290
Majukumu na Baraka za Ukuhani Kitabu cha Msingi cha Mwongozo kwa wenye ukuhani, Sehemu ya A

Wajibu na Baraka za Ukuhani

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Majukumu na Baraka za Ukuhani

Kitabu cha Msingi cha Mwongozo kwa wenye ukuhani, Sehemu ya A

Page 2: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Majukumu na Baraka za Ukuhani

Kitabu cha Msingi cha Mwongozo kwa wenye ukuhani, Sehemu ya A

Kimetolewa na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho

Jiji la Salt Lake, Utah

Page 3: Wajibu na Baraka za Ukuhani

© 1999 na Intellectual Reserve, Inc.

Haki zote zimehifadhiwa

Kiingereza kiliidhinishwa: 9/96

Tafsiri iliidhinishwa: 9/96

Tafsiri ya Duties and Blessings of the Priesthood Holders:Basic Manual for the Priesthood Holders, Part A

Swahili

Page 4: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Yaliyomo

Utangulizi........................................................................................................vHusisha Washiriki Walemavu........................................................................vii

Historia na Muundo wa Ukuhani1. Ukuhani ....................................................................................................12. Ukuhani kutoka Adamu mpaka Urejesho................................................83. Urejesho wa Ukuhani.............................................................................154. Jamii la Ukuhani.....................................................................................235. Kazi za Shemasi ....................................................................................306. Kazi za Mwalimu ....................................................................................397. Kazi za Kuhani .......................................................................................478. Kazi za Maaskofu na Maraisi wa Matawi...............................................569. Kazi za Mzee na Kuhani Mkuu ..............................................................61

10. Baba Mkuu na Baraka za Baba Mkuu...................................................6711. Umuhimu wa Viongozi Wakuu...............................................................75

Wajibu Binafsi na wa Kifamilia12. Wajibu wa Baba kwa Usitawi wa Familia Yake..........................................8313. Kushauriana na Jamii ............................................................................9014. Kuongoza Sala la Familia ......................................................................9715. Nyumba: Kituo cha Mafunzo ya Injili ...................................................10316. Kujitayarisha Kufundisha .....................................................................11017. Kufundisha Kutoka Kwenye Maandiko Matakatifu ..............................11918. Kufundisha kwa Nguvu za Roho Mtakatifu..........................................12719. Kufundisha Adabu na Maadili Mema Nyumbani.................................13320. Kutatua Matatizo ya Kifamilia kwa Amani ...............................................14021. Utunzaji wa Fedha za Familia..............................................................14722. Uzalishaji wa Nyumbani na Hifadhi .....................................................15423. Kusitawisha na Kuendeleza Ujuzi wa Kazi ..........................................16224. Kuweka Miili Yetu Katika Hali ya Afya Bora .........................................17125. Kuitumikia Jumuiya na Nchi ................................................................178

Kanuni za Injili na Mafundisho26. Ushuhuda wa Injili ya Yesu Kristo........................................................18527. Imani Katika Yesu Kristo ......................................................................19028. Toba.....................................................................................................199

iii

Page 5: Wajibu na Baraka za Ukuhani

29. Ubatizo, Agano la Kudumu..................................................................20630. Kipawa cha Roho Mtakatifu.................................................................21431. Maombi na Kufunga ............................................................................22132. Unyenyekevu .......................................................................................22733. Upendo na Utumishi............................................................................23334. Usafi wa Maadili...................................................................................24035. Familia ya Milele ..................................................................................245

Dondoo za Marejeo ...................................................................................253Kielelezo.....................................................................................................255Mahekalu na Majengo ...............................................................................264

iv

Page 6: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Utangulizi

Mpangilio wa SomoMasomo haya ya ukuhani yametungwa ili kutumika kwa wenye ukuhani waHaruni na Melkizedeki. Katika matawi madogo yenye upungufu wa idadi yawenye ukuhani, washiriki wa darasa watahitajika kukutana katika kikundikimoja. Palipo na idadi kubwa ya wenye ukuhani na nafasi ikiruhusu,mwalimu anaweza kupenda kugawanya madarasa katika viwango vya umriunaolingana na washiriki ili masomo yaweze kurekebishwa ili kukabilianana mahitaji ya makundi tofauti ya umri.

Mafunzo ya KibinafsiMasomo haya ya mafunzo kimsingi yameandikwa kwa ajili ya mtu binafsi.Kwa hivyo, kila mwenye ukuhani inampasa kusoma kitabu hiki katikati yawiki na kuja darasani na kitabu chake cha mwongozo pamoja na vitabuvya maandiko matakatifu akiwa tayari kujadili somo. Njia nzuri ambayomwalimu anaweza kuwatia moyo katika matayarisho haya ni kuwaombawashiriki wachache wa darasa wasome mapema na kujitayarisha kujadilikuhusu somo hilo darasani. Ni muhimu kwamba kila mtu alete vitabu vyakevya maandiko matakatifu darasani, na mwalimu anaweza kuendeleakuwakumbusha wana kikundi cha wenye ukuhani kuleta maandikomatakatifu mara kwa mara mpaka wazoee desturi hivyo.

Misaada kwa MwalimuMisaada kwa mwalimu inapatikana katika hiki kitabu na huonekana katikamaandishi ya chapa ndogo ndani ya kila somo. Misaada hii ina maswaliambayo mwalimu anaweza kuuliza, mapendekezo kwa ushiriki wa darasa,na mashauri ya kutumia picha na chati. Walimu wanaotumia kitabu hikiwanaweza kutaka kutumia mbinu nyingine au njia nyingine ya kufundishiawanayoona inafaa kama nyongeza ya kujadili maswali na mbinuzilizopendekezwa. Karibu kila somo linahitaji matumizi ya ubao, kwa hivyowalimu wanafaa waandae ubao na chaki darasani katika kila somo. (Vingikati ya vielelezo vya kufundishia vilivyopendekezwa kutumiwa kama chativyaweza kuwekwa ubaoni.)

Idadi ya MasomoMasomo thelathini na matano yametayarishwa, na kuacha nafasi kadhaawazi za mafunzo ambayo viongozi wanaweza kujadili kuhusu mawazo na

v

Page 7: Wajibu na Baraka za Ukuhani

hoja ambazo wanaamini zinahitajika kujadili katika vikundi maalumu vyaukuhani. Muda huu wa ziada unaweza kutumika kwa—

1. Kujadili na kupanga shughuli au miradi au mambo mahususi kamayanavyoelekezwa na viongozi wa ukuhani.

2. Kujadili taarifa za Viongozi Wakuu zilizotolewa katika mkutano mkuukama vile ilivyochapishwa katika magazeti ya kimataifa au Ensign.

3. Tumia zaidi ya wiki moja kwenye mambo yale yanayohitaji mafunzozaidi.

4. Tumia muda kama vile Roho wa Bwana anavyokuongoza kwa manufaaya wenye ukuhani.

vi

Page 8: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Husisha Washiriki WalemavuWakati wa huduma yake hapa duniani, Yesu alienda juu kwenye mlimakaribu na Bahari ya Galilaya.

“Na umati mkubwa ulikuja kwake, wakiwemo nao wale waliokuwa vilema,vipofu, visiwi, viwete na wengineo wakitupwa mbele ya Yesu naaliwaponya:

“Kwa jinsi ambayo umati ulistaajabu, walipoona mabubu wanaongea,viwete wamekuwa wazima, vilema wakitembea na vipofu kuona: Nawalimtukuza Mungu wa Israeli” (Mathayo 15:30–31).

Mwokozi alitoa mfano kwetu katika kuonyesha huruma kwa wale walio naupungufu. Alipowatembelea Wanefi baada ya ufufuko wake alisema:

“Tazama, moyo wangu umejawa na huruma juu yenu.

“Kuna wagonjwa wowote kati yenu? Waleteni hapa. Mnao walio vilema, auvipofu, wanaochechemea au viwete au wenye ukoma au wale waliofifia auwalio mabubu au walioteseka kwa njia yoyote? Waleteni hapa naminitawaponya kwa vile nina huruma juu yao; moyo wangu umejawa narehema” (3 Nefi 17:6–7).

Mwalimu katika Kanisa yuko kwenye nafasi nzuri ya kuonyesha hurumakwa mshiriki mlemavu. Inampasa afahamu na atamani kuwahusishawashiriki hawa kwenye shughuli za kujifunza darasani. Washiriki wa darasawalio na ulemavu wa aina yoyote wanahitaji uangalifu maalumu:Mwongozo ufuatao waweza kuwasaidia walimu kuwasaidia washiriki wenyemahitaji maalumu:

• Jua mahitaji na uwezo wa kila mshiriki wa darasa.

• Wahoji mapema washiriki wa darasa walio walemavu kabla ya kuwaitakusoma, kusali au vinginevyo. Uliza maswali kama, “Unajisikia namnagani kuhusu kusoma darasani?” “Je! unaweza kutoa sala kwenyeumati?”

• Wahoji viongozi wa ukuhani, wana familia na kama inafaa, na washirikiwalemavu wenyewe ili upate kujua mahitaji yao maalumu.

• Jaribu kuongeza na kuboresha ushiriki na kujifunza kwa washiriki waliona ulemavu.

• Hakikisha kwamba kila mshiriki wa darasa anatoa heshima na uelewanokwa kila mshiriki mwingine wa darasa.

• Kuwa mwema na mwenye upendo. Kila mwana wa Mungu ana haja yaupendo wa kawaida na maelewano hata kama anao au hana ulemavu.

vii

Page 9: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Walimu katika Kanisa lazima wakumbuke kwamba kila mshiriki, bila kujalikama ana uwezo wa kimwili, kiakili, kimasomo au kijamii wanao uwezo wakuendelea mpaka kuinuliwa. Mwalimu lazima aone kwamba kila mmojaanajifunza yale yote ambayo anaweza kujifunza. Kumbuka maneno yaMwokozi:

“Kadiri mlivyomtendea mmoja wao wa hao ndugu zangu walio wadogo,mlinitendea mimi” (Mathayo 25:40).

viii

Page 10: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ukuhani

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa ukuhani ni nini nanamna tunavyoweza kuikuza miito yetu katika ukuhani.

Utangulizi Fikiria wakati ule ulipopokea ukuhani. Roho wa Bwana bila shakaalikuwepo wakati wenye ukuhani walipokuwekea mikono juu ya kichwachako na kusema maneno fulani. Wanaume wenye mamlaka ya ukuhanikwa kufanya hivyo walikupatia ukuhani. Unapotafakari juu ya tukio hili,jiulize:

• Ni nini hasa kilitokea kwangu siku hiyo?

• Je! nilibadilika baada ya kupokea ukuhani?

• Je! mimi ni mtu tofauti leo kwa sababu nina ukuhani?

• Je! nimeweza kuwatumikia wengine kupitia katika ukuhani wangu?

• Baba yangu wa mbinguni anafurahia namna ninavyoutumia ukuhani?

Ukuhani ni Nguvu za Mungu“Tunapotenda katika jina la Bwana kama wenye ukuhani, tunafanya hivyokatika jina na kwa niaba ya Baba yetu wa Mbinguni. Ukuhani ni nguvuambazo Baba yetu wa Mbinguni hutumia kupitia kwa watu.” (Harold B.Lee, “Follow the Leadership of the Church,” Ensign, July 1973, p. 98.)

Ukuhani ni nguvu za Mungu. Mungu hutekeleza kazi zake kwa ukuhanialionao. Aliumba vitu vyote kwa nguvu hizi na hutawala ulimwengu naselestia kwazo. Kwa vile ukuhani ni nguvu za Mungu, ni wa milele.Tunasoma katika Lulu ya Thamani Kubwa kwamba ukuhani, “ambaoulikuwepo hapo mwanzo utakuwepo mwisho wa dunia pia” (Musa 6:7).

Mungu na Yesu Kristo wamewapatia watu nguvu za ukuhani ili wawezekusaidia “kuleta maisha na uzima wa milele kwa mwanadamu” (Musa1:39). Ukuhani, kwa hivyo, ni mamlaka ya Mungu aliyowapa watu kutendakatika mambo yote kwa ajili ya wokovu wa binadamu.

Sisi ambao tuna ukuhani tunayo mamlaka ya kumuwakilisha Mungu. Nabiiwa Mungu Raisi Joseph Fielding Smith aliwambia wenye ukuhani wote:“Sisi ni mawakala wa Mungu. Tunamwakilisha yeye; ametupa mamlakaambayo yanatuwezesha kufanya yote yaliyo ya muhimu ili kuokoa nakuinuliwa kwetu wenyewe pamoja na watoto wake wengine katika dunia.

1

Somo la 1

Page 11: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Sisi ni mabalozi wa Bwana Yesu Kristo. Jukumu letu ni kumwakilisha yeye. Tumeelekezwa . . . kufanya kile ambacho yeye angefanya kamaangekuwepo hapa mwenyewe.” (“Our Responsibilities as PriesthoodHolders,” Ensign, June 1971, p. 49.)

Safu ya Mamlaka ya UkuhaniKila mwenye ukuhani anapaswa kuweza kufuatisha “safu yake yamamlaka” mpaka kwa Yesu Kristo. Hii inamaanisha kuwa anapaswakumjua aliyemtawaza katika ukuhani na ni nani aliyemtawaza yulealiyemtawaza yeye. Anapaswa kuweza kufuatisha kutawazwa huko kutoka kwa mtu yule aliyemtawaza yeye hadi kwa Nabii Joseph Smith,aliyetawazwa na Petero, Yakobo na Yohana ambao walitawazwa na YesuKristo. Hii inajulikana kama “safu ya mamlaka.” Kama mtu hana nakalailiyoandikwa ya safu ya mamlaka, anaweza kupata moja kutoka kwa yulealiyemtawaza katika ukuhani.

Mwenye ukuhani aliyepewa jukumu hili mapema aonyeshe darasani cheti chake cha “safu yamamlaka” kikifuatisha mamlaka yake hadi kwa Yesu Kristo.

Nguvu za Ukuhani Huja kwa Kuishi Maisha ya Haki“Sisi sote wenye ukuhani tunayo mamlaka ya kumwakilisha Bwana, lakinimatokeo mazuri ya mamlaka yetu—au kama ungependa, nguvuzinazotokana na mamlaka hayo— zinategemea mwenendo wa maishayetu na uadilifu wetu.” (H. Burke Peterson, “Priesthood—Authority andPower,” Ensign, May 1976, p. 33.)

Bwana ametuonyesha wazi katika maandiko matakatifu kuwa ni lazimatuwe waadilifu ili tuweze kupokea, siyo mamlaka pekee, ila pia nguvu zaukuhani. “Tazama, kuna wengi walioitwa, lakini ni wachache walioteuliwa.Na ni kwa nini hawajateuliwa?

“Ni kwa sababu mioyo yao imewekwa sana kwenye vitu vya dunia hii, nawanatarajia heshima za watu, kwamba hawajifunzi somo hili moja—

“Kwamba haki za ukuhani zimeunganishwa na haziwezi kutenganishwa nanguvu za selestia, na kwamba nguvu za selestia haziwezi kudhibitiwa aukutumika ila tu kwa kanuni za haki.

“Kwamba zinaweza kutolewa kwetu, hii ni kweli; lakini tunapotumia kufichadhambi zetu, au tunapofurahisha majivuno yetu, tamaa zetu zizizo namaana, au kutawala au kushurutisha nafsi za wana wa watu katika njiayoyote ya uovu, tazama selestia hujitoa, Roho wa Bwana huhuzunika nainapojitoa; Amina kwa ukuhani au mamlaka ya mtu huyo” (M&M 121:34–37).

Ni kwa nini mambo haya yaweze kutuzuia sisi kuwa na nguvu katika ukuhani?

Chanzo cha nguvu za ukuhani ni Mungu, ambaye hutenda kupitia kwaRoho Mtakatifu. Ili Roho Mtakatifu aweze kutuongoza katika kutumiaukuhani, ni lazima tutii amri na kuishi kwa ustahilivu. “Safu yetu ya

2

Page 12: Wajibu na Baraka za Ukuhani

mamlaka” hufuatisha mpaka kwaYesu Kristo kupitia kwa wale waliowezakuwa na ukuhani, lakini nguvu katika ukuhani huja kwetu tu kutoka kwaBaba yetu aliye Mbinguni kupitia kwa Roho Mtakatifu. Tukiwa na nguvu zaukuhani, tunaweza kufanya kazi ya Bwana; bila nguvu hizo, hatuwezi.

Onyesha picha 1-a, “Mwenye ukuhani anambariki mgonjwa kama Kristo alivyofanya hapokale.”

“Kama tukiishi kwa ajili hiyo, zetu zinaweza kuwa nguvu tulizopewa naBaba yetu wa Mbinguni ambazo zitaleta amani katika nyumba iliyo namatatizo. Zetu zinaweza kuwa nguvu za kubariki na kutuliza watotowadogo, zitakazoleta usingizi kwenye macho yaliyojawa na machozimapema asubuhi. Zetu zinaweza kuwa nguvu za kuleta furaha katikamkutano wa jioni ya familia, nguvu za kutuliza wasiwasi wa mke aliyechoka.Zetu zinaweza kuwa nguvu za kutoa maongozi kwa kijanaaliyechanganyikiwa na asiye thabiti. Zetu, nguvu za kubariki binti kabla yakwenda nje na rafiki yake au kabla ya ndoa ya hekaluni au kubariki kijanakabla ya kuondoka kwenda misheni au chuoni. Zetu, ndugu zanguwadogo, zinaweza kuwa nguvu za kuzuia fikira potofu za mkusanyiko wavijana wanaojihusisha na matamshi mabaya. Zetu zinaweza kuwa zakuponya wagonjwa na kufariji wapweke. Haya ni kati ya madhumunimuhimu ya ukuhani.” ( H. Burke Peterson, “Priesthood—Authority andPower,” Ensign, May 1976, p. 33.)

Muulize mwenye ukuhani aliyeulizwa awali kueleza uzoefu wake wa kuonyesha nguvu zaukuhani katika maisha yake.

Kukuza Nguvu Katika UkuhaniKuna mambo kadhaa ambayo tunaweza kufanya ili kusitawisha nguvukatika ukuhani:

TAMAA

Ni lazima kwanza tuwe na tamaa ya kukuza nguvu zetu katika ukuhani. Maandiko matakatifuyanafundisha kwamba watu hupokea kutoka kwa Mungu kulingana na tamaa yao (tazamaAlma 29:4; M&M 4:3; M&M 6:8; M&M 7:1–3).

ISHI MAISHA YA HAKI

Tunapaswa kujitahidi kuzishika amri zote za Baba wa Mbinguni. Kwa kuishimaisha ya haki, tunaweza kuwa na Roho Mtakatifu kama mwenzi wetu kilamara na atatuongoza sisi katika kufanya mambo ambayo tunapaswakufanya (tazama 2 Nefi 32:5).

KUWA MNYENYEKEVU

“Yeye ambaye hujinyenyekeza kweli, na anatubu dhambi zake, na kuvumiliahadi mwisho, ndiye atakayebarikiwa” (Alma 32:15). Inatupasa kuwa tayarikukubali kufuata ushauri na kukamilisha kazi tulizopewa na viongozi wetuwa ukuhani, tuwe tayari kufanya lililo muhimu kwa ajili ya usitawi wa watuwengine, na kusikiliza na kufuata ushawishi wa Roho.

3

Somo la 1

Page 13: Wajibu na Baraka za Ukuhani

1-a

Page 14: Wajibu na Baraka za Ukuhani

SOMA

Ni lazima tusome na kutafakari juu ya maandiko matakatifu. Ni kwakusoma maandiko matakatifu kibinafsi tu ndiyo tunaweza kujua mapenzi yaMungu, na bila kujua mapenzi ya Mungu, hatuwezi kuishi kulingana nainjili. Kwa sababu hiyo hiyo, pia sisi tunahitajika kujifunza vitabu vyetu vyamwongozo wa ukuhani ili tuweze kujua wajibu wetu kama wenye ukuhani.

SALI

Ni lazima tumuulize Baba yetu wa Mbinguni kile ambacho anatutaka sisitufanye. Tunapaswa kusali kila mara kwa maongozi katika kutumia ukuhaniwetu ipasavyo. “Ni lazima tuangalie na kuomba kila mara ili tusiingie katikamajaribio, kwani Shetani hutamani kutupata sisi” (3 Nefi 18:18).

WAPENDE WENGINE

Yesu Kristo ametufundisha kwamba nguvu za ukuhani zimejengwa juu yaupendo na kwamba tunapaswa kuwapenda watu wote (tazama M&M121:41–42, 45–46). Upendo huanzia nyumbani. Tunapaswa kuwapendawake zetu na watoto wetu na kushugulikia mambo yao. Njia moja wapotunayoweza kuonyesha upendo wetu kwa familia zetu ni kwa kutumiaukuhani wetu kuongoza na kubariki maisha yao.

TUMIA UKUHANI

Tunapotumia ukuhani, tunaonyesha mfano kwa wale wengine wenyeukuhani, kwa ulimwengu, na zaidi sana kwa familia zetu. Kama familiazinatuona tukitumia ukuhani, watajua ya kwamba sisi ni watumishi waMungu na watakuja kwetu wanapohitaji msaada. Ni jambo la kuhuzunishakufikiria kwamba kuna familia ambazo hazijui kamwe baraka zinazokujawakati Baba na wanawe wa kiume wanapotumia ukuhani kwa manufaa yafamilia zao.

Ukuhani unaweza kuleta mabadiliko katika nyumba zetu. Raisi David O.McKay alisema: “Nyumba hubadilika kwa sababu mwanamume anaukuhani na ana uheshimu ukuhani huo.” (“Priesthood,” Instructor, Oct.1968, p. 378.)

Kama sisi wenye ukuhani tunaishi kwa haki, tutafanya yafuatayo:

• Kwa haki tutaangalia matakwa mema ya kila mwana familia hata kamahayatakuwa sawa na matakwa yetu.

• Sikiliza—hata yule mtoto mdogo kabisa.

• Weka mambo ya familia yako mbele ya faraja zako.

5

Somo la 1

1-a, Wenye ukuhani wanawabariki wagonjwa kama Kristo alivyofanya hapo kale

Kristo akimponya kipofu, na Carl Bloch. Picha ya asili kwenye kiti cha sala cha mfalme katikakanisa la Frederiksborg Castle, Udeni. Imetumiwa kwa ruhusa ya National Historic Museumkule Frederiksborg.

Page 15: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Tujifunze kujitawala sisi wenyewe.

• Tuongee kwa sauti inayoonyesha upendo na kuwajali wengine.

Ni njia gani za nyongeza ambazo tunaweza kuzitumia kukuza ukuhani?

Mwisho“Sisi sote tunapaswa kufahamu kwamba hakuna kitu chochote katikadunia hii kilicho na nguvu kama ukuhani wa Mungu.” (N. Eldon Tanner,“Are You Taking Your Priesthood for Granted?” Ensign, May 1976, p. 41.)

Raisi N. Eldon Tanner alieleza umuhimu wa kuwa mwenye kustahilikupokea ukuhani katika hadithi ifuatayo:

“Nilipokuwa askofu, nilikuwa na vijana sita katika kata yangu waliokuwa naumri wa kutosha kutawazwa kuwa wazee. Ningeweza kuwapendekezawatano kati yao kwa sababu mmoja hakuwa tayari. Tulikuwa tumeongeakuhusu jambo hili mara kadhaa lakini aliniambia, ‘Mimi sistahili.’ Alijisikiavibaya sana juu ya haya na hakutarajia kupendekezwa . . . Mjomba wakealikuja kwangu na akasema, ‘Unahakika hautamzuia kijana huyu halimarafiki zake watano wanaendelea mbele.’ Alinisihi nimwache aendelee.Alisema: ‘Utakuwa unamfukuza kijana huyu kutoka katika Kanisa kamahautafanya hivyo.’

“Nilimuelezea mtu huyo, ‘Ukuhani ni kitu cha muhimu sana ambachotunaweza kumpatia kijana huyu. Hatukabidhiani ukuhani . . . Kijana huyuna mimi tunaelewana na yeye hayuko tayari kutawazwa kuwa mzee.’ Nahakupendekezwa.

“Miaka michache baadaye, nilikuwa ninahudhuria mkutano mkuu, . . . nakijana mmoja alikuja kwangu na kusema, ‘Raisi Tanner, hautanikumbuka.Mimi ndiye yule kijana ambaye haukumpendekeza kutawazwa kuwa mzee.’Aliponyoosha mkono wake na kusema, ‘Nataka kukushukuru kwa jambohilo. Sasa mimi ni askofu katika California. Kama ungenipendekeza wakatinilipokuwa sistahili, singeweza kujua maana ya ukuhani na ni ninikilichohitajika kutoka kwangu, na kwa kweli singekuwa askofu ambayenimekuwa leo.’ ” (“Priesthood Responsibilities,” Ensign, July 1974, p. 94.)

Ni lazima zote tujifunze kanuni hizi muhimu ili tuweze kutumia ukuhani kwa mafanikio mazuri. Ni lazima tujifunze kwamba “Haki za ukuhanizimeunganishwa na haziwezi kutenganishwa na nguvu za selestia, nahaziwezi kutawaliwa au kutumiwa ila tu kwa kanuni za haki” (M&M 121:36).Ili kupokea nguvu kutoka kwa Mungu, lazima tuwe wenye kustahili.

Tunapaswa kila mara kukumbuka kwamba sisi tuna mamlaka na nguvu zaMungu na kwamba tunamwakilisha yeye. Tunapotumia ukuhani,tunapaswa kujiuliza “Yesu Kristo angependa nifanye nini katika hali kamahii? Je mimi ninatenda kama yeye anavyonitarajia kutenda?”

6

Page 16: Wajibu na Baraka za Ukuhani

7

Somo la 1

Changamoto1. Jiahidi mwenyewe kujifunza kwa makini mwongozo wa ukuhani katika

kitabu hiki cha mwongozo na kubali changamoto zinazotolewa katikakila somo. Kwa kutekeleza changamoto hizi, utakuza nguvu katikaukuhani na kuwa karibu na Baba yetu wa Mbinguni na kuwa mwenyehuduma kubwa kwa wengine.

2. Weka kumbukumbu ya mamlaka yako ya ukuhani. Unapaswa uwezekufuatisha ukuhani wako hadi kwa Yesu Kristo.

3. Andika mamlaka yako ya ukuhani kwenye karatasi au kadi na uwapewale unaowatawaza katika ukuhani.

Maandiko Matakatifu ZaidiM&M 107:1–14 (tofauti kati ya ukuhani wa Melkizedeki na ukuhani waHaruni)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma somo la 13, “Ukuhani,” na 14, “Muundo wa Ukuhani,” katika kitabu cha Kanuni zaInjili.

2. Jifunze M&M 121:34–46.

3. Pata mwenye ukuhani mmoja alionyeshe darasa “safu yake ya mamlaka” akifuatishampaka kwa Yesu Kristo.

4. Pata mwenye ukuhani mwingine atoe uzoefu alionao kuonyesha nguvu za ukuhani.

5. Waulize kila mwenye ukuhani kuleta vitabu vyake vya maandiko matakatifu darasani kilawiki na kuwa tayari kusoma na kuweka alama kwenye maandiko maalumu katika kilasomo.

6. Kumbuka kwamba hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili yanaweza kutolewa nawashiriki wa darasa.

Page 17: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ukuhani kutoka Adamu mpaka UrejeshoMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kwamba ukuhaniambao tumeupokea ni sawa na ukuhani ambao alipewa Adamu na watuwengine waadilifu katika miaka yote.

UtanguliziAdamu alikuwa mtu wa kwanza kuwa na ukuhani wa Baba Mkuu. Hiiinamaanisha kuwa Mungu alimpatia mamlaka ya kuiongoza familia yake nakufanya ibada walizohitaji ili kurudi mbele zake. Pia alikuwa nabii wakwanza kupokea funguo za uRaisi au mamlaka ya kuliongoza kanisa laMungu hapa ulimwenguni. Kwa mamlaka hayo aliwapatia watu wengiukuhani na akawapa mashauri jinsi watakavyoutumia. MaRaisi wote waKanisa kutoka Adamu wamekuwa na mamlaka haya.

Mamlaka haya ya kuwaongoza wenye ukuhani wote wa Kanisa katika afisina majukumu yao mengi yanashikiliwa na mtu mmoja tu katika wakatimmoja—Raisi wa Kanisa (tazama M&M 81:1–2; M&M 132:7). Ijapokuwa nimtu mmoja tu mwenye kushikilia aina hii maalumu ya mamlaka ya ukuhanileo, wengi wanao ukuhani, na ni ukuhani ule ule ambao manabii wotewamekuwa nao tangu Adamu alipoupokea. (Kwa maelezo zaidi juu yafunguo za ukuhani, tazama somo la 11 katika kitabu hiki.)

Adamu alipokea UkuhaniMara tu baada ya Adamu na Hawa kufukuzwa kutoka kwenye bustani yaAdeni, malaika aliwatokea na kuwafundisha Injili (tazama Musa 5:4–9).Kanisa lilianzishwa pia na Adamu alibatizwa kwenye maji kwa namna ile ileambayo tumeelekezwa tubatize siku hizi (tazama Musa 6:64–65). Adamualipatiwa ukuhani ili kwamba awe na mamlaka ya kufanya ibada zote zainjili kwa ajili ya familia yake. Kwa mamlaka haya aliwabatiza watu wote wafamilia yake na kuwapatia ukuhani wanawe walioishi kwa haki.

Onyesha picha 2-a, “Ukuhani katika Vizazi Vyote.” Eleza kwamba chati imegawanywa katikavipindi vinane vinavyoitwa enzi. Soma ufafanuzi wa enzi hapo chini ya chati. Eleza ya kwambahatujui kulikuwa na enzi ngapi za injili lakini hizi nane zinasimamia kama mojawapo ya zilekuu. Angalia kila picha inayohusika kulingana na enzi ambayo imetajwa katika somo nausome maandiko matakatifu yaliyomo kwenye kila picha. Maandiko matakatifuyanatufundisha kwamba kila Nabii alikuwa na ukuhani wa Melkizedeki.

8

2-a, Ukuhani katika vizazi vyote“Wale wanaoupokea ukuhani wananipokea mimi, asema Bwana” (M&M 84:35).

Somo la 2

Page 18: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2-a

Enz

i ya

Utim

ilifu

wa

nyak

ati

Ka

nis

a

lina

reje

sh

wa

(M&

M 2

0:1

)

Uku

ha

ni

un

are

jesh

wa

(M&

M 1

3;

M&

M

27:8

, 12, 13)

Enz

i za

Mer

idia

ni

(Wa

eb

ran

ia 5

:9,

10;

Ma

tha

yo

16:1

9;

3 N

efi

11:2

1, 22,

12:1

)12:1

)

Enz

i ya

Leh

i

(Mo

sia

h 6

:3;

Alm

a 1

3:1

–2, 8–9)

Enz

i ya

Mus

a

(M&

M 8

4:6

)

Enz

i ya

Ab

rah

amu

(M&

M 8

4:1

4;

Ab

rah

am

u 1

:16,

18)

Enz

i ya

Nuh

u

(M&

M 1

07:5

2, 53)

Enz

i ya

Eno

ki

(M&

M 1

07:4

8, 53)

Enz

i ya

Ad

amu

(M&

M 1

07:4

0, 41)

Uku

han

i kat

ika

Viz

azi V

yote

Man

abii

katik

a ki

la e

nzi w

alik

uwa

na u

kuh

ani m

kuu.

(Ta

zam

a M

&M

84:

17.)

Enz

i: K

ipin

di c

ha

wak

ati a

mb

ao in

jili n

a m

amla

ka y

a uk

uhan

i yak

iwa

na f

ung

uo m

aalu

mu

zim

eto

lew

a kw

a w

ale

wal

ioch

agul

iwa

na B

wan

a ili

kuf

und

ish

a na

kuw

aong

oza

wat

oto

wa

Mun

gu

wan

aois

hi h

apa

ulim

wen

gun

i.

Ad

amu

Eno

kiN

uhu

Ab

rah

amu

Mus

aLe

hi

Jose

ph

Sm

ithK

rist

o, M

itum

e na

Waf

uasi

kat

ika

Mar

ekan

i

Karib

u miak

a 400

0 kab

la ya

ku

zaliw

a Yes

u Kris

toKa

ribu m

iaka 3

765 k

abla

ya

kuza

liwa Y

esu K

risto

Karib

u miak

a 300

0 kab

la ya

ku

zaliw

a Yes

u Kris

toKa

ribu m

iaka 2

000 k

abla

ya

kuza

liwa k

wa Ye

su K

risto

Karib

u miak

a 150

0 kab

la ya

ku

zaliw

a Yes

u Kris

toM

ei tet

ai 60

0 mata

iti i m

ua ak

e i te

Mes

iaM

ei te

tai 4

00 m

atai

ti i

mur

i i te

mat

eang

a o

te M

esia

Mwa

ka w

a 183

0

Uas

iU

asi

Uas

iU

asi

Uas

iU

asi

Uas

i Mku

u

Mile

nia

Maf

urik

o

Page 19: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Enzi ya Baba MkuuAdamu alifundisha injili kwa watoto na wajukuu wake na alihakikisha kuwawamepokea ibada muhimu za ukuhani na alilianzisha Kanisa kulingana nautaratibu wa Baba Mkuu. Utaratibu wa Baba Mkuu unamaanisha kwambamuundo wa Kanisa unaitegemea familia na kwamba ukuhani unarithishwakutoka kwa baba kwenda kwa mwana. Miongoni mwa Baba Mkuu walioishikatika enzi hii ni Sethi, Enosi, Kainani, Mahalalel, Yaredi na Enoki (tazamaM&M 107:40–52).

Tazama picha 2-a, “Ukuhani katika Vizazi Vyote.” Onyesha picha ya enzi ya Adamu na usomeM&M 107:40–41 kama ilivyoonyeshwa kwenye chati.

Uasi Mkuu wa KwanzaWatu wana wakala au uhuru wa kuchagua. Kwa uwakala huu watotowengine wa Adamu walichagua kuvunja amri. Idadi iliyofanya uchaguzi huuilipozidi na wakageuka kutoka kwenye ukweli, walianza “toka wakati huokuwa wenye tamaa za kimwili, anasa na ukatili” (Musa 5:12–13). Wakatikuanguka kwa namna hii kutoka kwenye ukweli kunapotokea huitwa uasi.

Adamu na wale ambao walizishika amri walihubiri kwa watu hawa nawalijaribu kuwafanya watubu. Watu wengi hawakutubu, lakini walewaliotubu waliungana na nabii Enoki na wakaitwa Sayuni. Maandikomatakatifu yanatuambia kwamba “Enoki na watu wake wote walitembea naMungu . . . na ilikuja kupita kwamba Sayuni haikuwepo tena kwa sababuMungu aliitwaa na kuipokea mbinguni” (Musa 7:69).

Tazama picha ya enzi ya Enoki katika chati na usome M&M 107:48–53.

Baada ya Enoki na watu wa Sayuni kuchukuliwa kutoka ulimwenguni, watuwaovu waliongezeka mno. Bwana alimtuma Nabii Nuhu ili awaonye nakuwaambia watubu. Nuhu aliwambia watu waovu kwamba kamahawatatubu watafagiliwa mbali kutoka kwenye ulimwengu na mafurikomakuu. Familia ya Nuhu, hata hivyo, ndiyo pekee waliomsikiliza na kushikaamri. Mafuriko yalikuja kama vile Nuhu alivyokuwa amewaonya watu nayeye na familia yake tu ndio pekee waliookoka.

Tazama picha ya enzi ya Nuhu katika chati na usome Musa 8:19–20.

Ukuhani baada ya MafurikoBaada ya mafuriko, Nuhu alitoa ukuhani kwa wanawe na wajukuu zakewaliokuwa waadilifu. Mmoja kati ya watu waadilifu walioishi baada ya Nuhuni Melkizedeki. Melkizedeki alikuwa muadilifu sana hata kwamba ukuhaniukaitwa kwa jina lake (tazama M&M 107:2–4). Melkizedeki alimwekeamikono na kumpa ukuhani Abrahamu na Abrahamu akawapa wengine.Hivyo, ukuhani wa Melkizedeki uliendelea mpaka wakati wa Musa.

Tazama picha ya enzi ya Abrahamu katika chati na usome M&M 84:14.

10

Page 20: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ukuhani wa Melkizedeki Unaondolewa Kutoka IsraeliKama vile Maandiko matakatifu yanavyotueleza, Abrahamu alimpatiamwanawe Isaka ukuhani na Isaka naye akampa mwanawe Yakobo. Na jinala Yakobo likabadilishwa kuwa Israeli na kutokea hapo hadi sasa kizazi chaYakobo kinajulikana kama wana wa Israeli.

Katika siku za Musa, baada ya kuwaongoza wana wa Israeli kutoka Misri,Bwana aliwapa wana wa Israeli injili kamili. Lakini waliikataa, kwa hivyo,Bwana aliuondoa kutoka kwao ukuhani wa Melkizedeki na ibada kuu zainjili. Walibakia na ibada ndogo ndogo tu za injili (kama vile sheria yadhabihu), na hizi zilisimamiwa na ukuhani mdogo ulioitwa kwa jina landuguye Musa, Haruni.

Bwana pia aliwaachia baadhi ya Kanuni za usafi na maadili ya injili. Zaidi yasheria hizi za kiroho kulikuwa na sheria zingine za kuendesha mambo yakimwili au mambo ya muda ya shughuli za watu. Baadhi ya sheria hizizinapatikana katika Kutoka, Mambo ya Walawi, na Kumbukumbu la Torati.Hazikutarajiwa kuchukua nafasi ya injili lakini zilitolewa kama nyongeza yasehemu ya injili ambayo ilibaki kama njia ya kuwatayarisha wana wa Israelikuishi kulingana na injili katika ukamilifu wake wakati wa baadaye.

Ingawaje ukuhani wa Melkizedeki ulitwaliwa kutoka Israeli kama taifa,haukuwa umetwaliwa kutoka ulimwenguni kabisa. Kati ya wakati wa Musa nakuja kwa Yesu Kristo, manabii kadhaa walikuwa na ukuhani wa Melkizedeki.Mmoja wapo wa hawa manabii ni Eliya, Isaya, Yeremia, Danieli na Ezekieli.

Tazama enzi ya Musa kwenye chati na usome M&M 84:6, 19–27.

Ukuhani katika Nyakati za Kitabu cha MormoniWakati Lehi na familia yake walipoondoka Yerusalemi na kusafiri hadiMarekani walikuwa na ukuhani. Hivyo, katika historia ya Kitabu chaMormoni watu waadilifu waliwafanyia ibada za ukuhani watu. Watu wawiliwaliozungumzia kuhusu ukuhani nyakati za Kitabu cha Mormoni ni MfalmeBenjamin na Alma.

Tazama chati na usome Mosiah 6:3 na Alma 13:1–2, 8–9.

Ukuhani Katika Nyakati za Yesu KristoWakati Yesu Kristo alipokuja ulimwenguni alirudisha injili yake katikautimilifu wake. Alikuwa mwenye funguo au mamlaka yote ya ukuhani nakwa hivyo aliwawekea mikono mitume (Mathayo10:1–4) na sabiini (Luka10:1). Alianzisha Kanisa lake miongoni mwa wafuasi wake na mwishowealipotoka hapa ulimwenguni, mitume walipewa mamlaka ya kuwawekeamikono wengine kwenye afisi mbali mbali katika ukuhani (tazama Matendoya Mitume 14:23). Katika njia hii, ukuhani uliendelea na kubaki kuwa msingiwa Kanisa la Yesu Kristo.

Tazama chati na usome Mathayo 16:19; Waebrania 5:5–10; na 3 Nefi 11:19–22; 12:1.

11

Somo la 2

Page 21: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Uasi MkubwaKwa muda baada ya Yesu Kristo kupaa mbinguni, Kanisa liliendeleakufundisha ukweli na maelfu ya watu kutoka miji mingi walijiunga naKanisa. Hata hivyo, kwa wakati, historia ilijirudia. Baadhi ya wale ambaowalikuwa wamejiunga na Kanisa walikataa kutii sheria na ibada za injili nawakazibadilisha ili zilingane na jinsi ya mawazo yao. Na wakati huo huo,waumini wengi wakiwemo Mitume na viongozi wa ukuhani, waliteswa nakuuawa. Watu hawa walipouawa na wengine walianguka kutoka kwenyeukweli, Kanisa likapoteza mamlaka ya ukuhani. Wakati ulikuja ambapohakukuwepo tena ukuhani katika Kanisa.

Kwa karne nyingi giza lilitawala juu ya ulimwengu. Makanisa yaliyoanzishwawakati wa uasi mkuu hayakuwa na ukuhani. Kama matokeo, hawakuwezakupata maongozi ya Mungu au kufanya ibada za wokovu. Kama vile Isayaalivyosema watafanya, “walizivunja sheria na kubadilisha ibada na kuvunjaagano la milele” (Isaya 24:5).

Onyesha picha 2-b, “Watu hupewa ukuhani kwa kuwekewa mikono na wale waliopewamamlaka ya Mungu.”

Kurejeshwa kwa UkuhaniUasi huu Mkuu uliendelea ulimwenguni hadi siku moja, katika majira yakuchipua mwaka wa 1820, kijana alimuuliza Mungu katika sala kujua nikanisa lipi ambalo angejiunga nalo. Kwa kujibu sala hili, Mungu Baba namwanawe Yesu Kristo walimtokea. Yesu alimwambia asijiunge na Kanisalolote, akisema. “Wanasogea karibu nami kwa midomo yao lakini mioyoyao iko mbali nami. Wanafundisha mafundisho kama amri za watu, yakiwana mfano wa ucha Mungu, lakini wanakataa nguvu yake.” (Joseph Smith—Historia 1:19.)

Kupitia kwa Joseph Smith, Bwana alirejesha ulimwenguni Kanisa lake lakweli na akarejesha kanuni na ibada zote muhimu za injili yake. Ili kufanyahivyo, Bwana alimpa Joseph Smith ukuhani mtakatifu ambao ulishikiliwa naAdamu na watu wengine waadilifu miaka yote. Tunao ukuhani huu siku hizina Bwana ameahidi kuwa katika enzi hii, enzi ya utimilifu wa nyakati,ukuhani hautatwaliwa tena. Utakuwepo hapa hata wakati Yesu atakaporuditena ulimwenguni.

Tazama picha ya enzi ya utimilifu wa nyakati katika chati na usome M&M 20:1; M&M 13; M&M27:8, 12–13 na M&M 86:10.

MwishoUkuhani ambao tunao leo ni sawa na ukuhani ule aliopewa Adamu, na nisawa na ule ambao Yesu anao. Kama Adamu na manabii wengine, sisi niwawakilishi wa Bwana hapa ulimwenguni. Kwa sababu sisi ni wawakilishi

12

2-b, Wanaume wanapewa ukuhani kwa kuwekewa mikono na wale waliopewa mamlaka ya Mungu

Page 22: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2-b

Page 23: Wajibu na Baraka za Ukuhani

wake, tunao uwezo wa kujisaidia sisi wenyewe, familia zetu na Kanisa ilituweze kurudi katika uwepo wa Mungu. Tunapopewa ruhusa na Askofu auRaisi wa tawi, tunaweza kubatiza watoto wetu na kuwapatia kipawa chaRoho Mtakatifu na kuwawekea mikono wana wetu ili kuwapa ukuhani.Katika njia hizi na zingine ukuhani unaweza kuleta furaha katika maishayetu na maisha ya wengine.

Changamoto1. Jadili kuhusu ukuhani na familia yako. Angalia njia za kuwasaidia vijana

wako kuwa wastahilifu kupokea ukuhani.

2. Kwa wakati unaofaa na ikiwa umepewa ruhusa ya kufanya hivyo, batizana kuwathibitisha watoto wako na kuwawekea mikono katika kuwapaukuhani.

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 14 “Muundo wa Ukuhani,” katika kitabu cha Kanuni za Injili. 2. Wakumbushe wenye ukuhani kuleta vitabu vyao vya maandiko matakatifu kwenye mkutano

wa ukuhani.

3. Pata mshiriki wa darasa atoe hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

14

Page 24: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Urejesho wa Ukuhani

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa urejesho wa ukuhanimtakatifu ambao uliondolewa kutoka duniani baada ya wakati wa Kristo.

Utangulizi Kama wenye ukuhani, tunayo mamlaka sawa na yale ambayo Mungualiwapa watumishi wake hapo zamani.

Onyesha picha 3-a, “Kristo aliwawekea mikono Mitume kumi na wawili na akawapatia funguoza ukuhani.”

Zifuatazo ni baadhi ya ibada ambazo tunaweza kufanya tukitumia ukuhani:

• Kubatiza, kama Yohana Mbatizaji na Wanefi walivyofanya (tazamaMathayo 3:15–17 na 3 Nefi 11:19–26).

• Kusimamia sakramenti kama Yesu alivyofanya (tazama Luka 22:19–20).

• Kutoa Roho Mtakatifu kama Paulo na Wanefi walivyofanya (tazamaMatendo 19:5–6 na 3 Nefi 18:37).

• Kuponya wagonjwa, kama Petro alivyofanya (tazama Matendo 3:1–8).

Ibada hizi za ukuhani zilifanywa hapo zamani na makuhani wengiwaliokuwa waaminifu.

Ni kwa nini tunaweza kufanya majukumu haya ya ukuhani leo?

Tunaweza kufanya kazi za ukuhani leo kwa sababu ukuhani wa Munguupo hapa ulimwenguni leo. Sababu watu wastahilivu katika Kanisa lakewamepewa ukuhani sawa na watumishi wake wa kale waliokuwa nao,Mungu hutambua kazi inayofanywa kwa ukuhani.

Uasi Mkuu na UrejeshoKama tulivyojadiliana katika somo la 2, uasi mkuu ulitokea baada ya wakatiwa Kristo. Hii inamaanisha kwamba kwa sababu ya uovu wa watu, ukuhanina mengi kati ya mafundisho ya Kristo yaligeuzwa au kupotezwa. Manabiiwengi wakuu walitabiri kwamba wakati utakuja ambapo watu wataasikutoka kwenye ukweli. Mmoja wa manabii hawa alikuwa Isaya.Akizungumza kuhusu Uasi, alisema kwamba watu “wamevunja sheria,wamezibadilisha ibada na kuvunja agano la milele” (Isaya 24:5). Utabiri waIsaya ulitimia. Kwa sababu ya uvunjaji wa sheria baada ya wakati waKristo, mpango wa kweli wa ukuhani uliondolewa kutoka ulimwenguni.Watu wa Kitabu cha Mormoni kwa muda walikuwa watu pekee waliofurahia

15

Somo la 3

Page 25: Wajibu na Baraka za Ukuhani

3-a

Page 26: Wajibu na Baraka za Ukuhani

baraka za ukuhani, lakini mwishowe hata wao pia waliasi kutoka kwenyeukweli. Kwa sababu ya uasi huu, watu ulimwenguni hawakuweza tenakuisikia injili ya kweli na kupokea ibada za kuokoa za ukuhani.

Lakini Baba wa Mbinguni anataka watoto wake wote warudi kwake. Ilikuwamuhimu, kwa hivyo, kwake kurudisha ukuhani na ibada zake na ukweliwote mwingine ambao unahitajika ili turudi kwake.

Manabii wengi walitazamia kuja kwa wakati huu. Isaya kwa mfano, alitabirijuu ya wakati ambao Bwana “atafanya kazi ya ajabu miongoni mwa watuhawa, hata kazi ya maajabu na ya kushangaza” (Isaya 29:13–14). Petro piaalitabiri juu ya wakati ambao “kutakuwa na kurejeshwa kwa mambo yote”(Matendo 3:19–21). Kurejeshwa maana yake ni kurudishia kitu ambachokiliondolewa mahali pake au kupotea. Ukuhani na injili ilibidi virejeshwe auwanadamu wote wangelipotea. Urejesho huu ulianza katika mwaka 1820wakati Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo walipojifichua wenyewe kwaJoseph Smith.

Joseph Smith na Urejesho wa UkuhaniJoseph Smith alikuwa mmoja wa wana wa kiroho waliokuwa “bora nawakuu” wa Baba yetu wa Mbinguni. Kama Ibrahimu, alikuwaamechaguliwa kabla ya kuja hapa ulimwenguni kwa ajili ya kazi maalumu.(Tazama Abrahamu 3:22–23.) Kwa sababu hii, kazi ya Joseph Smithilijulikana na wengi kati ya manabii waliomtangulia. Wote Joseph wa Misri,mwana wa Yakobo na Lehi, wa Kitabu cha Mormoni walimfahamu JosephSmith na wajibu wake. Lehi alizungumza na mwanawe Joseph kuhusuunabii uliotolewa na Joseph wa Misri kuhusu nabii katika siku za baadayeambaye pia ataitwa Joseph.

Soma 2 Nefi 3:6–15.

Joseph Smith alianza upelelezi wake kuhusu ukweli akiwa na umri mdogosana. Alipokuwa na umri wa miaka kumi na minne, alienda kwenye bustanina akamwomba Mungu amwambie ni kanisa gani ambalo angejiunga nalo.Kama matokeo ya sala yake, Mungu na Yesu Kristo walimtokea katikaumbile la watu wenye miili ya nyama na mifupa. Miaka mitatu baadaye,katika mwaka wa 1823, malaika Moroni alimtokea Joseph Smith nakumwambia juu ya Kitabu cha Mormoni. Hatimaye Moroni alimpatiaJoseph Smith kumbukumbu tukufu ya wenyeji wa hapo zamani waMarekani. Kwa msaada wa Mungu, Joseph aliweza kutafsiri kumbukumbuhizo. Kitabu cha Mormoni na ufunuo aliopokea Joseph Smith ulirejeshaukweli mwingi uliokuwa umepotea wakati wa uasi.

Lakini urejesho wa ukweli kuhusu Mungu na mafundisho yake haukutosha.Joseph Smith alizaliwa wakati hakukuwa na ukuhani hapa ulimwenguni.

17

Somo la 3

3-a, Kristo aliwatawaza mitume kumi na wawili na kuwapa funguo za ukuhani

Page 27: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kwa sababu hangeweza kutimiza wajibu wake bila ukuhani, ilikuwa nilazima ukuhani urejeshwe kwake na wale waliokuwa na funguo aumamlaka ya kumtawaza yeye katika ukuhani. Katika mwaka wa 1838,Joseph Smith aliandika yafuatayo kuhusu yeye na Oliver Cowderywalivyopokea ukuhani wa Haruni.

Onyesha picha 3-b, “Yohana Mbatizaji alitoa ukuhani wa Haruni kwa Joseph Smith na OliverCowdery.”

“Sisi . . . tuliendelea na kazi ya kutafsiri na katika mwezi uliofuata wa (Mei1829) katika siku fulani tulienda kwenye kichaka kusali na kumuulizaMungu juu ya ubatizo kwa ajili ya msamaha wa dhambi ambao tulikuwatumeona umetajwa katika tafsiri ya mabamba. Wakati tulipokuwa . . .tukisali na kumlilia Bwana, Malaika kutoka mbinguni aliteremka katikawingu la mwanga na baada ya kutuwekea mikono juu yetu, alitutawaza . . .kwenye ukuhani wa Haruni.

“ . . . Mjumbe aliyetutembelea katika tukio hili na kutupatia ukuhani huualisema kwamba aliitwa Yohana Mbatizaji wa katika Agano Jipya nakwamba alitenda hivyo chini ya mashauri ya Petero, Yakobo na Yohanaambao wanazo funguo za ukuhani wa Melkisedeki, ukuhani ambaotutapewa hivi karibuni . . . Ilikuwa tarehe 15 ya mwezi Mei, 1829 ambapotulitawazwa katika ukuhani chini ya mikono ya mjumbe huyu na kubatizwa.”(Historia ya Joseph Smith 1:68–72; tazama pia M&M 13.)

Baadaye mwaka ule wa 1829, Joseph Smith na Oliver Cowdery walipewaukuhani wa Melkizedeki. Mitume wa kale wa Yesu, Petro, Yohana naYakobo waliwatokea na kuwawekea mikono juu ya vichwa vyao nakuwatawaza (tazama M&M 27:12). Hivyo Joseph Smith alipokea ukuhaniwote wa Haruni na wa Melkizedeki. Mamlaka ya ukuhani yalikuwayamerejeshwa: wale walioyashikilia katika nyakati za awali walikuwawamerejesha tena nguvu za Mungu ulimwenguni.

Ukuhani wa HaruniUkuhani wa Haruni ni sehemu ya ukuhani wa Melkizedeki na hudumu chiniya uongozi wake. Wakati Yohana Mbatizaji alipowapa ukuhani wa HaruniJoseph Smith na Oliver Cowdery, aliwaambia kuwa alikuwa ameelekezwana Petro, Yakobo na Yohana waliokuwa na funguo za ukuhani waMelkizedeki.

Ukuhani wa Haruni uliitwa kwa jina la nduguye Musa. Haruni alitenda kaziyake ya ukuhani chini ya uongozi wa Musa. Hivyo hivyo, wenye ukuhani waHaruni wana mamlaka madogo kuliko wale walio na ukuhani waMelkizedeki. Kwa sababu hii, ukuhani wa Haruni wakati mwingine huitwaukuhani mdogo, “kwa sababu uko chini ya ule mkuu au ukuhani wa

18

3-b, Yohana Mbatizaji aliwapatia Joseph Smith na Oliver Cowdery ukuhani wa Haruni

Page 28: Wajibu na Baraka za Ukuhani

3-b

Page 29: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Melkizedeki” (M&M 107:14). Hii haimanishi kwamba ni mdogo na haunamaana. Kupitia kwa ukuhani wa Haruni, wanaume, vijana kwa wazee,hufanya kazi kubwa.

Nguvu na wajibu wa ukuhani wa Haruni ni kama ifuatavyo—

• Kuwa na funguo za kuhudumiwa na malaika. Inamaanisha kuwatunakuwa na haki ya kuwa na malaika ili waweze kutusaidia katikakutekeleza kazi ya Mungu.

• Kuwapatia wengine ukuhani wa Haruni.

• Kuhubiri toba na kubatiza.

• Kusimamia ibada takatifu ya sakramenti.

• Kufundisha injili na kuimarisha ushuhuda wa waumini wa Kanisa.

• Kukusanya matoleo kwa niaba ya Kanisa.

• Kusaidia kujenga mahekalu, kanisa, na majengo mengine.

• Kuwaangalia maskini, wajane na mayatima.

• Kushugulikia mambo yote ya kimwili ya Kanisa (kama kusafisha kanisa)kama inavyoelekezwa na Askofu au Raisi wa jamii la ukuhani.

Wajibu wa mashemasi, walimu na makuhani katika Ukuhani wa Haruniunatofautiana. Wajibu huu umeonyeshwa katika M&M 20:46–59.

Soma M&M 20:46–59.

Ukuhani wa Haruni kwa kifupi ni ukuhani wa matayarisho. Hutayarisha njiakwa wale wanaotoa baraka za Ukuhani wa Melkizedeki na unawapatiawenye ukuhani wa Haruni ujuzi wanaohitaji ili kupokea ukuhani waMelkizedeki.

Nguvu na mamlaka ya ukuhani wa Melkizedeki ni nini?

Ukuhani wa MelkizedekiUkuhani wa Melkizedeki uliitwa kutokana na Melkizedeki aliyeishi katikawakati wa nabii Abrahamu wa agano la kale. Kabla ya siku zake uliitwaUkuhani Mtakatifu kulingana na Utaratibu wa Mwana wa Mungu. Lakinikuepuka kurudia jina la Mungu kila mara, Kanisa la kale lilielekezwa kuitaukuhani huu kwa jina la Melkizedeki “kwa sababu Melkizedeki alikuwakuhani mkuu wa namna hiyo” (M&M 107:1–6).

Mafundisho na Maagano yanatufunulia kwamba ukuhani wa Melkizedekiuna haki ya usimamizi wa afisi zote katika Kanisa. Hii inamaanisha kwambaafisi zote katika Kanisa ni sehemu ya ukuhani wa Melkizedeki. Hakunamamlaka au ukuhani mkuu kuliko huu. Kwa nyongeza, ukuhani huu unamamlaka ya kusimamia ibada zote za kiroho tunazohitaji ili kurudi kwaBaba yetu wa Mbinguni. (M&M 107:8–19.)

20

Page 30: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Uwezo na wajibu wa ukuhani wa Melkizedeki ni—

• Kutoa kipawa cha Roho Mtakatifu.

• Kuwatawaza wanaume wanaostahili katika ukuhani wa Melkizedeki.

• Kufanyiza ndoa ya milele.

• Kufanyiza kazi ya hekalu kwa wanaoishi na wafu.

• Kuwahudumia wagonjwa.

• Kushugulikia usitawi wa kiroho na wa kimwili kwa watu wote.

• Kupokea maarifa kutoka kwa Mungu kwa ajili ya Kanisa.

Afisi ya mzee, kuhani mkuu, Baba Mkuu, Sabini na Mitume zinatofautianakulingana na majukumu yake maalumu. Wenye ukuhani wa Melkizedekiwanaweza kufanya kazi zote za ukuhani wa Haruni kwa sababu ukuhani waHaruni ni sehemu ya kazi za ukuhani wa Melkizedeki. Kupitia kwa ukuhaniwa Melkizedeki, tunajitayarisha sisi wenyewe na wengine siku moja kuingiakatika ufalme wa mbinguni.

Uliza mwenye ukuhani aliyeandaliwa mapema kusoma au kueleza tukio katika Matendo19:1–6 ambapo Paulo aliwabatiza tena wafuasi wengine. Kwa nini ilikuwa ni muhimu kwa watuhawa kubatizwa tena?

MwishoKama ukuhani usingekuwepo ulimwenguni, hatungeweza kufanya kazi yaMungu na Kanisa la kweli halingeweza kuwepo. Kwa sababu hiyo, hakunamtu ambaye angepata uzima wa milele. Uzima wa milele huja kwa wale tuwanaoshika kanuni na ibada za injili na ibada za kanuni za injili haziwezikufanywa bila ukuhani. Kwa sababu ukuhani ni nguvu za Bwana na siyo zamtu, mtu hawezi kujipa mwenyewe ukuhani. Wala kuwatawaza wenginempaka awe amepokea kutoka kwenye mamlaka inayostahili (tazama M&M42:11). Kwa sababu hizi ukuhani ulirejeshwa kwa Joseph Smith nawajumbe kutoka mbinguni. Siku hizi ukuhani unapatikana katika Kanisa lakweli la Kristo ambalo lilirejeshwa ili kufanya kazi ya Mungu kwa manufaaya wanadamu wote (tazama M&M 84:17).

Kila muumini wa kiume wa Kanisa ambaye amepokea ukuhani wa Munguana jukumu kubwa la kujisaidia mwenyewe, familia yake na watu wotewalio karibu naye ili aweze kufurahia baraka za uzima wa milele.

Changamoto1. Jifunze kazi na wajibu wa ukuhani wako. Unaweza kufanya hayo kwa

kusoma maandiko matakatifu, kufunga na kuomba, kujifunza kitabuchako cha mwongozo wa ukuhani na kupokea maagizo kutoka kwaviongozi wako.

21

Somo la 3

Page 31: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2. Timiza wajibu wako wa ukuhani kwa uwezo wako wote na daima tafutakuboresha utendaji wako.

3. Waunge mkono wale wenye mamlaka juu yako na jihadhari na kujipatiauwezo au mamlaka ambayo haujapewa.

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 13; 20; 84:107; 121; na 124 ili uweze kuelewa ukuhani.

2. Jifunze sura ya 14, “Muundo wa Ukuhani” na sura ya 17 “Kanisa la Yesu Kristo la WakatiHuu,” katika Kanuni za Injili.

3. Wapangie washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

22

Page 32: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Jamii la Ukuhani

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa njia ambazo jamii yaukuhani inaweza kuwasaidia watu binafsi, familia na Kanisa.

Utangulizi Kama wenye ukuhani, tunao uhuru na jukumu la kufanya mambo mengibinafsi bila kuambiwa kufanya hivyo na viongozi wetu wa Kanisa (tazamaM&M 58:26–29). Tunaweza kufanya kazi zetu; tunaweza kutunza familiazetu; tunaweza kuwa watiifu na kufanya mambo mengi mazuri kwa ajili yetuwenyewe na kwa familia zetu na wengineo. Hata hivyo, yatupasa zotekufahamu kuwa nyakati fulani tutahitaji msaada kutoka kwa mtu mwingine.Tunaweza kukwama kwenye matope, kuwa wagonjwa na kukosa nguvu zakwenda kutafuta msaada, kuvunjika moyo kwa sababu ya ukaidi wa mtotoau kukata tamaa kwa sababu hakuna mtu yeyote anayejali.

Siku moja mkulima alikuwa anajitayarisha kukusanya nyasi za malisho yaakiba katika ghala lake alipoona mvua kubwa ikikaribia kunyesha. Kamahataweza kukusanya nyasi kwenye ghala kabla ya mvua kunyesha,zingeharibika, kwa hivyo alihitaji msaada wa haraka. Aliwaomba msaadamajirani zake na wakamsaidia kuweka nyasi kwenye ghala kabla ya mvuakuiharibu. Kwa sababu ya msaada wao aliweza kuokoa zao lake.

Kwa njia hiyo hiyo, tukiwa na shida za kibinafsi au za kifamilia ambazohatuwezi kuzitatua peke yetu, tusiogope kuwaomba wengine kutusaidia.

Nani anaweza kutusaidia? Tunaweza kwenda wapi ili tuweze kupata msaada?

Madhumuni ya Jamii za UkuhaniBaba wa Mbinguni alianzisha Jamii za ukuhani ili kuwasaidia wenyeukuhani kukuza ukuhani na kufanya kazi pamoja ili kuwahudumia wenginena kuliimarisha Kanisa. Pia yameundwa kwa kuwasaidia wauminikusaidiana wakati wa shida.

Jamii la ukuhani ni kikundi kilichoundwa cha wanaume ambao wanashikiliaafisi moja katika ukuhani. Katika sehemu zingine za Kanisa ambako idadiya wanaume wanaoshikilia ukuhani ni wachache, wenye ukuhani wote, bilakujali ni afisi gani wanayoishikilia, huongozwa katika kikundi kimoja.

Katika sehemu za Kanisa ambako idadi ya wanaume wanaoushikiliaukuhani ni kubwa, Jamii za makuhani wakuu, wazee, makuhani, walimu, namashemasi hutengenezwa. Kila jamii, ila la makuhani, huongozwa na Raisina washauri wawili. Jamii la makuhani katika kata husimamiwa na askofu

23

Somo la 4

Page 33: Wajibu na Baraka za Ukuhani

na makuhani wawili kama wasaidizi wake. Raisi wa kigingi na washauriwake ndio uRaisi wa jamii la makuhani wakuu kwa makuhani wakuu wotekatika kigingi.

Katika kuwasaidia washiriki wa jamii kutekeleza wajibu wao wa kusaidianana kufundishana wenyewe majukumu yao, mikutano ya jamii hufanyika kilaJumapili. Katika mikutano hii, shughuli za jamii zinatekelezwa, kazi zaukuhani zinatolewa, injili inafundishwa, ushuhuda unaimarishwa na kilamshiriki hukua kiroho.

Tumeambiwa katika maandiko matakatifu jinsi ya kutekeleza majukumu nakazi zetu za ukuhani.

Soma M&M 107:99–100.

MaRaisi wa jamii au viongozi wa makundi ndio wenye jukumu lakutufundisha kazi zetu za ukuhani na kutupatia nafasi ya kujifunza katikakufanya kazi hizi. Baada ya kujifunza kazi zetu, jukumu letu ni kutumika kwajuhudi kubwa katika afisi zetu tulizoteuliwa katika ukuhani. Tunavyokuzamiito yetu ya ukuhani kwa kuwatumikia wenzetu na kukubali kazi kutokakwa maRaisi wa jamii zetu, tunaongeza ufahamu wetu na uwezo wetu wakutumikia.

Waulize washiriki wa darasa kujadili kuhusu kazi ambazo wamejifunza na kuzitekeleza.

Namna gani Jamii za Ukuhani Hufanya KaziJamii za ukuhani zinakubali na kutumia kanuni zote za injili ambazo Bwanaamefunua kwetu kupitia manabii wake. Mojawapo ya kanuni hizo muhimuni haki, umoja, usaidizi na urafiki.

HAKI

Bwana amesema kwamba “haki za ukuhani zimeshikana na nguvu zambinguni, na hazitenganishwi na kwamba nguvu za selestia haziwezikutawaliwa wala kutumiwa bali tu kwa kanuni za haki” (M&M 121:36).Nguvu za jamii letu la ukuhani hutegemea nguvu za waumini wake. Jinsitunavyokuwa waadilifu ndivyo tunavyopokea nguvu na maongozi zaidikutoka kwa Bwana.

UMOJA

“Jamii linapaswa kuwa limeungana zaidi kiasi cha kuweza kusaidiana, siyo tukiroho lakini pia kifedha na vinginevyo. Kama tunaweza kupata Roho waumoja katika jamii zetu za ukuhani, basi tunaanza kufahamu maana kamili yamuundo wa ukuhani katika Kanisa.” ( David O. McKay, “The FundamentalBasis for Home Teaching,” Improvement Era, July 1963, p. 615.)

MSAADA

“Jamii zote za ukuhani . . . ‘zameamriwa’ (na Bwana) kuweka tayarimajeshi yao, na chini ya Roho na nguvu za ukuhani, ili kuona kwamba kila

24

Page 34: Wajibu na Baraka za Ukuhani

mtu aliye katika dhiki amesaidiwa na Jamii yake aweze kujitegemea.”(Harold B. Lee, “The place of the Priesthood Quorum in the ChurchSecurity Program,” Improvement Era, Oct. 1937, p. 634.)

URAFIKI

Katika siku za mwanzo Kanisani wanaume walitoa kwa Jamii “zao uaminifuwao usiogawanyika . . . Hatutajua kamwe nguvu kamili na uzuri wa urafikiuliobuniwa katika Jamii hizo za ukuhani. Wanaume walitunza familia zawenzao waliokuwa wameenda misheni. Shida binafsi na huzuniwalishirikiana, na uaminifu ukabuniwa . . . Wanaume walitoa maisha yaokwa ajili ya wenzao . . .

“Ni kweli hatukabiliani na hatari kama hizo ambazo zilikuwepo wakati huolakini tunakumbwa na madhara mengi ambayo nayaogopa kwani maranyingine matokeo yake ni mabaya zaidi kuliko yale yaliyowakumbawaliotutangulia. Je! Tunahitaji marafiki kutusaidia katika hali hizi? Ndiyo!”(Stephen L. Richards, “The Priesthood Quorum: A Three Fold Definition,”Improvement Era, May 1939, p. 294.)

“Inapaswa kuwa chimbuko la faraja kwetu kufahamu kwamba ikiwatunahitaji kuimarishwa katika injili, ndugu wote waaminifu katika jamii letu laukuhani wataungana ili kutuonya, kutuimarisha kiroho na kutusaidia kupatanjia ya kurudi katika shughuli. Mzee Boyd K. Packer alisema: “Mtuanayelegea katika kuja kanisani hapotezi uanachama wake katika jamii laukuhani. Anaweza kukosa kujali lakini jamii halitakosa kumjalia. Jamii linajukumu la daima na la kudumu kwa kila muumini wa jamii. Kutojali muuminimlegevu na kutomtembelea ni [kumnyima[ haki zake kama muuminimwenye ukuhani.” (A Royal Priesthood [Melchizedek Priesthood StudyGuide, 1975], p. 134.)

Kanisa linamhitaji “kila muumini ili wote waweze kuimarishwa kirohopamoja, ili mpango uwekwe kamili” (M&M 84:110). Utaratibu wa Kanisandiyo utaratibu ulio mkamilifu zaidi sasa ulimwenguni, na majamii yaukuhani ni sehemu muhimu sana ya utaratibu huu. Kadiri jamii la ukuhanilinavyotekeleza majukumu yake, kila mshiriki wa jamii lazima afikiriwe. ElderPacker amesema: “Kama jamii lake la ukuhani linafanya kazi barabara, mtu(au mvulana) aliyekubaliwa na ndugu katika jamii lake, hawezi kushindwakatika jukumu lolote katika hatua za maisha yake.” (A Royal Priesthood,Melchizedek Priesthood Study Guide, 1975, p. 134.)

Jamii hufanya kazi sawa sawa kama kila mshiriki wake anafanya sehemuyake. Kwa kutumika kama mwalimu wa nyumbani, kwa mfano, wenyeukuhani wanatumika kama viungo kati ya Raisi wa jamii la ukuhani na kilafamilia katika jamii. Vile shida zinavyotambulika na mahitaji kuripotiwa nawalimu wa nyumbani, jamii ya ukuhani inaweza kutekeleza kwa vitendo.Pamoja na habari hizi, jamii, chini ya mashauri ya uRaisi wa jamii, inawezakuwasaidia washiriki wa jamii wanaohitaji msaada.

25

Somo la 4

Page 35: Wajibu na Baraka za Ukuhani

26

Baada ya familia, jamii ndiyo chanzo cha kwanza cha msaada. Kwasababu hii, washiriki wa jamii inawapasa kuitikia wito wa kuwasaidiawashiriki wa jamii walio na haja ya msaada.

Ni njia gani nyingine ambazo washiriki wa jamii wanaweza kutumikiana wenyewe kwawenyewe kama kaka katika ukuhani?

Kutimiza Sehemu Yetu kama Washiriki wa Jamii la UkuhaniWa eleze washiriki wasome na kuweka alama M&M 108:7. Andiko hili linatuambia tufanye ninikatika kuimarishana?

Andika kwenye ubao njia zilizotajwa kwenye maandiko matakatifu haya.

Miongoni mwa mambo mengine, Bwana ametaja kwamba mwenyeukuhani anaweza kuimarisha ndugu zake kwa yale anayosema juu yao nakile anachowafundisha. Raisi J. Reuben Clark Mdogo, alisema kwambajamii halina nguvu kushinda upendo binafsi wa washiriki wa jamii walionaokati yao.

“Msaada wa [jamii] unaweza kuchukua sura ya kumsaidia ndugu mwenyeshida katika shida na matatizo yake ya kweli, kama kujenga nyumba, aukuanzisha biashara ndogo, au kama yeye ni fundi, kumpatia vifaa vyaufundi, au kama yeye ni mkulima, kumpatia mbegu au kumsaidia kupandaau kuvuna mazao au kupata mkopo wa haraka anaohitaji kulingana namahitaji au kumpatia nguo au mahali pa kuishi au chakula au msaada wamatibabu au masomo kwa watoto au kutoa msaada kwa njia nyinginyinginezo.” (“Church Welfare Plan,” a discussion by President J. ReubenClark before the First Citizens’ Conference on Government Management atEstes Park, Colorado, June 20, 1939. p. 20.)

Jamii letu litakuwaje kama tungependana kwa kiukweli?

Madhumuni ya jamii la ukuhani ni kumsaidia kila mwenye ukuhani kujifunzajinsi anavyoweza kutumia ukuhani wake katika kuwasaidia wenzake katikajamii wakati wa shida. Madhumuni haya yanaweza kutekelezwa tu kamakila mshiriki yuko tayari kusaidia na kama mahitaji halisi ya washiriki wajamii yametambuliwa. Kwa sababu hii, ni lazima viongozi wetu wa jamiiwawe wameelezwa kuhusu shida tunazoziona na tuwe tayari kuombamsaada tunapokuwa na shida. Washiriki wa jamii hawawezi kuwasaidiawengine ikiwa hawajui shida zao. Bila shaka, kila mtu anapaswa kujaribukutatua shida zake lakini wakati hutokea ambapo tunahitaji msaada wajamii. Inatupasa kutosikia haya kwa kuomba msaada, kwa sababu hiiitawapatia nafasi wengine kuhudumia.

Hadithi ifuatayo inaonyesha jinsi jamii lilimsaidia mmoja wa washiriki wake:

“Wakati wa masika mwaka wa 1918, mwaka uliokuwa na hali ya kuogofyasana ya hali ya Vita vya Kwanza vya Dunia ambapo watu zaidi ya millioni14 walifariki kutokana na pigo baya la ‘tauni nyeusi’ au homa ya mafua yakihispaniola . . . Majira ya baridi yalikuja mapema . . . na kugandisha

Page 36: Wajibu na Baraka za Ukuhani

ardhini mazao ya viazi vya kutengeneza sukari. Baba yangu na kaka yanguFrancis walikuwa wakijaribu sana kutoa mzigo mmoja wa viazi hivyo kutokakwenye ardhi iliyoganda kwa barafu kila siku ambavyo walivilima kutokakwenye ardhi halafu wakatoa matawi na kutupa viazi kwenye gari kubwa lakubebea viazi na kulikokota hadi kwenye kiwanda cha sukari. Ilikuwa kaziya pole pole na ya kuchosha kwa sababu ya barafu na ukosefu wa wafanyikazi mashambani, kwani mimi na kaka yangu Floyd tulikuwa jeshini . . .

“Wakati walipokuwa wakiendelea kuvuna zao pekee la biashara kwa familiana walipokuwa wakila chakula cha jioni siku moja, simu ililia kutoka kwakaka yetu mkubwa George Albert . . . ikileta habari za kuhuzunisha za kifocha Kenneth, mwanawe Charles wa miaka tisa . . . aliyefariki kutokana naile homa ya kuogofya ya mafua, baada ya masaa machache tu ya kuuguavibaya sana, akaaga dunia kwenye paja la Baba yake; na akamwombaBaba kama angeweza kuja Ogden na kumchukaa mvulana huyo nyumbanina kumlaza kwenye kiwanja cha familia katika makaburi ya Lehi.

“Baba yangu . . . alielekea Five Points Ogden kumleta mjukuu wake wakiume nyumbani kwa mazishi. Alipowasili nyumbani alimkuta ‘Charl’ akiwamnyonge juu ya mwili baridi wa mpendwa wake, . . . akiwa na joto jingikwa ajili ya homa.

“ ‘Peleka mtoto wangu nyumbani,’ alisema Baba huyu mchanga, ‘naumlaze katika kiwanja cha familia na urudi kunichukua mimi kesho.’

“Baba alimleta Kenneth nyumbani, akatengeneza jeneza katika karakanayake ya useremala, na mama na dada zetu . . . wakaweka mto navitambaa ndani yake, halafu Baba na Franz pamoja na majirani wawiliwenye huruma walienda kuchimba kaburi. Kwa vile ni wengi waliokuwawakifariki, ilibidi familia ichimbe kaburi. Sala fupi kando ya kaburi ndiyopekee iliyokubaliwa.

“Punde tu waliporudi kutoka makaburini, simu ililia tena na George Albert(Bert) alikuwa kwenye simu na ujumbe mwingine wa kustusha: Charlalikuwa amefariki na wawili kati ya wasichana wake wadogo na warembo—Vesta miaka 7, Elaine miaka 5—walikuwa wagonjwa mahututi na watotowawili wachanga—Raeldon mwenye miaka 4 na Pauline miaka 3—walikuwa wagonjwa.

“Binamu zetu wazuri . . . waliweza kupata jeneza na kuutuma mwili waCharl nyumbani kwa gari la moshi kwenye behewa la mizigo. Baba naFranz waliuleta mwili kutoka kwenye kituo cha gari moshi . . .

“Siku iliyofuata, baba yetu, mzee mwenye nguvu na asiyeshindwa aliitwakwa kazi nyingine ngumu ya maombolezo—wakati huu kumleta nyumbaniVesta, mwenye kutabasamu na mwenye nywele nyeusi na macho yasamawati.

27

Somo la 4

Page 37: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Alipowasili nyumbani alimkuta Julliet, mama aliyekumbwa na huzuni,akiwa amepiga makoti kando ya kitanda cha Elaine malaika mwenyemacho ya samawati na nywele za dhahabu. Julliet alikuwa akilia nakusali . . .

“Kabla ya Baba kuwasili nyumbani na Vesta, ujumbe wa kustusha ulikuwaumefika tena. Elaine alikuwa ameenda kujiunga na babake, kaka yakeKenneth, na dadake Vesta. Kwa hiyo baba alifanya safari nyingine yakuvunja moyo ya kumleta nyumbani na kumlaza mtu wa nne katika familiayake, wote katika wiki moja.

“Simu haikulia tena jioni hiyo walipomlaza Elaine wala hakukuwa naujumbe wa kuhuzunisha wa kifo asubuhi iliyofuata . . .

“Baada ya kifungua kinywa, Baba alimwambia Franz, ‘Basi mwanangu,twende shambani na tuone kama tunaweza kupata mzigo mwingine waviazi vyekundu vya kutengeza sukari kwenye ardhi kabla haijaganda zaidikwa barafu. Funga farasi na twende.’

“Francis aliendesha kikundi cha farasi wanne na baba akapanda juu.Walipokuwa wakienda kwenye barabara ya Saratoga, walikutana na garibaada ya gari yakiwa yamejaa viazi vya kutengeneza sukari yakikokotwakuelekea kwenye kiwanda na yaliendeshwa na wakulima majirani.Walipowapita, kila dereva aliwasalimu kwa kuinua mkono: ‘Jambo mjombaGeorge!’ ‘Tunasikitika George,’ ‘George tunajua ulivyotaabika,’ Unamarafiki wengi sana George.’

“Kwenye gari la mwisho . . . alikuwa Jasper Rolfe. Aliinua mkono kwasalamu za furaha na kusema: ‘Hii ndiyo yote, Mjomba George!’

“Baba alimgeukia Francis na kusema: ‘Natamani hii ingekuwa yetu.’

“Walipofika kwenye lango la shamba, Francis alishuka chini na kufungualango, na walipoingia shambani, alisimamisha farasi na kungoja kwa mudamfupi halafu akaangalia shamba kushoto hadi kulia, na nyuma hadi mbelena tazama hakukuwa na viazi vyovyote kwenye shamba. Ndipoakakumbuka kile alichomaanisha Jasper Rolfe aliposema: ‘Hii ndiyo yoteMjomba George.’

“Baba alishuka chini kutoka kwenye gari na kuchukua mchanga wenyerotuba mwekundu alioupenda sana, na katika mkono wake wa kushotousiokuwa na kidole gumba, alichukua majani ya viazi na kuyaangalia kwamuda yakiwa ishara ya kazi yake ngumu kama vile hakuamini macho yake.

“Halafu baba akakaa chini kwenye majani ya viazi—huyu mtu ambayealiwaleta wanne aliowapenda nyumbani kwa mazishi katika siku sita tu;alitengeneza majeneza, alichimba makaburi na hata akasaidia nautengenezaji wa mavazi ya kuzikia—mtu huyu wa kushangaza ambayehakusita wala kutingika katika matatizo haya alikaa kwenye majani na kuliakama mtoto.

28

Page 38: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Halafu akasimama na kupangusa machozi yake na kitambaa chakechekundu na kuangalia juu kwenye selestia na kusema: ‘Asante, Baba kwawazee wa kata yetu.’ ” (LesGoates, as quoted by Vaughn J. Featherstone,“Now Abideth Faith, Hope and Charity,” Ensign, July 1973, pp. 36–37.)

MwishoJamii zote za ukuhani katika Kanisa zimetengenezwa ili zitimizemadhumuni ya Bwana. Kama wenye ukuhani, ni lazima tutekelezemajukumu tunayopewa.

Raisi Joseph Fielding Smith ameandika: “Haijapata kutokea kamwe katikahistoria ya Kanisa ambapo jukumu lile ambalo limetolewa kwa wenyeukuhani likawa na umuhimu mkubwa wa kutekelezwa kushinda siku hizi.Haijatokea hapo awali kuwa na jukumu kubwa la kumtumikia Bwana nakushika amri zake na kutekeleza miito ambayo tumepewa.” (Doctrines ofSalvation, 3:117.)

Changamoto1. Tekeleza kazi ulizopewa.

2. Kufahamu mahitaji ya washiriki wengine wa jamii la ukuhani.

3. Kuomba msaada wa jamii la ukuhani ukiwa na haja ya msaada.

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 107:21–26, 58–66, 85–100.

2. Tayarisha chaki na ubao. Utahitaji vifaa hivi katika masomo mengi, kwa hivyo panga jinsiutakavyokuwa navyo darasani kila wiki.

3. Wape nafasi washiriki wa darasa kutoa hadithi na kusoma maandiko matakatifu katikasomo hili.

4. Panga kuanza somo kwa kuimba “Dunia Inahitaji Watu Wanaojitolea,” Hymns, Namba 206.

29

Somo la 4

Page 39: Wajibu na Baraka za Ukuhani

30

Somo la 5Kazi za Shemasi

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kazi za shemasi.

UtanguliziAskofu Msimamizi wa Kanisa alitoa ushauri ufuatao kwa mashemasi waKanisa:

“Wanaume wote ni wana wa Mungu, lakini ninyi mnacho kitu cha ziada.Mnayo mamlaka ya kutenda katika jina lake. Hii huwafanya ninyi kuwatofauti na wengine wa ulimwengu. Haikufanyi wewe kuwa bora kulikowengine bali inakupa wewe wajibu wa kuishi maisha bora zaidi kulikowengine.

“Kwa sababu unajua kuwa wewe ni mwana wa Mungu na unao ukuhaniwake, mengi yanatarajiwa kutoka kwako kuliko wale ambao hawanabaraka hizi kuu.” (Victor L. Brown, “The Aaronic Priesthood—A SureFoundation,” Ensign, July 1972, p. 90.)

Majukumu ya ShemasiKama mashemasi tuko kwenye kazi ya Bwana (tazama M&M 64:29). Kaziya Bwana ni kazi yetu. Tunapoheshimu ukuhani kwa kutekeleza majukumuyetu, tuna mheshimu Mwokozi. Moja ya njia bora ambazo tunawezakuonyesha upendo wetu kwa Mwokozi ni kwa kutekeleza majukumu yetukama shemasi. Kazi hizi ni pamoja na kuliangalia Kanisa na kupitishasakramenti.

Andika “Kuliangalia Kanisa” na “Kupitisha Sacramenti” kwenye ubao.

Kuliangalia Kanisa kunamaanisha, kati ya mengineyo, ni kuwasaidiawaumini katika mahitaji ya kimwili. Kuwa na chakula, mahali pa kulala namavazi ndio mahitaji ya kimwili. Mashemasi humsaidia Askofu katikakushugulikia mahitaji ya kimwili ya Kanisa kwa kukusanya matoleo yamfungo, kufanya kazi za miradi ya usitawi wa jamii na kutoa huduma kwawale walio na shida.

Hadithi ifuatayo juu ya kukusanya matoleo ya mfungo inaonyesha jinsishemasi mmoja alivyojifunza umuhimu wa jukumu hili. Tukio hili lilitokeamiaka mingi iliyopita wakati waumini walipokuwa wakitoa michango yachakula, nguo na mafuta kama matoleo ya mfungo ili igawanywe kwawenye shida.

“Kama shemasi, nilipewa kazi ya kukusanya matoleo kwenye mtaa wetu.Mtu mmoja mwenye ndevu na mtu wa makamo ambaye aliitwa Peter Reid,

30

Page 40: Wajibu na Baraka za Ukuhani

ndiye aliyekuwa msimamizi, na jukumu lake lilikuwa kuhakikisha kuwamatoleo ya mfungo yamekusanywa na kugawanywa kwa wale wenyeshida . . .

“Kazi yangu ilikuwa ni kutembelea kila nyumba katika mtaa wetu . . . nakuwapatia nafasi ya kutoa kitu kwa manufaa ya maskini. Nyumba mojainatoa kiasi kikubwa cha mkaa, nyingine inatoa kuni, nyingine unga,kikombe cha sukari, kipande cha nyama ya nguruwe na vinginevyo . . .

“Jumamosi moja timu yetu ya wacheza kandanda ilikuwa na mchezouliokuwa umepangwa nami nilikuwa na hamu ya kucheza. Nilijua kwambailikuwa kazi yangu kukusanya ‘matoleo ya mfungo’ na ingekuwa makosakama nisingefanya hivyo lakini nilitaka kucheza katika mchezo huo kulikokitu kingine chochote. Nilichagua starehe kuliko kazi, na nikachezakandanda . . .

“Mapema asubuhi siku iliyofuata, Kaka Reid alibisha hodi kwenye mlangowetu wa nyuma na kuniulizia mimi. Nilijisikia kuwa mwenye hatia—nilitakakukimbia na kujificha—lakini nilienda na kukutana naye nikiwanimeinamisha kichwa. Yote aliyosema ni: ‘Wilard, una nafasi tutembeekidogo pamoja?’

“Ilikuwa ni siku ya baridi.

“Nilienda naye, kwanza kwenye nyumba za mbao karibu na kona ya mitaaya First North na Third West. Aligonga pole pole kwenye mlango mmoja namwanamke mdogo maskini alifungua mlango.

“Alisema: ‘Kaka Reid, hatukupata chakula chetu jana na hatuna chochotenyumbani cha kula.’

“Kaka Reid alisema: ‘Nasikitika, Dada, lakini nina hakika kuwa kabla yamwisho wa siku tutakuwa na kitu cha kukupatia.’

“Tulienda kwenye mlango mwingine karibu na mwisho wa mlango. Majibuya kugonga mlango yalikuwa ni sauti iliyotuambia tuingie ndani.

“Tuliingia na kumkuta mzee mkongwe kitandani na mkewe. Alisema: ‘KakaReid, hatuna makaa kwa hivyo imetubidi tukae kitandani ili tupate joto.’

“Katika sehemu nyingine ya uwanja, tulisalimiwa na mama mdogoaliyekuwa na watoto wadogo waliojikunyata pamoja. Mtoto mchangaalikuwa akilia na wale watoto wengine walikuwa na machozi usoni.

“Hiyo ilitosha! . . .

“Nilikuwa karibu kulia—nilifadhaika sana kwa uzembe wangu wakutokutimiza kazi yangu . . . Watu wale walipata chakula na makaa yaojioni na mapema—na nilijifunza somo la thamani sana.” (“Program Outlinefor Teaching Observance of the Law of the Fast, 1965, pp. 19–20.)

Kukusanya matoleo ya mfungo, hata hivyo, ni moja tu ya njia za kuliangaliaKanisa. Njia nyingine yawezekana kuwa kumsaidia mjane kupanda bustani

31

Page 41: Wajibu na Baraka za Ukuhani

yake, kumwagilia maji na kupalilia. Wakati wa kuvuna tunaweza kumsaidiakwa kukusanya na kuhifadhi chakula. Kwa kufanya mambo haya,tunamsaidia yeye kukabiliana na mahitaji yake ya kimwili.

Onyesha picha ya 5-a, “Mojawapo ya kazi za shemasi ni kukusanya matoleo ya mfungo,” na5-b, “Kufanya kazi kama familia katika mradi wa usitawi wa jamii ni mojawapo ya njiamashemasi wanaliangalia Kanisa.”

Kuliangalia Kanisa pia inamaanisha kuwasaidia waumini kuzishika amri.

Tunawezaje kuwasaidia waumini kushika amri? (Tunaweza kufanya hayo kwa kuwafundishainjili kwa maneno na vitendo vyetu.)

Pata mshiriki wa darasa asome M&M 20:58–59. Ni njia gani zingine ambazo tunawezakuwatahadharisha, kuwafundisha na kuwaalika wote waje kwa Kristo?

Tunapowatahadharisha, kuwaalika na kuwafundisha tunakabiliana namahitaji ya kiroho ya waumini wa Kanisa. Njia moja wapo tunayowezakutumia ni kuzungumza Kanisani. Tunapojitayarisha kwa sala kuongeakatika Kanisa, Roho Mtakatifu atashuhudia ukweli wa maneno yetu kwawaumini. Njia nyiingine tunayoweza kutekeleza kazi hii ni kuwaarifuwaumini juu ya mikutano na kufanya kazi ya ualimu wa nyumbanitunapoombwa kufanya hivyo.

Njia moja takatifu zaidi tunayoweza kuwasaidia waumini kutimiza mahitajiyao ya kiroho ni kwa kupitisha sakramenti. Tunapofanya hivi, inatupasakuhisi Roho wa Bwana na umuhimu wa ibada. Kwa sababu tunatoasakramenti kwa watakatifu kwa niaba ya Bwana, inatupasa kuwa wastahiliili kuwa wawakilishi wake. Inatupasa kutenda na kuvaa kama vile yeyeangependa tutende na tuvae.

Kiongozi Mkuu mmoja alikumbuka utumishi wake kama shemasi kwamaneno haya: “Nakumbuka ni namna gani niliona heshima kushughulikakwenye utumishi mtakatifu, wa sakramenti. Nakumbuka jinsi wazazi wanguwalivyonifundisha kwamba mikono na moyo wangu inapaswa kuwa safi iliniweze kustahili kushiriki katika ibada hii.” (Victor L. Brown, “The AaronicPriesthood—A Sure Foundation,” Ensign, July 1972, p. 89–90.)

Tunapopitisha sakramenti katika njia inayostahili tunatekeleza kazi nyingineya shemasi. Kazi hiyo ni kurekebishana na kujengana (tazama M&M107:85). Kwa kuona kujitoa kwetu kwa dhati katika kazi yetu, wauminiwatarekebika na watakuwa na hamu kubwa ya kutekeleza wajibu wao.

Onyesha picha 5-c, “Kupitisha sakramenti ni jukumu takatifu.”

Ni mambo gani maalumu tuliyoyataja ambayo shemasi anaweza kufanya ili kutimiza witowake? Andika majibu haya kwenye ubao au kwenye chati. (Yanatakiwa kuwa pamoja namawazo yaliyoandikwa kwenye “Matayarisho ya Mwalimu.”)

32

5-a, Mojawapo ya kazi za shemasi ni kukusanya matoleo ya mfungo5-b, Kufanya kazi kama kikundi katika mradi wa usitawi wa jamii ni mojawapo

ya njia ambazo mashemasi wanatumia kuliangalia Kanisa5-c, Kupitisha sakramenti ni jukumu takatifu

Page 42: Wajibu na Baraka za Ukuhani

5-a

Page 43: Wajibu na Baraka za Ukuhani

5-b

Page 44: Wajibu na Baraka za Ukuhani

5-c

Page 45: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Jinsi Mashemasi Wanavyojifunza Majukumu YaoKama mashemasi tunaweza kulifunza majukumu yetu kwa njia nyingi nakatika mahali pengi. Njia moja ya kujifunza ni kupitia katika mafunzo yakibinafsi na sala. Kufanya hili, tunaweza kutafuta wakati na mahali ambapotunaweza kuwa pekee yetu ili kujifunza majukumu yetu kama yalivyoelezwakatika maandiko matakatifu na kusali ili tuweze kupata msaada katikakuelewa.

Pia tunajifunza kazi zetu nyumbani kutoka kwa wazazi au kaka zetuwakubwa. Kazi hizi zinaweza kufundishwa wakati wa jioni katika mkutanowa jioni ya familia. Somo hili pia linafundishwa siku ya Jumapili katikamikutano ya ukuhani na Raisi wa kikundi cha Mashemazi. Bwanaamemwamuru Raisi wa kikundi cha mashemasi kusimamia mashemasikatika kikundi chake na kuwafundisha majukumu yao (tazama M&M107:85). Anaweza kutusaidi sisi kuelewa majukumu yetu na namna yakutenda katika afisi ya Shemasi. Anaweza kufanya hivi kwa sababuamefundishwa kazi hizi na mshauri wa ukuhani au mmoja wa maaskofu auuRaisi wa tawi. (Pale ambapo vikundi vya ukuhani wa Haruni havipo,uaskofu, uRaisi wa tawi au afisa wa ukuhani husimamia ukuhani wa Harunina kufanya kazi za maRaisi wa vikundi vya ukuhani wa Haruni.)

Mojawapo ya njia bora za kujifunza kazi zetu ni kuzitekeleza. Wakatitunapotekeleza kazi zetu, tunazielewa vizuri zaidi na tunamfurahishaBwana. Na Bwana anapotufurahia, atatufunulia mambo mengi kupitia kwaRoho Mtakatifu. Kama mashemasi, inatulazimu kila mara kuwa wenyekustahi kuwa na Roho Mtakatifu.

Jinsi Jamii ya Mashemasi Huwasaidia MashemasiWana kikundi wanaweza kusaidiana katika njia nyingi. Tunapokutanapamoja wakati wa mkutano, tunaweza kushikiriana pamoja. Tunawezakusaidiana pia kujifunza kazi zetu na kupanga shughuli ambazozitatusaidia kuzifanya. Hii ni pamoja na kusaidia wana kikundi kukabilianana mahitaji yao ya kimwili, kujitayarisha na kutoa huduma ya umisionari,kufanya kazi ya historia ya vizazi na kubatizwa kwa niaba ya wafu,kuwaamsha vijana wa umri wa wana kikundi ambao hawaji kanisani kujakanisani na kujifunza injili. Kikundi kinatupa nafasi ya kufanya kazi pamojakatika kutimiza majukumu haya. Na kwa kufanya kazi zetu, tunasaidiakujenga ufalme wa Mungu.

Kupitia huduma ya kikundi chetu, tunaweza pia kupata uzoefu wa kukuakibinafsi katika injili. Tunakua kimaarifa tunapojifunza injili na kutekelezamajukumu yetu na tunaongeza uwezo wetu wa uongozi kwa kutumikakama maafisa wa kikundi.

Waulize washiriki wa darasa kusoma M&M 107:60–62, 85. Nani anatakiwa kusimamia kikundicha mashemasi? Kazi zake ni zipi?

36

Page 46: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Wale wenye mamlaka juu yetu huchagua Raisi wa jamii na kumwitaatumikie. Raisi halafu huchagua washauri wawili ambao ni lazimawaidhinishwe na kuitwa na wale wenye mamlaka. Mshauri wa jamiihuwafundisha maafisa hao kazi zao. Pia hufundisha somo la injili katikamkutano wa jamii. Maafisa wa kikundi huwaelekeza washiriki wa jamii juuya kazi zao za ukuhani. Katika njia hizi na nyingine zinazofanana nazowashiriki hujifunza jinsi ya kuliangalia Kanisa.

Kikundi chetu pia hutupa nafasi za kupata urafiki na msaada. Kamatumevunjika moyo au hatuna uhakika juu ya ukweli, tunaweza kutiwa moyona kupata majibu ya matatizo yetu kutoka kwenye kikundi. Hadithi ifuatayoinatuonyesha jinsi tunavyoweza kujengana kwa kuonyesha hali ya kuwajaliwenzetu. Katika kisa hiki, kujali kulionyeshwa kwa mshiriki ambaye hajimara kwa mara katika mikutano ya Kanisa.

Shemasi mmoja alikuwa hashiriki sana katika Kanisa, hii inamaanisha kuwahakuhudhuria mikutano ya Kanisa. Jumapili kwa kawaida alikuwa akifanyakazi hapo nyumbani. Mara nyingi, alifikiria kuhusu mkutano wa ukuhani naakahisi kuhitaji ushiriki. Lakini kwa sababu hakuna yeyote aliyemkaribishakuhudhuria mkutano alijiona kuwa hapendwi. Jumapili moja, alipokuwaakipaka rangi chumba katika nyumba yao, uRaisi wa jamii ya mashemasiwalimtembelea. Walimuuliza kama angependelea kuhudhuria mkutano waukuhani Jumapili itakayofuata. Alisema hapana. Jibu lake lingewezakuwavunja moyo lakini walikataa kushindwa. Watatu hao waliendeleakumtembelea kila jumapili wakiwa na maneno hayo hayo.

Hata hivyo kijana huyu ambaye hakuwahi kufika Kanisani kama shemasi,upendo na kujali kwa uRaisi wa kikundi kulimjenga na kumfanya apatemawazo moyoni. Fikira hizi zilimtia moyo alipokuwa mkubwa kulitafutaKanisa. Hivi leo anashiriki katika Kanisa na kufanya kazi zake za ukuhani.

MwishoTunapojifunza kazi zetu na kukuza ukuhani wetu kama mashemasi,tunajijenga sisi wenyewe na kuwasaidia wengine kufanya hivyo hivyo. Hiindiyo maana ya “kuliangalia kanisa, na kuwa mhuduma aliyesimama katikakanisa” (M&M 84:111).

Changamoto1. Ishi kulingana na injili na kuwa mfano mzuri wa mwenye ukuhani.

2. Jifunze na kuomba kuhusu Maandiko Matakatifu yanayotufundishakuhusu majukumu ya shemasi.

3. Kusanya matoleo ya mfungo tunapoombwa kufanya hivyo.

4. Kuwa mnyenyekevu wakati wa ibada ya Sakramenti na wakati wakupitisha sakramenti, tenda na kuvaa kama vile mwakilishi wa Bwanaanavyopaswa kuvaa na kutenda.

37

Somo la 5

Page 47: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Maandiko Matakatifu ZaidiTimoteo 3:8–10 (sifa za shemasi)

M&M 84:30–32 (afisi ya shemasi kama kiambatisho cha ukuhani mdogo)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 20:38–60 na M&M 107.

2. Jitayarishe kuandika kazi za shemasi zifuatazo kwenye ubao wakati wa mjadala darasani.Kama ubao haupatikani andika kwenye chati.

Majukumu ya Shemasi

1. Kuliangalia Kanisa

2. Kupitisha sakramenti

Njia za Kutekeleza Majukumu

1. Fundisha injili kwa maneno na vitendo

2. Julisha washiriki kuhusu mikutano

3. Wasaidie washiriki wenye shida za kimwili kwa—

A. Kukusanya matoleo ya mfungo

B. Kufanya kazi katika miradi ya usitawi wa jamii

4. Kubali kazi ya kupitisha sakramenti

38

Page 48: Wajibu na Baraka za Ukuhani

39

Somo la 6Kazi za Mwalimu

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kufahamu majukumu yamwalimu.

Majukumu ya MwalimuKazi zetu kama walimu zinajumulisha kazi zote za shemasi. Tutakuwadaima na mamlaka na majukumu ya shemasi bila kujali ni afisi gani yaukuhani tunayoshikilia. Vivyo hivyo, wakati tunapotawazwa kuwa makuhani,kazi zetu zitakuwa ni pamoja na zile za shemasi na mwalimu. Kwa vilewengine wetu ni walimu na wengine watakuwa siku moja, inatupasakujifunza kazi za afisi hiyo.

Waulize washiriki wa darasa kusoma M&M 20:53. Ni zipi baadhi ya kazi za mwalimu? Andikamajibu kwenye ubao. (Yafaa ziwemo pia zile zilizoandikwa kwenye “Matayarisho ya Mwalimu”yaliyo mwisho wa somo hili.)

Kuwa pamoja na waumini na kuwaimarisha inamaanisha kupata kuwajua,kushiriki pamoja nao katika shughuli za Kanisa, kuwasaidia katika kutimizamahitaji yao na kuwasaidia ili waweze kuwahudumia wengine.

Waeleze washiriki wa darasa kusoma M&M 20:54–55. Ni zipi kazi nyingine za mwalimu?Orodhesha majibu kwenye ubao.

Mstari wa 54 unatuambia kwamba walimu wanatakiwa kujenga umoja naupendo kati ya waumini wa Kanisa. Tunaweza kufanya hivi kwa kuwasaidiakusuluhisha tofauti zao na kuwatia moyo katika kuwatumikia wenzao.Mstari wa 55 unatuambia sisi kwamba walimu pia wanapaswa kuwasaidiawaumini kutimiza wajibu wao.

Mwalimu Anatekelezaje Kazi Zake?Kuna njia nyingi ambazo mwalimu anaweza kutekeleza majukumu yake.Anaweza kuweka mfano wa kufaa, kuwa mwalimu mzuri wa nyumbani,kuwasalimu waumini kanisani, kutayarisha sakramenti, kusaidia katikanyumba na kuwa mtengeneza amani.

KUWEKA MFANO WA KUFAA

Njia moja ambayo tunaweza kuwaimarisha waumini ni kupitia kwa mfanowetu. Alma, katika maongezi na mwanawe Koriantoni, alimwambiakwamba wakati Wazoramu walipoona mwenendo wake wa kidhambi,“hawangeweza kuamini katika maneno yangu” (Alma 39:11). Maisha yetu,kama ya Koriantoni, yanaweza kuwaongoza wengine bila kujali mahalitulipo au kile tunachofanya. Ni muhimu kwamba tuwe mfano mzuri wauadilifu wakati wote na mahali popote.

Page 49: Wajibu na Baraka za Ukuhani

KUWA MWALIMU MZURI WA NYUMBANI

Onyesha picha 6-a, “Ualimu wa nyumbani ni kazi muhimu ya mwalimu.”

Tunaweza kukuza miito yetu ya kufundisha na kuwaimarisha waumini kwaufundishaji wa nyumbani. Katika kutekeleza jukumu hili inatupasakukumbuka kwamba tuna haki ya kupata maongozi ya Bwana. Bwanaamesema kwamba wale wote ambao wametawazwa kuhubiri injiliwanatakiwa kufanya hivyo kwa “Roho, hata Mfariji aliyetumwa kufundishaukweli” (M&M 50:13–14).

Tunawezaje kujua kile ambacho tutafundisha familia tulizopangiwa kufundisha?

Mwalimu wa nyumbani aliyemfundisha Nabii Joseph Smith na familia yakeanatuonyesha katika hadithi ifuatayoni nini tunachotakiwa kufanya kwa ajiliya wale tunaowafundisha.

“Nilijisikia udhaifu wangu katika kumtembelea Nabii Joseph Smith nafamilia yake katika kiwango cha mwalimu. Nilikuwa karibu kukinyaa kutokakwa kazi yangu. Mwishowe nilienda kwenye mlango wake na kubisha nadakika ile ile Nabii alikuja mlangoni. Nilisimama hapo nikitetemeka nanikamwambia:

“ ‘Kaka Joseph, nimekuja kukutembelea katika kiwango cha mwalimu wanyumbani, kama unayo nafasi.’

“Alisema, ‘Kaka William, ingia ndani, nina furaha sana kukuona; kaa chinikatika kiti kile pale na nitaenda kuita familia yangu.’

“Na punde si punde waliingia ndani na kukaa kwenye viti. Halafu akasema,‘Kaka William, nimejiweka na familia yangu chini ya mikono yako”, nandipo akakaa chini. ‘Sasa Kaka William,’ alisema ‘uliza maswali yoteunayojisikia kuuliza.’

“Kufikia wakati huo, hofu yangu yote na kutetemeka kulikuwa kumeisha nanikasema, ‘Kaka Joseph, unajaribu kuishi kulingana na dini yako?’

“Alijibu ‘Ndiyo.’

“Halafu nikasema ‘Unasali katika familia yako?’

“Alisema ‘Ndiyo.’

“ ‘Unaifundisha familia yako kanuni za injili?’

“Alijibu ‘Ndiyo, ninajaribu kufanya hivyo.’

“ ‘Unaomba baraka kwa chakula chenu?’

“Akajibu ‘Ndiyo.’

“ ‘Unajaribu kuishi kwa amani na maelewano na familia yako yote?’

“Alisema kwamba anafanya hivyo.

40

6-a, Ualimu wa nyumbani ni kazi muhimu ya mwalimu

Page 50: Wajibu na Baraka za Ukuhani

6-a

Page 51: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Halafu nikamgeukia Dada Emma, mke wake, na nikasema ‘Dada Emma,unajaribu kuishi kulingana na dini yako? Unawafundisha watoto wako kutiiwazazi wao? Unajaribu kuwafundisha wao kusali?’

“Kwa maswali haya yote alijibu ‘Ndiyo, ninajaribu kufanya hivyo.’

“Halafu nikamgeukia Joseph na kusema, ‘Sasa nimemaliza maswali yangukama mwalimu; sasa kama una mashauri ya kunipatia, nitakuwa na furahakuyapokea.’

“Alisema ‘Mungu akubariki, Kaka William; na kama wewe ni mnyenyekevuna mwaminifu, utapata nguvu za kutatua matatizo yote yale yatakayokujambele yako katika nafasi ya mwalimu.’

“Halafu nikamuachia baraka zangu za mwisho juu yake na familia yake,kama mwalimu, na nikaondoka.” (William Farrington Cahoon, “Recollectionsof the Prophet Joseph Smith,’ Juvenile Instructor, Aug. 15, 1896, pp.492–93.)

Kama mwalimu huyu wa nyumbani, tunaweza kuziimarisha familiatulizopangiwa kufundisha nyumbani kwa kuomba pamoja nao, kuwahimizakatika kutekeleza majukumu yao ya kifamilia na kuwafundisha kuishikulingana na injili. Kama familia tunazozifundisha zinahitaji msaada,inatupasa kuripoti mahitaji yao kwa viongozi wetu wa ukuhani.

Tunapotembelea familia tulizopangiwa, ni lazima tukumbuke kwambatunafanya hivyo kwa ruhusa ya viongozi wa familia hizo. Kwa sababu waondio wana wajibu kwa Bwana kwa familia zao, inatupasa kila marakufundisha familia zao chini ya mashauri yao. Ni kwa kufundisha chini yamashauri yao tu ndio tunaweza kutimiza kazi zetu kama walimu.

Tunapofanya ufundishaji wa nyumbani jinsi Bwana anavyotaka tufanye,tunajenga upendo na umoja katika Kanisa. Hadithi ifuatayo ni mfano mzuriwa kile kinachoweza kutokea endapo tunachukulia wito wetu kama walimukwa uzito unaostahili:

“Hivi majuzi . . . mwanamume mmoja na mwanawe wa umri wa mwalimuwalipangwa kuwa walimu wetu wa nyumbani. Tulijua juhudi za baba huyokatika injili lakini hatukujua kile ambacho tungetarajia kutoka kwa mwanaweingawaje maumbile na tabia ya kijana huyo yalikuwa yakionyesha juhudikama ya baba yake. Walipotutembelea mara ya kwanza, nilimwangalia sanakijana huyu. Ijapokuwa alinyamaza kama kawaida yake, kila kitu alichofanyaau kusema kilileta heshima kwa ukuhani aliokuwa nao. Punde walijuakwamba kijana wetu mdogo alikuwa ameaga dunia mwaka mmoja uliopitana kwamba tulikuwa tunamtarajia mtoto mwingine. Kutoka wakati huowalikuwa sehemu muhimu ya maisha yetu kwa kutuombea na kututia moyo.Mwishoni mwa matembezi hayo ya mara ya kwanza, nilimwomba kijana

42

Page 52: Wajibu na Baraka za Ukuhani

huyu asali. Katika sala yake alimwomba Bwana atusaidie katika msiba wetuna kumbariki mtoto ambaye alitazamiwa kuzaliwa karibuni. Alisali kuwa mkewangu asipate shida atakapokuwa akijifungua mtoto huyu. Mke wangunami tulishangazwa na uaminifu na busara ya mwalimu huyu kijana. Katikasiku na wiki zilizofuata, ndugu hawa walitujulia hali kila mara (zaidi ya maramoja kwa mwezi). Kufuatia kuzaliwa kwa mtoto, kijana huyu na babakewalileta zawadi. Tulipopiga magoti zote katika sala, yule mwalimu alitoashukrani kwa Bwana kwa kumuwezesha mke wangu kujifungua mtotosalama.” (As retold by H. Burke Peterson in “The Role of theTeacher,” NewEra, May 1974, pp. 10–11.)

Tunaweza kufanya nini ili tuwe walimu wazuri wa nyumbani?

SALIMIA KANISANI

Tunaweza kukuza wito wetu kwa kuwa mfano mzuri kwa kusalimia wauminiwanapoingia kwenye jumba la mkutano. Tunawasalimu kwa mkono nakuwajulia hali zao. Tunapowakaribisha mlangoni kwa aina hii ya ukarimu naurafiki tunasaidia kuongeza upendo na umoja kati ya waumini.

KUTAYARISHA SAKRAMENTI

Mwokozi alitufundisha kwamba utumishi halisi ni kufanya kitu bila kutarajiapongezi. Kutayarisha sakramenti ni mfano mzuri wa kanuni hii. Wauminimara nyingi hawafahamu kwamba walimu hutayarisha sakramenti. Kwa vilemara nyingi hutayarishwa bila pongezi yoyote kutolewa kwa walewalioitayarisha. Hata hivyo, huduma hii hufanywa na Bwana hupendezwakwa sababu ni huduma ya kweli.

Tunaweza kufanya nini ili kujitayarisha sisi wenyewe kimwili na kiroho ili kutayarishasakramenti? (Weka pia wazo la kuwa wasafi kimwili.)

SAIDIA NYUMBANI

Kama walimu tunaweza pia kusaidia familia zetu wenyewe. Ni muhimukusaidia kusafisha na kutengeneza nyumba, kutunza bustani na kufanyakazi za nyumbani. Juu ya hayo, tunaweza kusaidia familia zetu kuishikulingana na injili.

Onyesha picha 6-b, “Mwalimu anayekuza wito wake wa ukuhani husaidia katika kuimarishafamilia yake.”

Hadithi imetolewa ya mwenye ukuhani asiyeshiriki kikamilifu aliyevutasigara na hakuchukua hatua muhimu za kumpeleka mke wake na kijanawake wa kiume kuunganishwa naye hekaluni. Mwanawe alivutiwa sana nafamilia ya milele asubuhi moja baada ya kusikiliza somo katika ukuhanikuhusu ndoa ya hekaluni. Somo hilo lilimuongoza kijana huyukuzungumuza na babake kuhusu jambo hilo. Matokeo ya mazungumzoyao ni Kwamba, maisha ya mtu huyo yalibadilika. Baba huyo alifahamu

43

Somo la 6

Page 53: Wajibu na Baraka za Ukuhani

6-b

Page 54: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kuwa alimpenda mwanawe na alitaka kuwa naye milele—Hatimaye, familiailiunganishwa hekaluni kwa muda na milele kwa sababu ya mmoja katikafamilia, mwalimu, aliyependelea kujenga upendo na umoja katika familiayake.

KUWA MTENGENEZA AMANI

Tunatimiza wajibu wetu kama walimu kwa kuwa watengeneza amani katikafamilia zetu na katika Kanisa. Njia moja ya kufanya hivi ni kutafuta mazurikutoka kwa wengine. Jinsi tunavyotafuta mazuri kutoka kwa wengine,tunaimarisha staha zao. Njia nyingine ni kuepukana na masengenyo nauvumi ambao unaweza kuharibu sifa za mtu mwingine na kila marakutumia upendo na ukarimu katika mwenendo wako na wenzako. Viletunavyoendeleza vyombo hivi na kuvitumia, tutaweza kuwasaidia watuwengi kupata amani katika maisha yao.

MwishoKama walimu, inatupasa kila mara kujaribu kuliimarisha Kanisa, kujengaumoja na upendo na kusaidia waumini kufanya kazi zao. Ingawajetunaweza kuwa wachanga au waongofu wapya katika Kanisa, tuna nguvuza kuwashawishi wengine kwa mazuri. Inatupasa kila mara kukumbukakwamba Bwana hatupi amri, “ila atatengenza njia [kwetu ya] kutimiza kilekitu ambacho ametuamuru” (1 Nefi 3:7).

Panga pamoja na darasa mradi maalum wa huduma ambao unaweza kusaidia kujengaumoja na upendo katika kitengo chenu katika kanisa.

Changamoto1. Kwa sala angalia mahitaji ya familia ulizopangiwa.

2. Tayarisha ujumbe unaofaa kwa mahitaji ya kila familia kama vile Rohoanavyoongoza.

3. Tembelea familia uliyopangiwa na mwalimu mwenzako wa nyumbanimapema katika mwezi.

4. Sali na familia ulizopangiwa.

5. Fanya huduma ambazo unaweza kufanya ambazo zinahitajika nafamilia zako ulizopangiwa. Wajulishe viongozi wa kikundi cha ukuhanikwa yale ambayo hauwezi kufanya.

Maandiko Matakatifu ZaidiYakobo 1:17–19 (namna walimu wanavyopaswa kukuza miito yao yaukuhani)

45

Somo la 6

6-b Mwalimu ambaye anakuza mwito wake wa ukuhani husaidia kuimarisha familia yake

Page 55: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 20:53–60 na somo la 4, “Jamii la Ukuhani.”

2. Pata chaki na ubao.

3. Jitayarishe kuorodhesha kazi zifuatazo za mwalimu katika ubao au chati wakati wa mjadaladarasani:

Kazi za Mwalimu

1. Fanya kazi yoyote ya shemasi.

2. Kuwa nao na kuimarisha Kanisa.

3. Jenga umoja na upendo katika Kanisa.

4. Saidia waumini kufanya kazi zao.

4. Wape nafasi washiriki wa darasa ili watoe hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

46

Page 56: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kazi za Kuhani

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kufahamu kazi za makuhani.

UtanguliziBwana ameamuru kila mwenye ukuhani “kusimama katika afisi yake nakufanya kazi katika mwito wake” (M&M 84:109). Kufanya hivi, ni lazimakwanza tujifunze na halafu tutekeleze majukumu yetu tofauti katikaukuhani. Kama makuhani, kazi zetu ni pamoja na kufundisha, kubatiza,kusimamia sakramenti, kuwatembelea waumini na kuwatawaza wenginekatika ukuhani. Tunapofanya kazi hizi, hatusaidii tu katika ujenzi wa ufalmewa Mungu bali tunajitayarisha wenyewe kupokea ukuhani wa Melkizedeki.Tunapopokea ukuhani wa Melkizedeki na kutawazwa katika afisi ya mzee,tunaweza kuitwa kuhudumu katika misheni. Kufaulu kwetu kamawamisionari, hata hivyo, kutategemea jinsi tulivyojitayarisha kutumika.Tunaweza kujitayarisha kutumika kama wamisionari wazuri kwa kuikuzamiito yetu kama makuhani.

Kazi za KuhaniBwana amewapatia makuhani kazi nyingi za kufanya, zikiwemo kazi zashemasi na walimu. Kazi maalumu za kuhani zinapatikana katikaMafundisho na Maagano.

Waulize washiriki wa darasa kusoma na kuweka alama M&M 20:46–48. Kazi za kuhani ni zipi?Andika majibu kwenye ubao. (Hizi ni pamoja na kazi zilizoandikwa chini ya “Matayarisho yaMwalimu” katika mwisho wa somo hili.

FUNDISHA

Mojawapo ya kazi zetu kama makuhani ni “kuhubiri injili, kufundisha,kufafanua, kuonya” (M&M 20:46). Hii inamaanisha kwamba tunatakiwakuwafundisha wengine kanuni za injili. Ili tufundishe kanuni za injili, nilazima kwanza tujifunze ni zipi. Bwana alisema: “Msitafute kulitangazaneno langu, ila kwanza litafuteni neno langu, na halafu ndipo ulimi wakoutafunguliwa; halafu, kama unapenda, utakuwa na Roho wangu, ndiyo,nguvu ya Mungu kwa kuwashawishi wanadamu” (M&M 11:21).

Tunapata neno la Mungu katika njia nyingi. Tunalipata nyumbani kutokakwa wazazi wetu, katika vikundi vyetu vya ukuhani, kutoka kwa walewanaotufundisha, katika shule ya Jumapili, na katika mkutano wasakramenti.

47

Somo la 7

Page 57: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Moja ya njia bora za kujifunza neno la Mungu ni kupitia mafunzo ya binafsiya maandiko matakatifu ya kila siku. Pasiwepo mwenye ukuhani ambayeana shughuli nyingi kiasi cha kukosa wakati wa kujifunza maandikomatakatifu. Kadiri tunapopekua na kutafakari kuhusu maandiko matakatifu,Bwana atatusaidia kuyafahamu. Mara, tunapofahamu injili, tutawezakuwafundisha wengine.

Tunaweza pia kutimiza kazi zetu za kufundisha wengine injili kwa kuwamfano mwema. Mara nyingi mfano wetu mwema unawatia moyo wenginekuishi kulingana na injili.

Ni mambo gani maalumu ambayo tunaweza kufanya ili tuweze kufundisha injili?

Onyesha picha 7-a, “Kuhani anapombatiza mtu, mtu yule huingia katika ufalme wa Mungu.”

KUBATIZA

Kazi nyingine ambayo makuhani wanayo ni kubatiza (tazama M&M 20:46).Ubatizo kwa mamlaka sahihi ni muhimu sana na ni moja ya ibada muhimuna takatifu katika Kanisa, kwani ni ibada ambayo kwayo tunaingia katikaufalme wa Mungu. Ni jukumu takatifu la kuhani kufanya ibada hii ya kuokoawakati anapopewa kibali na wale walio na mamlaka juu yake.

Onyesha picha 7-b, “Makuhani wanalo jukumu takatifu la kuhudumia sakramenti kwawaumini.”

KUSIMAMIA SAKRAMENTI

Heshima ya kusimamia sakramenti imetolewa hasa kwa makuhani. Ibadahii hufanyika kwa kutoa sala za sakramenti. Kama makuhani, inatupasakujua sala za sakramenti, kuvaa mavazi yanayofaa na kunawa mikono yetukabla ya kufanya ibada hii. Juu ya yote, inatupasa kuwa wenye kustahilikufanya ibada hii takatifu, kwani sisi ni wawakilishi wa Bwana.

KUWATEMBELEA WAUMINI

Bwana amewaamuru makuhani “kutembelea nyumba ya kila muumini nakuwahimiza kusali kwa sauti na kwa faragha na kufanya kazi zote zafamilia” (M&M 20:47). Tunaweza kutimiza haya tunapofanya mafundisho yanyumbani kwa familia ambazo tumepangiwa. Wakati wa matembezi hayo,tunaweza kujua mahitaji ya wana familia. Tunaweza kusali pamoja nao.Tunaweza kuwafundisha kanuni za injili na kuwatia moyo kufanya kazi zaoza kifamilia. Tunaweza kuwa marafiki wa wana familia katika mikutano yaKanisa letu na katika ujirani. Tunaweza kushirikiana nao katika shughuli zakanisani, shuleni na mtaani.

48

7-a, Wakati kuhani anapobatiza mtu, mtu huyo huingia katika ufalme wa Mungu

7-b, Makuhani wana jukumu takatifu la kusimamia sakramenti kwa waumini wa Kanisa

Page 58: Wajibu na Baraka za Ukuhani

7-a

Page 59: Wajibu na Baraka za Ukuhani

7-b

Page 60: Wajibu na Baraka za Ukuhani

KUWATAWAZA WENGINE

Makuhani pia wana mamlaka ya kuwatawaza makuhani wengine, walimuna mashemasi (tazama M&M 20:48), wanaweza tu kufanya hivi baada yakupokea ruhusa kutoka kwa mwenye mamlaka ya ukuhani juu yao ambaowanayo mamlaka au funguo za kutoa ruhusa. Uwezo huu wa kuwapatiawengine ukuhani ni mtakatifu. Ulirejeshwa ulimwenguni na YohanaMbatizaji alipowatawaza Joseph Smith na Oliver Cowdery katika ukuhaniwa Haruni (tazama M&M 13). Yohana Mbatizaji alipewa mamlaka yaukuhani na malaika akifanya hivyo kwa niaba ya Mungu (tazama M&M84:28). Kwa hiyo, uwezo wa kuwatawaza wengine unakuja kwetu, kutokakwa Mungu. Kufanya ibadi hii muhimu, tunapaswa kuwa wenye kustahili nakuwa na Roho Mtakatifu pamoja nasi. (Kwa maelezo zaidi tazama Sura ya3, “Urejesho wa Ukuhani.”)

Onyesha picha 7-c, “Kuwasaidia wamisionari ni wajibu na ni heshima.”

KUWA MMISIONARI

Wito wa kuhani pia ni pamoja na kusaidia katika kazi za umisionari. Witohuu ulikuwa ni sehemu ya Kanisa la kale na Joseph Smith aliamriwa naBwana kwamba washiriki wa ukuhani wa Haruni wa siku hizi piawanatakiwa kuwasaidia wazee na misheni zao. Kazi yao maalumu nikuweka ahadi na kutayarisha njia kwa ajili ya wazee. (Tazama M&M84:107–108.) Tunaweza kusaidia katika kazi ya umisionari siku hizi kwakuwasaidia wamisionari katika eneo letu kwa kutafuta familia za kufundishana kuweka ahadi na familia hizo. Tunaweza pia kusaidia katika kazi yaumisionari kwa kujitayarisha sisi weyewe kuwa wamisionari.

Kukuza Miito Yetu Ya UkuhaniKama makuhani, inatupasa kujifunza kazi zetu za kufundisha, kubatiza,kusimamia sakramenti, kutembelea waumini, kutawaza wengine nakusaidia katika kazi ya umisionari. Katika kujifunza na kufanya kazi hizi,tunayo haki ya kupata ulinzi na mwongozo wa Bwana. Raisi WilfordWoodruff, ambaye alitumikia misheni kama kuhani pamoja na mzee kamamwenzi wake, alisema hivi juu ya misheni yake:

“Nilienda kama kuhani na mwenzangu kama mzee na tulisafiri maelfu yamaili na mambo mengi yalijitokeza kwetu. Ninataka kusisitiza ukweli huukwako ya kwamba haina tofauti yoyote kama mtu ni kuhani au mtume,kama anaukuza mwito wake. Kuhani anashikilia funguo za kutumikiwa namalaika. Haijapata kuwa katika maisha yangu kama Mtume kama Sabiiniau kama Mzee kuwa nilipata ulinzi zaidi wa Bwana kuliko niliposhikilia afisiya kuhani. Bwana alinifunulia kwa maono kwa ufunuo na kwa RohoMtakatifu mambo mengi yale yaliolala mbele yangu.” (Millenial Star, Oct.1891, p. 629.)

51

Somo la 7

Page 61: Wajibu na Baraka za Ukuhani

7-c

Page 62: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Askofu Victor L. Brown alielezea tukio lifuatalo juu ya jinsi makuhaniwanavyopaswa kukuza miito yao:

“Kijana . . . aliandika yafuatayo: ‘Wakati mmoja nilihudhuria kata ambayohaikuwa na mwenye ukuhani wa Melkizedeki. Lakini haikuwa imefifia kirohokwa njia yoyote. Kwa kinyume, wengi wa waumini wake walishuhudiaonyesho kubwa sana la nguvu za ukuhani ambalo hawajawahi kuona kamwe.

“ ‘Uwezo huu ulikuwa kati ya makuhani. Kwa mara ya kwanza katikamaisha yao waliitwa kufanya kazi zote za ukuhani na kusimamia shida zawaumini wenzao katika kata. Waliitwa kuwa walimu wa nyumbani—na siotu kuwafuata wazee na kutimiza tu wajibu lakini kubariki kaka na dada zao.

“ ‘Kabla ya wakati huu niliwahi kuwa na wanne kati ya makuhani hawakatika mazingira tofauti. Hapo niliwachukulia kuwa ni majambazi wakawaida. Walimfukuza kila mwalimu wao wa seminari baada ya miezi miwiliau mitatu. Walizusha zogo nchini kote katika safari za maskauti. Lakiniwalipohitajika—wakati walipoaminiwa kwa kazi muhimu—walikuwamiongoni mwa wale waliongara zaidi katika utumishi wa ukuhani.“ ‘Siri ilikuwa kwamba askofu alitoa mwito kwa makuhani wake wa Haruniwasimame wima kama wanaume ambao malaika kweli wangewezakuwatokea; nao walisimama wima, wakisimamia misaada kwa wale ambaowangekuwa na shida na kuwaimarisha wale waliohitaji kuimarishwa. Sio tuwaumini wengine wa kata walioimarishwa lakini pia wana kikundi chaukuhani wenyewe. Ushirikiano mkubwa ulisambaa katika kata yote na kilamuumini alianza kuonja ni nini watu kuwa na nia moja na moyo mmoja.Hakukuwa na lolote lisiloelezeka katika haya yote. Ulikuwa ni matumizimazuri ya ukuhani wa Haruni.’ ” (“The Vision of the Aaronic Priesthood,”Ensign, Nov. 1975, p. 68.)

Uliza washiriki wa darasa kuelezea matukio ya manufaa ambayo wamepata katika kufanyakazi zao za ukuhani.

Kujitayarisha Kuwa Mmisionari Mwenye MafanikioKama tutafanya kazi zetu zote kama makuhani, tutapata uzoefu katikamambo ambayo tutafanya kama wamisionari: Tutafundisha injili kamawamisionari, tutabatiza waongofu, tutasimamia sakramenti wakatimwingine, tutawatembelea waumini na kuwatawaza wengine katikaukuhani. Tunapotekeleza majukumu haya, tutaimarika kiroho na tutakuwatumejifundisha vyema kutumika kama wamisionari wakati tutakapoitwa.

Mojawapo ya madhumuni ya ukuhani wa Haruni ni kuwatayarisha walewanaoushikilia kupokea ukuhani wa Melkizedeki. Wale makuhaniwanaostahili na ambao wanaukuza ukuhani wa Haruni watapokea ukuhaniwa Melkizedeki na kutawazwa katika afisi ya Mzee.

53

Somo la 7

7-c, Kuwasaidia wamisionari ni wajibu na heshima

Page 63: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kwa sehemu kubwa, kazi ya umisionari hutekelezwa na wazee. Wengi wetuambao tuna ukuhani wa Haruni tukistahili tutatawazwa kuwa wazeetunapofikia umri wa miaka kumi na minane. Hii inatupatia mwaka mmojawa kujifunza na kujizoeza kazi za mzee na kujitayarisha kutumikia katikamisheni. Matayarisho haya ni pamoja na kuweka mioyo yetu katika mamboya Mungu, kumtumikia Bwana na kuwasimamia wengine kwa uadilifu(tazama M&M 121:34–38). Tunapofanya mambo haya, tutajifunzakumwamini Bwana na kadiri tunavyomwamini Bwana, yeye atatusaidia nakutulinda katika majaribio na mateso yetu.

Wilford Woodruff alisema juu ya wakati ambao maisha yake yalilindwa naBwana. Siku moja aliongozwa na Roho ili amuonye muasi kwa jina la BabaHakeman, ambaye alisema Kitabu cha Mormoni kilitoka kwa Shetani. KakaWoodruff alisema:

“Nilichomwa moyoni mara tatu ili niende kumuonya Baba Hakeman . . .Mara ya tatu nilikutana naye, nyumba yake ilionekana kuwa imejaa pepowaovu, na nilitaabika Rohoni juu ya ono hili. Nilipomaliza onyo langu,nilimwacha. Alinifuata kutoka nyumbani kwake kwa nia ya kuniua. Sikuwana shaka juu ya nia yake kwa vile nilikuwa nimeonyeshwa katika maono.Alipofika mpaka pale nilipokuwa, alianguka na kufariki miguuni pangukama kwamba amepigwa na radi kutoka mbinguni. Wakati huo nilikuwakuhani lakini Mungu alinikinga na kuyalinda maisha yangu.” (TheDiscourses of Wilford Woodruff, pp. 297–98.)

Tukio la kupita kiasi kama hili laweza lisitokee katika maisha ya mwenyeukuhani mwadilifu. Hata hivyo, katika njia nyingi, zinazojulikana nazisizojulikana kwetu, Bwana huendelea kuwalinda watumishi wakewaaminifu.

Kwa nini ni muhimu kwa makuhani kujitayarisha na kupanga juu ya umisionari?

MwishoRaisi Spencer W. Kimball amesema, “Swali linaulizwa mara nyingi: Nilazima kila kijana atumike kwenye misheni? Na majibu yametolewa naBwana. Ni ‘ndiyo.’ kila kijana inampasa kutumikia katika misheni. Alisema:

“ ‘Watume wazee wa kanisa langu katika mataifa yote yaliyo mbali; . . .katika visiwa vya bahari; watume katika nchi za kigeni; nendeni kwamataifa yote, kwanza kwa mataifa, halafu kwa Wayahudi’ (M&M 133:8).”(“When the World Will Be Converted,” Ensign, Oct. 1974, p. 8.)

ChangamotoKiuaminifu fanya majukumu yako ya ukuhani wa Haruni ili—

1. Kuwaimarisha wana kikundi wenzako na kata au tawi.

2. Jitayarishe mwenyewe kupokea ukuhani wa Melkizedeki na kutumikakama mmisionari.

54

Page 64: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 20:46–49.

2. Pata ubao na chaki.

3. Tayarisha kuonyesha kazi zifuatazo za kuhani katika ubao au chati wakati wa majadilianodarasani:

Majukumu ya Kuhani

1. Kufanya kazi za shemasi na mwalimu.2. Fundisha injili.3. Batiza. 4. Simamia sakramenti.5. Tembelea waumini.6. Tawaza wengine katika ukuhani wa Haruni.7. Fanya kazi ya umisionari.

4. Pata washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

55

Somo la 7

Page 65: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kazi za Maaskofu na MaRaisi wa MatawiMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kazi za maaskofu namaRaisi wa matawi ili tuweze kujua namna ya kuwasaidia na kuwaungamkono.

UtanguliziKikundi cha msingi katika kanisa ni familia. Katika maeneo mengi dunianiambapo waumini wametawanyika, kila familia huwa kama kikundi chaKanisa. Chini ya uongozi wa mwenye ukuhani mwenye kustahili, familiainaweza kufanya mkutano wa sakramenti, familia zaweza kufanya Shule yaJumapili na mikutano mingine na kushugulika na shughuli nyingi ambazomakundi makubwa ya Kanisa hushugulika nazo.

Tawi la kanisa hutengenezwa wakati familia mbili au zaidi na watu binafsiwanaishi katika eneo na iwapo mmoja wa waumini ni kuhani mwenyekustahili au mwenye ukuhani wa Melkizedeki. (Tazama kitabu chamwongozo wa Tawi, p. 1). Tawi ni mfano mdogo wa kata na kwa kwelihutengenezwa kuwa kata wakati idadi ya waumini inapoongezeka.

MaRaisi wa matawi husimamia matawi; na Maaskofu husimamia kata.Kanisa linapoendelea kukua, wenye ukuhani wanaostahili zaidi huitwakwenye nafasi za madaraka katika uongozi. Wengi wao wana ujuzi mdogowa kikanisa na elimu ya Injili. Lakini ni wanyenyekevu na wanahitaji imani,maombi na kuungwa mkono na waumini wanaowatumikia.

Uteuzi wa Maaskofu na MaRaisi wa MatawiNani huwateua maaskofu? Askofu hushikilia ukuhani upi?

Askofu huitwa kulingana na maongozi ya Bwana na kutawazwa na Raisi wakigingi chini ya mashauri ya URaisi wa Kwanza wa Kanisa na jamii laMitume Kumi na Wawili (tazama M&M 68:14–15). Uaskofu wa Kataunajumulisha makuhani wakuu watatu—askofu na washauri wawili. Askofundiye kuhani mkuu msimamizi na husimamia waumini wote katika katayake. Zaidi ya hayo, yeye ni Raisi wa kundi la makuhani na kiongozi waukuhani anayewajibika kwa mambo ya kiroho na ya kimwili ya wasichanakatika kata. (Tazama M&M 107:13–17, 71–72.)

MaRaisi wa matawi wanaitwa kulingana na maongozi ya Bwana kuwawasimamizi wenye mamlaka juu ya matawi yao na Raisi wa Misioni auRaisi wa kigingi. Wanashikilia ukuhani wa Melkizedeki na hutumika pamojana washauri wake. Majukumu yao ni sawa na yale ya askofu.

56

Somo la 8

Page 66: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kumbukumbu za maandiko matakatifu zinazowataja maaskofu piazinamaanisha maRaisi wa matawi pia.

Waumini wengi wa kanisa huwaona askofu au Raisi wa tawi lao katikanafasi hizo kama msimamizi tu wa kata au tawi. Hawafahamu kuwa anakazi nyingine za kimwili na za kiroho na askofu au Raisi wa tawiasipoungwa mkono katika kazi hizi hawezi kutoa huduma kamilifu kwao.

Kazi za Kimwili Ya Maaskofu na MaRaisi wa MatawiMajukumu ya kimwili ni yale ambayo yanahusiana na hali njema ya kimwiliya waumini wa kata au tawi.

Jukumu moja la muhimu la kimwili ambalo maaskofu na maRaisi wamatawi wanalo ni kukusanya zaka na matoleo. Kama wawakilishi waBwana, askofu na Raisi wa tawi wanawajibika kwa Bwana katika kuipokea,kurekodi na kugawa matoleo haya. Matoleo ya mfungo hutolewa nawaumini waaminifu wanaofunga milo miwili mfulilizo kila mwezi ilikuwasaidia maskini. (Wale ambao hawajiwezi kimwili kufunga wanahitajikatu kutoa matoleo ya mfungo.) Askofu au Raisi wa tawi anawafahamuwaumini wa kata au tawi lake, na wakati wanapohitaji msaada anawezakuwasaidia kwa kutumia matoleo ya mfungo au kwa kuwaomba wauminiwa kata kusaidia. (Tazama M&M 84:112.)

Hadithi ifuatayo inaonyesha jinsi askofu alivyoisaidia familia katika shida:

“Chini ya barabara kuu inayotumiwa sana ambayo inazunguka jiji la SaltLake, kuna nyumba ya mwanamume mmoja mpweke wa miaka sitiniambaye kwa sababu ya ugonjwa wa kulemaza, alikuwa hajapata siku mojamaishani mwake iliyopita bila uchungu wala siku isiyo na upweke. Sikumoja katika majira ya baridi, nilipomtembelea, alichukua muda kujibukengele ya mlango. Niliingia katika nyumba yake iliyotunzwa vyema, hali yabaridi ilikuwa nyuzi 40 katika vyumba vyote ila katika chumba kimoja tu chajikoni. Sababu: ni ukosefu wa fedha za gharama ya kupasha joto vyumbavile vingine. Kuta zilihitaji kuwekwa karatasi, dari ilihitaji kuteremshwa namakabati yalihitaji kujazwa.

“Hangaisho na tukio la kumtembelea rafiki yangu, askofu alionwa kwaushauri na muujiza wa upendo uliosukumwa na ushuhuda ulitendeka.Waumini wa kata walikusanywa na kazi ya upendo ilianza. Mwezi mmojabaadaye, rafiki yangu Lou alinipigia simu na kuniuliza kamaningemtembelea kuona kilichotendeka kwake. Nilienda na kweli nilionamuujiza. Barabara ya kuingilia kwake iliyokuwa imeharibiwa na mizizi yamiti mikubwa iliyokuwa karibu ilikuwa imetengenezwa na sebule yanyumba ilikuwa imejengwa upya, mlango mpya wenye vitasa vya kung`arauliwekwa, dari liliteremshwa, kuta zikawekewa karatasi, mbao zikapakwarangi na paa likarejeshwa, na makabati yakajazwa. Nyumba haikuwa bariditena na isiyopendeza. Sasa ilionekana kama inanong`oneza ukaribisho wa

57

Page 67: Wajibu na Baraka za Ukuhani

ukunjufu. Lou alikombolewa mpaka mwishowe akanionyesha fahari nafuraha yake: juu ya kitanda chake kulikuwa na blanketi pana lenye urembona ilionyesha alama ya ukoo wa familia yake ya McDonald. Lilikuwalimefumwa kwa mikono ya upendo na ya kujali ya wanawake wa Jumuiyaya Kusaidiana ya akina Mama. Kabla ya kuondoka, niligundua ya kwambakila wiki, vijana walileta chakula cha jioni na kushirikiana naye katikamkutano wa jioni ya familia nyumbani.” (Thomas S. Monson, “The Way ofthe Lord,” Ensign, Nov. 1977, p. 9).

Maaskofu na maRaisi wa matawi wana kazi nyingine za kimwili kamakuweka rekodi za shughuli zote za Kanisa na kutunza majengo ya kanisana vifaa. Pia wanakusanya michango mingine kutoka kwa waumini waKanisa kama vile hazina ya kuwasaidia wamisionari.

Kazi za Kiroho za Maaskofu na MaRaisi wa MatawiMaaskofu na maRaisi wa matawi wanaitwa kutunza hali njema ya kiroho yawaumini katika matawi yao ya Kanisa. Wana kazi maalumu ya kuwa jaji wakawaida wa watakatifu wote (tazama M&M 107:74). Ili kuwasaidia katikakazi hizi, Bwana amewaahidi maaskofu na maRaisi wa matawi kipawa chautambuzi (tazama M&M 46:27).

Kipawa cha utambuzi kinamwezesha askofu au Raisi wa tawi kujua ukweli,kufahamu tofauti kati ya mema na maovu na hata kujua kile kilicho moyonimwa mtu. Kwa sababu ana kipawa hiki, tunaweza kuomba ushauri wakena anaweza kutuambia kile ambacho Bwana angependa sisi tufanye ilitusitawi kiroho.

Kupitia kipawa cha utambuzi, askofu katika hadithi ifuatayo aliwezakumsaidia kijana mmoja katika kata yake.

Craig, kuhani wa miaka 16, alikuwa kijana wa kuvutia. Alikuwa kila maratayari kufanya chochote alichoombwa na askofu wake. Siku moja, hatahivyo, askofu Wells alifahamu kuwa Craig alikuwa anamkwepa. Hatakwenye mkutano jamii ya makuhani, macho ya Craig daima yalikuwayanaangalia upande mwingine. Askofu Wells alikuwa anataka kumwitaCraig kama katibu jamii ya makuhani lakini alihisi kwamba kuna kituambacho si sahihi. Kwa hiyo alimuita Craig katika afisi yake kwamahojiano. Katika mahojiano, Craig aliungama alikuwa na kosa lakimaadili. Alisema kuwa aliona haya na kujisikia kutokuwa mstahilivu katikaukuhani wake. Askofu Wells alizungumza naye na kumhakikishia kwambaangeweza kutubu na kujisikia vizuri tena. Kupitia mazungumzo haya, Craigalijifunza jinsi ya kuyashinda matatizo yake, na kupitia toba, alisamehewana kuwa na furaha na shauku tena. Askofu Wells ndipo aliweza kumuitakuwa katibu wa familia ya makuhani.

Ni kwa namna gani kutumia kwa askofu kipawa cha utambuzi aliweza kumsaidia Craig kukuakiroho?

58

Page 68: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kwa sababu askofu au Raisi wa tawi ni jaji wa kawaida katika Israeli,tunaweza kuungama dhambi zetu kwake na anaweza kutusaidia kutubu.Wakati waumini wanapofanya dhambi nzito na hawatubu, wanawezakupoteza uanachama wao katika Kanisa. Katika mambo kama haya,askofu analo jukumu la kufanya kikao cha jamii la nidhamu. Katika majamiihaya, askofu hutoa hukumu na kuwasisitiza waumini hao kutubu. Majamiihaya ya nidhamu hufanywa katika upendo na yana kusudi la kuwasaidiawatu kutubu na kufurahia tena baraka za injili. (Tazama M&M 58:42–43 naM&M 58:14, 17–18). Kazi hii haiwezi kufanywa kirahisi kwa sababu askofuatawajibika kwa hukumu yake.

Wakati makosa ni lazima yashugulikiwe katika matawi yaliyo chini yamisioni, Raisi wa misheni ndiye atakayesimamia jamii la nidhamu (tazamathe General Handbook of Instructions).

Kazi nyingine za kiroho za maaskofu na maRaisi wa matawi ni pamoja nahizi zifuatazo:

• Kusimamia na kusaidia katika kupanga mikutano ya sakramenti.

• Kuelekeza ufundishaji wa nyumbani kwa familia zote.

• Kuendesha mikutano (kama vile kamati ya huduma ya usitawi wa jamii).

• Kuchagua na kuita waumini ili watumike katika nafasi mbali mbali katikakata au tawi.

• Kuidhinisha kutawazwa na kupanda daraja katika ukuhani wa Haruni.

• Kupendekeza akina kaka kupanda daraja la ukuhani wa Melkizedeki.

• Kuwahoji waumini ili wapokee kibali cha hekalu na baraka za BabaMkuu.

• Kuendesha mwafaka wa zaka.

• Kutoa baraka za faraja na ushauri.

• Kutayarisha mapendekezo ya wamisionari.

Kuwaunga Mkono Viongozi Wetu wa UkuhaniAskofu au Raisi wa tawi letu ameitwa na Mungu. Humwakilisha Bwana naRaisi wa Kanisa. Kwa sababu hii, ni muhimu kwamba tumuunge mkonokatika wito wake. Mzee Boyd K. Packer alisema, “Mtu ambaye anasemakuwa atamkubali Raisi wa Kanisa au Viongozi Wakuu wa Kanisa, lakinihawezi kumkubali Raisi wa tawi lake au askofu wa kata yakeanajidanganya. Mtu ambaye hawezi kumuunga mkono askofu wa katayake na Raisi wa kigingi lake hawezi kumuunga mkono Raisi wa Kanisa.”(Elder Boyd K. Packer, “Follow the Brethren,” Speeches of the Year, BYU,March 23, 1965, p. 4–5.)

Maandiko Matakatifu yanatufundisha sisi namna ya kuwaunga mkonoviongozi wa ukuhani.

59

Somo la 8

Page 69: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Waulize washiriki wa darasa kusoma pia kimoyo wakati Maandiko Matakatifu yanaposomwa.Baada ya Maandiko Matakatifu kusomwa, waulize washiriki wa darasa ni nini wanachoambiwatunaweza kufanya kwa kuwaunga mkono viongozi wetu.

MAANDIKO MATAKATIFU USHAURI

M&M 6:9 Fundisha toba na kuishi kulingana na amri

1Nefi 3:7 Kubali na timiza miito yote ambayo imetolewakwetu sisi

M&M 60:2 Tushirikishe vipaji vyetu

Malaki 3:8–10 Lipa zaka na matoleo

Waebrania 13:17 Kuwa mtiifu kwa ushauri wa viongozi wetu

M&M 64:9–10 Kuwa mwenye kusamehe udhaifu wa wengine, pamoja na ule wa viongozi wetu

Mafanikio ya askofu au Raisi wa tawi letu katika mwito wake hutegemeasana namna tunavyomuunga mkono. Inatupasa kila mara kumwombeakwamba Baba wa Mbinguni amuongoze ili apate kutuongoza katika njiasahihi.

MwishoHuduma inayofanywa na maaskofu na maRaisi wa matawi ni muhimu kwausitawi wetu. Wanaume wenye kustahili wanaitwa kutumika kamamaaskofu na maRaisi wa matawi huitwa kutoa mashauri kwa waumini waKanisa. Wanatutumikia na wanatupenda, na inatupasa kufanya kilatuwezalo kuwasaidia kutimiza kazi zao.

Changamoto1. Waombee viongozi wako wa kanisa katika maombi yako binafsi na ya

familia.

2. Jizuie kuwalaumu au kuwasengenya viongozi wako wa Kanisa.

3. Waunge mkono viongozi wako wa Kanisa kwa kufuata ushauri waomwema.

Maandiko Matakatifu Zaidi1 Timotheo 3: 1–7 (sifa za Maaskofu)

Tito 1:5–9 (sifa za Maaskofu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Mwalike askofu au Raisi wa Tawi kujibu maswali kuhusu mwito wake.

2. Wakumbushe washiriki wa darasa kuja na vitabu vya Maandiko Matakatifu katika mkutanowa Ukuhani.

3. Waeleze washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

60

Page 70: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kazi za Mzee na Kuhani Mkuu

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kazi za wazee namakuhani wakuu.

UtanguliziKama tunavyojifunza kazi zetu za ukuhani na kuzitimiza, tunayabarikimaisha ya wengine kwa sababu sisi ni wawakilishi wa Mwokozi.Ametupatia ukuhani wake ili kwamba kwa kutekeleza majukumu yetu,tunaweza kuwasaidia wale tunaowahudumia kuendelea mbele kuelekeakwenye uzima wa milele. Hii ni kweli hususani kwa wale miongoni mwetuwanaoshikilia ukuhani wa Melkizedeki kwa sababu ukuhani huu una“funguo za baraka zote za kiroho za kanisa” (M&M 107:18). Kati yetu walewaliopokea ukuhani wa Melkizedeki wametawazwa katika afisi ya mzee aukuhani mkuu katika ukuhani huu. Kila afisi ina kazi zake maalumu lakinimengi ya majukumu yao yanafanana.

Majukumu ya Ukuhani wa MelkizedekiKwa kuwa waaminifu katika majukumu yetu kama wenye ukuhani waHaruni, tunajitayarisha sisi wenyewe kupokea ukuhani wa Melkizedeki.Wakati unapowadia wa kutawazwa katika ukuhani wa Melkizedeki,tunahojiwa na wale walio katika mamlaka. Mmoja wa wenye ukuhani waHaruni aliandika habari ifuatayo kuhusu kile alichofikiria na kuona baada yamahojiano yake ya kupandishwa kwenye ukuhani wa Melkizedeki:

“Raisi wa kigingi aliniangalia ndani kabisa ya macho yangu alipokuwaakiniuliza swali lake la mwisho na akasikiza kwa makini jibu langu. Halafualisema, “George ninaona kuwa wewe uko tayari na ni mwenye kustahilikupewa ukuhani wa Melkizedeki na kutawazwa kuwa Mzee. Muda mfupibaadaye, nilikuwa nikitembea katika angani ya usiku . . . Sijawahi kuwamtulivu na mwenye furaha kama hivi . . . Punde nilipiga magoti kando yakitanda changu. Niliamua nitafanya kila niwezalo kutumia ukuhani wangukwa heshima. Niliamua kwamba sitaapa tena au kusema hadithi chafu aukumuumiza yeyote. Niliamua kwamba nitajaribu kuwa mtu wa Mungu.Daima nitakumbuka usiku huo maishani mwangu. Huo ndio ulikuwamwanzo wa kila kitu. Ilikuwa vizuri sana kuitwa kushikilia ukuahni huu. Nivizuri sana sasa kujitahidi na moyo wangu wote ili kuchaguliwa kamammoja wa wenye kustahili kutumia ukuhani huo; kuwa baraka kwa familiayangu, . . . na kwa wanadamu wenzangu.” (George D. Durrant, KentuckyLouisville Mission News Letter, Oct. 19, 1974.)

61

Somo la 9

Page 71: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ni ahadi gani ambayo kijana huyu alijiwekea baada ya mahojiano yake? Ni ahadi ganinyingine ambazo tunaweza kujiwekea wakati tunapokuwa wenye ukuhani wa Melkizedeki?

Inatupasa kujitahidi kujifunza kazi zetu na kuwa wenye kustahili kutumiaukuhani wetu (tazama M&M 107:99–100). Kama wenye ukuhani waMelkizedeki, sote tunayo majukumu fulani bila ya kujali ni afisi ganitunayoshikilia.

Onyesha picha 9-a, “Mamlaka ya ukuhani yanatolewa kwa kuwekewa mikono na wale ambaowamepewa mamlaka ya Mungu.”

Yafuatayo ni majukumu ya ukuhani wa Melkizedeki:

UONGOFU BINAFSI

Yatupasa kuongoka kibinafsi katika injili ya Yesu Kristo na kujiahidi kabisakuishi kulingana na kanuni zake.

NYUMBANI NA UHUSIANO WA KIFAMILIA

Yatupasa kufundisha familia zetu kanuni za injili na kuwaongoza katika kazizao zote kuwa wenye upendo na uelewano.

HISTORIA YA FAMILIA NA KAZI ZA HEKALUNI

Yatupasa kufuzu kwa ajili ya kupokea kibali cha hekalu, na kupatabaraka za hekalu kwa ajili yetu wenyewe na familia zetu, kutafuta majinaya mababu zetu na kufanya ibada ya hekaluni kwa niaba yao. Inatupasakukuza “kugeuza mioyo ya baba kwa watoto na mioyo ya watoto kwababa zao” kwa kuweka rekodi za familia (kama kitabu cha kumbukumbu,historia ya familia) na kumbukumbu ya makundi ya familia (tazamaM&M 128:17–18).

HUDUMA YA USITAWI WA JAMII

Inatupasa kujitegemea sisi wenyewe na familia zetu na kusaidiakukabiliana na mahitaji ya maskini na wenye dhiki katika njia ya Bwana.

KAZI YA UMISIONARI

Inatupasa kujishugulisha na mambo sahihi ya umisionari, kama vilekusaidia wana familia kujitayarisha kwa kutumikia misheni kwa muda wote,kufanya urafiki na wasio waumini, kuwapatia wamisionari watu wakuwafundisha na kusaidia kazi ya misheni kifedha.

UFUNDISHAJI WA NYUMBANI

Inatupasa kuelewa jukumu letu kamili kama walimu wa nyumbani na kwabidii “kuliangalia na kuwa nao na kuwaimarisha” wale ambao wanaitwakutumikia (tazama M&M 20:53).

62

9-a, Mamlaka ya ukuhani hutole wa kwa kuwekwa mikono na wale walio na mamlaka kutoka kwa Mungu

Page 72: Wajibu na Baraka za Ukuhani

9-a

Page 73: Wajibu na Baraka za Ukuhani

KUSHIRIKI NA KUTOA HUDUMA KATIKA KUNDI LA UKUHANI NA KANISANI

Yatupasa kutumikia kwa juhudi katika miito yetu ya Kanisa, kufanya kazinyingine za Kanisa na kazi za kikundi na kushiriki katika mikutano sahihi yaKanisa na shughuli nyinginezo, kwa hayo kujenga ufalme wa Mungu.

KUSHIRIKI NA KUTOA HUDUMA KATIKA JAMII

Yatupasa kuheshimu, kutii na kudumisha sheria, kuwa wananchi waaminifuna majirani wema na kuboresha jumuiya tunapoishi. (From AnnualGuidelines 1978–9779, “The Melchizedek Priesthood,” p. 1.)

Onyesha picha 9-b,“Ukuhani wa Melkizedeki hubariki maisha ya kiroho ya wengine.”

Tunapopewa ukuhani wa Melkizedeki, tunapewa uwezo wa kubarikimaisha ya kiroho ya wengine. Ukuhani wa Melkizedeki “unasimamia injilina unashikilia funguo . . . za maarifa ya Mungu. Kwa hivyo, katika ibadahiyo, uwezo wa ucha Mungu huonyeshwa wazi” (M&M 84:19–21). Kupitiauwezo wa ukuhani wa Melkizedeki, tunaweza kuweka wakfu mafuta,kuwabariki wagonjwa, kutoa ukuhani na kipawa cha Roho Mtakatifu,kuwatawaza wengine katika afisi za ukuhani, kuweka makaburi wakfu,kutoa baraka za faraja, kutoa baraka za Baba kwa watoto wetu, nakushiriki katika ibada za juu za hekalu.

Ni jinsi gani uwezo wa Mungu huonyeshwa katika ibada hizi? Ni baraka gani ambazoumepokea kutokana na ukuhani wa Melkizedeki?

Kazi Maalumu za Wazee na Makuhani Wakuu

MZEE

Neno mzee lina maana mbili katika Kanisa. Kwa njia ya kawaida linahusuyeyote mwenye ukuhani wa Melkizedeki. Kwa mfano wamisionari, viongoziwasimamizi wa Kanisa na Viongozi Wakuu wote wanaitwa mzee. Mzee piani afisi maalumu katika ukuhani wa Melkizedeki.

Waulize washiriki wa darasa wasome M&M 124:137. Ni kazi gani ya afisi ya Mzee iliyotajwakatika maandiko matakatifu haya?

Zaidi ya kuwa watumishi wa Kanisa siku zote, wazee wanatakiwakusimamia mwito wowote ule ambao watahitajika kufanya. Raisi Joseph F.Smith alieleza kwamba wazee wanaweza kuombwa kufanya kazi kwenyemahekalu, kufanya huduma nyumbani, na kusaidia kuhubiri injili duniani(tazama Gospel Doctrine, pp. 184–85).

KUHANI MKUU

Makuhani wakuu wanalo jukumu la kusimamia uwezo wa kiroho na barakaza Kanisa (tazama M&M 107:10). Wameitwa pia kusimamia. Mwito wakusimamia ni pamoja na mengine, afisi ya Kiongozi Mkuu, Raisi wamisioni, Raisi wa kigingi na askofu. Kama makuhani wakuu wanasimamia

64

9-b, Ukuhani wa Melkizedeki hubariki maisha ya kiroho ya wengine

Page 74: Wajibu na Baraka za Ukuhani

9-b

Page 75: Wajibu na Baraka za Ukuhani

katika miito yao ya aina mbali mbali, wana uwezo wa kusimamia baraka zakiroho za mwito wao na kufanya yale yote mzee au mwenye ukuhani waHaruni anayoweza kufanya.

MwishoUkuhani wa Melkizedeki unashikilia funguo za baraka zote za kiroho katikaKanisa. Kazi tofauti za mzee na kuhani mkuu ni kazi za ukuhani waMelkizedeki. Kwa hivyo, wakati tunapoongoza katika afisi zetu za ukuhanikama wazee au makuhani wakuu, tunaweza kubariki maisha yote ya kirohona ya kimwili ya wale tunaowatumikia.

Changamoto1. Zitambue kazi za afisi yako katika ukuhani na ufanye mpango wa

kuzitekeleza vizuri.

2. Tambua hitaji maalumu katika nyumba yako mwenyewe. Amua juu yanjia ya kuwa baba bora au mmoja katika familia kwa kutekeleza ukuhaninyumbani kwako kwa uadilifu.

Maandishi Matakatifu ZaidiMosia 18:7–30 (kazi za waumini wa Kanisa)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma M&M 107.

2. Wapangie washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

66

Page 76: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Baba Mkuu na Baraka za Baba MkuuMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kazi za Baba Mkuu nakujitayarisha kupokea baraka za Baba Mkuu.

UtanguliziBwana anawapenda watoto wake wote na anataka kuwabariki. Matendo nauchaguzi wetu, hata hivyo, vinaamua ni kwa kiwango gani atubariki. RaisiJoseph F. Smith alisema: “Kila mtu atapokea zawadi yake ya haki kwawema atakaoufanya na kwa kila tendo lake. Lakini ikumbukwe kwambabaraka zote ambazo tutapokea iwe hapa au hapo baadaye, lazima zijekwetu kama matokeo ya utiifu wetu kwa sheria za Mungu ambazohusababisha baraka hizi.” (“What Is to Become of Such As Me?”Improvement Era, Nov. 1912, p. 71.)

Wakati tunapopokea baraka zetu za Baba Mkuu, tunaambiwa mapemabaraka nyingi ambazo Baba wa Mbinguni ameziweka kwa ajili yetu sisikatika dunia hii na milele. Baraka hizi zitakuwa zetu kama tukiishi maisha yaukweli na uaminifu. Tukijua mambo haya mapema yanaweza kutuvutiakuwa wenye kustahili vya kutosha kupokea baraka zilizoahidiwa kwetu.

Baba Mkuu ni Nini?Baba Mkuu ni baba. Kwa vile Adamu alikuwa baba wa jamii ya binadamu,yeye alikuwa Baba Mkuu wa kwanza. Kama Baba Mkuu, alikuwa najukumu la kuwabariki wazao wake na kuwasaidia kuishi vyema. Mojawapoya tendo la mwisho la Adamu kuwafanyia watoto wake ilikuwa ni kuwapatiabaraka za Baba Mkuu.

Washiriki wa darasa wasome M&M 107:53–57.

Katika ono Joseph Smith alimuona Adamu akiwaita watoto wake pamoja nakuwapatia baraka za Baba Mkuu. Halafu alimuona Bwana akiwatokea wao,na Adamu alitabiri kile ambacho kingetokea kwa familia yake katika wakatiujao. Akizungumzia juu ya tukio hili kuu, Nabii Joseph Smith alisema, “Hiindiyo sababu Adamu aliubariki uzao wake; alitaka kuwaleta kwenye uwepowa Mungu.” (Teachings of the Prophet Joseph Smith, p. 158–59.)

Neno Baba Mkuu pia ni cheo katika ukuhani wa Melkizedeki. Katikautaratibu wa Kanisa wakati wa Yesu, Baba Mkuu waliitwa wainjilisti (tazamaWaefeso 4:11). Wakati Kanisa liliporejeshwa, afisi hii ya ukuhani ilirejeshwapia. Joseph Smith alielezea kwamba “mwinjilisti ni Baba Mkuu . . . popote

67

Somo la 10

Page 77: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kanisa la Kristo lilipoanzishwa katika ulimwengu, lazima pawepo na BabaMkuu kwa manufaa ya uzao wa watakatifu.” (Teachings, p. 151.)

Onyesha picha 10-a, “Baraka za Baba Mkuu hufunua nasaba na kuahidi baraka ambazozinaweza kupatikana kwa kuishi vyema.”

Karibu makigingi yote ya Kanisa yana angalao mwenye ukuhani waMelkizedeki mmoja mwenye kustahili ambaye ameitwa na kutawazwa chiniya mashauri ya Jamii la Mitume Kumi na Wawili kuwa Baba Mkuu wakigingi. Kwa vile yeye ni kuhani mkuu, ana mamlaka ya kufanya kazi yoyotekuhani mkuu anayoweza kufanya; lakini kwa sababu yeye ni Baba Mkuuanalo jukumu maalumu la kuwapatia baraka waumini wa kigingi wanaotakabaraka za Baba Mkuu.

Baba Mkuu wanayo haki na hupata maongozi ya kutoa baraka za BabaMkuu katika jina la Bwana. Baraka hizi zinaweza kuleta faraja katika wakatiwa huzuni au shida, zinaweza kuimarisha imani, na zinaweza kututiahamasa sisi tuweze kufanikiwa kupata baraka ambazo Bwanaametuwekea. (Tazama Doctrines of Salvation, 3:170.)

Baraka za Baba Mkuu ni Nini?Katika mwaka wa 1957, URaisi wa Kwanza wa Kanisa ulieleza kwambabaraka za Baba Mkuu zinajulisha ukoo. Pia tunapokea mwongozounaotoka kwa Mungu na mashauri ya kinabii na ahadi kuhusu majukumuyetu duniani. Baraka hizi ni pamoja na ahadi za vipawa vya kiroho nabaraka za kimwili, ushauri, na ilani ambazo zitatusaidia kutekeleza ujumbewetu katika maisha. (Tazama General Handbook of Instructions, p. 49.)

Mojawapo ya sehemu muhimu katika baraka za Baba Mkuu nikufahamisha nasaba yako, ambayo inatueleza ni katika kabila gani laIsraeli tunaopokea baraka zetu. Kwa sababu ya jadi yetu, tuna haki yakupokea kulingana na haki yetu, baraka sawa na zile ambazo zilipewaAdamu, Ibrahimu, Yakobo na wale manabii wengine wakuu wa Mungu.(Tazama Eldred G. Smith, “All May Share In Adam’s Blessing,” Ensign,June 1971, pp. 100–101.)

Tulipojiunga na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho,tumekuwa wariithi wa Baba wa Mbinguni. Hii inamaanisha kwambatumepewa haki ya kupokea baraka zote ambazo Baba wa Mbingunializotuwekea sisi—kama tukiishi maisha ya haki. Ni wana wa Israeli tundiyo wenye haki hii. Waumini wa Kanisa ni wa uzao halisi wa Abrahamuau wamepandikizwa katika kabila moja la Israeli kwa sababu wamekubaliinjili ya kweli. (Tazama Warumi 8:14–17; Wagalatia 3:26–29; M&M 86:8–10;na M&M 63:20.)

Sehemu nyingine muhimu ya baraka hizi ni ufahamu tunaopatiwa juu yahuduma yetu tukiwa katika maisha haya. Kupitia kwa baraka zetu za Baba

68

10-a, Baraka za Baba Mkuu zinafunua nasaba na kuahidi baraka ambazo zinaweza kupatikana kwa kuishi kwa haki

Page 78: Wajibu na Baraka za Ukuhani

10-a

Page 79: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mkuu, Baba wa Mbiguni anatuambia makusudi yetu ya kuja hapa dunianini nini na namna ya kuyatimiza. Utimilifu wa baraka zetu, hata hivyo, ni wamasharti.

Mzee John A. Widstoe alifundisha kwamba baraka nyingine zinaweza zisijekatika maisha haya: “Inapaswa daima kuwa akilini kwamba kupatikana kwaahadi zilizofanywa kunaweza kuwa katika maisha haya au maisha yabaadaye. Watu wamefadhaika wakati mwingine kwa sababu ya ahadiwalizopewa ambazo hazijatimia katika maisha haya. Wameshindwakukumbuka kwamba katika injili, maisha na mambo yake yote huendeleamilele na kwamba kazi za ulimwenguni zitaendelea katika Selestia.”(Evidences and Reconcilations, p. 323.)

Uliza Mshirki aliyepangiwa kutoa darasani ushuhuda wa kuongozwa na kusaidiwa na barakaza Baba Mkuu maishani mwake.

Kupokea Baraka za Baba MkuuKupokea baraka zetu za Baba Mkuu, ni lazima tutimize masharti fulani yakibinafsi. Ni lazima—

• Tuwe wenye kustahili, waumini waliobatizwa katika Kanisa.

• Tuwe na hamu ya kupokea maongozi kutoka kwa Bwana.

• Tuwe tumejifunza injili na kujua madhumuni ya baraka za Baba Mkuu.

• Tuwe tumekua kiasi cha kutambua umuhimu wa baraka hizo na kutiwamoyo kutokana na baraka hii.

• Tupate mapendekezo kutoka kwa askofu wetu au Raisi wetu wa tawi.

• Kupanga ahadi na Baba Mkuu sahihi ili kupokea baraka zetu za BabaMkuu.

Tunapokwenda kupokea baraka zetu, yatupasa kusali na kamainawezekana, kufunga ili kujitayarisha wenyewe kiroho. Yatupasa piakumwombea Baba Mkuu kwamba aweze kupata maongozi kwa niaba yetu.

Muulize mtu aliyepangiwa kueleza jinsi alivyojitayarisha ili kupokea baraka kutoka kwa BabaMkuu.

Wakati Baba Mkuu wanapotupatia baraka zetu, huwa wanazirekodi.Wanafanya hivyo ili watupatie sisi nakala ya baraka zetu. Nakala nyinginehuhifadhiwa katika rekodi rasmi za Kanisa. Kwa njia hii, tukipoteza nakalazetu tunaweza kupata nakala nyingine kutoka Kanisani.

Kwa sababu baraka za Baba Mkuu ni za kibinafsi na ni takatifu, inatupasakuweka mahali pa salama. Yaliyomo yanafaa kuelezwa tu wale walio karibunasi na kama tunavyoongozwa na Roho Mtakatifu. Ili baraka zetu za BabaMkuu zitusaidie, ni lazima tuzisome kwa makini kila mara. Tunapofanya hivi,tutajua ni nini inatulazimu tufanye ili tuweze kupokea baraka tulizoahidiwa.

70

Page 80: Wajibu na Baraka za Ukuhani

MwishoHadithi ifuatayo inaonyesha jinsi mtu mmoja alivyobarikiwa alipokuwamwaminifu katika kufuata ushauri aliopewa katika sehemu moja ya barakazake za Baba Mkuu.

“Kila mara nilihisi kuwa ninayo malengo fulani katika maisha na kwambanitakamilisha kazi kubwa, lakini sikujua namna ambavyo ningefanya ilikutimiza jambo hili, kwani nilifika umri wa utu uzima bila kujua kusoma nakuandika vizuri.

“Nilifikiri kuwa nami nilikuwa mwerevu kama wavulana wengine, lakinirekodi ya usomi wangu ilionyesha vingine—nilikuwa mwanafunzi wa Fmoja kwa moja. Mitihani maalumu ya kipimo cha kuingizwa shule, ambayoilitegemea usomaji ilionyesha kwamba sikuwa mwerevu sana—kiasikwamba sipaswi kutembea pekee yangu. Masomo rahisi sana ambayowavulana wenzangu waliyoweza kumaliza kwa urahisi kwangu yalikuwamagumu sana. Nilipokuwa kijana, wakati mmoja niliulizwa na wavulanafulani kutaja herufi za neno ‘gas’, kitu ambacho sikuweza kufanya. Sikuwana rekodi yoyote ila kushindwa, nilianza kuhisi kuwa kweli mimi lazima nimpumbavu kama watu wanavyoniita wakati mwingine, na sasa hasawanaanza kusema juu yangu.

“Nilihitimu shule ya sekondari kwa sababu tu hii ilionekana ndiyo njia rahisikwa shule kutupilia mbali shida ya kumwelimisha mwanafunzi ambayewalikuwa wameona kuwa hawezi hata kusoma masomo ya darasa la tatuyaliyokuwa rahisi.

“La ajabu zaidi, kukutana kwangu kwa mara ya kwanza na ukweli wa injiliiliyorejeshwa kulitokea wakati nilipokuwa na miaka kumi na nne na kujaribukusoma kitabu kimoja nilichokipata katika kabati la vitabu la familia yetu.Nilikutana na Kitabu cha Mormoni ambacho kilikuwa cha mama yanguambaye alikuwa amebatizwa na kuwa muumini aliyeishi mashambani hukokusini mwa Tennessee miaka mingi kabla. Lakini kwa sababu ya kuwambali na waumini wengine wa Kanisa, hakufundishwa mengi kuhusu injilina mara akapatwa na ulegevu, hivyo alikuwa na upungufu katika elimu nautashi wa kuwafundisha wanawe injili iliyo kuwa ndani ya Kitabu hicho chaMormoni.

“Nikajitahidi kumaliza ushuhuda wa Joseph Smith, nikisoma tu manenoyaliyokuwa rahisi na nikiruka maneno mazito ambayo sikuyaelewa. Siajabukwamba, nyakati zingine nilisoma bila kupata maana yoyote lakini kwasababu fulani Roho alinijia na nikashawishika kuamini kwamba yaleniliyokuwa nikisoma yalikuwa ya kweli. Yale niliyoweza kusoma yalinipahamu ya kujua zaidi juu ya Kanisa, hivyo Jumapili iliyofuata, nilitembeampaka upande mwingine wa mji kuhudhuria katika Kanisa la Mormoni.Huu ulikuwa mwanzo wa miaka minane wa kukusanya ushuhuda wangu

71

Somo la 10

Page 81: Wajibu na Baraka za Ukuhani

wa injili, kunitosha kwamba hatimaye niliacha hali yangu ya kuwa Mormonimkavu na nikaingia katika maji ya ubatizo nikiwa na umri wa miaka ishirinina miwili.

“Sasa kwamba nilikuwa muumini wa Kanisa na nilikuwa nimeingia katikanjia ya kwenda mbinguni, sikuwa nimeridhika na kutokuwa na maendeleoya kibinafsi na kukosa mafanikio. Nilitaka kukua kama mtu na mwenyeufanisi katika ufalme wake, na kutimiza haya, nilikuwa na menginiliyohitajika kujifunza, yakiwemo kujifunza jinsi ya kusoma.

“Nilifanya kama kila mara tunavyoshauriwa kufanya wakati tunapofanyamaamuzi na mipango ile inayoweza kuathiri maendeleo yetu milele—Nilimgeukia Bwana kwa maongozi yake, na nilipewa haya katika baraka yaBaba Mkuu ambapo niliambiwa:

“ ‘Wewe ni mteule katika macho ya Mungu, kama vile Paulo wa kale,mtumishi aliyechaguliwa na kupewa nguvu na uwezo wa kutimiza kazinjema. Endelea katika kuitafuta elimu na sali kwa ajili ya hekima ili uwezekumtukuza Baba yako wa Mbinguni kwa akili yako.’

“Kama Bwana alifikiria kuwa mimi naweza kujifunza, kwa hiyo nawezakujifunza! Lakini nilifahamu kuwa hizi baraka si za kuchukulia hivi hivi,kwamba hazitimiliki tu zenyewe, bila ya fikira au matendo kutoka upandewangu. Kutimilika kwa baraka hizi, kama ilivyo katika kila baraka za BabaMkuu, zilitegemea ustahilivu wangu, na ni uhiari wangu wa kufanya mamboyanayohitajika ili kuleta baraka hizo.

“Sasa nilikuwa na imani kwamba kwa msaada wa Bwana ningewezakujifunza kama tu ningejishughulisha mwenyewe, na nilifanya hivyo,kuanzia saa 12 asubuhi hadi usiku wa manane, siku sita katika wiki.

“Nilitumia dola mia tatu kwa kununua rekodi ambazo zilikuwa na herufi zalugha na matamshi ya herufi hizo ili nijifundishe mwenyewe kusoma nakuandika. Usiku hadi usiku nilikariri alfabeti na sauti. Bado nilikuwa siwezikunena herufi moja kwa moja vizuri lakini niliweza kusoma kwa kukatamaneno kwa sauti ya usemi mpaka nilipoyaelewa.

“Nikiwa nimejawa na kujiamini katika uwezo mpya nilioupata wa kusomana kunena herufi, nilijiunga na Chuo Kikuu cha Taifa cha Ohio. Nilijaribukuandika wakati maprofesa walipokuwa wakifundisha kwa kuzungumza,lakini nilikuwa na matatizo ya kuweza kutamka herufi za maneno vizuri iliniweze kuyarekodi. Nilikuwa bado ninakata maneno katika sauti za usemiili niweze kuyarekodi na kwa hivyo niliweza kurekodi sehemu ndogo tu yamasomo ya maprofesa katika muhtasari wangu. Na bila maandishi yotena yaliyo sahihi, ilikuwa vigumu kwangu kusoma na kujitayararisha kwamitihani, hivyo tena, majaribu yangu ya kisomo yalianguka na nikalazimikakutoka chuoni.

72

Page 82: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Nilivunjika moyo na nikaanza kujishuku juu ya uwezo wangu wakufanikiwa kielimu lakini nilikuwa nimepewa baraka na kupewa ahadikwamba naweza kujifunza. Kwa hivyo, nilipofahamu kwamba kutimilika kwaahadi kulitegemea imani na matendo yangu, niliendelea katika kazi yakuboresha kuandika na kusoma kwangu.

“Kuamini neno la Bwana, ya kwamba atanibariki nikifanya sehemu yangu,nilijiunga na chuo cha Ricks. Sikukosa kufanya kazi yangu ya ufundishajiwa nyumbani na kufanya kwa uaminifu majukumu yote niliyopatiwa naKanisa—na kusoma masaa kumi na nane kila siku. Bado nilihitajikakufanya kazi ya kujifunza kusoma, lakini sana nilikuwa naweza kuyatambuamaneno mara moja, lakini awali nililazimika kuyavunja. Nilipokwendakufanya mtihani, nilikariri kila neno katika muhtasari wangu ili niwezekuyaandika wakati wa mtihani. Kufikia wakati nilipoondoka Ricks, niliwezakusoma vizuri na nilipewa tuzo, nikiwa nimehitimu katika daraja la wastaniwa alama 3.6!

“Sasa nina shahada ya B. A kutoka Chuo Kikuu cha Brigham Young,nikiwa nimekamilisha masomo niliyotamani kwa wastani wa alama 3.2.

“Ahadi ya Bwana, ‘kwamba nimepewa uwezo wa kutimiza kazi njemaimetimilika kama vile ahadi zingine nilizopewa katika baraka za Baba Mkuu,kama nikiwa na imani katika yeye na kufanya kazi ili kuleta utimilifu wabaraka hizo.” (Doris Rodgers, “You Shall Glorify Your Father in HeavenWith Your Intelligence,” When Faith Writes the Story, pp. 34–37.)

Kijana huyu alijitayarisha na kuwa mtiifu; kama matokeo, baraka zake zaBaba Mkuu zilikuwa chanzo cha kumwongoza na kumfariji yeye. Inatupasakuonyesha imani kama hii katika kufikia kupata baraka zinazoahidiwakatika baraka zetu za Baba Mkuu.

Changamoto1. Jitayarishe kupokea baraka zako za Baba Mkuu kama bado

haujapokea.

2. Kama umepokea baraka yako, isome kila mara na jitahidi kuishi kwaustahilivu ili upokea baraka zilizoahidiwa.

Maandiko Matakatifu ZaidiMwanzo 49:1–28 (baba Mkuu Israeli huwabariki wanawe)

M&M 107:39–56 (kumi na Wawili kuwatawaza wahudumu, ukuhani waBaba Mkuu katika nyakati za kale)

M&M 124:91–92 (baba Mkuu hupokea funguo za kutoa baraka )

Musa 6:1–6 (kitabu cha ukumbusho kiliwekwa kwa ajili ya kuwabarikiwatoto wa Adamu)

73

Somo la 10

Page 83: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Mweleze mshiriki wa darasa ambaye amepokea baraka za Baba Mkuu atoe ushuhudawake juu ya maongozi na baraka zilivyo katika maisha yake. (Mtahadharishe kwambabaraka za Baba Mkuu ni za kibinafsi na hazisomwi na watu wengine. Kwa sababu hiyoasieleze yote yaliyomo wazi wazi)

2. Mweleze mshiriki mwingine wa darasa kueleza alichofanya ili kupokea baraka za BabaMkuu.

74

Page 84: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Umuhimu wa Viongozi Wakuu

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia kuelewa kwa nini Bwana huwateuaViongozi Wenye Mamlaka Wakuu na kwa namna gani tunabarikiwa kwakuwaidhinisha.

UtanguliziWakati Mwokozi alipokuwa akiishi hapa duniani, alilianzisha kanisa naakawateua wanaume katika ukuhani. Miongoni mwa wale aliowateuawalikuwa mitume kumi na wawili na maafisa wengine ili kumshuhudia yeyena kutunza Kanisa lake. Baada ya kifo na kufufuka kwake, aliwaendeaWanefi waliokuwa Marekani na akalianzisha Kanisa lake kwa jinsi ile ile.Aliwateua wanafunzi ili wawahudumie Wanefi jinsi vile wale mitume kumi nawawili walilihudumia Kanisa katika ulimwengu wa Kale.

Katika siku hizi za mwisho, Bwana kwa mara nyingine tena amelianzishakanisa la kweli la Yesu Kristo kupitia Nabii Joseph Smith. Lilianzishwa kwaufunuo na linao mitume kumi na wawili kama Kanisa lilivyokuwa wakatimwokozi alipokuwa duniani. Kama nyongeza kwa mitume, Bwana aliwaitawengine kusaidia katika kuliongoza na kulielekeza Kanisa lote. Watu hawahuitwa Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu.

Kiongozi mwenye mamlaka mkuu ni mwenye Ukuhani wa Melkizedekialiyeitwa na Bwana kutumika katika nafasi zifuatazo:

Onyesha picha 11-a, “Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu wa Kanisa la Yesu Kristo laWatakatifu wa Siku za Mwisho.”

URAISI WA KWANZA

URaisi wa Kwanza unaundwa na Raisi wa Kanisa pamoja na washauriwake wawili ambao pia ni Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu. Raisi ndiyemwenye uwezo na mamlaka yote yaliyorejeshwa kwa Kanisa katika hizisiku za mwisho. Pamoja na washauri wake, Raisi husimamia Kanisa lote naanao uwezo na mamlaka ya kuongoza afisi zote zilizopo katika ukuhani nakatika Kanisa.

Raisi wa kanisa anazo “funguo” za ukuhani za kusimamia mambo yote yaKiroho na ya muda yahusuyo Kanisa. Anayo haki ya kuwapatia MaRaisi waVigingi, Maaskofu, Baba Wakuu na wengineo “funguo” zinazohusu afisizao kwa kadiri ya maeneo yao ya kijiografia.

Raisi Joseph F. Smith aliandika juu ya jambo hili kwamba “kila mtuanayeteuliwa katika daraja lolote la ukuhani anayo mamlaka ambayo

75

Somo la 11

Page 85: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu

wa Siku za Mwisho

URaisi wa Kwanza

11-a

Raisi Thomas S. Monson

Mshauri wa Kwanza

Raisi Gordon B. Hinckley Raisi James E. Faust

Mshauri wa Pili

Familia la Mitume Kumi na Wawili

Boyd K. Packer L. Tom Perry David B. Haight Neal A. Maxwell

Russell M. Nelson Dallin H. Oaks M. Russell Ballard Joseph B. Wirthlin

Richard G. Scott Robert D. Hales Jeffrey R. Holland Henry B. Eyring

Page 86: Wajibu na Baraka za Ukuhani

yamedhaminiwa kwake. Lakini ni muhimu kwamba kila tendo lifanywalochini ya mamlaka haya linapaswa kutendeka kwa wakati wake na mahalipake, katika namna yake na kwa utaratibu wake. Uwezo wa kuelekeza kazihizi hushirikisha funguo za ukuhani.” (Gospel Doctrine, p. 136.)

JAMII YA MITUME KUMI NA WAWILI

Mitume Kumi na Wawili huitwa na Bwana kuwa mashahidi maalumu waKristo. Hufanya kazi yao chini ya mashauri ya URaisi wa Kwanza.

SABINI

Sabini watatenda kazi katika jina la Bwana, chini ya mashauri ya MitumeKumi na Wawili katika kulijenga Kanisa na kudhibiti maswala yoteyanayohusu kanisa katika mataifa yote (tazama M&M 107:34).

ASKOFU WASIMAMIZI

Askofu wasimamizi ni URaisi wa Ukuhani wa Haruni wakifanya kazi chini yamashauri ya Jamii ya Mitume Kumi na Wawili na URaisi wa Kwanza. AskofuMzimamizi na washauri wake wawili husimamia mambo ya muda na yaKanisa.

Katika nyongeza kwa Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu, idadi kubwa yawanaume huitwa kuwa wawakilishi wa Mitume Kumi na Wawili katikamaeneo mbali mbali. Hawa sio Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu balihuitwa kuwawakilisha wale Kumi na Wawili na kusaidia kulijenga Kanisakatika sehemu maalumu ya dunia.

WAJIBU WA VIONGOZI WENYE MAMLAKA WAKUU

Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu ni wawakilishi wa Yesu Kristo. Mwokozimwenyewe ndiye kichwa cha Kanisa naye huliongoza kwa ufunuo kupitiakwa Nabii na viongozi wengine Wenye Mamlaka Wakuu. Kupitia kwa watuhawa, Bwana hudhihirisha nia yake na kutufundisha kila kitu kilichomuhimu kwa ajili ya wokovu wetu.

Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu humuwakilisha Mwokozi katika njia nyingitofauti:

• Husafiri duniani kote kusaidia na kuwaelekeza washiriki wa Kanisa naviongozi wao.

• Huliweka Kanisa katika hali ya umoja na kuhakikisha Kanisa linafundishamafundisho sahihi.

• Huwawekea mikono viongozi wa Ukuhani wenyeji wa maeneo kama vileMaRaisi wa vigingi na baba wakuu wa vigingi.

77

Somo la 11

11-a, Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Tazama katika gazeti la Mkutano mkuu wa mwisho wa Kanisa ili kupata picha za viongozi wapya

Page 87: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Hutayarisha na kutoa hotuba katika mkutano mkuu, mikutano yamaeneo, na mikutano mingine. Wakati watu hawa wanapozungumzakwa kuongozwa na Roho Mtakatifu ni sawa kabisa na vile Kristomwenyewe angelizungumza. “Lile ambalo Mimi Bwana nimelisema,nimelisema. . . . iwe kwa sauti yangu mwenyewe au kwa sauti yawatumishi wangu, ni sawa tu” (M&M 1:38). Kwa jinsi hii inamaanisha waohufundisha na kuwashawishi wote washiriki na wasio washiriki waKanisa.

• Wale Kumi na Wawili wana mwito wa kuwa mashahidi maalumu wa YesuKristo duniani kote. Wao hutoa ushuhuda wa utukufu wa Kristo popotewaendapo. Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu wengine pia hutoaushuhuda wao juu ya Mwokozi.

• Wanao wajibu wa kusimamia shughuli zote za usimamizi wa Kanisa.

• Pamoja na kazi hizi zote, wao pia ni baba na waume. Sawa na akinababa wengine katika Kanisa, wao wanao wajibu wa kuzisimamia familiazao na kuziongoza kwenda kwenye ufalme wa Selestiali.

Uhitaji wetu wa Viongozi Wenye Mamlaka WakuuHistoria yote hutueleza ya kwamba Baba yetu wa Mbinguni kwa wakatiwote amekuwa akifichua matakwa yake au siri yake kwa wanadamuduniani kupitia manabii wake. Hiyo ni kweli iwe tutazungumzia kuhusuwakati wa Musa au wa Kristo au wa Joseph Smith. Hali yaweza kubadilika,lakini ukweli haubadiliki, wala uhitaji wetu wa mashauri ya Mungu. Kwasababu ya mapenzi ya Bwana kwetu sisi, hivyo basi, ametupa sisi Nabii naMitume na Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu wengine ili watuongoze leo.

Hadithi ifuatayo inatueleza jinsi kikundi cha watu kilivyobarikiwa kwa kuwawatiifu kwa nabii.

“Hatimaye mnamo Julai 1959 mipango ilikamilika. Watahiti thelathiniwaaminifu walifanya kazi, wakajiwekea akiba na wakajitolea mhanga ilikupata fedha zilizohitajika kulipia safari ya kwenda hekaluni Hawaii. Ilikuwakazi kubwa iliyofanyika kuileta Paraita (maana yake Chifu Mkuu), mashuaya misheni, katika gudi, kuikarabati na kuipaka rangi. Halafu pakatokeatatizo na serikali ya Kifaransa. [Nahodha, Kaka Tapu, hatimaye aliwezakumshawishi mkuu wa bandari na wawili hawa waliweza kumshawishiGavana wa Kifaransa kuwaruhusu watakatifu wapande Paraita kusafirikwenda Hawaii.]

“Kaka Tapu siyo tu alipata ruhusa kutoka kwa maafisa wa kifaransa, balipia aliandika barua kwenda jijini Salt Lake ili kupata ruhusa kutoka kwaRaisi David O. McKay. Ruhusa hiyo ilipatikana na kila kitu kilikuwa tayari.

“Ndipo kwa bahati simu kutoka afisi ya misheni ilikuja. Kila mmojaaliyetazamia safari, wote wakusanyike kwenye mkutano katika nyumba yamisheni kabla ya kuondoka . . .

78

Page 88: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Siku ile mjumbe maalumu, Ernest C. Rossiter . . . aliwasili kutoka kwa Raisi McKay mwenyewe huko jijini Salt Lake. Taarifa aliyoleta ilikuwa yakufadhaisha. Watakatifu waliombwa wasifanye safari hiyo ndefu waliyokuwawametayarisha. Kulingana na maelezo ya Kaka Tapu, Raisi McKay hakutoamaelezo yoyote. Alimwomba tu kaka Rossiter kwenda na kuwakatazawasifanye safari hiyo na kama tutawaruhusu waje, tutakuwa matatizoni naserikali [Kifaransa]. Tutawajibika juu yao. Kwavyo nenda na ukawakataze.’

“Katika kumbukumbu ya misheni, Raisi Christiansen [Raisi wa misieni]aliandika akielezea mashaka aliyokuwa nayo ya kuwaambia Watakitifuambao walikuwa tayari kuondoka:

“ ‘Nilikuwa nimeguswa sana, na nilijihisi kuhitaji msaada wa Bwana katikakutoa maelezo kwa washiriki hawa waaminifu na wanyenyekevu walio namatumaini makubwa ya kujiweka wakfu katika Nyumba yake Takatifu.Nilifunga na kusali juu ya jambo hili. Niliitisha mkutano wa makuhani Julai 15,1959, saa mbili na pia niliwaomba akina kaka sita kuja nyumbani kwangusaa moja na nusu na kwa msaada wa Raisi Rossiter tuliwaambia juu yauamuzi uliokuja toka kwa URaisi wa Kwanza na tuliwaambia kwambatunahitaji imani na sala zao katika kuwasilisha ujumbe huu kwa waumini waUkuhani watakaokusanyika hapo asubuhi saa mbili kamili. Baada ya RaisiRossiter nami kumaliza kuongea na akina kaka hawa, nao kwa kuchangiawalitoa mawazo yao, na kadiri nilivyosikiliza furaha kubwa ilinijaa moyoni palewalipoelezea dhamira yao ya kutii mashauri ya nabii wetu hapa duniani.

“ ‘Tulienda kwenye mkutano na akina kaka wa Ukuhani. Baada ya kusikiaujumbe kutoka kwa URaisi wa Kwanza, [wao] walieleza kusadiki kwaokwamba neno hili limekuja kutoka kwa viongozi wa Kanisa basi ni lazimalimekuja kama ono kutoka kwa Bwana na njia pekee wanayowezakumuonyesha upendo na shukrani kwa baraka hizo alizowapa ni kuwawatiifu kwa ushauri waliopewa. Ndipo nilipoitisha kura, mikono yoteilinyanyuliwa juu kama ishara ya kukubaliana na uamuzi wa URaisi waKwanza.’

“Hivyo safari ilifutwa na wala si Raisi Rossiter, wala Raisi Christiansen, walawatakatifu waaminifu wa Tahiti waliojua kwa nini nabii wa Mungualiwaambia wasiende. Waliifuta safari hiyo kwa sababu walikuwa na imanikatika Nabii.

“Baadaye, Kaka Tapu, nahodha, alirejea katika mashua lake na fundi wamashua hiyo akamweleza ya kwamba gia ndogo ilikuwa imeharibika naingeliweza kufanya kazi kwa mwendo wa masaa 100 hadi 150 tu basi.Licha ya ukweli huu, ililazimu mashua kusimama na kutia nanga . . .

“ ‘Vema [alisema Kaka Tapu, nahodha wa mashua], siku kadhaa baadayenilipokea simu. Nilikuwa katika afisi ya misieni nikishughulikia gazeti letu laKanisa. Simu ilitoka kwa mkuu wa bandari. Alisema, “Ha; mashua yakoinazama.” Na nikasema, “Nini, nimeitoa hivi karibuni kutoka gudini!”

79

Somo la 11

Page 89: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Aliendelea kusema, “Mashua yako inazama. Fanya haraka!” Niliendaharaka bandarini na mashua ilikuwa nusu imezama majini. Msaidizi wanguwa kwanza alikuwa chini ya mashua akikagua ni nini kinachoendelea.Aligundua kwamba bomba la moshi kutoka jikoni lilikuwa limeoza. Mafundiwa ukarabati walikuwa wamepaka rangi sehemu ya mbao iliyooza nabomba lililoshika kutu. Lilivunjika na maji yalingia ndani kupitia pale.

“ ‘Hivyo ungelisemaje endapo tungelikuwa kiasi cha maili mia mbili au tatumbali juu ya mashua ya dharura ya kuokoa maisha? Kama tungelisafirikama tulivyopanga, tungelikuwa katika umbali huo kwenye safari yetuwakati ambapo sehemu hiyo ya bomba iliyooza na mbao hiyo ingeliachia.

“Kwa wakati ule watakatifu wa Tahiti walipoukubali ushauri wa nabii,hawakuweza kuelewa sababu za wasiwasi wa Raisi McKay. Lakini sasawalizielewa njia za Mungu. Kaka Tapu anaelezea juu ya jambo hilialiposema, ‘Ndiyo maana daima nilikuwa na ushuhuda wa Raisi McKay,Nabii wa kweli wa Bwana.’ ” (R. Lanier and JoAnn M. Britsch, “A Prophet’sWarning,” New Era, Mar. 1976, pp. 12, 14.)

Viongozi Wenye Mamlaka wakuu huzungumza kwa niaba ya Kristo. Bwanaamesema kwamba “lolote walisemalo wakiongozwa na Roho Mtakatifulitakuwa andiko takatifu, yatakuwa mapenzi ya Bwana, litakuwa ndilo wazola Bwana, litakuwa ndilo neno la Bwana, litakuwa ndiyo sauti ya Bwana nanguvu ya Mungu kwa wokovu” (M&M 68:4).

Kwa sababu watu hawa ni wawakilishi wa Mwokozi hapa duniani, nimuhimu kwamba tujue yale wanayoyasema na kufuata mafundisho yao.Fikiria baadhi ya mafundisho ya Bwana ambayo yameendelea kutiliwamkazo na Viongozi Wenye Mamlaka wakuu katika siku zetu. Wametushaurituwe na mikutano ya jioni ya familia. Wametuomba tusaidie kujengamahekalu na kufanya historia ya vizazi vyetu. Wametufundisha sisi juu yamaandalizi ya binafsi na ya kifamilia (pamoja na utunzaji wa vyakula). Nawameelezea umuhimu wa kila mushiriki kufanya kazi ya umisieni.

Waulize washiriki wa darasa watafakari jinsi ulimwengu ulivyobadilika ghafla katika kipindi chamiaka kumi au ishirini iliyopita. Ni kwa namna gani kumsikiliza nabii kunatusaidia sisikukabiliana na matatizo tunayokutana nayo kila siku.

Kuwaidhinisha Viongozi Wenye Mamlaka WakuuBwana hatamlazimisha yeyote miongoni mwetu kuwatii Watumishi wake.Tunaweza kuwakubali au kuwakataa. Ni baraka kubwa, hata hivyo, kuwezakuwakubali na kuwaidhinisha Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu na viongoziwetu wengine. Hii kwa utaratibu hufanyika katika mikutano fulani ambayotunaombwa kupiga kura ya kuwaidhinisha kwa ajili ya Uongozi wa Kanisa.Tunaonyesha ridhaa zetu za kuwakubali kwa kuinua juu mkono wetu wakuume. Bali kuwaidhinisha Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu kwahitajikazaidi ya kuinua juu mkono wetu wa kuume. Kwa hakika kuwaidhinisha

80

Page 90: Wajibu na Baraka za Ukuhani

81

Somo la 11

Viongozi Wenye Mamlaka wakuu kwahitaji kuyapokea mafundisho yao nakufuata ushauri na uongozi wao.

Watu hawa ni wawakilishi wa Yesu Kristo na hupokea ufunuo daima kutokakwake. Tunaonyesha heshima kwa Mwokozi tunapowaheshimu wawakilishiwake. Tunawaheshimu na kuwaenzi manabii waliohai kwa kutii mafundishoyao, kuwaombea na kuomba tupewe uwezo wa kuwafuata. (TazamaWaebrania 13:17–18 na M&M 107:22.) Na pia tunawakubali waotunapowakubali Maaskofu au Raisi wa tawi letu, kwani yeye hufanya kazichini ya mashauri yao.

Baraka nyingi huja kwa wale ambao wanaowakubali Viongozi WenyeMamlaka Wakuu. Bwana amesema kwamba wale wanaoamini mafundishoya manabii na kuvumilia katika imani hadi mwisho watapokea vile vyotealivyonavyo Mungu (tazama M&M 84:36–38). Kitabu cha Mormonichaelezea juu ya mtu mmoja maarufu aliyeitwa Amuleki aliyempokea Nabiiwa Mungu. Malaika alimtokea Amuleki na kumuambia kwamba Nabii Almaatakuja kwake. Malaika alisema: “Wewe utamkaribisha nyumbani mwakona utampa chakula naye atakubariki wewe na nyumba yako na baraka yaBwana itakuwa juu yako wewe na nyumba yako” (Alma 10:7). Amulekialimpokea Alma nyumbani kwake na baadaye alitoa ushuhuda wake juu yabaraka nyingi zilizomnyea yeye pamoja na familia yake kwa sababualimpokea nabii.

Soma Alma 10:10–11. Twawezaje kupokea baraka zilizoelezwa na Amuleki?

Yawezekana pasitokee Kiongozi Mkuu kutembelea nyumba zetu, lakinitwaweza kupokea baraka kama hizo kama tutawapokea Viongozi WenyeMamlaka Wakuu kwa kufuata ushauri wao katika nyumba zetu.

Kama kuna mshiriki yeyote wa darasa ambaye amewahi kukutana na Kiongozi Mkuu aukumsikia akizungumza, aelezee hisia zake juu ya jambo hilo na ni kwa nini anadhani nimuhimu kuwasikiliza na kuwatii Viongozi Wakuu.

MwishoViongozi Wenye Mamlaka Wakuu ni wawakilishi binafsi wa Mwokozi.Wanao ukuhani na wanazo funguo za kulielekeza Kanisa la Bwana. Kadiritutakavyofuata ushauri wao na kuwakubali wao kwa imani yetu, utii wetu,na kwa sala zetu, tutapata baraka nyingi.

Raisi Harold B. Lee alisema: “Mtu fulani alisema . . . na ninaamini ya kuwani kweli kabisa: ‘Mtu hajaweza kuongolewa kiukweli hadi pale atakapoonanguvu za Mungu zikiwa juu ya viongozi wa Kanisa hili na hata hiiitakapoingia moyoni mwake kama vile moto.’ Mpaka hapo washiriki wakanisa hili watakaposhawishika ya kwamba wanaongozwa katika njia yahaki na sahihi na kushawishika ya kwamba watu hawa wa Munguwanaongozwa na ya kwamba wameteuliwa kwa mkono wa Mungu, hakikawatakuwa hawajaongelewa.” (“The Strength of the Priesthood,” Ensign,July 1972, p. 103.)

Page 91: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Changamoto1. Katika sala ya familia na ya kibinafsi leo, muombe Bwana awabariki

Viongozi Wenye Mamlaka Wakuu.

2. Sali kwa ajili ya ushuhuda na nguvu za kumfuata nabii na ViongoziWenye Mamlaka Wakuu wengine.

Maandiko Matakatifu ZaidiHesabu 12:6 (bwana hujionyesha kwa manabii wake)

Amos 3:7 (bwana huwafunulia siri yake watumishi wake manabii)

Luka 1:59–79 (bwana mara zote amesema na watu kupitia kwa manabii)

M&M 21:4–6 (manabii hunena maneno kama vile yanavyotoka kinywanimwa Mungu)

M&M 43:1–7 (ufunuo kwa ajili ya Kanisa hutolewa tu kupitia kwa nabii)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Panga kuanza au kumaliza kipindi kwa wimbo wa “tunakushuru Mungu kwa Nabii,” WimboNa. 19.

2. Wape kazi washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko yanayohusiana na somo hili.

82

Page 92: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Wajibu wa Baba kwa Usitawi wa Familia yakeMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa wajibu wa baba alionaokatika kupanga na kutimiza mahitaji ya familia yake.

UtanguliziNabii wa Bwana alisema: “Familia ni taasisi muhimu katika wakati huu nahata milele. Madhumuni ya maisha yetu ni kuweza kujijengea taasisi hiyoya familia ya milele.” (Joseph Fielding Smith, “Counsel to the Saints and tothe World,” Ensign, July 1972, p. 27.)

Familia ya milele ni familia ya ukoo au kibaba mkuu. Haya yanamaanishakwamba baba ndiye kichwa cha familia na ile ya kwamba mume na mkewamefunganishwa hekaluni. Familia zote zapaswa kuwa kielelezo chafamilia za milele, na baba akiwa ndiye kichwa cha kweli cha familia yake.

Yampasa Baba Kuyatimiza Mahitaji ya Familia yakeMaandiko matakatifu hutufundisha kwamba baba ndiye kichwa cha familia(tazama Waefeso 5:23). Kama hivyo, yampasa kutimiza mahitaji ya kimwilina ya kiroho ya familia yake (tazama Mosia 4:14–15). Wajibu huu mtakatifutumepewa na Bwana na ni kazi muhimu ambayo baba aweza kufanyakuliko kazi nyingine yoyote. Raisi David O McKay alieleza “hakunamafanikio yanayoweza kufidia kushindwa katika nyumba.” (David O.McKay, Conference Report, Apr. 1964, p. 4.)

Ni katika familia ambako watoto watalelewa na kufundishwa kanuni zamilele. “Kazi muhimu zaidi za Bwana ni zile tuzifanyazo ndani ya nyumbazetu,” alisema Raisi Harold B. Lee (Regional Representatives SeminarReport, Apr. 1972, p. 2). Hakuna mwalimu awezaye kuwafundisha vyemawatoto wetu zaidi yetu sisi wazazi. Kwa sababu hiyo, tunalazimikakuwafundisha watoto wetu kwa mifano na kwa maneno yetu. Ahadi nikwamba kama sisi, wake zetu na watoto wetu tutafunganishwa pamojahekaluni na kwa uaminifu kabisa tukaishi kwa kanuni za injili, tutawezakuishi pamoja kama familia ya milele katika ufalme wa mbinguni (tazamasura 47, “Uzima wa Milele,” katika kitabu cha Kanuni za Injili).

Kutimiza Mahitaji ya Kawaida ya FamiliaKama baba, tunatarajiwa kutimiza mahitaji ya kawaida ya familia zetu. Ilikutimiza mahitaji muhimu ya familia zetu yatupasa—

• Kufanya kazi ya kiuaminifu ili kutimiza mahitaji ya familia.

• Kukadhiria mapato ya familia kwa kushirikiana na wake zetu.

83

Somo la 12

Page 93: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Kuwafundisha watoto wetu kufanya kazi.

• Kuelekeza mpango wa uzalishaji na uhifadhi nyumbani.

Maandiko Matakatifu ya kisasa yanatufundisha kwamba wale ambaowangeliweza kufanya kazi lakini hawafanyi, “wasile mkate wala kuvaamavazi ya wafanyikazi” (M&M 42:42). Bwana amesema ya kwamba hadihapo mvivu atakapobadili njia zake, hatapokea baraka ambazowafanyikazi huzipokea. Hataweza hata kutunza nafasi yake katika Kanisa(tazama M&M 75:29). Ndiyo, hiyo bila kujali ni kazi gani tuifanyayo ili mradiiwe kazi halali na kazi ya kuridhisha.

Pamoja na mke wake, mume yampasa kutengeneza kadhirio la familia.Mapato ayapatayo siyo yake peke yake—ni mali ya familia yote, yeye nimtunzaji tu wa mali hiyo. Ni wajibu wake kuona mahitaji ya kifedha ya kilamtu katika familia yanatimizwa, siyo yake tu. Anapojitahidi kwa uwezo wakewote kutimiza mahitaji ya kimwili ya familia yake, Bwana humbariki yeye,mkewe na watoto wake wataendelea kutekeleza majukumu yao katikafamilia.

Onyesha picha 12-a, “Familia zifanyazo kazi kwa pamoja hubarikiwa kimwili na kiroho.”

Watoto yapasa wahimizwe na waruhusiwe kupata elimu kadiriiwezekanavyo ili kuhakikisha kuwa wamejiandaa kufanya kazi katikamaisha yao. Kadiri itakavyowezekana, wasiachishwe shule kwa sababu yakufanya kazi. Hii haimaanishi kwamba watoto wetu wasifanye kazi zanyumbani. Raisi Harold B. Lee alielekeza wazazi kupanga kazi maalumukwa watoto wao ili kuwaepusha na uchovu wa kukaa bila kazi nakuwaruhusu wao kujijengea tabia ya kupenda kazi (tazama “Preparing OurYouth,” Ensign, Mar. 1971, p. 3).

Kazi moja ambayo watoto wanaweza kupewa ni kuitunza bustani yafamilia. Tumeshauriwa tuwe na bustani za familia ili kuzalisha baadhi yavyakula tunavyohitaji na kisha kuhifadhi vyakula vingi kadiriinavyowezekana. Raisi Spencer W. Kimball ameshauri kila familia“kupanda vyakula vyote vinavyoweza kumea katika maeneo yenu . . .Endelezeni ujuzi ndani ya nyumba zenu kwa kutunza na kuhifadhi.Tunarudia kusisitiza ushauri wa awali uliotolewa kwa Kanisa tena na tena,wa kutafuta na kutunza akiba ya mwaka mmoja.” (Spencer W. Kimball,“Family Preparedness,” Ensign, May 1976, p. 124.)

Ni kazi gani nyingine tunazoweza kufanya kama familia ili kuwafundisha watoto, wetu kazi?Tunapokuwa hatuwezi kutimiza mahitaji ya kimwili ya familia zetu, tunaweza kupata wapimsaada huo? (Daima yatupasa kuomba msaada huo kutoka katika familia zetu kwanza najamaa zetu ambao watakuwa katika hali ya kuweza kutusaidia. Kama hawawezi kutusaidia,ndipo tuligeukie Kanisa kwa kuwasiliana na viongozi wa Jamii zetu. Taasisi za misaada zaserikali zifuatiliwe tu endapo Kanisa halitaweza kutusaidia kwa namna tunavyohitaji msaadahuo.)

84

12-a, Familia zifanyazo kazi pamoja hubarikiwa kimwili na kiroho

Page 94: Wajibu na Baraka za Ukuhani

12-a

Page 95: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kutoa Mahitaji ya Kiroho ya Familia ZetuIli kufikia mahitaji ya Kiroho ya familia zetu, tunaweza kufanya yafwatayo—

• Tufundishe injili kwa wake zetu na watoto wetu.

• Tuwe na sala la pamoja la familia kila siku.

• Tuzifanye nyumba zetu kuwa mahali patakapoweza kumkaribisha Rohowa Bwana kuishi pamoja nasi.

• Tulipe fungu la kumi na matoleo mengine kwa Bwana.

• Kuwa na mikutano mizuri ya jioni ya familia kila mara.

Haya yote ni majukumu matakatifu. Mafundisho na Maagano yanaonyeshaumuhimu wa moja ya majukumu hayo:

Washirikishe washiriki wa darasa wasome M&M 68:25, 28. Bwana ametuamuru tuwafundishenini watoto wetu?

Baba ni lazima ahakikishe kuwa familia yake inafundishwa injili nyumbani.Njia nzuri ya kuanza utaratibu huu ni kwa kufanya mikutano ya jioni yafamilia. Hii hutoa nafasi kwetu kuzungumza na kuzifundisha familia zetumara kwa mara . URaisi wa Kwanza unasihi wazazi wote “kukutana marakwa mara na familia zao kila Jumatatu jioni ili kuwafundisha MaandikoMatakatifu . . . na kutoa ushuhuda. Wazazi imewapasa watumie nafasi hiikuwa karibu na watoto wao, kusikiliza matatizo yao na (malengo) nakuwapa mashauri binafsi wanayoyahitaji.” (“Message from the FirstPresidency,” Family Home Evening manual, 1976–77, p. 3.)

Kwa baba kuwafundisha vyema watoto wake, yambidi kupanga vyemamuda wa kuwa nyumbani pamoja na familia yake mara kwa mara. Piayampasa kuonyesha furaha aliyonayo katika kuishi misingi ya injili katikamaisha yake binafsi kwa kulipa zaka kwa uaminifu na matoleo mengineyokwa kanisa, kukubali na kutekeleza miito ya Kanisa na kuweka amrinyinginezo.

Kanisa hutusaidiaje kuwafundisha watoto wetu?

Baraka kwa Baba na FamiliaOnyesha picha 12-b, “Mfalme Benjamin aliweza kutimiza mahitaji yote muhimu ya kimwili nakiroho kwa familia yake.”

Kitabu cha Mormoni hutufundisha juu ya Nabii-Mfalme maarufu, MfalmeBenjamin (tazama Mosiah 2:12, 14). Ingawa alikuwa ni Mfalme na Nabii,alifanya kazi kwa mikono yake. Hakuwategemea watu wengine wamtunze.Kama baba, yatupasa kuiga mfano wake kwa kutimiza mahitaji ya familiazetu.

Abrahamuu ni mfano mwingine wa kuigwa katika maisha yetu. Kwasababu ya imani yake, aliahidiwa familia njema na uzao mkubwa (tazama

86

12-b, Mfalme Benyamini alitimiza mahitaji yote ya lazima ya kimwili na kiroho ya familia yake

Page 96: Wajibu na Baraka za Ukuhani

12-b

Page 97: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mwanzo 17:3–8). Abrahamu alibarikiwa kwa sababu ya juhudi yake yakumfuata Bwana na kwa kuihudumia vyema familia yake. Kwa vile sisi tuwa uzao wa Abrahamu, twaweza kupata baraka kama hizo tutakapowezakuzitunza familia zetu katika mahitaji yote ya kimwili na kiroho. Mara ghafla,upendo utaongezeka nyumbani mwetu na familia zetu zitakua kiroho.

MwishoHadithi ifuatayo yaelezea jinsi baraka zilivyokuja kwa baba na familia yakebaada ya kuipokea na kuishi kulingana na injili. Kabla ya Joseph Garciakujiunga na Kanisa, alitumia muda wake kunywa na marafiki zake naalitumia muda mchache sana wa kuwa na familia yake. Matokeo yake,mkewe ilimbidi mara kwa mara afanye vibarua vya kufanya usafi ili apatefedha ya kuweza kusaidia kuitunza familia. Watoto wake hawakumfahamuvyema. Walimuogopa zaidi kuliko walivyomheshimu au kumpenda.

Siku moja, hata hivyo, alitambulishwa kwa wamisieni wa Kimormoni. Baadaya miezi sita ya mikutano na wamisionari hao, maisha yake yalibadilikakabisa. Aliachana na marafiki zake katika mabaa na mara akajiunga naKanisa. Akaanza kutumia muda wake kuwa na watoto wake, kufanyamikutano ya jioni ya familia na kufurahia kwenda nje pamoja nao na mkewake. Alipanga kwa uangalifu kadhirio la familia ambayo ilimwezesha mkewake kuacha kufanya vibarua na kuutumia muda wake wote kuwanyumbani.

Haraka sana aligundua kwamba alifurahia nyumba yake na wakatialioutumia pamoja na mke wake kuliko alivyofurahi alipokuwa na marafikiwake. Watoto wake walijifunza kumpenda yeye na leo wanajaribu kuigamfano wake mwema katika kuishi.

Changamoto1. Tazama ni jinsi gani unatimiza vyema mahitaji ya kimwili na kiroho ya

familia yako.

2. Jitahidi kutimiza mahitaji ya familia yako.

3. Tengeneza mpango ukishirikiana na mke wako na watoto wenu wakuyaweka maisha yenu katika hali inayolingana na Maandiko Matakatifuna ushauri wa viongozi wa Kanisa.

Maandiko Matakatifu Zaidi1 Timotheo 5:8 (akina baba ni lazima watunze familia zao)

Mosiah 27:14, 22–24 (bwana huzisikia sala za akina baba kwa ajili yawatoto wao)

M&M 68:30–31 (watoto wa wavivu hukua katika uovu)

M&M 75:25, 28–29 (akina baba watimize mahitaji ya kila mtoto katikafamilia)

88

Page 98: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 27, “Kazi na Wajibu wa Kibinafsi wa kujitunza wenyewe,” na sura ya 36,“Familia Yaweza Kuwa Pamoja Milele,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.

2. Pata ubao na chaki.

3. Kama unataka orodhesha ubaoni au kwenye karatasi kubwa njia ambazo baba anawezakukabili mahitaji ya kimwili na kiroho ya familia yake.

4. Washirikishe washiriki wa darasa watoe hadithi na wasome Maandiko matakatifu katikasomo hili.

89

Somo la 12

Page 99: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kushauriana na Jamii

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia kuziimarisha familia zetu kwakushauriana na wake zetu na watoto wetu.

UtanguliziImba “Kuna urembo kila mahali.”

Mwenye Ukuhani Huongoza katika Nyumba YakeNyumba zetu za hapa duniani ni mwanzo wa nyumba zetu za mbinguni.Uzazi, kwa maana halisi ni mafunzo ya Uungu. Kwa akina baba wanaojuahaya wanatambua kwamba wanao wajibu mtakatifu wa kuongoza,kuzilinda na kuzielekeza familia zao katika haki. Raisi N. Eldon Tanneramesema: “Kila nyumba ya Mtakatifu wa Siku za Mwisho yapaswa kuwanyumba ya mfano, mahali ambapo baba ndiye kiongozi wa nyumba lakiniakiongoza kwa upendo na kwa kukubaliana na utashi mwema wa hakikutoka kwa mama. Kwa pamoja wanapaswa kuwa na malengo mamojakwa ajili ya familia, na watoto wanapaswa kuhisi upendo na ushirikianouliopo.” (“Fatherhood,” Ensign, June 1977, p. 2.)

Kama wenye ukuhani waliooa, tunao wajibu wa kuilea familia yenye wema.Lakini hatufanyi hivyo pekee yetu. Tunapata msaada wa wake zetu. Kwapamoja tunaweza kuijenga ndoa imara na kuirejesha familia yetu mbele zaBwana. Hii inamaana kwamba inatubidi tuwapende na kushauriana nawake zetu kama tunahitaji kuwa na Roho wa Bwana katika nyumba zetu.

Kuonyesha Upendo na Kuwajali Wake ZetuSoma Mosiah 4:14.

Bwana anatufundisha sisi katika maandiko matakatifu haya kwambatuziimarishe nyumba zenye upendo na amani. Kuwa na nyumba za namnahiyo, lazima tuhakikishe tunakielelezo cha upendo wa dhati na waushirikiano katika hatua za awali kabisa za ndoa zetu. Kama mfano huuhaupo sasa katika nyumba zetu, yatupasa kuuanzisha mara moja. Hiiyahitaji kusali pamoja daima, kuonyesha upendo na heshima kwa kilammoja na kujifunza Maandiko Matakatifu kwa pamoja. Pengine muhimuzaidi, ni kuweka amri za Mungu na maagano tuliyofanya wakati tulipofanyaviapo vya ndoa zetu.

Kiongozi imara wa Ukuhani ni mwema na mwenye kumjali mke wake(tazama Waefeso 5:25). Raisi J. Reuben Clark, jr. alisema kwamba kamafamilia yataka kuwa familia ya selesitiali, mume na mke lazima wapendane

90

Somo la 13

Page 100: Wajibu na Baraka za Ukuhani

na waheshimiane. Ni lazima wavumiliane na wawe watiifu kwa viapo vyandoa yao. Imani yao yapaswa “kuifunika nyumba yao kama nuru karimu.”Kama watafanya mambo haya, utii wao kwa Mungu “utawaongoza nakuwachangamsha.” (Tazama Immorality and Eternal Life, Vol. 2[Melchizedek Priesthood study guide, 1969], pp. 14–15.)

Ni mambo gani mengine tuwezayo kufanya ili kuonyesha upendo na kuwajali wake zetu? Nikwa namna gani kuonyesha kwetu upendo na kuwajali wake zetu kwaweza kutusaidiakuzianzisha nyumba zenye amani na upendo?

Kushauriana na Wake ZetuOnyesha picha 13-a, “Uongozi katika familia huwa rahisi zaidi kama mume anashauriana namke wake.”

Ni muhimu kuwasiliana na wake zetu. Matatizo mengi katika ndoa nafamilia twaweza kuyashinda tukishauriana pamoja na wake zetu—nakutafuta msaada na mwongozo wa Bwana.

Soma Alma 37:37. Ni kwa namna gani kushauriana na Bwana kwaweza kutusaidia sisi?

Kama twataka kuwa makuhani wenye hekima, ni lazima kwa njia yamaombi tujadili matatizo na malengo yetu pamoja na wake zetu nakuwashirikisha tunapofanya maamuzi. Kama tunawapenda wake zetu,daima tutahitaji mawazo yao na msaada wao kuliko kujaribu kuyatatuamatatizo pekee yetu. Ili kufanya haya, yatupasa kutenga muda maalumutunaoweza kujadili juu ya watoto, fedha, dini, jioni ya familia na wazo lolotela kibinafsi au la kifamilia alilonalo kila mmoja wetu. Ni kwa njia hizi zake tundipo tutaweza kuziunganisha na kuziongoza familia zetu.

Wake zetu ni washiriki-wenzetu katika ndoa na hivyo ni sehemu muhimukatika shirikisho la ndoa. Ni lazima kuwafanya wajue umuhimu wao.Wanaume wengine hudhani kuwa kwa vile wao wanao ukuhani wanayonafasi ya kufanya maamuzi yote, lakini maandiko matakatifu yanatuambiakwamba hilo ni kosa.

Soma M&M 121:39, 41.

Ni matumizi mabaya ya ukuhani “kufanya ukandamizaji usio wa haki.”Kama wenye Ukuhani wa Melkizedeki, tunao wajibu wa kuwasikiliza wakezetu katika upendo na pia wanapokuwa katika, mashaka. Natunapowasikiliza, tusiwasikilize kama sisi ni wakubwa wao, kwani wao niwashiriki wenzetu na tuko sawa. Uzoefu ufuatayo unaelezea jinsi mwenyeUkuhani mmoja alivyokuwa akishauriana na mke wake.

Kaka Jackson alikuwa mtu msomi na mwenye hekima. Angeliweza kabisakufanya maamuzi yote ya kifamilia pekee yake. Lakini badala yake, daimaalikaa chini na kushauriana kuhusu matatizo na njia za utatuzi pamoja na mkewake. Angalao mara moja kila wiki, mara nyingi jumapili jioni, walikaa katikameza ya jikoni wakizungumza kuhusu matatizo ya familia. Wakati mwinginewatoto wakishirikishwa katika mjadala. Kwa kujadiliana pamoja, mtu huyu namke wake mara nyingi waliweza kuafikiana jinsi watakavyowalea watoto wao.

91

Page 101: Wajibu na Baraka za Ukuhani

13-a

Page 102: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Hawakuwahi kubishana au kugombana bali walipendana. Mtu huyu alikuwana hekima ya kumwuliza kila mara mkewe ushauri wa thamani. Alijiwekeautaratibu wa kuwa na nyumba iliyokaribia nyumba ya selestia hadi wanawewa kiume wote sita wanaiga mfano wake majumbani mwao.

Ni kwa namna gani kushauriana kati ya baba na mama kunaweza kuzuia kugombana namatatizo katika nyumba zetu? Kunawezaje kuongeza upendo katika ndoa yao?

Kushauriana Na Familia ZetuOnyesha picha 13-b, “Kuwa na mabaraza ya familia kunamsaidia baba kuiongoza familiayake kwa haki.”

Baada ya mume kushauriana na mke wake, inawapasa wawaite watotowao pamoja na kujadiliana pamoja nao juu ya malengo na mipango yafamilia. Kufanya baraza la familia yote ni jambo la thamani kubwa. Lawezakuinua kiwango cha maisha ya familia na kuongeza upendo miongoni mwawanafamilia. Watoto wanaofahamishwa mipango ya familia mapemawatajua yale yatakayofanywa na wenzao na hali ya utaratibu na amaniitajitokeza. Inapowezekana, watoto waruhusiwe kuchangia kutoa uaamuzina pia wasaidie katika kutekeleza maamuzi hayo.

Ni wakati gani unaofaa kufanya baraza la familia? (Mkutano wa jioni wa Familia ni wakatimuafaka, ila baraza la Familia linapaswa lisichukue nafasi ya somo.) Ni sehemu gani zawezakujadiliwa katika familia kama hili?

Onyesha picha 13–c, “Baba yampasa kuwahoji watoto wake mara kwa mara.”

Pia ni muhimu kwa baba kushauriana na kila mtoto kibinafsi. “Matokeomazuri huja endapo baba atawahoji wanawe na binti zake mara kwa mara.Ataweza kujua shida zao na matumaini yao. Anaweza kuwaonyesha kuwayeye ni rafiki yao asiye na masharti yoyote.” (A. Theodore Tuttle, “The Roleof Fathers,” Ensign, Jan. 1974, p. 67.)

Mambo gani mengine ambayo wewe unaweza kujadili na mwanao katika mohojiano haya?Jambo hili lawezaje kukuweka karibu nao? (Wahimize wakina kaka kutumia wakati huu wamahojiano kusikiliza mawazo ya watoto wao.)

Kushauriana na watoto wetu si lazima wakati wote kuwa na utaratibumaalumu. Inatupasa tutumie kila nafasi wakati wowote na mahali popoteinapotokea kusikiliza shida zao. Tunaposhauriana nao yatupasakayatazama matatizo yao katika mtazamo wao. Tusicheke au kuyapuuzabali kwa upendo tuyasikilize na kujaribu kuyaelewa na kuwasaidia.

“Ni jambo la kupendeza sana kama baba au mama atakaa chini na mwanaau binti yake na kujadili matatizo yake binafsi (na wanayo matatizo ambayokama tutatumia hekima hatutayapuuza. Kuna shirikizo, mvuto na hatalawama zisizo za haki juu ya wana na binti zetu ambazo wanahitajikukingwa . . . katika mazungumzo ya moyo kwa moyo, wazazi watawasaidia

93

Somo la 13

13-a, Uongozi wa Familia huwa rahisi na wenye kufaa endapo mume atashauriana na mke wake

13-b, Kuitisha mabaraza ya familia kunamsaidia baba kuwaongoza watoto wake kwa haki

13-c, Baba yampasa kuwahoji watoto wake mara kwa mara

Page 103: Wajibu na Baraka za Ukuhani

13-b

Page 104: Wajibu na Baraka za Ukuhani

13-c

Page 105: Wajibu na Baraka za Ukuhani

watoto wao kujiwekea malengo.” (ElRay L. Christiansen, “SuccessfulParenthood—A Noteworthy Accomplishment,” Ensign, July 1972, p. 55.)

Ni mambo gani ambayo kijana wa kiume anapaswa kujadili na wazazi wake? Ni mambo ganibaba anapaswa kujadili na watoto wake? (Ni jambo la hekima kuwatahadharisha washiriki wadarasa kutokubali mawazo ya watu wengine. Kwani tatizo la mtu mmoja siyo sawa na la mtumwingine.)

Mzee Richard L. Evans akizungumza nasi juu ya kushauriana na watotowetu alisema: Wewe na wao kwa pamoja mnapata nafasi, haki na wajibuwa kukaa pamoja na kushirikiana kimawazo na kufikia uamuzi wa pamojana kwamba nyote kwa pamoja mnasikilizana na kuheshimiana, kufanyakazi, kusali na kupanga kwa pamoja kwa ajili ya furaha yenu nyote—daimana milele.” (“As Parents and Children Come to Common Ground,”Improvement Era, May 1956, p. 342.)

MwishoAhadi ni hii kwamba tutaishi kwa furaha na amani katika ufalme waSelestia. Lakini inatulazimu kuanza sasa kupata umoja na upendo kwanihaitatokea tu. Raisi David O. McKay alisema: “Ninaweza kuwazamachache, kama yapo, mambo magumu nyumbani kuliko kukosekanakwa umoja na furaha. Kwa upande mwingine, najua kwamba katikanyumba ambayo umoja na ushirikiano na upendo upo ni kama selestiandogo hapa duniani.” (“Unity of Purpose Important to the Accomplishmentof God’s Work,” Improvement Era, Dec. 1967, p. 34.)

Tukiwa tunashauriana na wake zetu na watoto wetu, tutakuwa tunajiimarishasisi wenyewe na wao na kuongeza upendo na umoja katika familia zetu.

Changamoto1. Sali na ushauriane mara kwa mara na mke wako.

2. Fanya baraza la familia.

3. Weka wakati wa kumhoji kila mtoto wako, ukikumbuka kuwa mwenyekusali na kuwa mwenye kujali unapozungumza nao.

Maandiko Matakatifu ZaidiWagalatia 5:22 (matunda ya Roho)

Yakobo 2:35 (madhara ya mifano mibaya kwa familia)

Yakobo 3:7 (umuhimu wa upendo baina ya mume na mke)

M&M 121:36–38 (ni kwa namna gani Ukuhani unapatikana na jinsi tunavyoweza kuudhibiti)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 37, “Wajibu wa Familia” Katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Likumbushe darasa kuleta vitabu vyao vya maandiko matakatifu darasani.

96

Page 106: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kuongoza Sala la Familia

Madhumuni ya somo hili ni kutuhimiza kufanya sala la familia kila siku.

UtanguliziOnyesha picha 14-a, “Maombi ya familia yanapaswa kufanywa mara mbili kwa siku.”

Kama baba, tunapaswa kuwaita wanafamilia pamoja na kusali kwa kutoashukrani na kuomba mwongozo kutoka kwa Baba yetu wa Mbinguni. RaisiSpencer W. Kimball alisema:

Nimewahoji viongozi wengi wa familia mbali mbali . . . ambao walikiri kuwasala zao za familia siyo za mara kwa mara na mara nyingi zaidihazikufanyika kuliko zile siku zilipofanyika. Wengine wamesema sala lafamilia hufanyika mara moja kwa siku na wengine hupuuza kwa kusemahawawezi kuwakusanya watu wote katika familia na kufanya sala pamoja.Tabia hii ya kutokujali jambo hili muhimu la sala au maombi ya familialinanikera sana . . . Kanisa linasisitiza kwamba ni muhimu kufanya sala yafamilia kila siku usiku na asubuhi. Yapaswa kuwa sala la kupiga magoti . . .wengi wameona ni rahisi kuifanya wakati wa kufungua kinywa asubuhi nawakati wa chakula cha jioni au usiku. Ndivyo sivyo vigumu kuwapata watukwa pamoja. Sala hili inapaswa kuwa fupi na hasa kama kuna watotowadogo waliopiga magoti. Wana familia wote pamoja na hao wadogo pialazima wapate zamu ya kusema sala.” (“I Kneeled Down before MyMaker,” Instructor, Apr. 1966, p. 132.)

Maombi ya Familia: Ni msaada wa Kinga ya MajaribuTumeamriwa kuomba kwa Baba yetu wa Mbinguni, hasa tukiwa pamoja nafamilia zetu.

Soma maneno ya Kristo katika 3 Nefi 18:18–21. Ni kwa madhumuni gani muhimu ambayoMwokozi ameshauri ombi?

Sala huzisaidia familia zetu kushinda vishawishi vya shetani. Kwa njia yasala, tunaweza kupata nguvu na kuweza kwa namna iliyo bora kuyashindamatatizo yetu.

Kama akina baba tuziite familia zetu pamoja kwa ajili ya sala na tuonyeshemfano. Katika Mafundisho na Maagano, akina baba na akina mamawanaamriwa kuwafundisha watoto wao kusali (tazama M&M 68:28). Njiabora ya kuwafundisha watoto wetu kusali ni kwa kuwaonyesha mfano.Tukifanya jitihada ya kusali nao, watoto wetu watajifunza umuhimu wa salanao watafanya hivyo katika maisha yao.

97

Somo la 14

Page 107: Wajibu na Baraka za Ukuhani

14-a

Page 108: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kuongoza na kuwafundisha watoto wetu ni majukumu waliyonayo akinababa wote. Mtu hahitajiki kuwa na Ukuhani wa Melkizedeki ili kuiongozafamilia yake katika sala.

Kuifanya Maombi ya Familia Kufaulu Nyumbani MwakoWatakatifu wa Siku za Mwisho wameambiwa “wasali kila mara” M&M 10:5.Nabii ameelezea namna gani yawezekana kusali kila mara, hata paletusipoweza kupiga magoti.

Soma Alma 34:27. Ina maana gani kuwa na sala moyoni mwetu daima?

Kwa kuyasema mawazo na utashi wetu kwa Bwana pale inapowezekanatunaweza kuwa na sala daima mioyoni mwetu.

Ili kufanya maombi ya familia ifanyike majumbani mwetu, yatupasatupange wakati maalumu wa maombi nyumbani. Viongozi wetu wa Kanisawametueleza tuzikusanye familia zetu pamoja mara mbili kwa siku.Kufanya hivyo yahitaji tutafute wakati watoto wetu wote wako nyumbani.Nyakati hizi mara nyingi huwa ni asubuhi kabla ya kutawanyika kwendashule na kazini na muda mfupi kabla watoto kuenda kulala usiku.

Sala zetu hazitakiwi kuwa ndefu. Kwa kweli, sala fupi huwatia moyowatoto wadogo kusali, kwa sababu kwa kawaida sala zao ni fupi sana.Sala zetu za asubuhi zijumuishe mipango yetu ya siku hiyo. Sala zetu zausiku ziwe ni kumshukuru Mungu kwa ulinzi na mwongozo wake wa sikunzima. Sala la kubariki chakula isichukue nafasi ya sala ya kawaida yafamilia lakini yaweza kuunganishwa ndani yake tunapofanya sala ya familiakabla ya kula.

Baraka nyingine ambazo tunapaswa kuomba zimetajwa na Amuleki katikaKitabu cha Mormoni.

Soma Alma 34:23–25.

Orodha yetu ya vitu vya kuomba yaweza kuwa tofauti na ile ya Amulekilakini kanuni alizozizungumza ni sawa. Kanuni mojawapo ni kwambalazima tuombe kwa ajili ya shughuli zetu za kila siku. Nyingine ni kwambalazima tusali ili tupate nguvu ya kushinda majaribu ya shetani. Kila familiayapaswa kutazama mahitaji yake na malengo yake na kuomba kwa dhatijuu ya mambo yale yaliyo muhimu sana kwao. Tukifanya hivyo, sala zetuzitakuwa za dhati na zenye mafanikio na siyo maneno matupu tuyarudiayokila siku. Kama akina baba, tutawasaidia watoto wetu wadogo kutokurudiamaneno yale yale kila siku wanaposali. Tufanyapo hayo, tuombemwongozo wa Roho Mtakatifu (tazama M&M 42:14). Chochote tufanyachokwa kuwafundisha watoto wetu kusali, inatulazimu kutowalazimisha aukuwafedhehesha.

99

Somo la 14

14-a, Sala ya Familia yapaswa kufanyika angalao mara mbili kwa siku

Page 109: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Lazima tusikate tamaa kama tunapata matatizo katika kufanya sala yafamilia lenye mafanikio. Mara nyingi, Shetani yupo nyuma ya matatizo hayo.

Soma 2 Nefi 32:8.

Shetani atajaribu kutuzuia kufanya sala binafsi na la familia kwa sababuanaweza kwa urahisi kabisa kuzishawishi familia zile zisizofanya sala lafamilia mara kwa mara. Tabia ya kuwa na sala la familia, hivyo, inapaswakuwa imara kiasi kwamba hata kama akina baba hawapo nyumbani, wakezao wataziita familia zao pamoja. Kama zote yaani sisi pamoja na wakezetu tupo mbali na nyumbani, tumteue mtoto mkubwa kuongoza familiakutika sala.

Ni kwa namna gani kijana mwenye ukuhani wa Haruni anaweza kusaidia na kuishawishifamilia kusali?

Baraka za Kiroho Kupitia Sala la FamiliaBaraka kuu zitatukujia kwetu endapo tutafanya sala la familia. Upendo nauelewano utaongezeka na ushawishi wa shetani kwa familia zetuutapungua. Hisia za amani zitaijaza mioyo yetu pale tutakapotambua yakwamba tunatimiza amri yake kikamilifu.

Sala la familia ni hatua moja ya kujenga nyumba ya milele. Raisi SpencerW. Kimball alisema kwamba, “wakati tunapopiga magoti katika sala yafamilia, watoto wetu . . . hujifunza tabia ambazo zitadumu maisha yaoyote. Bali kama hatuna muda wa sala kwa kweli tunachosema kwa watotowetu ni, “Wala, siyo muhimu sana, hata hivyo . . . ‘Na kwa upandemwingine, ni furaha iliyoje inayoimarisha desturi na tabia hii katika nyumbahizi na kwamba wazazi watakapowatembelea watoto wao . . . baada yakuwa wameoa au kuolewa kama desturi watapiga tu magoti pamoja naokatika hali ya kawaida, iliyoimarishwa kwa ajili ya sala!” (The Miracle ofForgiveness, p. 253.)

MwishoWakati mwingine tunashindwa kuelewa kama watoto wetu wanajifunzalolote juu ya Kristo na kuhisi uwepo wake katika sala la familia. Lakini watoto wakati mwingine wapo karibu zaidi na Roho wa Mungu kulikotunavyodhania. Raisi Heber J. Grant aliandika kuhusu uzoefu alioupatakutokana na sala akiwa bado mtoto katika nyumba ya Raisi Brigham Young:

“Nilipiga magoti . . . ndani ya nyumba ya [Brigham Young] . . . wakati wasala la familia, nikiwa mtoto na pia kijana. Natoa ushuhuda wangu kwambakama mtoto, zaidi ya mara moja, kwa sababu ya maongozi ya Bwana kwaBrigham Young wakati akiwa . . . [akiomba mwongozo wa Mungu, niliinuakichwa changu, niligeuka na kutazama mahali alipokuwa Brigham Youngakisali, kuona kama Bwana alikuwa . . . hapo. Ilionekana kwangu kwambaalikuwa akiongea na Bwana kama vile mtu anavyoongea na mwingine.”(Heber J. Grant, Gospel Standards, pp. 223–24.)

100

Page 110: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Sala yapaswa kuwa ni jambo la kusisimua na kuzoeleka kwa watoto wetukama ilivyokuwa kwa Heber J. Grant. Hadithi ifuatayo yaonyesha ni ninikinaweza kutokea endapo sala ya familia itatumika kwa njia inayopaswaitumike:

Baba mmoja, mkimya, asiye na makuu, aliona vigumu sama kuelezeaupendo wake kwa familia yake. Kwa kusaidiwa na mke wake wakaanzakufanya sala ya familia, na hiyo ikawa fursa ya kusema yaliyokuwa moyonimwake. Kwa binti yao ambaye alikuwa amemuelewa babake vingine,jambo hili lilikuwa kama ufunuo. Sala zake zilikuwa fupi na wakati mwinginemaneno hayakuelezwa vizuri, lakini kumsikia akisema “Mubariki binti yangumpendwa afanye yaliyo mema” ilimsisimua sana.

Mvulana mwoga aliyejidhania kama ‘paka mwoga’, alijisikia fahari mpya namwenye heshima baba yake na mama walipomshukuru Mungu kwa kuwana kijana mpole na mwenye huruma. Na hali ya kujiamini kwa yule kijanailiendelea kukua kutokana na sala wakati hata kaka wake mdogoalipokuwa akimshukuru Baba yetu wa Mbinguni kwa kumpa kaka mkubwana mwenye nguvu.

“Katika matayarisho ya kutoka nje pamoja na familia yetu mume wangualimwomba Bwana aibariki familia yetu ili twende vyema na kila mmojaafurahie kuwa pamoja. Mahubiri tuliyofanya hayakusikika ila sala ile yaunyenyekevu ilituletea ushirikiano.

“Kijana wetu alikuwa amekasirika na mwenye uzito kila tulipojaribukujadiliana tatizo pamoja naye. Tuliamua kufanya mazungumuzo nayewakati atakapokuwa ametulia na ilionekana wakati muafaka ni katika salala familia la saa za asubuhi. Ilikuwa ni wakati nyumba yote ilikuwa kimya natulishirikiana kwa unyenyekevu, hisia zetu za dhati. Tuliona hasira ikipunguakadiri sala ilivyotangulia mazungumzo yetu.

“Katika wakati huo mtulivu wa sala la familia, tunakuwa karibu sisi kwa sisina pia karibu na Baba yetu wa Mbinguni.” (Ann H. Banks, “The ExtraBlessings of Prayer,” Ensign, Jan. 1976, p. 37.)

Waulize washiriki wa darasa waeleze wanayofanya katika kujenga utaratibu wa sala ya familiakatika nyumba zao. Jadili mbinu za kufanya sala zetu ziwe na mafanikio zaidi. Akina kakawaeleze maoni yao kuhusu mafanikio ya sala ya familia zao.

Changamoto1. Fanya sala la familia kama hufanyi hivyo sasa.

2. Thamini sala zako kama tayari unafanya sala ya familia kila mara.Jadiliana na mke wako na watoto jinsi ya kuzifanya bora sala zenu.

Maandiko Matakatifu ZaidiMathayo 5:44 (tuwaombee maadui zetu)

Mathayo 7:7 (majibu hutolewa kwa sala za dhati)

101

Somo la 14

Page 111: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mathayo 26:41 (yatupasa kusali kwa ajili ya kinga dhidi ya majaribu)

Alma 13:28 (yatupasa kusali kwa ajili ya kinga dhidi ya majaribu)

Alma 37:36–37 (yatupasa kusali kwa ajili ya shughuli zetu zote)

M&M 88:119 (yatupasa kuanzisha nyumba za sala)

M&M 88:126 (yatupasa kusali daima)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Somo Sura ya 8, “Kumwomba Baba wa Mbinguni,” Katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Kama unataka, wape kazi washiriki wa darasa kuelezea mafanikio waliyoyapata katika sala

za familia zao.

3. Fungua au funga kipindi kwa wimbo wa “Mungu, Baba yetu, Tusikize Tukiomba” or “Sala niUtashi wa Moyo.”

4. Wape kazi washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko yanayohusiana na somo hili.

102

Page 112: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Nyumba: Kituo cha Mafunzo ya InjiliMadhumuni ya somo hili ni kututia moyo sisi kwa kuifanya nyumba kuwakituo cha kujifunzia injili.

UtanguliziEnos alikuwa mwana wa nabii na mara nyingi alimsikia baba yakeakizungumza juu ya ukweli wa milele. Siku moja alikwenda msitunikuwinda. Alipokuwa huko alisema, “Maneno niliyokuwa nikimsikia babayangu daima akiyasema kuhusu uzima wa milele . . . yalizama sanamoyoni mwangu. Na nafsi yangu ikatamani; nami nilipiga magoti chinimbele ya Muumba wangu” (Enos 3–4). Baada ya kusali mchana kutwa,alisikia sauti ikimwambia kwamba dhambi zake zimesamehewa. Tukio lilelilikuwa muhimu sana kwa Enos kiasi kwamba aliifundisha injili nakuifurahia katika maisha yake yote yaliyosalia.

Enos ni mfano wa kijana mdogo aliyefundishwa vizuri injili nyumbanimwao. Mwandishi mmoja wa Agano la Kale aliandika: “Mfundishe mtotokatika njia impasayo aende, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.”(Proverbs 22:6). Kama tutafuata ushauri huu kama baba, nasi piatunaweza kubarikiwa kuwa na watoto wenye kututii sisi na Bwana pia.

Kuzifanya Nyumba Zetu kuwa Vituo vya KujifunzaFamilia ni taasisi muhimu sana katika Kanisa na katika familia. Ndiyo, nitaasisi ambayo itadumu milele. Kwa sababu hiyo Bwana ametuamurukuzifanya nyumba zetu kuwa mahali ambapo watu wazima na watotowanaweza kujifunza Injili na kukua kwa pamoja.

Soma M&M 68:25–28. Ni wapi ambapo watoto wetu hupata elimu ya msingi juu ya ulimwengutunamoishi? Ni wapi ambapo wanaweza kujifunza juu ya uzima wa milele?

Watoto hujifunza juu ya maisha haya nyumbani, shuleni na kutoka kwamarafiki wanaocheza nao. Lakini si shule wala marafiki wanaowezakuwafundisha watoto wetu injili. Jukumu hili takatifu ni letu sisi ambalotumepewa na Mungu mwenyewe. Na kama tunashindwa kuwafundishawatoto wetu yale ambayo anataka tuwafundishe katika maisha haya,tunayo hatari ya kuwapoteza watoto hao katika maisha ya milele.

Kabla hatujawafundisha watoto wetu injili, tunalazimika kujifunza kwanzasisi wenyewe. Raisi Marion G. Romney alisema: “Wacha kila mwenyeukuhani katika enzi na nguvu za mwito wake aweke utaratibu katikanyumba yake na mara kwa mara afanye mkutano wa jioni wa familia nakwa namna nyingine awalee “watoto wake katika nuru na ukweli’ (M&M

103

Somo la 15

Page 113: Wajibu na Baraka za Ukuhani

93:40).” (“Home teaching and Family Home Evening,” Improvement Era,June 1969, p. 97.)

Hii inamaanisha kwamba kwa kushirikiana na wake zetu, tunalo jukumu lakufundisha kanuni za injili kwa watoto wetu. Ili kutimiza jukumu hili,tunalazimika kuanzisha mazoea ya kujifunza injili katika nyumba zetu kwakushirikiana na wake zetu na kuwatia moyo watoto waige mfano wetu.Mfalme Benyamini aliwaambia wazazi kwamba. “Msikubali kuwaachawatoto wenu . . . ya kwamba wazivunje amri za Mungu, na kupigana nakugombana wao kwa wao na kumtumikia shetani . . .

“Bali wafundisheni kuenenda katika njia za ukweli na kiasi muwafundishekupendana na kutumikiana wao kwa wao.” (Mosia 4:14–15.)

Mpango Wetu wa Familia wa Kujifunza InjiliKama tutafuata ushauri wa manabii tunahitajika kupanga kwa kushirikianana wake zetu namna bora ya kuwafundisha watoto wetu. Ingawaje kilammoja wetu aweza kutimiza madhumuni hili kwa njia tofauti, tunalazimikakutengeneza mpango ulio bora wa kuifanya nyumba yetu kuwa mahali pakujifunza injili.

Andika ubaoni mapendekezo yafuatayo wakati yanapojadiliwa.

TENGENEZA MAZINGIRA YA KUJIFUNZA

Nyumbani kunastahili kuwa mahali ambapo watoto wetu watakuwa hurukuongea nasi. Nyumba ambazo zimejaa ugomvi na hasira haziwatii moyowatoto kuuliza maswali na kuelezea hisia za mawazo yao. Raisi David O.McKay anatuambia kwamba, “wazazi lazima . . . waonyeshe kuwa radhikwa kujibu maswali. Mtoto aulizaye maswali huchangia furaha katikamaisha yako.” (Gospel Ideals, p. 480.) Yatupasa kuwatia moyo watoto wetukuuliza maswali. Hasa kuhusu maswala yahusuyo injili. Yawezekana tusijuemajibu ya maswali yao yote, lakini yawezekana daima tukatafuta majibuhayo pamoja.

Ni kwa njia gani hasa ambazo tunaweza kutumia kuendeleza majadiliano ya injili majumbanimwetu?

KUSALI PAMOJA NA FAMILIA

Njia mojawapo ambayo tunaweza kuwafundisha watoto wetu ni kwa kupitiasala ya familia. Tunaposali, tunaweza kuwasilisha matumaini yetu,mashaka yetu na matakwa ya familia zetu. Twaweza kuwafundisha kuwajalina kuwafikiria wengine tunapoomba kwa ajili ya watu wengine katika familiazetu na wengine. Na tunaweza kufundisha kushukuru kwa baraka paletunapoelezea shukrani zetu kwa Baba yetu wa Mbinguni.

KUWA NA MAJADILIANO YA INJILI WAKATI WA KULA NA KULALA

Nyakati zingine za kushawishi majadiliano ya injili ni nyakati za kula chakulana za kulala. Majadiliano yetu inapasa yashirikishe uzoefu wetu wa kidinikila siku. Watoto wanaweza kutiwa moyo ili waulize maswali juu yao na

104

Page 114: Wajibu na Baraka za Ukuhani

wakubwa waelezee kanuni za injili zilizohusika katika uzoefu. Wakati mzurizaidi wa majadiliano ya namna hii ni wakati wa kuwalaza vitandani watotowadogo usiku. Ili kuwatia moyo waulize maswali, tunaweza kuwaelezahadithi kutoka katika kitabu cha Mormoni au Biblia au kutoka katika uzoefuwetu wa kiroho.

Onyesha picha 15-a, “Nyumba yapaswa kuwa kituo cha Mafunzo ya Injili.”

KUJIFUNZA MAANDIKO MATAKATIFU MARA KWA MARA

Ili kuendeleza mafunzo ya Maandiko Matakatifu, rafu ya vitabu yawezakutengwa kuwa kama maktaba ya injili. Hapa, vitabu, picha, kanda zanyimbo, na radio kaseti na zana zingine za ziada zaweza kuwekwa kwa ajiliya matumizi ya familia yote. Vitabu vya maandiko matakatifu ya Kanisa naKanuni za Injili ndivyo vitabu vya msingi au kanda katika maktaba zetu zanyumbani. Kama yawezekana, kila mtoto yampasa kuwa na nakala yakebinafsi ya kitabu cha Mormoni na Biblia.

Tunaweza kujifunza Maandiko Matakatifu kibinafsi au kama familia. Ilikuimarisha usomaji binafsi wa Maandiko Matakatifu, ni lazima tuwekemfano. Zifuatazo ni njia tunazoweza kujifunza Maandiko kibinafsi.:

• Kwa kusoma Maandiko Matakatifu kutoka mwanzo wa kitabu hadimwisho, kwa kusoma sura moja au zaidi kila siku, au kwa dakika kumi natano kila siku.

• Kwa kujifunza Maandiko Matakatifu kwa mada (kama sala au utii),ukionyesha vipengele vya marejeo juu ya mada hiyo.

• Kwa kutafiti maandiko ili kupata majibu ya matatizo fulani yanayotukabili.

• Kwa kuorodhesha maandiko yale yanayotugusa moyoni.

• Kwa kulinganisha andiko moja na jingine katika mpango wako wakawaida wa kujifunza maandiko.

Washawishi washiriki wa darasa kufikiria njia nyingine wanazoweza kujifunza MaandikoMatakatifu.

Ili kujifunza injili kama familia, kila baba yampasa kupanga mudakushirikiana na mkewe na watoto wakati watakapopata nafasi mahususikwa ajili ya jambo hili. Zifuatazo ni baadhi ya njia tunazoweza kujifunzamaandiko kama familia:

• Panga kwa muda wa dakika kumi na tano kujifunza maandiko kilaasubuhi kabla ya kuondoka kwenda kazini na watoto kabla ya kwendashule, au fanya familia dogo la jioni kujifunza maandiko kabla ya watotokwenda kulala.

• Wasimulie watoto wadogo hadithi zilizomo katika maandiko matakatifu

• Chagua mistari maalumu ya maandiko, iandike kwenye kadi, nauibandike kadi hiyo katika ubao wa matangazo au ukutani mahaliambapo wanafamilia wote wataiona.

105

Somo la 15

Page 115: Wajibu na Baraka za Ukuhani

15-a

Page 116: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Watie moyo wanafamilia kuikariri mistari ya maandiko.

• Chagua andiko ambalo linafundisha kanuni na fanyeni uamuzi wa jinsi yakuitekeleza kanuni iliyofundishwa. Kwa mfano, soma Mathayo 25:31–40;halafu kama familia isaidieni familia yenye shida. Soma Yakobo 1:26–27na Wagalatia 6:2, halafu wasaidieni watu walio wazee.

• Someni hotuba za mkutano mkuu wa Kanisa uliopita na yafanyieni kazimambo yaliyoshauriwa na viongozi wa Kanisa.

Njia yoyote tutakayoichagua kuifuata, lazima tuanze mafundisho hayo kwasala, tukimuomba Baba wa Mbinguni kwa mwongozo na kuelewa. Baadaya kipindi cha kujifunza, yatupasa kuyatafakari yale tuliyojifunza na jinsitunavyoweza kuzitumia kanuni za Injili tulizozisoma katika maisha yetu.

Askofu H. Burke Peterson wa Maaskofu Wasimamizi amesema:“Hapapaswi kuwepo— wala pasiwepo—familia moja katika Kanisa hiliambao haina muda wa kujisomea Maandiko Matakatifu kila siku. Kilafamilia yaweza kufanya hivyo kwa namna yake.” (“Helps for Parents,”Ensign, May 1975, pp. 53–54.)

Uwe na Mshiriki wa darasa aliyepewa kazi hapo mwanzo na akajipatia mafanikio, siyo tukatika kusoma, atoe taarifa ya mbinu alizotumia kufikia hatua hiyo. Au kijana wa ukuhani waHaruni aeleze ni kwa nini yeye anahisi kuwa ni muhimu kujifunza injili katika ujana wake, hasakabla ya kwenda katika misieni. (Pengine atataka kusoma Alma 37:35.)

Onyesha picha 15-b, “Jioni ya Familia nyumbani ni wakati mzuri wa kujifunza injili kamafamilia.”

KUFANYA MIKUTANO YA JIONI YA FAMILIA KILA MARA

Mafunzo ya familia ya Jumapili au jioni ya familia nyumbani siku yaJumatatu jioni ni nyakati nzuri za kuwafunza watoto injili. Kwa walemiongoni mwetu walio na vitabu vya mwongozo vya Mkutano wa Jioni waFamilia Nyumbani wanapaswa kuvitumia. Kama hakuna kitabu hicho,yatupasa kujifunza Maandiko na Kanuni za Injili, kusikiliza kanda za injili aukusimuliana hisia zetu juu ya Kanisa. Kujenga mazingira mazuri na yakufurahisha yatawasaidia watoto kufaidika jioni hiyo na kuweza kushirikikwa urahisi na kwa ridhaa yao. Jioni ya familia nyumbani siyo wakati wakuzihubiria familia.

KUTOA USHUHUDA KWA WATOTO WETU

Nafasi inapojitokeza yenyewe, inatulazimu kutoa ushuhuda wetu kwawatoto wetu. Nafasi hiyo yaweza kuja wakati wa chakula, wakati wakujifunza injili, wakati wa jioni ya familia au katika kujadili injili pamoja nawatoto wetu. Kwa kutusikia tukitoa ushuhuda wetu na kutuona tukiwekaamri za Mungu maishani mwetu kutawaongezea ufahamu wao juu ya injili.

Washiriki wa darasa waeleze uzoefu wao walioupata katika kuwafundisha watoto wao injili.

107

Somo la 15

15-a, Nyumba yapaswa kuwa kituo cha mafunzo ya injili

Page 117: Wajibu na Baraka za Ukuhani

15-b

Page 118: Wajibu na Baraka za Ukuhani

MwishoKadiri tunavyojifunza injili kibinafsi na pamoja na familia zetu, ushuhudawetu na nyumba zetu zitaimarika. Kwa sababu tunajaribu kuishi karibu naYesu Kristo na Baba yetu wa Mbinguni, tutapata majibu ya matatizo yetuna kuwa na amani kubwa akilini mwetu. Mzee Bruce R. McConkiealisema: Tunataka kuwa na amani na raha na furaha katika maisha hayana kuwa warithi wa uzima wa milele katika ulimwengu ujao. Hizi ni barakakubwa mbili ambazo yawezekana watu kuzirithi. Tunaweza kuzipata kwakusoma na kujifunza maneno ya uzima wa milele, hapa na sasa na kwakuziweka amri.” (Bruce R. McConkie, “Drink from the Fountain,” Ensign,Apr. 1975, p. 70.)

Changamoto1. Soma injili kila mara.

2. Fanya sala la familia kila siku.

3. Tumia kila nafasi kwa kuifundisha injili familia yako.

Maandiko Matakatifu ZaidiWarumi 15:4 (maandiko Matakatifu yote yaliandikwa ili kutusaidia sisi)

2 Timotheo 3:14–17 (haja ya Maandiko Matakatifu)

2 Nefi 4:15 (yatupasa tuyatafakari Maandiko Matakatifu na kuwafundishawatoto wetu)

M&M 1:37 (inatulazimu kuyatafiti Maandiko Matakatifu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma maandiko matakatifu zaidi yaliyotolewa mwisho wa somo hili.

2. Tayarisha orodha ubaoni ya njia za kupata utaratibu wa kujifunza injili uliojadiliwa katikasomo hili.

3. Kama unataka, chagua washiriki wa darasa waweze kuelezea uzoefu walioupata au kwakujifunza au kwa kufundisha injili.

4. Wachague washiriki wa darasa watoe hadithi na maandiko matakatifu yanayohusiana nasomo hili.

109

Somo la 15

15-b, Jioni ya Familia Nyumbani ni wakati mzuri wa kujifunza injili kwa pamoja kama familia

Page 119: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kujitayarisha Kufundisha

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kutambua wajibu wetu kwakujitayarisha kufundisha injili kwa mafanikio mazuri.

Utangulizi“Usitake kulitangaza neno langu, bali kwanza utafute kulipata neno languna ndipo ulimi wako utalainishwa; na endapo ukitaka, utapata kuwa naRoho wangu na neno langu, ndio nguvu za Mungu katika kuwashawishiwanadamu” (M&M 11:21).

KufundishanaWaulize washiriki wa darasa kusoma M&M 88:77–78. Tunapaswa kumfundisha nani?

Nafasi za kufundisha injili ni nyingi na zinatofautiana. Tunaweza kufundishafamilia zetu, marafiki, majirani, wafanyikazi wenzetu na wanafunzi wenzetu.Tunaweza kuwafundisha waumini wenzetu wa Kanisa katika madarasamaalumu, na wale wasio waumini wa Kanisa tuwapo pamoja nao kazini.

Onyesha picha 16-a, “Baba anawajibu wa kuwafundisha watoto wake injili.”

KUFUNDISHA KATIKA NYUMBA

Toka kuumbwa kwa dunia, tumeambiwa na Bwana kwamba tunalo jukumukubwa la kuwafundisha watoto wetu injili. Wakati mzuri wa kuzifundishafamilia zetu ni siku za Jumapili au wakati wa jioni ya familia nyumbani sikuya Jumatatu, lakini pia zipo nafasi nyingi na nyakati tofauti. Hadithi ifuatayoinaelezea jinsi baba mmoja alivyojifunza kuifundisha familia yake:

Akina baba kadhaa walijihusisha na mafunzo yahusuyo jioni ya familianyumbani. Wengi wao walieleza hisia zao kama ifuatavyo, “Mimi siyomwalimu; sijawahi kuwa na wala sitakuwa.” Waliahidiwa kuwa kamawataziita familia zao pamoja kila wiki katika hali ya utulivu, sehemu yaufundishaji haitakuwa tatizo kama wao wanavyodhania.

Baba mmoja, ambaye jina lake lilikuwa Jerry hakuonekana kuwa mwenyeuju juu ya jambo hilo. Alijaribu kujitoa katika jambo hilo kwa kusema,“Siwezi kufundisha.” Lakini alijiwekea ahadi binafsi na aliiheshimu ahadialiyojiwekea.

Miezi mitatu baadaye, alipoulizwa juu ya uzoefu wake, alikuwa amefurahia nakuwa mchangamfu na watoto wake walionyesha shauku waliyokuwa nayokwa yale yaliyokuwa yakitendeka katika wakati wa jioni ya familia nyumbani.

110

Picha 16-a, Baba analo jukumu la kuwafundisha watoto wake injili

Somo la 16

Page 120: Wajibu na Baraka za Ukuhani

16-a

Page 121: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mke wake alisema, “Limekuwa ni jambo la kupendeza sana kwetu.Masomo mazuri tuliyoyapata yamekuwa ni yale ambayo Jerryalitufundisha.”

Jerry aliinama chini kwa muda na kubaki kimya. Hatimaye alisema; “Ah,sikuwa nimefanya vizuri sana.”

Mke wake alimaka na kwa dhati akajibu, “Jerry, wakati ulipokuwaukitufundisha ilionekana kutuingia kwa nguvu. Ilionekana kwamba sisi nifamilia. Hatutasahau mambo uliyoyasema.”

Jerry aliguswa sana na maneno hayo ya moyoni. Alitazama juu na kusema,“nadhani nilifanya vizuri sana. Sikutaka kufanya mafundisho ya jioni yafamilia, sikutegemea kwamba ningeliweza kufanya vizuri. Lakini usikummoja baada ya mke wangu kuwa amefundisha somo wiki moja na bintiyangu wiki iliyofuata, niliamua nami nitajaribu moja.”

Macho yake yalilengalenga machozi na akasema: “Sitasahau hisianilizokuwa nazo moyoni wakati nikizungumza juu ya mambo mazuri nafamilia yangu. Ilionekana kwamba kwa mara ya kwanza nimekuwa babaniliyetakiwa kuwa.” (Tazama George D. Durrant, Love at Home, StarringFather, pp. 41–43.)

Hadhithi hii inaonyesha ni nini chaweza kutokea tunapopokea majukumuyetu ya kufundisha familia yetu.

Waulize ndugu waelezee uzoefu walionao katika kufundisha injili kwa watoto wao.

Mzee Boyd K. Packer alisema: “Mengi tuyafanyayo ni kufundisha.Kumwonyesha kijana jinsi ya kufunga kamba za viatu vyake, . . . kumsaidiabinti kutengeneza chakula kipya, kuhubiri Kanisani, kutoa ushuhuda,kuongoza mikutano ya viongozi na pia kufundisha darasa—haya yote nikufundisha na tunayafanya mara kwa mara . . . Tunafundisha tunapohubiriau tunapojibu maswali katika mikutano.” (Teach Ye Diligently, pp. 2–3.)

KUFUNDISHA KATIKA KANISA

Sehemu kubwa ya mafundisho hufanyika bila mpangilio kama tuongeapona wenzetu. Lakini Kanisa pia hutupa sisi nafasi nyingi za kufundisha katikamadarasa yaliyoandaliwa.

Mzee Boyd K. Packer ameandika: “Kila mshiriki wa Kanisa hufundishakatika kipindi chote cha maisha yake . . . tunao walimu ambao hufundishakatika taasisi zote katika Kanisa. Sehemu kubwa ya kazi hii hufanyikakatika Vikundi vya ukuhani ndiyo kila mwenye ukuhani anayohaki yakupangiwa kuwa mwalimu wa nyumbani . . . Kanisa linasonga mbelelikisimamiwa ni uwezo wa kufundisha uliokamilika. Kazi ya ufalme[huchelewa] kama ufundishaji siyo mzuri.” (Teach Ye Diligently, pp. 2–3.)

Wakati mwingine kufundisha kwetu hakufanyiki darasani, lakini kwa kupitiamahusiano yetu na wengine katika Kanisa. Ifuatayo ni mifano yakufundisha kunakofanyika nje ya darasa:

112

Page 122: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Askofu Fred Caroll alitokezea pichani wakati familia yetu ilipohamia katikakata yake nilipokuwa na umri wa kumalizia daraja la shemasi katikaukuhani wa Haruni. Mtu huyu maarufu aliongea nami si zaidi ya manenohamsini tukiwa ana kwa ana; hata hivyo ishirini na tano kati ya manenohayo yamebaki kama chapa akilini mwangu. Nina hakika kwamba askofuhuyu mwema hakujua athari kubwa aliyoiacha juu yangu kwa maneno yaleishirini na tano ya dhahabu aliyonipa siku moja kwa ukimya na kwafaragha: ‘Nimekuwa nikiona vile umekuwa kimya katika mikutano yetu yakanisa. Ni mfano mzuri unaouweka kwa wavulana wenzako waufuate.’

“Ni maneno machache tu, lakini Ah, yana nguvu kiasi gani! Kwangu mimiyalikuwa na athari kubwa kuliko kazi zote nilizoweza kupewa. Mpaka wakatihuo sikuwa nikijiona kama mtu mnyenyekevu. Nina hakika kabisa AskofuCaroll aliodhania kuwa haya yangu ni aina ya unyenyekevu. Hata hivyosikujali. Tokea wakati huo na kuendelea nilikuwa nikitafakari maana yaunyenyekevu au heshima katika maisha yangu. Ghafla nikaanza kujisikiamnyenyekevu. Yawezekana, kama Askofu Caroll alidhania kwambanilikuwa mnyenyekevu labda ni kweli ilikuwa hivyo! Wazo hilo liliendeleakukua ndani yangu kwa sababu Askofu Caroll aliipanda mbengu hiyo nayoimekuwa na kuwa mwongozo wa kunishawishi katika maisha yangu.” (LynnF. Stoddard, “The Magic Touch,” Instructor, Sept. 1970, pp. 326–27.)

Mzee Thomas S. Monson ameandika: “Wakati walimu waliojitolea kwadhati wanapoitikia [Mwokozi] katika mwito wake; Njoo ujifunze kwangu,’hujifunza, lakini pia wao hupokea nguvu zake za kimungu. Nilipatwa najambo hili nilipokuwa mvulana mdogo nilifundishwa na mwalimu wa ainahiyo. Katika darasa letu la shule ya Jumapili, alitufundisha juu ya muumbajiwa dunia, anguko la Adamu na upatanisho wa Yesu Kristo. Aliwaletadarasani kama wageni waheshimiwa Musa ,Yoshua, Petro, Tomasi, Paulona Yesu Kristo. Ingawa hatukuwaona, tulijifunza kuwapenda, kuwaheshimuna kuwafuata.

Mafundisho yake hayakuwa na nguvu sana wala athari zake hazikuwa zakudumu kama ilivyokuwa asubuhi ya Jumapili moja kwa huzuni kubwaalipotutangazia kifo cha mama wa mwanafunzi mwenzetu. Asubuhi ile Billyhakuwa nasi lakini hatukujua sababu ya kukosekana kwake. Somo lilelilionyesha mada; ‘Ni baraka kubwa kutoa kuliko kupokea.’ Katikati yasomo, mwalimu wetu alifunga kitabu na akatufungua macho, masikio namioyo yetu kwa ajili ya Utukufu wa Mungu. Alituuliza, Tunazo pesa kiasigani katika mfuko wetu wa Tafrija wa darasa?

“Siku za mdororo wa shughuli za uchumi zilichochea jibu la majivuno,‘Dola nne na senti sabini na tano.’

“Halafu kwa upole alishauri: ‘Familia ya akina Billy wako na dhiki na niwenye huzuni. Jee mnafikiri kuna uwezekano wa kuwatembelea asubuhi hiina kuwapa wao akiba yenu?’

113

Somo la 16

Page 123: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Daima nitakumbuka kikundi hiki kidogo kikitembea hatua za mitaa mitattatu na kuingia katika nyumba ya akina Billy kumsalimia yeye, kaka yake, dada zake na baba yake. Tulijua wazi kabisa mama yao ndiyealiyekosekana. Daima nitakumbuka na kuthamini machozi yaliyokuwayakingara machoni mwao wote wakati bahasha nyeupe yenye akiba yetu yapesa za tafrija kutoka katika mikono laini ya mwalimu wetu kwenda kwenyemikono yenye kuhitaji ya baba aliyevunjika moyo. Karibu tuipotee njia yakurudi kanisani kwetu. Mioyo yetu ilikuwa myepesi kuliko siku yoyote; furahayetu ilifurika; na ufahamu wetu ulikuwa mkubwa na wa uhakika. Mwalimualiyeongozwa na Mungu amewafundisha wavulana na wasichana somo lamilele na ukweli wa Kimungu. ‘Kuna baraka kubwa katika kutoa kuliko katikakupokea.’ ” (“Only a Teacher,” Ensign, May 1973, p. 29.)

KUFUNDISHA KATIKA ULIMWENGU

Kila mshiriki wa Kanisa ni mmisieni akiwa na majukumu ya kufundisha injilikwa maneno na vitendo kwa kila mtu anayemjua. Tulifanya agano wakatiwa ubatizo “kusimama kama mashahidi wa Mungu wakati wote na katikamambo yote, na mahali pote na kwamba tuwe hivyo hata mpaka kifo.”(Mosia 18:9). Tunapowafundisha marafiki na majirani zetu yatupasakufanya hivyo kwa upole na kwa uvumilivu (tazama M&M 38:40–41).

Tumepewa jukumu kubwa, siyo tu kuwafundisha watoto wetu, au washirikiwa Kanisa bali kila mtu ambaye tunakutana naye.

Onyesha picha 16-b, “Masomo sharti yatayarishwe tukifikiria juu ya kila mshiriki wa darasa,”na 16-c, “utayarishaji wa somo ni pamoja na kujifunza Maandiko Matakatifu na sala.”

Kujitayarisha Kufundisha InjiliKama twataka kuwa walimu wazuri, yatupasa kujiandaa vyema. “Hakunamwalimu awezaye kufundisha mambo asiyoyajua.” Raisi David O McKayalituambia. “Hakuna mwalimu awezaye kufundisha kile ambacho [yeye]hakioni wala hakisikii.” (Treasures of Life, p. 476.)

Kwa nini ni muhimu kwetu sisi zote, pamoja na wavulana, kujitayarisha kufundisha vizuri? Nimbinu gani za utayarishaji ambazo waweza kuzipata katika taarifa hii?

Tenga muda na mahali maalumu kwa ajili ya kupanga somo lako. Patavifaa vyako— Maandiko Matakatifu, vitabu vya maelezo, kumbu kumbu,karatasi, penseli—ziwe tayari. Anza somo lako kwa kumshirikisha Bwana—Mpangaji Mkuu. Hii ni injili yake; wewe ni mwalimu wake, ukiwafundishawatoto wake. Muulize Bwana ni namna gani anataka ujumbe ufundishwe.Unapohisi mahitaji maalumu yanahitajika, basi kufunga hapana budikuambatane na sala kama njia ya kutafuta msaada wa Roho wa Bwana.(Teacher Development Program, Basic Course, revised 1972, p. 133.)

Orodhesha ubaoni vitu ambavyo utahitaji kufanya na vifaa ambavyo utakuwa navyo kwa ajiliya kuandaa somo.

114

Picha 16-b, Somo litayarishwe kwa kumfikiria kila mshiriki wa darasa

Page 124: Wajibu na Baraka za Ukuhani

16-b

Page 125: Wajibu na Baraka za Ukuhani

16-c

Page 126: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Raisi David O. McKay alikuwa mwalimu aliyehitimu kabla ya kuitwa kuwaKiongozi wa Jumla Katika Kanisa. Alipendekeza hatua nne za utayarishajiwa somo kwa ajili ya darasa:

DHIHIRISHA SHABAHA YA SOMO

Ujumbe ni wazo ambalo unataka washiriki wa darasa wajifunze nakuufanyia kazi. Andika lengo lako na ulitafakari wakati ukitayarisha somo.

VIFAHAMU VIFAA VYA SOMO

Ulifahamu vyema somo kiasi kwamba utaweza kulifundisha kwa manenoyako. Ijapo kuwa, maandiko matakatifu na nukuu zaweza kusomwa kutokakwenye vitabu vidogo vya maelezo.

KUSANYA VIELELEZO VYA KUFUNDISHIA KUTOKA NANA UTAFITI NA MAFUNZO

Ili kujenga hali ya uchangamfu katika somo, tumia vielelezo, kama vitu,ramani, picha, au vitu vingine vinavyosaidia. Kujenga hali ya uchangamfuni muhimu katika kuwafundisha watu wa rika zote.

PANGA VIELELEZO VYA SOMO NA VIFAA

Weka kila kitu utakachohitaji tayari wakati wa somo lako kama vile chaki,ufutio, karatasi, penseli na vielelezo vya kufundishia. Vitu hivi yapaswakupangwa kwa namna ambayo umepanga kuvitumia ili kukusaidiakuepuka hali ya kuchanganya wakati wa kufundisha somo.

Kujifunza Kuwapenda Wale TunaowafundishaMzee Boyd K. Packer amesema: “Mwalimu mzuri ni yule ambayeamekwisha kujifunza somo. Na mwalimu bora pia hujifunza juu yawanafunzi wake—hujifunza juu yao kwa dhati na kwa makini . . .Unapojifunza kwa uangalifu maumbile na mienendo ya wanafunzi wakondipo kunaweza kukawepo ndani ya moyo wako huruma ya Kikristo . . .Huruma ni hisia inayofanana; ni upendo ambao utatufanya au tulazimishakufanya kazi za Bwana—Kulisha Kondoo Wake.” (“Study Your Students,”Instructor, Jan. 1963, p. 17.)

Kwa upande mwingine, wanafunzi wanaopendwa huwa na uwezo mkubwawa kujiamini na huwa na ari ya kujiendeleza wenyewe, watakuwa wasikivu,wenye ushirikiano na wenye msaada katika darasa. Zaidi ya yote,wanafunzi wanaopendwa watajifunza kuwapenda wenzao.

Kufundisha kwa Kuongozwa na RohoKama mwalimu atataka kuwapenda wanafunzi wake ni lazima awe makinikwa mwongozo toka kwa Mungu. Ni kwa njia hii tu ndipo ataweza kwauhakika kutambua mahitaji ya wanafunzi wake. Raisi Brigham Youngalisema: “Baada ya jitihada yetu yote ya kutafuta hekima kutoka kwenye

117

Somo la 16

Picha 16-c, Matayarisho ya somo hufanyika kwa kujifunza maandiko matakatifu kwa maombi

Page 127: Wajibu na Baraka za Ukuhani

vitabu vilivyo bora na kadhalika, bado patabakia kisima kilicho wazi kwaajili ya watu wote; ‘Kama mtu yeyote wa Kwenu akipungukiwa hekima naaombe kwa Mungu.’ ” (Discourses of Brigham Young, p. 262.)

Uwezo wa kufundisha ni kipawa tupewacho na Baba yetu wa Mbinguni.Endapo tutamuomba yeye, atatupa mwongozo wakati tukitayarisha somo,tukitafuta kuwajua na kuwapenda wanafunzi wetu, na tukifundisha. Natukifundisha na Roho wake, tunafundisha kwa nguvu zake. (Kwa habarizaidi, angalia somo la 18 “Kufundisha kwa Nguvu za Roho Mtakatifu.”)

Mwisho“Raisi David O. McKay alisema: ‘Hakuna jukumu kubwa zaidi dunianikuliko kuifundisha nafsi ya mwanadamu.’ Sehemu kubwa ya utumishibinafsi wa kila mzazi na mwalimu katika Kanisa ni kufundisha na kuandaa.”(Vaughn J. Featherstone, “The Impact Teacher,” Ensign, Nov. 1976, p.103.) Tunalo jukumu la kufundisha injili ya Yesu Kristo kwa watoto wetu nawashiriki wenzetu wa Kanisa na majirani zetu wasiokuwa waumini. Ilikufanya hivi yatupasa kujitayarisha kwanza sisi wenyewe kwa kujifunza nakuiishi injili hiyo.

Ni kwa namna gani maisha ya haki hutusaidia kuifundisha kwa mafanikio?

Changamoto Tayarisha na fundisha somo kwenye mkutano ujao wa jioni ya familia kwakujifunza na kwa maombi kwa ajili ya kupata mwongozo wa Roho Mtakatifu.

Maandiko Matakatifu ZaidiKumbuKumbu la Torati 6:1–7 (umuhimu wa kuwafundisha watoto wetudaima)

Mosia 4:14–15 (namna ya kuwafunza watoto wetu kwa ufasaha)

M&M 68:25–28 (wazazi yawapasa kuwafunza watoto wao injili)

M&M 130:18 (tutakuwa na elimu tuliyopata katika maisha haya wakatitutakapofufuliwa)

Matayarisho ya mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Wakumbushe washiriki wa darasa kuja na vitabu vyao vya maandiko matakatifu darasani.

2. Kama unataka waulize washiriki kadhaa waelezee uzoefu walionao katika kuwafundishawatoto wao.

3. Wapangie washiriki kadhaa wa darasa kutoa hadithi na maandiko yahusianayo na somohili.

118

Page 128: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kufundisha Kutoka Kwenye MaandikoMatakatifuMadhumuni ya Somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kwa nini yatupasakufundisha kutoka kwenye Maandiko Matakatifu wakati tunapofundishakatika Kanisa.

UtanguliziOnyesha picha 17-a, “Inatulazimu kujifunza Maandiko Matakatifu endapo twataka kufundishayaliyomo ndani yake,” na 17-b, “Kufundisha Injili kunataka uwe na elimu nzuri juu yaMaandiko Matakatifu.”

Raisi J. Reuben Clark, Jr. wakati fulani alielezea kikundi cha walimu katikaKanisa: “Kazi yenu . . . muhimu ni kufundisha injili ya Bwana YesuKristo . . . Mtaifundisha injili hiyo kwa kutumia kama chanzo na mamlakaya Maandiko Matakatifu ya Kanisa na maneno ya wale ambao Bwanaamewateua kuwaongoza watu wake katika hizi siku za mwisho.” (TheCharted Course of the Church in Education, p. 9.)

Kuyafahamu Maandiko Matakatifu na kuyatumia tunapofundisha nikielelezo kikubwa cha msaada wa kufundishia tulionao.

Umuhimu wa Kufundisha Kutoka Kwenye Maandiko MatakatifuBwana kwa uwazi kabisa ametufundisha umuhimu wa kuyajua nakuwafundisha wengine juu ya Maandiko Matakatifu. Wakati alipowatembeleaWanefi, yeye alisema. “Amri ninawapeni ninyi ya kwamba yatafitini mambohaya (Maandiko Matakatifu) kwa bidii kubwa.” (3 Nefi 23:1.) Tunapaswakuyatafiti kwa sababu yanatufundisha juu ya Yesu Kristo na kwa sababu “niya kweli na ya uaminifu na utabiri na ahadi zilizomo ndani yake zote zitakujakukamilika.” (M&M 1:37 2; pia tazama 1 Nefi 19:23.)

Soma M&M 68:1–4. Ni maandiko matakatifu gani tuliyonayo leo kama nyongeza juu ya yaleya kawaida? Ni wapi ambapo tunaweza kuyapata maandiko hayo? (The Ensign and GeneralConference Reports.)

Kufundisha Maandiko Matakatifu kwa MafanikioWakati Lehi na familia yake walipofika katika nchi ya ahadi, Nefialiwafundisha nduguze Maandiko Matakatifu katika namna ambayowaliweza kuelewa: Kwani niliyalinganisha maandiko matakatifu hayo na sisi.” Alisema, “ya kwamba yaweze kuwa ya faida kwetu na pia kwamaarifa.” (1 Nefi 19:23). Kuyalinganisha Maandiko Matakatifu yote na sisini muhimu sana kama tunataka kufundisha kwa mafanikio. Nabii Joseph

119

17-a, Tunalazimika kujifunza maandiko kama tunataka kuyafundisha17-b, Kufundisha Maandiko Matakatifu kwahitaji elimu nzuri ya maandiko hayo

Somo la 17

Page 129: Wajibu na Baraka za Ukuhani

17-a

Page 130: Wajibu na Baraka za Ukuhani

17-b

Page 131: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Smith alisema: “Tafitini maandiko, watafitini manabii na jifunze sehemugani yawahusu ninyi.” (Teachings of the Prophet Joseph Smith, p. 12.)Walimu wazuri mara nyingi huyalinganisha Maandiko Matakatifu na halihalisi ya wakati wetu kwa kuonyesha namna matukio ya kaleyanavyokaribiana na ya wakati huu.

Onyesha picha 17-c, “Nefi na Lehi wanaiona Liahona.”

Hadithi ifuatayo kutoka katika Kitabu cha Mormoni ilitumika kwa namna hiina Raisi Spencer W. Kimball:

“Jifikirie wewe ukiwa Nefi ambaye alimsikia Baba yake kwa shauku akiwaitakwa ajili ya kitu alichokigundua kikiwa nje ya mlango wa hema lake. Ilikuwakidude cha mviringo.. .. kilichofanyizwa kwa ustadi mkubwa,kilichotengenezwa kwa shaba iliyo nzuri na hakuna hata mmoja waoaliyewahi kuona kitu cha aina hiyo awali. (1 Nefi 16:10.)

“ . . . Kama ungelikuwa umependezwa zaidi na ukachunguza kwa makinikazi iliyokuwa ikifanywa na kitu hiki, ungegundua ya kwamba kilifanya kazikulingana na imani na bidii na utii ambao unao kuhusu njia upasayokwenda (1 Nefi 16:28) . . . Kwa uchunguzi wa karibu ungegundua kuwakulikuwa na maandishi juu ya kidude hicho na kwamba yalikuwa ‘wazikuzomeka’ na . . . yalielezea njia za Bwana. [Na kama ungetoa maombikwa Bwana, mashauri yangelibadilika. Mabadiliko ya mashauri yalikuwakwa kulingana na imani na juhudi ya familia yako. (1 Nefi 16:28).]

“ . . . Kidude au Liahona—ambacho tafsiri yake inamaanisha dira—kilitayarishwa rasmi ili kumwonyesha Lehi njia ambayo alipaswa kuifuatahuko nyikani. Wewe ungelipenda kuwa na kitude kama hicho—kila mmojawenu—ili kwamba wakati uwapo katika makosa kiweze kukuonyesha njiailiyosahihi na kuandika ujumbe kwako, ili kwamba daima uweze kujuauwapo katika makosa au katika njia isiyo sahihi?

“Kwamba, ndugu zangu, nyote mnacho, Bwana amempa kila mvulana, kilamwanamume, kila mtu dhamira ambayo kila mara humjulisha anapoanzakwenda katika njia isiyosahihi. Kila mara huambiwa endapo atasikiliza lakiniwatu wanaweza kuwa wamezoea kiasi kwamba wanapuuza sauti hiyompaka mwishowe hawaisikii kabisa.

“Lazima ujue ya kuwa unacho kitu kama dira kama Liahona katika mfumowako. Kila mtoto amepewa . . . Na kama ataipuuza Liahona aliyonayokatika maumbile yake mwenyewe, hatimaye itaacha kumnongonezea.Lakini kama tutakumbuka ya kwamba kila mmoja wetu anayo (Liahona)ambayo itatuongoza katika usahihi, meli yetu haitaenda mrama . . . kamatutasikiliza mwongozo wa Liahona zetu ambazo tunaziita dhamiri.” (Ensign,Nov. 1976, pp. 77–79.)

122

17-c, Nefi na Lehi waiona Liahona

Page 132: Wajibu na Baraka za Ukuhani

17-c

Page 133: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ni kwa namna gani Raisi Kimball alitumia Maandiko Matakatifu kufundisha ukweli tunaowezakuuona leo?

Wakati tukiwa na elimu juu ya Maandiko Matakatifu, tunaweza kutumiakanuni tulizofundishwa kwenye hali zilizo katika maisha yetu sasa. Mfanoufuatao unaonyesha namna baba huyu alivyofundisha maandikomatakatifu kwa watoto wake:

“USIHUKUMU. ILI NAWE USIJE UKAHUKUMIWA”

Lara na Todd wameambiwa mara nyingi wasiache baiskeli zao barabarani.Siku moja Baba yao alirudi nyumbani na kuzikuta baiskeli zote ziko kwenyekibarabara cha kuingia nyumbani. Baba alimkabili Todd kwanza. “Todd,”alimwambia, “Nimeikuta baiskeli ya Lara kwenye kibarabara cha kuingiahuku nyumbani. Je nifanye nini?”

“Unapaswa kumsimamisha kwa kiasi cha juma zima, kama ulivyotuambiautafanya,” Todd alijibu.

Na baadaye Baba alimwambia Lara; “Nimeikuta baiskeli ya Toddbarabarani, nifanye nini?”

“Msamehe leo; atakumbuka siku nyingine,” Lara alijibu.

Baba sasa aliwaita wote pamoja ili wasome Mathayo 7:1–2.

Someni Mathayo 7:1–2.

Walipomaliza kusoma mistari hii, Baba alisema, “Todd, weweumesimamishwa kwa juma moja. Nitaichukulia hii kuwa kama onyo kamautaenda nje na kuondoa baiskeli yako sasa hivi.”

“KIBARUA NI THAMANI YA UJIRA WAKE”

Ron alipatana na baba yake kuosha madirisha yote ya nyumba yao kwamalipo ya dola kumi. Kaka yake, Rick, alipatana kupaka rangi chumba chakulia pia kwa dola kumi. Ilimchukua Roni nusu ya siku kuweza kusafishamadirisha yote. Na ilimchukua Rick siku mbili kupaka rangi chumba kile.Wakati baba alipowalipa wote dola zao kumi kila mmoja, Rick alipinga kwamadai kwamba yeye alipaswa kulipwa zaidi kwa sababu alifanya kazi kwamuda mrefu. Kwa kumjibu, Baba alimwambia asome Mathayo 20:1–15.

Someni Mathayo 20:1–15.

Baba alimalizia kwa kusema kuwa yeye ametimiza ahadi yake yamakubaliano, hivyo basi Rick yampasa kukubali na wala asimkasirikie.

Namna gani tunaweza kuyatumia kila aina ya Maandiko Matakatifu yafuatayo katika hali halisiya maisha yetu leo? Someni na mjadili moja baada ya nyingine Mathayo 25:1–13; Enos 2–8na M&M 40:1–3.

Kujitayarisha Kufundisha Kutoka Kwenye Maandiko MatakatifuRaisi Harold B. Lee alisema, “Nasema ya kwamba tunahitajikakuwafundisha watu wetu kupata majibu yao katika Maandiko Matakatifu . . .Lakini kitu cha bahati mbaya ni kwamba wengi wetu hatusomi maandiko

124

Page 134: Wajibu na Baraka za Ukuhani

hayo. Hatujui kilichomo ndani yake na hivyo basi tunakisia au otea juu yamambo ambayo tunapaswa kuwa tumeyaona katika maandiko sisiwenyewe. Ninafikiri ya kwamba humu ndimo” ilimo moja ya hatari kubwakwetu leo.” (“Tafuta Majibu katika Maandiko Matakatifu,” Ensign, Dec. 1972,p. 3.)

Hakuna mtu atakayetulazimisha kusoma Maandiko Matakatifu. Kamatunataka, tunaweza kupata sababu dhaifu nyingi zinazotuzuia tusijifunzewala kuyatafiti maandiko. Ni lazima tujitahidi kujifunza maandiko nakuitengenezea ratiba ya mafunzo hayo. Kama tutafanya hivyo,tunapokutana na haja ya kufanya uamuzi wa kusoma Maandiko Matakatifuau hatari nyinginezo au magazeti ya michezo tutachagua MaandikoMatakatifu kwa sababu tayari tumekwishafanya uamuzi.

Uwezo wa kusoma, kufurahia, na kufundisha Maandiko Matakatifu siyo tuhuhitajika kupangwa, pia huhitaji maandalizi na maombi.

Soma Moroni 10:3. Moroni anatuambia nini kuhusu kusoma Maandiko Matakatifu?

Tunaposoma maandiko matakatifu, yatupasa kuyatafakari mioyoni mwetu.Raisi Marion G. Romney alisema, “Ninaposoma maandiko matakatifu,ninakuwa nakabiliwa na neno tafakari . . . Kamusi inasema kwamba nenotafakari maana yake ni kupima akilini, kufikiri kwa kina juu ya, fikiri sana,taamali, zingatia . . . kutafakari ni katika hisia zangu, aina ya sala. Imekuwa,ni njia ya kumwendea Roho wa Bwana.” (“Magnifying One’s Calling in thePriesthood,” Ensign, July 1973, p. 90.)

Moroni 10:4 anatuambia kwamba baada ya kuyatafakari maandikomatakatifu (kujifunza katika akili zetu yale tuliyoyasoma), yatupasakumwuliza Baba yetu wa Mbinguni “kama mambo hayo siyo ya Kweli,” na“yeye atatufunulia ukweli wa mambo hayo kwa nguva za Roho Mtakatifu.”

MwishoIli kufundisha injili kwa mafanikio, inatulazimu kujitayarisha kwa kuyasomamaandiko matakatifu mara kwa mara. Inatulazimu kuyatafakari mambotuliyoyasoma kwa kufikiri juu yake kuhisi na kuomba kwa nia iliyo thabiti.Na ni lazima tujizoeshe yale tuliyoyafahamu na kuyajua kwa kupitia RohoMtakatifu: Tunapokuwa tumefanya hivi, tunaweza kufundisha maandikokwa nguvu na kwa ushawishi.

Changamoto1. Usomapo Maandiko Matakatifu kila siku, piga mstari au weka alama

mistari ambayo ni muhimu kwako. Yapime yanawezaje “kulinganishwana sisi.”

2. Fundisha familia yako kutoka kwenye Maandiko Matakatifu katika Jioniya familia, katika meza ya chakula au katika mambo mengine yakifamilia kwa kutumia hadithi za maandiko matakatifu na uyatumiekatika kuyahusisha na mahitaji ya familia yako.

125

Somo la 17

Page 135: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Maandiko Matakatifu Zaidi2 Nefi 4:15–16 (furaha ya Nefi katika Maandiko Matakatifu)

M&M 11:21–22 (yatupasa kujifunza kabla ya kufundisha)

M&M 42:12–15 (yatupasa kufundisha kutoka kwenye Maandiko Matakatifu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya Kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 10, “Maandiko Matakatifu,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Wakumbushe washiriki wa darasa kuleta vitabu vyao vya Maandiko Matakatifu darasani.

3. Waulize washiriki wa darasa kutoa hadithi na Maandiko Matakatifu katika somo hili.

126

Page 136: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kufundisha kwa Nguvu za Roho MtakatifuMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kwamba inatulazimukufundisha injili kwa nguvu za Roho Mtakatifu.

UtanguliziRaisi David O. McKay alisema: “Walimu, anzeni matayarisho ya masomoyenu kwa sala. Funzeni masomo yenu kwa moyo wa sala. Halafu ombenikwamba Mungu austawishe ujumbe wenu . . . kwa mwongozo wa Rohowake Mtakatifu.” (Gospel Ideals, p. 223.)

Kama tunataka kufundisha injili ya Yesu Kristo ni lazima tupate mwongozowa Roho Mtakatifu. Ni kwa njia hiyo pekee tutaweza kufundisha ukwelikwani, mawazo yetu siyo mawazo ya Mungu; na njia zetu siyo njia zaMungu. (Tazama Isaya 55:8–9.)

Kufundisha kwa Mwongozo wa Roho MtakatifuWaulize washiriki wa darasa wasome M&M 42:12–14. Andiko hili linatuambia tufundishe nini?Tutazipata wapi kanuni hizi? Ni kwa namna gani tutampata Roho huyo ambaye tutafundishakwa uwezo wake? Kama hatutapata mwongozo wa Roho Mtakatifu, kwa nini tusifundishe?

Ili kujua ni nini na lini tutafundisha, inatulazimu kujifunza kutambuamwongozo wa Roho Mtakatifu. Mzee A. Theodore Tuttle alifafanua ni hisiagani huwepo uongeapo kwa nguvu za Roho Mtakatifu:

“Je unakuwa na hisia wakati ufunuo unapokujia? Acha nikueleze uzoefu watukio hili.

“Nilikuwa nikisafiri [na Mzee Marion G. Romney] tukielekea Salt Lakebaada ya mkutano, mmoja wa akina kaka [waliokuwa] nasi alisema, ‘KakaRomney, ulikuwa ukizungumza kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu usikuwa leo.’

“Kaka Romney alisema, ‘hiyo ni kweli, Je, wataka kujua ni kwa namna ganinilijua? Kwa sababu, nami pia, nilijifunza kitu ambacho nilijua sijakijua.’ ”(“Teaching the Word to the Rising Generation,” unpublished talk given July10, 1970, at BYU Summer School, pp. 9–10.)

Ni kwa namna gani Roho Mtakatifu alimwongoza Raisi Romney? Ni kwa namna gani RohoMtakatifu anaweza kuongeza uwezo wetu wa kufundisha?

Roho Mtakatifu siyo tu humfundisha mwalimu, lakini pia husababishamaneno ya mwalimu kuzama mioyoni mwa wale wanaomsikiliza. “Kwanimtu aongeapo kwa nguvu za Roho Mtakatifu, nguvu za Roho Mtakatifuhuyachukua na kuyaweka katika mioyo ya wanadamu.” (2 Nefi 33:1).

Roho Mtakatifu huwaongozaje wale wanaofundishwa?

127

Somo la 18

Page 137: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Onyesha picha 18-a, “Mfalme Benjamin alibadilisha maisha ya watu wengi wakatialipowafundisha kwa nguvu za Roho Mtakatifu.”

Nabii wa Kitabu cha Mormoni, Mfalme Benjamin, aliwaita watu wakepamoja katika siku za mwisho za maisha yake na kuwapa mashaurimaalumu na kuwaimarisha kiroho.

Uliza darasa lisome Mosia 5:1–2. Ni kitu gani kilisababisha watu wale wayaamini maneno yaMfalme Benjamin? Wacha darasa lisome. Mosiah 5:3–4. Kwa nini watu hawa walikuwa wepesikupokea mwongozo wa Roho Mtakatifu?

Kupata Mwongozo wa Roho MtakatifuKitabu cha Mormoni chatuambia kwamba wengi wa manabii nawamisionari wa wakati ule walikuwa wakiongozwa na Roho Mtakatifu katikamafundisho yao. Wanne kati ya watu hawa walikuwa ni Wana wa Mosiah.

Uliza darasa lisome Alma 17:2–3. Ni hatua tatu zipi ambazo wana wa Mosiah walizichukuazilizowasaidia kufundisha kwa nguvu? Andika hatua hizo tatu (tafiti maandiko matakatifu,kufunga na kusali) ubaoni.

Raisi Marion G. Romney alielezea tukio la mkewe alilopata wakatialipofuata hatua hizi katika kutayarisha somo ambalo alipangiwakufundisha juu ya ono la kwanza la Joseph Smith juu ya Baba na Mwana.Katika darasa lake alikuwepo dada mmoja msomi wa Chuo kikuu naalikuwa siyo mshiriki wa Kanisa. Dada Romney alikuwa bado msichanamdogo asiye na uzoefu na mwenye uoga kwamba somo lake huendalisikubalike na msichana huyu msomi.

“[Katika kujadili tatizo lake na mama yake, dada Romney] alisema, ‘Mamasiwezi kufunza somo hili. Mimi sijui kama Joseph Smith alipata ono hilo’ . . .

“Mama yake hakuwa mwanamke mwenye elimu kubwa, lakini alikuwa naushuhuda. Alimwambia binti yake, ‘Wewe unajua namna Nabii alivyopataono, ama sivyo?’

“ ‘Ndiyo,’ binti yake alijibu, ‘alipata kwa kumuomba Mungu hekima’ . . .

“[Ndipo Dada Romney] alienda chumbani kwake na akajaribu; alipambanana Mungu, kama ilivyokuwa kwa Enos. Matokeo yake yakawa . . . alitoasomo kwa ushawishi mkubwa kwa nguvu zaidi ya uwezo wake wa asili. Nikwa namna gani aliweza kuyafanya haya? Ndiyo, Roho Mtakatifu alikujakwake kama jibu la maombi yake. Alipata mchomo mkali nafsini mwake.Alijua kwamba Joseph Smith aliona ono hilo. Kama yeye alivyojua.Hakuona kwa macho yake mambo yale ambayo Nabii aliyaona, lakinialikuwa na ufahamu ule ule. Alijua kutoka kwa Joseph Smith katikamaelezo yake kile alichokiona na alipata ushuhuda kutoka kwa RohoMtakatifu kwamba habari hizo ni za kweli.” (“How to Gain a Testimony,”New Era, May 1976, pp. 10–11.)

128

18-a, Mfalme Benjamin alibadilisha maisha ya watu wengi wakati alipowafundisha injili kwa nguvu za Roho Mtakatifu

Page 138: Wajibu na Baraka za Ukuhani

18-a

Page 139: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ni kwa namna gani dada Romney alijiandaa kwa somo lake? Kwa nini kujifunza pekee yakehakukumpa ujasiri wa kutoa somo lile? Tunaitaje ushahidi ule ambao Dada Romney aliupata?

Nini tofauti kati ya kusoma ukweli na kumpata mtu akikushuhudia juu ya ukweli wake? Muulizemshiriki mmoja asome Moroni 10:4–5. Ni katika njia zipi Roho Mtakatifu hutusaidia kujifunzaukweli? Jee yatupasa kufanya nini kupokea ushuhuda huo?

Ushuhuda Hutupa Nguvu za KufundishaKufundisha kwa ushuhuda ni kufundisha ukiwa na elimu kuwa injili ni yakweli. Tukiwa na ushuhuda wa kile tunachofundisha, wale wanaotusikilizahuisikia nguvu ya Roho Mtakatifu na kuielewa injili vyema. Tunapotoaushuhuda juu ya ukweli, Roho Mtakatifu huwashuhudia walewanaotusikiliza ukweli juu ya ushuhuda wetu (tazama M&M 50:21–22).

Onyesha picha 18-b, “Roho Mtakatifu huthibitisha ushuhuda wa wale watoao ushuhuda waukweli wa injili.”

Mzee Alvin R. Dyer alisimulia hadithi ifuatayo:

Wamisieni wawili walifika jioni moja katika nyumba fulani. Familia ilikuwaikijiandaa kwa chakula cha jioni hivyo wamisionari hao hawakupatamafanikio katika ujumbe wao pale mlangoni. Yule mama alipokuwaakifunga mlango, wazee wale walipata nafasi ya kutoa ushuhuda juu yaukweli wa injili. Mmoja wao kwa makusudi alipandisha sauti yake juu iliiweze kusikiwa na wale watu waliokuwemo ndani. Halafu, kwa sababumvua ilikuwa inaanza kunyesha, wamisionari wale waliharakisha kuondoka.Baada ya kutembea kitambo kidogo, walisikia mtu akiwaita nyuma yao.Kijana mwenye umri upatao miaka kumi na nne aliwafikia na kusema.“Baba anawataka ninyi mrudi.” Walirejea katika nyumba ile. Babaakawaeleza kuwa alisikiliza ujumbe wao kutoka mlangoni. Hakuvutiwasana hadi pale mmoja wao alipotoa ushuhuda wake. Ndipo aliposema,“Hisia ya ajabu ilinijia. Nilijua tulikuwa tumefanya vibaya kuwaachia ninyimuende.” Ushuhuda, uliotolewa na mzee (Mmisionari) yule mnyenyekevu,uliiongoza familia kwenye ubatizo. (Tazama “When Thou Art Converted,”Instructor, July 1961, p. 225.)

Kwa nini baba yule aliwaita wale wamisionari warudi? Waulize washiriki wa darasa ambaowalipewa kazi ya kufundisha injili waelezee hisia walizopata wakati wakifundisha.

MwishoKama wazazi na walimu, katika Kanisa, tunalo jukumu la kubadili maishaya wale tunaowafundisha. Tunaweza kufanya hili, hata hivyo, ni kwakufundisha kwa nguvu za Roho Mtakatifu pekee. Tunapofundisha kwauwezo wa Roho Mtakatifu, tunaongeza maarifa na imani siyo tu kwa waletunaowafundisha, bali pia hata kwetu sisi wenyewe.

Ni kwa kufundisha kwa nguvu za Roho Mtakatifu tu ndiyo tutawezakufundisha ukweli. Lakini ili tufundishe kwa nguvu za Roho Mtakatifu,

130

18-b, Roho Mtakatifu huthibitisha ushuhuda wa walewanaotoa ushuhuda wa ukweli wa injili

Page 140: Wajibu na Baraka za Ukuhani

18-b

Page 141: Wajibu na Baraka za Ukuhani

inatulazimu kuwa wastahilivu na kujitayarisha. Maandalizi hayo ni pamojana kujifunza, kusali na kuishi kwa kuweka amri za Mungu.

“Na Roho atatolewa kwenu ninyi kwa sala yenye imani na kamahamtampokea Roho Mtakatifu msifundishe . . .

“Na kadiri mtakavyozipaza sauti zenu juu kwa uwezo wa Mfariji, mtanenana kutabiri nionavyo mimi kuwa ni vyema.

“Kwani tazama, Mfariji ajua mambo yote.” (M&M 42:14, 16, 17.)

Changamoto1. Kwa kujiandaa kufundisha, omba mwongozo wa Roho Mtakatifu kwa

kujifunza maandiko matakatifu, maombi kwa ajili ya mwongozo na kwakufunga.

2. Tafuta nafasi ya kuwafundisha watoto, marafiki na majirani.

Maandiko Matakatifu ZaidiLuka 24:32 (namna unavyojisikia ukiwa unaongozwa na Roho Mtakatifu)

Yohana 14:26 (mfariji hutufundisha mambo yote)

2 Nefi 32:7–8 (Roho Mtakatifu hututia moyo wa kusali)

Mosia 23:14 (yatupasa kuwaamini waalimu wale tu wanaoweka amri zaMungu)

Alma 5:43–52 (kufunga na kusali hutia moyo mwongozo kutoka kwa RohoMtakatifu)

Moroni 10:7–10 (vipawa kutoka kwa Mungu hupokelewa kwa njia ya imani)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Fuata hatua zilizobainishwa katika somo hili ili kuweza kupata mwongozo wa RohoMtakatifu wakati wa kutayarisha somo.

2. Kama unataka, waulize washiriki wa darasa kuelezea hisia walizozisikia wakati walipokuwawakifundishwa injili.

3. Pata ubao na chaki.

4. Wachague washiriki wa darasa kutoa hadithi na Maandiko Matakatifu katika somo hili.

132

Page 142: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kufundisha Adabu na Maadili Mema NyumbaniMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujua jinsi ya kufundisha adabuna maadili mema nyumbani.

UtanguliziMzee Boyd K. Packer, akizungumza kuhusu uzuri wa adabu na maadilimema, alisema: “Wajibu na haki ya kufundisha mambo haya matakatifu nikazi ya wazazi katika nyumba. Siamini ya kuwa jukumu hili ni juu ya shuleza uma, wala si jukumu la vitengo vya Kanisa. Mchango wa Kanisa katikajambo hili ni kuwafunza wazazi viwango sahihi ambavyo Bwana amefunuana kuwasaidia wao katika jukumu lao la kufundisha mafundisho hayamatakatifu kwa watoto wao.” (Teach ye Diligently, p. 256.)

Nabii Mormoni aliandika barua kwa mwanawe Moroni ambayoalimfundisha thamani kubwa ya usafi wa mwili. Alisema kuwa ubikira nauadilifu ni bora zaidi na wa thamani kuliko kitu kingine chochote (tazamaMoroni 9:9). Miili yetu ni mitakatifu; na daima yatupasa tuvae kwa adabu nakujiweka safi na waadilifu.

Adabu na Maadili MemaBwana ana thamini sana maadili yaliyo mema. Ni muhimu, kwa hivyo,kuelewa ni nini Bwana anamaanisha juu ya adabu na maadili mema.Adabu kwa kawaida ni juu ya namna tunavyoongea na kuvaa. Maadilimema ni jinsi tunavyotenda. Raisi Spencer W. Kimball amesema:

“Kingine kati ya vitu vingi vinavyotuongoza kuvunja amri ya usafi wa mwilini kukosa adabu. Leo vijana wengi wa kike na wa kiume wanajifanya kuwawanajua kila kitu juu ya maisha. Wanafikiri wanajua majibu yote.Wanaongea juu ya kufanya mapenzi kama vile wanavyoongea juu yamagari, sinema na mavazi. Na roho ya kukosa adabu imezidi mpakainaonekana kuwa hakuna kitu kilicho kitakatifu.

“Kitu kimoja kinachosababisha ukosefu wa adabu na kuvunjika kwauadilifu wa tabia ni mavazi ya kisasa. Nina hakika kuwa mavaziyanayovaliwa na baadhi ya vijana wa kike na mama zao, yanachangia kwanjia moja au nyingine ukosefu wa adabu katika wakati huu. Na hata akinababa wakati mwingine huwatia moyo. Nashindwa kuelewa kama dada zetuwadogo wanajua majaribu wanayoyaweka mbele ya wavulana wakatiwanapoacha sehemu za miili yao nusu wazi . . .

133

Somo la 19

Page 143: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Nina hakika kuwa nguo tunazovaa zaweza kuwa sababu kubwa yakuvunjika pole pole kwa upendo wetu wa kuwa waadilifu na uthabiti wetujuu ya sheria ya usafi wa kimwili.” (Faith Precedes the Miracle, p. 163, 168.)

Ni jinsi gani kujua kuwa miili yetu ni mitakatifu hugeuza kuvaa na kutenda kwetu?

Ni jinsi gani kujua kuwa sisi ni watoto wa Baba yetu wa Mbinguni kutageuza kuvaa na kutendakwetu?

Mzee Vaughn J. Featherstone alisimulia hadithi juu ya mwana wa mfalmealiyejielewa yeye alikuwa nani na jinsi ilivyompasa kutenda. Mfalme LouisXVI wa Ufaransa alichukuliwa kutoka kwenye ufalme wake na kuwekwagerezani. Mwanawe mdogo pia alichukuliwa na watu hao waliomkamata.Kwa sababu mwana huyo wa mfalme ndiye ambaye angekuwa mfalmebaada ya baba yake walitaka kumharibu kitabia. Walijua kwambawakifanya hivyo, hataweza kamwe kuwa mfalme wa Ufaransa.

Watu hawa walimpeleka mwana huyo wa mfalme katika mji uliyokuwambali kabisa ambako walimjaribu kijana huyu kwa kila aina ya kitu kibayaambacho walikipata. Walijaribu kumfanya ale vyakula ambavyovingemfanya ajisahau. Walitumia lugha mbaya wakati wote wakiwa naye.Walimjaribu kwa wanawake waovu. Walimweka wazi katika hali yakufedhehesha na kutoaminika. Kwa masaa ishirini na nne kila sikualizungukwa na kila kitu ambacho kingeweza kumfanya mtu kupotezamaadili yake mema. Kwa Zaidi ya miezi sita alifanyiwa mambo hayo. Lakinihata mara moja kijana huyu hakukubali majaribu hayo. Mwishowe, baadaya kufanya yale yote walivyoweza kuyafikiria, walimuuliza kwa ninihakufanya mambo yale. Alijibu, “Siwezi kufanya hayo mnayotaka, kwaninilizaliwa kuwa mfalme.” (Adapted from “The King’s Son,” New Era, Nov.1975, p. 35.)

Sisi pia tumezaliwa kuwa wafalme (tazama 1 Petro 2:9; Ufunuo 1:6). Kusudila maisha yetu, hata hivyo, ni kubwa zaidi kuliko kuwa mfalme wa nchi. Sisini watoto wa Mungu na tumezaliwa ili kuwa kama yeye. Kufikia lengo hilohaiwezekani kama sisi siyo wenye adabu na wenye maadili mema.

Umuhimu wa MfanoMoja kati ya wajibu wetu mkuu kama waumini wa Kanisa la Mungu nikuonyesha mfano mzuri wa adabu na uadilifu. Siyo tu kwa kuweka akili namwili kuwa mtakatifu, bali ni lazima kuonyesha kuwa tunachukulia miili yetukuwa mitakatifu kwa njia ya kuongea, vitu vinavyotufurahisha na vitabutunavyovisoma. Hii ni muhimu hasa kwa wazazi na watoto walio wakubwa.Tukionyesha mfano mwema, watoto wetu au ndugu na dada zetuwataweza kuiga tabia hizo ambazo tunazo nao watajiheshimu kama sisi.

Washiriki wa darasa watafakari kwa muda juu ya mitazamo na tabia zao na wajiulize maswaliyafuatayo:

“Je kuna kitu chochote katika mwelekeo na tabia yangu ambacho kinaweza kuwadhuru waleambao ninajaribu kuwafundisha?”

134

Page 144: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Je kuna kitu ambacho mimi hukifikiria au hukifanya ambacho nisingetaka watoto wangukukifanya au kufikiria juu yake?”

Soma katika Yakobo 2:35 Yakobo alivyowakemea Wanefi juu ya mifano yao mibaya. Kwa ninini muhimu kuonyesha mfano mzuri?

Kufundisha Adabu na Maadili MemaKufundisha adabu na maadili mema kunahitaji kujiingiza sana katikamambo ya kiroho. Mzee Boyd K. Packer amesema: “Kama kuna kitukimoja cha muhimu kwa ajili ya kufundisha maadili mema na thamani yamambo ya kiroho . . . ni kuwa na Roho wa Bwana tunapofundisha.”(Teach Ye Diligently, p. 272.)

Pia ni muhimu kuliendea somo hili kwa unyenyekevu na heshima. Njia yakufundisha ya Mzee Boyd K. Packer ni mfano mzuri wa njia ya kufundishaadabu na maadili kwa njia ya unyenyekevu zaidi:

“Katika miili yetu tumepewa, kitu ambacho ni kitakatifu, nguvu ya kuumba.Mwangaza, tunaweza kusema, ambao una nguvu kuwasha miangazamingine. Kipawa hiki ni lazima kitumiwe katika dhamana takatifu ya ndoapekee. Kupitia kutumia nguvu hii ya kuumba, mwili wa mwanadamuunaweza kutungwa na roho inaingia ndani yake na nafsi mpya huzaliwakatika maisha haya. Nguvu hii ni nzuri. Inaweza kuumba na kudumishamaisha ya familia na ni katika maisha ya familia, ndipo tunapatachemchem ya furaha tele. Hupewa karibu kila mtu ambaye amezaliwakatika dunia. Ni nguvu takatifu na ya muhimu . . .

“Mnakua katika mazingara ambamo mbele yenu, kila wakati, kunamakaribisho ya kuziharibu nguvu hizi takatifu . . . Usikubali mtu yeyotekugusa au kushika mwili wako! Wale ambao wanakuambia vinginewanakukaribisha kushiriki katika hatia zao. Tunakufundisha kuendeleakuwa bila hatia . . . Njia moja nzuri pekee ya kutumia nguvu hii takatifunayo ni katika agano la ndoa. Usijaribu kamwe kutumia vibaya nguvu hizitakatifu.” (Teach Ye Diligently, pp. 259, 262.)

Kama tunataka kufaulu kufundisha kanuni hizi katika familia zetu, ni lazimatuwe waangalifu zaidi katika kuzilinda nyumba zetu dhidi ya uchafuwowote. Mzee A. Theodore Tuttle ametuambia kuwa “baba ndiye mlinzi wanyumba. Analinda uovu usijipenyeze kutoka nje. Awali, aliilinda nyumbayake kwa silaha na kufunga madirisha. Siku hizi kazi hii ni ngumu zaidi.Milango na madirisha yaliyofungwa vinaweza tu kutulinda kutokana na vitu[vionekanavyo]. Si kitu rahisi kulinda familia zetu kutokana na [uovu ambaounazikabili] akili na roho za watu wote katika familia. Vitu hivi vinaweza navinatiririka bila kuzuiwa katika nyumba. [Shetani ni mwerevu sana].“Hahitaji kuvunja mlango.” (“The Role of Father,” Ensign, Jan. 1974 p. 67.)

Ni njia gani ambayo uovu unaweza kuingia majumbani mwetu katika siku hizi? (Magazetimaovu, vipindi vya redio, maonyesho katika televisheni na vitabu ni baadhi ya njia hizo.)

135

Somo la

Page 145: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ni kitu gani ambacho baba analazimika kufanya ili kuilinda familia kutokana na vitu vya ainahii? (Kwa makini chagua vitabu vya kusoma na vipindi ambavyo vinaonyeshwa na kusikilizwakatika televisheni na radio.)

Soma na jadili M&M 93:40–43.

Bwana alimkemea Fredrick G. Williams kwa sababu hakutimiza wajibuwake wa kuwalea watoto wake katika mwangaza na ukweli.

Unaweza kujisikiaje kama Bwana angekuambia kuwa wewe haukuwa mwaminifu katikakufundisha watoto wako umuhimu wa adabu na maadili mema?

Wakati Unaofaa wa KufundishaOnyesha picha 19-a, “Baba inampasa kuwahoji watoto wake mara kwa mara.”

Mkutano wa jioni wa familia nyumbani ni wakati mzuri wa kuwafundishaadabu na maadili mema. Baba wengi pia huona ni msaada mkubwawakiwa na mahojiano na watoto wao na wake zao. Baba mmoja, kwamfano, huwa na mahojiano na kila mtoto kila mwezi siku ya Jumapili yakufunga. Anawauliza maswali kuhusu maadili mema na kusikiliza matatizoyoyote ambayo wanaweza kuwa nayo. Yeye hufundisha, hutoa ushuhuda,na kuwaambia juu ya upendo wake kwao.

Ni matokeo gani unafikiri mahojiano haya yanaweza kuleta kwa watoto wako?

Onyesha picha 19-b, “Nafasi za kufundisha huja wakati usiotarajiwa.”

Ingawa ni muhimu kuwafundisha watoto wetu wakati wa kawaida kamakatika mahojiano na mkutano wa jioni wa familia nyumbani, inafaa tuwewepesi kujali mahitaji yao kila wakati. Ni lazima tutazamie wakati ambaowataelewa vizuri kabisa kile tunachotaka wajue. Kama tunaongea nao kilawakati na kuwaonyesha upendo, watoto wetu watakuja kwetu wakatiwanapohitaji kuongea kuhusu maoni yao na matatizo yao.

MwishoBwana ametuamuru kutumia kila nafasi ili kuwafundisha watoto wetu(tazama Kumbukumbu ya Torati 6:5–7). Kama tunatafuta nafasi yakufundisha, wakati mwingine tunaweza kufundisha kwa nguvu zaidi katikahali ambazo hatukutarajia. Tunaweza kufundisha ukweli muhimu juu yamaadili na adabu, kwa mfano, wakati wa kuburudika, baada ya mkutanowa sakramenti, mnapotembea ndani ya gari, wakati wa likizo, njianimnapoenda shuleni, au wakati unapopatwa na janga kubwa.

Je? Waweza kufikiria tukio lolote ambalo lilitokea ukiwa na watoto wako au wazazi wakoambapo mawasiliano kamili na mafunzo yalifanyika? Ilikuwa wapi? Ilikuwa lini? Ilikuwaimepangwa au tukio hilo lilitokea bila kutazamiwa?

Changamoto1. Panga mkutano wa jioni wa familia nyumbani ili kujadili juu ya maadili

mema na adabu.

136

19-a, Baba yampasa kuwahoji watoto wake mara kwa mara

Page 146: Wajibu na Baraka za Ukuhani

19-a

Page 147: Wajibu na Baraka za Ukuhani

19-b

Page 148: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2. Onyesha mfano wa adabu na maadili mema kwa mavazi na matendoyako.

3. Kama wewe ni mvulana, wahimize wasichana unaowajua wavae kwaadabu.

Maandiko Matakatifu Zaidi1. Timotheo 4:12 (umuhimu wa mfano)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili.

1. Panga kwa uangalifu namna utakavyofundisha somo hili. Kama kuna vijana wadogo wenyeukuhani katika darasa la ukuhani, usifanye wakati huu kama wakati wa kudadisidadisi.Ungetaka kujadiliana nao jinsi vijana wadogo wanavyoweza kusaidia wazazi wao kuongeanao juu ya somo hili. Jadili ni kwa nini sheria ya usafi wa kimwili na adabu ni kitu muhimu,na ni nini washiriki wa darasa wanaweza kufanya kuonyesha mfano mwema kwa wengine.

2. Kama unataka, muulize mmoja wao kulielezea darasa juu ya tukio ambalo mawasilianokamili na mafundisho yalifanyika kati ya wazazi na watoto. Jadili kuhusu tukio hilo nadhihirisha kwa nini wazazi na watoto waliweza kuwasiliana. (Wakati mzuri kwa mjadala huu,unaweza kuwa wakati unapozungumzia mawazo hayo katika sehemu ya tano, “WakatiMzuri wa Kufundisha.”)

3. Wapange washiriki wa darasa waelezee hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

139

Somo la 19

19-b, Wakati wa kufundisha mara kwa mara huja wakati usiotarajiwa

Page 149: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kutatua Matatizo ya Kifamilia Kwa AmaniMadhumuni ya somo hili ni kututia moyo ili tuweze kutatua matatizo katikafamilia kwa amani ili tujenge nyumba yenye maisha ya furaha.

UtanguliziOnyesha picha 20-a, “Upendo ndiyo msingi wa amani katika maisha ya familia.”

Raisi Joseph F. Smith ametuambia kile tunacholazimika kufanya ili tuwe nafamilia nzuri

“Nyumba nzuri . . . ni ipi . . . ? Ni ile . . . ambayo baba amejitolea kwafamilia ambayo Mungu amembariki nayo, akiwapa umuhimu wa kwanza,nao pia wanamkubali kuishi ndani ya mioyo yao. Ni ile ambayo kunakujiamini, umoja, upendo, utakatifu wa kujitolea kati ya baba, na mama nawatoto na wazazi.” (Gospel Doctrine, pp 302–3.)

Ingawa sisi sote tunajaribu kuwa na nyumba nzuri, wakati mwinginekunatokea kutoelewana. Hata Nabii Joseph Smith alipata kutokuwa naamani katika nyumba yake wakati mwingine.

Asubuhi moja, kwa mfano, wakati alipokuwa akitafsiri Kitabu cha Mormoni,alikasirishwa na kitu kimoja ambacho mke wake alikuwa amefanya.Baadaye, alipojaribu kutafsiri Kitabu Cha Mormoni, alishindwa. Ndipoalikwenda kwenye bustani ya matunda na kuomba na wakati aliporudialimuomba Emma msamaha. Ndipo tu aliweza kutafsiri. (From a statementby David Whitmer given September 15, 1882, Comprehensive History of theChurch, Vol 1, p. 131.)

Pia Bwana anatutarajia kutambua chanzo cha kukosekana kwa amanikatika nyumba zetu na kuyasuluhisha matatizo yetu.

Chanzo cha Kukosekana Kwa Amani Katika Nyumba ZetuMaandiko matakatifu yanatueleza kuwa ushawishi wa shetani ndiyo kitukikubwa kinacholeta kukosekana kwa amani na kugombana.

Soma 3 Nefi 11:29–30.

Roho wa mabishano aingiapo ndani ya nyumba zetu, Roho wa Bwanahutoka. Na bila Roho wa Bwana katika nyumba zetu, hatuwezi kuwa nafuraha, pia hatuwezi kuhisi furaha ya Bwana na ya injili yake.

140

20-a, Upendo ndiyo msingi wa amani katika maisha ya kifamilia

Somo la 20

Page 150: Wajibu na Baraka za Ukuhani

20-a

Page 151: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Udhaifu wetu binafsi pia unaweza kutufanya tubishane na wengine (tazamaYakobo 4:1). Kama mtu hana amani ndani yake ni vigumu yeye kuishi kwaamani na wengine. Kati ya udhaifu unaoweza kuleta kutokuwa na amani nitamaa ya usherati, uchoyo, tamaa chafu, na kutokuwa na msimamo. RaisiSpencer W. Kimball ametaja udhaifu mmoja zaidi: “Mume na mkewanaweza kuwa na umaskini, ugonjwa, uchungu, kutofanikiwa, na hata kifokatika familia, lakini hayo yote hayatawanyang’anya amani. Ndoa yaoinaweza kufanikiwa ikiwa uchoyo hautaingia. Shida na matatizo zitawaletapamoja katika umoja ambao hauwezi kuvunjika, kama uchoyo haupokabisa.” (Marriage and Divorce, pp 19, 22.)

Raisi Kimball alisema ni kitu gani mara nyingi husababisha kutokuwa na mapatano na furahandani ya ndoa?

Kama vile Raisi Kimball alivyotaja, shida ambazo hufikiriwa kuwa zakawaida katika kusababisha kutokuwa na furaha, kama umaskini, naugonjwa, vinaweza kuileta familia kuwa pamoja.

Ni vitu gani vitatu ambavyo tumevizungumzia ya kuwa huleta kutopatana katika nyumba zetu?(Andika majibu katika ubao. Lazima viwe ni ushawishi wa shetani, ubishi wa kibinafsi nauchoyo.)

Jinsi ya Kutatua Matatizo KifamiliaZifuatazo ni njia ambazo Bwana ametupa ili kuzuia au kutaua matatizokifamilia:

KUBALI MAJUKUMU

Wazazi na watoto wote wana wajibu kwa kila mmoja.

Soma baadhi ya majukumu hayo katika Waefeso 6:1–4. Ni wajibu gani kijana wa kiumealionao kwa wazazi wake? Ni wajibu gani wazazi walionao kwa watoto wao? Kukubalimajukumu haya kutasaidiaje kuleta amani katika nyumba?

EPUKA MATAMSHI MABAYA

Maneno ya ghadabu hayana nafasi katika nyumba zetu. Mzee Boyd K.Packer ametushauri: “Unapoingia katika agano la ndoa, [usiongee tena]neno baya— hata moja. Haihitajiki wala haipendezi. Kuna wengiwanaofundisha kuwa ni kitu cha kawaida na kutarajiwa kuwa na shida zanyumbani na kubishana na ugomvi kuwa ni sehemu ya ndoa . . . Miminajua kwamba, inawezekana kuishi pamoja kwa upendo bila kutumiamatamshi mabaya kamwe kutoka kati yenu.” (Eternal Marriage, “Speechesof the Year, BYU, April 14, 1970, p. 6.) Jibu laini, huleta maelewano nautulivu; maneno yenye hasira huleta mabishano zaidi (tazama Methali 15:1).

Ni tofauti gani ipo kati ya kujadili tofauti na kubishana?

KUBALI MAKOSA

Raisi Spencer W. Kimball alitupatia ushauri huu:

“Kwa sababu sisi ni binadamu, siku moja utakuwa na maoni tofautiyanayoweza kusababisha ubishi mdogo . . . Ikiwa jeraha limetokea;

142

Page 152: Wajibu na Baraka za Ukuhani

maneno mabaya yamezungumzwa, mioyo imevunjika na kila mmojaanahisi kuwa ni yule mwingine ndiye mwenye makosa. Hakunakinachofanywa kutibu kidonda hicho. Masaa yanapita. Mioyo inagongausiku wote na mchana wa huzuni na kutokuwa na huruma na kuongezekazaidi kwa kutoelewana. Jeraha huongezwa juu ya jeraha mpaka wakilihupewa kazi, nyumba huvunjika na maisha ya wazazi na watoto huteketea.

“Lakini kuna kitulizo cha kuponya, ambacho kikiwekwa mapema, kwadakika chache kitakurudisha katika mawazo mazuri; . . . na mengi yakiwahatarini—upendo wako, ninyi wenyewe, familia yako, matazamio yako,kuinuliwa kwako na maisha yako ya milele—hauwezi kujaribu kubahatisha.Lazima uwe na unyenyekevu na kwa ujasiri, [muambie mke wako:]’Mpenzi, pole. Sikutaka kukuumiza. Tafadhali nisamehe.’ Na [mke wakoatajibu]’ Mpenzi, ni mimi ndiye nilikuwa na makosa kuliko wewe. Tafadhalinisamehe.’ Na hapo mnakumbatiana na maisha [yatakuwa mazuri] tena.Na wakati unapoenda kulala usiku, yote yamesahaulika na hakunapingamizi kati yenu wakati mnapokuwa na maombi ya kifamilia.” (FaithPrecedes the Miracle, pp 134–135.)

Ni mambo gani huleta kutokuelewana na mabishano? Kutambua chanzo cha matatizo hayokunawezaje kutusaidia kuyasuluhisha? Kwa nini ni vigumu kukubali makosa yetu?

Raisi Spencer W. Kimball anatuelezea tukubali makosa yetu na kusema“samahani.” Tukifanya hivi kwa dhati, tutakuwa tumechukua hatua kubwakatika kutatua kutokuwa na amani katika familia. Wazazi yawapasa kufanyahivi kwa watoto wao pia, siyo tu kwao wenyewe.

SALA

Amani nyumbani huhimizwa wakati tunapomwomba Bwana katika maombiya familia na ya kibinafsi ili kutusaidia kushinda tofauti zetu.

Soma Nefi 18:19–21. Tambua kuwa ni jukumu letu kusali katika familia zetu. Ni kwa namnagani sala hutusaidia katika kutatua matatizo ya kifamilia?

WEMA

Moja kati ya kanuni ambazo maandiko matakatifu yametupatia kutusaidiakatika kudumisha furaha majumbani mwetu ni wema. Hata hivyo,tumeamriwa kuwa watu wema, wenye upendo na moyo wa kusamehe.Watoto na hata watu wazima katika familia wameshauriwa kukaa na watuwengine kwa heshima na wema kama vile Kristo alivyotuonyesha. Kwamambo haya, ni lazima tumweke Kristo kuwa mfano wetu. (TazamaWaefeso 4:29–32.)

Mwulize Kuhani mwenye Ukuhani wa Haruni ambaye amechaguliwa kueleza vitu ambavyokijana wa kiume anaweza kufanya ili kuleta amani katika nyumba.

Raisi Spencer W. Kimball ametufundisha mamna tunavyoweza kuwa nafamilia yenye furaha katika maneno haya: “Jiulize, ‘bei ya furaha ni nini?’Utashangazwa na urahisi wa jibu lake. Nyumba yenye hazina ya furaha

143

Somo la 20

Page 153: Wajibu na Baraka za Ukuhani

inaweza kufunguliwa na kubaki wazi kwa wale wanaotumia funguozifuatazo: Kwanza, yakupasa kufuata injili ya Yesu Kristo kwa usafi naurahisi wake . . . Pili lazima ujisahau na kumpenda mwenzi wako kushindaunavyojipenda. Ukifanya mambo haya, furaha itakuwa yako kwa wingi naisiyokwisha.” (Faith Precedes the Miracle, p. 126.)

Ni kwa namna gani wema na sala vinaweza kuzuia na kutatua matatizo ya kifamilia?

Hadithi ifuatayo inatueleza jinsi mama mmoja alivyopata amani katikanyumba yake:

“Ilikuwa baada ya wiki moja baada ya kumchukua Wayne ambaye alikuwana umri wa miaka kumi katika nyumba yetu kupitia mpango wa (ChurchIndian Placement Program). Alikuwa mtoto mwerevu na mwenye sura nzurilakini ilikuwa aonyeshe uhodari wake kwa watoto wengine. Alipigana naowakati mwingi, na aliweza kuwashinda hata wale waliokuwa hodari.

“Siku moja nilipata simu kutoka kwa mwalimu wake wa shuleni. Mwalimualiniambia kwamba alikuwa na shida na Wayne shuleni. Wayne alikosaheshima kwake na kwa walimu wengine. Hili lilikuwa pigo kwangu. Nilikuwasijawahi kupata shida kama hiyo kwa watoto wangu na nilikasirishwa sana.Kwa kweli hasira zilinipanda kama kawaida na nikaanza kufikiria vitu vyoteambavyo ningemwambia Wayne atakaporudi nyumbani kutoka shuleni.‘Lazima nirekebishe tatizo hili kabla halijakuwa kubwa,’ Nilijiambia.

“Kuongeza kwa kosa hilo, Wayne alichelewa kurudi nyumbani kwa sababuya ugomvi na mtoto wa jirani. Walipigana njia nzima kwenye kutoka kituocha basi hadi nyumbani. Mwishowe walikuwa mbele ya nyumba yetu. Wotewalikuwa wakipigana vibaya sana. Niliwaangalia kwa muda mfupi hadiwakati nilipoona kuwa ugomvi huo umekuwa hatari kabisa, ndiponikasogea mlangoni na kumwita Wayne ili aje nyumbani.

“Hakunisikiliza. Hakuwa tayari kuonyesha uoga mbele ya mtoto huyomwingine. Nilikasirishwa zaidi nilipoendelea kumwangalia. NilimuamuruWayne aingie nyumbani. Nilikuwa nimekasirika sana na nikajua ya kwambasiwezi kutatua tatizo hili katika hali hiyo, nilimwamuru kuingia chumbanimwake na ajisomee.

“Nikitetemeka kwa hasira, nikaingia katika chumba changu cha kulala nakupiga magoti na kuomba. Niliomba ili nipate hekima ya kutatua tatizo hili.Pia nikaomba, ili kupitia Roho Mtakatifu nijue kile nitakachosema.Niliposimama baada ya maombi, nilihisi joto, ambalo lilinifariji katika hisiazangu. Lilianzia katika kichwa changu na kuteremka polepole hadi kwenyemiguu yangu.

“Nilipofungua mlango wa Wayne nilimwona amekaa katika kitanda chakena kitabu mikononi mwake, fikira milioni zilipita katika akili yangu.Alionekana kama amepotea katika chumba kile, pengine ingempendezazaidi kuwa nje ya nyumba mahali ambapo angecheza bila kizuizi chochote

144

Page 154: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kama alivyokuwa amezoea. Hapo hapo, moyo wangu ulimhurumia sanamtoto huyu ambaye alikuwa pekee yake, mtoto mdogo ambayeamechukuliwa kwa ghafla kutoka katika mazingara kama hayo na kuletwaulimwengu mwingine kuishi kwa amri tofauti. Ilibidi awaonyeshe watoto haowengine kuwa alikuwa mzuri tu kama wao, kama siyo, kuwashinda wao.

“Nilikaa kando ya kitanda karibu naye na nikamwekea mkono wangu katikabega lake. Maneno ya kwanza niliyoongea yalinishangaza pia mimimwenyewe kwani nilisema hivi, ‘Wayne nisamehe mimi kwa kukukasirikiawewe.’ Ndipo nikamwambia juu ya simu niliyopata kutoka kwa mwalimuwake na nikampa nafasi ya kujieleza. Tulikuwa na mazungumzo mazurisana; aliniamini zaidi na tuliendelea kuongea na tulifanya hivyo kwakunong’ona. Hii ilikuwa tofauti na sauti ambayo nilitegemea kuitumia kablaya kuomba msaada wa Baba wa Mbinguni. Hakika hili lilikuwa tukio lafundisho la kiroho na lilisaidia sana katika uhusiano baina yangu na Waynekuliko jambo jingine.

“Tushukuru kuwa tunayo maombi na kipawa cha Roho Mtakatifukutuongoza kama tutaomba.” (Myrna Behunin, “We Talked in Whispers,”Ensign, Jan. 1976, pp. 51–52.)

MwishoVitu vinavyozuia au kutatua matatizo katika familia ni—

• Kukubali wajibu.

• Kuepuka matamshi Mabaya.

• Kukubali makosa.

• Maombi.

• Wema.

• Kutii Injili kikamilifu.

• Kupenda wake zetu kuliko tunavyojipenda wenyewe.

Changamoto1. Jenga na kuboresha furaha ya nyumba yako kwa kutambua vyanzo vya

kukosekana kwa amani miongoni mwa wanafamilia.

2. Kama umesema maneno mabaya na mtu mmoja katika familia, kubalimakosa yako.

3. Watendee mema watu wa familia yako.

Maandiko Matakatifu ZaidiMathayo 7:12 (uhusiano wetu na wengine)

Wagalatia 5:22 (matunda ya Roho)

M&M 88:119–26 (ushauri wa Bwana kwa waumini wa Kanisa)

145

Somo la 20

Page 155: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma Sura ya 36, “Jamii Yaweza Kuwa ya Milele,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Pata chaki na ubao.

3. Kama unapenda, mpange Kuhani mwenye ukuhani wa Haruni aelezee namna wavulanawanavyoweza kuleta amani katika nyumba.

4. Jitayarishe kuimba “Kuna Urembo Kila Mahali” mwisho wa Somo.

5. Wape kazi washiriki wa darasa kueleza hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

146

Page 156: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Utunzaji wa Fedha za Familia

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujifunza na kutumia kanuni zahekima ya msingi za usimamizi wa fedha.

UtanguliziMitajo mingi katika maandiko matakatifu kuhusu mambo ya pesa na utajiri,mingi imetuonya tusitamani sana mali. Kwa sababu hii, watu wengihuogopa kuwa pesa yote ni ovu na kwamba wanaweza kumkasirikishaBwana wakitumia wakati na nguvu zao kwa kujipatia na kujiwekea akiba yapesa. Lakini hii siyo kweli. Ni upendo wa pesa ndiyo “asili ya uovu wote,”siyo pesa yenyewe (tazama 1 Timotheo 6:10).

Raisi Spencer W. Kimball amesema: “Siyo pesa zote ni chafu. Kuna pesasafi—pesa safi ambazo tunanunua chakula, mavazi na nyumba, na zileambazo tunatoa michango.” Raisi Kimball aliendelea kuelezea kuwa pesasafi ni mshahara tunaopata baada ya kazi ya haki. Alisema kuwa pesahuwa chafu tu endapo imepatikana kwa njia isiyo ya haki. (Tazama FaithPrecedes the Miracle, pp. 235–36).

Si mali wala umaskini kilicho kielelezo cha kustahili kwa mtu. Watu wakuuwengi wa Mungu walikuwa matajiri na wengine walikuwa maskini. Kiasi chapesa tulizonazo siyo muhimu lakini ni namna gani tumezipata na kuzitumia.Kutumia pesa kwa mahitaji ya kimwili ya familia zetu, kwa mfano, siyo vizuritu, bali pia ni amri kutoka kwa Mungu (tazama 1 Timotheo 5:8). Amri yakukidhi mahitaji ya familia zetu hufanywa kuwa rahisi kutii kwa kujifunza nakutumia kanuni za msingi za hekima za utunzaji wa pesa.

Kanuni za Hekima za Utunzaji wa PesaIngawa kila kitu duniani ni cha Bwana (tazama Zaburi 24:1), anaturuhusukuvitumia na kuvimiliki baadhi ya vitu vyake vya duniani. Tumeonywa hatahivyo kuwa Bwana atatuwajibisha kwa jinsi tulivyosimamia vitu ambavyoameturuhusu kuvitumia. Katika hadithi ya talanta, kwa mfano, Mwokozialitufundisha umuhimu wa kusimamia mali yetu ya dunia kwa hekima.

Uliza mshiriki wa darasa uliyechagua kuelezea juu ya hadithi ya talanta katika Mathayo25:14–30. ( Katika siku za Yesu,talanta ilikuwa ni kipimo cha pesa.)

Kuna kanuni nyingi za msingi ambazo yatupasa kuzichunguza katikakutunza pesa zetu kwa hekima.

Andika kila kanuni ya hekima ya utunzaji wa pesa katika ubao wakati mnapoendelea namjadala.

147

Somo la 21

Page 157: Wajibu na Baraka za Ukuhani

MUWEKE BWANA KWANZA

Kitu cha kwanza na cha muhimu ni kulipa fungu la kumi. Bwana ameahidiwale watakaolipa fungu la kumi kwa uaminifu kuwa “atafungua . . .madirisha ya mbinguni, na kumimina . . . baraka, hata isiwepo nafasi yakutosha ya kuzipokea” (tazama Malaki 3:10). Ingawa Bwana hajatuahidimali nyingi tunapolipa fungu la kumi na sadaka, anatuahidi baraka zakimwili na za kiroho.

KAZI

Mbali na kuwa laana, kazi ni baraka ambayo inatuwezesha kuzilisha familiazetu. Uhakika wa mali waweza kuja tu kwa kufanya kazi kwa bidii. (Somo la23 katika kitabu hiki linatushauri jinsi ya kuendeleza na kukuza ustadi wakazi.)

EPUKA MADENI YASIYO YA LAZIMA

Inatupasa kuwa waaminifu kwa binadamu wenzetu. Kama tuna deni, nivizuri kulitoa kwa kuanza kulipa kila wakati, hata kama ni kidogo kwa wakatimmoja. Raisi Ezra Taft Benson wa Baraza la Mitume Kumi na Wawiliamesema, “Wacha tuishi kadiri ya uwezo wetu. Wacha tulipe kadiritunavyoendelea . . . wacha tufuate ushauri wa viongozi wa Kanisa.Jiondoe katika madeni!” (“Pay Thy Debt and Live,” Speeches of the Year,BYU, Feb 28, 1962, p. 12.)

Ni vipi tunaweza kuepuka madeni yasiyo ya lazima?

PANGA KABLA YA KUTUMIA

Soma Luka 14:28. Ina maana gani “kuhesabu gharama?”

Kama tunavyoelezwa katika maandiko matakatifu, ni lazima tupange kwauangalifu kabla ya kutumia pesa zetu. Watu wengi wanajikuta katikamadeni kwa sababu wanashindwa kudhibiti matumizi yao ya pesa. Kamafamilia itapanga jinsi ya kutumia pesa zao, watajikomboa kutoka katikamatatizo ya kifedha.

WEKA AKIBA

Kwa watu wengi, kuweka akiba ya pesa ni kitu kigumu sana. Lakini kamawaumini wa Kanisa, tumeshauriwa kuweka akiba ya sehemu ya mshaharawetu kila wakati. Kama tutaamua katika akili zetu kuweka akiba hata kamani sehemu ndogo ya mshahara wetu, hata kama ni pesa au vifaa, sikumoja tutafurahia kwa kuwa tulifanya hivyo. Kwa kuanzisha mpango wakuweka akiba ni vizuri kuelewa kuwa ni rahisi kuweka akiba kama tunaazimio muhimu, kama kwenda misheni au kwenda hekaluni ilikuunganishwa.

TUMIA KWA UANGALIFU

Yatupasa kufikiria kwa uangalifu umuhimu wa kitu chochote ambachotunataka kabla ya kukinunua. Vitu vingi ambavyo tunanunua kwa kweli siyo

148

Page 158: Wajibu na Baraka za Ukuhani

vya manufaa kwetu au familia zetu. Kama tukichukua muda kufikiria juu yamatumizi ya baadaye kila kitu kabla ya kukinunua, tutaepuka kununua vituambavyo kwa kweli hatuvihitaji. Karibu sisi sote tunaweza kuboresha kwanjia moja au nyingi katika mambo haya. Bwana atatusaidia kuboreshatunapomweka mbele na kufuata kanuni za hekima za utunzaji wakusimamia pesa.

Soma 2 Nefi 9:51. Ni vitu gani “visivyo vya maana” ambavyo tunajaribiwa kutumia pesa zetu.

Kutumia Baraza la Familia Kwa Kusimamia PesaMara nyingi, tunatumia pesa jinsi tunavyopata mshahara. Mahitaji yetuyanaongezeka kwa haraka kuliko mshahara wetu. Kwa hivyo ni muhimu,hata hivyo, kuweka bajeti ya pesa zetu kwa uangalifu. Ingawa kila familiaina matakwa tofauti, lakini familia nyingi zinapata unafuu mkubwa zikifuatampango kama huu:

Onyesha picha 21-a, “Baraza la Familia ni wakati mzuri wa kupanga bajeti.”

Watu wote katika familia yawapasa kujadiliana kuhusu mambo yote yakifedha na kukubaliana kuhusu njia ya kutumia fedha. Hii inawezekana kwakufanya mkutano wa baraza la familia ambao baba huongoza na wenginekatika familia hushiriki. Katika baraza hili, familia inapasa itengenezeorodha ya vyanzo vyote vya mapato katika familia. Katika orodha hiitunaweza kuwa na pesa ambazo ni mishahara ya watu katika familia,mboga na nafaka kutoka katika shamba, au vifaa ambavyovimetengenezwa nyumbani na kuwauzia watu wengine.

Cha pili, familia inapaswa kuandika mahitaji na matakwa yao yote, nakuandika katika orodha kwanza yale mahitaji ambayo ni ya muhimu halafuvitu ambavyo tunatamani ambavyo sivyo vya muhimu. Orodha inawezakuwa pamoja na michango ya Kanisa, akiba (kwa vitu kama kwendahekaluni, kutumika kwa kazi ya umisionari na kupata elimu), kodi namakadirio ya hesabu ya pesa za kulipia nyumba, chakula, mavazi, vifaa,usafiri na burudani.

Mwishowe, familia ikubaliane kuwa ni sehemu gani ya pesa itatengwakando kwa kila kitu.’ Vitu vingine vilivyo katika mwisho wa orodha penginehavitanunuliwa’ lakini ni hekima tukinunua vitu muhimu kuliko kununua vituvisivyo na manufaa kwanza na kukosa pesa ya kutosha kununua vitumuhimu. Raisi Brigham Young siku moja alisema, “Mahitaji yetu ni mengi,lakini mahitaji yetu ya muhimu ni madogo sana. Kwa hivyo wacha tutawalematakwa yetu kwa mahitaji yetu na tutajikuta kuwa hatutalazimika kutumiapesa zetu kwa vitu visivyo na umuhimu.” (Discourses of Brigham Young, p.297.) Mahali pengine alielezea kuwa umaskini hutokana na kukosa maamuziyenye hekima. Alikumbusha kuwa watu wengi ambao mapato yao nimadogo sana hutumia pesa zao kwa vitu visivyo na umuhimu na kujiingizandani ya madeni makubwa (Discourses of Brigham Young, p. 317).

149

Somo la 21

Page 159: Wajibu na Baraka za Ukuhani

21-a

Page 160: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Onyesha picha 21-b, “Mfano wa kadhirio.”

Tutabarikiwa sana endapo tutapanga kwa uangalifu na kubajeti pesa zetu.Kuweka malengo, kufanya mipango na kufanya kazi pamoja ilikuyafanikisha, kutatuwezesha kuzitunza familia zetu jinsi Bwanaalivyotuamuru. Baraka nyingine iliyoongezwa kwa kufanya kazi pamoja niupendo mkuu na umoja ambao familia zetu zitafurahia.

Muulize aliyechaguliwa awali kati ya washiriki wa darasa kuelezea juu ya hadithi ifuatayo juuya mmoja wa watakatifu walio Pasifiki Kusini, Vaha ‘i’ Tonga.

“Niliwaahidi watoto wetu wanne kwamba kama wakisaidia, tutaendahekaluni pamoja. Nilifikiria mimi mwenyewe, ‘Jinsi gani unavyowezakuwaambia kuwa mvulana mzuri au kuwa msichana mzuri, kama badosijaunganishwa nao hekaluni?’ Nilikuwa na hisia kuwa hawakuwa wangu.

“Kwa miaka miwili tulijitolea karibu katika kila kitu. Niligawa mshaharawangu kutoka shuleni kwa kila mmoja wetu na tukaweka akiba. Lakinitulilipa zaka na sadaka ya mfungo. Tulibaki na senti 70 mikononi mwetukila mwezi. Hivi ndivyo niliishi na familia yangu, kwa senti 70 kwa kila mwezikwa miaka miwili. Tuliishi kwa kula yale tuliyoweza kupanda na kukusanya.Nakumbuka mke wangu akiamka asubuhi na mapema kutengeneza saladina ndizi na tui la nazi. Watoto wangu walikuwa hawawezi kununuaperemende au viatu au kwenda sinema kwa sababu walikuwa wakijiwekeaakiba ili waende hekaluni . . .

“Kwa njia ya kujitolea tuliweza kuwapeleka watoto wetu katika hekalu laNew Zealand ili kuunganishwa. Ilitubidi kufanya vitu vingine vya ziada ilikutimiza malengo yetu, lakini ilikuwa baraka kubwa kwetu.” (“We Lived on70 Cents a Month for the Temple,” Ensign, Feb. 1976, p. 31.)

MwishoBaba yetu wa Mbinguni ametushauri tutunze pesa zetu vizuri ili tuwezekuzitunza familia zetu na kuwa wenye furaha. Kama hatutaweza kuzileafamilia zetu, Bwana atatuadhibu. Ili kuweza kuzilea familia zetu, inatupasakufuata hatua za msingi na kanuni za mwongozo wa hekima wa utunzajiwa pesa. Tukiweka vitu vya kiroho kwanza, Bwana atatusaidia kuzitunzafedha zetu.

ChangamotoChunguza tabia yako ya kutumia pesa na tengeneza bajeti ya pesa zakoukifuata kanuni zilizoelekezwa katika somo hili.

Maandiko Matakatifu ZaidiMethali 22:7 (mkopaji ni mtumishi wa mkopeshaji)

Malaki 3:8–11 (ulipaji wa zaka na sadaka huleta baraka)

151

Somo la 21

21-a, Baraza la Familia ni wakati mzuri wa kupanga bajeti

Page 161: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Jumla ya Mapato

Zaka—10 kwa kila mia moja

Michango ya Kanisa

Akiba

Chakula

Mavazi

Nyumba

Matibabu

Uchukuzi

Matumizi

Mengine

Mengine

Mengine

Jumla ya matumizi yote

Khadirio

21-b

Page 162: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Jacob 2:18–19 (yatupasa kuutafuta ufalme wa Mungu kabla ya kutafutautajiri)

M&M 56:16-17 (maonyo kwa matajiri na masikini)

M&M 104:11–13 (watu wote wanawajibika kwa usimamizi juu ya baraka zaulimwengu huu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili.

1. Soma sura ya 27, “Kazi na Wajibu Binafsi, “Katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Soma sura ya 23, “Kusitawisha na Kuendeleza Ujuzi wa Kazi,” katika kitabu hiki

3. Pata chaki na ubao.

Wapange washiriki wa darasa uliowachagua kutoa hadithi na maandiko matakatifu katikasomo.

153

Somo la 21

21-b, Mfano wa kadhirio

Page 163: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Uzalishaji wa Nyumbani na Hifadhi

Madhumuni ya Somo hili ni kumsaidia kila Mwenye Ukuhani kuelewa nakutenda kulingana na kanuni ya uzalishaji nyumbani na hifadhi.

UtanguliziRaisi Spencer W. Kimball ameshauri Watakatifu wote wa Siku za Mwishowawe huru na wenye kujitegemea. (Tazama “Family Preparedness,”Ensign, May 1976 pp. 124–26). Kuna sababu muhimu juu ya ushauri huu.Raisi Marion G. Romney ameeleza kuwa “tunaishi katika siku za mwisho.Tunaishi katika enzi inayotangulia kuja kwake Bwana Yesu Kristo kwa maraya pili. Tumeelezwa kujitayarisha na kuishi kwa njia itakayotuwezeshakuwa . . . huru kutokana na kiumbe chochote chini ya ufalme wa selestia.”(Conference Report, Apr. 1975, p. 165; see also M&M 78:13–14).

Onyesha picha 22-a, “Janga linaweza kutokea wakati ambao hatutarajii.”

Raisi Kimball ametuhimiza tuwe wenye kujitegemea kwa sababu utabiri wakale unakuja kukamilika. Alisema: “Sasa nafikiri wakati unakuja ambaokutakuwa na taabu nyingi, wakati kutakuwa na mafuriko mengi na tufaninyingi . . . matetemeko ya ardhi mengi . . . Nafikiri vitaongezeka kadiritunavyosogea mwisho wa dunia na kwa hiyo ni vizuri kujitayarisha kwahayo.” (Conference Report, Apr 1974, p. 184.)

Alisema pia kuwa: “Wakati wa uovu ukija, wengi wangetamani chupa zaoza matunda zingekuwa zimejaa na kulima shamba dogo nyuma yanyumba zao na pia kuwa wamepanda miti ya matunda na kutoshelezamahitaji yao kwa bidhaa zao. Bwana alipanga kuwa tuwe huru kutokana nakila kiumbe lakini tunaona kuwa hata wakulima wengi wananunua maziwakutoka kwenye maduka ya maziwa na wenye nyumba hununua mbogakutoka sokoni. Na ikiwa magari yangekosa kujaza rafu za maduka yao,wengi watakaa na njaa.” (Conference Report, Oct. 1974, p. 6.)

Akina kaka wafikirie kuwa maduka yote yamefungwa na inawapasa sasa kutegemea akibazao kwa kila kitu. Waulize ni nini wangetaka kuwa nacho au kuzalisha nyumbani mwao kamahali hiyo ingekuwa imetokea?

Kujitafutia Mahitaji Yetu WenyeweRaisi Kimball ametuagiza “tujifunze njia bora za kujipatia chakula chetuwenyewe. Kama kuna watoto katika nyumba yako, wahusishe katikampango huo na kuwapa majukumu.” (“Family Preperedness” p. 124.)

154

22-a, Janga linaweza kutokea wakati usiotarajiwa

Somo la 22

Page 164: Wajibu na Baraka za Ukuhani

22-a

Page 165: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Askofu Vaughn J. Featherstone ametueleza ni ujuzi gani ambaoinatupasa kuuendeleza ili kujipatia mahitaji yetu. “Sasa kuhusu uzalishajiwa nyumbani: Fuga wanyama kama unaweza na pia kama sheria za mjiunapokaa zinaruhusu. Panda miti ya matunda, mizabibu, matundamadogo madogo na mboga. Utailisha familia yako, sehemu kubwa yavyakula ambavyo vitaliwa vikiwa bado safi. Vyakula vingine ambavyounaweza kuvizalisha vinaweza kukingwa na kuhifadhiwa kama sehemuya akiba ya nyumbani. Kama inawezekana, tengeneza yale mahitajiambayo siyo vyakula wewe mwenyewe. Tengeneza au jenga vifaavinavyohitajika. Pia ninaweza kuongeza kuwa, rembesha, rekebisha , nahifadhi mali yako.” (“Food Storage,” Ensign, May 1976, p. 117.)

Onyesha mchoro unaoonyesha yafuatavyo:

Fuga wanyama.

Panda miti ya matunda, kama miti ya mizabibu.

Panda bustani ya mboga.

Kinga na hifadhi akiba ya chakula.

Tengeneza au jenga vifaa vinavyohitajika.

Rekebisha na tunza mali yako.

FUGA WANYAMA

Onyesha picha 22-b, “Kuku ni rahisi kufuga na kuwatunza.”

Kama tuna shamba la kutosha na tunaishi mahali panapokubaliwakufuga wanyama, inafaa tununue na kuwafuga wanyama fulani. Hatahivyo, kabla ya kukata shauri ni wanyama gani tutafuga, ni lazimatujitayarishe kuwatunza vizuri. Hii ina maana kuwa tutajifunza juu yachakula, nyumba na jinsi ya kuwatunza ili wawe wenye afya bora.Wanyama ambao ni rahisi kufuga ni kama kuku, sungura, bata na mbuziwa maziwa.

Jadili kuhusu aina ya mifugo ambayo inafugwa katika eneo lenu. Jadili kuhusu aina yavyakula, nyumba na matunzo ambayo kila mnyama anahitaji.

PANDA MITI YA MATUNDA, MIZABIBU NA KADHALIKA

Kwa sababu miti ya matunda, msitu, na mizabibu huzaa matunda kilamwaka, haihitaji kupandwa tena kama mboga. Haitazaa matunda marabaada ya kupandwa ila baada ya miaka kadha baada ya kupandwa. Kwahivyo ni vizuri kupanda haraka iwezekanavyo ili tule matunda yake wakatitunapoyahitaji. Kabla ya kupanda inafaa tujifunze ni nafasi kiasi gani kila mtiau msitu utahitaji wakati ukiwa umekomaa na pia jinsi ya kuutunza vizuri.

Jadilianeni kuhusu aina gani ya miti ya matunda, mizabibu na misitu ya fuu inayositawi vyemakatika eneo lenu. Jadili kuhusu aina ya utunzaji unaohitajika kwa kila mmoja.

156

22-b, Kuku ni rahisi kufuga na kutunza

Page 166: Wajibu na Baraka za Ukuhani

22-b

Page 167: Wajibu na Baraka za Ukuhani

PANDA BUSTANI YA MBOGA

Onyesha picha 22-c, “Kila familia inapaswa kuwa na shamba la mboga.”

Raisi Kimball ameomba kila familia katika Kanisa kuwa na shamba lamboga. Amesema kuwa hata kama hatuokoi fedha yoyote katika mradihuo kila jamii inahitaji kujifunza kujilisha. Bustani hutupa chakula kibichi napia zaidi ambayo tunaweza kukikinga na kuihifadhi kama akiba.

KINGA CHAKULA

Katika nchi zingine kuna sheria inayopinga kuweka akiba ya chakula.Raisi Kimball amesema kwa wale wanaoishi katika nchi hizi inawabidiwaheshimu, watii na kudumisha sheria ya nchi na wasiweke akiba yachakula. (Tazama “Family Preparedness,” p. 124.) Lakini kule ambakokuweka akiba ya chakula kumekubaliwa, yatupasa kufuata ushauri waBwana wa kuweka akiba ya chakula, ili tuwe tayari kukitumia wakatihakuna chakula chochote. Wakati tufani ilipotokea Honduras mwaka wa1974, waumini wa Kanisa waliokuwa wamekausha na kuweka akiba yachakula walimshukuru Mungu kuwa walifanya hivyo. Miezi kadha kablaya tufani hiyo, Raisi wa Misheni alikuwa amewaonya juu ya jangalinalokuja, na kuwakumbusha kuanza mpango wa akiba ya chakula.Maharagwe, unga, mchele na vyakula vingine viliwaokoa watakatifukutokana na njaa. (Tazama Bruce B. Chapman, “Hurricane inHonduras,” New Era, Jan. 1975, p. 31.)

Kuna njia nyingi za kukinga na kuhifadhi akiba ya chakula chetu.Tunaweza—

Kuweka akiba ardhini. Njia hii ni nzuri kwa mboga za mzizi, mboga zamajani za kijani kibichi kama mahali pa kuweka akiba ni baridi na nipakavu. Mvua nyingi na kutiririka kwa maji kutaziharibu.

Zikaushe. Kama ni wakati wa joto na jua, matunda na mboga zawezakukaushwa kwenye jua. Shida ni kuwa ni lazima zifunikwe au kurudishwandani kama mvua inanyesha.

Weka ndani ya chupa. Njia hii ni rahisi, lakini ni hatari ikifanywa vibaya.Ikifanywa vizuri, kuweka ndani ya chupa ni njia nzuri ya kuweka akiba yachakula na hutunza ladha yake. Kuweka akiba ya chakula kwenye chupainahitaji mtambo wa barafu. (Mtambo unaotumiwa waweza kutumiwa nafamilia nyingi.) Nia hii pia inahitaji kwamba chupa hizi ziangaliwe sanakutokana na kupasuka.

Weka chumvi au maji ya chumvi. Njia hii siyo ghali kwa kuhifadhi matunda,mboga na nyama na inahitaji vifaa vichache au haihitaji vifaa kabisa.

158

22-c, Kila familia inapaswa kupanda bustani ya mboga

Page 168: Wajibu na Baraka za Ukuhani

22-c

Page 169: Wajibu na Baraka za Ukuhani

TENGENEZA AU UNDA VIFAA VINAVYOHITAJIKA

Kama tungelipatwa na janga la kawaida, tungependa kuwa tayari kupika,kupasha joto nyumba zetu na kusafisha nguo zetu, miili yetu na mahalitunapokaa. Kwa sababu hii ni muhimu sisi kuweka akiba ya mafuta nasabuni au kujifunza kuzitengeneza wakati wa majanga. Pia cha muhimu nivifaa vya huduma ya kwanza, dawa uliyoandikiwa na dakitari, sabuni navifaa vya kuosha, mshumaa, viberiti na vitu vingine muhimu kwa usitawi wafamilia. Kama inawezekana tusiwe tu wenye kuweka akiba ya vifaa hivi, balitujifunze kuvitengeneza.

KARABATI NA TUNZA MALI

Wakati wa janga, tunaweza kukumbwa na haja ya kutengeneza nyumba,ghala, au zizi. Kwa hiyo ni muhimu kwa watu wa familia zetu kujifunzakufanya kazi ya useremala na vifaa vingine vya ujenzi ili kuwezakutengeneza na kukarabati vifaa vinavyohitajika. Tunapojifunza kukarabatina kuhifadhi mali yetu, tunaweza kupunguza gharama ya pesa na kuepukana kuwategemea wengine.

Kwa nini ni muhimu kuweka mali yetu katika hali nzuri?

Kujifunza Ujuzi MpyaWengine wetu tumejifunza ujuzi ambao tunaweza kuwafunza wengine.Kama kuna ujuzi ambao hakuna hata mmoja alionao, tunaweza kujifunzakutokana na magazeti au vitabu na darasa, watumishi wa serikali aumipango ya shule.

Ni nani kati yetu ambaye ana ujuzi anaoweza kufundisha wengine? Wako wapi watuwanaoweza kutufunza ujuzi ambao tungependa kujifundisha? Ni darasa gani tunalowezakuwahimiza watoto wetu waende ili kujifunza ujuzi wenye manufaa. Tunawezaje kuwahimizawana familia zetu kujifunza ujuzi huu?

MwishoShida na majaribu ni vitu vya kawaida na ni sehemu ya maisha yaulimwenguni. Kama tutajifunza, hata hivyo, kupanda na kuvuna chakulachetu wenyewe, hatutaogopa wakati mgumu kwa sababu tutakuwatumejitayarisha. Bwana amesema, “Kama mmejitayarisha, hamtaogopa”(M&M 38:30).

Changamoto1. Tenga wakati wiki hii ili kuongea na mke na watoto wako juu ya

uzalishaji nyumbani na hifadhi.

2. Tambua kile utakachohitaji kwa mwaka moja.

3. Tayarisha mpango wa kukabili na mahitaji ya familia yako kwakuanzisha au kuendeleza bustani yako, kujifunza ujuzi, au kufanya kazikatika mradi mwingine.

160

Page 170: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Kutana na wafanyi kazi wa serikali au watu wenye uzoefu.

A. Chunguza ni aina gani ya mifugo inafugwa katika eneo lenu na ambao ni rahisi kufuga.

B. Chunguza ni miti gani ya matunda, mizabibu na kadhalika ambayo inamea vizuri katikaeneo lenu na utunzaji ambao unahitajika.

C. Chunguza kama kuna darasa linaloweza kuwafundisha watu wa familia jinsi ya kujenganyumba, kutengeneza vifaa vya nyumbani na vinginevyo vinavyohitajika. Kama hakunamadarasa, tafuta watu wenye ujuzi huu ambao wangependa kuwafundisha.

2. Tayarisha bango kubwa lililotajwa katika somo hili.

3. Chagua washiriki wa darasa watakaotoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

161

Somo la 22

Page 171: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kusitawisha na Kuendeleza Ujuzi wa KaziMadhumuni ya Somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa umuhimu ambaoBwana ameuweka juu ya kazi, jinsi ya kuchagua kazi kwa hekima, nanamna ya kuboresha ujuzi wa kazi.

UtanguliziAgizo la kwanza lililoandikwa chini alililopewa Adamu mara baada yakuanguka kwake lilikuwa ni kanuni ya milele ya kazi. Bwana alimwambiaAdamu, “ Kwa jasho lako utakula mkate mpaka utakaporudi mavumbini”(Mwanzo 3:19).

Baba yetu wa Mbinguni ametupa amri hiyo hiyo. Uraisi wa Kwanza waKanisa unasema, “Ni baraka kwamba tunapaswa kufanya kazi nainatupasa kufanya kazi hiyo bila kulazimishwa na bila kulalamika.” (“FirstPresident Urges Frugality,” Ensign, Mar 1975, p. 75.) Kazi ni ufunguomojawapo ya uzima wa milele. Baba yetu wa Mbinguni mwenye hekima naupendo anajua kwamba tutajifunza mengi, tutafaulu na kuwa na ufanisizaidi kupitia maisha ya kufanya kazi kuliko maisha ya kukaa bila kazi.

Onyesha picha 23-a, “Kazi ni baraka ambayo tumepewa na Baba wa Mbinguni.”

Kuchagua Kazi Kwa HekimaKuchagua kazi yetu ni kitu cha muhimu sana. Inatupasa kupata habari,kukata shauri kwa maombi, kupata mafunzo na ujuzi, halafu ndipo tutafutekazi ambayo itatuwezesha kutunza familia zetu.

Andika hatua nne zifuatazo katika ubao.

KUSANYA TAARIFA

Tukiwa bado tu vijana inatupasa kuamua ni aina gani ya kazi ambayo nibora kwetu kwa kufikiria vipawa, uwezo na kinachotupendeza. Tutambuekwamba tutafanikiwa zaidi endapo tutafanya kitu ambacho kinatufurahisha.Ingawa wengine wetu ambao tunazo kazi hatukupata nafasi ya kuchaguakazi, tunaweza kufuata hatua hizo hizo kuboresha hali ya ajira zetu.

Kabla ya kuchagua kazi yetu, inatupasa kufikiria juu ya matokeo ya wakatiujao wa kazi hiyo. Kupitia mabadiliko ya maya kwa maya duniani kazinyingi huwa zinakoma na nyingine kubuniwa. Njia mojawapo ambayotunaweza kujifunza juu ya wakati ujao wa kazi yoyote tunayofikiria ni kwa

162

23-a, Kazi ni baraka ambayo tumepewa na Baba yetu wa Mbinguni

Somo la 23

Page 172: Wajibu na Baraka za Ukuhani

23-a

Page 173: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kuuliza marafiki, jamaa zetu, ndugu wenye ukuhani na viongozi wa Kanisajuu ya mambo haya. Katika miji mingine kuna washauri wa kazi na afisizinazoweza kutusaidia. Mara nyingi shule za ufundi, shule za sekondari, navyuo vikuu vinaweza kutuelezea ni kazi zipi zinapatikana. Kama magazetiyanapatikana, sehemu ya “matangazo ya kazi” inaweza kutuonyesha kaziambazo zinapatikana.

Tunapochagua kazi, inatupasa kutafuta kazi ambayo itatusaidia kuwakaribu na Kanisa. Kuna kazi zingine ambazo zinatuhitaji kuwa mbali nanyumbani kwa muda mrefu au kutupatia masharti ambayo yatatuzuiakuishi kulingana na injili kikamilifu. Hali kama hiyo tunaweza kuiepuka kwakuchagua kazi kwa makini. Tukipata yenye masharti yasiyoturidhisha,tunaweza kuendelea kuifanya kujiendeleza ili kuweza kupata kazi nyingine.

Onyesha picha 23-b, “Bwana ataithibitisha kazi ambayo tumeichagua kama tukimuuliza.”

SALI

Ni kitu cha muhimu kuomba msaada wa Bwana tunapotafuta kazi.Maamuzi ni yetu wenyewe, lakini Bwana atatusaidia kuchagua kwahekima tukiomba kwa dhati. Lakini maombi pekee hayatoshi. RaisiBrigham Young alisema, “Imani yangu hainiongozi kufikiri kuwa Bwanaatatupatia nyama ya nguruwe iliyochomwa tayari [na] mkate ambao tayariumepakwa siagi . . . atatupatia uwezo wa kupanda nafaka, kupatamatunda ya ulimwengu na kujenga mahali pa makazi.” (Discourses ofBrigham Young, p. 291.)

Tunapofanya uamuzi wa mwisho inatupasa kuomba na kupata amanikatika akili ambayo inakuja wakati tunapojua kuwa tunaongozwa na RohoMtakatifu. Halafu inatupasa kutenda kulingana na maamuzi yetu. Ndugummoja ambaye alitumia kanuni hizi ili kubadilisha maisha yake na kaziyake ni Taisho Komura kutoka Japan.

Soma hadithi ifuatayo:

Taisho Komura aliajiriwa kazi kama kinyozi huko Japan. Siku mojawamisionari walimtembelea na baadaye akabatizwa.

Wakati wa mijadala yao, alijifunza jinsi kuifanya siku ya sabato kuwatakatifu. Lakini siku ya sabato ndiyo siku iliyokuwa na kazi nyingi sanakatika duka lake la kunyoa. Halafu, baada ya kuomba juu ya shida hiyo yakuiweka siku ya sabato kuwa takatifu, aliamua kurudi shuleni ili kubadilishakazi yake.

Washiriki kadhaa wa darasa waeleze jinsi maombi yalivyowasaidia kufanyamaamuzi mazuri.

164

23-b, Bwana atadhihirisha chaguo letu la kazi tukimuuliza

Page 174: Wajibu na Baraka za Ukuhani

23-b

Page 175: Wajibu na Baraka za Ukuhani

KUENDELEZA UJUZI WA KAZI

Onyesha picha 23-c, “Kuendeleza ujuzi kunahitaji wakati na bidii.”

Kuendeleza ujuzi wa kazi kunahitaji wakati na bidii. Kama tunatakakuboresha hali zetu za kazi ni lazima tupende kusoma na kufanya kazi ilikupata ujuzi na mafunzo yaliyo ya lazima.

Kufundishwa kazi, masomo ya nadharia, mafunzo kazini, shule za ufundi,vitabu vya mwongozo na vitabu vinginevyo vyote vinaweza kutusaidiakuendeleza ujuzi wetu. Mahojiano na wale wanaoweza kutuajiri,kutembelea mahali pa kazi na kufanya aina nyingi za kazi pia zitatusaidiakuongezea elimu, ujuzi na ufundi.

Kusoma na kuandika ni vitu viwili vya msingi ambavyo vinaweza kukusaidiakupata kazi. Kama tunatafuta kazi na hatuwezi kusoma na kuandika,inatupasa kuomba msaada kutoka kwa wale wanaoweza. Tusisite kutumiaelimu na maarifa ya wenzetu katika Kanisa, familia zetu na ya jumuiya zetu.

Ni vipawa na ujuzi gani ambao tunaweza kushirikiana na makuhani wenzetu katika baraza?Wacha mtu ambaye awali ulikuwa umemchagua kutoa taarifa kuhusu nafasi za kazi ambazozinapatikana katika eneo lenu afanye hivyo.

Kama tuna lengo tunalotaka kulifikia, ni lazima tujitayarishe kujitolea ilikulifikia. Hii ina maana kuwa tuko tayari kufanya lolote linalohitajika ilikuendeleza ujuzi wetu. Mafanikio huja tunapotimiza na kufanya kila juhudivile inavyohitajika na kuweza kufanikisha. “Kwani chochote mwanadamuanachopanda ndicho atakachovuna” (Wagalatia 6:7).

Hadithi ifuatayo inatuonyesha jinsi muumini wa Kanisa huko South Pacificalivyofanikiwa katika jitihada zake za kuendeleza ujuzi wa kazi yake nakuitunza vyema familia yake.

Akiwa mvulana, Viliami Havili alikuwa amejifunza umuhimu wa bidii yakibinafsi katika kujifunza na kuendeleza ujuzi ule ambao ungemwezeshakuitunza familia yake hapo baadaye. Mwishowe alipofunga ndoa, NduguHavili alifanya kazi kwa bidii ili kupata pesa na hata kuweka akiba yakutosha ili kununua shamba ambalo lilikuwa likiuzwa kwa bei nafuu.

Shamba alilonunua lilifikiriwa kuwa la thamani ndogo kwa sababu lilikuwakwenye mlima karibu na bahari,mahali ambapo upepo ungeharibu mimeakwa urahisi. Lakini alifanya kazi kwa bidii ili kutayarisha shamba lake nakupanda. Pia alitumia muda mwingi kusoma na kujifunza njia za kisasa zaukulima. Kwa sababu taarifa aliyoihitaji ilipatikana katika vitabu vyakifaransa tu, alijifunza kifaransa vizuri kabisa na kuweza kuelewa yaleyalioandikwa juu ya kilimo.

Kutoka katika vitabu hivyo alijifunza jinsi ya kutia mbolea ambayo wakulimawengi katika eneo hiyo walikuwa hawajawahi kuitumia. Alijifunza jinsi ya

166

23-c, Ili kuendeleza ujuzi tunahitaji muda na juhudi

Page 176: Wajibu na Baraka za Ukuhani

23-c

Page 177: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kutumia dawa za kuua wadudu na kutibu magonjwa. Alipata kujua nimazao gani yaliyokuwa yakiuzwa nje na kwa bei ya juu. La kushangaza,kutokana na bidii yake na kwa msaada wa Bwana, Ndugu Havili alikuwamkulima maarufu.

Je! kuna uwezekano wa kupatikana kazi katika eneo lenu?

Kazi hizi na nyinginezo zinaweza kuwa zetu ikiwa tutajitayarisha kwa kupataujuzi unaohitajika.

TAFUTA KAZI

Mtu ambaye amehitimu hawezi kupata kazi hadi awatembelee watuwanaoweza kumuajiri. Wala mtu ambaye anataka kujiajiri hawezi kuuzabidhaa zake au huduma yake bila ya kukutana na wale wanaowezakuzinunua. Kwa hiyo Kuhani ambaye hana kazi analo jukumu la kutafutakazi.

Kama inakuwa vigumu kupata kazi, anaweza kuomba msaada kutoka kwamakuhani wenzake. Kiongozi mmoja wa Kanisa alisema kuwa, “ni kupitiakwa mawasiliano katika Baraza la Makuhani ndipo milango ya kazihufunguka na habari zake kusambaa. Mabaraza yetu yanapaswakuwatambua wale wanaohitaji kazi au wanahitaji kazi nzuri ya kufanya, nakufanya lolote wawezalo ili kuwasaidia makuhani wenzetu kupata kazi.”(Howard W. Hunter, “Prepare for Honorable Employment,” Ensign, Nov.1975, p. 123.)

Tunaweza kufanya nini kama waumini wa Baraza la Ukuhani ili kuwasaidia ndugu zetu kupatakazi?

Kuboresha Tabia za KaziMtume Paul amewashauri wanaume katika Kanisa wasiwe ‘wazembekatika shughuli’ (Warumi 12:11). Yatupasa daima kujaribu kwa bidii nakutafuta njia za kuboresha tabia zetu za kazi. Kufanya hivi, yatufaa kuwa namtazamo mzuri juu ya kazi. Orodha ifuatayo inaweza kutusaidia sisi kuwana tabia muhimu za kazi akilini mwetu.

• Je! nautumia wakati wangu vizuri?

• Je! ninashirikiana vizuri na mwajiri wangu, msimamizi wangu na wafanyikazi wenzangu?

• Je! ninatumia vifaa vya mwajiri wangu kwa kazi zangu binafsi aukuvitumia kwa Kanisa bila ruhusa au bila kuvilipia.

• Je! ninaweza kufika kazini mapema na kurudi kazini mara moja baada yamapumziko?

• Je! mimi ninafanya kazi kwa uwezo wangu wote?

• Je! mimi ni mtu mwenye maelewano mazuri na wafanya kazi wenzangu,msimamizi na mwajiri wangu?

Soma hadithi ifuatayo:

168

Page 178: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Raisi Heber J. Grant alipokuwa kijana alijifunza umuhimu wa kujiendelezakwa ujuzi wa kazi kwa kuongeza bidii zaidi. Siku moja alipokuwa akichezagololi pamoja na vijana wenzake walimwona mhasibu wa benki. Kijanammoja kati yao akasema, “Mtu yule hupata $150.00 kila mwezi. Heberalifikiria yeye itambidi apige rangi viatu jozi 120 kila siku kwa mwezi mzimaili kupata pesa kama hizo. Hapo ndipo alipoamua kuwa siku moja atakuwamhasibu wa benki.

Siku hizo kumbukumbu, mahesabu yote ya benki yaliandikwa kwa kalamu,na kitu kimoja ambacho kilihitajika ili kuwa karani mzuri wa hesabu za pesailikuwa ni maandishi mazuri. Ili kupata kazi hiyo, Heber alijifunza kuandikavizuri.

Mwanzoni mwandiko wake ulikuwa mbaya sana na marafiki zakewalimcheka sana: “Hii ilimsikitisha sana, na akasema, siku moja nitawezakuwafunza ninyi jinsi ya kuandika vizuri.” Kwa sababu ya bidii yakealiendeleza ujuzi huo na hata kuwa mwalimu wa kufundisha jinsi yakuandika mandiko mazuri. Katika chuo kikuu. Aliandika kadi za salamu,kadi za harusi, hati za bima, hati za mali na hati za kisheria.

Alisema, “Wakati fulani nilijipatia $20.00 siku ya mwaka mpya kwa kuandikakadi kumi na mbili za, “Mwaka mpya” na jina la mtu huyo pembeni mwakadi hizo. Jioni ya mwaka mpya uliofuata, nilichelewa kutoka katika afisinikiandika kadi za mwaliko. Bwana Wadsworth ambaye alikuwa mkubwawangu wa kazi akaingia na kusema kwa mzaha kwamba biashara ilikuwanzuri. Aliongelea juu yangu kwa kuweka mahesabu ya kampuni nyinginebila malipo. Alisema vitu vingi vizuri juu yangu ambavyo vilinifanya kuwa nafuraha sana. Halafu alinipa $100.00 ambazo ni mara mbili zaidi kwa kazi yaziada niliyofanya. Hali ya kuridhika ambayo niliifurahia na kupata shukranina kutiwa moyo kutoka kwa mwajiri wangu yalikuwa na thamani kubwakuliko mara mbili ya $100.00.” (Tazama Bryant S. Hinckley, Heber J. Grant:Highlights in the Life of a Great Leader, pp. 39–42.)

MwishoUwezo wa kufanya kazi ni baraka. Bwana ametuambia kupitia manabiiwake, kuwa ni jukumu letu kufanya kazi na kuzilisha familia zetu. Tunawezakujifunza tabia nzuri za kazi na ujuzi wa ufundi kwa kujizoesha na piakutoka kwa wale ambao wana uzoefu.

ChangamotoJiendeleze katika moja ya maeneo yaliyoelezwa katika orodha ya binafsi yatabia za kazi ambazo hupatikana katika sura hii.

Maandiko Matakatifu ZaidiM&M 31:5 (mshahara ni thamani ya mfanyikazi)

M&M 42:42 (mvivu hawezi kupata baraka za anayefanya kazi)

169

Somo la 23

Page 179: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma Sura ya 27, “Kazi na Wajibu Binafsi,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Rudia Somo la 12, “Wajibu wa Baba kwa Usitawi wa Familia yake,” katika kitabu hiki.

3. Pata chaki na ubao.

4. Kama unapenda, uliza washiriki wa darasa kutafuta ni shule gani na huduma zilizoko katikaeneo kwa ajili ya kuendeleza ujuzi na nafasi za kazi.

5. Chagua washiriki wa darasa watakaoelezea hadithi na maandiko matakatifu katikafundisho hili.

170

Page 180: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kuweka Miili yetu katika Hali ya Afya BoraMadhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa kwa nini ni muhimukuiweka miili yetu katika afya bora.

UtanguliziSababu moja wapo ya kuja hapa duniani ilikuwa ni kupata mwili. RaisiBrigham Young alisema, “Hii miili tuliyo nayo ni muhimu sana kwetu; bilamiili hii hatuwezi kamwe kutukuka katika maisha ya milele ambayotutakuwa nayo.” (Discourses of Brigham Young, p. 56.)

Ingawa miili yetu itatukuzwa katika maisha ya milele (tazama Alma11:42–44), katika maisha haya tunapatwa na magonjwa, uchungu namaumivu. Wengine wana ulemavu wa muda. Wengine ni vilema maishani.Lakini katika hali iwayo yoyote, miili yetu ni muhimu kwetu kwaniinatusaidia kukua kuelekea kwenye ukamilifu.

Mtu ni kiumbe cha kiroho na kimwili. Mwili na roho haviwezi kutenganishwa.Roho na akili haviwezi kufikia ukamilifu wake kabisa bila msaada na nguvuza mwili (tazama M&M 93:33–34). Licha ya ukweli huo Makuhani wengiwanajiendeleza wenyewe kiroho na kiakili na wanashindwa kujiendelezawenyewe kimwili.

Raisi David O. Mckay amesema, “Mtu mwenye afya njema ambaye huujalimwili wake, ana nguvu na uzima: hekalu lake ni mahali pazuri pa rohoyake kuishi . . . kwa hiyo ni muhimu kuitunza vyema miili yetu na kufuataamri za afya ya mwili na furaha.” (“The Whole Man,” Improvement Era,Apr. 1952, p. 221.)

Faida za AfyaZifuatazo ni baadhi ya faida zinazopatikana kwa kuwa na mwili mwenyeafya njema:

TUNAKUWA NA UWEZO WA KUTUMIKIA VYEMA

Kadiri tuwavyo afya njema, ndivyo tunavyokuwa na uwezo wa kuwatumikiawengine na kuwaletea wengine furaha na pia sisi wenyewe.

TUNAKUWA VIONGOZI BORA

Kwa sababu ya masharti yaliyowekwa kwa kiongozi, yampasa kuwa nanguvu na afya bora. Wito wake unamhitaji yeye kuwa na afya nzuri.

171

Somo la 24

Page 181: Wajibu na Baraka za Ukuhani

TUNAJISIKIA VIZURI JUU YETU WENYEWE NA WENGINE

Tukiiweka miili yetu katika afya njema, tunajisikia vizuri juu yetu wenyewena kuwa na shauku ya kazi zetu. Pia tunakuwa na upendo, wema nauvumilivu kwa wengine.

TUNAWEZA KUJITAFUTIA MAHITAJI YETU SISI WENYEWE

Kadiri tuwavyo na afya njema, ndivyo tunavyoweza kufanya kazi nakujipatia mahitaji ya familia zetu na sisi wenyewe.

Kudumisha Afya ya MwiliMatatizo mengi ya kiafya hutokana na kuishi katika hali ya uchafu,magonjwa, uzito mkubwa kupita kiasi, lishe duni, uchovu na kukosakufanya mazoezi. Bila kujali tunaishi wapi, tunaweza kuathirika na matatizohaya ya kiafya. Ili kuzuia au kutatua matatizo haya ya kiafya ni lazima tujuematatizo ya afya zetu. Mara tunapojua hayo, tunaweza kutengenezautaratibu kulingana na hali yetu ambayo unaweza kutusaidia kudumishaafya ya miili yetu.

Vituo vya afya ambavyo viko karibu yetu ni mahali pazuri pa kupatamsaada wa kutayarisha mpango wa afya wa kibinafsi.

Pata mshiriki wa darasa aliyepangwa awali ili kutoa taarifa juu ya ziara yake kwenye kituo chaafya kilichoko mtaani kwake.

Mpango wa afya zetu na wa familia zetu yafaa kuwa pamoja na yafuatayo:

UTII KWA NENO LA HEKIMA

Bwana ametueleza kuwa kuna vitu vingine ambavyo havifai kuingizwandani ya miili yetu. Hivi ni pamoja na tumbako, chai, kahawa, pombe navyakula vingine. Kwa upande mwingine ametushauri juu ya vyakula navinywaji ambavyo tunaweza kutumia ili kudumisha miili yenye afya bora.Wale wanaofuata Neno la Hekima wameahidiwa afya, hekima na kinga(tazama M&M 89:18–21).

Pata mshiriki wa darasa atoe ripoti ya yaliyomo katika Neno la Hekima yanayopatikana katikaM&M 89:1–17.

Hadithi ifuatayo inatuelezea baadhi ya baraka zinazopatikana kutokana nakutii Neno la Hekima.

“Nilikuwa bado kabisa kufikia miaka kumi na miwili lakini nilifanya kazi yakuvuna nafaka sambamba na baba yangu miaka 60 iliyopita. Alikata naminiliweka nafaka hizo katika [vifurushi]; ilikuwa kazi ya kuchosha, siku baadaya siku.

“Jumamosi moja, tulianza kufanya [kazi] kutoka wakati mwangazaulipochomoza mpaka saa 2:30 usiku. Nilikuwa nimechoka sana na nilitakakulala hata kabla ya kula chakula cha usiku.

“Baba yangu aliniangalia na kusema kwa upole, ‘Lee, nafaka niliyokata leoilikuwa kijani kibichi sana. Kama tukingojea hadi jumatatu ili [kuiweka

172

Page 182: Wajibu na Baraka za Ukuhani

pamoja], kokwa zake zitajikunja. Lazima tufanye kazi hiyo leo usiku. Kunambalamwezi nje, Je unafikiria kuwa unaweza kunisaidia?’

“Nilizuia machozi yangu na nikaitika kwa kichwa.

“Baba yangu alisema, ‘sawa, tutakula chakula cha usiku.’

“Punde tulimaliza mkate na maziwa lakini bado nilikuwa nimechoka nailikuwa vigumu kwangu kuinua kichwa changu. Wakati baba yangualipoenda kulisha nguruwe nilikaa mezani na kufikiria kwa uchungu,sijawahi kamwe kuvuta sigara au kunywa pombe, nimekuwa wakati wotenikitii Neno la Hekima na maagizo yanasema kuwa ukitii neno la hekimautakimbia lakini hautachoka na kutembea lakini hautalegea. Na sasanimechoka kiasi hata siwezi kuinua kichwa changu.’ Mdomo wanguulichezacheza nilipojaribu kuzuia machozi ya uchovu.

“Ni vigumu kuelezea kilichotokea lakini ilionekana ni kama kiangazi kizuricheupe kiliingia ndani ya mwili wangu na kupenya kila sehemu ya mwiliwangu. Niliamka mara baba yangu aliporudi na tukaenda pamoja shambani.

“Baba yangu alikuwa akifanya kazi kwa haraka, lakini usiku huo hakuwezakufanya kazi sambamba na mimi, ingawa alifanya kazi kwa haraka jinsialivyoweza. Nilikimbilia vifurushi vya nafaka ambavyo vilikuwa kando nakuvitupa mahali palipofaa, vingine vilikuwa vizito kunishinda. Sitasahaumshangao katika macho ya baba yangu.” (Leo W. Spencer, “To Run andNot Be Weary,” Ensign, March 1974, p. 45.)

KAZI

Kazi ni baraka, wala siyo laana. Haituwezeshi tu kujipatia mahitaji na afyaya familia zetu, bali hata huiweka miili na akili zetu kuwa makini. (Tazama 1Wathesolonika 4:11–12 na Zaburi 128:2–3.)

MAPUMZIKO YA KUTOSHA

Watu wengine hukosa kulala vya kutosha na hivyo kukosa mapumziko yakutosha. Watu wengine pia wanalala kupita kiasi. Bwana ametuonya sisikuwa tupate usingizi tunaohitaji lakini siyo zaidi ya ule tunaohitaji. Sisi sotetunatofautiana lakini yatupasa tupumzike kulingana na mahitaji yetu, lakiniametuambia kuwa tulale mapema na kuamka mapema ili miili na akili zetuziweze kuimarika. (Tazama M&M 88:124.)

USAFI WA KIBINAFSI

Ili kuzuia magonjwa, inatupasa kuoga, kusugua meno, na kunawa mikonoyetu mara kwa mara. Inatupasa pia kuosha nguo zetu, matandiko yakitanda na vyombo vyetu vya chakula mara kwa mara.

Tunaweza kuzuia ugonjwa na maradhi kwa kuzuia viini vinavyoletaugonjwa. Tunaweza kuvizuia kwa kuondoa wadudu na wanyama ndani yanyumba na kuondoa vinyesi vya wanyama na watu. Kwa sababu hiyo hiyo,chakula kinapaswa kuhifadhiwa mahali pasafi na salama.

173

Somo la 24

Page 183: Wajibu na Baraka za Ukuhani

CHAKULA BORA

Chakula bora ni kile ambacho kina aina tatu ya vyakula katika kila mlo.Tunahitaji nyama na bidhaa za wanyama ili kukua; matunda na mboga kwakuzuia magonjwa, na nafaka na mizizi yenye wanga kwa kutupa nguvu.(For more information see The Latter Day Saint Woman: Basic Manual forWomen, Part A, Lesson 22: “Nutrition for the Family.”)

TIBA NA UTUNZAJI WA MENO

Tunaweza kjikinga wenyewe na familia zetu kutokana na magonjwamengine kwa kupata chanjo. Katika sehemu nyingi duniani, chanjohupatikana katika vituo vya afya au kwa daktari. Inatupasa pia kuhakikishakuwa daktari wa meno anayaangalia meno yetu mara kwa mara.

MAZOEZI YA VIUNGO

Onyesha picha 24-a, “Kufanya Mazoezi ya viungo kwa Kawaida ni muhimu ili kuwa na afyanjema.”

Mazoezi ni kitu ambacho kitaifurahisha familia na sisi wenyewe. Njia mojabora ya kufanya mazoezi ambayo karibu kila mtu anaweza kufanya nikukimbia. Tunaweza kukimbia karibu kila mahali, na kila wakati, na kuletamafanikio katika muda mfupi. Kukimbia mahali pamoja na kutembea pia nimazoezi mazuri. Mpira wa vikapu, kandanda, mpira wa mikono, kuogeleana michezo mingine inaweza kutusaidia kutupatia mazoezi na starehe.

Kabla ya kuingilia mpango wa mazoezi magumu, ni lazima tuangaliwe nadaktari. Kupata na kufuata ushauri wa daktari juu ya mpango wetu wamazoezi itatulinda kufanya mambo ambayo yatatudhuru badala yakutusaidia.

Onyesha picha 24-b, “Mazoezi ni mradi ulio bora kwa familia.”

BURUDANI

Kwa sababu mazoezi ya viungo huondoa uzito na maudhi yanayotokanana majukumu yetu ya kila siku, burudani inafaa kuambatana na mazoezi.Hii inatusaidia kwa afya ya mwili na akili. Faida moja wapo ya mpango wamazoezi kwa burudani ni kuwa tunapata nafasi ya kuwa na familia zetu.Kila mtu katika familia siyo tu atatiwa moyo wa kufanya mazoezi, baliatajisikia kuwa karibu na watu wengine wa familia.

MwishoUsawa ni muhimu kwa maisha ya furaha. Hii ina maana kuwa lazimatujaribu kufikia usawa katika kazi, mapumziko na burudani. Raisi BrighamYoung alishauri:

“Tujitahidi kuyarefusha maisha haya kadiri iwezekanavyo kwa kutii kila amriya afya na kuweka viwango sawa kwa kazi, masomo, mapumziko na

174

24-a, Mazoezi ya viungo ni muhimu kwa afya nzuri

Page 184: Wajibu na Baraka za Ukuhani

24-a

Page 185: Wajibu na Baraka za Ukuhani

24-b

Page 186: Wajibu na Baraka za Ukuhani

burudani . . . Jitayarishe kwa maisha bora. Tuwafundishe kanuni watotowetu, ili . . . wawe wamefunzwa kujenga msingi wa nguvu na afya.”(Discourses of Brigham Young, p. 186.)

Kanisa linahitaji makuhani ambao wamejitayarisha kiroho, kiakili na kimwili,kwani afya nzuri inatusaidia kufanya majukumu yetu vizuri.

Changamoto1. Chunguza matatizo yako ya kibinafsi ya afya.

2. Tayarisha mpango wako na wa familia yako wa mazoezi.

Maandiko Matakatifu ZaidiMethali 23:19–23 (inatupasa kuwa na hekima tunapochagua kile tunachokunywa au kula)

Methali 31:1–4 (tusiichafue miili yetu kwa pombe na usherati)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 27, “Kazi na Wajibu Binafsi,” na 29 “Sheria ya Bwana ya afya,” katika kitabucha Kanuni za Injili.

2. Chagua mshiriki wa darasa kutembelea na kutoa taarifa juu ya kituo cha afya katika eneolenu ambacho kinaweza kuwasaidia makuhani kutimiza mahitaji yao ya kiafya.

3. Chagua mshiriki mmoja wa darasa kutoa ripoti ya dakika tano juu ya yale yaliyomo katikaNeno La Hekima (M&M 89:1–17).

4. Chagua washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

177

Somo la 24

24-b, Mazoezi ni mradi bora kwa familia

Page 187: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kuitumikia Jumuiya na Nchi

Madhumuni ya Somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa wajibu wetu katikajumuiya na nchi yetu.

UtanguliziKama waumini wa Kanisa la Yesu Kristo, tunapaswa kujisikia hali yaundugu na upendo kwa watu wote na wa nchi zote za ulimwengu na hasakwa wale walio katika ujirani nasi, jumuiya na nchi zetu. Inatupasa kuwawatiifu kwa nchi yetu na watu wake na kufanya kila tuwezalo kuisaidiaserikali kutekeleza mahitaji ya wale inaowatawala.

“Tunaamini ya kuwa serikali ziliwekwa na Mungu kwa faida yamwanadamu,” kama inavyotangazwa katika Maagano na Mafundisho“kuwa Mungu atawawajibisha wanadamu kwa matendo yao kulingana naserikali hizo” (M&M 134:1).

Wajibu Wetu binafsiShida nyingi za jumuiya hutokea kwa sababu watu wengine katika jumuiyahizo hawaishi maisha ya haki na yaliyo safi au hawafanyi kazi ili kujimudu.Kabla ya kuitumikia jumuiya au nchi zetu, ni lazima sisi wenyewe tuishimaisha ya haki na mema. Yatupasa kwanza kujisaidia sisi wenyewe nafamilia zetu na kujaribu kushinda matatizo yoyote ambayo yanakabili.

Kama kawaida, wajibu wetu mkuu ni kufuata na kuishi injili; Kwa kufanyahivi, hatujisaidii sisi wenyewe pekee bali pia wengine. Mfano mzuri wamaisha yetu utawashawishi wengine kuliko chochote tunachowezakusema. Katika Kitabu cha Mormoni, kwa mfano, watu waliokuwa katikamji mwovu waliambiwa kuwa Bwana amewaachilia tu kwa sababu yamaombi ya watu wema ambao waliokuwa katika mji huo.

Waulize washiriki wa darasa wasome Alma 10:22–23.

Wakati mwingine Bwana ataibariki jumuiya nzima kwa sababu ya watuwachache ndani yake walio wema. Raisi David O. McKay ameongelea juu yaumuhimu wa waumini wa Kanisa kuonyesha mfano mwema: “Sote yatupasakujivunia kwa kulifanya neno Mormoni kuwa la kuaminika, kutokulewa, sheriaya usafi wa kimwili, uaminifu, haki—kanuni hizi muhimu za Kanisa la YesuKristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, na kwa kuzishika kwetu katikamaisha yetu tunachangia katika mabadiliko ya jumuiya, tunaitafsiri dini yetukuwa ni mahali pazuri katika jamii na kuleta wokovu na amani kwawanadamu hapa na sasa.” (Conference Report, Oct. 1927, p. 14.)

178

Somo la 25

Page 188: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Tunaweza kuzipa nguvu jumuiya na nchi zetu kwa kuishi maisha mema naya haki, kwa kuzitunza vyema familia zetu wenyewe, na tukiomba ili tupatenguvu ya kuwa mfano mwema.

Wajibu Wetu katika Ujirani na JumuiyaBwana anatutarajia sisi kuwapenda na kuwatumikia majirani na marafikizetu. Hii haihitaji matendo makubwa ya kujitolea; ila msingi wa urafiki nimatendo madogo ya wema. Sehemu moja wapo ya kuwa jirani mwema nikushughulika na mahitaji ya wengine, pamoja na yale ya wajane namayatima. Huduma kubwa sana ambayo tunaweza kuwafanyia jirani zetuni kuwapelekea injili. Hata kama watakubali au wakatae, inatupasakuendelea kuwapenda na kuwatumikia.

Jumuiya yetu ina mahitaji makubwa ya watu waaminifu na wenye hakiambao wako tayari kusaidia.

Waulize washiriki wa darasa wasome M&M 58:27–28. Tafakari kwa muda mfupi shida ambazozinawapata watu katika jumuiya zetu. Ni mambo gani mazuri tunayoweza kufanya ili kusaidiamji au jiji letu?

Onyesha picha 25-a, “Wajibu wetu kwa Mungu ni pamoja na kuwatumikia wanadamuwenzetu.”

ELIMU

Katika mahali fulani, shule zinahitajika kujengwa au kupanuliwa. Mahalipengine, shule zinahitaji vitabu vizuri vya kusoma, vifaa vya kufundishia nakozi za mafunzo. Hadithi ifuatayo inatueleza jinsi Watakatifu fulani wa Sikuza Mwisho walivyoboresha elimu katika shule za watoto wao:

“Kitu kimoja katika jiji letu tulipendalo, Seattle, Washington, kulikuwa nampangilio mzuri wa ujirani na shule za umma. Kwa miaka ishirini ambayotuliishi huko, mara nyingi tulipata kishawishi cha kuhamia nje ya mji ulelakini baadaye tuliamua kuishi katika mji huu, kwa sababu moja tu ikiwa niheshima yetu kubwa tuliyokuwa nayo kwa ajili ya nafasi za kielimuwalizopata watoto wetu watatu katika shule za umma . . .

“Katika miaka ya karibuni, tuliona mabadiliko ya uongozi wa shule ukianzakutofautiana na ule wa awali ambao ulikuwa thabiti na imara kifedha nakatika sera za elimu . . . Walianza kufanya mabadiliko makubwa katikataratibu na mitaala . . . Maongozi mengine yaliwavunja moyo wanafunzi,yakileta matatizo makubwa ya usalama, maadili na utumiaji wa madawa zakulevya.

“Uharibifu huo wa kutia hofu ulitufanya wengi wetu tuongeze bidii nahuduma zetu katika chama chetu cha Ushirikiano wa Wazazi na Walimu naBaraza teule la Ushauri la shule. Katika eneo kubwa la shule ya sekondariiliyo karibia kulingana na mpaka wa kata yetu, wazazi na marafikiwaliokuwa wakiifuatilia hali ile [waliwachagua] watu miongoni mwetukuwemo katika mabaraza yote mawili.

179

Page 189: Wajibu na Baraka za Ukuhani

25-a

Page 190: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Kutokana na historia ya Kanisa ya kufanya mambo kwa ushirikiano katikamikutano, waumini wa Kanisa walianza kupata umaarufu na kuwezakushawishi uongozi wa shule. Tukiwa tunaunga mkono mipango mizuri,tuliweza kufanikiwa kwa kupiga kura kurejea katika utaratibu wa zamani napia mbinu zake za kufundisha. Kwa kupunguza uchokozi na ugomvi katikamabweni na madawa ya kulevya na maadili mabaya, ilitubidi tuongezeulinzi. Hapo tulipata kuungwa mkono na wazazi wengi zaidi na hivyo[tukawashirikisha wanafunzi katika mabaraza yetu] . . . Tuliuthibitishiaumma kwamba wao wanayo sauti katika yaliyofanywa na viongoziwaliowateua . . .

“Matukio haya tena yalithibitisha kuwa Watakatifu wa Siku za Mwishowakiungana pamoja na wakijitolea wenyewe, wanaweza kutoa mvutoutakaowafanya watu wengi kuwafuata.

“Ushuhuda huu umeniongoza kwenye maeneo mengine ya jumuiya,biashara, siasa na (kushiriki) kikatiba. Imenishawishi mimi kuamini kuwaWatakatifu wa Siku za Mwisho siyo tu lazima, lakini wanaweza kusaidiakuleta mabadiliko ya jumuiya ambayo tunayahitaji sana.” (David L.Tomlinson, “We Changed Our Children’s Schools,” Ensign, June 19976,pp. 52–53.)

Ni mahitaji gani ya kielimu ambayo jumuiya yetu inayahitaji? Ni nini sisi kama watu binafsi nakama kundi la makuhani tunaweza kufanya ili kusaidia?

MAADILI MEMA

Kila wakati, usherati, vitabu au picha chafu, na uovu mwingine unawezakukomeshwa ikiwa tu watu wataungana na kukabili uovu kwa pamoja. Hiiina maana kuwa lazima kuwe na mtu ambaye atakiunganisha kikundihicho, na ni nani ambaye yuko tayari kuongoza ili kupigana na maovu hayokama si mtu mwenye ukuhani? Wenye ukuhani huko jijini Salt Lake kwamfano, waliungana na kufunga majumba ambayo yalikuwa yakionyeshasinema chafu.

Ni matatizo gani ya kimaadili tuliyonayo katika jumuiya zetu? Ni nini tunachoweza kufanya ilikutatua matatizo hayo?

AFYA NA USALAMA

Jumuiya nyingi zinahitaji kuboresha hali zao za kiafya na usalama. Mijimingine inahitaji udhibiti mzuri zaidi wa magari au sheria nzuri za usalama.Mahali pengine panahitaji maji au vifaa vya afya.

Katika kujaribu kuhudumia jumuiya zetu, ni lazima tuangalie mahitajimaluum ya jumuiya yetu. Baada ya kuamua ni shida gani ambayoinatakiwa kutatuliwa kwanza, hapo ndipo tunaweza kuanza kuchagua hitajimoja na kutengeneza mpango wa kulitatua. Waumini wa Kanisawameweza kuwa msaada mkubwa katika miradi mingi ya jumuiya.

181

Somo la 25

25-a, Jukumu letu kwa Mungu ni pamoja na kuwatumikia wanadamu wenzetu

Page 191: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Waumini wengine, kwa mfano, wanashikilia afisi za kisiasa, wanahudumukatika kamati au wanafanya kazi za kujitolea ili kuendeleza jumuiya zao.

Ted Brewerton, mwenye ukuhani huko Calgary, Canada, ni mfano wa jinsimtu mmoja anavyoweza kuendeleza jumuiya yake. Aliheshimiwa kamamtaalamu maarufu wa madawa katika mkoa wake katika mapambanodhidi ya matumizi ya madawa ya kulevya. Alisambaza vijitabu, kutoamihadhara, kutembelea shule na kuwasaidia maafisa wa serikali kudhibitiutumiaji wa madawa ya kulevya. Kwa kweli alileta tofauti kubwa katikamaisha ya mamia ya watu. (Tazama Janice Smith, “Making a Difference,”Ensign, June 1976, p. 50.)

Watakatifu wengine wa siku za mwisho wamejiondoa katika kutoa wakatiwao kwa jumuiya zao wakitoa hoja kuwa hawangeweza kuleta mabadilikoyoyote katika jumuiya zao au kwamba wana shughuli nyingi zaidi. LakiniBwana anatutarajia sisi kushiriki na kufanya kitu kingine mbali na kulitumikiaKanisa. Kuboresha hali ya maisha katika jumuiya pia ni kazi ya Bwana.

Jadili kuhusu mahitaji ya afya na usalama katika eneo letu. Ni nini ambacho sisi kama watuwenye ukuhani tunaweza kufanya ili kuyakabili mahitaji haya?

HUDUMA YA USTAWI

Ni kitu muhimu kwamba Watakatifu wa Siku za Mwisho kukubalikuwasaidia watu wengine wakati wa janga. Mfano mzuri wa huduma hiyo niule ambao ulitokea mwaka wa 1976 wakati bwawa la maji lilipopasuka namafuriko kutokea katika miji kadhaa karibu na Rexburg, Idaho. Waumini waKanisa katika nchi jirani waliamua kusaidia kwa kusafisha miji ambayoilikuwa imeharibiwa. Vijana na makundi ya wenye ukuhani walikodishamabasi na kusafiri hadi katika eneo lililofurika. Walisaidia kusafisha,kutengeza, na kujenga nyumba mpya. Wanaume na wanawake wengiwaliwalea watoto ili kuwawezesha wazazi wao kufanya kazi kwenyenyumba zao zilizoharibiwa. Kwa wiki chache, sehemu kubwa ya kazi yakusafisha ilikuwa imefanyika, shukrani kwa Watakatifu wa Siku za mwishowaliojitolea kuwahudumia wanadamu wenzao.

Njia zingine ambazo tunaweza kuimarisha ujirani na jumuiya ni—

• Kushirikisha injili kwa marafiki na majirani zetu.

• Kuwapenda na kuwahudumia majirani zetu kwa kuwatendea matendomadogo madogo ya wema mara kwa mara.

• Kufanya kazi kama mtu anayejali mambo mazuri katika jumuiya.

• Kusaidia kuyajua na kuyatatua matatizo ya jumuiya.

• Kutumikia katika nafasi ya uongozi katika jumuiya.

Wajibu wetu kwa Nchi YetuRaisi N. Eldon Tanner amesema, “Tungetarajia kila mtu kuwa mtiifu kwanchi yake ya asili—nchi ambayo amezaliwa, nchi ambayo anaishi,

182

Page 192: Wajibu na Baraka za Ukuhani

anafanya kazi na ambayo analea familia yake.” (“If They Will But Serve theGod of the Land,” Ensign, May 1976, p. 48.) Tunahitaji kuhisi upendo kwanchi yetu na watu wake na kuwatakia heri. Upendo huo hutokea kwaurahisi tunapojifunza kufahamu historia na kujitolea kulikofanywa na watuwa nchi yetu.

Kuwa waaminifu kwa nchi yetu haimaanishi kuwa ni lazima tukubaliane nawale wote wanaoiongoza serikali. Maafisa wengi wa serikali, kwa kweli,hujaribu kufanya yaliyo mema, inatupasa kuwaunga mkono. Inatupasakuomba kila siku ili wafanye maamuzi mazuri na kufanya vitu sahihi. RaisiHarold B. Lee wakati mmoja alikuwa na mkutano na Raisi wa Muunganowa Nchi za Amerika. “ambapo alimthibitishia kuwa bila kujali jina lake auchama chake cha siasa, sisi (Kanisa) wakati wote tunapiga magoti chinitukimwomba Mungu ili yeye na viongozi wengine wa taifa hili, na wa dunianzima watusaidie kuyashinda matatizo ya wakati wetu.” (“A Time ofDecision,” Ensign, July 1972, p. 29.)

Kutumikia nchi yetu pia kunahitaji utiifu wa sheria. Amani inawezakupatikana ikiwa kila mtu atatii sheria. Makala ya kumi na mbili ya imaniyanasema: “Tunaamini kuwa chini ya wafalme, maraisi, watawala,mahakimu, na katika kutii, kuheshimu na kuziidhinisha sheria.”

Kama kuna wenye ukuhani wenye umri mdogo katika darasa, zungumzia njia wanazowezakuonyesha heshima kwa mamlaka na kutii sheria. Ni kwa namna gani mvulana anawezakujitayarisha kuitumikia jumuiya na nchi yake?

Kila nchi ina njia tofauti ya kutengeneza sheria. Nchi zingine zinawakubaliraia kuwachagua kwa kupigia kura watu watakaowawakilisha ili kusaidiakutengeneza sheria. Hasa katika nchi hizi, Watakatifu wa Siku za Mwishowanalo jukumu la kujua juu ya mambo yanayowahusu raia na kuwasaidiawatu wazuri kupata ofisi. Katika nchi ambazo uchaguzi hufanyika, kila raiainampasa kupiga kura.

MwishoKama Watakatifu wa Siku za Mwisho tunao wajibu kwa jumuiya na nchizetu. Tunalo jukumu la kuishi maisha ya haki na kusaidia kutatua matatizona kuyakabili mahitaji ya jumuiya yetu yote.

Njia nyingine ambazo tunaweza kutumia ili kutimiza jukumu letu kwa nchiyetu ni—

• Kuwa waaminifu kwa nchi yetu na watu wetu.

• Kuwaombea viongozi wetu.

• Kutii sheria.

• Kujua mambo yanayohusu umma.

• Kuwasaidia viongozi waaminifu na wenye hekima.

183

Somo la 25

Page 193: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Changamoto1. Chagua njia moja unayoweza kuisaidia jumuiya na ujirani wako.

Tengeneza ratiba ya binafsi na anza kufuatilia ratiba hiyo wiki hii.

2. Na kundi lako la wenye ukuhani, amua kile mtakachofanya ili kuboreshajumuiya yenu.

3. Katika maombi yako ya kifamilia, ombea viongozi wa jumuiya na nchi iliwawaongoze vyema.

Maandiko Matakatifu Zaidi1 Timotheo 1:8–10 (umuhimu wa sheria)

1 Timotheo 2:1–2 (inatupasa kuwaombea viongozi wa serikali)

Tito 3:1 (inatupasa kutii serikali zetu)

1 Petro 2:13–14 (inatupasa kutii sheria zilizowekwa na serikali zetu)

Mosiah 29 (mfalme Mosiah anafundisha juu ya serikali)

M&M 134 (mafundisho juu ya umuhimu wa sheria na kanuni za serikali)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Chunguza ni njia gani nzuri katika ujirani na jumuiya yako, ambazo zinaweza faidikakutokana na msaada wa baraza la makuhani.

2. Chagua washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

184

Page 194: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ushuhuda wa Injili ya Yesu KristoMadhumuni ya Somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa jinsi ya kupata nakukuza ushuhuda wenye nguvu wa injili ya Yesu Kristo.

UtanguliziUshuhuda wa Injili ya Yesu Kristo ni kitu kimoja chenye thamani kubwaambacho tunaweza kuwa nacho. Raisi David O. McKay alitambua hivyokatika ujana wake. Alisema: “Niliutamani; Nilihisi kuwa kama ningeupatahuo [ushuhuda], vingine vyote vitakuwa siyo vitu vya muhimu.” (“APersonal Testimony,” Improvement Era, September 1962, p. 628.)

Ushuhuda wetu utatusaidia katika maisha yetu yote wakati wa majaribu nawakati mgumu unapokuja. Wakati kama huo, hatuwezi kusaidiwa naushuhuda wa watu wengine. Bali itatubidi kusimama kwa ushuhuda wetuwenyewe ili kushinda majaribu yetu kwa imani.

Ushuhuda ni nini?Pengine tutakumbuka wakati tulipokutana na wamisionari kwa mara yakwanza na kujifunza injili au kushirikiana pamoja na mtu aliyetusaidiakupata ushuhuda. Au pengine tunakumbuka hisia njema tulizokuwa nazowakati tulipomsikia mtu akitoa ushuhuda wake kwetu. Hisia hizo ni RohoMtakatifu akitushuhudia katika nafsi zetu kuwa kile tunachosikia ni kweli. Nihisia tulivu zisizo na mashaka yoyote. Kwa hisia hizo, tunajua kwambaYesu Kristo ni Mwana wa Mungu na Joseph Smith ni nabii na kuwa Kanisala Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ndio Kanisa pekee la kwelihapa duniani. Hisia hizi pia zinaweza kutupatia ushuhuda wa Neno laHekima, kanuni ya zaka au ukweli wa Kitabu cha Mormon.

Kama muumini wa Kanisa katika siku hizi za mwisho, pia ni muhimu sisikuwa na ushuhuda wa manabii wanaoishi. Raisi Harold B. Lee alielezeaumuhimu wa ufahamu huu:

“Nataka kutia haya ndani ya moyo wako. Mtu mmoja amesema hivi, na ninaamini kuwa ni ukweli kabisa: ‘Mtu huwa bado hajaongolewa kwa ukwelimpaka atakapoona nguvu za Mungu zikiwa juu ya viongozi wa Kanisa hili.’Mpaka iteremke ndani ya roho yake kama moto. Mpaka waumini wa Kanisahili wawe na thibitisho hilo kuwa watu hawa wa Mungu ni watu ambaowanawaongoza katika njia sahihi, na wanashawishika kuwa watu hawa niwatu ambao wanaongozwa na Mungu na kwamba wameteuliwa kwamkono wa Mungu, kwa kweli wanakuwa bado hawajaongoka.” (“TheStrength of the Priesthood,” Ensign, July 1972, p. 103.)

185

Somo la 26

Page 195: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Wacha washiriki wa darasa wafikirie kwa muda juu ya ushuhuda wao. Waulize kukumbukawakati ukweli wa injili ulipofunuliwa kwao na namna walivyopokea ushuhuda wa kiroho kuwaKanisa ni la kweli, kuwa Yesu ndiye Kristo au kuwa Kitabu cha Mormoni ni cha kweli. Waulizewao matukio haya yalikuwaje na jinsi walivyojua kuwa wameupata ushuhuda.

Kupokea UshuhudaMsingi wa ushuhuda ni ufunuo kutoka kwa Roho Mtakatifu. Unakuja wakatiRoho wa Bwana anapoongea nasi moyoni, akilini na Rohoni akithibitishaukweli huo kwetu (tazama M&M 8:2–3). Kristo alimweeleza Petro kuwaushuhuda wake haukutoka kwa binadamu yeyote bali kwa Mungu (tazamaMathayo 16:13–17).

Mzee Parley P. Pratt aliandika matokeo yafuatayo juu ya ushuhudaaliopokea kuwa Kitabu cha Mormoni kilikuwa cha kweli:

“Nilifungua [kitabu cha Mormoni] kwa shauku,” akasema, “na kusomaukurasa wa kwanza. Halafu tena nikasoma ushuhuda wa mashahidikadhaa kulingana na namna kitabu kilivyopatikana na kutafsiriwa . . .Nilikisoma mchana wote; kula kwangu kulikuwa ni mzigo. Sikutamanichakula, kulala niliona kama mzigo wakati usiku ulipofika, kwaninilipendelea kusoma kuliko kulala.

“Wakati nilipokuwa nikisoma, Roho wa Bwana alikuwa nami, na haponilijua na kuelewa kuwa kitabu kile kilikuwa cha kweli kwa urahisi na uwazikama vile mtu ajuavyo kuwa yeye anaishi. Furaha yangu ilikamilika nanilifurahi kiasi cha kulipia uchungu wote, kujitolea kwangu na shida zote zamaisha yangu.” (Autobiography of Parley P. Pratt, p. 37.)

Kwa baadhi ya watu, kupokea ushuhuda ni tukio la wazi kabisa. Kwawengine, siyo tokeo la wazi, hata hivyo haipunguzi umuhimu au thamaniyake. Mzee Loren C. Dunn alisema, “Pengine haitakuja kama mwangazawa ghafula (sijui namna Bwana atakavyowasiliana nawe) kwa kawaidalitakuwa thibitisho na hisia katika moyo wako. Thibitisho ambalo litakujakwa upole, urahisi, lakini kwa njia ya kweli siku baada ya siku mpaka upatekujua kuwa ni kweli).” (Watch Therefore: For Ye Know Not What Hour,”University of Utah Institute Devotional, Nov. 10, 1972 p. 5.)

Raisi Marion G. Romney alielezea kuwa hivi ndivyo alivyopokea ushuhudawake:

“Wakati mwingine ushuhuda humjia mtu polepole baada ya muda mrefu.Sikumbuki wakati nilipopokea ushuhuda kwa ghafula . . . Sikumbuki piawakati ambapo sikuwa na ushuhuda. Umekuwa hata hivyo ukiimarika miakainapopita, lakini sikumbuki wakati ambapo sikuamini. Hata kama ushuhudaunakuja kwa ghafula au polepole, unafanya kitu fulani kwa mtu. Mtu huwatofauti baada ya kupokea ushuhuda.” (“How to gain a Testimony,” New Era,May 1976, p. 11.)

Kuna vitu kadhaa tunavyopaswa kufanya ili kupata ushuhuda. Njia tanozifuatazo ni za muhimu zaidi.

186

Page 196: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Andika njia tano zifuatazo katika ubao:

1. Hamu ya kuamini. Alma anaelezea kuwa njia ya kwanza ya kupata kujuaukweli ni kuwa na hamu kuamini (tazama Alma 32:26–27).

2. Kupekua Maandiko Matakatifu. Nabii Joseph Smith anatuagiza sisi kuwa“pekueni maandiko matakatifu, pekueni mafunuo ambayoyamechapishwa, mwulizeni Baba yenu wa Mbinguni, katika Jina laMwanawe Yesu Kristo awafunulieni ukweli, na mkifanya hayo kwa ajili yautukufu wake bila mashaka yoyote, atawajibu kwa nguvu za Roho wakeMtakatifu. Hapo ndipo utajua wewe mwenyewe na siyo kwa mtumwingine. Na hapo hautamtegemea mtu ili kumjua Mungu; walahapatakuwa na nafasi ya kubahatisha.” (Teachings of the ProphetJoseph Smith, pp. 11–12.)

3. Tenda Mapenzi ya Mungu. Mwokozi anatueleza wazi kuwa kabla ya mtukujua kama fundisho ni la kutoka kwa Mungu, ni lazima alifuate fundishohilo (tazama Yohana 7:16–18).

4. Tafakari Kanuni za Injili. Kutafakari maandiko matakatifu kunamaanishakuwa kujifunza kwa bidii na kufikiria juu ya yale tuliyojifunza, halafutuombe kwa imani kupitia Kristo ili tupate maarifa kutoka kwa RohoMtakatifu kama fikira zetu ni sawa au siyo. (Tazama Moroni 10:3–5.)

5. Kufunga na Kuomba kila Mara. Nabii Alma alikuja kujua yeye mwenyewekuwa injili ilikuwa ya kweli kwa sababu aliomba na kufunga kwa sikunyingi. Baada ya kufunga, Roho Mtakatifu alimshudia kuhusumafundisho ya Mungu katika nafsi yake. (Tazama Alma 5:45–46.)

Wacha mshiriki wa darasa aliyechaguliwa hapo mapema kuelezea yaliyotokea wakatialipopokea ushuhuda.

Kukuza Ushuhuda ImaraMara tunapopata ushuhuda, je! tutakuwa nao wakati wote? Raisi Harold B.Lee alisema, “Ushuhuda siyo kitu ambacho unacho leo na utakuwa nachowakati wote. Ushuhuda ni kitu dhaifu. Ni vigumu kukishika sawa na mbalamwezi. Ni kitu cha kukishikilia katika kila siku ya maisha yako.” (ChurchNews, July 15, 1972, p. 4.)

Ili kuimarisha ushuhuda wetu na kuendelea kuwa na furaha katika injili, nilazima tujaribu kuishi vyema, kutekeleza majukumu yetu katika ukuhani nakuwahudumia wengine. Ushuhuda lazima uwe kanuni ya matendo kamatunataka uimarike.

Onyesha picha 26-a, “Tunaweza kuimarisha ushuhuda wetu tunapowashuhudia wengine.”

Tunapowashuhudia wengine hatuimarishi ushuhuda wetu pekee, bali piaushuhuda wa wale ambao wanatusikiliza. Tumepewa nafasi ya kuelezeaushuhuda wetu mara moja kila mwezi katika mkutano wa mfungo naushuhuda, lakini tunatakiwa kuchukua kila nafasi kutoa ushuhuda wetu kwamarafiki na familia zetu.

187

Somo la 26

Page 197: Wajibu na Baraka za Ukuhani

26-a

Page 198: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kama waumini wa Kanisa, tunalo jukumu la kuwaelezea wengineushuhuda wetu kwa waumini na wasio waumini. Tunaonyesha ushuhudawetu kwa yale tunayoyatenda na kusema kila siku. Tunapotoa ushuhudawetu, utawaimarisha wengine na hata sisi pia. Tunapaswa kuwa shujaakatika ushuhuda wa Yesu (tazama M&M 76:79).

Petro alituonya kuwa: “Muwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizayehabari za tumaini lililo ndani yenu” (tazama 1 Petro 3:15). Ushuhuda wetuunawaleta wengine kwenye ukweli na unawapa hamu ya kutaka kujuamengi. Ushuhuda wetu unawaimarisha hao na hata sisi wenyewe.

Wacha mshiriki wa darasa asome M&M 62:3 na M&M 84:61. Ni kitu gani ambacho Bwanaamewaahidi wale ambao wanatoa ushuhuda wao?

Ushuhuda wetu unaweza kuwa chanzo cha nguvu katika familia zetu. Babaambaye alikuwa akihudumu kama mmissionari mwaka wa 1868alimwandikia mwanawe mvulana: “Ee, mwanangu, ushuhuda wa babayako na uwe kwako kama nyota ya mwongozo katika maisha yako yote”(ilidondolewa na Reinhard Maeser kutoka katika Karl G. Maeser, p. 57).

Uliza wavulana jinsi ushuhuda wa baba zao unavyoweza kuwa “nyota ya mwongozo” katikamaisha yao. Uliza akina baba jinsi kutoa ushuhuda wao unaweza kuwasaidia watoto waokupata ushuhuda.

Changamoto1. Tafuta kupata, imarisha na toa ushuhuda wako wa injili ya Yesu Kristo.

2. Jaribu kuishi maisha yanayostahili ya ushahidi unaoongezeka wa ukwelikwa kuishi karibu na Bwana na kuhudumu kwa uaminifu katika witowako katika ukuhani.

3. Panga mkutano wa jioni ya familia juu ya somo hili. Katika mkutano huotoa ushuhuda wako kwa familia yako.

4. Toa ushuhuda wako katika mkutano wa mfungo na ushuhuda.

Maandiko Matakatifu ZaidiZaburi 19:7 (thamani ya ushuhuda)

1 Wakorintho 12:3 (ushuhuda unatoka kwa Roho Mtakatifu)

2 Timotheo 1:8 (tusione haya kutoa ushuhuda)

M&M 76:22–23 (ushuhuda wa Joseph Smith na Sidney Rigdon)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili.

1. Pata ubao na chaki.

2. Kama unapenda, chagua mshiriki mmoja wa darasa kuelezea namna yeye alivyopataushuhuda.

3. Tayarisha kufungua mkutano kwa kuimba “Ninajua kuwa Mkombozi Wangu Anaishi,”Wimbo, nambari 136.

189

Somo la 26

26-a, Tunaweza kuziimarisha shuhuda zetu kwa kuwashuhudia wengine

Page 199: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Imani Katika Yesu Kristo

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia kuimarisha imani yetu katika YesuKristo.

UtanguliziOnyesha picha 27-a, “Imani katikaYesu Kristo ndiyo kanuni ya kwanza ya injili.” Onyeshapicha hii katika kipindi chote cha somo hili.

Imani katika Yesu Kristo ndiyo kanuni ya kwanza ya injili. Kama tuna imanikwa Yesu Kristo, tuna tumaini kwake; tunamuamini na kuyakubalimafundisho yake. Mtume Paulo aliandika kuwa “maana twaenenda kwaimani, wala si kwa kuona” (2 Wakorintho 5:7). Hii ina maana kwamba imanini kielezo cha kiroho kuwa vitu ambavyo hatuwezi kuviona au kuvisikia vipona kuwa ni vya kweli. Kwa mfano, hatukumwona Yesu wakati alipotufia aukuteseka kwa ajili ya dhambi zetu, lakini tunajua hayo kwa njia ya imani.Alma alisema, “Imani siyo kuwa na ufahamu kamili juu ya mambo, kwahiyo kuwa na imani ni kutumainia mambo ambayo hayaonekani, ambayo niya kweli” (Alma 32:21).

Imani katika Yesu KristoKuwa na imani katika Yesu Kristo huwawezesha wanadamu kujitolea aukufanya kazi ambazo ni ngumu. Kwa sababu ya imani yao, kwa mfanoAbrahamu alikubali kumtoa mwanawe kama dhabihu, Enoch alipalizwa, naNoah aliokolewa kutokana mafuriko (tazama Waebrania 11). Hii na miujizamingine mingi ilitokana na imani katika Yesu Kristo. Kwani kutokana naimani miujiza hufanyika” (Moroni 7:37).

Imani pia inatuwezesha kustahimili masumbuko, majaribu, na mateso.Ayub aliweza kustahimili masumbuko yake makubwa, kwa mfano, kwasababu alikuwa na imani katika Kristo. Bwana alimwimarisha Ayub kwasababu Bwana anajua na anawasaidia wale ambao wanaweka imani yaokwake. (Tazama Nahum 1:7.)

Ingawa Ayub alisumbuka kushinda wengi wetu tutakavyosumbuka lakinikamwe hakukana ushuhuda wake wala hakumgeuka Mungu. Watoto wakewote waliuawa wakati nyumba yake ilipobomolewa na tufani. Mwili wakeulikuwa umejaa majipu. Marafiki zake na hata mke wake walimchekeleawakisema kuwa anateseka kwa sababu alikuwa mtu mwovu. Lakini kwasababu ya imani yake, Ayub aliweza kustahimili majaribu yake. Katikati

190

27-a, Imani katika Yesu Kristo ndiyo kanuni ya kwanza ya injili

Somo la 27

Page 200: Wajibu na Baraka za Ukuhani

27-a

Page 201: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kilele cha masumbuko na uchungu wake, Ayub aliweza kumtukuza Munguna kushuhudia; “Najua ya kuwa Mkombozi wangu yu hai na ya kuwahatimaye atasimama juu ya nchi. Na ingawa ngozi yangu huharibiwa hivi,walakini, katika mwili wangu nitamwona Mungu” (Ayub 19:25–26). Imaniyake mwishowe ililipwa: masumbuko yake yaliisha na akabarikiwa kwawingi.

Hadithi ya Ayub inatuonyesha namna imani, kama nanga, inavyowezakutusaidia kwa uthabiti kushikilia ushuhuda wetu wakati majaribuyanapokuja (tazama Ether 12:4.) Tunaweza kusumbuka kwa ugonjwa,umaskini, kifo, au majaribu, lakini tukijitahidi kwa imani katika Yesu Kristo,tutaimarishwa na kubarikiwa.

Ni matatizo gani ambayo tunaweza kuwa nayo katika maisha yetu? Ni kwa nini tusiwahukumuwale ambao wana matatizo?

Kuimarisha Imani Yetu katika KristoWakati wote yatupasa kutafuta njia za kuimarisha imani yetu. Tunapofanyahivyo tutapata furaha ya kuwa karibu na Bwana na kupokea baraka zake.Alma anatueleza kuwa kukuza imani katika Kristo ni kama kupanda,kustawisha na kuvuna mti wa matunda.

Onyesha picha 27-b, “Imani huanza kwa kupanda mbegu moja.”

Hatua ya kwanza ya kuimarisha imani inaweza kufananishwa na kupandambegu. Alma alisema: “Jaribu maneno yangu na jitahidi ijapokuwa kiasicha chembe ya imani hata kama ni kutamani kuamini, wacha tamaa hiiifanye kazi ndani yako . . . ili mbegu ipandwe” (Alma 32:27–28).

Tunawezaje kupanda mbegu ya imani katika mioyo yetu?

Njia moja ambayo imani huanzia ni wakati tunaposikia au kusoma neno laMungu na kutamani kuliamini. Tunapoyajaribu yale tuliyoyasikia autuliyoyasoma na kufanya jitihada ya kuamini na kuishi kanuni ambazotumefundishwa, hapo tunaanza kuhisi ndani ya mioyo yetu kuwa yaleambayo tumefundishwa ni ya kweli. (Tazama Yohana 7:16–17.)

Onyesha picha 27-c, “Kama vile mmea unavyohitaji mwangaza, hewa, na maji, imani piainahitaji kulishwa wakati wote.”

Hatua ya pili ni sawa na ya kukuza mmea. Kama vile mmea unavyohitajimwangaza wa jua na maji ili ukue, imani yetu pia inahitaji kurutubishwa iliiweze kukua.

Tunawezaje kurutubisha au kuikuza imani yetu katika Yesu Kristo?

Tunaweza kuirutubisha imani yetu kwa kusoma na kutafakari maandikomatakatifu, kufunga na kuomba, kumtumikia Bwana, kuwakubali viongoziwetu wa Kanisa, na kutii amri za Mungu. Kama vile mmea bila maji utakufa,

192

27-b, Imani inaanza kwa kupanda mbegu moja27-c, Kama vile mmea unavyohitaji mwangaza jua, hewa

na maji, imani pia inahitaji kulishwa kila mara

Page 202: Wajibu na Baraka za Ukuhani

27-b

Page 203: Wajibu na Baraka za Ukuhani

27-c

Page 204: Wajibu na Baraka za Ukuhani

imani bila matendo itakufa. Kila wakati inatupasa ili kulisha imani yetu kwakufanya matendo mema. (Tazama Yakobo 2:14–26.)

Onyesha picha 27-d, “Mavuno ya imani ni amani, furaha na uzima wa milele.”

Kwa sababu ya bidii yetu katika kulisha imani yetu, tutaweza kufurahiabaraka nyingi, kama vile utunzaji wa mmea utatuwezesha kufurahiamatunda yake.

Je! kuna baraka au matunda gani yapatikanayo kwa kuwa na imani katika Yesu Kristo?

Imani inatuwezesha—

• “Kushikamana na mambo yote mazuri” (tazama Moroni 7:28).

• Kuwa na amani na furaha, kwani hatuogopi ya siku za usoni.

• Kupata majibu ya maombi yetu.

• Kurahisishwa kwa mizigo yetu na Mungu (tazama Mathayo 11:28–29).

• Kusamehewa dhambi zetu tunapotubu.

• Kutumia nguvu za ukuhani.

• Kuwa na Roho Mtakatifu (tazama Moroni 7:32).

• Kupata miujiza katika maisha yetu (tazama 2 Nefi 26:13).

• Kurudi kuishi na Baba yetu aliye Mbinguini baada ya ufufuko.

Biblia inatuelezea juu ya mwanamke mmoja ambaye alikuwa mgonjwa kwamiaka kumi na miwili. Alitumia vyote alivyokuwa navyo akijaribu kutibiwa namadaktari, lakini walikuwa hawawezi kumtibu. Siku moja Yesu alikuja katikakujiji chao. Alikuwa amewahi kusikia kuhusu Yesu na alikuwa na imanikuwa ataponywa hata kama ataweza kushika tu vazi lake. Na kwa kutumiaimani yake, aliligusa vazi Mwokozi alipopita karibu naye. Mara alipogusavazi lake, mara moja akaponywa na Yesu aligeuka na akamwambia, “Binti,na ufarijike: imani yako imekuponya.” (Tazama Luka 8:43–48.)

Katika hadithi hii mwanamke huyu aliikuza imani yake katika Kristo katikakuweka imani yake kwa matendo. Aligusa vazi la Mwokozi na hapoakapata baraka ya imani yake kwa kuponywa.

Kwa nini ni muhimu kutumia imani yetu katika Yesu Kristo tunapowabariki wagonjwa natunapobarikiwa?

Wacha mshiriki wa darasa uliyemchagua mapema asome au wewe mwenyewe soma hadithiifuatayo.

Randall Ellsworth alikuwa Mmisionari ambaye alitumia imani yake kubwabaada ya kupata majeraha mabaya yaliyotokana na tetemeko la ardhi hukoGuatemala. Wakati wa tetemeko hilo alikuwa ndani ya nyumba ambayoilimwangukia. Kiongozi Mkuu mmoja alielezea tukio hilo kwa njia ifuatayo:

“[Alikuwa] amefukiwa chini, nafikiri kwa masaa kumi na mawili. Alijikutakuwa amepooza kabisa kutoka kiunoni hadi chini. Figo yake pia ilikuwahaifanyi kazi. Hapakuwa na tumaini la kutembea tena kamwe . . .

195

Somo la 27

Page 205: Wajibu na Baraka za Ukuhani

27-d

Page 206: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Alipelekwa na ndege hadi . . . Maryland na . . . hapo hospitali alikuwa namahojiano na mwandishi wa habari wa televisheni. Mwandishi huyo watelevisheni alimwambia, ‘Madaktari wanasema kuwa hutatembea tena. Je!unafikiriaje, Mzee Ellsworth? Alijibu na kusema, ‘siyo sitatembea tena tulakini nina wito kutoka kwa nabii kutumikia misheni huko Guatemala, nanitaenda tena huko Guatemala ili kumalizia misheni yangu.’ . . .

“Alifanya mazoezi [mara mbili zaidi] ya vile alivyoelezwa na madaktari.Aliongeza imani. Alipokea baraka kutoka kwa wenye ukuhani na kuponakwake kulikuwa ni kwa miujiza. Kuliwashangaza madaktari na wenyemaarifa. Alianza kusimama mwenyewe halafu akaweza kutembea namagongo, na baadaye madaktari wakamwambia, ‘Unaweza kurudi kwenyeeneo la misheni yako kama Kanisa litakubali uende.’ Alienda. TulimtumaGuatemala. Alirudi kwenye nchi ambayo alikuwa ameitwa na kwa watuambao alikuwa amewapenda sana.

“Wakati alipokuwa huko alikuwa akitembea, akifundisha masaa yotekulingana na ratiba akiwa na gongo katika kila mkono. Siku moja Raisi wamisheni alimwangalia na kusema, ‘Mzee Ellsworth, kwa imani ambayounayo, kwa nini hutupi magongo hayo na kutembea?’ Aliyaweka chinimagongo na wala hajayatumia tena.” (Tazama Marion G. Romney, “Trustin the Lord,” Ensign, Nov. 1977, p. 42.)

Wacha aliyechaguliwa mapema katika baraza la makuhani kuelezea hadithi juu ya kujiungakwake na Kanisa au wakati ambao aliishi kwa imani wakati alipopatwa na tatizo au majaribuya kibinafsi.

MwishoIli imani yetu ikue, ni lazima tuirutubishe wakati wote. Ni zawadi na barakaambayo tunaihitaji wakati wote na mahali popote. Kila kitu tunachofanyaKanisani kinahitaji imani katika Yesu Kristo. Kulipa zaka, kwa mfano, aukulitumikia Kanisa, au kuweka akiba ya pesa ya kutosha ili kwendahekaluni inahitaji imani. Tunapolisha imani yetu katika Yesu Kristo kwakumtii yeye, kusoma injili yake, kuomba, tunapofunga, kwenda mikutanoni,na kutumikia katika Kanisa, tutapokea baraka nyingi za ajabu. Baraka kuuzaidi ya kuimarisha imani yetu ni kwamba tutakuwa wenye kustahili kurudikwa Baba yetu aliye Mbinguni.

Changamoto1. Tumia imani yako katika Yesu Kristo wakati unapoitwa kufanya ibada ya

ukuhani kama kumbariki mgonjwa.

2. Tumia kanuni ya imani katika kukabiliana na shida zako za kibinafsi.

197

Somo la 27

27-d, Mavuno ya imani ni amani na furaha na uzima wa milele

Page 207: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Maandiko Matakatifu ZaidiMarko 6: 5–6 (miujiza haiwezi kufanyika pasipo imani)

Waebrania 11 (mafundisho juu ya nguvu za imani)

1 Petro 1:3–9 (wokovu huja kwa imani)

Enos 4–8, 15 (dhambi husamehewa kwa imani)

Esther 12:12–21 (mifano ya nguvu za imani)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 18 “Imani katika Yesu Kristo,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Jifunze Waebrania Sura ya 11.

3. Chagua washiriki wa darasa watakao toa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

198

Page 208: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Toba

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa jinsi toba inavyowezakututayarisha kurudi kwa Baba yetu aliye Mbinguni.

UtanguliziNabii Joseph Smith siku moja alitupatia changamoto hii: “Acha sisituanze upya siku hii, na sasa tuseme kwa mioyo yetu yote, tutawachakutenda dhambi na kuwa watu wema.” (Teachings of the Prophet JosephSmith, p. 364.)

Kwa sababu sisi sote tupo duniani ili kujifunza na kukua, sisi zotetunafanya makosa. Kuna aina nyingi ya makosa. Wakati mwinginetunafanya vitu ambavyo hatufai kufanya kama kuwa wabaya au kuchukuakitu ambacho siyo chetu. Hizi huitwa dhambi za kutenda. Wakati mwinginepia tunakosa kufanya vitu ambavyo inatupasa kufanya kama kulipa zaka aukuwa rafiki wa majirani zetu. Hizi zinaitwa dhambi za kuacha.

Haja ya TobaWakati tunajua kuwa tumefanya makosa, hatuwezi kuwa na furaha.Tunaona aibu kwa makosa yetu na tunajikuta hatuwezi kumtumikia Bwanavizuri. Wakati mwingine, tunapokosa furaha sisi wenyewe, inawezakutusababisha sisi kuwatendea wengine mabaya. Baba yetu aliyeMbinguni hataki tukose furaha. Anataka sisi zote kupokea barakaalizonazo, lakini hatatupatia baraka ambazo hatustahili. Hii haimaanishikuwa ametugeuka au hatupendi kabisa. Bali ina maana kuwa anataka sisikushinda udhaifu wetu na hatutaweza kuzishinda kama angetubariki kwakutenda mabaya. Toba, kwa hivyo, ni mpango wa Mungu wa kutusaidiakushinda udhaifu wetu na hivyo kustahili kuishi naye.

Kwa sababu hii, ametuambia tuyachunguze maisha yetu na kujua mahalitunapohitaji kujirekebisha. Raisi Joseph Fielding Smith alifundisha: “Nijukumu letu kuwa wazuri leo kuliko jana na wazuri kesho kuliko leo. Kwanini? Kwa sababu tuko katika barabara hiyo . . . ya ukamilifu, na hiyoinaweza kuja tu kupitia utii na tamaa ya mioyo yetu ya kushinda dhambizetu.” (Doctrines of Salvation, vol. 2, pp. 18–19.)

Soma Alma 11:37. Kwa nini toba ni kitu cha lazima? Soma 1 Yohana 1:8–10, Alma 34:33–34;3 Nephi 30. Kwa nini ni lazima kutubu haraka iwezekanavyo?

Ni Namna Gani Mtu Anatubu?Dhambi ni kama uchafu katika miili yetu. Inatufanya kuwa wachafu kiroho.Toba ni kama kuosha uchafu huo na sabuni na maji. Baada ya kutubu

199

Somo la 28

Page 209: Wajibu na Baraka za Ukuhani

tunahisi kuwa wapya na wasafi. Mzee A.Theodore Tuttle anaelezea kwanjia hii:

“Toba ni kama sabuni. Ni sabuni ya maisha. Kama sabuni, inaoshadhambi za maisha. Inafaa kutumiwa wakati wote inavyohitajika. Mtuyamfaa kuweka akilini, hata hivyo, kwamba kutumia vibaya—upungufu wakutojisafisha kabisa na juhudi za nusu nusu— matokeo yake nikutokung’ara. Ikitumiwa vizuri, hata hivyo, sabuni ya maisha itatusafishavizuri kabisa na daima . . .

Siku moja sisi . . . tutaenda mbele ya baraza la hukumu la Bwana. Hapotutasimama kama tuna madoa ya dhambi, uchafu na wachafu au kwakukubali na kutumia zawadi kuu na ya ajabu ya kusafishwa—kwa sabuni yamaisha—, hapo tutaweza kusimama tukiwa wasafi, tuliosamehewa, nawasafi mbele za Bwana. Wakati mwingine utakapotumia sabuni, ungependapia kufikiria juu ya kusafishwa kiroho, kwa kutumia sabuni ya maisha,ambayo ni sheria ya ulimwengu ya toba.” (“Repentance,” Improvement Era,Nov. 1968, p. 64.)

Ili kutubu, inatupasa kufuata hatua fulani zifautazo.

Onyesha picha 28-a, “Toba ya kweli huchukua muda na juhudi.”

Jadili sehemu saba za toba kama zilivyoelezwa katika kitabu cha Kanuni za Injili, sura ya 19.Kama yawezekana, baadhi ya washiriki wa darasa na kila mmoja achukue sehemu moja,wajitayarishe kujadili na halafu kuleta mjadala huo darasani. Onyesha orodha iliyoorodheshwasehemu hizo saba za toba wakati zikijadiliwa. (Sehemu hizo ni kuitambua dhambi, kuwa nahuzuni kuhusu dhambi, kutupilia mbali dhambi, kuisema dhambi, kurekebisha au kulipaulichoharibu, kuwasamehe watu wengine na kuweka za Mungu.)

Toba ya kweli siyo rahisi. Inachukua muda na jitihada. Kwa sababu hii,hatuwezi kusogesha mbele siku yetu ya toba (tazama Alma 13:37).

Furaha ya TobaOnyesha picha 28-b, “Toba inawezekana kwa sababu Yesu Kristo alilipia dhambi zetu.”

Tunatubu ili kupata msamaha wa dhambi zetu. Lakini kama Yesu Kristohangekuwa amelipia dhambi zetu na kufa kwa sababu yetu, hatungewezakusamehewa. Ni kupitia malipo yake ya kujitolea pekee ndipo rehemainaweza kutosheleza haki na hapo ndipo dhambi zetu zinaweza kuoshwa(tazama Alma 34:10–16). Hii ni baraka kubwa, na wakati wote yatupasakuwa na shukrani kwa sababu yake.

Yesu alilipia dhambi zetu, lakini haziondolewi kutoka kwetu haditunapotubu. Wakati Alma mdogo alipotambua kuwa alikuwa amefanyadhambi, alisema, “nilikumbuka dhambi na matendo yangli yote mabayaambayo kwayo nilitaabika kwa uchungu kama wa Jehanum . . .

“Nilikumbuka pia kuwa nilimsikia baba yangu akiwatabiria watu juu ya kujakwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ili kulipia dhambi za ulimwengu.

200

28-a, Toba ya kweli inahitaji muda na jitihada

Page 210: Wajibu na Baraka za Ukuhani

28-a

Page 211: Wajibu na Baraka za Ukuhani

28-b

Page 212: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Nilipokuwa nikifiria juu ya utabiri huu, nililia ndani ya moyo wangu: EweYesu, uliye Mwana wa Mungu, unihurumie.

“Na sasa, tazama, nilipokuwa nikilitafakari jambo hili, sikuweza kukumbukauchungu wangu tena . . .

“Na Loo! Furaha gani, na ni nuru ya ajabu niliyoiona; ndiyo, na nafsi yanguilijaa furaha kupita uchungu wangu.” (Alma 36:13, 17–20.)

Pata mshiriki wa darasa kuelezea juu ya fumbo ya mwana mpotevu (Luka 5:11–32). Ni ninimwana mpotevu alifanya wakati alipojisikia na kuanza njia ya toba? Baba yake alijisikiaje?

Kwa sababu wanadamu wanaendelea kutenda dhambi na kuhitaji kutubu,hadithi ya mwana mpotevu inarudiwa mara kwa mara, kama katika hadithiifuatayo:

Wachia mshiriki wa darasa aliyechaguliwa mapema kueleza hadithi ya mwana mpotevu wawakati huu. Washiriki wa darasa wakae kimya wakijaribu kutambua hatua za toba ambazoalifuata.

“Mpaka nilipokuwa na miaka 17, nilikuwa karibu na Kanisa, nikiendakwenye mikutano yangu yote na kufanya kazi zangu za ukuhani. Sikuwahikufikiria kufanya vingine. Nililipenda Kanisa na mipango yake.

“Nikiwa na miaka 17, hata hivyo, nilianza kulegeza misuli yangu ya ujana,na kuasi maongozi ya familia na kutaka uhuru wangu wa kuchagua. Mmojakati ya rafiki zangu alikuwa wa imani nyingine. Hapo nilianguka katikamtego na kujaribu vitu vingine ambavyo alinipatia—pombe, tumbako. Pianilikuwa na urafiki na wasichana ambao siyo Watakatifu wa Siku zaMwisho. Muda usiyo mrefu nilikuwa katika mapenzi na msichana mmojamrembo. Wazazi wake walinikaribisha katika banda lao la kukaa wakati wakiangazi siku za mwisho wa wiki nyingi na hii ndiyo ilinifanya mimi kukosakushiriki shughuli za Kanisa.

“Hapo vita vya pili vya ulimwengu vilitokea na wakati askofu wangualiponiuliza kama ningependa kwenda misheni, nilisema ni afadhalinijiunge na jeshi na kutumikia nchi yangu. Bado ninaamini kuwa kutumikianchi yangu ni muhimu, lakini ninajua sasa kuwa ningefanya jambo lahekima kama ningetumikia misheni ya Baba yangu wa Mbinguni kwanza.

“Pia, kwa wakati huu, niligundua kuwa wauminii wengine wa Kanisa ambaoniliwaheshimu kabisa walikuwa hawafuati kanuni zote za Kanisa. Nilijiwekakuwa hakimu wao na kwangu walikuwa wanafiki. Nilijifanyia agano mimimwenyewe kuwa kama sitaweza kufuata kanuni zetu, badala ya kuwamnafiki kwa kufundisha kitu kimoja na kufanya kingine, nitakaa mbali naKanisa. Hili lilikuwa kosa lingine baya, kwani hivi ndivyo nilivyofanya nandivyo shetani alichokuwa akitaka.

“Miaka minne kama rubani katika jeshi la maji na miaka 15 nikisafiri katikataaluma ya mauzo, ilifanya kuwa rahisi kwangu kukosa kushiriki kikamilifu,

203

Somo la 28

28-b, Toba inawezekana kwa sababu Yesu Kristo alilipia dhambi zetu

Page 213: Wajibu na Baraka za Ukuhani

lakini miaka hii yote niliamini ukweli ambao ulikuwa ndani ya nafsi yangu.Wakati nilipokuwa na miaka 38, ndugu yangu mdogo, Tom, alikuja kuishinasi kwa wiki sita. Kila Jumapili alienda pekee yake kwenye mkutano waukuhani na mikutano mingine, na dhamira yangu ilianza kunisumbua.Sikuwa na furaha. Nilijua kulikuwa na kitu kibaya na hisia hizi zilikuwa zikijakwa nguvu kila wakati. Hapo zamani niliweza kuacha kuvuta sigara wakatinilipotaka lakini sasa niliona kuwa siwezi. Ningeweza kumtembelea Tomkatika afisi yake, nilijikuta nikiongea vibaya juu ya Kanisa na baadaye,ingawa singeweza kumwambia hivyo, nilihisi nimekosa.

“Nilikuwa nikijiongezea shida na ilikuja usiku mmoja baada ya karamu nakucheza dansi. Nilienda kulala nikiwa nimechelewa lakini sikupata usingizi,kitu ambacho si cha kawaida kwangu. Mwishowe niliamka ili nisimsumbuemke wangu mpenzi na kwa mara ya kwanza katika maisha yangunilitembeatembea nikiwa na mawazo tele, mwishowe nilitambua kuwalazima nibadilike.

“Nilikuwa bado sijawahi kuonyesha mshtuko wa moyo wala machozi naunyenyekevu, lakini kitu kilichofuata ambacho nakumbuka, nilikuwa chinikwenye magoti nikimsihi Baba yangu aliye Mbinguni kunisaidia kwa maraya kwanza katika miaka 19. Nilipokuwa nikiomba hisia ya upendo nahuruma na furaha iliijaza nafsi yangu na Roho Mtakatifu alinizunguka kwanguvu ambayo ilinifanya kulia kwa masaa mengi. Wakati nilipoamka,nilijiskia vizuri. Shukrani na asante ziliujaza moyo wangu. Katika maishayangu sikuwahi kamwe kujua hisia ya joto na kujazwa na moto ndani yanafsi yangu kwa nguvu hata nikafikiri kuwa nitaungua.

“Nilienda katika chumba chetu cha kulala na nikamwamsha mke wangu.Nilikuwa bado ninalia na akaniuliza ni nini. Nikamwelezea hamu yangu yakubadili maisha yangu na kuishi kulingana na injili ya Yesu Kristo na maramoja aliniambia kuwa ataniunga mkono. Kutoka wakati huo sijawahi kuwana tamaa ya sigara, pombe ya aina yoyote, au kikombe cha kahawa.

“Bwana alianza kunibariki na hajaacha kamwe hadi siku ya leo. Kwa mudawa mwaka moja niliweza kuwabatiza watoto wangu, baada ya muda mfupi,mke wangu. Baada ya mwaka mmoja tulienda katika Hekalu la Logan nakufunga ndoa ya milele na watoto wetu kuunganishwa nasi.

“Natoa ushuhuda kwamba Bwana hufurahi wakati kondoo aliyepoteaanaporudi nyumbani. Yeye huonyesha upendo wake na wema kwa sisisote tunapotubu dhambi zetu na kufuata amri zake.” (Lewis W. Cottle, “TheReturn of the Prodigal,” Ensign, Mar. 1974, pp. 43–44.)

Ni hisia gani alizokuwa nazo mwana huyu mpotevu wa siku hizi alipotubu? Soma Luka 15:10.Ni namna gani Baba yetu aliye Mbinguni anaitazamia toba yetu? (Tazama M&M 58:42 naIsaya 1:18.) Yatupasa kumchukulia vipi mtu aliyetubu?

204

Page 214: Wajibu na Baraka za Ukuhani

MwishoSisi sote tunahitaji kutubu kama tunataka kuwa kama Baba yetu aliyeMbinguni na kuishi naye tena. Kwa sababu hii Yesu Kristo alituwezeshakutubu dhambi zetu kwa upatanisho wake. Wakati tunapotubu dhambi zetutunajiletea furaha kwetu na kwa Baba yetu wa Mbinguni.

Raisi Harold B. Lee alifundisha: “Amri muhimu kabisa ya Mungu ni ile mojaambayo inakuwa vigumu sana kwako kuifuata leo. Ikiwa ni kukosauaminifu, ikiwa ni kukosa usafi wa kimwili, ikiwa ni udanganyifu, kukosakusema ukweli, leo ndiyo siku ya kuifanyia kazi hadi uweze kushindaudhaifu huo. Halafu anza ile inayofuatia ambayo pia ni vigumu kwakokuifuata.” (Church News, May 5, 1973, p. 3.)

Changamoto1. Mlilie Bwana katika maombi yako ya kibinafsi ili akusaidie katika tatizo

ambalo unalishugulikia. Mpatie habari kila siku jinsi unavyoendelea nakadiri unavyojaribu kujibadilisha, endelea kuomba msamaha kwadhambi za zamani.

2. Onyesha furaha katika toba ya wengine, hasa watu wa familia yako.

Maandiko Matakatifu ZaidiZaburi 51:10 (Daudi aliomba ili kupata msamaha)

Isaya 1:16–18 (tumeamriwa kutubu)

Luka 15:7 (selestia hufurahia juu ya wale wanaotubu)

2 Wakorintho 7:10 (sikitiko la mcha Mungu huleta toba)

Mosiah 4:1–3 (msamaha wa dhambi hupatikana kwa sababu yaupatanisho wa Kristo)

Alma 7:15 (ubatizo ni ishara ya toba)

Alma 12:14–15 (imani na toba huleta wokovu)

Alma 34:8–9 (Kristo alilipia dhambi za dunia)

M&M 19:16–17 (Kristo aliteseka kwa wale ambao watatubu)

M&M 76:40–42 (Yesu alikufa ili kulipia dhambi za dunia)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 19, “Toba” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Kumbusha washiriki wa darasa kuleta vitabu vyao vya Maandiko Matakatifu katika darasa.

3. Kama ungependa, chagua washiriki wa darasa watakaozungumzia juu ya hatua saba zatoba zilizoonyeshwa katika sura ya 19 ya kitabu cha Kanuni za Injili.

4. Chagua washiriki wa darasa watakaoelezea na kutoa hadithi na maandiko matakatifukatika somo hili.

5. Tayarisha Somo ili kuepuka kuzungumza juu ya matatizo ya kibinafsi ya wana Jamii.

205

Somo la 28

Page 215: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Ubatizo, Agano la Kudumu

Madhumuni ya Somo hili ni kutuhimiza kuendelea kuyashika maaganoambayo tulifanya wakati wa ubatizo.

UtanguliziKila mmoja wetu ambaye amebatizwa, amebatizwa kama ishara kwambaamebadilisha maisha yake na yuko tayari kutii kanuni ambazozinamuongoza mbinguni. Lakini kubatizwa pekee hakutoshi. Wakati huo,tulianza njia mpya ya maisha; na ili kupata baraka ya hayo maisha mapya,inatulazimu kuendelea mbele na kujibadilisha wenyewe.

Nabii Alma, akifikiria juu ya ndugu zake wenye ukuhani baada ya ubatizowao akiwaambia: “Tazama sasa nawauliza ndugu zangu, katika kanisa,mmezaliwa kiroho katika Mungu? Je! mmepata mfano wake katika nyusozenu? Je! mmepata mabadiliko haya makuu ndani ya mioyo yenu?”(Tazama Alma 3:14.) Hili swali ni la muhimu hata kwa wakati huu. Je!tumeweza kuona tofauti katika mioyo yetu na kuhisi kuzaliwa upya kirohotangu tulipobatizwa katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku zaMwisho?

Watu wengi wanafurahia hisia za kiroho wakati wa ubatizo wao. Muuminimmoja alielezea hivi: “Sitasahau furaha ndani ya nafsi yangu kuwa msafina kuanza upya kama mtoto wa Mungu . . . Ilikuwa furaha isiyo na kifani!”(No More Strangers, Vol. 3, p. 175.)

Agano Letu la Ubatizo Onyesha picha 29-a, “Wakati wa ubatizo tunafanya agano na Mungu kuwa tutafuata amrizake.”

Agano ni mapatano baina ya watu wawili au zaidi. Wakati wa ubatizotulifanya agano muhimu sana na Mungu. Raisi Spencer W. Kimballalisema: “kubatizwa ni kuingia katika agano (na Mungu) kufanya, siyo tukuacha, bali ni kufanya kazi ya wema na kuepuka uovu.” (Miracle ofForgiveness, p. 94.)

Washiriki wa darasa wasome na kutia alama katika M&M 20:37, Mosiah 18:8–10. Ni maaganogani hasa tuliyoyafanya na Bwana tulipokuwa tukibatizwa? (Orodhesha maagano hayoubaoni.)

206

29-a, Wakati wa ubatizo tunafanya agano na Mungu kufuata amri zake

Somo la 29

Page 216: Wajibu na Baraka za Ukuhani

29-a

Page 217: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Tuliagana ku—

• Kuingia katika Kanisa la Yesu Kristo.

• Kuitwa kwa jina lake.

• Kumtumikia Mungu na kufuata amri zake.

• Kutumikiana na kusaidiana katika shida zetu.

• Kuwa shahidi wa Kristo na Kanisa lake.

Haya maandiko Matakatifu yanatueleza pia juu ya sehemu ya Mungukatika agano la ubatizo.

Bwana alituahidi nini wakati tulipobatizwa? (Andika majibu katika ubao.)

Bwana aliahidi—

• Kusamehe dhambi zetu.

• Kutupatia maongozi ya Roho Mtakatifu.

• Kutuwezesha kufufuka wakati wa ufufuo wa kwanza.

• Kutupatia uzima wa milele.

Ubatizo ndiyo mwanzo wa haya “mabadiliko makuu” ambayo sisi zoteinatupasa kuyapata ili kurudi kwa Baba yetu aliye Mbinguni (tazama Alma5:13–14 na Mosiah 5:7–9). Wengine wetu hatubadiliki wakati huo ambaotumebatizwa, lakini kadiri tunavyoshika maagano yetu, tamaa na matendoyetu hubadilika na tunakuwa kama Baba yetu aliye Mbinguni. Ubatizo wetukwa kifupi hutupatia mwanzo mpya na kuzaliwa upya kiroho. Sisi, kamaKristo, “tulizikwa” katika maji wakati wa ubatizo, na tena kuinuliwa juu kwamaisha mapya (tazama Warumi 6:3–4). Maisha haya mapya yalianza kwamapatano yasiyo na mwisho na Mungu; Na kama tutafanya sehemu yetu,atafanya sehemu yake. Tukiendelea kumtii, atatusaidia kubadilika nakutuongoza kurudi kwenye uwepo wake.

Acha kaka wawili uliowachagua awali waelezee hadithi zao binafsi juu ya namna walivyojisikiawakati walipobatizwa na namna maisha yao yalivyobadilika tangu ubatizo wao. Husisha vijanakatika sehemu hii ya somo.

Maendeleo Yetu baada ya UbatizoWatu wengine wanafikiria kuwa wokovu unakuja tu kwa sababuwamebatizwa. Hata hivyo, ubatizo ni mwanzo tu. Inatupasa kuendeleakukua kwa haki baada ya ubatizo kama tunataka kupata uzima wa milele.Kutusaidia kufanya hivyo, Bwana ametupatia amri fulani ambazotunapaswa kuzishika baada ya ubatizo.

Washiriki wa darasa wasome Moroni 6:4–9. Tunalo jukumu gani baada ya ubatizo? (Andikamajibu katika ubao. Jibu moja ni kufuata maongozi ya Roho Mtakatifu, lakini haya tutayajadilikatika somo la 30.)

Wajibu wetu baada ya ubatizo ni—

• Kuomba wakati wote.

208

Page 218: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Kufunga juu ya mahitaji muhimu.

• Kuhuthuria na kushiriki katika mikutano ya kanisa.

• Kupokea sakramenti kila mara.

• Kujali usitawi wa kila mmoja wetu.

• Kutubu wakati tumefanya makosa.

• Kufuata maongozi ya Roho Mtakatifu.

Wakati tulipobatizwa na kupewa kipawa cha Roho Mtakatifu, Mungualifanya ahadi nasi ambazo atazitimiza ikiwa tutaishi kulingana na ahadizetu. Lakini tunaposhugulika katika majukumu yetu ya kujilisha, kwendashuleni, na kufanya kazi zingine muhimu tunajiingiza katika, matatizo yaulimwengu na kusahau maagano yetu. Tatizo ambalo zote linatukabili nijinsi tunavyoweza kuwa kiroho na kuenenda katika maisha yetu mapya.Vitu ambavyo Moroni amevitaja ni vya kutusaidia kuendelea katika maishamapya ambayo tulianza wakati tulipobatizwa na hapo kuzaliwa hasa kirohomara ya pili.

MAOMBI

Maombi ya kibinafsi ni muhimu kama tunataka kuwa na nguvu tunazohitajiili kufuata amri za injili. Maombi yanatuweka karibu na Baba yetu aliyeMbinguni na yanatuwezesha kuonyesha shukrani zetu kwake na pia kujadilimatatizo yetu naye. Inatupasa kuiona kama baraka kubwa hivyo basi,kufungua na kufunga kwa maombi kila siku ya maisha yetu.

KUFUNGA

Angalao mara moja kwa mwezi maombi yaambatane na mfungo. KamaKanisa, kwa kawaida tunafunga kwa milo miwili wakati wa Jumapili yamfungo. Sisi binafsi tunaweza kufunga wakati tunapohitaji faraja na nguvuza kiroho. (Tazama Somo la 31 katika kitabu hiki.)

KUHUDHURIA MIKUTANO YA KANISA

Sisi wote tunapata nguvu ya kiroho kwa kuhudhuria kila wakati katikamikutano ya Kanisa, mahali ambapo tunajifunza mengi juu ya injili nakujenga ushuhuda wetu. Inatupasa kuhimiza wana familia wote kwendakatika mikutano yao yote ya Kanisa. Tunapohudhuria katika mikutano hiiyote, inatulazimu kushiriki kwa kuimba, kutafakari, kutoa mahubiri na kuwawanyenyekevu.

KUPOKEA SAKRAMENTI

Onyesha picha 29-b, “Tunafanya tena upya maagano za ubatizo tunapopokea sakramenti.”

Sababu moja ya kuhudhuria katika mkutano wa sakramenti ni kupokeasakramenti. Maagano tunayofanya wakati tunapopokea sakramenti ni sawana yale tuliyofanya wakati wa ubatizo. Kwa njia hii, kila wiki wakati wa

209

Somo la 29

Page 219: Wajibu na Baraka za Ukuhani

29-b

Page 220: Wajibu na Baraka za Ukuhani

sakramenti tunakumbuka maagano yetu ya ubatizo na kuahidi tenakwamba tutayashika.

KUWASAIDIA WENGINE

Mshiriki aliyechaguliwa awali alinganishe M&M 20:37 na M&M 20:77.

Wakati tulipobatizwa, tulimuahidi Bwana kuwa tutakuwa tayari “kusaidiawengine katika shida zao, . . . Kuhuzunika na wale ambao wako katikahuzuni, na kuwafariji wale ambao wanahitaji faraja” (Mosiah 18:8–9).Kuwatumikia wanadamu wenzetu—kusaidia wenye shida, kufundishafamilia zetu, na kujali usitawi wa watu wengine ni sehemu ya mapatano yaubatizo na Bwana. Ni sehemu muhimu ya maisha mapya ambayotunalazimika kufanya sisi wenyewe baada ya ubatizo.

KUTUBU DHAMBI ZETU

Ni kweli, sisi sote hufanya makosa, na kwa hiyo, lazima tutubu ili kushikamaagano ya ubatizo. Tunatubu kwa kujua na kukubali mbele ya wenyemamlaka sahihi kwamba tumefanya makosa (tazama somo la 28 katikakitabu hiki). Kwa njia ya toba tunaweza kusafishwa tena kutokana nadhambi zetu na ndipo kuwa wenye kustahili kupata maongozi ya RohoMtakatifu.

Njia ya Kuelekea UkamilifuJe! Kutakuwa na wakati ambao hatutahitaji agano letu la ubatizo? Jibu,kwa kweli, hapana . . . siyo mpaka tutapokuwa wakamilifu kama vileMungu alivyo mkamilifu. Mpaka wakati huo ni lazima tuendeleekuyakamilisha maisha yetu, kubadilisha tabia mbaya kwa zile nzuri. RaisiSpencer W. Kimball alisema: “Ni kweli kwamba kujitawala mwenyewe nijambo la kuendelea—safari, siyo kuanza pekee. Wanadamu hawawi wemamara moja kama vile mbegu ya mti haiwezi kuwa mti mara moja.Kujiendeleza kuwa mkamilifu inaweza kufanyika kwa haraka kama kwaunyenyekevu tutapiga hatua zinazotuelekeza kwenye matarajio yetu.” (TheMiracle of Forgiveness, p. 210.)

Nabii Nephi anafundisha kuwa baada ya ubatizo “lazima tuendelee mbele”na ‘kuvumilia hadi mwisho’. Ametuahidi kuwa Mungu atatupatia uzima wamilele tukionyesha upendo wetu kwa kumtii (tazama 2 Nephi 31:19–21).Tunapomtii Bwana na kushika maagano tuliyofanya naye wakatitulipobatizwa, tutapata furaha katika maisha haya na furaha ya milelekatika maisha yanayokuja.

Raisi Joseph Fielding Smith alielezea hitaji letu la kuvumilia hadi mwishokwa kuweka agano letu kwa njia hii: “Kusudi moja kubwa la Kanisa la kwelini kuwafundisha wanadamu mambo ya lazima kufanya baada ya ubatizo ili

211

Somo la 29

29-b, Tunafanya upya maagano yetu ya ubatizo tunapopokea sakramenti

Page 221: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kupata baraka kamili za injili . . . Lazima tuvumilie hadi mwisho: Lazimatushike amri baada ya ubatizo, lazima kuufanyia kazi wokovu wetu . . .Lazima tuishi ili kuwa na tabia za uungu na kuwa kama watu ambaowanaweza kufurahia utukufu na maajabu ya ufalme wa selestia.” (“ThePlan of Salvation,” Ensign, Nov. 1991, p. 5.)

MwishoAliyekuwa mtawa wa kike wa Katoliki ambaye aliongoka na kuingia katikaKanisa alielezea jinsi ubatizo wake ulivyo na maana kwake:

“Kila kitu ambacho nilikiona na kusikia katika Kanisa kilinifurahisha sana.Hali na upendo pamoja na jinsi waumini wanavyo wajali waumini wenzao,ilinifanya kutambua kuwa dini hii lazima ina kitu fulani ndani yake . . .

“Nilitambua kuwa nilikuwa katika Kanisa potovu na kuwa Kanisa la YesuKristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ndilo Kanisa la kweli pekee hapaduniani. Nilijua pia kwamba . . . lazima nijiunge nalo . . .

“Kugeuka kwangu kutoka katika maisha ya zamani na maisha ya wakatihuu haikuwa rahisi, lakini kitu ambacho kimeniwezesha mimi kwa wakatihuo wote ni kuwa kufanya tena maagano ya ubatizo kila wiki katikamikutano ya sakramenti—agano langu la kuchukua jina la Mwokozi juuyangu na wakati wote kumkumbuka na kuzishika amri zake, na agano laBwana kwangu, kuwa nikiheshimu ahadi hizo, Roho wake utakuwa namiwakati wote.

“Halafu nakumbuka ubatizo wangu na kutumbukizwa kabisa ndani ya maji.Kwangu ni mfano wa kufa kwa uchoyo na dhambi na kuinuliwa katikamaisha mapya kama mtoto wa Mungu. Tendo hili la ubatizo pia, nafikiri, niishara ya njia ambayo Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuishi—kushindauchoyo na kupigana na majaribu. Kwa njia hii ‘tunakufa’ kwa ubinafsi nadhambi na kuinuka na kuendelea mbele kila siku katika barabara ambayoinatuongoza kurudi kwa Baba.

“Halafu kwa kimya nafanya upya agano langu la kuchukua jina la YesuKristo juu yangu, na kumwambia kuwa nafanya upya ahadi ya kumkubali,kanuni za injili na mafundisho yake, kulikubali Kanisa na kumkubali nabii nawengine wenye mamlaka katika Kanisa, ndiyo pekee waliochaguliwa naMungu ili kutuongoza. Katika maombi yangu ya kimya naongeza kuwaninafanya tena agano la kumkumbuka wakati wote, kwa mfano, kutambuauwepo wake, hasa wakati wa majaribu na uchovu. Mwishowe nafanya tenaagano la kufuata amri zake, nikijua kuwa nikifanya haya kwa uaminifu,nitakuwa na Roho wake daima.” (Miriam Spain Peterson, “The Lord TakesCare,” No More Strangers, Vol. 3, pp. 154–59.)

212

Page 222: Wajibu na Baraka za Ukuhani

ChangamotoChunguza umeshafanya nini na maisha yako toka ulipobatizwa. wakati huopengine ulihisi “mabadiliko ya moyo” yakianza ndani yako. Kama vile nabiiAlma alivyouliza, “Unaweza kujisikia hivyo sasa?” (Alma 5:26). Je! badowaweza kuhisi “maisha mapya” ambayo yameelezwa katika maandikomatakatifu? Kama kuna upungufu anza leo kutubu na kurekebisha tatizo hilo.

Maandiko Matakatifu ZaidiWagalatia 3:27–29 (tunajichukulia juu yetu jina la Kristo wakati wa ubatizo)

1 Petro 3:21 (ubatizo ni lazima ili kupata wokovu)

M&M 27:2 (tunapokea sakramenti kwa ukumbusho wa Kristo)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 20, “Ubatizo” katika kitabu cha Kanuni za Injili2. Soma somo la 28 na 31 katika kitabu hiki.

3. Pata ubao na chaki au tengeneza karatsi kubwa yenye maagano ya ubatizo na ushaurikatika Moroni 6:4–9.

4. Kwa hiari: chagua mshiriki wa darasa kufananisha maagano ya ubatizo na yale yasakramenti.

5. Chagua washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

213

Somo la 29

Page 223: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kipawa cha Roho Mtakatifu

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa baraka kubwazinazoweza kuja kwetu kwa njia ya kipawa cha Roho Mtakatifu.

UtanguliziNyakati fulani fulani kabla ya kujiunga na Kanisa, yawezekana kuwa RohoMtakatifu alikuja kwetu. Hisia nzuri tulizokuwa nazo wakati tulipowasikilizawamisionari kwa mfano alikuwa ni Roho Mtakatifu akitusaidia kuelewa nakukubali injili. Lakini hatukuwa na haki ya kuambatana na Roho Mtakatifuwakati wote hadi baada ya kubatizwa na kuthibitishwa. Wakati huo, kupitianguvu ya ukuhani wa Melkizedeki, tulipewa kipawa cha Roho Mtakatifu kwakuwekelewa mikono.

Raisi Lorenzo Snow alitushauri: “Inatupasa kujifunza juu ya huyu roho ilikuelewa vidokezo vyake na ndipo wakati wote tutaweza kufanya sawasawa . . . Kutoka wakati tunapopokea [kipawa cha Roho Mtakatifu] tunayerafiki, kama hatutamfukuza kutoka kwetu kwa kufanya mabaya. Rafiki huyoni Roho Mtakatifu.” (Conference Report, Apr. 1899, p. 52.)

Onyesha picha 30-a, “Kipawa cha Roho Mtakatifu ni haki ya kuwa naye Roho Mtakatifu kamarafiki wakati wote.”

Ni kwa namna gani Roho Mtakatifu ni kama rafiki? Washiriki wa darasa wasome Yohana14:16, 17, 26 and Yohana 16:13.

Kwa nini tunamhitaji Roho Mtakatifu kuambatana nasi wakati wote kama rafiki? (Andika majibuubaoni.)

Baadhi ya njia zingine ambazo Roho Mtakatifu anatusaidia ni:

• Anatufunulia ukweli.

• Anatusaidia kufundisha injili.

• Anatusaidia kukumbuka vitu.

• Anatufariji wakati wa huzuni.

• Anatulinda kutokana na uovu.

• Anatusaidia kufundisha injili katika mahubiri na masomo.

• Anatutahadharisha wakati tukiwa katika hatari.

• Anatuelezea mambo yote tunayopaswa kufanya.

Soma 2 Nefi 32:5.

214

30-a, Kipawa cha Roho Mtakatifu ni haki ya kuwa na Roho Mtakatifu wakati wote

Somo la 30

Page 224: Wajibu na Baraka za Ukuhani

30-a

Page 225: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mzee Le Grand Richards alisema yafuatayo: “Ningependa wanangu nawana wa wanangu kufurahia kuambatana na Roho Mtakatifu kuliko kuwapamoja na kitu kingine cho chote katika dunia hii kwa sababu kamawatafuata maongozi ya Roho, atawaongoza katika ukweli wote nakuwaona wakirudi salama kwa Baba yao aliye Mbinguni.” (ImprovementEra, June 1966, p. 540.)

Kwa sababu Roho Mtakatifu ni rafiki ambaye tunatamani kuwa naye,yatupasa kufanya kila tuwezalo ili kuwa naye kama rafiki anayeambatananasi wakati wote.

Utunzo wa Roho Mtakatifu Kuwa NasiKuna vitu vingi tunavyoweza kufanya ili kuwa na Roho Mtakatifu. Njia mojawapo ni kupokea sakramenti kama kistahilifu. Kila wakati tunapopokeasakramenti, tunaahidi kuwa tutatii amri za Bwana. Tukiweka ahadi zetu,Bwana ametuahidi sisi kuwa tunaweza kuwa na Roho wake “wakati wote.”(Tazama M&M 20:77.)

Njia nyingine ya kuwa na Roho Mtakatifu pamoja nasi ni kuiweka miili yetukuwa safi. Bwana anatueleza kuwa miili yetu ni kama hekalu ambalo nilazima tusilichafue (tazama 1 Wakorintho 3:16–17). Roho Mtakatifu hawezikuishi katika mahekalu machafu, kwa hivyo, ni kitu cha muhimu kuwekamiili yetu kuwa safi na pia kuwa na usafi wa mawazo, matamshi, mavazi navitendo, na kuepukana na mfano wowote wa uovu. Mzee Melvin J. Ballardalisema: “Roho Mtakatifu ni roho mwepesi zaidi ambayo nimeweza kuijua”(1967–68 Priesthood Study Course, Deacons Jamii, p. 70.) Kwa sababuRoho Mtakatifu ni mwepesi, anaweza kukasirishwa na vitu ambavyotunafikiria kuwa siyo vya maana.

Ili kuwa na Roho Mtakatifu, ni lazima tuishi kwa amani na wale ambao waliokaribu nasi. Akiongea na Wanefi, Kristo alisema kuwa roho ya mabishanohutoka kwa ibilisi (tazama 3 Nefi 11:29). Roho Mtakatifu hawezi kuwa katikamahali ambapo hakuna umoja na amani. Kwa maana hii, mabishano nawake zetu au kubishana na ndugu au dada kunafukuza Roho Mtakatifumbali nasi na nyumba zetu pia.

Kwa mfano, Nabii Joseph Smith hangeweza kupata maongozi kutoka kwaBwana isipokuwa ameweza kuwa na hisia nzuri kwa kila mtu. Asubuhi mojaalikasirishwa na kitu fulani ambacho mke wake alikuwa amefanya.Baadaye wakati alipojaribu kutafsiri sehemu ya Kitabu cha Mormonialishindwa. Kwa kujali, alienda kwenye bustani ya matunda na kuomba,halafu akaenda nyumbani kwake na kumuomba Emma msamaha. Hapondipo aliweza kutafsiri. (Kutoka na maelezo ya David Whitmer aliyoyatoaSeptember 15, 1882, Comprehensive History of the Church Vol. 1, p. 131.)

Uhitaji wetu wa Roho Mtakatifu ni mkubwa kama vile Nabii alivyomhitaji.Tunamhitaji Roho Mtakatifu kutuongoza katika majukumu yetu na hasa

216

Page 226: Wajibu na Baraka za Ukuhani

katika kuziongoza familia zetu. Wakati watoto wanafanya makosa haifaikupandwa na hasira ila inatubidi kumwomba Roho Mtakatifu atuongozekatika kuwarekebisha (tazama M&M 121:43).

Ni mambo gani mengine ambayo sisi hufanya ambayo humzuia Roho Mtakatifu kuwa nasidaima? Ni nini tunaweza kufanya ili kuwa naye pamoja nasi? (Andika majibu katika orodhambili kwenye ubao.)

Raisi Joseph Fielding Smith alisema: “Roho Mtakatifu hawezi kukaa ndaniya mtu ambaye hataki kutii na kufuata amri za Mungu . . . Katika nafsikama hiyo Roho Mtakatifu hawezi kuingia.

“Kipawa hiki kikuu huja kwetu kwa njia ya unyenyekevu imani na utiifu . . .Je! umeshawahi kutafakari kwa kina upendeleo huu mkubwa tulio nao wakuwa na mmoja wa washirika wa Mungu? Umeshawahi kufikiria kwa namnahiyo? Hiyo ndiyo fursa tuliyo nayo, kama tutazishika amri ambazo Bwanaametupa.” (Church News, Nov. 4, 1961, p. 14.)

Njia Ambazo Roho Mtakatifu HutusaidiaTukionyesha kwa uaminifu wetu kuwa tunatamani kuambatana na RohoMtakatifu, atatusaidia kwa njia zifuatazo kuishi maisha yenye furaha namema zaidi.

ANATUSAIDIA KUWA WATU WEMA

Roho Mtakatifu “anaongoza maadili, wema, uzuri, huruma, utulivu, naupendo.” (Parley P. Pratt, Key to the Science of Theology, p. 101.)

ANATUONYESHA CHA KUFANYA

Roho Mtakatifu anaweza kutusaidia kufanya maamuzi ya maana.

Soma M&M 6:15 na M&M 8:2 Je! Roho Mtakatifu anatusaidiaje kufanya uamuzi?

ANATUSAIDIA KUKUA KATIKA KANISA

Mzee Franklin D. Richards alieleza jinsi Roho Mtakatifu alivyomwongoza:“Nilisikia sauti ndogo na tulivu au mnong’ono wa Roho, kama vileninavyoshauriana nanyi ndugu na dada zangu, kama vile nilivyowapaukuhani wanaume; kama jinsi nilivyowatawaza wanaume na wanawakekatika nafasi fulani za Kanisa; kama namna nilivyowabariki wagonjwa, kamanamna nilivyotoa ushuhuda wangu kwa waumini na wale wasio waumin;kama vile nilivyokuwa nikitoa mahubiri, na kwa mara nyingine nyingi.” (“TheContinuing Power of the Holy Ghost,” Ensign, July 1973, p. 117.)

ANATUONYA

Kuna wakati ambao Roho Mtakatifu anatuonya juu ya hatari au majaribu.Mzee Franklin D. Richards alitueleza kuhusu baba mmoja ambaye“aliamshwa usiku mmoja kwa sauti ambayo ilimwambia kwa uwazi kabisakuwa atoke kitandani na kwenda chini ya ghorofa lile. Alitii onyo hilo naalipoenda jikoni aliona kwamba ukuta mmoja unawaka moto. Kwa harakaaliamsha familia yake na kuwaita wazima moto na kwa msaada wa familia

217

Somo la 30

Page 227: Wajibu na Baraka za Ukuhani

yake waliweza kupambana na moto huo hadi wazima moto walipokuja nakuuzima kabisa.

“Hakukuwa na swali katika fikira zake kuwa onyo hilo ni dhihirisho la ulinziambao Roho Mtakatifu huwapatia watu ambao wanayaweka maisha yaokulingana na matakwa ya Roho.” (Ensign, July 1973, p. 117.)

Uliza mshiriki aliyechaguliwa mapema kuelezea juu ya tukio ambalo alionywa na RohoMtakatifu kutoka na majaribu au hatari.

ANAWEZA KUTUFARIJI

Kazi moja wapo ya Roho Mtakatifu ni kutufariji wakati ambao tuna uchunguau huzuni. Wakati kama huo, Roho Mtakatifu anaweza kutusaidia kupataamani na mapatano. Mzee Franklin D. Richards alielezea juu ya tukiolifuatalo. “Ilikuwa heshima kubwa kukutana na wanawake wawili, waliomarafiki wa karibu, ambao walikuwa wamepoteza waume wao katika ajaliya ndege. Wadhani niliwakuta wamekata tamaa au katika huzuni kubwa?La, hasha. Sijawahi kushuhudia ujasiri zaidi na nguvu kubwa. Walitoaushuhuda kuwa kwa kweli walihisi faraja ya Roho, kwamba—walikuwa nauhakika kuwa mambo yote yatakuwa sawa kwao na kwa familia zaowakiwa wataishi karibu na Kanisa na wakizishika amri za Bwana.” (Ensign,July 1973, p. 117.)

Mshiriki wa darasa aliyeteuliwa awali aeleze hadithi ifuatayo.

Raisi Heber J. Grant alielezea namna Roho Mtakatifu alivyoleta maarifa nafaraja kwa watu wa familia yake:

“Saa moja kabla ya mke wangu kufa niliwaita watoto wangu katika chumbachake na kuwaelezea kuwa mama yao alikuwa akikaribia kufariki na kwahivyo ni vizuri wakimpa mkono wa kwaheri. Mmoja kati ya wasichanawadogo wa karibu miaka kumi na miwili alinieleza: “Baba, sitaki mamayangu afe. Nimekuwa nawe katika hospitali . . . kwa miezi sita; . . . [kilawakati] mama alipohangaika ulimbariki na uchungu uliondoka na kwaupole alienda kulala. Nataka wewe umwekelee mikono mama yangu naumponye.”

“Nilimwambia msichana wangu mdogo kuwa sisi zote tutakufa kwa wakatitofauti na nilikuwa na uhakika katika moyo wangu kuwa wakati wa mamayao ulikuwa umefika. Yeye na watoto wengine walitoka nje ya chumba.

alikuwa amepoteza fahamu) na nilimwambia Bwana kuwa nilikubali mkonowake katika maisha, katika kifo, katika furaha, katika huzuni, katika kustawiau shida. Nilimshukuru kwa ufahamu niliokuwa nao kuwa mke wangualikuwa wangu milele . . . Lakini nilimwelezea Bwana kuwa sikuwa nanguvu za kustahimili mke wangu afe na kuishawishi imani ya watoto wanguwadogo . . . na nilimwomba Bwana kwa nguvu zote ambazo nilikuwa nazokuwa ampe msichana wangu mdogo ufahamu kwamba yalikuwa nimapenzi yake mama yake afariki.

218

Page 228: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Baada ya saa moja mke wangu alifariki na nikawaita tena watotochumbani. Mwanangu mvulana aliyekuwa karibu miaka mitano na nusu ausita alikuwa akilia kwa uchungu na yule msichana mdogo ambaye alikuwana miaka kumi na miwili alimkumbatia na kusema, ‘wacha kulia na kutoamachozi Heber; kwa sababu kutoka wakati tulipotoka nje ya chumba hikisauti ya Bwana kutoka mbinguni imeniambia,’ ‘kwa kifo cha mama yako,mapenzi ya Bwana yamefanyika.” ‘ . . .

“Najua . . . kuwa Mungu anasikiliza na kujibu maombi! [Najua] kuwa wakatiwa majaribu Watakatifu wa Siku za Mwisho wanafarijiwa na kubarikiwa nakutulizwa kushinda watu wengine wote.” (Gospel Standards, p. 361.)

ANASHUHUDIA UKWELI

Ni kupitia kwa Roho mtakatifu ndio tunapata ushuhuda wa injili. Kwa njiahiyo hiyo, Roho Mtakatifu ndiye atatusaidia sisi kujua wakati viongozi wetuwanapoongea kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Mzee Henry D. Moylealifundisha: “Tunaweza kujua wakati wale wanaoongea wanaongozwa naRoho Mtakatifu iwapo tu sisi wenyewe tunaongozwa na Roho Mtakatifu.Kwa hivyo, ni kitu cha muhimu kwamba waumini wa Kanisa wawe na bidiikatika imani yao kama viongozi wao.” (“Revelation: Yesterday and Today,”Improvement Era, June 1962, p. 407.)

Baraka za Roho Mtakatifu ni za kweli na zipo kwa ajili yetu kama sisiwaumini wa Kanisa tukizitafuta kwa haki.

Mkaribishe aliyechaguliwa mapema miogoni mwa washiriki wa darasa kuelezea tukio ambaloalihisi kuwa pamoja na Roho Mtakatifu.

MwishoKipawa cha Roho Mtakatifu ni baraka kuu wanayopewa watu ambaowamethibitishwa kuwa waumini wa Kanisa. Tukiishi maisha yanayostahiliyeye kuwa nasi, atatusaidia kumaliza kwa fanaka misheni yetu hapaduniani. Atafanya haya kwa kutuongoza sisi, kutulinda, kutufariji nakutusaidia katika maeneo yote ya maisha yetu.

ChangamotoTafuta kuambatana pamoja na Roho Mtakatifu katika maisha yako ya kilasiku. Ili kujua maeneo ambayo unatakiwa kujirekebisha ili kuwa na RohoMtakatifu pamoja nawe wakati wote, jiulize maswali yafuatayo:

Je! mimi hujaribu kutii amri zote?

Je! mimi huomba kila mara?

Je! ninaonyeshaje upendo wangu kwa Mwokozi?

Je! ninaonyeshaje upendo wangu kwa wengine?

Je! mawazo na matendo yangu ni safi?

Je! ninamshukuru Bwana kwa baraka zake, pamoja na kipawa cha RohoMtakatifu?

219

Somo la 30

Page 229: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Maandiko Matakatifu ZaidiMatendo ya Mitume 5:32 (Roho Mtakatifu anakuja kwa wale walio watiifu)

1 Nefi 10:17–19 (nguvu na elimu kutoka kwa Roho Mtakatifu huja kwaimani katika Kristo)

2 Nefi 31:13 (Roho Mtakatifu hupatikana baada ya imani, toba, na ubatizo)

Musa 6:61 (nguvu na baraka za Roho Mtakatifu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 21, “Kipawa cha Roho Mtakatifu,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Kumbusha washiriki wa darasa kuleta vitabu vya Maandishi Matakatifu darasani.

3. Kama huwezi kupata chaki na ubao, tengeneza karatasi kubwa yenye orodha yayaliyodokezwa.

4. Chagua washiriki wa darasa watakaotoa hadithi na Maandiko Matakatifu kwenye somo hili.

220

Page 230: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Maombi na Kufunga

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujifunza jinsi ya kuziimarishafamilia zetu na vikundi kwa njia ya maombi na kufunga.

UtanguliziWacha washiriki wa darasa waliochaguliwa kuelezea kwa kifupi kanuni za kufunga na maombikama inavyofundishwa katika kitabu cha Kanuni za Injili.

Kusali na Kufunga Hutuimarisha sisi na Familia ZetuKusali na kufunga kunaweza kutusaidia kujiimarisha sisi na familia zetu.Sala zetu ili kupata mwongozo zinatiwa nguvu zaidi kwa sababu kufungakunatilia mkazo umuhimu wa sala. Zaidi ya hayo, tunapofunga na kuomba,tunaacha mambo ya dunia na kutambua kumtegemea kwetu Bwana. Kwanjia hii, tunafungua mioyo yetu kwa kujifunza na kukubali mapenzi yaMungu juu yetu na juu ya familia zetu.

Maombi na kufunga pia huongeza uwezo wetu wa kutumia ukuhani kwanjia inayofaa. Sisi pamoja na wengine hubarikiwa wakati tunapojifunzanamna ya kudhibiti nguvu za ukuhani na ukuhani unaweza kudhibitiwa tutunapotumia kanuni za haki. (Tazama M&M 121: 34–36.)

Onyesha picha 31-a, “Kufunga na kusali kunaweza kumsaidia mwenye ukuhani kubarikiwagonjwa.”

Hadithi ifuatayo inatueleza jinsi mwenye ukuhani mmoja alivyojifunza juu yanguvu ya kufunga na kusali katika kumsaidia yeye kutumia ukuhani wake:

Wakati John na mvulana mdogo wa Bonnie walipokuwa wagonjwamahututi, madaktari kwa uchunguzi wao walisema kuwa ni ugonjwa wa utiwa mgongo. Waliwambia wazazi wao kuwa mtoto huyo atafariki au kuwamlemavu wa mwili na akili. Kama mwenye Ukuhani wa Melkizedeki, Johnaliamua kupatia mwanawe baraka. Alipokuwa akijitayarisha kufungampako wa mafuta, alitambua kuwa hakujua mapenzi ya Bwana kwamwanawe. Na hivyo alimbariki mwana huyo ili aweze kufarijiwa.

Baada ya baraka hiyo, John na Bonnie walianza kufunga ili kujua mapenziya Bwana na kuweza kuyakubali. Mwisho wa mfungo wao, John na Bonniewalikuwa katika hali ya kuweza kukubali mapenzi ya Bwana. Johnalimbariki tena mwanawe. Wakati huu Roho alimnong’oneza kuwa ambarikimwanawe kuwa apate kupona kabisa. Mwana wao aliponywa, na baada yasiku tatu walimrudisha nyumbani kutoka hospitali.

Ni jinsi gani kufunga kuliwasaidia John na Bonnie kama jibu la sala yao lingekuwa tofauti?

221

Somo la 31

Page 231: Wajibu na Baraka za Ukuhani

31-a

Page 232: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kufundisha na Kuimarisha Familia Zetu Kwa Njia ya Sala naKufungaKama wazazi, inatupasa kuomba kila wakati ili kujua mahitaji ya watotowetu na jinsi ya kukabiliana na mahitaji hayo. Kama mmoja wa watotowetu ana shida fulani, kwa mfano, tunaweza kumwombea katika sala yafamilia. Inatupasa kuwa waangalifu, hata hivyo, kufanya hivyo kwa njianzuri. Baba mmoja alimwombea kijana wake kwa maneno haya: “Babayetu uliye [Mbinguni], tunajua kwamba John anajitahidi kuzuia hasirazake. Tunakushukuru kumwona akikua na kwa kumbariki mtoto wetu.Tafadhali uendelee kumbariki na sisi utubariki ili tusimkasirishe mwanawetu ila tuonyeshe upendo wetu na mapenzi yetu kwa kumsaidia.”(Ensign, May 1973, p. 34.)

Ni kwa namna gani maombi kama haya yanaweza kumsaidia mvulana kuyashinda matatizozake?

Mzee M. Russell Ballard, Jr. alielezea tukio la mwanawe wa miaka mitanoambaye aliogopa kuanza shule. Alipotambua kuwa mwanawe alikuwaanaogopa, alisema, “Craig, unaye rafiki ambaye atakuwa nawe wakatiwote. Wacha tupige magoti pamoja na tumwombe yeye akusaidie.”(Ensign, Nov. 1976, pp. 87–88.)

Kufunga na kusali kama familia kunaweza kuleta nguvu zaidi na umojandani ya familia kama vile hadithi ifuatayo inavyotuelezea:

Alan alikuwa mvulana ambaye alikuwa amepata mwito wa kumtumikiaBwana misheni katika nchi ya kigeni. Alikuwa na shauku ya kuhudumulakini alipojaribu kujifunza lugha hiyo, alitia shaka kwani hakuwezakujifunza lugha hiyo.

Mara babake Alan alipogundua shida ya mtoto wake, aliita familia yakepamoja. Aliwaomba kufunga na kuomba ili Alan aweze kushinda shida hiyona kwamba aweze kumaliza misheni yenye mafanikio.

Ni kwa namna gani tukio kama hilo linaweza kuwaimarisha watoto wetu? Ni kwa namna ganikufunga na kuomba kwa pamoja kuna iunganisha familia? Soma 3 Nefi 18:21.

Kukamilisha Kazi ya Bwana Kupitia Kuomba na KufungaMtu mmoja alikuja kwa Yesu, na kupiga magoti mbele yake na kusema:

“Bwana umrehemu mwanangu: kwa kuwa ana kifafa na akili na kuteswavibaya. Maana mara nyingi anaanguka katika moto, na ndani ya maji. Nanilimleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponya.”

Bwana mara moja alimfukuza ibilisi kutoka kwa mvulana huyo. Wanafunziwakaja kwa Yesu na kumwuliza. “Mbona sisi hatukuweza kumtoa?” Yesuakawaambia ni kwa sababu ya kutokuamini kwao, na tena akaongeza, “lakininamna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga” (tazama Matayo 17:14–21).

223

Somo la 31

31-a, Kuomba na kufunga kunaweza kusaidia mwenye ukuhani kubariki wagonjwa kwa mafanikio makubwa

Page 233: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Katika hadithi ifuatayo Mzee Mathew Cowley anaelezea juu ya askofuambaye alielewa umuhimu wa sala na kufunga:

“[Askofu mmoja kijana tajiri huko Honolulu] aliitwa siku moja kutokaHospitali ya Queens ili kuja kumbariki mtoto ambaye alikuwa na ugonjwawa polio. Dada mmoja aliwahi kumwita. Yeye alikuwa askofu wake naakasema, ‘Askofu, njoo haraka, mwanangu ana ugonjwa wa polio nanataka uje hapa ili umhudumie na umbariki.” Siku nzima alimngojea, lakiniaskofu hakufika. Usiku mzima pia hakufika. Asubuhi iliyofuata piahakuonekana, lakini mapema alasiri alikuja. Mwanamke huyoalimgombeza. Alimwita majina yote ambayo aliweza kufikiria. ‘Wewe,askofu wangu, ninakupigia simu kuwa mwanangu yuko na polio. Na wewendiye tajiri wako mwenyewe, una magari na chombo cha kupendeza chabaharini; Una kila kitu unachotaka na wakati wako ni wako tu na hukuwezakuja. Unakuja sasa baada ya siku moja.’ Na baada ya kumaliza nahakuweza kufikiria kitu kingine chochote cha kumwita, Askofu alitabasamuna kusema, ‘Kweli, baada ya kuweka simu chini jana, nilianza kufunga nanilikuwa nikifunga na kuomba kwa masaa ishirini na manne. Sasa nikotayari kumbariki mtoto wako.’ Saa kumi na moja jioni mtoto huyoaliondolewa hospitali akiwa amepona kabisa kutokana na polio. “(Lakini)namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.”

“Sasa natia shaka sana kama angeenda kule siku iliyopita kamakingelitokea. Nafikiri kuwa sala na mfungo vilihitajika. Kwa hivyo nafikirikuwa sisi ambao tuna ukuhani wakati mwingine hatuutumii vya kutosha.Lazima kushika masharti nzuri, lazima tuendelee kujifunza na huu ukuhaniambao tunao, ndipo daima tutakuwa tayari kuhudumu katika afisi zaukuhani kutoa baraka.” (Mathew Cowley Speaks, p. 150.)

Siyo lazima daima kungojea wakati huo wote kabla ya kumbariki mgonjwa,lakini daima inatupasa kupata maongozi kutoka kwa Bwana kabla yakufanya ibada ya ukuhani.

Kwa nini ni muhimu sisi kuwa tayari kiroho wakati tunapofanya ibada za ukuhani?

Kama vile mwenye ukuhani anavyohitaji kujitayarisha ili kufanya ibada, waleambao wanataka baraka pia yawapasa kujitayarisha wenyewe na familiazao kufanyiwa ibada hiyo. Hadithi ifuatayo inatuelezea jinsi wazazi wamtoto walitumia sala na mfungo kujitayarisha pamoja na mwana wao kwaajili ya baraka.

“Yapata kama mwaka mmoja hivi, mume na mke walikuja katika afisiyangu wakiwa wamembeba mtoto mdogo. Baba yake aliniambia, ‘Mimi namke wangu tumekuwa tukifunga kwa siku mbili, na tumemleta mtoto wetumdogo ili umpe baraka. Tumetumwa kwako.’

“Nikasema, ‘Ni shida gani aliyonayo?

“Walisema alikuwa amezaliwa kipofu, kiziwi na bubu, misuli yake haifanyikazi, hakuweza hata kutambaa wakati akiwa na miaka mitano. Nilijiambia, hii

224

Page 234: Wajibu na Baraka za Ukuhani

ndiyo hiyo. “(Lakini) namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.” Nilikuwa naimani kamili kwa kufunga na maombi ya wazazi hao. Nilimbariki mtoto huyo,na baada ya wiki kadha nilipokea barua: “Ndugu Cowley, tungependaumwone mtoto wetu mdogo sasa. Anatambaa. Tukitupa mpira katika sakafuanatambaa kwa kasi ili kuuchukua, anaweza kuona. Tunapopiga makofi juuya kichwa chake yeye huruka. Anaweza kusikia. Utabibu wa sayansi ulikuwahaukuweza kuondoa mzigo. Mungu ameuchukua.” (Mathew Cowley,“Miracles,” Speeches of the Year, BYU, 1953, p. 8.)

Wamisionari wengi wametambua baraka zinazotokana na maombi nakufunga kwa pamoja. Raisi Ezra Taft Benson alielezea tukio alilolipataakiwa mmisionari walipokuwa wakifunga na kuomba pamoja na mwenziwe.

“Kutoka na uzoefu wa kibinafsi, najua manufaa ya nguvu ya maombi.Wakati nilipokuwa mmisionari kijana kaskazini mwa Uingereza mwaka wa1922, upinzani dhidi ya Kanisa ulikuwa mkubwa sana. Upinzani ulikuwawenye nguvu mno hadi Raisi wa Misheni akaomba kusimamisha mikutanoyote mitaani, na mahali pengine huduma ya nyumba hadi nyumbailisimamishwa.

“Mimi na mwenzangu tulikuwa tumealikwa kusafiri hadi kusini mwa Shieldskuzungumza katika mkutano wa sakramenti. Katika karibisho hilo walisema,‘Tunahisi kuwa tunaweza kujaza kanisa hili dogo. Wengi wa watu ambaowanakaa hapa hawaamini uongo ambao umeandikwa juu yetu. Kamamtakuja, kwa kweli tutakuwa na mkutano wenye mafanikio.’ Tulikubali.

“Tulifunga na kuomba kwa dhati na tukaenda kwa mkutano huo.Mwenzangu alikuwa amepanga kuongea juu ya kanuni za kwanza.Nilikuwa nimesoma na tayari kuzumgumzia juu ya uasi. Kulikuwa na rohonzuri katika mkutano huo. Mwenzangu aliongea kwanza na kutoa manenoya kuvutia. Nilijibu na kuongea kwa uhuru ambao bado haukuwahi kutokeakatika maisha yangu. Wakati nilipokaa chini ndipo nilipokumbuka kuwanilikuwa sijasema chochote juu ya uasi. Nilikuwa nimeongea juu ya NabiiJoseph Smith na kutoa ushuhuda wangu kuhusu ujumbe wake na ukweliwa Kitabu cha Mormon. Mkutano huo ulipokwisha, watu kadhaa walikujambele, wengine wao siyo waumini na kusema, ‘Usiku huu tumepataushuhuda kuwa injili ni ya kweli kama ninyi wazee mnavyoifundisha. Sasatuko tayari kwa ubatizo.’

“Hili lilikuwa jibu kwa maombi na kufunga kwetu, kwani tuliomba tusememambo yale tu ambayo yatagusa mioyo ya rafiki zetu na wachunguzi waKanisa.” (“Prayer”, Ensign, May 1977, pp. 33–34.)

Mwisho Kuna wakati mwingi ambapo mfungo na sala vinaweza kutusaidia kutimizakazi ya Bwana. Kwa mfano, tunaweza kufunga na kuombea familiaambazo tunazifundisha nyumbani. Tunaweza pia kuomba na kufunga kwaajili ya mmoja kati ya washiriki wa baraza la ukuhani au familia yake.

225

Somo la 31

Page 235: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Kupitia sala na mfungo, tunaweza kubarikiwa kimwili na kuongeza imani nanguvu za kiroho. Nguvu kama hizo zinahitajika kama tunataka kufanikiwakatika kazi zetu na kujiimarisha sisi wenyewe na wengine.

Changamoto1. Tambua mambo ambayo unahitaji kufunga na kuomba juu yake katika

maisha yako mwenyewe na familia yako.

2. Fikiria juu ya mahitaji fulani ya washiriki wenzako katika Jamii yaUkuhani.

3. Jitahidi kuomba na kufunga kwa ajili ya moja kati ya malengo haya.

Maandiko Matakatifu Zaidi

MAOMBI

Matayo 6:5–15 (mwokozi anaelezea namna ya kuomba)

Luka 18:1–14 (yatupasa kuomba bila kuchoka)

2 Nefi 32:8–9 (yatupasa kuomba kabla ya kufanya kazi ya Bwana)

Alma 34:17–28 (yatupasa kuomba juu ya kila kitu ambacho tunafanya)

Moroni 10:3–5 (tunaweza kujua ukweli wa mambo yote kwa kupitiamaombi)

M&M 19:28 (yatupasa kuimarisha nyumba ya maombi na kufunga)

M&M 88:119 (yatupasa kuomba hadharani na sirini)

KUFUNGA

Kutoka 34:27–28 (Musa alifunga kabla ya kupata ufunuo kutoka kwaMungu)

Luka 2:36–37 (Anna alimtumikia Mungu kwa kuomba na kufunga)

Matendo ya Mitume 13:2–3 (kufunga kunaweza kuleta mwongozo wa RohoMtakatifu)

Mosiah 27:23 (maombi na kufunga yalimsaidia Alma kupona)

Alma 6:6 (wanefi walifunga na kuomba kwa ajili ya wale ambaohawakumjua Mungu)

Alma 17:9 (wamisionari waliomba na kufunga ili wawe na Roho)

Alma 45:1 (kufunga na kuomba ndiyo njia mojawapo ya kumwonyeshaMungu shukrani)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili.

1. Soma somo la 8, “Maombi kwa Baba yetu aliye Mbinguni,” katika kitabu cha Kanuni zaInjili. Chagua mshiriki wa darasa kuelezea kwa kifupi kwa dakika tatu somo hilo.

2. Soma somo la 25, “Kufunga,” katika kitabu cha Kanuni za Injili. Chagua mshiriki wa darasakuelezea kwa kifupi kwa dakika tatu somo hilo.

226

Page 236: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Unyenyekevu

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujifunza jinsi ya kufundishaunyenyekevu kwa familia zetu na kuboresha unyenyekevu wetu sisi wenyewe.

UtanguliziOnyesha picha 32-a, “Unyenyekevu katika kanisa huonyesha upendo na heshima kwaMungu.”

Andika maneno ya maneno ya Walawi 19:30: “Zishikeni Sabato Zangu, mpaheshimupatakatifu pangu; mimi ndimi Bwana Mungu wenu.”

Yafuatayo yaliandikwa na Raisi Spencer W. Kimball. Yalichapishwa mwakawa 1976 kama kitabu maluum kilichoitwa We Should Be a Reverent People.

Sisi ni watu ambao tumebarikiwa sana. Bwana ametupatia injili ya YesuKristo, nguvu ya ukuhani, ahadi za ubatizo, maagano ya hekaluni, ukweliwa maandiko matakatifu, familia zetu, mali zetu za duniani. Tunafaa kuwawatu wenye furaha kabisa hapa duniani. Inatupasa kuwa watu wenyefuraha zaidi hapa duniani. Wengi wetu, hata hivyo huwa na matatizo yakuwa watu wanyenyekevu zaidi. Inatupasa kujiuliza sisi wenyewe kamamatendo yetu katika nyumba zetu, na katika Kanisa yanaonyeshaunyenyekevu kwa Muumba wetu.

Unyenyekevu ni Nini?Unyenyekevu ni hisia ya kuonyesha heshima, upendo na kujitolea kwa Mungu.Wengi wa viongozi wetu wa Kanisa wamesema kuwa unyenyekevu ni tabia ya hali juu kabisa ya nafsi, kwani inahusisha imani ya kweli katika Mungu,utamaduni wa hali ya juu, na upendo kwa vitu vizuri zaidi katika maisha.

Kama vile kanuni nyingine za injili, unyenyekevu unatuongoza kwenyefuraha. Siyo kuhuzunika, tabia za muda tunazokuwa nazo Jumapili, bali ni matokeo ya kufuata injili kila siku. Unyenyekevu wa kweli huleta furaha,upendo, heshima na shukrani. Ni maadili ambayo yanapaswa kuwasehemu ya maisha yetu.

Unyenyekevu kwa MunguKupitia ufunuo wa kisasa, Bwana ametusaidia sisi kuelewa maana naumuhimu wa unyenyekevu. Katika Mafundisho na Maagano, sehemu ya 76,kwa mfano, Joseph Smith na Sidney Rigdon wanafafanua unyenyekevukuwa ni hali ya tabia muhimu ya wale ambao watapata Ufalme wa Mbinguni:

“Na hivyo tukaona utukufu wa mbinguni, ambao ulizidi vitu vyote—ambapoMungu, aliye Baba, hutawala katika kiti chake cha enzi milele na milele;

227

Somo la 32

Page 237: Wajibu na Baraka za Ukuhani

32-a

Page 238: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Mbele ya kiti chake cha enzi vitu vyote hupiga magoti kwa unyenyekevuna kumpatia utukufu milele na milele.

“Wao ambao huishi katika uwepo wake ni wale wa Kanisa la Mwana WaKwanza; na wanavyoona kama wanaonekana na kujua vilewanavyojulikana, wakiwa wamepokea ukamilifu wake na rehema zake.

“Na huwafanya kuwa sawa katika uwezo, nguvu na utawala” (M&M76:92–95).

Ufunuo mwingine wa kisasa unatuongoza kushikilia kwa unyenyekevu hatajina lenyewe la Mungu; tunaambiwa tusilitaje bure jina la Baba na Mwana nahata kuepuka na kuyataja kila wakati (tazama M&M 107:2–4). Moja ya amrikumi husomeka: “Usitaje bure jina la Bwana Mungu wako; maana Bwanahatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure” (Kutoka 20:7).

Heshima kwa Mungu na jina lake ni tabia moja muhimu ya unyenyekevu.Hata pia unyenyekevu katika nyumba yake takatifu. Katika ufunuo muhimualiopewa Joseph Smith unaojulikana kama maombi ya kuweka wakfu kwaHekalu la Kirtland, Bwana alimwelekeza kuwa hili, sawa na mahekalumengine matakatifu ambayo yamejengwa na Watakatifu, yanapaswa kuwamahali pa unyenyekevu kwake (tazama M&M 109:16–21).

Katika maana halisi, yale yanayosemwa kuhusu mahekalu matakatifu yaKanisa ni kweli pia kwa kila “nyumba ya Bwana,” hata kama mahali hapo nimahali watakatifu wanapoabudu au nyumba ya Mtakatifu wa Siku za Mwisho.

Unyenyekevu na NyumbaniNi wapi unyenyekevu huanzia na ni vipi tunaweza kuuendeleza? Sawa nakila tabia nzuri ya uungu, nyumbani ndiyo ufunguo wa unyenyekevu. Niwakati wa maombi ya kibinafsi na ya kifamilia watoto wanajifunzakuinamisha vichwa vyao, kukunja mikono yao na kufumba macho yaotunapoongea na Baba yetu aliye Mbinguni. Mtoto ambaye amejifunzakuomba nyumbani mara moja anaelewa kuwa ni lazima kunyamaza nakutulia wakati wa maombi katika mikutano ya Kanisa.

Vile vile, tunapokuwa na mkutano wa jioni ya familia nyumbani, watoto wetuwanajifunza kuwa kuna wakati maalum, siyo tu Kanisani, bali hatanyumbani, wakati kila mtu anahitajika kuwa na tabia nzuri kabisa.

Tunaweza pia kuwasaidia watoto wetu kujifunza unyenyekevu kupitianyimbo. Nyimbo ni furaha maalumu kwa watoto. Tukiimba nyimbo zaKanisa nyumbani, watoto wetu watazizoea na kuziimba wakati wa mikutanoya Kanisa. Hasa watoto wadogo watafaidika zaidi tukiwasaidia kujifunzanyimbo rahisi nyumbani. Kwa njia hii, watoto wetu watatazamia kuimbanyimbo hizo.

229

Somo la 32

32-a, Unyenyekevu katika kanisa unaonyesha upendo na heshima kwa Mungu

Page 239: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Unyenyekevu KanisaniKwa kawaida, kama wazazi, inatupasa kwenda kwenye mikutano yajumapili na watoto wetu. Katika kuwatayarisha watoto wetu kwendaKanisani, inatupasa kufanya kazi hiyo kwa pamoja na wake zetu ilikuhakikisha kuwa matayarisho hayo ni matukio muhimu kwa familia. Mbioza dakika za mwisho za kuwakusanya watoto pamoja, kuwavalisha nakukimbia kwenye mkutano kunaharibu unyenyekevu. Tunapoharakishakujitayarisha, mara nyingi tunachelewa kufika Kanisani na mara nyingi kunamaneno mabaya yanayotamkwa ambayo yanaumiza hisia ambazozinaweza kuwafanya watoto wetu kukasirika na kukosa kusikilizakinachoendelea katika mkutano. Tutahisi unyenyekevu zaidi tukijitayarishavizuri kabla ya wakati wa mikutano, na kufika kanisani kabla ya mikutanokuanza na kukaa pamoja ili kusikiliza nyimbo kabla ya mkutano kuanza. Nakuchukua wakati wetu kutafakari juu ya Mwokozi na injili yake.

Wale ambao tuna watoto wadogo wakati mwingine huwa na wakati mgumukuwanyamazisha watoto wetu mkutano unapoendelea. Mafundisho mazurinyumbani, hata hivyo, yanaweza kutatua tatizo hilo. Kamatunachanganyikiwa jinsi ya kukaa na watoto wetu kanisani, tunawezakutafuta mawaidha ya wale waliofanikiwa kunyamazisha watoto wao.

Mara kwa mara, kabla na baada ya mikutano, tunapenda kubaki kanisani ilikusalimiana. Haya yanaweza kufadhaisha, ingawa tunayafanya kwa hisiaza urafiki kwa wale ambao tunakutana nao siku ya Sabato tu. Hata hivyo,wazazi wanapaswa kuonyesha mfano mzuri kwa familia zao kwakusalimiana nje ya kanisa kabla na baada ya mikutano. Baada ya mkutano,inatupasa kusaidia kupeleka roho ya ibada katika nyumba zetu kwakuzungumza juu ya wazo la kanisani nyumbani, nambari ya nyimbo, au vituvizuri vilivyotokea katika mkutano na familia zetu.

Kuboresha UnyenyekevuTunawezaje kuwasaidia watoto wetu kufurahia mikutano ya kanisa na kuwa wanyenyekevuzaidi? Baada ya darasa kutoa majibu yao, pata mtu mmoja asome hoja zifuatazo:

Wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao kufurahia mikutano ya kanisakwa—

• Kuwa mfano mwema.

• Kufanya matayarisho kwa ajili ya mikutano kuwa mazuri na bila haraka.

• Kufika dakika tano au kumi kabla ya mkutano kuanza.

• Kukaa pamoja kama familia.

• Kuzungumza juu ya mahubiri, nambari ya wimbo, au sehemu nyingine yamkutano baadaye.

Tunawezaje kufundisha unyenyekevu kwa watoto wadogo? Baada ya washiriki wa darasakutoa majibu, pata mtu mmoja kusoma hoja zifuatazo:

Wazazi wenye watoto wadogo wanapaswa kujaribu—

230

Page 240: Wajibu na Baraka za Ukuhani

• Kuwasaidia watoto kuelewa kile kinachofanyika. Watoto wadogowanaweza kuwa wanajishugulisha wenyewe pole pole kwa kupaka vitaburangi au kazi ya kitabu, lakini ni muhimu kuwasaidia kuelewa juu yamikutano. Mara kwa mara kuwanong’onezea maneno ili kuelezayanayoendelea katika kata au mahubiri yanaweza kusaidia watotokuelewa kile kinachoendelea. Kwa mfano, baba anawezakuwanong’onezea, “Yule ni baba wa Gordy anayeongea sasa. Anaongeakuhusu waanzilishi.”

• Tilia mkazo nyimbo. Kuimba kunaweza kuwa moja wapo ya sehemu yafuraha katika mkutano kwa watoto. Tia moyo watoto kupenda nyimbokwa kuimba nyimbo rahisi nyumbani na kwa kuwafundisha nyimbo hizo.Anayeongoza nyimbo katika tawi anaweza kukupatia orodha ya nyimbozitakazoimbwa katika mkutano ujao.

• Imarisha tabia zilizofundishwa nyumbani, kwenye mafundisho ya msingina katika shule ya Jumapili. Saidia watoto kukumbuka kukunja mikonoyao na kuinamisha vichwa vyao wakati wa maombi na kukaa kwa utulivuwakati wa sakramenti. Watoto wanapaswa kuelewa kuwa haifai kuchezaau kutembea ndani na nje ya Kanisa wakati wa mkutano.

• Onyesha mfano. Onyesha mfano mwema kwa kuonyesha kupendezwana mkutano, kwa kuongea tu wakati unapolazimika na kwa kunong’onatu, na kutilia mkazo watoto kufanya hivyo.

• Hakikisha kuwa watoto wako tayari kwa mikutano. Kwenda chooni nakunywa maji yafaa kufanyika kabla ya mikutano kuanza.

Ni nini tunaweza kufanya ili kuboresha unyenyekevu katika darasa letu?

MwishoUnyenyekevu unaweza kuboreshwa tu kama viongozi wa matawi na familiawataunganisha jitihada zao ili kushinda matatizo yao ya ukosefu waunyenyekevu. Hoja na kupewa moyo kutoka makao makuu ya Kanisainaweza kutusaidia kujua jinsi ya kutatua matatizo yetu ya kukosaunyenyekevu, lakini kazi halisi inapaswa kufanyika katika tawi na katikanyumba zetu.

Unyenyekevu wa kweli ni muhimu kwetu ili tuwe karibu na Baba yetu aliyeMbinguni. Lakini kadiri nguvu za ibilisi zinavyotapakaa hapa duniani,unyenyekevu unaharibiwa. Hatujui mazuri ambayo tungeweza kufanya,kama sisi, waumini wa Kanisa la kweli la Kristo, tungeweza kutumika kamamfano wa tabia ya unyenyekevu. Kupitia mfano wetu, tunaweza kubadilishamaisha ya watu wengi, na hasa maisha ya watu wa familia zetu.

Changamoto1. Ongea na familia yako kuhusu yale mnayoweza kufanya ili kuongeza

unyenyekevu kanisani.

231

Somo la 32

Page 241: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2. Fanya moja kati ya hoja hizo kwa matendo Jumapili ijayo.

3. Kama una watoto wadogo amua kupanga kuwafundisha juu yaunyenyekevu nyumbani na kanisani.

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Kumbusha washiriki wa darasa kuleta vitabu vya maandiko matakatifu katika darasa.

2. Panga kupata ubao na chaki.

232

Page 242: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Upendo na Utumishi

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujifunza kuwa upendo nautumishi kwa wengine ni muhimu kwa mwito wetu wa ukuhani.

UtanguliziOnyesha picha 33-a, “Kristo ndiye mfano mkuu wa upendo.”

Yesu Kristo anawapenda watu wote. Uwezo wake wa kupenda nimkamilifu. Upendo wake ni timilifu hata Maandiko Matakatifu yanatuelezakuwa yeye ni upendo (1Yohana 4: 7–12). Upendo wa Kristo unaonekanakwa matendo ya utumishi aliyowafanyia wanadamu.

Kama wenye ukuhani, tunalo jukumu la kuwa kama Kristo. Lakini ili tuwezekufanya hivyo, ni lazima tujifunze kupenda jinsi anavyopenda na kutumikajinsi anavyotumika. Askofu H. Burke Peterson alitufundisha kuwa, “katikadunia na jumuiya ambayo ibilisi anaanzisha vita vikali kila wakati kwa watotowa wanadamu, hatuna zana kuu za vita kuliko upendo wa Kristo ulio safi nabila “choyo.” (“The Daily Portion of Love,” Ensign, May 1977, p. 69.)

Tumeamriwa KupendanaSiku moja Kristo alipokuwa akifundisha, mmoja kati ya waandishiakamwuliza ni amri gani iliyo ya kwanza katika zote. Yesu akajibu ‘MpendeBwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwaakili zako zote, na kwa nguvu zako zote: hii ndiyo amri ya kwanza.

Na ya pili ni sawa na hiyo: “Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakunaamri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.” (Marko 12:28–31.)

Kwa nini amri hizi mbili ni kuu kuliko amri zingine? (Tunapompenda Mungu na wanadamuwenzetu, tutafanya chochote tuwezacho ili kuwafanya kuwa na furaha, na hapo, tutafuata amrihizo nyingine.)

Sehemu kubwa ya maisha ya Mwokozi ilitumika kufundisha juu ya upendo.Wakati mwingine injili yake huitwa “injili ya upendo.” Alifundisha kuwatukiwapenda wenzetu tutakuwa wanafunzi wake (tazama Yohana 13:35.)Alileza pia kuwa tunapaswa kuwapenda hata maadui wetu (tazamaMathayo 5:43–44.) Saa chache kabla ya kusulubiwa kwake, Yesu alisema:“Amri mpya ninawapa, Mpendane; kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyimpendane vivyo hivyo (Yohana 13:34).

Raisi N. Eldon Tanner, akitia mkazo umuhimu wa amri ya upendo alisema,“Maneno tunayohitaji ili kuwa na furaha ni . . . Tupendane kila mmoja—maneno matatu rahisi.” (“The Great Commandment,” Improvement Era,June 1967, p. 29).

233

Somo la 33

Page 243: Wajibu na Baraka za Ukuhani

33-a

Page 244: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Upendo Halisi wa KristoWacha washiriki wa darasa wasome Moroni 7:45–47. Upendo ni nini?

Mzee Mark E. Peterson alielezea kuwa hisani ni “upendo halisi wa Kristoambao unatusaidia kumpenda Mungu na wanadamu wenzetu.” (“Do untoOthers,” Ensign, May 1977, p. 75.) Hadithi ifuatayo iliyoelezwa na MzeeMarion D. Hanks inaonyesha jinsi baba mmoja alivyomfundisha binti yakejinsi ya kukuza na kuonyesha upendo.

“Nafikiria juu ya mwanamke mmoja mpendwa aliyekuwa na ulemavu wamwili. Aliongea kuhusu tukio la utoto wake. Watoto ambao alicheza naowalimuita majina . . . na kumletea uchungu na majonzi. Alipofika nyumbanibaba yake alimkumbatia katika mikono yake yenye nguvu na kumsikilizaalichokuwa akisema wote wakilia pamoja . . . Babake alimwelezea kuwatukio hili lingeweza kufanya maisha yake kuwa yenye furaha na fanaka.‘Mpendwa’ alisema, una nundu kwa mgongo wako na matatizo menginemazito. Lakini haya siyo makosa yako. Siyo makosa ya wazazi wako auBaba yetu aliye Mbinguni. . . . Yote ambayo wavulana na wasichana haowalisema ni ya kweli, lakini siyo haki wala siyo wema. Kama maisha yakoyote utajaribu kuwa mwenye haki na mwema kwa wengine kuliko baadhiyao watakavyokufanyia, ndipo utakuwa mwenye furaha na maisha yakoyatakuwa makamilifu na yenye maana”. (“More Joy and Rejoicing,” Ensign,Nov. 1976, p. 32.)

Je! Hadithi hii ina maoni gani kwa kila mmoja wetu juu ya kile tunachoweza kufanya ili kuwamwenye hisani? Wacha washiriki wa darasa wasome 1 Wakorintho 13:1.

Mzee Theodore M. Burton alieleza kuwa “Hisani ni . . . upendo mkuukabisa ambao hata tuko tayari kutoa sehemu yetu sisi wenyewe kwawengine . . . Ni rahisi kusema, ‘Nakupenda’ Lakini upendo siyo kitu chakusema tu, bali unapaswa kuonyeshwa kwa vitendo. Upendo kama badohaujaonyeshwa ni kama matuazi au ngoma inayopiga kelele na kuumizamasikio wala haiifurahishi nafsi.” (“More Joy and Rejoicing,” The Instructor,June 1970, p. 201.)

Kuwa na hisani kutatusaidia kuishi maisha yenye furaha na yenye maana.Kama hatuwezi kuboresha hisani, tutakuwa “vyombo visivyofaa ambavyowafuaji huvitupa nje” (kwani havina kazi) na kukanyagwa na miguu yawanadamu (Alma 34:29).

Utumishi wa KikristoOnyesha picha 33-a, “Kristo ndiye mfano kuu wa upendo.”

Upendo wetu kwa Baba yetu aliye Mbinguni na watoto wake hufunuliwakupitia utumishi wetu kwa wanadamu wenzetu. Raisi Harold B. Lee alisemakuwa usiku mmoja aliona kile “lazima kilikuwa ni ono” ambalo aliambiwa,”

235

Somo la 33

33-a, Kristo ndiye mfano mkuu wa upendo

Page 245: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“Kama unataka kumpenda Mungu ni lazima ujifunze kuwapenda nakuwatumikia watu. Hii ndiyo njia ya kuonyesha upendo wako kwa Mungu.”(Stand Ye in Holy Places, p. 189.)

Utumishi wa “Kikristo” ni utumishi unaotolewa kwa moyo na mara nyingibila kutegemea zawadi kwa yule mhitaji. Inaweza kuwa bila kuombwa aukupendezwa na yanahitaji bidii nyingi kwa upande wetu. Unawezakuhitajika katika wakati ambao ni vigumu sisi kutoa. Bila kujaliumetolewaje, ni utumishi ambao umetolewa kwa sababu tunawapendawatoto wa Baba yetu aliye Mbinguni.

Kwa nini tutumikiane? Ni nani tunaweza kumtumikia?

Yatupasa kuwatumikia wanadamu wote kadiri tuwezavyo na kulingana namahitaji yao. Lakini Mzee Thomas S. Monson, anatukumbusha kuwa watuwengine wanahitaji msaada wetu zaidi kuliko wengine: “Wagonjwa, wenyetaabu, wenye njaa, walio uchi, walioumia, walio pweke, wazee,wanaotangatanga wote wanaolilia msaada wetu.” (“Your Jericho Road,Ensign, May 1977, p. 73.) Hadithi ifuatayo inaelezea jinsi mvulana mmojaalivyojifunza umuhimu wa utumishi.

Mpe nafasi mshiriki wa darasa aliyechaguliwa mapema kuelezea hadithi ifuatayo.

Askofu alimwita Steve katika afisi yake baada ya mkutano wa sakramenti ilikuongea naye. “Haya sasa,” alifikiria Steve. “Naenda kuwa Raisi mpya wajamii ya waalimu. Washiriki wote wa kata watataka kunisalimia nakunipongeza. Mama ataona fahari!”

“Steve, tuna kazi yakukupa,” askofu alisema. Hii ni kazi ya kipekee ya kuwa‘jirani mwema.’ Tunamashaka sana juu ya Hasty McFarland. Anahitaji mtukuwa rafiki yake. Yeye siyo muumini wa Kanisa, lakini upendo wa Munguhumfikia kila mtu, na tumepewa nafasi ya kuonyesha upendo huo.”

Steve alishangaa. Na kuwaza jinsi yeye na rafiki zake wiki mbili zilizopitawalivyomtania mzee huyu kwa kuimba na kusema kwa sauti maneno yautani waliyotunga juu yake. Kwa kukata na kuhisi makosa, alimsikia askofuakisema, “Ningependa wewe utembelee mzee huyu mara mbili au tatu kwawiki. Sasa kama kazi hii itakuwa ngumu kwako usiogope kusema.”

Steve alifikiria kidogo na kumwambia askofu kuwa atafanya kazi hiyo.Askofu alimpatia maongozi kuhusu kazi hiyo. “Unaweza kukata kuni zamoto na kumpelekea chakula, blanketi—chochote anachohitaji ilikumsaidia kuhisi kuwa anatakiwa. Kuwa rafiki. Baba yako anajua juu yakazi hii, na aliniambia kuwa atakusaidia. Baba yako aliye Mbinguni piaatakuwa akikusaidia.”

Akiwa na miaka kumi na tano, Steve angefikiria vitu vingi ambavyoangeweza kufanya . . . kucheza kandanda, kuwinda, kuvua samaki aukucheza na rafiki zake. Lakini alijua kuwa alikuwa amekubali kufanya kazialiyopewa.

236

Page 246: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Hasty aliishi pekee yake katika nyumba ndogo ya mbao nje ya mji. Maramoja kwa mwaka alioga katika hoteli ambayo gharama yake ililipwa namkuu wa sehemu yao. Alivaa kiraka cheusi kwenye macho na alikuwa nanundu kwenye upande wa kichwa chake. Watoto wengi na hata baadhi yawatu wazima walikuwa na tabia ya kusema maneno mabaya juu yake.

Steve aliwasili katika nyumba ya Hasty akiwa anaogopa. Aligonga mlango,lakini hakupata majibu. Mwishowe baada ya kuita, aliamua kusukuma nakufungua mlango. Kulikuwa na baridi na giza katika nyumba ya Hasty.Alimwona Hasty amekaa kwenye blanketi chafu na kukuu katika kitandachake.

“Hasty, naweza kukufanyia kitu chochote?” Steve alisema kwa ghafla.Alimwambia mzee huyu jina lake na kuwa askofu wa Kanisa la Yesu Kristola Watakatifu wa Siku za Mwisho alikuwa amemtuma. Mtu huyu mzeehakusema chochote bali aliangalia sakafuni. Steve alitoka nje ya nyumbana kwenda kukata kuni. Aliwaza wakati wote alipokuwa akikata kuni nashoka kwa nini alikuwa mahali hapo. “Wacha kunung’unika,” sauti ndaniyake ilisema. “Mtu huyu mzee anahisi baridi na anahitaji msaada.”

Steve aliwasha moto na alijaribu kumsemesha Hasty ambaye hakujibu.Aliamua kuwa Hasty hakuwa akisikiliza, basi alimwambia kuwa atakujakesho na blanketi safi lenye joto. Kesho yake alirudi na blanketi mpya,kama alivyoahidi. Kila siku kwa wiki nne zilizofuatia alimtembelea Hasty.Mwishowe, mzee huyu alianza kuongea naye. Siku moja alisema, “Kijana,kwa nini wewe huwa unakuja? Nina hakika kuwa kijana mdogo wa miakayako anaweza kupata vitu vizuri vya kufanya kuliko kumtembelea mtuasiyependeza kama mimi.” Na hapo alitabasamu.

Siku ya Shukrani, Steve alimkaribisha kwa chakula cha jioni. Hakuja, lakinifamilia ya Steve walimpelekea sehemu ya chakula chake. Machozi yalitokakatika macho ya Hasty alipokuwa akijaribu kuwashukuru.

Baada ya muda, Steve akaja kujua juu ya maisha ya Hasty kamamchungaji wa kondoo. Alijua ya kwamba mke wake na watoto wakewalifariki kutokana na homa mbaya, ugonjwa ambao pia uliharibu jicho laHasty. Baada ya kumsikiliza mzee huyu aliyeishi pekee yake hakuonekanakuwa mtu mwenye sura mbaya tena. Na Steve kila wakati baada ya shulealienda kwake ili kusikiliza hadithi zake na kumsaidia mzee huyu.

Wakati Krismasi ilipofika, familia ya Steve walimkaribisha Hasty kwachakula cha jioni tena. Wakati huu alikuja akiwa yeye ni msafi, amevaa suti,na kuonekana mwenye sura nzuri. Baada ya chakula cha jioni mzee huyualitoa shukrani kwa Steve na familia yake. Alisema kuwa maisha yakeyalikuwa hayana mwelekeo, lakini upendo ambao walimuonyeshaulimfanya yeye kuwa mtu tofauti.

237

Somo la 33

Page 247: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Steve alimwangalia Hasty na kuona jinsi alivyokuwa na furaha; alihisi moyowake umeanza kuwa na furaha.” (“Hasty,” New Era, Nov. 1974, pp. 48–49.)

Je! utumishi alioupata Hasty ulikuwa utumishi kama wa Kristo? Ni vipi mvulana huyualibarikiwa kwa huduma aliyompatia Hasty? Ni nani alibarikiwa zaidi?

Tulipobatizwa, tulimwahidi Bwana kuwa “tutabeba mizigo ya wengine, . . .tutahuzunika na wale wenye huzuni . . . , na kuwafariji wale ambaowanahitaji faraja (tazama Mosiah 18:8–9). Tunalo jukumu la kuwatafutawale ambao wana mahitaji. Halafu tuna jukumu la kuwasaidia katikaupendo na unyenyekevu bila kushurutishwa wala kuamriwa. (tazamaM&M 58:26–29.)

MwishoAskofu Burke H. Peterson ametukumbusha: “Bwana alitoa amri hii katikawote—siyo wachache kwa nchi moja au watu kadha kwa nyingine, siyo tukwa familia hapa au pale, lakini kwa watoto wake wote, kila mahali.Dhihirisha upendo sasa! Uonyeshe sasa.” (Ensign, May 1977, p. 69.)

Upendo kama huo huwanufaisha siyo tu wale ambao tunawatumikia, bali piasisi wenyewe. Raisi Spencer W. Kimball alisema, “Ni kwa kutumikia ndiyotunajifunza jinsi ya kutumika. Tukiwa katika utumishi wa wanadamu wenzetu,siyo tu matendo yetu yanawasaidia lakini pia tunaweka shida zetu wenyewekatika mtazamo tofauti . . . na tunakuwa na muda mdogo wa kushughulikiashida zetu . . . tunajiweka katika hali ya juu zaidi kibinafsi tunapowatumikiawengine.” (“Small Acts of Service,” Ensign, Dec. 1974, p. 2).

“Tunao wajibu mkubwa kuliko hapo awali wa kuzifanya nyumba zetu kuwa kivutio kwa jirani, upendo, jukumu za jamii, uaminifu. Wacha jiranizetu kuona na kusikia hayo . . . Mungu tusaidie kama washiriki wenyeukuhani, kama washiriki wa Kanisa, kutoa . . . mwangaza . . . upendo, . . .ufadhili . . . na utumishi!” (David O. McKay, “Radiation of the Individual,”Instructor, Oct. 1964, p. 374.)

Changamoto1. Omba kwa unyenyekevu na kweli ili kuwa na uwezo wa kupenda jinsi

Kristo anavyopenda.

2. Onyesha upendo kwa familia yako kwa kufanya matendo mema kwakila mmoja wa watu wa familia yako.

3. Onyesha upendo wako kwa mtu mwenye shida kwa kumfanyiamatendo mema.

4. Saidia familia yako ya ukuhani kupanga shughuli ya utumishi kwa mtufulani.

Maandiko Matakatifu ZaidiMathayo 25:31–46 (tunamtumikia Mungu tunapowatumikia wanadamuwenzetu)

238

Page 248: Wajibu na Baraka za Ukuhani

1 Wakorintho 13 (hisani ndiyo tabia kuu ya uungu)

Moroni 7:45–48 (hisani ni upendo halisi wa Kristo na ni kipawa kutoka kwaMungu)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 28, “Upendo,” na sura ya 30, “Hisani,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Chagua washiriki watakaotoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

239

Somo la 33

Page 249: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Usafi wa Maadili

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kuelewa umuhimu wa usafi wamaadili.

UtanguliziKatika dunia ya sasa kuna viwango tofauti vya maadili. Viwango hivi marakwa mara hubadilika na wakati na hali. Kinyume chake, viwango vyaMungu huwa havibadiliki, kwani yeye ni sawa, jana, leo, na milele. Kipimokimojawapo ambacho Mungu anatutazamia tufuate ni maadili ya usafi.

Maandiko Matakatifu yanatuelezea kuwa “hakuna kitu kichafu ambachokinaweza kuishi na Mungu” (1 Nefi 10:21). Mtume Paulo aliaandika kuwa“Hamjui kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho waMungu anakaa ndani yenu. Kama mtu yeyote atachafua hekalu la Mungu,Mungu atamuangamiza mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu,ambalo ndilo ninyi.” (1 Wakorintho 3:16–17.) Miili yetu ni mitakatifu. Bwanaametupatia miili yetu kwa kusudi takatifu, na anatarajia tuiweke safi nayenye kustahili kumpokea Roho wake.

Miili Yetu ni MitakatifuNi muhimu sisi kama watu wenye ukuhani kujiweka katika maadili ya usafi,kwani baraka ambazo ni muhimu kwetu zinaambatana na maadili yetu yausafi. Mzee Boyd K. Packer anatueleza kuwa “Moja ya nguvu nyingi zaMungu, ambayo anaithamini sana, ni nguvu ya kutoa na kuchukua uhai.Ametukataza kuondoa uhai, lakini ametushirikisha nguvu yake ya kuumbana kutukubali kuleta watoto katika dunia. Kwa sababu nguvu hizi ni takatifu,ameamrisha watoto wake wote kuzitumia ipasavyo na kutumia nguvu hizindani ya ndoa peke yake. Ametuelezea pia kuwa tamaa za nguvu hizi kuuni lazima zidhibitiwe na kutumiwa ndani ya masharti ambayo ameweka nasiyo kwa uchoyo wa kujiridhisha au starehe tu . . . Furaha ambayo itakujakwetu katika maisha haya itategemea jinsi [tunavyotumia] nguvu hii yauumbaji.

“Nguvu hii ya uumbaji huja na tamaa ya nguvu na ashiki zenye nguvu,zenye nguvu ili ziweze kuwashawishi wanaume wakubali wajibu wanyumba na familia. Lakini kwa sababu tamaa hii ni yenye nguvu, wakatimwingi tunashawishika kutumia vibaya nguvu hizi za kuumba. Ni kwakutumia nguvu hizi vibaya ndipo tunakuwa na familia ambazo zimevunjikana furaha kupotea. Kwa sababu hii [hatupaswi] kutumia nguvu hizi na mtuyeyote ila [wake zetu] . . . Kama nguvu ya kuumba yenyewe, [miili yetu]

240

Somo la 34

Page 250: Wajibu na Baraka za Ukuhani

pia [ni] mitakatifu. Tusikubali miili yetu kushikwa na sisi wenyewe auwengine kwa njia ya majaribio au kwa njia zisizo za kawaida. Njia sahihipekee na ya haki kutumia nguvu hii ni ndani ya pingu za ndoa.” (“Why StayMorally Clean?” New Era, July 1972, pp. 4–6.)

Moroni anatueleza kuwa maadili ni ‘kitu kizuri na cha thamani kushindavitu vyote.’ (Moroni 9:9). Ni lazima sisi wenyewe kuiweka safi miili ilikuimarisha jamii zetu sisi wenyewe kwa wema, kutuwezesha sisi kuishikwa amani na umoja.

Sheria ya Mungu ya UsafiMungu hajabadilisha sheria na amri zake juu ya dhambi ya uzinzi, ingawamwanadamu amejaribu kuzibadilisha ili kukidhi starehe zake. Sheria yausafi wa mwili ina maana kuwa mtu ni lazima asiwe na urafiki wa kimwili namtu yeyote bali mke wake pekee yake. Bwana ametuamuru kuwa, “usizini”(Kutoka 20:14). Sheria ya usafi wa mwili siyo tu uzinzi, lakini. Inaendeleapia matumizi yasiyo sahini ya nguvu hizi takatifu.

Ni njia gani ambazo mwanadamu hutumia nguvu hizi vibaya? (Andika majibu ubaoni)

Baadhi ya njia ambazo mwanadamu hutumia nguvu hizi takatifu vibaya ni—

• Uzinzi na usherati (pamoja na kuishi pamoja bila ndoa).

• Watu wa jinsi moja kufanya mapenzi.

• Kuondoa mimba.

• Kujichua

Sheria ya usafi wa kimwili ni pamoja na katika mawazo na heshima katikamavazi. Maandiko Matakatifu yanatuambia kwamba matendo yetu nimatokeo ya kufikiri kwetu (tazama Methali 23:7). Kwa sababu hiyo,inatupasa kuwa na mawazo mema kama tunataka kujiweka katika maadilisafi. Njia mojawapo ambayo mawazo yetu hujionyesha katika maisha yetuni namna tunavyovaa. Wale wanaovaa kiheshima huonyesha kwambawanaijali miili yao kuwa ni mitakatifu.

Wacha aliyechaguliwa mapema kati ya washiriki wa darasa kueleza hadithi ifuatayo ya RaisiKimball.

“Dhambi, kama safari, huanza na hatua ya kwanza; na hekima na uzoefuhutufundisha kuwa ni rahisi kuzuia kishawishi mara ya kwanza kuliko vilevitakavyofuatia ndipo mlolongo wa makosa umeanza kufuatana. Hiiinaonyeshwa katika hadithi ya ndege mwenye sauti tamu. Alipokuwaamekaa juu ya tawi mbali na hatari yoyote, alimwona msafiri akipita katikatiya msitu akiwa amebeba kisanduku cheusi cha ajabu. Ndege huyu alirukachini hadi na kukaa kwenye bega la msafiri huyu. “Umebeba nini ndani yasanduku hiki kidogo?”

“ ‘Minyoo,’ msafiri akajibu.

“ ‘Ni ya kuuza?’

241

Page 251: Wajibu na Baraka za Ukuhani

“ ‘Ndiyo na kwa bei rahisi. Bei ni nyoya moja kwa mnyoo mmoja.’

“Ndege huyu alifikiria kwa muda. ‘Nina manyoya millioni. Si vibaya nikitoamoja.’ Huu ni wasaa wa kupata chakula kizuri cha jioni bila kazi yoyote.Kwa hiyo alimwambia mtu huyo kuwa atanunua mmoja. Alitafuta kwamakini chini ya bawa lake ili kupata nyoya dogo. Alinywea kidogoalipokuwa akitoa nyoya hilo, lakini ukubwa na uzuri wa mnyoo huoulimfanya yeye kusahau uchungu huo. Huko juu ya mti alianza kutoa sautinzuri kama hapo awali.

“Siku ya pili alimwona mtu yule yule na kwa mara nyingine alinyofoa tenanyoya lake kwa ajili ya mnyoo. Ooh! hii ni njia ya ajabu, bila juhudi yoyoteunajipatia chakula cha jioni!

“Kila siku ndege huyu alitoa nyoya na kila aliponyofa ilionekana maumivuyakipungua kidogo kidogo. Mwanzoni alikuwa na manyoya mengi lakinisiku zilipokuwa zikiendelea alijiona kuwa ni vigumu kuruka. Mwishowe,baada ya kupoteza mojawapo ya nyoya lake la msingi, hakuweza kufikakileleni mwa mti, wala kuruka hewani. Kwa kweli aliweza tu kurukaruka futichache hewani na akalazimika kung’ang’ania chakula chake nashorewanda wenye makelele na mabishano.

“Mtu yule mwenye minyoo hiyo hakuoneka tena, kwani kulikuwa hakunanyoya la kulipia chakula. Ndege huyu hakuimba tena kwa sababu alikuwaakiona haya kuhusu hali aliyokuwa nayo.

“Hivi ndivyo tabia zisizo stahili zinavyotukamata—kwanza kwa uchungu,halafu kwa urahisi hadi mwishowe tunajikuta sisi wenyewe tumevuliwachochote kile kinachotufanya kuimba na kupuruka juu. Hivi ndivyo uhuruhupotea. Hivi ndivyo tunavyozama kwenye mtego wa dhambi.” (TheMiracle of Forgiveness, pp. 214–15.)

Udhibiti wa fikira zetu, mavazi yenye adabu na kusikiza na kutii amri zaBaba yetu aliye Mbinguni ni njia ambazo zitatuhakikishia kuwahatutaendeleza tabia zisizo stahili na kupoteza usafi wetu wa kimwili.

Wakati mwana wa Alma alipozini, Alma alimwambia, “ haujui kuwa mambohayo ni machukizo machoni mwa Bwana; ni ya kuchukiza kabisa kulikodhambi zote isipokuwa kumwaga damu isiyo na hatia au kumkana RohoMtakatifu?” (Alma 39:5).

Tunahitaji kujua na kuelewa kwa wazi uzito wa uzinzi. Haitufai tu kuishimaisha safi sisi wenyewe lakini pia inatupasa kufundisha na kuhimiza usafiwa kimwili kwa wengine hasa watoto wetu.

Tunawezaje kuhimiza watoto wetu kuvaa mavazi ya heshima na usafi wa kimwili?

Nguvu ya Ukuhani katika Usafi wa MaadiliHakuna anayeweza kukosa kufuata amri ya usafi wa kimwili na kutarajiakupata amani mpaka atakapotubu dhambi hiyo. Kitabu cha Mormonikinatueleza kuwa Roho Mtakatifu hawezi kukaa ndani ya hekalu chafu

242

Page 252: Wajibu na Baraka za Ukuhani

(tazama Helaman 4:24). Na tukipoteza nguvu ya Roho Mtakatifu,hatutaweza kutumia mamlaka ya ukuhani ambayo tulipewa. Bwanaamesema “na vitu vyote vifanywe kwa usafi mbele yangu” (M&M 42:41).Wakati tukiwa wasafi kimwili, Roho Mtakatifu anaweza kufanya kazi ndaniyetu na kutusaidia kutumia nguvu yetu ya ukuhani ipasavyo. Katika njia hii,ukuhani ni mlinzi mkuu dhidi ya dhambi. Kama tujiitumia kwa haki, siyo tutunawatumikia wenzetu vyema bali tunapata nguvu ya kufukuza majaribu.Mzee A. Theodore Tuttle anatupa mfano wa jinsi uovu unavyotuzuiakutumia mamlaka yetu ya ukuhani:

“Mvulana mmoja mjinga alikuwa amekwisha fanya mahojiano ili kwendamisheni,” aliandika Mzee Tuttle, “na ingawa aliulizwa maswali yaliyo rahisi,yeye alijibu kwa uongo. . . . Halafu alienda nje na kujaribu kufundisha injili.Hiyo, kwa kweli, lilikuwa jaribio la mwisho na jaribio ambalo alianguka.Mmisionari huyu alifahamu ya kwamba hangeweza kufanya kazi ya umisionaribila Roho wa Bwana . . . kwa hiyo mmisionari huyu ilimbidi kutubu nakukubali kuwa alisema uongo . . . kwa wale ambao walikuwa na mahojianonaye kabla ya Roho wa Bwana kurejea kwake.” (“Men with Message,”Address given to Seminary and Institute faculty at B.Y.U., 1958, p. 2.)

Raisi Spencer W. Kimball alitupatia ushauri ambao ungekuwa wenyemsaada mkubwa kwa mmisionari katika hadithi iliyo hapo juu. Anatuelezakuwa “matembezi ya pamoja na msichana katika sehemu za burudaniyafaa kuahirishwa mpaka angalao umri wa miaka 16 au zaidi, na hata hivyoyafaa kuwa maamuzi yamefanyika katika uchaguzi na utani. Wavulana nawasichana yafaa kuweka mipaka ya kukaribiana kwa miaka kadha, kwanimvulana atakuwa akienda misheni wakati akiwa na miaka kumi na tisa.”(“The Marriage Decision,” Ensign, Feb. 1975, p. 4.)

Raisi Kimball anaelezea kuwa “miongoni mwa dhambi za kawaida zausherati kwa wavulana na wasichana ni kushikanashikana na kupiganabusu. Siyo tu uhusiano huu huwaongoza katika kuzini . . . na kutoa mimba—ambazo zote ni dhambi mbaya—lakini zenyewe ni uovu wenye madhara, nawakati mwingi ni vigumu kwa vijana kutofautisha mahali ambapo mojainaishia na nyingine inaanzia.” (The Miracle of Forgiveness, p. 65.)

Ni namna gani ushauri wa Raisi Kimball ungemsaidia kijana huyu mmisionari?

Kujiweka safi na katika wema inaruhusu Bwana kutubariki kwa nguvu zakiroho. Wakati mwingine, hata hivyo, tunafanya makosa. Kama tumefanyamakosa, Inatubidi kuongea na raisi, askofu au raisi wa misheni juu yajambo hilo. Atatushauri na kutusaidia kupata msamaha.

Bwana yuko tayari kutusamehe wakati tunapotubu dhambi zetu kama vilealivyo tayari kutusaidia sisi kubaki wasafi kimwili. Anajua udhaifu wetu naatatupatia njia ya kutusaida kushinda majaribu (tazama 1 Wakorintho10:13). Kama msaada wa nyongeza, amewatuma manabii kutuongoza nakutufundisha jinsi ya kuishi na kufuata viwango ambavyo ametuwekea.

243

Somo la 34

Page 253: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Tukifanya yote yatakiwayo ili kuwa wasafi kimwili mbele ya Bwana,tutaweza “kusimama kwa ujasiri—bila uoga na haya wala aibu mbele yaMungu. Hii ni ahadi ya kila mwanaume au mwanamke mwenye maadilimema.” (Gordon B. Hinkley, “From My Generation to Yours, With Love,”Improvement Era, Dec. 1970, p. 73.)

Ni kwa namna gani mfano wetu wa usafi wa kimwili unaweza kushawishi tabia za watotowetu? Tunaweza kufanya nini ili kuwa mfano mwema?

Kama wenye ukuhani, hatuwezi kufanya kazi za kiroho kama sisi siyowasafi kimwili. Njia bora ya kuweza kutimiliza ni kutokubali aina yoyote yauchafu wa mwili kuingia ndani ya maisha yetu. Tukionyesha mfano wa kutiisheria za usafi wa mwili, tutajifunza umuhimu wa usafi wa mwili nakujitahidi kubaki wasafi kimwili.

MwishoBwana ametupatia amri ili sisi tuwe na furaha. Wakati wowote tunapotiiamri za Mungu, tunapata baraka lakini wakati tunapovunja amri, tunaumiakama matokeo yake. Kuwa na maisha ya usafi wa kimwili huwa na faidakwa njia nyingi. Maisha safi yanaimarisha ndoa na nyumba zenye furaha.Hutuweka huru dhidi ya kukosa kuaminika na majuto. Hutuweka kuwawastahili na kumtumikia Mungu. Inatuwezesha sisi kama wenye ukuhanikutumia ukuhani vizuri kwa niaba ya wengine. La muhimu zaidi, inatusaidiasisi kuishi ili kwamba tuweze kuishi na Baba yetu aliye Mbinguni milele.

Changamoto1. Chukua hatua zinazohitajika ili kuwa safi kimwili.

2. Zungumza na familia yako juu ya umuhimu wa usafi wa kimwili na jinsiya kuwa msafi kimwili.

Maandiko Matakatifu ZaidiMatayo 5:27–28 (tusifanye uzinzi katika mioyo yetu)

1 Timotheo 2:9–10 (umuhimu wa maadili)

2 Nefi 9:36, 39 (zawadi ya usafi wa mwili, malipo ya uchafu wa mwili)

Yakobo 2:27–28 (bwana anafurahishwa na usafi wa kimwili)

M&M 42:22–24, 80–81 (adhabu za uchafu wa kimwili)

M&M 88:86 (usafi wa mwili unahifadhi uhuru wa kibinafsi)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 39, “Amri ya Usafi wa Kimwili,” katika kitabu cha Kanuni za Injili.2. Pata chaki na ubao.

3. Chagua washiriki wa darasa kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo.

244

Page 254: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Familia ya Milele

Madhumuni ya somo hili ni kutusaidia sisi kujua wajibu wetu wa kuanzishafamilia ya milele.

UtanguliziNdoa ya milele ni fundisho la msingi la Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifuwa Siku za Mwisho na ni sehemu muhimu ya mpango wa Bwana kwetusisi. Bila hiyo hatuwezi kuwa na furaha ya kweli katika maisha haya aukuinuliwa katika ufalme wa mbinguni milele. Raisi Joseph Fielding Smithaliandika: “Ndoa, kama inavyoeleweka kwa watakatifu wa siku za Mwisho,ni agano [la milele] . . . Ni msingi wa kuinuliwa milele, kwani bila hiyo,hapawezi kuwa na ukuaji wa milele katika ufalme wa Mungu.” (Doctrine ofSalvation, 2:58.)

Raisi Spencer W. Kimball amesema, “Baba yetu wa Mbinguni anao mpangowa makuzi ya mtu kutoka utotoni hadi uungu—Alidhaminia kwamba watuwote waishi maisha ya kustahili [kuoa] kwa muda na kwa milele yote.” (“TheLord’s Plan for Men and Women,” Ensign, Oct. 1975, p. 2, 4.) Ndoa yahekaluni ni mwanzo wa familia ya milele. Kama mume na mke waliooanakatika hekalu wapatapo watoto na kushika amri, wanaumba familia ambayoitawaletea wao raha na furaha milele.

Kujitayarisha Kuwa Familia ya MileleOnyesha picha 35-a, “Familia za milele huanza hekaluni.”

Kwa Watakatifu wa Siku za Mwisho, hekalu ni mahali palipo muhimu sanahapa dunia. Ndani ya hekalu, ibada hufanyika ambazo huwezesha familiakuishi pamoja milele katika uwepo wa Mungu. Kama viongozi wa nyumbazetu na watu wenye ukuhani, tunao wajibu wa kuziongoza familia zetukuelekea kuinuliwa mbinguni. Hii inamaanisha kwamba tunao wajibu wakuzitayarisha familia zetu kuhudhuria hekaluni. Maandalizi ya namna hiyohuanza na sisi wenyewe tunapojitahidi kuheshimu ukuhani na kuishimaisha yaliyo safi.

Wakati wanaume na wanawake wanapooana katika hekalu, wanaozwa kwamaisha haya, na pia wanaunganishwa pamoja kwa milele. Baada ya hapo,watoto wote watakaowapata wanakuwa tayari wameunganishwa kwao nawanazaliwa ndani ya agano. Ikiwa mke na mume tayari kisheriawamekwishaoana na wakaenda hekaluni ili kuunganishwa milele, mume namke kwanza wanaunganishwa pamoja, na halafu watoto wanaunganishwakwa wazazi wao. Baada ya kuunganishwa kwao, watoto watakaozaliwa

245

Somo la 35

Page 255: Wajibu na Baraka za Ukuhani

35-a

Page 256: Wajibu na Baraka za Ukuhani

kwao wanakuwa moja kwa moja wamekwisha unganishwa kwao kamasehemu ya familia yao ya milele.

Iwe tunajitayarisha kuoa katika hekalu au kujitayarisha na familia yetukuunganishwa katika hekalu, ni lazima tujitayarishe kwa njia hizo hizo.Hatua yetu ya kwanza iwe ni kuweka lengo la kwenda hekaluni. Yatupasakujadiliana na wake zetu na watoto mambo ambayo tunahitaji kufanya ilikuwa tayari, na kwa pamoja tupange tarehe. Inatupasa kuandika tarehehiyo chini, tusali kuomba msaada wa Bwana ili tufikie siku hiyo, na halafutufanye kila tuwezalo kujitayarisha. Zaidi ya hayo, kwa sababu hekalu nimahali patakatifu, tunalazimika kujitayarisha wenyewe kiroho kuingia hapo.Ndani ya hekalu, tunaweka maagano yenye umuhimu mkubwa kiroho,kwani tunamwahidi Bwana kwamba tutashika amri zake zote na kumtii yeyekwa namna yoyote ile. Ni muhimu, hivyo basi, kwamba tuishi kwa haki nakutafuta kumfuata Roho Mtakatifu kama tunataka kuwa tayari kufanyamaagano haya.

Tunaweza kufanya nini kwa kujitayarisha vyema sisi wenyewe kiroho? (Andika majibu ubaoni.)

Baadhi ya njia ambazo tunaweze kujitayarisha ni—

• Sali kila mara na kwa dhati.

• Soma maandiko matakatifu kila mara.

• Uwe msafi kimaadili.

• Uwe mnyenyekevu na mwenye kutubu.

• Kwa uaminifu fanya mkutano wa jioni wa familia nyumbani na sala yafamilia.

Tunapokuwa kwa dhati tunafanya tuwezalo huwa tunajitayarisha kiroho,tutapokea msaada kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Mweleze mshiriki wa darasa aliye pangwa mapema kusimulia hadithi ifuatayo.

Mwanamke mmoja alielezea namna familia yake ilivyojenga furaha yao kwapamoja walipokuwa wakijitayarisha kuunganishwa pamoja katika hekalu:

“Hata kama mtoto, niliweza kuhisi hasira, kuumwa kichwa, chuki, wakatiwazazi wangu wakibishana. Daima nilikuwa nikilia hadi kulala kwa sababunilijua mambo hayapo kama yanavyopaswa kuwa.

Niliweza kuhisi tofauti katika nyumba ya rafiki zangu ambazo familia zaozilikuwa na umoja katika injili . . . [Shukrani kwa Askofu na Walimu waNyumbani, mambo yalianza kubadilika]. Injili pole pole ilianza kuwasehemu ya maisha yetu . . . Mabishano yakawa madogo . . . kwambali . . . Familia yetu ilihisi wajibu wa kuishi kama tulivyokuwatumefundishwa, hususani sasa kwamba tulikuwa na lengo la kufanyia kazi[hekalu]. Kama ni maneno makali yalizungumzwa kwa woga, tulijibishana

247

Somo la 35

35-a, Familia za milele huanza katika hekalu

Page 257: Wajibu na Baraka za Ukuhani

maneno ya upendo, kwa upole na kwa dhati . . . Tulishikia shauku yakusaidiana. Mama na Baba hawakuwa daima wakiuliza jambo mara tatuau mara nne; kazi za nyumbani zilifanyika kimya kimya, haraka na maramoja. Upendo na hamu ya kusaidia uliushinda ukale wa hasira, kiburi, naugomvi wa mara kwa mara miongoni mwetu.

“Ni nini kilichofanya mabadiliko? Mambo mengi sana. Pengine ilikuwa niukweli wa ndoto iliyosubiriwa kwa muda mrefu iliyokuja kuwa kweli. Kadirisala za kifamilia na mikutano ya jioni ya familia nyumbani ilipokuja kuwasehemu ya maisha yetu, tulijifunza kujua na kupendana. Njia tulizokuwatukiishi ziliruhusu shuhuda zetu kukua . . . shuhuda za sala ya kifamilia,kusoma maandiko matakatifu, jioni ya familia nyumbani, kuhudhuriamikutano ya kanisa. Ushuhuda wetu halisi ulikuwa ni wa kanuni ya toba. Nasisi pia tulijua kwamba Mungu aliishi. Baada ya kipindi cha muda napamoja na ushuhuda huu na uhakika kwamba tulikuwa wenye kustahili,tulikuwa tayari kwenda kwenye hekalu la Bwana na kuunganishwa pamojakama familia kwa muda na kwa milele yote . . .

“Tulipokuwa tumesimama langoni pa hekalu, donge lilinikaa kooni.Kulikuwa na kusita kwa muda—na halafu tukaingia . . . Mhudumu alikujakutuchukua sisi hadi kwenye chumba cha kuunganishwa. Mama na Babawalikuwa hapo, nyuso zao zikingara, wamevalia mavazi yao ya hekaluni.Tulipiga magoti kuizunguka altare tukiwa tumeshikana mikono. Mhudumualimshikilia mtoto mchanga ili kwamba naye, vile vile, alikuwa sehemu yamzunguko wa familia.

“Na halafu maneno yakatamkwa ambayo yalituunganisha sisi kama familiakwa muda na kwa milele yote.

“Najua wazazi wangu wananipenda, kwa sababa wamenifanya miminiunganishwe kwao kwa muda na kwa milele yote.” (Brenda Bloxham, “MyParents Took Us to the Temple,” Ensign, Aug. 1974, pp. 61–62.)

Maandalizi ya kifedha pia ni sehemu muhimu ya kujiandaa kwendahekaluni. Wakati mwingine hii humaananisha miaka mingi ya kupanga,kujiwekea akiba, na kufanya kazi pamoja. Familia nyingi zimejitoamuhanga kila kitu walichokuwa nacho ili kwenda hekaluni. Fikiria kwamuda ni jinsi gani familia zetu zilivyo na thamani kubwa kwetu. Jee kunakiasi chochote cha fedha kilicho na thamani kubwa kuliko familia zetu?

Kwa kukabili gharama za kwenda hekaluni, tunahitaji kutafuta ni gharamakiasi gani ya kutusafirisha kwenda na kurudi hekaluni na kukadiria gharamanyinginezo kama za chakula na malazi. Tunapopata makadirio hayo,tunapaswa kakadiria ni kiasi gani tunaweza kujiwekea kila mwezi. Kamatukifanya hivi, hatimaye tutaweza kwenda hekaluni. (Tazama ushuhuda waKaka Vahai Tonga Katika somo la 21). Chochote tunachohitajika kufanya ilikujitayarisha sisi wenyewe na familia zetu kwenda hekaluni, yatupasakuanza sasa. Faida zake zinashinda muda na gharama tunazotumia.

248

Page 258: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Mshiriki mmoja wa familia ambaye amewahi kwenda hekaluni pamoja na familia yake asimuliejinsi alivyojitayarisha na uzoefu wake.

Vijana ambao hawajaoa wameshauriwa mara nyingi na manabiikujitayarisha kwa ajili ya ndoa ya hekaluni. Raisi Kimball amesema:“Ingawa vijana wengi hawana kwa wakati huu mahekalu katika jumuiyazao, kwa ujumla yapo mahekalu katika umbali ambao si wa kutisha . . . Nitumaini letu kwamba wakati utakapokuwa umefanya uchumba sahihi,kwamba uweze . . . kwenda katika moja ya mahekalu ya karibu nawe ilimuunganishwe kwa milele yote ili kwamba watoto wenu wawe wenu wakudumu na kwamba ninyi muwe wazazi wao wa kudumu na hivyo muwendoa ya milele.” (“The Marriage Decision,” Ensign, Feb. 1975, p. 4).

Kujenga Familia ya MileleOnyesha picha 35-b, “Familia zilizounganishwa pamoja katika hekalu zina ahadi kwamba,kama watabakia waaminifu, watakuwa pamoja milele.”

Ndoa katika hekalu ni mwanzo wa familia ya milele. Lakini huu ni mwanzotu. Ili kuweza kujenga uhusiano wa kifamilia ambao utadumu milele, lazimatuwe waaminifu kwa ahadi tunazofanya katika hekalu. Ni lazimatuheshimiane kila mmoja kama kwamba tunataka kuwa pamoja kamafamilia kwa milele yote. Inatupasa tujitahidi kufanya nyumba zetu kuwaselestia ndogo hapa duniani.

Kama baba, tunaweza kufanya mengi ili kujenga familia za milele.Hatuhitajiki kuwa matajiri au wasomi bali ni lazima tuuheshimu ukuhaniwetu. Kama tutafanya, tutabadilishwa na kuimarishwa kwa ukuhani natutapokea ushawishi wa ndani kutoka kwa Roho Mtakatifu ambayeatatusaidia sisi kujenga familia za milele. Baadhi ya mambo tunayowezakuyafanya ili kujenga familia za milele ni—

• Kuita familia zetu pamoja kusali sala ya familia.

• Kumuita mtu mmoja ili aombe baraka juu ya chakula wakati wa kula.

• Kuzipeleka familia zetu kanisani.

• Kulipa zaka na matoleo mengineyo.

• Kuwa mwaminifu katika mambo yote tunayofanya.

• Piga magoti daima katika sala ya binafsi na tumuombe Bwana msaadatunapowafundisha na kuwapenda wake zetu na watoto.

• Tumia kila nafasi kufundisha familia zetu injili, hususani wakati wa jioni yafamilia nyumbani.

Tunapozibariki familia zetu kwa njia hizi tutafaidi furaha ya sehemu yafamilia ambayo ni ya milele.

Makuhani wasiooa wanaweza pia kusaidia familia zao kuwa na furaha nakuishi kama familia ya milele. Wakati tunapoelewa mpango wa Bwana kwaajili ya familia zetu, tunaweza kuona watu wa familia zetu ni watu muhimu

249

Somo la 35

Page 259: Wajibu na Baraka za Ukuhani

35-b

Page 260: Wajibu na Baraka za Ukuhani

sana katika maisha yetu. Inatupasa kuwatendea wao kwa upendo nawema, na kufanya yote tunayoweza kuwatia moyo na kuwaimarisha.

Kama kuna vijana makuhani wasiooa katika darasa lenu, Jadileni njia ambazo wao wanawezakujitayarisha kwa ajili ya ndoa ya hekaluni. Waulize wao kuelezea kwa nini ndoa ya milele nimuhimu kwao. Jadili mambo ambayo wao wanaweza kufanya familia zao ziwe na furaha sasahivi.

MwishoMuulize mshiriki wa darasa aliyepangwa toka awali kusimulia hadithi ifuatayo.

Kijana mmoja kutoka Mexico alisimulia hadithi ifuatayo juu ya shangazi namjomba wake. Inaeleza furaha ambayo inaweza kuja kutokana na msingiwa maisha uliojengwa juu ya ndoa ya hekaluni:

“Mjomba wangu David na Shangazi yangu Guadalupe . . . daimawalikuwa wakigombana. Nyumba yao ilikuwa maafa na watoto waowalikuwa wakiteseka kwa kushuhudia ugomvi kila siku. Hatimaye ShangaziGuadalupe na watoto waliondoka na kwenda kuishi na wazazi wake.

“Wakati wa utengano huu, Mjomba David alikutana na wamisionari naakabatizwa siku kadhaa baadaye. Ufahamu wake mpya juu ya injiliulimfanya atambue kwamba familia ilikuwa ni taasisi ya milele. Aliwatumawale wamisionari kwa mke wake na watoto, lakini wakakataa kuwasikiliza.[Hatimaye] waliikubali injili wakajiunga na Kanisa na wakaanza kuishipamoja tena. Hata hivyo, kupigana na kugombana kuliendelea kamamwanzoni.

“Walijadili umuhimu wa ndoa ya hekaluni, lakini matatizo ya kiuchumi nakugombana kwa mara kwa mara kuliwazuia kufikia lengo lao. [Lakini baadaya kujitolea muhanga kwingi hatimaye waliweza kwenda hekaluni.]Shangazi yangu na mjomba waliunganishwa pamoja baadhi ya watotowao, na wakarudi Mexico wakiwa na pesos 15 tu . . . na mjomba wanguakawa hana kazi.

“Kuoa katika hekalu hakukufuta matatizo haya, lakini yaliwapa shangazi namjomba wangu nguvu ya kuendelea mbele, hata bila pesa na badowalijisikia furaha.

“Kidogo kidogo walipata chakula cha kuwatosha, na njomba wangualiweza kupata kazi.

“Niliweza kuona mabadiliko makubwa juu ya nyuso zao na maisha yao.Walikuwa wenye furaha zaidi kuliko awali, lakini mshangao wangu mkubwaulikuwa kwamba sikuwahi kusikia tena wakigombana. Katika nyumba yaomilisikia maneno ya upendo . . .

“Hivi karibuni, mjomba wangu aliniambia, ‘Jorge, baada ya kuoa kwamiaka 24 na kuteseka mno, tumeigundua furaha yetu. Ni kama tu vijana

251

Somo la 35

35-b, Familia zilizounganishwa pamoja katika hekalu zimeahidiwa kwamba, kamawatabakia waaminifu, watakuwa pamoja milele yote

Page 261: Wajibu na Baraka za Ukuhani

wadogo ambao ni wasafi ambao tumeoana kwa mara ya kwanza naambao sasa tunasherekea fungate letu la milele.’ ” (Jorge Carlos TejadaPeraza, “Eternal Honeymoon,” Ensign, Aug. 1974, pp. 62–63).

Tunaweza kupata furaha kubwa kwa sababu ya uhusiano wetu wa familiaya milele. Majaribu na ugumu huhamisishwa wakati tunaposhirikiana nafamilia zetu. Maisha yetu huwa tajiri na ya kufurahisha kwa sababu yaupendo tunaoshirikiana. Na tunajisikia amani kubwa na faraja kwa sababutunao uhakika kwamba tunaweza kuwa pamoja milele.

Changamoto1. Kama haujaoa katika hekalu, fanya mpango na anza maandalizi yako ya

kuunganishwa pamoja na familia yako. Kama inawezekana, pata pichaya hekalu na itundike mahali ambapo itaweza kuonekana kwa urahisi.Halafu, chini ya picha hiyo ya hekalu, andika tarehe ambayo familiayako imechagua kama lengo.

2. Kama umeoa hekaluni, fikiria mambo unayolazimika kuyafanya ili kuishipamoja na familia yako milele. Chagua njia moja ambayo familia yakoinaweza kuboresha na anza wiki hii kuifanyia kazi.

Maandiko Matakatifu ZaidiM&M 131:1–4 (lazima tuunganishwe katika ndoa ili kuingia katika utukufuwa juu wa ufalme wa mbinguni)

M&M 132:19, 55 (baraka walizoahidiwa wale ambao wameunganishwapamoja kama familia za milele)

Matayarisho ya Mwalimu

Kabla ya kufundisha somo hili:

1. Soma sura ya 36, “Familia Yaweza kuwa ya Milele,” katika kitabu cha Kanuni za injili.

2. Chagua Washiriki kutoa hadithi na maandiko matakatifu katika somo hili.

3. Mpange mshiriki wa familia ambaye amefika hekaluni pamoja na familia yake kusimuliamaandalizi yake na uzoefu alioupata.

252

Page 262: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Dondoo za Marejeo

Cowley, Matthew. Matthew Cowley Speaks. Salt Lake City: Deseret BookCompany, 1943.

Durant, George D. Love at Home, Starring Father. Salt Lake City: Bookcraft,1973.

Kanuni za Injili. Salt Lake City: Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Sikuza Mwisho, 1978.

Grant, Heber J. Gospel Standards. Kimetungwa na G. Homer Durham. SaltLake City: Improvement Era, 1941.

Jensen, Margie Calhoun. When Faith Writes the Story. Salt Lake City:Bookcraft, 1973.

Kimball, Spencer W. Faith Precedes the Miracle. Salt Lake City: DeseretBook Company, 1972.

—Marriage and Divorce. Salt Lake City: Deseret Book Company, 1976.—The Miracle of Forgiveness. Salt Lake City: Bookcraft, 1969.Lee, Harold B. Stand Ye in Holy Places. Salt Lake City: Deseret Book

Company, 1974.McKay, David O. Gospel Ideals. Chapa ya Pili. Salt Lake City: Improvement

Era, 1954.—Treasures of Life. Kimetungwa na Clare Middlemiss. Salt Lake City:

Deseret Book Company, 1962.Maeser, Reinhard. Karl G. Maeser. Provo: Brigham Young University, 1928.Packer, Boyd K. Teach Ye Diligently. Salt Lake City: Deseret Book

Company, 1975.Pratt, Parley P. Autobiography of Parley Parker Pratt. Kimehaririwa na Parley

P. Pratt, mdogo. Chapa ya 11. Salt Lake City: Deseret Book Company,1975.

—Key to the Science of Theology. 9th ed. Salt Lake City: Deseret BookCompany, 1966.

Rector, Hartman, na Connie Rector. No More Strangers. Vol. 3. Salt LakeCity: Bookcraft, 1976.

Roberts, B. H. A Comprehensive History of The Church of Jesus Christ ofLatter-day Saints, Century One. 6 vols. Salt Lake City: Kanisa la YesuKristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, 1930.

Smith, Joseph. Teachings of the Prophet Joseph Smith. Yaliyochaguliwa naJoseph Fielding Smith. Salt Lake City: Deseret Book Company, 1938.

Smith, Joseph F. Gospel Doctrine. 5th ed. Salt Lake City: Deseret BookCompany, 1939.

Smith, Joseph Fielding. Doctrines of Salvation. 3 vols. Kimetungwa na

253

Page 263: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Bruce R. McConkie. Salt Lake City: Bookcraft, 1954–56.Widtsoe, John A. Evidences and Reconciliations. 3 vols. in 1. Kupangwa na

G. Homer Durham. Salt Lake City: Bookcraft, 1946.Woodruff, Wilford. The Discourses of Wilford Woodruff. Kimetungwa na G.

Homer Durham. Salt Lake City: Bookcraft, 1946.Young, Brigham. Discourses of Brigham Young. Yaliyochaguliwa na John

A. Widtsoe. Salt Lake City: Deseret Book Company, 1941.

254

Page 264: Wajibu na Baraka za Ukuhani

255

Kielelezo

AAdam

abatizwa, 8watoto wa, kutumia uwakala, 10fukuzwa kutoka Bustani ya Edeni, 8Kanisa lililoundwa, 9, 10pokea ukuhani, 8alifundisha injili kwa watoto wake, 9, 10

Afya, maumbilemafao ya,, 171kutunza, 171–77maelezo juu ya, na Brigham Young,

177maelezo juu ya, na David O. McKay,

121Ajira

kuendeleza na kuboresha, ujuzi,162–70

uzoefu wa, na Heber J. Grant, 169baraza kusaidia kupata, 163maelezo juu ya, na Howard W. Hunter,

163kuchagua, 162–67

Akiba, na utawala wa fedha, 148Askofu

uteuzi wa, 56kazi za, 57–58

kimwili, fafanuliwa na Thomas S.Monson, 57–58

BBaba

baraka kwa, 86–88kushauriana na wanafamilia, 90–96

maelezo juu ya, na ElRay L.Christensen, 93–96

maelezo juu ya, na Richard L.Evans, 96

wajibu wa, kwa ustawi wa familia, 83–89Baba mkuu, afisi ya ukuhani wa, 67–74

maelezo juu ya, na Joseph Smith, 67Baraka za Kibaba mkuu, 68–69

maelezo juu ya, na Eldred G. Smith, 68

maelezo juu ya, na John a. Widtsoe, 70maelezo juu ya, na Joseph Smith, 67maelezo juu ya, na Joseph F. Smith,

67Baraka, kibaba mkuu. Tazama Baraka za

Kibaba mkuuBaraka kutegemea na utii, 67

maelezo juu ya, na Joseph FieldingSmith, 67

Baraza la ukuhanikufanya sehemu yetu kama washiriki

wa, 25–26maelezo juu ya, na J. Reuben Clark,

mdogo, 26–29hadithi inayoelezea, na Vaughn J.

Featherstone, 26–29namna, kazi, 24

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,25

maelezo juu ya, na David O.McKay, 24

maelezo juu ya, na Harold B. Lee,24–25

maelezo juu ya, na Stephen L.Richards, 25

madhumuni ya, 23–30Batiza

kazi ya kuhani ku, 47–51Burudani, umuhimu wa, kwa afya ya mwili,

174maelezo juu ya, na Brigham Young,

174–77Bustani ya Eden, Adamu na Eva

wafukuzwa kutoka, 8

CChakula, umuhimu wa, kwa afya ya mvili,

179

DDanieli, 11Deni na utunzaji wa fedha, 198

maelezo juu ya, na Ezra Taft Benson,198

Page 265: Wajibu na Baraka za Ukuhani

256

EEliya, 11Enoki alianzisha Sayuni, 10Eva alifukuzwa toka Bustani ya Edeni, 8Ezekieli, 11

FFamilia

baraka kwa, 86–88mabaraza na utunzaji wa fedhe,

149–51milele, 245–52

kujenga, 249–51kujitayarisha kuwa, 245–49maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 249baba kushauriana na, waumini, 90–96

maelezo juu ya, na ElRay L.Christiansen, 93–98

maelezo juu ya, na Richard L.Evans, 96

baba anawajibika kwa mahitaji ya,83–89

fedha, 147–51nyumbani jioni, 107sala

baraka za, 100, 108baba kuongoza, 97–102ni msaada katika kushinda

vishawishi, 97–99kufanya, kazi katika nyumba,

99–100maelezo juu ya, na Heber J. Grant,

100maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 97, 100matatizo, kuyamaliza kwa amani, 140–46

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,142

maelezo juu ya, na Spencer W.Kimball, 142–44

uhusiano, wajibu wa wenye ukuhani wa Melkizedeki, 65

kutoafikiana katikauzoefu na, wa Joseph Smith, 140chanzo cha, 140–42imarishwa kwa sala na kufunga,

221hadithi inayoelezea, na M. Russell

Ballard, Mdogo. 223

utendaji wa, na makuhani wenye haki,6

Fedhautawala, 147–51maelezo juu ya, na Brigham Young,

149maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 147Fedha, familia, 147–51Fomu ya bajeti, 150Fundisha

kazi ya kuhani ku, 49–50kuwapenda wale tunao wa, 117–18

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,117

kujitayarisha kwa, injili, 114–17hatua katika, orodheshwa na David

O. McKay, 117ushuhuda hutupa nguvu ya, 130

iliyoelezewa katika hadithi na AlvinR. Dyer, 130

Funga kwa ajili ya ushuhuda, 186–87Funguo

ya uraisi wa ukuhanishikiliwa na maraisi wote wa Kanisa,

8ulipokelewa na Adamu, 8

za baraka za kiroho na nguvu zilizoshikiliwa na Ukuhani wa Melkizedeki,66 Sheria

Viongozi wa Ukuhani wa Melkizedekiyawapasa kuheshimu, kutii nakuikubali, 64

HHaki

hitajika kwa nguvu za baraza laukuhani, 25

hitajika kwa kupata nguvu za ukuhani, 3Haruni, Kaka wa Musa, 11Huduma ya jamii, 174–84

nikazi ya wenye ukuhani waMelkizedeki, 67

wajibu wa kibinafsi kwa, 174–83maelezo juu ya, na David O. McKay,

178Huduma ya Kanisa kazi ya mwenye

Ukuhani wa Melkizedeki, 67Huduma ya usitawi, wajibu wa mwenye

Ukuhani wa Melkizedeki, 65

Page 266: Wajibu na Baraka za Ukuhani

IImani. Tazama Yesu Kristo, imani katikaInjili

kujitayarisha kufundisha, 114–17maelezo juu ya, na David O.

McKay, 114hutua katika, orodheshwa na David

O. McKay, 117fundishwa na Adamu kwa watoto

wake, 10Israeli

wazao wa Yakobo wajulikana kamawatoto wa, 11

jina la Yakobo lilibadilishwa kuwa, 11Ukuhani wa Melkizedeki umechukuliwa

kutoka kwa watoto wa, 11

KKaini, 10Kanisa la Yesu Kristo

lilianzishwa na Yesu, 11kuhani msingi wa, 11

Kazini amri na baraka, 148, 162, 173tabia, 168

Kazi ya umisionari, wajibu wa mwenyeUkuhani wa Melkizedeki, 62

Kazi ya hekalu, wajibu wa mwenyeUkuhani wa Melkizedeki, 61

Kipindicha utimiklifu wa nyakati, alichopewa

Joseph Smith, 11kibaba mkuu, 11

Kristo. Tazama Yesu KristoKufundisha nyumbani

kazi ya mwenye Ukuhani waMelkizedeki, 61

kazi ya mwalimu katika Ukuhani waHaruni, 39–46

nguvu ya, maelezo juu ya, na H. BurkePeterson, 42–43

Kufundishakatika Kanisa, 112–14

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,112-19

umuhimu wa, 119maelezo juu ya, na David O.

McKay, 118maelezo juu ya, na Vaughn J.

Featherstone, 118

kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, 127–32maelezo juu ya, na A. Theodore

Tuttle, 127maelezo juu ya, na Brigham Young,

117–18maelezo juu ya, na David O.

McKay, 127kujitayarisha kwa ajili ya, 110–18

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer, 112, 117–18

maelezo juu ya, na David O.McKay, 114–17

maelezo juu ya, na Thomas S.Monson, 113–14

kutoka kwenye maandiko matakatifu,119–26

mfano wa, na Spencer W. Kimball,122

maelezo juu ya, na J. Reuben Clark,119

maelezo juu ya, na Joseph Smith,122

maelezo juu ya, na Marion G.Romney, 125

pamoja na Roho, 117katika ulimwengu, 114

Kufunga, 221–27na agano la ubatizo, 209hadithi inayoelezea nguvu ya, na Ezra

Taft Benson, 225hadithi inayoelezea nguvu ya, na

Matthew Cowley, 224–25Kuhani mkuu, kazi za, 61–66, ?Kuhani, kazi za, 47–55Kujifunza

nyumba kituo cha injili, 103–09maelezo juu ya, na Marion G.

Romney, 103–04kitabu cha mwongozo muhimu kwa

kujua kazi za ukuhani, 2maandiko matakatifu muhimu kwa

kujua mapenzi ya Mungu, 5Kujifunza, kutengeneza mazingira kwa,

katika nyumba, 104maelezo juu ya, na David O. McKay,

104Kujitegemea, maelezo juu ya, na Spencer

W. Kimball, 154Kukuza miito ya ukuhani, 51–53

maelezo juu ya makuhani

257

Kielelezo

Page 267: Wajibu na Baraka za Ukuhani

258

na Victor L. Brown, 53na Wilford Woodruff, 54

Kusalimia Kanisani kazi ya mwalimu katikaukuhani wa Haruni, 43

Kutoa mimba, 241Kutumia na utawala wa fedha, 148Kuwasaidia wengine na agano la ubatizo,

211

MMaadili ya usafi, 240–45

ukuhani nguvu katika, 242–44maelezo juu ya, na A. Theodore Tuttle,

243maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,

240–41maelezo juu ya, na Gordon B.

Hinckley, 243–44maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 243hadithi inayoelezea kupotea kwa, na

Spencer W. Kimball, 243Maandiko Matakatifu

maelezo juu ya, na Bruce R.McConkie, 109

mafunzo yakatika nyumba, 105hitajika kwa kujua mapenzi ya

Mungu, 5hitajika kwa kupokea ushuhuda,

186–87maelezo juu ya, na H. Burke

Peterson, 107maelezo juu ya, na Joseph Smith,

187kufundisha kutoka, 119–26

mfano wa, na Spencer W. Kimball,122

maelezo juu ya, na Harold B. Lee,124

maelezo juu ya, na J. Reuben Clark,119

maelezo juu ya, na Marion G.Romney, 125

Mababa mkuu wa kipindi cha kibabamkuu, 10

Mamlaka, safu ya ukuhani, 2, 8, 12Manabii kati ya wakati wa Musa na wakati

wa Yesu Kristo, 11

Matoleo ya mfungo, 31–32Mazoezi, umuhimu wa, kwa afya ya mwili,

174Melkizedeki, 10Melkizedeki Ukuhani. Tazama Ukuhani,

MelkizedekiMfano

umuhimu wa, 134wenye ukuhani kuonyesha, 5–6, 39

Miadi, mwongozo kwa, na Spencer W.Kimball, 243

Mikutano, kuhudhuria Kanisa, 209Mitume

tawazwa na Yesu, 11Familia la Kumi na Wawili, 77

Msaadakwa wenye dhiki kazi ya mafamilia ya

ukuhani, 25taarifa juu ya, na Harold B. Lee,

24–25taarifa juu ya, na J. Reuben Clark,

Jr., 26hadithi inayoelezea, na Vaughn J.

Featherstone, 26–29Mtengeneza amani, akiwa ni, kazi ya

mwalimu katika ukuhani wa Haruni,40–43

Mungualitoa ukuhani kwa Adamu, 8ni chanzo cha nguvu ya ukuhani, 3ukuhani ni nguva ya, 1mapenzi ya, hujulikana kwa sala, 5mapenzi ya, hujulikana kwa kujifunza

maandiko matakatifu, 5hufanya kazi kupitia Roho Mtakatifu, 3

Musaaliwaongoza watoto wa Israeli kutoka

Misri, 11alipokea sheria na ibada, 11

Mwalimu, Ukuhani wa Haruni, kazi ya,39–46

Mwili, maumbile, maelezo ya, na BrighamYoung, 171

Mzee, kazi za, 61–66

NNasaba, wajibu wa mwenye ukuhani wa

Melkizedeki, 62

Page 268: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Nchiwajibu kwa, 182–83

maelezo juu ya, na Harold B. Lee,183

huduma kwa, 178–84maelezo juu ya, na David O. McKay,

178Ndoa, milele, 245–51. Tazama pia

Familia, milelemaelezo juu ya, na Joseph Fielding

Smith, 245Neno la Hekima

baraza za kutii, 172–73hukataza vitu fulani, 172

Nyumbakituo cha kujifunza injili, 103–09

maelezo juu ya, na Marion G.Romney, 103–04

kutoafikiana katika, chanzo cha,140–42

kaafikiana katika, 90, 96maelezo juu ya, na David O. McKay,

96kusaidia

kazi ya mwalimu katika ukuhani waHaruni, 40–43

maadili, maelezo juu ya na Joseph F.Smith, 140

mwenye ukuhani huongoza katika, 90wajibu wa mwenye Ukuhani wa

Melkizedeki, 61

PPumzika, umuhimu wa, kwa afya ya mwili,

173

RRaisi wa tawi, utenzi wa. Tazama Askofu,

uteuzi wa, 56–57Raisi wa tawi, kazi za. Tazama, Askofu,

kazi zaRoho Mtakatifu

Mungu hufanya kazi kupitia, 3msaada wa, 217–18

maelezo juu ya, na Franklin D.Richards, 217–18

maelezo juu ya, na Heber J. Grant,218–19

maelezo juu ya, na Henry D. Moyle,219

kupata mwongozo wa, 128

maelezo juu ya, na Marion G.Romney, 128

kufundisha kwa nguvu ya, 127–28maelezo juu ya, na A. Theodore

Tuttle, 127maelezo juu ya, na David O.

McKay, 127Roho Mtakatifu, kipawa cha, 214–20

kushika, 216–17maelezo juu ya, na Joseph Smith,

216maelezo juu ya, na Joseph Fielding

Smith, 217maelezo juu ya, na Melvin J.

Ballard, 216maelezo juu ya; na LeGrand Richards,

216maelezo juu ya, na Lorenzo Snow, 214

Roho, kufundishwa pamoja na, 117.Tazama pia Roho Mtakatifu

SSabini

Mabaraza ya, 77Sakramenti

na agano la ubatizo, 209–11kazi ya kuhani kusimamia, 50na kipawa cha Roho Mtakatifu, 216matayarisho ya

kazi ya mwalimu katika ukuhani waHaruni, 39

utakatifu wa, maelezo juu ya, na VictorL. Brown, 32

Sala, 221–26na agano la upatizo, 208familia. Tazama Familia, sala

Salikwa maongozi ya kutumia ukuhani

ipasavyo, 5kwa kujua mapenzi ya Mungu, 5kwa ushuhuda, 192

Sayuniya Enoki, aliochukuliwa mbinguni, 10anzishwa na Enoki, 10

Shemasikazi za, 30–38

maelezo juu ya, na Victor L. Brown,30, 32

namna baraza la mashemasilinavyosaida, 36–37

259

Kielelezo

Page 269: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Smith, Josephalitawazwa na Yohana Mbatizaji, 18alitawazwa na Petro, Yakobo na

Yohana, 2, 18–20ukuhani ulirejeshwa kupitia, 12–14,

18–22Staha

kufundisha, katika nyumba, 133–36maelezo juu ya, na A. Theodore

Tuttle, 135maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,

133, 135maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 227maelezo juu ya, na Vaughn J.

Featherstone, 134

TTaifa, utumishi kwa, 178–83

maelezo juu ya, na David O. McKay,178–79

Tamaa ni muhimu kwa ajili ya kupatanguvu katika ukuhani, 3

Tawaza katika ukuhani wa Haruni, kazi yakuhani ku, 51

Tembelea waumini, kazi ya kuhani ku, 48Tiba, umuhimu wa, kwa afya ya mwili, 174Toba, 199–205

na agano la ubatizo, 218furaha ya, 200–04haja ya, 199

maelezo juu ya, na Joseph FieldingSmith, 199

maelezo juu ya, na Harold B. Lee, 205maelezo juu ya, na Joseph Smith, 199

Tubu, namna ya ku, 199–200maelezo juu ya, na A. Theodore Tuttle,

200

UUasi, 10

mkuu wa kwanza, 10mkuu, 12, 115–17

Uaskofu Msimamizi, 77Ubasha, 249Ubatizo

agano la, 206–13maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 206kuendelea baada, 208–11

Ufadhili. Tazama UpendoUhuru, maelezo juu ya na Spencer W.

Kimball, 154Ukamilifu, njia ya, 211–12

maelezo juu ya, na Spencer W.Kimball, 211

Ukuhani, Melkizedek, 10ulitolewa kwa Joseph Smith na Oliver

Cowdery, 20–21ulitolewa kwa Isaka na Ibrahim, 11ulitolewa kwa Yakobo na Isaka, 11ulishikiliwa na manabii kutoka Musa

mpaka Yesu Kristo, 11uliitwa kwa mtu Melkizedeki, 11nguvu na kazi za, 20uliondolewa katoka kwa wana wa

Israeli, 11Ukuhani, Haruni

ulitolewa kwa Joseph Smith na OliverCowdery, 18–20

uliitwa kwa ajili ya Haruni, kaka yaMusa, 18

nguvu na kazi za, 18–20UkuhaniAdamu alipokea, 8

mamlaka na nguvu, 1–2mwenye nao huongoza katika nyumba,

90mwenye nao kumpenda na

kushauriana pamoja na mke wake,90–93

katika nyakati za Kitabu cha Mormoni,11

katika siku za Yesu, 11maelezo juu ya, na J. Reuben Clark,

mologu, 90–91baada ya mafuriko, 10historia ya, 8–14mwenye, aweza kubadilisha nyumba, 3

maelezo juu ya, na David O.McKay, 5

mwenye, kuonyesha mfano, 5–6ni nguvu ya Mungu, 1

maelezo juu ya, na Harold B. Lee, 1maelezo juu ya, na Joseph Fielding

Smith, 1–2funguo za

zilitumiwa katika utimilifu na Rais waKanisa tu, 8

shikiliwa na Adam, 8

260

Page 270: Wajibu na Baraka za Ukuhani

safu ya mamlaka, 2potezwa na Kanisa katika uasi mkuu, 12kukuza

maelezo juu ya, na Joseph FieldingSmith, 29

maelezo juu ya, na WilfordWoodruff, 51

nguvu itokayo kwa Mungu, 2nguvu itokanayo na kuishi maisha ya

haki, 2nguvu ya, kuendelea, 3–6

maelezo ya, na A. Theodore Tuttle,243

nguvu ya, iliyojengeka juu ya upendo, 5maelezo juu ya, na H. Burke

Peterson, 2nguvu ya, na usafi wa kimaadili,

242–44nguvu ya, maelezo juu ya, na N. Eldon

Tanner, 6madhumuni ya, maelezo juu ya, na H.

Burke Peterson, 3urejeshowa, 15–22

kupitia Joseph Smith, 12, 17–21maelezo juu ya, na Joseph F. Smith,

75–77ustahili wa kushika, maelezo juu ya, na

N. Eldon Tanner, 6Ulinzi kwa watumishi wa Bwana, hadithi

inayoelezea, na Wilford Woodruff, 54Umisionari

kazi ya kuhani kuwa, 51yeye matokeo mazuri, kazi ya kuhani

kijitayarisha kuwa, 53–54maelezo juu ya, na Spencer W.

Kimball, 54Umoja ni muhimu kwa utendaji wa kazi wa

baraza la ukuhani, 23–24Unyenyekevu, maelezo juu ya na Spencer

W. Kimball, 227–32Unyenyekevu, muhimu kwa kupata nguvu

za ukuhani, 3Uongofu, wajibu wa mwenye ukuhani wa

Melkizedeki, 61Upendo

amri kwa, 232maelezo juu ya, na H. Burke

Peterson, 238maelezo juu ya, na N. Eldon

Tanner, 233

maelezo juu ya, na Spencer W.Kimball, 238

nguvu za ukuhani zilizojengwa juu ya,wa wengine, 5

na utumishi, 232–39maelezo juu ya, na David O. McKay,

238maelezo juu ya, na Mark E. Petersen,

235maelezo juu ya, na Theodore M.

Burton, 235wa wake na watoto, 3

Upigaji Pusu, 243Urafiki

shughuli ya mabaraza ya ukuhani,24–25

maelezo juu ya, na Stephen L.Richards, 25

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,25

Uraisi wa ukuhani, fungo za, shikiliwa namaraisi wote wa Kanisa, 8

Uraisi wa Kwanza, 75–78Urejesho wa ukuhani, 15–22Usafi, umuhimu kwa maumbile yenye

afya, 173Usafi wa Kimwili. Tazama usafi wa maadiliUshuhuda wa injili, 185

uliofafanuliwa, 185maelezo juu ya, na Harold B. Lee,

185hutupa nguvu ya kufundisha, 130

iliyoelezewa katika hadithi na AlvinR. Dyer, 130

wazazi yawapasa kutoa, kwa watoto,102

kupokea, 186–87maelezo juu ya, na Joseph Smith,

187maelezo juu ya, na Loren C. Dunn,

186maelezo juu ya, na Parley P. Pratt,

186kuimarisha, 187–89

maelezo juu ya, na Harold B. Lee,187

Ustahili wa kuwa na ukuhani,maelezo juu ya, na N. Eldon Tanner, 6

Utaratibu wa kibaba mkuu wa ukuhani, 10

261

Kielelezo

Page 271: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Utawala usio wa hakijuu ya wake, utumiaji mbaya wa

ukuhani, 91maelezo juu ya, na David O.

McKay, 24Utii, baraka zinazotegemea, 70

maelezo juu ya, na Joseph FieldingSmith, 70

Utumishi, kama Kristo, 235–38maelezo juu ya, na David O. McKay, 238maelezo juu ya, na Harold B. Lee,

235–36maelezo juu ya, na Thomas S.

Monson, 236Utumishi wa baraza kazi ya wenye

Ukuhani wa Melkizedeki, 61Utunzaji wa meno, umuhimu wa, kwa afya

ya mwili, 174Uwakala, 10

ulifanywa na watoto wa Adam, 10Uzalishaji nyumbani na hifadhi, 154–61

maelezo juu ya, na Spencer W.Kimball, 84, 154, 158

maelezo juu ya, na Vaughn J.Featherstone, 156

Uzinzi, 241

VViongozi Wakuu

haja ya, 75–82iliyoelezewa katika hadithi

inayomshirikisha David O. McKay,78–80

wajibu wa, 77–78maelezo juu ya, na Harold B. Lee, 81kuwakubali, 80

Viongozi wa ukuhaniumuhimu wa kuunga mkono, 59

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,59

uradhi wa kufuata, muhimu kwa kupatanguvu za Ukuhani, 3

WWake

wenye ukuhani kuwapenda nakushauriana pamoja na, 91–96

maelezo juu ya, na J. Reuben Clark,Jr., 90–91

utawala usio wa haki juu ya, nimatumizi mabaya ya ukuhani, 91

Watotowazazi yawapasa kutoa ushuhuda

kwa, 107wazazi yawapasa kushauriana pamoja

na, 90–96maelezo juu ya, na ElRay L.

Christiansen, 93–96maelezo juu ya, na Richard L.

Evans, 96Wazazi

yawapasa kushauriana pamoja nawatoto, 93

maelezo juu ya, na ElRay L.Christiansen, 93–96

maelezo juu ya, na Richard L.Evans, 96

Wema, kufundisha, katika nyumba,138–39

maelezo juu ya, na A. Theodore Tuttle,135

maelezo juu ya, na Boyd K. Packer,135

maelezo juu ya, na Spencer W.Kimball, 133–34

maelezo juu ya, na Vaughn J.Featherstone, 134

YYakobo, 11Yesu Kristo, imani katika, 190–198

huwezesha watu kujitolea muhanga,190

kanuni ya kwanza ya injili, 196maelezo juu ya, na Brigham Young,

164hadithi kuielezea, na Marion G.

Romney, 103kuimarisha, 192–198

Yesu Kristoalishikilia funguo za ukuhani, 11aliwatawaza mitume, 2, 11alianzisha Kanisa, 11alirejesha utimilifu wa injili, 12

ZZaka, na utunzaji wa fedha, 147–49

262

Page 272: Wajibu na Baraka za Ukuhani
Page 273: Wajibu na Baraka za Ukuhani

264

Mahekalu na Majengo

1. Hekalu la Salt Lake

2. Hekalu la Provo

3. Hekalu la Mto Yordai

4. Hekalu la Washington

5. Hekalu la Arizona

6. Hekalu la Ogden

7. Hekalu la Logan

8. Hekalu la São Paulo

9. Hekalu la Hawaii

10. Hekalu la Tokyo

11. Hekalu la Uswizi

12. Hekalu la Los Angeles

13. Hekalu la Mt. George

14. Hekalu la Maporomoko ya Idaho

15. Hekalu la Oakland

16. Helaku la London

17. Hekalu la Alberta

18. Hekalu la New Zealand

19. Hekalu la Seattle

20. Hekalu la Manti

21. Hekalu la Samoa

22. Kisima cha ubatizo cha hekalu la Oakland

23. Chumba cha Selestia cha hekalu la Provo

24. Chumba cha kuunganishia cha hekalu la Arizona

25. Chumba cha kuunganishia cha hekalu la Salt Lake

26. Chumba cha mbinguni cha hekalu la Salk Lake

27. Hekalu la Herodi katika Yerusalemu ya kale (jiji la mfano)

28. Jengo la afisi za Kanisa katika jiji la Salt Lake

29. Jengo la afisi za utawala la Kanisa katika jiji la Salt Lake

30. Mlima wa Matale uliokumbukumbu ya njia ya chini ya ardhi karibu na jijia Salt Lake

31. Nyumba za mikutano za WSM (Watakatifu wa Siku za Mwisho) koteulimwenguni

Page 274: Wajibu na Baraka za Ukuhani

12 3

Page 275: Wajibu na Baraka za Ukuhani

4

65

Page 276: Wajibu na Baraka za Ukuhani

78 9

Page 277: Wajibu na Baraka za Ukuhani

1110

12

Page 278: Wajibu na Baraka za Ukuhani

13

1514

Page 279: Wajibu na Baraka za Ukuhani

1617 18

Page 280: Wajibu na Baraka za Ukuhani

20 21

19

Page 281: Wajibu na Baraka za Ukuhani

22

Page 282: Wajibu na Baraka za Ukuhani

23

Page 283: Wajibu na Baraka za Ukuhani

2524

Page 284: Wajibu na Baraka za Ukuhani

26

Page 285: Wajibu na Baraka za Ukuhani

27

Page 286: Wajibu na Baraka za Ukuhani

28

Page 287: Wajibu na Baraka za Ukuhani

29

Page 288: Wajibu na Baraka za Ukuhani

30

Page 289: Wajibu na Baraka za Ukuhani

3132 33

Page 290: Wajibu na Baraka za Ukuhani

Majukumu na Baraka za Ukuhani

Kitabu cha Msingi cha Mwongozo kwa wenye ukuhani, Sehemu ya A

Sehemu ya A

Kitabu cha M

singi cha Mw

ongozo kwa w

enye ukuhani