14

MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

  • Upload
    others

  • View
    5

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za
Page 2: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

2

Kiini cha mradi huu ni kusaidia waumini katika Bonde la

Witzenberg kutimiza utume Wake hapa duniani. Tunapata

kusudi letu katika utume Wake na tunataka maisha yetu

kuonyesha Ufalme Wake hapa duniani.

Sisi ni mtandao tunaoshirikiana na kuendeshwa na maono,

maadili na utamaduni wa Ufalme. Mtandao wa Viongozi

waliojitolea sana hasa kuwa wa mfano, kuwa tayari kuongoza

kutoka nyuma ama kwa kuwa mstari wa mbele. Washirika

wenye nguvu ambao wanapatika kuitumikia jamii.

Tunatumia wakati pamoja katika kushirikishana uzoefu tukiwa

na lengo la kuona kila nyumba kwenye Bonde la Witzenberg

ina Bibilia. Kwa pamoja tunaonyesha jinsi ya kuishi Injili kupitia

kufanya wanafunzi kamili.

Mtandao unakubali utofauti wa miaka, jinsia, tamaduni, karama

huku ukipunguza utumiaji wa majina, haswa majina ambayo

hulisha egos zetu.

Tuna ndoto ya kuona timu toka tamaduni mbalimbali zinaleta

mabadiliko katika jamii zetu.

MUHTASARI WA MRADI

Page 3: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

3

Maono ni kuona Biblia ndani ya kila nyumba katika Bonde

la Witzenberg pamoja na timu ya watu wa tamaduni tofauti

tofauti zinazoonyesha jinsi ya kuishi Injili kupitia kufanya

wanafunzi kamili.

Ndoto ni kuona viongozi wenyeji katika Bonde la

Witzenberg wanachukua hatua za kimkakati na kukomboa

utamaduni katika muktadha wao kwa kutumia kanuni za

Ufalme.

Jukumu letu ni kuhudumia na kutoa mafunzo ya

kuwawezesha viongozi wenyeji ili kupanua Ufalme katika

jamii zao.

MAONO

Page 4: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

4

JINSI YA KUSHIRIKI

OMBA NENDA TOA

Page 5: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

5

OMBA "Tuma watendakazi katika shamba lako la mavuno." - Mathayo 9:38

Ni maombi rahisi lakini yana nguvu katika kujenga Ufalme wa Mungu. Tunamtumaini Mungu kuona

mtandao wa maombi wa watu 1000 wakiomba kila wiki kwa ajili ya watendakazi zaidi kwenda

kushirikisha Habari Njema katika Bonde la Witzenberg.

Weka kengele/alamu yako saa 9:38 kila siku asubuhi / jioni na uombe kama vile Bwana alivyotuamuru

katika Mathayo 9:38.

NENDA Nenda na ushirikishe jinsi ya kuishi maisha mapya kupitia Biblia katika jamii yako.

Maono ni kuona Biblia kwenye kila nyumba katika mkoa wa Witzenberg (Biblia 40,000) na kuonesha jinsi

ya kuishi Injili kupitia kufanya wanafunzi kamili. Baba na Mwanawe pamoja na Roho wanaota juu ya

ulimwengu uliobadilishwa — ulimwengu huu sisi tunaoishi, sio tu ujayo. Je! Hii itatokeaje? Hapa kuna

agizo: Fanye wanafunzi! Fanya wanafunzi, watu ambao wameamrisha maisha yao karibu na matakwa ya

Muumba.

TOA Washirika wa rasilimali ni watu ambao hushiriki fedha zao, muda, na ujuzi ili kuwezesha huduma kutokea. Washirika wa rasilimali wanataka kualikwa kuwa sehemu ya kile Mungu anafanya kupitia mradi huu. Inakuwa ushirikiano wa familia katika Ufalme wa Mungu na uhusiano uliojengwa juu ya uaminifu, heshima, na uaminifu.

Page 6: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

6

Maombi yalichukua jukumu kubwa katika maisha ya wanafunzi wa Yesu katika

Kanisa la kwanza.Watu walimwomba Mungu mwongozo katika maombi. Maombi

ni njia ya kupokea uelewa na mwelekeo wa nini cha kufanya, jinsi ya kufanya, na

wapi pa kwenda.

MAOMBI &

ROHO

MTAKATIFU

Wakati ambapo ugunduzi binafsi wa Bibilia unasababisha utii, uanafunzi hufanyika

na kuleta kukua kwa jamii ya waaminio wenye utiifu katika kujitolea kutoa muda

wao, karama/vipawa, mali na maisha na wengine (2 Wakorintho 5: 14-19, Matendo

2: 42-47) . Onyesha maisha mapya mazuri tunayoshiriki ambayo yatadumu milele.

Ushiriki wa Biblia ni wito wa kukusudia kugundua Neno la Mungu ili kuondoka,

'kutomjua Mungu' hadi 'kumpenda na kumtii kupitia Yesu.

UGUNDUZI

BINAFSI WA

MAANDIKO

Kupitia utii wa amri za Mungu, tunaelezea utegemezi wetu kwake na tunakubali

hekima yake juu yetu. Kuwa mwanafunzi ni kuwa unakua katika utii wako kwa yote

ambayo Yesu aliamuru. Usisome tu vifungu; watekeleze kwa vitendo. Utii ndio

lengo! Kuhama kutoka kwa maarifa yaliyolenga (uhamishaji wa yaliyomo) hadi utii

uliozingatia (uzoefu wa mabadiliko).

UTIIFU WA

MARA MOJA

MOYO WA MRADI

Page 7: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

7

Tunaishi kama watu waliotumwa kuwajenga wengine kwa Neno la Mungu na

kuzidisha wafanya wanafunzi kwa kupitia mfano wa sisi wenyewe. Tunaendelea

kuzingatia kufundisha kizazi kijacho cha viongozi. Kila kitu ambacho Mungu

huumba - mimea, wanyama, na watu - imeubwa kujizidisha. Mungu aliwabariki

watu wa kwanza kuongezeka na kuijaza nchi. Kuzidisha kupo katikati kiini cha

moyo wa Mungu tangu mwanzo wa uumbaji wa ulimwengu hadi picha ya siku

zijazo katika kitabu cha Ufunuo.

Tunapaswa kurahisisha ikiwa tunataka kuzidisha. Hatuhitaji majengo,

wafanyikazi, mipango au bajeti kubwa kumpenda Mungu, wengine na kufanya

wanafunzi ambao hufanya wanafunzi. Hatulaani vitu hivi, Mungu ametumia na

labda ataendelea kuvitumia. Vitu vimebadilika sana katika modeli kwa sababu ya

janga la covid-19. Jambo kuu katika kurahisisha ni kutafuta Ufalme wa Mungu na

haki ya ufalme wake kwanza halafu kila kitu muhimu kitakuja kwa mpangilio wake

sahihi. (Mathayo 6: 25-33) Kurahisisha hutuweka huru kupokea utoaji wa Mungu

kama zawadi ambayo sio yetu kutunza na inaweza kugawanywa kwa wengine

kwa uhuru.

UWAJIBIKAJI Mungu humwajibisha kila mmoja wetu kulingana na mwitikio wetu wa kweli ya

neno la Mungu. Jukumu letu ni kuhakikisha kila mtu anayo nafasi ya kusoma na

kutii kweli mwenyewe.

ZIDISHA

RAHISISHA

Page 8: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

8

Uhamasishaji wa maombi (Mathayo 9:38). "Tuma watendakazi katika shamba lako la mavuno."

Maombi rahisi kama haya lakini yenye nguvu katika kujenga Ufalme wa Mungu. Tunamtumaini Mungu

kuona mtandao wa maombi wa watu 1000 wakiomba kila wiki kwa ajili ya watendakazi zaidi kwenda

kuleta mavuno yake. Weka kengele ya simu yako saa 9:38 asubuhi / jioni kila siku na uombe kama vile

Bwana alituamuru tufanye katika Mathayo 9:38.

Mafunzo, kutendea kazi mafunzo, na ushauri. Mafunzo, kufundisha, na ushauri ni kiini cha kuchochea

mabadiliko katika jamii na mwishowe mataifa. Harakati za mabadiliko huishi kwa ushauri mzuri na

ufundishaji. Kiini cha njia hii ni kuishi Injili na haipaswi kutazamwa kama programu ya mara moja au kozi

ya mafunzo, lakini kama safari ya kubadilisha maisha ya kuamuru ulimwengu wetu mara kwa mara, wa

ndani na wa nje, karibu na mawazo na matakwa ya Baba yetu wa mbinguni. Kuwa mwanafunzi ni kuwa

unakua katika utii wako kwa yote ambayo Yesu aliamuru.

Washirika wa Rasilimali / Kukuza Msaada. Washirika wa rasilimali ni watu ambao hushiriki fedha zao,

wakati, ujuzi, na sala ili kuwezesha huduma kutokea. Washirika wa rasilimali wanataka kualikwa kuwa

sehemu ya kile Mungu anafanya kupitia mradi huu. Inakuwa ushirikiano wa familia mbili katika Ufalme wa

Mungu na uhusiano uliojengwa juu ya uaminifu, heshima, na uaminifu. Sisi ni washirika wa Injili.

JINSI TUNAVYOFANYA

Page 9: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

9

Uhamasishaji

wa maombi

Mafunzo,

kutendea kazi

mafunzo, na

ushauri.

Uanafunzi

Washirika wa

Rasilimali /

Kukuza

Msaada.

Ndoto ni kuona

viongozi wenyeji

katika

Bonde la

Witzenberg

wanachukua hatua

za kimkakati na

kukomboa

utamaduni katika

muktadha wao

kwa kutumia

kanuni za Ufalme.

Jukumu letu ni

kuhudumia na

kutoa mafunzo ya

kuwawezesha

viongozi wenyeji

ili kupanua Ufalme

katika jamii zao.

Kiini cha mradi huu ni kusaidia

waumini katika Bonde la

Witzenberg kutimiza utume Wake

hapa duniani. Tunapata kusudi letu

katika utume Wake na tunataka

maisha yetu kuonyesha Ufalme

Wake hapa duniani.

MUHTASARI WA MRADI

Page 10: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

10

Jiunge na moja ya timu nane zinazofanya kazi ili kuchochea hoja ya ufalme katika mkoa wetu

kwa lengo la kuipatia kila kaya fursa ya kusoma na kutii ukweli wao wenyewe.

WhatsApp to 071 594 1539.

TIMU MBALIMBALI

Page 11: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

11

Injili inatakiwa kushikwa na wala sio

kufundishwi tu kwa hiyo tunahimiza sana

kupata uzoefu kwa vitendo, pamoja,

ambapo tunatumia mara moja kile

tunachogundua kutoka kwenye Bibilia.

Tunafanya hivyo kwa kufanya matukio

ya mafunzo katika jamii tofauti ambayo

huimarisha uzoefu wa mafunzo. Matukio

ya mafunzo msingi wake ni timu kwa

sababu tunaamini kwamba ukamilifu wa

Mungu unaweza kupatikana tu katika

umati wa watu tofauti. Ni muhimu

kuzingatia kwamba kunatofauti kubwa

kati ya ufundishaji na mafunzo.

Mafundisho mengi yanajulisha wakati mafunzo huandaa na hubadirisha. Hatujaribu tu

kufundisha yaliyomo. Tunataka kufundisha washiriki kuishi kama wanafunzi ambao hufanya

wanfunzi katika maisha ya kila siku

KWENYE MAFUNZO YA KWENDA

Page 12: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

12

OMBA

Maombi ndio mahali pa kuanzia katika yote tunayofanya. Kwa maombi tunahitaji kumwomba Mungu

atufunulie utume Wake na atusaidie kuelewa na kutii Neno Lake. Katika maeneo ambayo Injili haijawahi

kutangazwa, au ambapo mifumo ya imani za jadi zimetawala kwa muda mwingi, maeneo ambayo sio

jambo la kushangaza kwa wale wanaohusika katika shughuli za kufanya wanafunzi wakabiliwa na

mashambulizi ya kiroho kuanzia ya kukasirisha hadi ya kutishia maisha ( Waefeso 6:12, Mathayo 10: 16-

23). Ili kupenya, tunahitaji kuanza maombi ya kimkakati ili kumpinga adui.

OMBA

ZIDISHA UNGANA

TAFUTA KUGUNDUA

MZUNGUKO WA KUFANYA WANAFUNZI Mzunguko wa kufanya wanafunzi ni njia rahisi, inayoweza kurudiwa ya kumchukua mtu yeyote kwenye

uhusiano wa kumfanya mwanafunzi na kumwonesha jinsi ya kuungana na Mungu kupitia kusoma, kutii,

na kushirikisha wengine Biblia. Njia hii yenye asili ya kujirudia inaiokoa injili kutoka tamaduni za jadi/

mapokeo na kuiruhusu Injili kuendelea bila vizuizi kwa kupitia mahusiano mbalimbali katika jamii

Page 13: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

13

TAFUTA

UNGANA

Maombi ndio mahali pa kuanzia katika yote tunayofanya. Kwa maombi tunahitaji kumwomba Mungu

atufunulie utume Wake na atusaidie kuelewa na kutii Neno Lake. Katika maeneo ambayo Injili haijawahi

kutangazwa, au ambapo mifumo ya imani za jadi zimetawala kwa muda mwingi, maeneo ambayo sio

jambo la kushangaza kwa wale wanaohusika katika shughuli za kufanya wanafunzi wakabiliwa na

mashambulizi ya kiroho kuanzia ya kukasirisha hadi ya kutishia maisha ( Waefeso 6:12, Mathayo 10: 16-

23). Ili kupenya, tunahitaji kuanza maombi ya kimkakati ili kumpinga adui.

KUGUNDUA

Tafuta udongo mzuri. Kila mtu ameumbwa kumpenda Mungu na kupenda watu (Mathayo 22: 36-40), na

pia kumaliza kazi ya kufanya wanafunzi (Mathayo 28: 18-20). Sio kila mtu anaitikia Injili kwa wakati

mmoja na kwa njia ile ile, kwani ni Baba ambaye huwavuta watu kwa Yesu (Yohana 6: 44-45). Tunahitaji

kupata watu wa amani na kutangaza Injili katika kila fursa inayoongozwa na Roho.

Ushiriki wa Biblia ni wito wa kukusudia kugundua Neno la Mungu ili kutoka, 'kutomjua Mungu' kwenda

'kumpenda na kumtii kupitia Yesu' Wakati ugunduzi wa kibinafsi wa Biblia unasababisha utii, uanafunzi

hufanyika ambapo tunakua katika jamii ya watiifu. waumini ambao wamejitolea kutoa muda wao, vipawa,

mali na maisha na wengine (2 Wakorintho 5: 14-19, Matendo 2: 42-47). Onyesha maisha mapya mazuri

tunayoshiriki ambayo yatadumu milele.

ZIDISHA

Tunaishi kama watu waliotumwa kuwajenga wengine kwa Neno la Mungu na kuzidisha wafanya

wanafunzi kwa kupitia mfano wa sisi wenyewe. Tunaendelea kuzingatia kufundisha kizazi kijacho cha

viongozi.

Page 14: MUHTASARI WA MRADI - thegoproject.co.za

14