
A A
RD
HI,
NY
UM
BA
, MA
JI N
A N
ISH
ATI
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Page
4 o
f 6
80Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
ii) U
jenz
i wa
Uw
anja
wa
Nde
ge w
a P
emba
1,00
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
jenz
i wa
Ban
dari
ya M
piga
duri
3,00
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
ii) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
1,90
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
88,1
30,0
0025
,000
,000
10,5
00,0
0035
,500
,000
014
1,91
0,37
317
7,41
0,37
3Q
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
ai)
Usa
wa
wa
Kijin
sia
na K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en18
0,00
018
0,00
0ii)
Mra
di w
a Ji
nsia
UN
FPA
470,
628
470,
628
Mira
dii)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
waz
ee40
0,00
01,
100,
000
1,1
00,0
00
1,10
0,00
0ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a K
ulea
na
Kut
otol
ea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
1,00
0,00
0
1
,000
,000
1,
000,
000
iii) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a Ja
mii
UN
ICE
F12
1,00
012
1,00
0iv
) Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Wat
oto
UN
ICE
F38
7,52
338
7,52
3JU
MLA
YA
FU
NG
U1,
000,
000
2,10
0,00
00
2,10
0,00
01,
159,
151
03,
259,
151
G10
i) M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a U
patik
anaj
i wa
Hak
i40
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
1,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
400,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
i) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a M
afun
zo y
a S
heria
na
Uta
fiti
600,
000
600,
000
60
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U60
0,00
060
0,00
0
600,
000
E06
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Utu
mis
hi w
a U
mm
a - I
I20
0,00
040
0,00
040
0,00
0
400,
000
Mra
dii)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsm
issi
on
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k P
hase
II10
0,00
0-
0JU
MLA
YA
FU
NG
U30
0,00
040
0,00
00
400,
000
00
400,
000
E05
ii) U
jenz
i wa
Ofis
i ya
ZAE
CA
800,
000
1,00
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U80
0,00
01,
000,
000
01,
000,
000
00
1,00
0,00
0J0
1Pr
ogra
mu
Mju
mui
sho
ya K
uend
elez
a U
talii
2,40
0,00
0
2,
700,
000
2,70
0,00
0
2,
700,
000
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Jeng
o la
Ofis
i na
Stu
dio
za R
edio
Mka
njun
i-P
emba
1,50
0,00
0
1,
400,
000
1,40
0,00
0
1,
400,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U3,
900,
000
4,10
0,00
0
-
4,10
0,00
0
-
-
4,10
0,00
0
J02
G04
MK
UR
UG
ENZI
WA
MA
SHTA
KA
KA
MIS
HEN
I YA
UTA
LII
WIZ
AR
A Y
A H
AB
AR
I, U
TALI
I NA
MA
MB
O Y
A K
ALE
WIZ
AR
A Y
A K
AZI
, UW
EZES
HA
JI,
WA
ZEE,
WA
NA
WA
KE
NA
WA
TOTO
OFI
SI Y
A R
AIS
- K
ATI
BA
NA
SH
ERIA
OFI
SI Y
A R
AIS
- U
TUM
ISH
I WA
UM
MA
NA
UTA
WA
LA B
OR
A
MA
MLA
KA
YA
KU
ZUIA
RU
SHW
A N
A U
HU
JUM
U W
A U
CH
UM
I
Page
5 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
Prog
ram
u Sh
iriki
shi y
a A
fya
ya U
zazi
wa
Mam
a na
M
toto
700,
000
500,
000
500,
000
UN
FPA
/ W
HO
/ U
NIC
EF
9,57
4,37
210
,074
,372
Prog
ram
u ya
Kud
hibi
ti M
arad
hi y
a U
kim
wi,
Hom
a ya
Ini,
Kifu
a K
ikuu
na
Uko
ma
248,
000
248,
000
248,
000
G
F/TH
PS
/ U
NIC
EF
5,09
0,36
25,
338,
362
JUM
LA Y
A F
UN
GU
17,8
96,0
0011
,100
,000
9,89
6,00
020
,996
,000
21,6
51,0
980
42,6
47,0
98N
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a M
aji
Miji
ni2,
948,
000
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jini
3,86
3,00
0M
iradi
i) M
radi
wa
Uhu
isha
ji na
Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Usa
mba
zaji
Maj
i Zan
ziba
r (IN
DIA
)46
6,22
046
6,22
0
IND
IA67
,129
,316
67,5
95,5
36ii)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah4,
000,
000
4,00
0,00
0
4,
000,
000
iii) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 65
0,70
050
0,00
050
0,00
0
500,
000
iv) M
radi
wa
Kui
fany
ia M
abad
iliko
Sek
ta y
a N
isha
ti (Z
ES
T)-
WO
RLD
B
AN
K17
,850
,000
17,8
50,0
00v)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
arN
OR
AD
3,50
0,00
03,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
7,46
1,70
050
0,00
04,
466,
220
4,96
6,22
0
3,
500,
000
84,9
79,3
1693
,445
,536
P01
Prog
ram
u ya
uje
nzi w
a ba
raba
rai)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a Tu
nguu
-Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
ke C
hake
- M
koan
i (31
km)
2,80
0,00
0-
0ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
9,00
0,00
0-
0iii)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
(km
7.2)
na
Ju
mbi
-Koa
ni (k
m 6
.3)
2,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
B
AD
EA
2,00
0,00
0iv
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e1,
000,
000
8,00
0,00
08,
000,
000
BA
DE
A8,
990,
000
16,9
90,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(3
1 km
), M
kwaj
uni-K
ijini (
9.4
km),
Pal
e K
iong
ele
- M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni -
K
ombe
ni (k
m 8
.6) n
a B
ubub
u P
olis
i - C
huin
i (km
3)4,
000,
000
1,50
0,00
0
1,
500,
000
AfD
B8,
334,
300
9,83
4,30
0vi
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya J
ozan
i-Cha
raw
e-U
kong
oron
i (k
m 2
3)3,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, Kin
yasi
ni -
Kiw
engw
a na
Dun
ga -
Chw
aka
400,
000
2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
viii)
Uje
nzi w
a D
araj
a la
Uzi
- N
g'am
bwa
5,00
0,00
0
5,
000,
000
5,00
0,00
0ix
) Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya F
umba
- K
isau
ni (1
2 km
)1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
gei)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
61,0
30,0
005,
500,
000
5,50
0,00
0
12
4,58
6,07
313
0,08
6,07
3
WIZ
AR
A Y
A A
RD
HI,
NY
UM
BA
, MA
JI N
A N
ISH
ATI
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Page
4 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
ii) U
jenz
i wa
Uw
anja
wa
Nde
ge w
a Pe
mba
1,00
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
jenz
i wa
Band
ari y
a M
piga
duri
3,00
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
ii) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
1,90
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
88,1
30,0
0025
,000
,000
10,5
00,0
0035
,500
,000
014
1,91
0,37
317
7,41
0,37
3Q
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
ai)
Usa
wa
wa
Kijin
sia
na K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en18
0,00
018
0,00
0ii)
Mra
di w
a Ji
nsia
UN
FPA
470,
628
470,
628
Mira
dii)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
waz
ee40
0,00
01,
100,
000
1,1
00,0
00
1,10
0,00
0ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ku
lea
na K
utot
olea
W
ajas
iriam
ali (
Incu
bato
r)60
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0iii)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Jam
iiU
NIC
EF12
1,00
012
1,00
0iv
) Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Wat
oto
UN
ICEF
387,
523
387,
523
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,00
0,00
02,
100,
000
02,
100,
000
1,15
9,15
10
3,25
9,15
1G
10i)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Upa
tikan
aji w
a H
aki
400,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U40
0,00
01,
500,
000
01,
500,
000
00
1,50
0,00
0
i) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a M
afun
zo y
a S
heria
na
Uta
fiti
600,
000
600,
000
60
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U60
0,00
060
0,00
0
600,
000
E06
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Utu
mis
hi w
a U
mm
a - I
I20
0,00
040
0,00
040
0,00
0
400,
000
Mra
dii)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsm
issi
on
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k Ph
ase
II10
0,00
0-
0JU
MLA
YA
FU
NG
U30
0,00
040
0,00
00
400,
000
00
400,
000
E05
ii) U
jenz
i wa
Ofis
i ya
ZAEC
A80
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
800,
000
1,00
0,00
00
1,00
0,00
00
01,
000,
000
J01
Prog
ram
u M
jum
uish
o ya
Kue
ndel
eza
Uta
lii2,
400,
000
2,70
0,00
0
2,
700,
000
2,70
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Je
ngo
la O
fisi n
a St
udio
za
Red
io M
kanj
uni-
Pem
ba1,
500,
000
1,40
0,00
0
1,
400,
000
1,40
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3,90
0,00
0
4,
100,
000
-
4,
100,
000
-
-
4,
100,
000
J0
2
G04
MK
UR
UG
ENZI
WA
MA
SHTA
KA
KA
MIS
HEN
I YA
UTA
LII
WIZ
AR
A Y
A H
AB
AR
I, U
TALI
I NA
MA
MB
O Y
A K
ALE
WIZ
AR
A Y
A K
AZI
, UW
EZES
HA
JI,
WA
ZEE,
WA
NA
WA
KE
NA W
ATO
TO
OFI
SI Y
A R
AIS
- K
ATI
BA
NA
SH
ERIA
OFI
SI Y
A R
AIS
- U
TUM
ISH
I WA
UM
MA
NA
UTA
WA
LA B
OR
A
MA
MLA
KA
YA
KU
ZUIA
RU
SHW
A N
A U
HU
JUM
U W
A U
CH
UM
I
Page
5 o
f 6
81Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MAK
ISIO
YA
KAW
AIDA
20
20/2
1
DHIM
A 20
20/2
1
JUM
LA Y
A M
AKIS
IO Y
A SM
Z 20
20/2
1 M
UHIS
ANI
RUZ
UKU
MIK
OPO
KIF
UNG
UJI
NA L
A PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
K
WA
MW
AKA
2019
/202
0 SM
Z
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
1 SM
Z
MIC
HANG
O Y
A W
AHIS
ANI
JUM
LA Y
A BA
JETI
Kuim
aris
ha U
talii
kwa
Wot
e1,
500,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A FU
NGU
1,50
0,00
0
2,
000,
000
-
2,
000,
000
-
-
2,
000,
000
S0
1Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Vi
wan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
2,00
0,00
0
2,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JU
MLA
YA
FUNG
U4,
000,
000
2,50
0,00
0
2,
000,
000
4,50
0,00
0
-
-
4,50
0,00
0
D01
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u1,
110,
000
1,00
0,00
0
1
,000
,000
M
ILEL
E/
GPE
/ PC
D2,
896,
230
3,89
6,23
0M
IRAD
Ii)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi7,
000,
000
8,00
0,00
0
8
,000
,000
8,
000,
000
ii) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
)4,
500,
000
2,50
0,00
0
2
,500
,000
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
12,6
10,0
003,
500,
000
8,00
0,00
0
11,
500,
000
2,89
6,23
00
14,3
96,2
30D
12i)
Mra
di w
a Ku
imar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a Vi
zazi
na
Vifo
1,00
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,00
0,00
0
-
1,00
0,00
0
-
-
1,00
0,00
0
D04
i) Ku
imar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i
2,9
00,0
00
4,80
0,00
0
4
,800
,000
4
,800
,000
ii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a Ka
mbi
na
Nyu
mba
za
KMKM
1
,000
,000
700,
000
7
00,0
00
7
00,0
00
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,90
0,00
05,
500,
000
0
5
,500
,000
0
05,
500,
000
D06
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i50
0,00
01,
500,
000
1,5
00,0
00
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U50
0,00
01,
500,
000
0
1
,500
,000
-
-
1,50
0,00
0D
03i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga1,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
D02
i) U
jenz
i wa
Skul
i ya
Seko
ndar
i na
Ufu
ndi -
Mto
ni3,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0ii)
Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a Ka
mbi
za
JKU
50
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,50
0,00
04,
500,
000
04,
500,
000
00
4,50
0,00
0D
05U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
500,
000
2,50
0,00
00
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA K
UBW
A18
2,40
0,00
086
,570
,000
110,
762,
220
197,
332,
220
72,1
63,3
7834
0,49
5,42
060
9,99
1,01
8
JUM
LA Y
A FE
DHA
ZA W
AHIS
ANI
JESH
I LA
KUJ
ENG
A UC
HUM
I
KIK
OSI
CHA
ZIM
AMO
TO N
A UO
KO
ZI
412,
658,
798
WIZ
ARA
YA V
IJAN
A, U
TAM
ADUN
I, SA
NAA
NA M
ICHE
ZO
OFI
SI Y
A R
AIS
TAW
ALA
ZA M
IKO
A, S
ERIK
ALI Z
A M
ITAA
NA
IDAR
A M
AALU
M Z
A SM
Z
WAK
ALA
WA
USAJ
ILI W
A M
ATUK
IO Y
A K
IJAM
II ZA
NZIB
AR
KIK
OSI
MAA
LUM
CHA
KUZ
UIA
MAG
ENDO
(KM
KM
)
KIK
OSI
CHA
VAL
ANTI
A
CHU
O C
HA M
AFUN
ZO
Page
6 o
f 6
MA
KIS
IO Y
A
KA
WA
IDA
20
20/2
1
DH
IMA
20
20/2
1
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
20/2
1 M
UH
ISA
NI
RU
ZUK
UM
IKO
POK
IFU
NG
UJI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
020/
21 S
MZ
M
ICH
AN
GO
YA
WA
HIS
AN
I
JUM
LA Y
A
BA
JETI
ii) U
jenz
i wa
Uw
anja
wa
Nde
ge w
a Pe
mba
1,00
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0M
iradi
i) U
jenz
i wa
Band
ari y
a M
piga
duri
3,00
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
5,
000,
000
ii) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
1,90
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
88,1
30,0
0025
,000
,000
10,5
00,0
0035
,500
,000
014
1,91
0,37
317
7,41
0,37
3Q
01Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
ai)
Usa
wa
wa
Kijin
sia
na K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en18
0,00
018
0,00
0ii)
Mra
di w
a Ji
nsia
UN
FPA
470,
628
470,
628
Mira
dii)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
waz
ee40
0,00
01,
100,
000
1,1
00,0
00
1,10
0,00
0ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ku
lea
na K
utot
olea
W
ajas
iriam
ali (
Incu
bato
r)60
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0iii)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Jam
iiU
NIC
EF12
1,00
012
1,00
0iv
) Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Wat
oto
UN
ICEF
387,
523
387,
523
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,00
0,00
02,
100,
000
02,
100,
000
1,15
9,15
10
3,25
9,15
1G
10i)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Upa
tikan
aji w
a H
aki
400,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U40
0,00
01,
500,
000
01,
500,
000
00
1,50
0,00
0
i) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a M
afun
zo y
a S
heria
na
Uta
fiti
600,
000
600,
000
60
0,00
0JU
MLA
YA
FU
NG
U60
0,00
060
0,00
0
600,
000
E06
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Utu
mis
hi w
a U
mm
a - I
I20
0,00
040
0,00
040
0,00
0
400,
000
Mra
dii)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsm
issi
on
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k Ph
ase
II10
0,00
0-
0JU
MLA
YA
FU
NG
U30
0,00
040
0,00
00
400,
000
00
400,
000
E05
ii) U
jenz
i wa
Ofis
i ya
ZAEC
A80
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
1,
000,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
800,
000
1,00
0,00
00
1,00
0,00
00
01,
000,
000
J01
Prog
ram
u M
jum
uish
o ya
Kue
ndel
eza
Uta
lii2,
400,
000
2,70
0,00
0
2,
700,
000
2,70
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Je
ngo
la O
fisi n
a St
udio
za
Red
io M
kanj
uni-
Pem
ba1,
500,
000
1,40
0,00
0
1,
400,
000
1,40
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3,90
0,00
0
4,
100,
000
-
4,
100,
000
-
-
4,
100,
000
J0
2
G04
MK
UR
UG
ENZI
WA
MA
SHTA
KA
KA
MIS
HEN
I YA
UTA
LII
WIZ
AR
A Y
A H
AB
AR
I, U
TALI
I NA
MA
MB
O Y
A K
ALE
WIZ
AR
A Y
A K
AZI
, UW
EZES
HA
JI,
WA
ZEE,
WA
NA
WA
KE
NA W
ATO
TO
OFI
SI Y
A R
AIS
- K
ATI
BA
NA
SH
ERIA
OFI
SI Y
A R
AIS
- U
TUM
ISH
I WA
UM
MA
NA
UTA
WA
LA B
OR
A
MA
MLA
KA
YA
KU
ZUIA
RU
SHW
A N
A U
HU
JUM
U W
A U
CH
UM
I
Page
5 o
f 6
MAK
ISIO
YA
KAW
AIDA
20
20/2
1
DHIM
A 20
20/2
1
JUM
LA Y
A M
AKIS
IO Y
A SM
Z 20
20/2
1 M
UHIS
ANI
RUZ
UKU
MIK
OPO
KIF
UNG
UJI
NA L
A PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
K
WA
MW
AKA
2019
/202
0 SM
Z
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
1 SM
Z
MIC
HANG
O Y
A W
AHIS
ANI
JUM
LA Y
A BA
JETI
Kuim
aris
ha U
talii
kwa
Wot
e1,
500,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A FU
NGU
1,50
0,00
0
2,
000,
000
-
2,
000,
000
-
-
2,
000,
000
S0
1Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Vi
wan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
2,00
0,00
0
2,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JU
MLA
YA
FUNG
U4,
000,
000
2,50
0,00
0
2,
000,
000
4,50
0,00
0
-
-
4,50
0,00
0
D01
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u1,
110,
000
1,00
0,00
0
1
,000
,000
M
ILEL
E/
GPE
/ PC
D2,
896,
230
3,89
6,23
0M
IRAD
Ii)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi7,
000,
000
8,00
0,00
0
8
,000
,000
8,
000,
000
ii) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
)4,
500,
000
2,50
0,00
0
2
,500
,000
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
12,6
10,0
003,
500,
000
8,00
0,00
0
11,
500,
000
2,89
6,23
00
14,3
96,2
30D
12i)
Mra
di w
a Ku
imar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a Vi
zazi
na
Vifo
1,00
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,00
0,00
0
-
1,00
0,00
0
-
-
1,00
0,00
0
D04
i) Ku
imar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i
2,9
00,0
00
4,80
0,00
0
4
,800
,000
4
,800
,000
ii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a Ka
mbi
na
Nyu
mba
za
KMKM
1
,000
,000
700,
000
7
00,0
00
7
00,0
00
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,90
0,00
05,
500,
000
0
5
,500
,000
0
05,
500,
000
D06
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i50
0,00
01,
500,
000
1,5
00,0
00
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U50
0,00
01,
500,
000
0
1
,500
,000
-
-
1,50
0,00
0D
03i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga1,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
D02
i) U
jenz
i wa
Skul
i ya
Seko
ndar
i na
Ufu
ndi -
Mto
ni3,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0ii)
Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a Ka
mbi
za
JKU
50
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,50
0,00
04,
500,
000
04,
500,
000
00
4,50
0,00
0D
05U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
500,
000
2,50
0,00
00
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA K
UBW
A18
2,40
0,00
086
,570
,000
110,
762,
220
197,
332,
220
72,1
63,3
7834
0,49
5,42
060
9,99
1,01
8
JUM
LA Y
A FE
DHA
ZA W
AHIS
ANI
JESH
I LA
KUJ
ENG
A UC
HUM
I
KIK
OSI
CHA
ZIM
AMO
TO N
A UO
KO
ZI
412,
658,
798
WIZ
ARA
YA V
IJAN
A, U
TAM
ADUN
I, SA
NAA
NA M
ICHE
ZO
OFI
SI Y
A R
AIS
TAW
ALA
ZA M
IKO
A, S
ERIK
ALI Z
A M
ITAA
NA
IDAR
A M
AALU
M Z
A SM
Z
WAK
ALA
WA
USAJ
ILI W
A M
ATUK
IO Y
A K
IJAM
II ZA
NZIB
AR
KIK
OSI
MAA
LUM
CHA
KUZ
UIA
MAG
ENDO
(KM
KM
)
KIK
OSI
CHA
VAL
ANTI
A
CHU
O C
HA M
AFUN
ZO
Page
6 o
f 6
82Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MAK
ISIO
YA
KAW
AIDA
20
20/2
1
DHIM
A 20
20/2
1
JUM
LA Y
A M
AKIS
IO Y
A SM
Z 20
20/2
1 M
UHIS
ANI
RUZ
UKU
MIK
OPO
KIF
UNG
UJI
NA L
A PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
K
WA
MW
AKA
2019
/202
0 SM
Z
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
1 SM
Z
MIC
HANG
O Y
A W
AHIS
ANI
JUM
LA Y
A BA
JETI
Kuim
aris
ha U
talii
kwa
Wot
e1,
500,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A FU
NGU
1,50
0,00
0
2,
000,
000
-
2,
000,
000
-
-
2,
000,
000
S0
1Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Vi
wan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
2,00
0,00
0
2,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JU
MLA
YA
FUNG
U4,
000,
000
2,50
0,00
0
2,
000,
000
4,50
0,00
0
-
-
4,50
0,00
0
D01
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u1,
110,
000
1,00
0,00
0
1
,000
,000
M
ILEL
E/
GPE
/ PC
D2,
896,
230
3,89
6,23
0M
IRAD
Ii)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi7,
000,
000
8,00
0,00
0
8
,000
,000
8,
000,
000
ii) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
)4,
500,
000
2,50
0,00
0
2
,500
,000
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
12,6
10,0
003,
500,
000
8,00
0,00
0
11,
500,
000
2,89
6,23
00
14,3
96,2
30D
12i)
Mra
di w
a Ku
imar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a Vi
zazi
na
Vifo
1,00
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,00
0,00
0
-
1,00
0,00
0
-
-
1,00
0,00
0
D04
i) Ku
imar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i
2,9
00,0
00
4,80
0,00
0
4
,800
,000
4
,800
,000
ii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a Ka
mbi
na
Nyu
mba
za
KMKM
1
,000
,000
700,
000
7
00,0
00
7
00,0
00
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,90
0,00
05,
500,
000
0
5
,500
,000
0
05,
500,
000
D06
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i50
0,00
01,
500,
000
1,5
00,0
00
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U50
0,00
01,
500,
000
0
1
,500
,000
-
-
1,50
0,00
0D
03i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga1,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
D02
i) U
jenz
i wa
Skul
i ya
Seko
ndar
i na
Ufu
ndi -
Mto
ni3,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0ii)
Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a Ka
mbi
za
JKU
50
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,50
0,00
04,
500,
000
04,
500,
000
00
4,50
0,00
0D
05U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
500,
000
2,50
0,00
00
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA K
UBW
A18
2,40
0,00
086
,570
,000
110,
762,
220
197,
332,
220
72,1
63,3
7834
0,49
5,42
060
9,99
1,01
8
JUM
LA Y
A FE
DHA
ZA W
AHIS
ANI
JESH
I LA
KUJ
ENG
A UC
HUM
I
KIK
OSI
CHA
ZIM
AMO
TO N
A UO
KO
ZI
412,
658,
798
WIZ
ARA
YA V
IJAN
A, U
TAM
ADUN
I, SA
NAA
NA M
ICHE
ZO
OFI
SI Y
A R
AIS
TAW
ALA
ZA M
IKO
A, S
ERIK
ALI Z
A M
ITAA
NA
IDAR
A M
AALU
M Z
A SM
Z
WAK
ALA
WA
USAJ
ILI W
A M
ATUK
IO Y
A K
IJAM
II ZA
NZIB
AR
KIK
OSI
MAA
LUM
CHA
KUZ
UIA
MAG
ENDO
(KM
KM
)
KIK
OSI
CHA
VAL
ANTI
A
CHU
O C
HA M
AFUN
ZO
Page
6 o
f 6
MAK
ISIO
YA
KAW
AIDA
20
20/2
1
DHIM
A 20
20/2
1
JUM
LA Y
A M
AKIS
IO Y
A SM
Z 20
20/2
1 M
UHIS
ANI
RUZ
UKU
MIK
OPO
KIF
UNG
UJI
NA L
A PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
K
WA
MW
AKA
2019
/202
0 SM
Z
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
1 SM
Z
MIC
HANG
O Y
A W
AHIS
ANI
JUM
LA Y
A BA
JETI
Kuim
aris
ha U
talii
kwa
Wot
e1,
500,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A FU
NGU
1,50
0,00
0
2,
000,
000
-
2,
000,
000
-
-
2,
000,
000
S0
1Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na2,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
2,00
0,00
0
Mira
dii)
Uje
nzi w
a Vi
wan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
2,00
0,00
0
2,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JU
MLA
YA
FUNG
U4,
000,
000
2,50
0,00
0
2,
000,
000
4,50
0,00
0
-
-
4,50
0,00
0
D01
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u1,
110,
000
1,00
0,00
0
1
,000
,000
M
ILEL
E/
GPE
/ PC
D2,
896,
230
3,89
6,23
0M
IRAD
Ii)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi7,
000,
000
8,00
0,00
0
8
,000
,000
8,
000,
000
ii) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
)4,
500,
000
2,50
0,00
0
2
,500
,000
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
12,6
10,0
003,
500,
000
8,00
0,00
0
11,
500,
000
2,89
6,23
00
14,3
96,2
30D
12i)
Mra
di w
a Ku
imar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a Vi
zazi
na
Vifo
1,00
0,00
01,
000,
000
1,0
00,0
00
1,00
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,00
0,00
0
-
1,00
0,00
0
-
-
1,00
0,00
0
D04
i) Ku
imar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i
2,9
00,0
00
4,80
0,00
0
4
,800
,000
4
,800
,000
ii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a Ka
mbi
na
Nyu
mba
za
KMKM
1
,000
,000
700,
000
7
00,0
00
7
00,0
00
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,90
0,00
05,
500,
000
0
5
,500
,000
0
05,
500,
000
D06
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i50
0,00
01,
500,
000
1,5
00,0
00
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U50
0,00
01,
500,
000
0
1
,500
,000
-
-
1,50
0,00
0D
03i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga1,
000,
000
1,50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0JU
MLA
YA
FUNG
U1,
000,
000
1,50
0,00
00
1,50
0,00
0
0
01,
500,
000
D02
i) U
jenz
i wa
Skul
i ya
Seko
ndar
i na
Ufu
ndi -
Mto
ni3,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0ii)
Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a Ka
mbi
za
JKU
50
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
2,
000,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
3,50
0,00
04,
500,
000
04,
500,
000
00
4,50
0,00
0D
05U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i50
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA Y
A FU
NGU
500,
000
2,50
0,00
00
2,50
0,00
0
2,
500,
000
JUM
LA K
UBW
A18
2,40
0,00
086
,570
,000
110,
762,
220
197,
332,
220
72,1
63,3
7834
0,49
5,42
060
9,99
1,01
8
JUM
LA Y
A FE
DHA
ZA W
AHIS
ANI
JESH
I LA
KUJ
ENG
A UC
HUM
I
KIK
OSI
CHA
ZIM
AMO
TO N
A UO
KO
ZI
412,
658,
798
WIZ
ARA
YA V
IJAN
A, U
TAM
ADUN
I, SA
NAA
NA M
ICHE
ZO
OFI
SI Y
A R
AIS
TAW
ALA
ZA M
IKO
A, S
ERIK
ALI Z
A M
ITAA
NA
IDAR
A M
AALU
M Z
A SM
Z
WAK
ALA
WA
USAJ
ILI W
A M
ATUK
IO Y
A K
IJAM
II ZA
NZIB
AR
KIK
OSI
MAA
LUM
CHA
KUZ
UIA
MAG
ENDO
(KM
KM
)
KIK
OSI
CHA
VAL
ANTI
A
CHU
O C
HA M
AFUN
ZO
Page
6 o
f 6
83Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MU
HIS
ANI
RU
ZUK
U M
KO
PO
PRO
GR
AMU
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i1,
000,
000
19,9
00,0
00KO
REA
47,1
93,4
64
67
,093
,464
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a K
ilim
o na
Uha
kika
wa
Cha
kula
(ER
PP)
80,0
00W
B2,
210,
522
2,21
0,52
2
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
2,20
0,00
0-
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Uvu
vi-
i) U
imar
isha
ji uv
uvi w
a ba
hari
kuu
1,40
0,00
02,
000,
000
JIC
A12
,151
,907
14
,151
,907
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
FAO
/ KO
REA
736,
479
73
6,47
9
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a20
0,00
030
0,00
030
0,00
0
Pr
ogra
mu
ya K
uend
elez
a Vi
wan
da2,
000,
000
-
i)
Uim
aris
haji
wa
Mae
neo
ya V
iwan
da (I
ndur
stria
l Par
k)1,
000,
000
1,00
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha v
iwan
da v
idog
o vi
dogo
na
vya
kati
(SM
IDA)
1,00
0,00
01,
000,
000
iii)
Kuw
asai
dia
Waj
asiri
amal
i Wad
ogo
Wad
ogo,
Wak
ati n
a W
akub
wa
4,50
0,00
0KH
ALIF
A FU
ND
4,60
0,00
0
9,
100,
000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
2,40
0,00
0
2,70
0,00
0
2,70
0,00
0
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a Ba
raba
ra-
i) U
jenz
i wa
Bara
bara
ya
Tung
uu-M
akun
duch
i (30
km) n
a C
hake
chak
e - M
koan
i (31
km)
2,80
0,00
0
-
ii)
Uje
nzi w
a Ba
raba
ra O
le-K
enge
ja9,
000,
000
-
iii)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a Ki
zim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni2,
000,
000
2,00
0,00
0BA
DEA
2,00
0,00
0
iv) U
jenz
i wa
bara
bara
ya
Cha
ke-W
ete
1,00
0,00
08,
000,
000
BAD
EA8,
990,
000
16,9
90,0
00
v)
Uje
nzi w
a Ba
raba
ra z
a Bu
bubu
-Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kijin
i (9.
4 km
), Pa
le K
iong
ele
- Mkw
ajun
i (4.
6 km
), M
atem
we
- Muy
uni (
7.6
km),
Fuon
i - K
ombe
ni (k
m 8
.6) n
a Bu
bubu
Po
lisi -
Chu
ini (
km3)
4,00
0,00
0
1,50
0,00
0
AfD
B8,
334,
300
9,83
4,30
0
vi) U
jenz
i wa
Bara
bara
ya
Joza
ni-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)3,
000,
000
2,
000,
000
2,
000,
000
vi
i) U
jenz
i wa
Bara
bara
ya
Kito
gani
- Pa
je, M
ahon
da -
Don
ge -
Mko
koto
ni, K
inya
sini
- Ki
wen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a40
0,00
0
2,
000,
000
2,
000,
000
vi
ii) U
jenz
i wa
Dar
aja
la U
zi -
Ng'
ambw
a5,
000,
000
5,
000,
000
ix)
Uje
nzi w
a Ba
raba
ra y
a Fu
mba
- Ki
saun
i (12
km)
1,00
0,00
0
1,00
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
ge-
i) U
jenz
i wa
Jeng
o Ji
pya
la A
biria
Zan
ziba
r61
,030
,000
5,50
0,00
0EX
IM C
HIN
A12
4,58
6,07
3
130,
086,
073
ii) U
jenz
i wa
Uw
anja
wa
Nde
ge w
a Pe
mba
1,00
0,00
01,
000,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
)40
,000
50
,000
WB
21,5
47,9
95
21
,597
,995
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO W
A FE
DH
A PR
OG
RAM
U M
IRAD
I 202
0/20
21 K
IMAE
NEO
MAK
UU
YA
MAT
OK
EO T
ZS ("
000"
)
JIN
A LA
PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
19/2
020
SMZ
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
021
SMZ
MC
HAN
GO
WA
MU
HIS
ANI
JU
MLA
YA
BAJE
TI
KR
A A:
KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI W
A U
CH
UM
I JU
MU
ISH
I NA
END
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UBW
A ZO
TE
Page
1 o
f 5
84Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MU
HIS
ANI
RU
ZUK
U M
KO
PO
JIN
A LA
PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
19/2
020
SMZ
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
021
SMZ
MC
HAN
GO
WA
MU
HIS
ANI
JU
MLA
YA
BAJE
TI
Prog
ram
u ya
Mpa
ngo
wa
Kur
asim
isha
Ras
ilim
ali n
a Bi
asha
ra
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(MK
UR
ABIT
A)50
0,00
055
0,00
0U
RT
100,
000
65
0,00
0
M
pang
o w
a K
uhui
sha
Uch
umi (
ERP)
7,00
0,00
07,
000,
000
M
IRAD
I-
i) U
sim
amiz
i wa
Shug
huli
za U
vuvi
wa
Kand
a ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a Ba
hari
ya H
indi
(SW
IOFI
SH)
50,0
00W
OR
LD B
ANK
8,65
1,37
6
8,
651,
376
ii)
Kui
mar
isha
Taa
sisi
ya
Viw
ango
Zan
ziba
r2,
000,
000
3,00
0,00
03,
000,
000
iii)
Uje
nzi w
a Ba
ndar
i ya
Mpi
gadu
ri3,
000,
000
5,00
0,00
05,
000,
000
iv
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atilia
ji w
a SD
Gs
230,
000
150,
000
150,
000
v) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
)4,
500,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
vi
) Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
500,
000
500,
000
vii)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsim
issi
on C
omm
unic
atio
n N
etw
ork
Phas
e II
100,
000
-
vi
ii) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
1,90
0,00
02,
500,
000
2,50
0,00
0
ix) M
fum
o M
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sekt
a Bi
nafs
i40
0,00
040
0,00
040
0,00
0
x)
Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,00
0,00
01,
000,
000
xi)
Kud
hibi
ti Su
mu
Kuvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
gu
(TAN
IPAC
)Af
DB
931,
698
93
1,69
8
xii
) Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
iU
ND
P3,
801,
497
3,80
1,49
7
xiii)
Kilim
o ch
a Ku
shaj
ihis
ha U
kulim
a w
a M
boga
Mbo
ga n
a M
atun
daED
F-EU
5,60
2,99
5
5,
602,
995
xiv
) Kui
mar
isha
Uta
lii kw
a W
ote
1,50
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
xv) K
uend
elez
a Ba
ndar
i ya
Man
gapw
ani
4,00
0,00
0-
xvi)
Uim
aris
haji
wa
Mae
neo
Hur
u M
iche
wen
i Pem
ba1,
800,
000
1,80
0,00
0
xvii)
Mae
ndel
eo y
a Ki
limo
na U
vuvi
IFAD
2,14
1,19
8
2,
141,
198
xv
iii) K
udhi
biti
Nzi
wa
Mat
unda
100,
000
IITA
120,
000
22
0,00
0
JU
MLA
YA
KR
A11
0,93
0,00
0
85
,950
,000
-
29,3
23,4
00
222,
376,
104
33
7,64
9,50
4
PRO
GR
AMU
Prog
ram
u ya
Ajir
a kw
a Vi
jana
2,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Jin
sia
-
i)
Usa
wa
wa
Kijin
sia
na K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en18
0,00
0
180,
000
ii) M
radi
wa
Kijin
sia
UN
FPA
470,
628
47
0,62
8
M
IRAD
Ii)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a Am
ali -
Aw
amu
ya P
ili1,
000,
000
-
ii) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ku
lea
na K
utot
olea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
1,00
0,00
01,
000,
000
JU
MLA
YA
KR
A3,
600,
000
3,00
0,00
065
0,62
80
3,65
0,62
8
KR
A B:
KU
KU
ZA U
WEZ
O W
A W
ATU
Page
2 o
f 5
85Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MU
HIS
ANI
RU
ZUK
U M
KO
PO
JIN
A LA
PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
19/2
020
SMZ
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
021
SMZ
MC
HAN
GO
WA
MU
HIS
ANI
JU
MLA
YA
BAJE
TI
PRO
GR
AMU
Prog
ram
u ya
Uku
zaji
Uch
umi J
umui
shi Z
anzi
bar (
BIG
- Z)
WB
19,9
64,0
00
19
,964
,000
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
alar
ia Z
anzi
bar
248,
000
248,
000
PM
I/GF
5,58
6,36
5
5,
834,
365
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
uind
ombi
nu y
a Af
ya-
i) Ku
ipan
dish
a ha
dhi H
ospi
tali
ya M
nazi
Mm
oja
2,65
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
ii) K
uzip
andi
sha
Had
hi h
ospi
tali
za W
ilaya
na
Hos
pita
li za
Vijij
4,25
0,00
05,
000,
000
5,00
0,00
0
iii) A
wam
u ya
Kw
anza
ya
ujen
zi w
a H
ospi
tali
ya R
ufaa
Bin
guni
6,50
0,00
06,
000,
000
6,00
0,00
0
iv) U
jenz
i wa
Boha
ri Ku
u ya
Daw
a-Pe
mba
1,00
0,00
02,
000,
000
2,00
0,00
0
v) U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mam
laka
ya
Daw
a na
Vip
odoz
i1,
000,
000
2,10
0,00
02,
100,
000
vi
) Uje
nzi w
a H
ospi
tal y
a W
agon
jwa
wa
Akili
1,30
0,00
01,
400,
000
Hop
elan
d U
n1,
400,
000
2,80
0,00
0
vii)
Kuim
aris
ha T
aasi
si y
a U
tafit
i wa
Afya
2,00
0,00
02,
000,
000
Prog
ram
u ya
Shi
rikis
hi y
a Af
ya y
a U
zazi
wa
Mam
a na
Mto
to70
0,00
050
0,00
0U
NFP
A/ W
HO
/G
F9,
574,
372
10,0
74,3
72
Pr
ogra
mu
ya K
udhi
biti
Mar
adhi
ya
UK
IMW
I, H
oma
ya In
i, K
ifua
Kik
uu n
a U
kom
a24
8,00
024
8,00
0G
F/TH
PS5,
090,
362
5,33
8,36
2
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i2,
948,
000
-
Pr
ogra
mu
ya U
sam
baza
ji M
aji V
ijijn
i3,
863,
000
-
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a El
imu
1,50
0,00
01,
000,
000
1,00
0,00
0
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u1,
110,
000
1,00
0,00
0M
ILEL
E/ G
PE/
PCD
2,89
6,23
0
3,
896,
230
M
IRAD
I-
i) Ku
jeng
a U
wez
o w
a Ku
kabi
liana
na
Maa
faU
ND
P18
6,00
0
186,
000
ii) U
imar
isha
ji w
a El
imu
ya M
aand
aliz
iG
PE/ M
ILEL
E/
SID
A3,
253,
333
3,25
3,33
3
ii) U
imar
isha
ji w
a El
imu
ya M
sing
i
GPE
/SID
A/
UN
ICEF
/ U
SAID
/ PC
D/O
FID
/M
ZF/W
B25
2,23
015
0,00
040
2,23
0
iii) U
imar
isha
ji w
a El
imu
ya L
azim
a3,
300,
000
3,50
0,00
0
BAD
EA/ O
PEC
/ KO
REA
/WB/
M
ZF2,
821,
521
8,48
5,00
014
,806
,521
iv) K
uend
elez
a Vi
sim
a vy
a R
as e
l Kha
imah
4,00
0,00
04,
000,
000
v) U
huis
haji
na U
imar
isha
ji w
a M
fum
o w
a U
sam
baza
ji M
aji Z
anzi
bar
466,
220
IND
IA67
,129
,316
67,5
95,5
36
vi
) Usa
mba
zaji
Um
eme
Vijij
ini
650,
700
500,
000
500,
000
vii)
Zanz
ibar
Ene
rgy
Sect
or T
rans
form
atio
n Pr
ojec
t (ZE
ST)
WB
17,8
50,0
00
17
,850
,000
KR
A C
: KU
TOA
HU
DU
MA
BOR
A K
WA
WO
TE
Page
3 o
f 5
86Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MU
HIS
ANI
RU
ZUK
U M
KO
PO
JIN
A LA
PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
19/2
020
SMZ
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
021
SMZ
MC
HAN
GO
WA
MU
HIS
ANI
JU
MLA
YA
BAJE
TI
viii)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
arN
OR
AD3,
500,
000
3,50
0,00
0
ix) U
hifa
dhi H
aki z
a W
atot
oU
NIC
EF38
7,52
3
387,
523
x) H
ifadh
i ya
Jam
iiU
NIC
EF12
1,00
0
121,
000
xi) K
uim
aris
ha H
udum
a za
Uza
mia
ji na
Uok
ozi
2,90
0,00
04,
800,
000
4,80
0,00
0
xii) U
jenz
i wa
Viw
anja
vya
Mic
hezo
vya
Wila
ya2,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
xii
i) U
jenz
i wa
Skul
i ya
Seko
ndar
i na
Ufu
ndi -
Mto
ni3,
000,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
xiv
) Uim
aris
haji
wa
Taar
ifa n
a U
sala
ma
wa
Mfu
mo
wa
Usa
jili1,
000,
000
1,00
0,00
01,
000,
000
xv
) Hifa
dhi y
a W
azee
400,
000
1,10
0,00
01,
100,
000
JU
MLA
YA
KR
A40
,567
,700
43,3
62,2
20
35
,068
,935
11
3,57
8,31
6
192,
009,
471
MIR
ADI
i) Ku
imar
isha
Usi
mam
izi w
a M
azin
gira
, M
alia
sili
na M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i-Zan
ziba
r30
0,00
030
0,00
0U
ND
P28
9,80
0
589,
800
JUM
LA Y
A K
RA
350,
000
300,
000
965,
712
01,
265,
712
PRO
GR
AMU
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a Af
isi z
a Se
rikal
i Za
nzib
ar10
,002
,300
19,5
00,0
0019
,500
,000
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a M
iji M
ipya
20,0
00,0
0020
,000
,000
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha30
0,00
0-
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
NO
RW
AY1,
639,
026
1,63
9,02
6
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Utu
mis
hi w
a U
mm
a - I
I20
0,00
040
0,00
0W
B40
0,00
0
M
IRAD
Ii)
Uim
aris
haji
Nyu
mba
za
Vion
gozi
na
Nyu
mba
za
Serik
ali
2,00
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
ii) U
wek
aji K
amer
a na
Vifa
a vy
a U
linzi
7,00
0,00
08,
000,
000
8,00
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bora
Aw
amu
ya T
atu
100,
000
-
iv
) Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a Af
ya y
a U
zazi
, Ji
nsia
na
Kupu
nguz
a U
mas
ikin
iU
NFP
A28
6,00
0
286,
000
v) U
imar
isha
ji w
a R
asilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi w
a M
alia
sili
50,0
0010
0,00
0Af
DB
4,54
1,00
0
4,
641,
000
vi
) Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a Pi
li w
a R
ais
350,
000
-
vi
i) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a Ka
mbi
na
Nyu
mba
za
KMKM
1,00
0,00
070
0,00
070
0,00
0
vi
ii) U
jenz
i wa
Nyu
mba
za
Mak
aazi
na
Mah
anga
za
Kiko
si c
ha
Maf
unzo
1,00
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
ix) M
radi
wa
Kuje
nga
Uw
ezo
Taas
isi z
a Se
rikal
i50
,000
20,0
00U
ND
P10
6,82
6
126,
826
x) U
ratib
u na
Usi
mam
izi w
a M
alen
go n
a M
aend
eleo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KUZA
III
20,0
00
100,
000
UN
DP
801,
150
90
1,15
0
xi)
Uje
nzi w
a O
fisi y
a ZA
ECA
800,
000
1,00
0,00
01,
000,
000
KR
A D
: KU
WEP
O M
AZIN
GIR
A EN
DEL
EVU
NA
UH
IMIL
I WA
MAB
ADIL
IKO
YA
TABI
A N
CH
I
KR
A E:
KU
SHIK
AMAN
A N
A M
ISIN
GI Y
A U
TAW
ALA
BOR
A
Page
4 o
f 5
87Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
MU
HIS
ANI
RU
ZUK
U M
KO
PO
JIN
A LA
PR
OG
RAM
U/M
RAD
I
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
19/2
020
SMZ
MAK
ISIO
KW
A M
WAK
A 20
20/2
021
SMZ
MC
HAN
GO
WA
MU
HIS
ANI
JU
MLA
YA
BAJE
TI
xii) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Kiko
si c
ha V
alan
tia50
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
xiii)
Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a Ka
mbi
za
JKU
500,
000
2,00
0,00
02,
000,
000
xv
i) U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i wa
KZU
500,
000
2,50
0,00
02,
500,
000
xv
) Uje
nzi w
a Ki
tuo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a68
0,00
01,
900,
000
1,90
0,00
0
xvi)
Usi
mam
izi w
a U
patik
anaj
i wa
Hak
i40
0,00
01,
500,
000
1,50
0,00
0
xvii)
Uje
nzi w
a Je
ngo
la O
fisi n
a St
udio
za
Red
io M
kanj
uni -
Pem
ba1,
500,
000
1,40
0,00
01,
400,
000
xv
iii) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a M
afun
zo y
a Sh
eria
na
Uta
fiti
600,
000
600,
000
xix)
Uen
dele
zaji
wa
Takw
imu
Zanz
ibar
(ZSD
P)U
N- W
OM
EN/
ADB/
EU/
UN
ICEF
/ U
NFP
A3,
321,
700
3,32
1,70
0
xx) M
tand
ao w
a U
ingi
zaji
wa
Taar
ifa z
a Ba
jeti
500,
000
500,
000
JUM
LA Y
A K
RA
26,9
52,3
0064
,720
,000
6,15
4,70
24,
541,
000
75,4
15,7
02JU
MLA
KU
BWA
182,
400,
000
197,
332,
220
72,1
63,3
7834
0,49
5,42
060
9,99
1,01
8JU
MLA
YA
FED
HA
ZA W
AHIS
ANI
412,
658,
798
Page
5 o
f 5
88Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
KIFUNGU JINA LA PROGRAMU/MRADI MAKISIO KWA
MWAKA 2019/20 SMZ
MAKISIO KWA MWAKA 2020/21
SMZ
i) Ujenzi wa Nyumba ya Makamu wa Pili wa Rais 350,000 JUMLA YA FUNGU 350,000 -
Programu ya Upatikanaji Rasilimali Fedha 300,000JUMLA YA FUNGU 300,000 0
Programu ya Kuimarisha Uvuvii) Uimarishaji Uvuvi wa Bahari Kuu 1,400,000 2,000,000
JUMLA YA FUNGU 1,400,000 2,000,000
i) Kuimarisha Taasisi ya Viwango Zanzibar 2,000,000 3,000,000JUMLA YA FUNGU 2,000,000 3,000,000
i) Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali - Awamu ya Pili 1,000,000
JUMLA YA FUNGU 1,000,000 0
Programu ya Kuimarisha Miundombinu ya Afyai) Ujenzi wa Hospital ya Rufaa Binguni (Awamu ya Kwanza) 6,000,000 6,000,000
JUMLA YA FUNGU 6,000,000 6,000,000
i) Kuendeleza Visima vya Ras el Khaimah 3,000,000 2,000,000ii) Usambazaji Umeme Vijijini 650,000 500,000
JUMLA YA FUNGU 3,650,000 2,500,000
Programu ya Ujenzi wa Barabarai) Ujenzi wa Barabara ya Chake Chake-Wete 1,000,000ii) Ujenzi wa Barabara za Ole- Kengeja 5,600,000iii) Ujenzi wa Daraja la Uzi-Ng'ambwa 5,000,000Mradii) Ununuzi wa Land Craft 1,900,000 2,400,000
JUMLA YA FUNGU 8,500,000 7,400,000
Ujenzi wa Ofisi ya ZAECA 800,000 1,000,000JUMLA YA FUNGU 800,000 1,000,000
Kuimarisha Utalii kwa Wote 1,500,000 2,000,000JUMLA YA FUNGU 1,500,000 2,000,000
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
WIZARA YA AFYA
WIZARA YA ARDHI, NYUMBA, MAJI NA NISHATI
WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI
MAMLAKA YA KUZUIA RUSHWA NA UHUJUMU WA UCHUMI
KAMISHENI YA UTALII
WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA
Kiambatisho namba 3: PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO CHINI YA MFUKO WA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE
FUND) TZS "000"
OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS
WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
C01
F01
L01
R01
K01
H01
N01
P01
G07
J02
Page 1 of 2
89Mwelekeo wa Uchumi 2020 na Mpango wa Maendeleo 2020/21
KIFUNGU JINA LA PROGRAMU/MRADI MAKISIO KWA
MWAKA 2019/20 SMZ
MAKISIO KWA MWAKA 2020/21
SMZ
Ujenzi wa Viwanja vya Michezo vya Wilaya 2,000,000 2,500,000JUMLA YA FUNGU 2,000,000 2,500,000
i) Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi 7,000,000 8,000,000ii) Ujenzi wa Kiwanda cha Ushoni (ZQTL) 3,600,000 1,400,000
JUMLA YA FUNGU 10,600,000 9,400,000
i) Ujenzi wa Skuli ya Sekondari na Ufundi - Mtoni 2,000,000 JUMLA YA FUNGU 0 2,000,000
i) Kuimarisha Huduma za Uzamiaji na Uokozi 2,900,000 4,800,000 JUMLA YA FUNGU 2,900,000 4,800,000
i) Ununuzi wa Vifaa vya Zimamoto 1,600,000 JUMLA YA FUNGU 0 1,600,000
JUMLA KUBWA 41,000,000 44,200,000
WIZARA YA VIJANA, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ
KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOZI
KIKOSI MAALUM CHA KUZUIA MAGENDO (KMKM)
JESHI LA KUJENGA UCHUMI
D05
S01
D01
D02
D04
Page 2 of 2