1
HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, MHESHIMIWA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO WA
MAENDELEO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA
KWA MWAKA 2013/2014
A. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, baada ya Bunge
lako Tukufu kupokea taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2012/13.
Aidha, naomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2013/2014. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote
napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru
Mwenyezi Mungu kwa kunilinda na kunipa nguvu ya kutekeleza majukumu yangu na kuniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha bajeti hii. 3. Mheshimiwa Spika, kwa heshima na
taadhima nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
2
kuendelea kuiongoza nchi yetu vyema na kwa utekelezaji mahiri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 pamoja na mipango na programu mbalimbali za kuiletea nchi yetu
maendeleo. Mheshimiwa Rais amekuwa mstari wa mbele katika kutafuta fedha za kutekeleza miradi iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ambayo pia inajumuisha barabara. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu kwa jinsi ambavyo wamemsaidia Mheshimiwa Rais kusimamia na kuongoza shughuli zote za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
4. Mheshimiwa Spika, naomba
nikupongeze wewe binafsi, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa hekima, umahiri na busara mnazotumia katika kuliongoza Bunge hili Tukufu. Namwomba Mwenyenzi Mungu azidi
kuwajalia busara na hekima katika kazi hiyo.
5. Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kutoa pole kwa kifo cha ghafla cha Mhe. Mbunge mwenzetu Hayati Salim Hemed Khamis, Mbunge wa Chambani kwa
tiketi ya CUF. Naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kutoa pole kwa familia, wewe Mhe. Spika, Bunge lako tukufu, ndugu,
3
jamaa na marafiki wa marehemu na wananchi wote wa Jimbo la Chambani. Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.
6. Mheshimiwa Spika, napenda nichukue
fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Peter Joseph Serukamba, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini na Mheshimiwa Athumani Juma Kapuya, Mbunge wa Jimbo la Urambo Magharibi kwa
kuteuliwa kuiongoza Kamati ya Bunge ya Miundombinu. Vile vile nawapongeza wajumbe wote wapya walioteuliwa kuunda Kamati ya Bunge ya Miundombinu. Ushauri wa Kamati na Wabunge wote kwa ujumla utaendelea kuzingatiwa katika utekelezaji wa majukumu ya
kila siku ya Wizara ya Ujenzi ili kuiletea nchi yetu maendeleo.
7. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na
Waheshimiwa Wabunge wenzangu, katika kumpongeza na kumshukuru Waziri Mkuu,
Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Mbunge wa Jimbo la Katavi kwa hotuba yake ambayo imetoa mwelekeo wa jumla katika masuala ya Mipango na Uchumi kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014. Naomba pia kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge waliochangia hotuba hiyo.
Ni matumaini yangu kuwa maoni yao yatasaidia kuboresha mipango ya Serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Ujenzi.
4
DIRA NA DHIMA YA WIZARA 8. Mheshimiwa Spika, Dira ya Wizara ni
kuwa na Barabara, Madaraja, Vivuko, Nyumba
za Serikali na Huduma za Ujenzi zenye ubora wa kiwango cha juu, zenye gharama nafuu na zinazozingatia usalama na utunzaji wa mazingira. Aidha, dhima ya Wizara ni kuwa na Barabara, Vivuko, Nyumba za Serikali na Huduma za Ujenzi zilizo na uwiano na ambazo
zinakidhi mahitaji kwa viwango bora na kwa bei nafuu zinazoendana na mikakati ya Serikali ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii na wakati huo huo zikiwa endelevu kiuchumi na kimazingira. MAJUKUMU YA WIZARA 9. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi ina
majukumu ya kusimamia Sera za ujenzi na usalama barabarani; ujenzi na matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko; ujenzi na
ukarabati wa majengo ya Serikali; pamoja na masuala ya ufundi na umeme. Aidha, Wizara inasimamia shughuli za usajili wa makandarasi, wahandisi, wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi; masuala ya usalama barabarani na mazingira katika sekta; uboreshaji utendaji na
uendelezaji wa watumishi wa Wizara; pamoja na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi zilizo chini ya Wizara.
5
MALENGO YA WIZARA 10. Mheshimiwa Spika, katika kufanikisha
utekelezaji wa majukumu yake, Wizara imelenga
kujenga barabara ili kufungua fursa za maendeleo na kuhakikisha miji yote mikuu ya mikoa inaunganishwa kwa barabara za lami ifikapo mwaka 2017/18; kufanya matengenezo ya barabara kuu na za mikoa; kujenga barabara za kupunguza msongamano wa magari mijini
hususan katika Jiji la Dar es Salaam; kuhakikisha kuwa usafiri wa vivuko unaimarishwa katika maeneo yote yanayohitaji huduma hiyo; na kusimamia ujenzi wa nyumba za Serikali na watumishi. Aidha, Wizara itaendelea kusajili na kusimamia Makandarasi,
Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kwa kutumia bodi husika pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kuvutia sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya Ujenzi. Wizara pia itaendelea kusimamia masuala ya usalama na mazingira katika barabara na vivuko pamoja
na kufanya matengenezo na ukarabati wa Magari ya Serikali na Mitambo. Vile vile Wizara itaendelea kushirikiana na taasisi husika katika kushughulikia masuala mtambuka kama vile kampeni za kupunguza maambukizi ya ugonjwa hatari wa UKIMWI, uhifadhi wa mazingira,
masuala ya jinsia pamoja na uendelezaji wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na
6
Mawasiliano (TEHAMA) katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Serikali.
MIKAKATI YA WIZARA KATIKA KUFIKIA MALENGO 11. Mheshimiwa Spika, ili kuweza
kutekeleza malengo yake, Wizara itaendelea kuzingatia kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa mwaka 2011/12 – 2015/16,
Ahadi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA). Aidha, Wizara ya Ujenzi inazingatia utekelezaji wa Programu ya
Uwekezaji katika Sekta ya Miundombinu ya Usafirishaji (Transport Sector Investment Program – TSIP) ambayo ni programu ya miaka kumi (2006/07-2016/17) inayolenga kuimarisha na
kuboresha miundombinu ya usafirishaji. Wizara inatekeleza Sera ya Taifa ya Ujenzi (2003), Sera ya Usalama Barabarani (2009) na Sera ya Ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP). Wizara pia itaendelea kusimamia utoaji elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya barabara kwa mujibu wa Sheria ya Barabara
Na. 13 ya mwaka 2007 pamoja na sheria nyingine ili miundombinu ya barabara iweze kutunzwa na kudumu kwa muda uliokusudiwa. Wizara vile vile itaboresha mfumo wa upimaji
7
magari ya mizigo kwa kuweka mizani itakayopima uzito wa magari yakiwa kwenye mwendo (weigh-in-motion) kwa lengo la kuzuia uharibifu wa barabara kutokana na magari
yanayozidisha mizigo. 12. Mheshimiwa Spika, mikakati mingine ni
pamoja na kusimamia fedha za Mfuko wa Barabara zinazopelekwa Mikoani ili kazi za matengenezo ya barabara zinazotekelezwa
zilingane na thamani ya fedha (value for money). Wizara pia itaendelea kutafuta vyanzo vipya ili kupanua wigo wa Mfuko wa Barabara. Aidha, Wizara itaendelea kuzifanyia marekebisho sheria za kisekta ili ziweze kuendana na mazingira ya sasa na kufikia viwango vinavyokubalika
kimataifa na kikanda kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Kusini mwa Afrika. Wizara itahakikisha kuwa Makandarasi, Wahandisi Washauri na Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi wa kizalendo wanahusishwa kikamilifu katika ujenzi wa
miradi mikubwa hususan miradi ya barabara, madaraja, nyumba na vivuko inayogharamiwa na Serikali badala ya kutegemea kampuni za nje. Lengo ni kuwajengea wananchi uzoefu stahili katika Sekta ya Ujenzi na kupunguza kasi na wingi wa fedha zinazotokana na vyanzo
vyetu kuhamishiwa nje ya nchi kwa kulipia kazi za kampuni za nje.
8
B: TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI YA MWAKA 2012/13
Ukusanyaji wa Mapato
13. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13, Wizara ilipanga kukusanya jumla ya Shilingi 15,628,580.00 kupitia Idara zenye vyanzo vya mapato. Idara hizo ni Utawala,
Huduma za Ufundi na Menejimenti ya Ununuzi. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya Shilingi 36,388,193.24 zilikuwa zimekusanywa. Sababu za kukusanya fedha zaidi ikilinganishwa na bajeti iliyopangwa ni kuongezeka kwa makusanyo ya ada za usajili wa vyombo vya
Serikali kufuatia zoezi la kufuta matumizi ya namba za kiraia kwenye magari, pikipiki, bajaj na mitambo ya Serikali na kusajiliwa kwa namba za Serikali. Zoezi hili lilianza tarehe 19 Novemba, 2012 na hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya magari, pikipiki, bajaji na mitambo ya
Serikali iliyosajiliwa kwa namba za Serikali ni 2,268.
Bajeti ya Matumizi ya Kawaida
14. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/13, Wizara ilitengewa kiasi cha Shilingi 329,085,354,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2013, Shilingi
9
257,177,456,588.75 zilikuwa zimetolewa na Wizara ya Fedha kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kiasi hicho ni asilimia 78.15 ya bajeti ya matumizi ya kawaida ya Wizara kwa mwaka
2012/13. Kati ya fedha zilizotolewa, Shilingi 15,490,538,152.00 zilikuwa za Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake, Shilingi 237,811,447,236.75 ni za Mfuko wa Barabara na Shilingi 3,875,471,200.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara, Taasisi na
Wakala. UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA 2012/13
15. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2012/13, Wizara iliidhinishiwa Shilingi 693, 948, 272,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi
296,896,892,000.00 zilikuwa fedha za ndani na Shilingi 397,051,380,000.00 zilikuwa fedha za nje. Hadi kufikia Aprili, 2013, Wizara ilishapokea fedha zote za ndani kiasi cha Shilingi 296,896, 892,000.00 na Shilingi 236,782,437,956.41 za nje.
Utekelezaji wa Miradi ya Barabara na Madaraja
16. Mheshimiwa Spika, nchi ya Tanzania ina mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 87,581. Kati ya hizo, kilometa 35,000
10
ni Barabara Kuu na za Mikoa zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS). Barabara zinazobaki ni za wilaya na zinasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu,
TAMISEMI. Aidha, kuna jumla ya Madaraja 4,880 katika Barabara Kuu na za Mikoa. 17. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ilipanga kukamilisha
ujenzi wa barabara kuu zenye urefu wa kilometa 414 kwa kiwango cha lami, kukarabati kilometa 135 kwa kiwango cha lami pamoja na kujenga na kukarabati madaraja 11. Hadi kufikia Aprili, 2013, ujenzi wa kilometa 374.65 za barabara kuu kwa kiwango cha lami na ukarabati wa
kilometa 140.63 kwa kiwango cha lami ulikamilika. Kuhusu matengenezo ya Barabara Kuu, lengo lilikuwa ni kuzifanyia matengenezo kilometa 10,534.3 na madaraja 1,154. Hadi kufikia Aprili, 2013 kilometa 6,052.8 za Barabara Kuu na madaraja 652 yalifanyiwa
matengenezo. 18. Mheshimiwa Spika, kwa upande
Barabara za Mikoa, Wizara ilipanga kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 31.9, kukarabati kwa kiwango cha changarawe kilometa 573.6 na
ujenzi wa madaraja 27. Hadi kufikia Aprili, 2013, kilometa 8.23 zilijengwa kwa kiwango cha lami, kilometa 198.9 zilifanyiwa ukarabati kwa
11
kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja 8 ulikamilika. Kuhusu matengenezo ya Barabara za Mikoa, Wizara ilipanga kuzifanyia matengenezo barabara zenye urefu wa kilometa
22,482 na madaraja 1,263. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya kilometa 13,459.2 zilikuwa zimekamilika na madaraja 758 yalikuwa yamefanyiwa matengenezo. 19. Mheshimiwa Spika, kazi ya kudhibiti
uzito wa magari iliendelea katika mwaka wa fedha 2012/13 kwa kutumia mizani 26 ya kudumu na 17 inayohamishika katika barabara kuu za lami. Hadi Aprili, 2013 magari yapatayo 2,321,526 yalikuwa yamepimwa ambapo magari
598,074 yalikuwa yamezidisha uzito. Hii ni asilimia 25.76 ya magari yote yaliyopimwa. Jumla ya fedha zilizokusanywa kutokana na tozo ya uharibifu wa barabara na malipo ya kupitisha mizigo mipana na isiyo ya kawaida ilikuwa ni Shilingi 3,913,898,889.45.
20. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza
maandalizi ya kujenga barabara ya Dar es Salaam - Chalinze (Expressway) kwa utaratibu wa ubia kati ya Serikali na Kampuni binafsi. Kufuatia tangazo lililotolewa na Wizara kupitia
TANROADS, Kampuni 19 zimewasilisha mapendekezo ya jinsi ya kujenga barabara hii kwa njia 6 kuanzia Dar es Salaam – Mlandizi na njia 4 kuanzia Mlandizi - Chalinze. Kazi za
12
kuchambua mapendekezo hayo ili kumpata mbia anayeweza kufanya kazi hiyo inaendelea.
21. Mheshimiwa Spika, Mkataba wa
ujenzi wa barabara ya Bagamoyo-Makofia-Msata (km 64) ulisainiwa tarehe 15 Agosti, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 89.608. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 55.4 za tuta la barabara, km 51.2 za tabaka la chini, km 51.2 za tabaka la juu na km 51.2 za lami
zimekamilika.
22. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa barabara ya Usagara – Geita – Bwanga – Buzirayombo – Kyamyorwa (km 422) umegawanyika katika sehemu tatu. Sehemu ya
kwanza ilihusisha ujenzi wa Barabara ya Kyamyorwa - Geita (km 220) ambayo ilikamilika Februari, 2008. Sehemu ya pili ilihusisha ujenzi wa barabara ya Geita - Usagara (km 90) ambapo ujenzi wake ulianza Februari, 2008 na umekamilika Januari, 2010. Sehemu ya tatu
itahusisha ujenzi wa barabara ya Uyovu - Biharamulo kupitia Bwanga (km 112). Mikataba ya ujenzi imesainiwa Oktoba, 2012 na Mkandarasi ameshapeleka vifaa na wataalamu kuanza kazi.
23. Mheshimiwa Spika, Mradi wa barabara wa Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 310.60) unahusisha ujenzi
13
wa Barabara ya Tabora - Urambo (km 94), ujenzi wa daraja la Malagarasi na barabara zake za maingilio (approach roads – km 48), barabara ya Uvinza – Kidahwe (km 76.6), Kigoma- Kidahwe
(km 36) na Kaliua – Kazilambwa (km 56). Aidha, utekelezaji wa miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-
• Tabora-Ndono (km 42):
Gharama za ujenzi wa mradi huu ni Shilingi bilioni 51.35. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 19 za tuta la barabara zimekamilika.
• Ndono-Urambo (km 52):
Gharama za ujenzi wa barabara ya Ndono – Urambo ni Shilingi bilioni 59.77. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 22 za tuta la barabara zimekamilika.
• Kaliua – Kazilambwa (km 50)
Mkataba wa ujenzi kwa sehemu ya Kaliua – Kazilambwa (km 56) umesainiwa tarehe 27 Machi, 2013 na kazi za maandalizi ya ujenzi
zinaendelea.
• Daraja la Kikwete
Kwa upande wa Daraja la Kikwete katika mto Malagarasi na barabara zake za maingilio, mkataba wa usanifu na ujenzi wa mradi huu
ulisainiwa tarehe 21 Oktoba, 2010. Mradi
14
huu unafadhiliwa na Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi (Economic Development Cooperation Fund) wa Korea Kusini. Utekelezaji wa mradi huu
umegawanyika katika awamu mbili; awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa madaraja 3 ambapo moja lina urefu wa meta 200, la pili meta 50 na la tatu meta 25 pamoja na ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 11 kwa kiwango cha lami. Kazi zinafanyika kwa
utaratibu wa Kusanifu na Kujenga (Design and Build). Hadi kufikia Aprili, 2013 kazi za ujenzi wa daraja zimekamilika kwa asilimia 81 na ujenzi wa tuta la barabara, tabaka la chini na tabaka la juu umekamilika. Kwa awamu ya pili inayohusisha ujenzi wa
barabara yenye urefu wa kilomita 37 kwa kiwango cha lami, Serikali ya Korea Kusini imekubali kutoa fedha na Mkataba wa Mkopo wa Nyongeza (Supplementary Loan Agreement) umesainiwa tarehe 11/12/2012. Kazi za ujenzi zimeanza tarehe 4/1/2013.
• Uvinza – Kidahwe (km 76.6)
Mkataba wa ujenzi wa barabara ya Uvinza – Kidahwe (km 76.6) ulisainiwa tarehe 24 Juni 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 78.241. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 74 za tuta
la barabara, km 73 za tabaka la chini, km 72 za
15
tabaka la juu na km 70.18 za lami zimekamilika. 24. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara
ya Marangu-Rombo Mkuu na Mwika-Kilacha (km 32), mkataba ulisainiwa tarehe 13 Mei, 2008 kwa gharama ya Shilingi bilioni 25.075. Hadi kufikia Aprili 2013, jumla ya km 32 za tuta la barabara, km 32 za tabaka la chini, km 32 za tabaka la juu na km 29.3 za lami zimekamilika.
Kwa barabara Sanya Juu (Siha) – Kamwanga (km 75), taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea.
25. Mheshimiwa Spika, mkataba wa ujenzi wa barabara ya Nangurukuru –
Mbwemkulu (km 95) ulisainiwa tarehe 14 Mei 2003 kwa gharama ya shilingi bilioni 39.239 na ulikamilika mwaka 2008. Hata hivyo Wizara ya Ujenzi haikupokea mradi huu kwa kuwa haukukamilika kwa kiwango kilichokusudiwa na hivyo kuwepo kwa marekebisho
yanayohitajika kufanyika. Kazi ya kufanya marekebisho imekamilika na mradi umepokelewa na Wakala wa Barabara tarehe 21 Februari, 2013.
26. Mheshimiwa Spika, mkataba wa ujenzi
kwa kiwango cha lami wa barabara ya Dodoma – Manyoni (km 127) ulisainiwa tarehe 12 Machi, 2003 kwa gharama ya shilingi bilioni 63.888.
16
Ujenzi wa barabara hii ulikamilika tarehe 22 Novemba, 2009 na kipindi cha uangalizi cha miaka mitatu kiliisha Novemba, 2012 na mradi umepokelewa na TANROADS.
27. Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi
wa barabara ya Dumila – Kilosa (km 63) kwa kiwango cha lami umegawanywa katika sehemu mbili; Dumila – Rudewa (km 45) na Rudewa - Kilosa (km 18). Utekelezaji wa sehemu hizi mbili
ni kama ifuatavyo:
• Dumila-Rudewa (km 45):
Mkataba wa ujenzi ni wa gharama ya Shilingi bilioni 41.929. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla
ya km 44.72 za tuta la barabara, km 31.85 za tabaka la chini, km 0.3 za tabaka la juu na km 0.3 za lami zimekamilika.
• Rudewa-Kilosa (km 18):
Usanifu umekamilika na Serikali inaendelea na
juhudi za kutafuta fedha za ujenzi.
28. Mheshimiwa Spika, mkataba wa ujenzi kwa upande wa mradi wa barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga Port (km 112) ni wa Shilingi bilioni 133.286. Hadi kufikia Aprili,
2013, jumla ya km 38 za tuta la barabara, km
17
27 za tabaka la chini, km 12 za tabaka la juu na km 12 za lami zimekamilika.
29. Mheshimiwa Spika, mkataba wa
mradi wa upanuzi wa barabara ya Kawawa Junction-Mwenge-Tegeta (km 17), sehemu ya Mwenge – Tegeta ulisainiwa tarehe 16 Desemba, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 88.403 kwa fedha za msaada kutoka Serikali ya Japan. Aidha, sehemu ya Mwenge – Kawawa Junction
(km 4.3) itafadhiliwa pia na Serikali ya Japan. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 21.67 za tuta la barabara, km 12.12 za tabaka la chini na km 21.66 za tabaka la juu zimekamilika. Aidha, kwa sehemu ya Morocco – Mwenge malipo ya fidia kwa mujibu wa Sheria ya Barabara ya
mwaka 2007 yamefanyika kwa nyumba zinazotakiwa kuondolewa ili kupisha ujenzi wa barabara. 30. Mheshimiwa Spika, kwa mradi wa
barabara ya Kyaka-Bugene (km 59.1), mkataba
ulisainiwa kwa gharama ya shilingi bilioni 64.96. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 11.8 za tuta la barabara na km 7.9 za tabaka la chini zimekamilika. 31. Mheshimiwa Spika, Lengo la mradi
wa barabara ya Isaka- Lusahunga (km 382) ni kufanya ukarabati wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali
18
ya Tanzania na umegawanyika katika sehemu tatu (3). Utekelezaji wa sehemu zote tatu ni kama ifuatavyo:
Lot 1: Isaka – Ushirombo (Km 132)
Mkataba wa ujenzi unagharimu Shilingi bilioni 145.329 na kazi zilianza tarehe 18 Februari, 2010. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 111.77 za tuta la barabara, km 107.72 za
tabaka la chini, km 107.64 za tabaka la juu na km 106.74 za lami zimekamilika.
Lot 2: Ushirombo – Lusahunga (Km 110)
Mkataba wa ujenzi utagharimu Shilingi bilioni
114.556 na kazi zilianza tarehe 18 Februari, 2010. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 53.5 za tuta la barabara, km 53.5 za tabaka la chini, km 53.5 za tabaka la juu na km 53.5 za lami zimekamilika.
Lot 3: Lusahunga – Rusumo/Nyakasanza – Kobero (km 150).
Lengo la mradi huu ni kufanya usanifu wa kina wa barabara hii yenye urefu wa kilomita 150 kwa ajili ya kuikarabati kwa kiwango cha lami. Usanifu wa kina utakamilika katika mwaka 2012/2013.
19
32. Mheshimiwa Spika, mradi wa kujenga barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora yenye urefu wa kilometa 264.35 kwa kiwango cha lami umegawanyika katika sehemu tatu kama
ifuatavyo-:
Lot 1: Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35)
Mkataba wa ujenzi ni wa gharama ya shilingi bilioni 109.642. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 39.8 za tuta la barabara na km 2.9 za tabaka la chini zimekamilika. Lot 2: Tabora – Nyahua (km 85)
Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 30 Julai, 2010 kwa gharama ya shilingi bilioni 93.401.
Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 16.19 za tuta la barabara zimekamilika.
Lot 3: Chaya – Nyahua (km 90):
Usanifu umekamilika na ujenzi umepangwa kuanza mwaka 2013/14 kulingana na upatikanaji wa fedha. 33. Mheshimiwa Spika, mkataba wa
ujenzi wa barabara ya Handeni – Mkata (km
53.2) ni wa gharama ya Shilingi bilioni 57.338. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 53.2 za lami zimekamilika.
20
34. Mheshimiwa Spika, kwa mradi wa barabara ya Korogwe – Handeni (km 65), mkataba wa ujenzi ni wa Shilingi bilioni 63.199. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 59 za
tuta la barabara, km 52 za tabaka la chini, km 51 za tabaka la juu na km 50 za lami zimekamilika. 35. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa
barabara ya Ndundu-Somanga (km 60)
unagharamiwa na Serikali ya Tanzania, KUWAIT Fund na OPEC. Mkataba wa ujenzi ni wa gharama ya Shilingi bilioni 58.814. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 52.38 za tuta la barabara, km 46 za tabaka la chini, km 36.53 za tabaka la juu na km 30 za lami zimekamilika.
36. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara
ya Makutano – Natta – Mugumu /Loliondo – Mto wa Mbu (km 328) lengo ni kufanya usanifu wa kina ikiwa ni pamoja na maandalizi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha
lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Mikataba kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina kwa sehemu ya Natta-Mugumu-Loliondo (km 239) na Mto wa Mbu – Loliondo (km 213) ilisainiwa tarehe 26 Agosti, 2009. Utekelezaji wa mradi umegawanyika kama
ifuatavyo:
21
Lot 1: Loliondo – Mto wa Mbu (km 213)
Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi utafanyika kwa awamu kulingana na
upatikanaji wa fedha.
Lot 2: Makutano - Natta – Mugumu (km 80)
Kazi ya usanifu wa barabara hii imekamilika na mkataba wa ujenzi kwa sehemu ya Makutano –
Sanzate (km 50) ulisainiwa Machi, 2013. 37. Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa
barabara ya Tanga - Horohoro (km 65) kwa kiwango cha lami, mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 22 Desemba, 2009 kwa gharama ya
Shilingi bilioni 69.894. Mradi huu umegharamiwa kwa fedha za msaada kutoka Mfuko wa MCC ya Marekani na mchango wa Serikali ya Tanzania. Hadi kufikia Aprili 2013, kazi za ujenzi wa barabara hii zimekamilika. Barabara ilifunguliwa rasmi tarehe 13 Aprili,
2013 na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 38. Mheshimiwa Spika, barabara ya
Nzega - Tabora (km 115) inaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami na mradi umegawanyika
katika sehemu kuu mbili. Utekelezaji wa sehemu hizi ni kama ifuatavyo:-
22
• Nzega-Puge (km 56.2):
Gharama ya mradi huu ni Shilingi bilioni 66.358. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 13.5 za tuta la barabara zimekamilika.
• Puge-Tabora (km 58.8):
Mradi huu unajengwa kwa mkataba wa
gharama ya Shilingi bilioni 62.737. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 23 za tuta la barabara na km 2.9 za tabaka la chini zimekamilika.
39. Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi wa barabara ya Sumbawanga – Mpanda– Nyakanazi (km 829) kwa kiwango cha lami umegawanyika katika sehemu kuu nne: Sumbawanga – Kanazi (km 75), Kanazi – Kizi -
Kibaoni (km 76.6), Kizi – Sitalike – Mpanda (km 95) na Mpanda – Uvinza –Nyakanazi (km 582.4). Utekelezaji wake ni kama ifuatavyo:
• Sumbawanga – Kanazi (km 75)
Gharama ya ujenzi kwa sehemu hii ni Shilingi
bilioni 78.84. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 25 za tuta la barabara, km 19.5 za tabaka la chini, km 6.4 za tabaka la juu na km 6.4 za lami zimekamilika.
• Kanazi – Kizi – Kibaoni (km 76.6)
Mkataba wa ujenzi unahusisha km 76.6 kwa gharama ya Shilingi bilioni 82.841. Hadi kufikia
23
Aprili, 2013 jumla ya km 19 za tuta la barabara zimekamilika.
• Kizi – Sitalike – Mpanda (km 95) Mkataba wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Sitalike – Mpanda (km 35) umesainiwa tarehe 22 Oktoba, 2012 kwa gharama ya Shilingi bilioni 37.097. Hadi kufikia Aprili, 2013 Mkandarasi ameshakamilisha
maandalizi (mobilization) na ameanza kazi za ujenzi.
• Mpanda – Uvinza –Nyakanazi (km 582.4) Usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika na ujenzi utafanyika kwa awamu kulingana na
upatikanaji wa fedha. 40. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa
ukarabati kwa kiwango cha lami barabara ya Nyanguge – Musoma (km 183), mkataba wa kazi kwa sehemu ya Simiyu/Mara border -
Musoma yenye urefu wa kilomita 85.5 ulisainiwa tarehe 30 Julai, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 85.368. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 75 za tuta la barabara, km 61.45 za tabaka la chini, km 50.97 za tabaka la juu na km 45.56 za lami zimekamilika. Kwa
upande wa ujenzi wa mchepuo wa Usagara - Kisesa (km 17), mkataba wa ujenzi ulisainiwa
24
tarehe 26 Machi, 2013. Mkandarasi yuko katika maandalizi ya kuanza kazi. Kwa sehemu ya Nyanguge hadi mpakani mwa Simiyu/Mara, Serikali inatafuta fedha za ukarabati.
41. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa
mradi wa barabara ya Mziha – Turiani – Magole (km 84.6) umegawanywa katika sehemu mbili zifuatazo:
• Magole – Turiani (km 48): Mkataba wa ujenzi ulisainiwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 41.89. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 34 za tuta la barabara na km 0.24 za tabaka la chini zimekamilika.
• Turiani – Mziha (km 36.6): Kazi ya usanifu wa barabara hii imekamilika na hatua inayofuata ni kutafuta fedha za ujenzi. 42. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa
barabara ya Bariadi-Lamadi (km 71.8), mkataba wa ujenzi utagharimu Shilingi bilioni 67.408. Mradi huu ni sehemu ya barabara ya Shinyanga – Mwigumbi – Maswa – Bariadi yenye urefu wa kilomita 171. Hadi kufikia Aprili, 2013 jumla ya km 6.88 za tuta la barabara na km 3.12 za
tabaka la chini zimekamilika.
25
43. Mheshimiwa Spika, maandalizi kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Mafia (Mafia Airport Access Road) yenye urefu wa km 14 yanaendelea. Mkataba wa
ujenzi wa barabara hii umesainiwa Machi, 2013 kwa gharama ya Shilingi bilioni 13.554 fedha za ndani. 44. Mheshimiwa Spika, Barabara ya
Dodoma – Chuo Kikuu cha Dodoma (Dodoma
University Road) (km 12) itajengwa kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za ndani. Hatua za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya mradi huu zinaendelea. 45. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
mradi wa barabara ya Tunduma-Sumbawanga (km 223.0) unaogharamiwa kwa fedha za ‘Millennium Challenge Corporation’ (MCC) ya Marekani umegawanyika katika sehemu tatu zifuatazo:-
• Lot 1: Tunduma – Ikana (km 63.7)
Mkataba wa ujenzi wa sehemu hii ya barabara unagharimu Shilingi bilioni 82.52. Hadi kufikia Aprili 2013, jumla ya km 43.75 za tuta la barabara, km 26.34 za tabaka la chini, km 24.88 za tabaka la juu na km 1.3 za lami
zimekamilika.
26
• Lot 2: Ikana – Laela (km 64.0)
Mkataba wa ujenzi wa sehemu hii ya barabara ni wa gharama ya Shilingi bilioni 76.076. Hadi
kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 55.1 za tuta la barabara, km 45.04 za tabaka la chini, km 43.66 za tabaka la juu na km 43.39 za lami zimekamilika.
• Lot 3: Laela – Sumbawanga (km 95.3)
Mkataba wa ujenzi wa sehemu hii ya barabara ni wa gharama ya Dola za Kimarekani milioni 97.141. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 44.3 za tuta la barabara, km 41.9 za tabaka la chini, km 41.76 za tabaka la juu na km 33.76 za lami zimekamilika.
46. Mheshimiwa Spika, mradi wa
barabara ya Kagoma- Biharamulo-Lusahunga (km 154) ni sehemu ya barabara ya Mutukula – Bukoba – Biharamulo – Lusahunga (km 294). Mkataba mpya wa kumalizia ujenzi wa sehemu
ya barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 154) kwa kiwango cha lami ulisainiwa tarehe 18 Juni, 2009 kwa gharama ya Shilingi bilioni 191.454. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania baada ya ADB kujitoa. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 150.9 za tuta la
barabara, km 150.9 za tabaka la chini, km
27
130.5 za tabaka la juu na km 121 za lami zimekamilika. 47. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Japan
imetoa msaada wa fedha za kugharamia ujenzi na upanuzi wa barabara ya Bendera Tatu – KAMATA. Kazi ya kuondoa mali zilizomo kwenye eneo la mradi imeanza. Utaratibu wa kumtafuta Mkandarasi unaendelea nchini Japan na ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha
2013/14.
48. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Minjingu – Babati – Singida (km 223.5) unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na mchango wa Serikali ya Tanzania. Ujenzi wa sehemu tatu za Singida-Kateshi (km 65.1),
Kateshi-Dareda (km 73.8) na Dareda-Babati-Minjingu (km 84.6) umekamilika.
49. Mheshimiwa Spika, barabara ya
Minjingu – Arusha (km 104) inafanyiwa ukarabati kwa kiwango cha lami kwa ufadhili
wa Benki ya Dunia kwa gharama ya Shilingi bilioni 75.511. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 12 za tuta la barabara, km 10 za tabaka la chini na km 9 za tabaka la juu zimekamilika.
28
50. Mheshimiwa Spika, ukarabati wa
barabara ya lami ya Dar es Salaam – Tunduma
(TANZAM) unahusisha ukarabati wa sehemu ya
Iyovi - Kitonga Gorge (km 86.3), Ikokoto - Iringa
(km 60.9), mchepuo wa kuingia Iringa mjini (km
2.1) na Iringa-Mafinga (km 68.9). Mradi huu
unagharamiwa kwa mkopo kutoka Serikali ya
Denmark pamoja na mchango wa Serikali ya
Tanzania. Ukarabati wa Sehemu ya Msimba –
Ruaha Mbuyuni/Ikokoto – Mafinga (km 149.6)
umekamilika. Ukarabati wa sehemu ya Iringa –
Mafinga (km 69.4), ulianza tarehe 9 Septemba,
2011 kwa gharama ya EURO milioni 38.5. Hadi
kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 70.1 za tuta la
barabara, km 54.64 za tabaka la chini, km
53.91 za tabaka la juu na km 53.11 za lami
zimekamilika.
51. Mheshimiwa Spika, kazi ya ukarabati
wa barabara ya Korogwe - Mkumbara –Same
(km 172) zimegawanyika katika sehemu mbili na utekelezaji wa sehemu hizo ni kama ifuatavyo:-
• Korogwe - Mkumbara (km 76)
Mkataba wa ujenzi wa barabara ulisainiwa
tarehe 16 Januari 2012 kwa gharama ya
29
Shilingi bilioni 62.866. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 19.1 za tuta la barabara, km 14.2 za tabaka la chini, km 13.7 za tabaka la juu na km 3.4 za lami zimekamilika.
• Mkumbara – Same (km 96)
Mkataba wa ujenzi wa barabara ulisainiwa tarehe 16 Januari 2012 kwa gharama ya Shilingi bilioni 65.130. Hadi kufikia Aprili, 2013,
jumla ya km 3.3 za tuta la barabara zimekamilika. 52. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea
na ujenzi wa barabara ya Mbeya – Chunya – Makongorosi (km 115) ambao umegawanywa
katika sehemu tatu zifuatazo:-
• Mbeya-Lwanjilo (km 36): Baada ya Mkandarasi wa awali (Kundan Singh) kushindwa kazi na kufukuzwa, Mkataba mpya wa ujenzi wa barabara ulisainiwa kwa gharama
ya Shilingi bilioni 55.385. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 3 za tuta la barabara zimekamilika.
• Lwanjilo-Chunya (km 36): Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Lwanjilo –
Chunya utagharimu Shilingi bilioni 40.28. Hadi
30
kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 3 za tuta la barabara zimekamilika. 53. Mheshimiwa Spika, kuhusu ukarabati
na upanuzi wa barabara ya Chalinze - Segera
hadi Tanga, ukarabati wa sehemu ya Chalinze –
Kitumbi (km 125) umekamilika. Mkataba wa
ukarabati wa sehemu ya barabara ya Kitumbi –
Segera – Tanga (km 120 ulisainiwa tarehe 24
Desemba 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni
67.237. Hadi Aprili, 2013, upanuzi umekamilika
kwa jumla ya km 24.45 za tuta la barabara, km
24.45 za tabaka la chini na km 24.45 za tabaka
la juu. Aidha, km 90 za kuongeza tabaka la lami
(resealing) zimekamilika.
54. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa
barabara ya Dodoma – Iringa (km 260) unagharamiwa na fedha za mkopo toka ADB na JICA. Mradi umegawanyika katika sehemu tatu
kama ifuatavyo:-
• Iringa – Migori (km 95.10):
Mkataba wa ujenzi wa sehemu hii ulisainiwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 84.216. Hadi kufikia Aprili 2013, jumla ya km 58.7 za tuta la
31
barabara na km 39.1 za tabaka la chini, km 10.7 za tabaka la juu zimekamilika.
• Migori – Fufu Escarpment (km 93.80)
Mkataba wa ujenzi wa barabara hii katika sehemu unagharimu Shilingi bilioni 73.612. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 56.4 za tuta la barabara na km 25.3 za tabaka la chini, km 9.4 za tabaka la juu zimekamilika.
• Fufu Escarpment – Dodoma (km 70.90)
Mkataba katika sehemu hii ya barabara unagharimu Shilingi bilioni 64.327. Hadi kufikia Aprili 2013, jumla ya km 64.8 za tuta la
barabara, km 39.2 za tabaka la chini, km 28 za tabaka la juu na km 6.9 za lami zimekamilika.
55. Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa
kiwango cha lami kwa barabara ya Dodoma – Babati (km 261) umegawanywa katika sehemu
zifuatazo:-
• Dodoma – Mayamaya (km 43.65)
Mkataba wa ujenzi wa barabara hii ulisainiwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 40.609. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 25.75 za tuta
la barabara, km 20 za tabaka la chini, km 18 za
32
tabaka la juu na km 17.35 za lami zimekamilika.
• Mayamaya - Mela (km 99.35)
Zabuni ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Mayamaya – Mela imetangazwa Novemba, 2012 na taratibu za kumpata Mkandarasi zinaendelea. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya
Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
• Mela – Bonga (km 98.8)
Zabuni ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Mela – Bonga imetangazwa Novemba, 2012 na
taratibu za kumpata Mkandarasi zinaendelea. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
• Bonga – Babati (km 19.2)
Mkataba wa ujenzi wa barabara ulisainiwa tarehe 31 Mei, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 19.687. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 18.5 za tuta la barabara, km 18.5 za tabaka la chini, km 18.5 za tabaka la juu na km 18.2 za lami zimekamilika.
33
56. Mheshimiwa Spika, mradi wa barabara ya Masasi- Songea – Mbamba Bay umegawanywa katika sehemu zifuatazo:-
• Mangaka – Nakapanya (km 70.50) Zabuni ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Mangaka - Nakapanya imetangazwa Mei, 2012 na mchakato wa kumpata Mkandarasi unaendelea. Mradi huu
unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
• Nakapanya - Tunduru (km 66.50) Zabuni ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa
sehemu ya Nakapanya - Tunduru imetangazwa Mei, 2012 na mchakato wa kumpata Mkandarasi unaendelea. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
• Mangaka – Mtambaswala (km 65.50)
Zabuni ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Mangaka - Mtambaswala imetangazwa Mei, 2012 na mchakato wa kumpata Mkandarasi
unaendelea. Mradi huu unagharamiwa kwa
34
fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
• Tunduru – Matemanga (km 58.70)
Mkataba ulisainiwa tarehe 24 Desemba, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 63.409. Mkataba wa ujenzi umefutwa tarehe 8 Januari, 2013 baada ya Mkandarasi M/s Progressive –
Higleg – Joint Venture (JV) kushindwa kutekeleza mradi kimkataba. Taratibu za kumpata mkandarasi mwingine zinaendelea.
• Matemanga – Kilimasera (km 68.20)
Mkataba ulisainiwa tarehe 24 Desemba, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 64.016. Mkataba wa ujenzi umefutwa tarehe 8 Januari 2013 baada ya Mkandarasi M/s Progressive – Higleg – Joint Venture (JV) kushindwa kutekeleza mradi kimkataba. Taratibu za
kumpata mkandarasi mwingine zinaendelea.
• Kilimasera - Namtumbo (km 60.70)
Mkataba ulisainiwa tarehe 24 Desemba, 2010 kwa gharama ya Shilingi bilioni 53.229. Mkataba wa ujenzi umefutwa tarehe 8 Januari
2013 baada ya Mkandarasi M/s Progressive –
35
Higleg – Joint Venture (JV) kushindwa kutekeleza mradi kimkataba. Taratibu za kumpata mkandarasi mwingine zinaendelea.
• Namtumbo – Songea (km 67.00) Mkataba wa ujenzi wa barabara ulisainiwa tarehe 25 Mei 2010 kwa gharama ya Dola za Kimarekani milioni 46.963. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 66 za tuta la barabara, km
58.5 za tabaka la chini, km 55 za tabaka la juu na km 52 za lami zimekamilika.
• Peramiho – Mbinga (km78.00) Mkataba wa ujenzi wa barabara ulisainiwa tarehe 2 Julai, 2010 kwa gharama ya Shilingi
bilioni 79.803. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya km 78 za tuta la barabara, km 78 za tabaka la chini, km 78 za tabaka la juu na km 78 za lami zimekamilika. Madaraja Makubwa 57. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/2013 Wizara inaendelea na ujenzi na ukarabati wa madaraja ya: Kirumi kwenye barabara ya Makutano – Sirari, daraja la Nanganga kwenye barabara ya Mingoyo – Masasi
– Tunduru, daraja la Sibiti kwenye barabara ya Ulemo – Gumanga – Sibiti, daraja la Maligisu
36
(Mwanza) kwenye barabara ya Bukwimba – Kadashi - Maligisu, daraja la Kilombero kwenye barabara ya Mikumi - Ifakara – Mahenge, daraja la Kavuu kwenye barabara ya Majimoto-Inyonga,
daraja la Mbutu kwenye barabara ya Igunga-Manonga, daraja la Ruhekei kwenye barabara ya Mbinga-Mbamba Bay, daraja la Ruhuhu (Ruvuma) na ununuzi wa madaraja ya Chuma ya dharura na mtambo wa kukagua madaraja (Compact Emergency Bridges na Crane Lorry).
Utekelezaji wa ujenzi wa madaraja hayo umefikia hatua zifuatazo:-
(i) Daraja la Kirumi
Hatua za kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya usanifu wa kina wa ukarabati wa
daraja la Kirumi zinaendelea. Kazi za usanifu zinatarajiwa kukamilika katika mwaka 2013/14.
(ii) Daraja la Sibiti
Mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 7 Agosti, 2012 kwa gharama ya shilingi bilioni 16.302.
Hadi kufikia Aprili, 2013 Mkandarasi ameshakamilisha maandalizi (mobilization) na tayari kazi za ujenzi zimeanza.
(iii) Daraja la Kilombero
Mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 24 Oktoba, 2012 kwa gharama ya Shilingi bilioni
53.214. Maandalizi ya kuanza ujenzi wa daraja yanaendelea.
37
(iv) Daraja la Maligisu
Hadi kufika Aprili, 2013 ujenzi wa Daraja hili umefikia asilimia 90.
(v) Daraja la Kavuu
Hatua za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa msingi na nguzo za daraja zinaendelea. Ununuzi wa vyuma vya daraja (Mabey parts) umekamilika.
(vi) Daraja la Mbutu
Mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 27 Aprili, 2012 kwa gharama ya Shilingi bilioni 10.456. Hadi kufikia Aprili, 2013 kazi za ujenzi zimekamilika kwa asilimia 54.3.
(vii) Daraja la Ruhuhu
Matayarisho kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa daraja na bwawa la kumwagilia maji la Ruhuhu
yanaendelea.
(viii) Ununuzi wa Madaraja ya Chuma ya
Dharura na Mtambo wa Kukagua Madaraja (Compact Emergency Bridges na Under Bridge Inspection Lorry).
Taratibu za ununuzi wa Madaraja ya Chuma ya Dharura (Compact Emergency Bridges) zinaendelea na mkataba wa ununuzi wa Mtambo wa kukagua Madaraja (Under Bridge
Inspection Lorry) umesainiwa.
38
58. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa Daraja la Kigamboni, mkataba wa ujenzi ulisaniwa tarehe 9 Januari, 2012. Mradi huu
unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Mkandarasi ameshakamilisha maandalizi (mobilization) kwa asilimia 90 na ameanza kazi za ujenzi.
59. Mheshimiwa Spika, mradi wa kujenga Daraja katika Mto Ruvu kwenye barabara ya Dar es Salaam – Tunduma (TANZAM),
ulikamilika mwaka 2009. Fedha za ndani zimetengwa katika bajeti ya 2012/2013 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai la mkandarasi. Miradi ya Kupunguza Msongamano wa Magari katika Jiji la Dar es salaam 60. Mheshimiwa Spika, Lengo la mradi
huu ni kusanifu, kujenga na kukarabati barabara za Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Jiji. Hadi Aprili, 2013, hatua za utekelezaji wa miradi
mbalimbali ni kama ifuatavyo:- (i) Ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo
kwa kasi kutoka Kimara hadi Kivukoni, Fire hadi Kariakoo na Magomeni hadi Morocco unaendelea. Aidha, kazi ya ujenzi wa Karakana na vituo vya mabasi
yaendayo kasi pamoja na uhamishaji wa
39
miundombinu ya umeme inaendelea vizuri.
(ii) Ujenzi wa Flyover ya TAZARA: Maandalizi
ya kumpata mkandarasi yanaendelea. Mradi huu unafadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA).
(iii) Ujenzi na upanuzi wa Barabara ya Gerezani (Bendera Tatu – KAMATA): Serikali ya Japan imekubali kugharamia mradi huu na taratibu za kumpata mkandarasi zinaendelea.
(iv) Barabara ya Kilwa (Bendera tatu – Mbagala Rangi Tatu): Ujenzi wa barabara hii umekamilika.
(v) Hadi kufikia Aprili, 2013, sehemu kubwa ya kazi kwa kiwango cha lami imekamilika
kwa barabara ya Ubungo Bus Terminal – Mabibo-Kigogo Roundabout (km 6.4); Kigogo Roundabout-Bonde la Msimbazi –Twiga/Msimbazi Junction (km 2.7) na Barabara ya Jet Corner – Vituka – Davis Corner (km 10.3).
(vi) Kuhusu Usafiri wa vivuko/boti kati ya Dar es Salaam – Bagamoyo; mkandarasi wa kujenga kivuko/boti chenye uwezo wa kubeba abiria 300 amepatikana. Usanifu
40
wa maegesho matatu (Magogoni, Jangwani Beach, Rungwe Oceanic) unaendelea. 61. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea
na miradi mingine ya barabara za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam kama ifuatavyo:-
(i) Kazi za ujenzi zinaendelea kwa barabara ya Tabata Dampo – Kigogo na Ubungo Maziwa External (km 2.25).
(ii) Kwa upande wa barabara za Old Bagamoyo na Garden Road (km 9.1), kazi za usanifu zimekamilika Februari, 2013; na
(iii) Kazi ya Usanifu imekamilika kwa barabara za Mbezi (Morogoro road) –Malamba Mawili – Kinyerezi - Banana (km 14); Tegeta - Kibaoni-Wazo – Goba - Mbezi Mwisho (km 20); Tangi Bovu-Goba (km 9); Kimara
Baruti-Msewe-Changanyikeni (km 2.6) na Kimara-Kilungule-External Mandela Road (km 9). Hatua za kuwapata Wakandarasi wa ujenzi zinaendelea.
62. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/13 Wizara imeendelea kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara mbalimbali. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika kwa barabara zifuatazo:- (i)
41
Mbinga – Mbamba Bay (km 66) (ii) Sehemu ya Signali-Ifakara (km 16.8) katika barabara ya Kidatu-Ifakara (km 30). Hii ni kwa ajili ya ujenzi
kwa kiwango cha lami nyepesi. (iii) Barabara ya Turiani – Mziha (km 36.6), (iv) Barabara ya Mafinga – Igawa (Km 140.6), (v) Barabara ya Chunya-Makongorosi (km 43), (vi) Barabara ya
Same – Himo – Marangu (km 99.73), (vii) Barabara ya Mombo – Lushoto (km 32), (viii) Barabara ya Makambako – Songea (km 295) na (ix) Barabara ya Arusha – Moshi – Himo – Holili
(km 140). Kwa barabara hizi, kazi inayofuata ni kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. 63. Mheshimiwa Spika, kazi za upembuzi
yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea katika barabara zifuatazo:-
(i) Barabara ya Mtwara – Mingoyo - Masasi (km 200.00),
(ii) Makongolosi- Rungwa-Itigi- Mkiwa (km 413),
(iii) Mpemba-Isongole (Tanzania/Malawi Border),
(iv) Handeni – Kiberashi - Kibaya –Kwamtoro - Singida (km 461), na
(v) Bagamoyo (Makurunge) – Saadani – Pangani - Tanga (km178).
Aidha, taratibu za kuwapata Wataalam Mshauri kwa ajili ya kazi za upembuzi yakinifu na
42
usanifu wa kina zinaendelea kwa barabara zifuatazo:-
(i) Matai- Kasesya (km 50), (ii) Ifakara-Mahenge (sehemu ya Lupilo-
Mahenge),
(iii) Kibondo-Mabamba (km 35), (iv) Omugakorongo – Kigarama- Murongo
(km 111), (v) Kyaka- Bugene/Benako (km 124), (vi) Kolandoto- Lalago- Mwanhuzi –Oldeani
(km 328),
(vii) Ipole – Rungwa (km 95), (viii) Mtwara – Newala – Masasi (km 209), (ix) Kidatu –Ifakara – Londo –
Lumecha/Songea (km 396) ambayo imepata ufadhili wa ADB na JICA kwa ajli ya Mtaalam Mshauri na
(x) Daraja la Wami.
Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Vivuko na Maegesho ya Vivuko 64. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Wizara kupitia TEMESA ilipanga:
i) Kuendelea na taratibu za kununua vivuko vipya vya Ilagala (Tani 50) Mkoani Kigoma, Kahunda/Maisome (Geita) na kivuko cha mwambao wa
43
Bahari ya Hindi kati ya Magogoni (Dar es Salaam) na Bagamoyo,
ii) Kukamilisha ukarabati wa vivuko vya MV. Chato (Geita), MV Kome I
(Mwanza), MV Kilombero I (Morogoro), Mv. Geita (Mwanza) na Itungi Port (Mbeya), pamoja na
iii) Kujenga maegesho katika vivuko vya Msanga Mkuu (Mtwara), Ruhuhu (Ruvuma), Maisome/Kahunda (Geita)
na Rugezi/Kisorya upande wa Ukerewe (Mwanza).
65. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia
Aprili, 2013, kazi za ujenzi na ukarabati wa vivuko ilikamilka kwa vivuko vifuatavyo:
i) Ujenzi wa kivuko cha Kilambo Mkoani
Mtwara, ii) Ujenzi wa kivuko cha Ilagala mkoani
Kigoma umekamilika huko Uholanzi na kivuko kimewasili hapa nchini tarehe
26 Aprili 2013, iii) Ujenzi wa maegesho ya Nkome, Rugezi
na Utete umekamilika na iv) Ukarabati wa vivuko vya MV Chato, MV
Sabasaba na MV Kyanyabasa umekamilika
44
66. Mheshimiwa Spika, Miradi ya vivuko na maegesho inayoendelea katika mwaka 2012/13 ni kama ifuatavyo:
i) Ujenzi wa Kivuko cha Kahunda-Maisome umeanza na utakamilika Desemba, 2013,
ii) Maandalizi ya Ununuzi wa kivuko cha Itungi Port (Kyela Mbeya) unaendelea,
iii) Ujenzi wa kivuko cha Msanga Mkuu
(Mtwara) unaendelea Bandarini Dar es salaam,
iv) Ujenzi wa maegesho ya kivuko cha Msanga Mkuu mkoani Mtwara upande wa Msanga Mkuu umekamilka na umeanza kwa upande wa Msemo,
v) Ujenzi wa maegesho ya Kahunda -Maisome na maegesho katika vituo vya Mharamba, Senga na Ikumbitare umeanza Machi 2013,
vi) Usanifu wa maegesho ya kivuko kwa ajili ya usafiri kati ya Dar es Salaam na
Bagamoyo unaendelea. Aidha, mzabuni amepatikana kwa ajili ya ununuzi wa kivuko cha Dar es salaam hadi Bagamoyo,
vii) Ujenzi wa uzio katika vivuko vya Magogoni Dar es salaam na Kinesi
Mkoani Mara umekamilika,
45
viii) Zabuni imetangwaza kwa ajili ya ukarabati wa vivuko vya MV Kome 1, na MV Kilombero 1, na
ix) Mkandarasi wa kukarabati kivuko cha
MV Geita amepatikana. Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali 67. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2012/13 Wizara kupitia Wakala wa Majengo imeendelea na utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi ya Viongozi na watumishi wa umma, majengo ya ofisi za Serikali na majengo ya biashara.
68. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2013 ujenzi wa nyumba za viongozi katika Wilaya za Bahi (2) na Kondoa (1), jengo la ghorofa 18 barabara ya Chimara (DSM); na jengo la ghorofa 8 barabara ya Haile Selasie Dar es salaam ulikamilika na yameanza kutumika.
69. Mheshimiwa Spika, awamu ya kwanza
ya ujenzi wa nyumba za Waheshimiwa Majaji; Dar es Salaam (2), Arusha (1), Songea (1), Tanga (1), Mbeya (1), Tabora (1), Mwanza (1), Iringa (1, Dodoma (1), pamoja na ujenzi wa nyumba za
viongozi Ukerewe(2) na Mvomero (1) upo kwenye hatua za mwisho za kukamilishwa. Taratibu za zabuni kwa ujenzi wa nyumba zingine 5
46
(Kagera,Shinyanga, Kilimanjaro, Mtwara na Dar es Salaam) zimeanza. 70. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa majengo
mawili ya ghorofa ya kupangisha kibiashara jijini Arusha (Wachaga Street na Simeoni Street) unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Juni, 2014. Miradi ya ujenzi wa ghorofa lenye nyumba 16 za kupangisha
kibiashara eneo la SIDA – Dar es Salaam, ghorofa lenye nyumba 8 Mbezi Beach – Dar es Salaam na nyumba 3 Arusha upo katika hatua za umaliziaji. Aidha, ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bariadi, zahanati katika Manispaa ya Lindi na zahanati katika eneo la
Mwangaza Dodoma pamoja na ukarabati wa jengo la karakana za MT. Depot na Dodoma unaendelea.
Usalama Barabarani
71. Mheshimiwa Spika, Wizara iliendelea na utekelezaji wa Sera ya Usalama Barabarani ya mwaka 2009 kwa kutekeleza yafuatayo katika mwaka 2012/13:- (i) Kutoa elimu ya usalama barabarani kwa
Shule za Msingi ili kupunguza ajali nchini, (ii) Kuandaa na kuendesha kampeni za
kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa usalama barabarani,
47
(iii) Kushirikiana na wadau muhimu kama vile Jeshi la Polisi, Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Sheria n.k. katika kutoa elimu ya Usalama barabarani na kusimamia
utekelezaji wa sheria zilizopo, (iv) Kudhibiti uzito wa magari yanayotumia
barabara na kufanya tafiti za kutumia tekinolojia ya kisasa katika kudhibiti uzito,
(v) Kuandaa taratibu za uanzishwaji wa Wakala wa Usalama barabarani,
(vi) Kuandaa mapendekezo ya rasimu ya Sheria ya Usalama barabarani,
Ushirikishwaji wa Wanawake katika Kazi za Barabara
72. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2012/13 masuala yafuatayo yametekelezwa ili kuongeza ushiriki wa wanawake katika kazi za barabara: Wizara imeteua Waratibu wa Mikoa katika mikoa yote Tanzania Bara ambao watakuwa na jukumu la
kuhamasisha wanawake kushiriki katika kazi za barabara katika mikoa husika. Wizara imefuatilia kujua idadi ya kampuni za makandarasi zinazomilikiwa na wanawake katika kila Mkoa ambao wako hai. Hadi sasa jumla ya kampuni za makandarasi 125
zinamilikiwa na wanawake. Aidha, Wizara kupitia Kitengo cha ushirikishaji Wanawake imeendesha mafunzo kwa vikundi vya
48
Wanawake na Makandarasi Wanawake 30 ili kuwaongezea uwezo wa kujenga na kuzifanyia matengenezo barabara kwa kutumia Tekinolojia Stahiki ya Nguvu Kazi. Washiriki wa warsha
hiyo wamepata sifa ya kuanzisha kampuni za ukandarasi na kusajiliwa na Bodi ya Usajili wa Makandarasi. Washiriki wa warsha hiyo walitoka mikoa ya Kilimanjaro, Singida, Manyara, Tanga, Geita, Dar es Salaam, Katavi, Njombe na Simiyu. Aidha, katika mwaka
2012/13 Wizara ilifanya kazi ya ufuatiliaji (Monitoring) kujua maendeleo na kiwango cha ushirikii wa wanawake katika miradi ya barabara. Wizara iliweza kujua kiwango cha ushiriki wa wanawake kwenye miradi ya
barabara hasa kwa wanawake wa kada za vibarua na wengineo ambao wanapata kipato kwa kazi za barabara. Ushiriki wa Wizara katika Jumuiya Mbalimbali za Kimataifa 73. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Wizara imeendelea kushiriki katika masuala yanayohusu Sekta ya Ujenzi katika Jumuiya za Kimataifa na Kikanda na hususan Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya
ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Kwa upande wa EAC Wizara imeshiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya barabara zinazounganisha nchi wanachama ukiwemo
49
mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha – Namanga kwa kiwango cha lami. Mradi huu umekamilika na kufunguliwa rasmi na Wakuu wa Nchi za Tanzania na Kenya tarehe 28
Novemba, 2012. Miradi mingine inayoendelea kutekelezwa ni ujenzi wa daraja la Rusumo linalounganisha Tanzania na Rwanda, usanifu wa barabara ya Bagamoyo – Saadani - Tanga, usanifu wa barabara ya Arusha – Himo – Holili/Taveta na ujenzi wa Vituo vya pamoja vya
mipakani (One Stop Border Posts) vya Namanga, Rusumo, Kabanga na Mutukula. 74. Mheshimiwa Spika, Wizara pia
ilishiriki katika maandalizi ya mswada wa Udhibiti wa Uzito wa Magari katika Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC Vehicle Load Control Bill, 2012) ambao unasubiri kupitishwa na Bunge la Afrika Mashariki. Aidha, Wizara ilishiriki katika Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi za EAC uliofanyika Nairobi tarehe 29 Novemba, 2012 ambao pamoja na mambo mengine ulipitisha
miradi ya kipaumbele kwa ajili ya kuimarisha ufanisi wa huduma za bandari. Kwa upande wa barabara zetu, miradi iliyokubaliwa na Wakuu wa nchi za EAC ni barabara za kupunguza msongamano katika kuingia na kutoka Bandari ya Dar es Salaam; barabara ya Nyakanazi –
Kasulu – Kidahwe – Mpanda; barabara ya Tanga – Saadani – Bagamoyo, barabara ya Nyanguge – Musoma – Sirari; barabara ya Lusahunga –
50
Rusumo na barabara ya Nyakasanza – Kobero. Miradi hii ya barabara ilijumuishwa kwenye mpango wa EAC wa kuboresha huduma za bandari na reli ambazo zinahudumia Tanzania
na nchi jirani. 75. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa
SADC, mwaka 2012/13 Wizara ilishiriki katika maandalizi ya Mpango wa Kuendeleza Miundombinu (SADC Regional Infrastructure
Development Master Plan) ambao ulipitishwa na Nchi Wanachama wa SADC mwezi Agosti, 2012 Maputo nchini Msumbiji. Lengo la Mpango huu ni kuwa na miundombinu ya uhakika
itakayoziunganisha nchi wanachama ili kupunguza gharama na kurahisisha biashara. Mpango huo unahusisha uendelezaji wa miradi ya kipaumbele ya miundombinu katika Sekta za Nishati, Uchukuzi, Utalii, Maji, Mawasiliano na Hali ya Hewa. Miradi ya barabara
inayojumuishwa katika Mpango Kamambe inahusisha: i) Barabara ya Dar es Salaam – Chalinze (Expressway - km 100) kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa za Burundi, DR Congo, Malawi, Rwanda, Uganda na
Zambia; ii) Barabara ya Mtwara – Mbamba bay
sehemu ya barabara ya Mbinga – Mbamba
51
Bay (km 66) inayoiunganisha Tanzania na nchi za Malawi na Zambia;
iii) TANZAM Highway sehemu ya barabara ya Makambako – Songea (km 289)
inayoiunganisha Tanzania na nchi ya Msumbiji; na
iv) Barabara ya Manyoni – Tabora – Kigoma sehemu za barabara ya Nyahua – Chaya (km 90) na Kidahwe – Kasulu – Nyakanazi (km 310) zitakazoiunganisha Tanzania na
nchi za DR Congo, Zambia na Burundi. Nchi Wanachama kwa kushirikiana na Sekretarieti ya SADC zinaendelea na mikakati ya kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kamambe wa Kuendeleza
Miundombinu.
Maendeleo ya Watumishi 76. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13, Wizara imeendelea kuwaendeleza
watumishi wake kitaaluma kwa kuwapeleka jumla ya watumishi 25 katika mafunzo ndani na nje ya nchi. Kati ya hao, watumishi 12 walishiriki mafunzo ya muda mrefu na watumishi 13 walipelekwa mafunzo ya muda mfupi. Watumishi 2 walipata mafunzo ya muda
mrefu na watumishi 2 walipata mafunzo ya muda mfupi nje ya nchi. Watumishi 10 walipata mafunzo ya muda mrefu na watumishi 11
52
walipata mafunzo ya muda mfupi ndani ya nchi. Aidha, watumishi 20 walipandishwa vyeo, watumishi 2 walibadilishwa kada, watumishi 3 walithibitishwa kazini na watumishi 11
waliajiriwa kazini.
Mikakati ya Kupambana na Ukimwi 77. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa
fedha 2012/2013 Wizara iliendelea kutoa elimu
ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI na VVU kwa watumishi kwa kutumia Wataalamu kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS). Aidha, watumishi wameendelea kuhamasishwa kupima afya zao pamoja na kuwapatia huduma ya lishe bora kwa watumishi walioathirika.
Vita Dhidi ya Rushwa 78. Mheshimiwa Spika, Wizara katika
mwaka wa fedha 2012/2013 iliendelea kuwaelimisha watumishi athari ya kutoa na
kupokea rushwa pamoja na kuwahimiza kupambana na rushwa katika mazingira yote ya kazi. Elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa ilitolewa kupitia vipeperushi, semina na mikutano mbalimbali kwa ushirikiano na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU).
53
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
79. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu sera na mipango ya Wizara ya Ujenzi, umuhimu wa
kutunza barabara na kuzingatia sheria na kanuni za matumizi ya barabara na sheria zingine zinazosimamia Sekta. Aidha, Wizara imeendelea kuboresha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kuongeza ufanisi na kutoa huduma kwa wakati.
Tovuti ya Wizara imeboreshwa ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa mbali mbali zinazohusiana na Sekta ya Ujenzi. Wizara imeshiriki katika mikutano na mafunzo yanayolenga matumizi ya TEHAMA ili kuboresha utendaji wa kila siku.
Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB) 80. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Bodi ya Mfuko wa Barabara ilikuwa na lengo la kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 429.664. Hadi tarehe 31 Machi, 2013 Bodi ya
Mfuko wa Barabara ilikusanya na kugawa kiasi cha Shilingi bilioni 333.7 ambazo ni sawa na asilimia 77.7 ya lengo la Shilingi bilioni 429.664 kwa mwaka 2012/13. Kazi nyingine iliyofanywa na Bodi katika mwaka 2012/13 ni kufuatilia na kukagua miradi ya matengenezo ya barabara
54
inayotumia fedha za Mfuko nchi nzima. Kwa mwaka 2012/13 bodi ilifanya ukaguzi katika mikoa kumi na moja (11) ambayo ni Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Rukwa, Tabora, Dar es
Salaam, Mwanza, Lindi, Mara, Katavi na Iringa. Pale inapobainika kuna udhaifu, mamlaka husika zilitaarifiwa na hatua stahiki zilichukuliwa. Wakala wa Ufundi na Umeme 81. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2012/13, Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imeendelea kusimamia uendeshaji wa vivuko 22 katika maeneo 15 hapa nchini kama ifuatavyo:
(i) Magogoni—Kigamboni;
• MV Magogoni, Tani 500,
• MV Kigamboni, Tani 170, (ii) Ilagala (Kigoma);
• MV Ilagala, Tani 50, (iii) Kinesi—Musoma (Mara);
• MV Musoma, Tani 85, (iv) Ifakara—Ulanga (Mto Kilombero);
• MV Kilombero I, Tani 50,
• MV Kilombero II, Tani 50, (v) Kisorya—Rugezi (Mwanza/Mara);
• MV Ujenzi, Tani 50,
• MV Sabasaba, Tani 85,
55
(vi) Rusumo - Nyakiziba (Mto Ruvuvu, Kagera);
• MV Ruvuvu, Ton 35, (vii) Kasharu - Buganguzi (Mto Ngono, Kagera);
• MV Kyanyabasa, Tani 7, (viii) Utete (Mto Rufiji);
• MV Utete, Tani 50, (ix) Pangani—Bweni (Mto Pangani – Tanga),
• MV Pangani II, Tani 50, (x) Kigongo—Busisi (Mwanza);
• MV. Misungwi, Tani 250,
• MV. Sengerema, Tani 170,
• MV. Geita, Tani 65, (xi) Nyakaliro—Kome (Sengerema),
• MV Kome I, Tani 25
• MV Kome II, Tani 40, (xii) Ilunga - Kipingu (Mto Ruhuhu – Ruvuma);
• MV Ruhuhu, Tani 50, (xiii) Bugolora—Ukara (Ukerewe/Ukara);
• MV Nyerere, Tani 25, (xiv) Chato—Muharamba—Zumacheli—Senga-
Bukondo—Nkome.
• MV Chato, Tani 75,
• MV Ukara, Tani 25. (xv) Kilambo - Namoto
• MV Kilambo Tani 50
82. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TEMESA imeendelea kusimamia huduma za ukodishaji magari ya viongozi. TEMESA pia
imetoa ushauri wa kihandisi kwa miradi ya
56
usimikaji wa mifumo ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na mabarafu katika majengo ya Serikali kama ifuatavyo:
(i) Miradi ya kuboresha vituo na vyuo vya Afya vya Mbeya, Mirembe (Dodoma), Tanga, Kairuki (Dar es Salaam), Sengerema, Rukwa na Mvumi,
(ii) Mradi wa maboresho ya ‘Theatre’
katika Hospitali ya Mawenzi Moshi, (iii) Mradi wa ujenzi wa Mahakama Kuu
ya Shinyanga, (iv) Mradi wa ukarabati wa Ofisi za muda
za TBA Mkoa wa Njombe,
(v) Mradi wa usimikaji wa lifti katika jengo la Ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria,
(vi) Miradi ya ununuzi na usimikaji wa jenereta katika Ofisi za Wizara ya Maji, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, TANROADS – Lindi, Chuo cha Uvuvi Mbegani na Chuo cha Maji,
(vii) Miradi ya ujenzi wa karakana za vyuo vya maendeleo ya Jamii katika
mikoa ya Tanga, Tabora, Pwani na Mara,
(viii) Miradi ya ujenzi wa nyumba za Makazi ya Majaji katika miji ya Dar
57
es Salaam, Arusha, Tanga, Tabora, Dodoma, Mbeya, Iringa na Mwanza,
(ix) Mradi wa ujenzi wa Ofisi za SIDO Mkoa wa Pwani,
(x) Mradi wa ukarabati wa nyumba za makazi za Majaji mikoa ya Mwanza, Iringa na Tabora.
83. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Wizara kupitia TEMESA ilipanga
kutengeneza magari katika Karakana zake zote zilizopo kila Mkoa. Hadi kufikia Aprili, 2013 TEMESA ilitengeneza magari 5,938. Matengenezo ya mifumo ya Umeme, Elektroniki Viyoyozi na Majokofu katika ofisi mbalimbali umeendelea kufanyika. Aidha, TEMESA
imeendelea kuimarisha karakana zake kwa vifaa vya umeme, elektroniki na mitambo. Mashine za kutambua matatizo ya magari (Computerized Diagonistic Machine) imepatikana. Mashine nyingine 10 kama hiyo ziko katika hatua ya manunuzi kwa ajili ya karakana 10.
Bodi ya Usajili wa Wahandisi 84. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Bodi ya Usajili wa Wahandisi ilipanga kusajili Wahandisi 955, kampuni za ushauri wa
kihandisi 25 na kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo ya vitendo kwa Wahandisi wahitimu 1,000. Hadi Aprili, 2013 Bodi ilisajili
58
Wahandisi 838 na kampuni za ushauri wa kihandisi 10 na kufikisha jumla ya Wahandisi 12,102 waliosajiliwa katika ngazi mbalimbali na kampuni za ushauri wa kihandisi 237. Kati yao,
jumla ya Wahandisi waliosajiliwa 10,694 ni wazalendo, na 1,408 ni wageni. Kampuni za ushauri wa kihandisi 169 ni za kizalendo na 68 ni za kigeni. Aidha, katika kipindi hicho, Bodi ilisajili Wahandisi Washauri 17 na kufanya jumla ya Wahandisi Washauri kuwa 386, kati
yao 299 ni wazalendo na 87 ni wageni. Bodi ilifuta usajili kwa Wahandisi washauri 3 na kampuni ya ushauri wa Kihandisi 1.
85. Mheshimiwa Spika, Bodi ya Usajili wa
Wahandisi imetekeleza majukumu mengine
kama ifuatavyo:
i) Kusimamia mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa Wahandisi wote ili kuwafanya Wahandisi kwenda sambamba na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia
na hivyo kuweza kufanya shughuli zao za kihandisi kwa ufanisi. Lengo pia ni kuwafanya Wahandisi kumudu ushindani unaoletwa na utandawazi. Wahandisi watalaamu zaidi ya 3,000 wamenufaika na mpango huu.
ii) Kukagua miradi ya ujenzi wa barabara na
majengo ili kuhakikisha kuwa inajengwa
59
na Wahandisi waliosajiliwa. Katika kipindi hiki, jumla ya miradi 504 ilikaguliwa. Aidha, Wahandisi wa kigeni 15 walibainika kufanya kazi bila usajili. Kati yao 8
walikuwa na sifa na hivyo walisajiliwa na 7 walikataliwa usajili kwa sababu hawakuwa na sifa za kutosha.
iii) Kuendelea kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa Wahandisi Wahitimu. Katika kipindi hiki Bodi ilisimamia mafunzo ya Wahandisi
wahitimu 651. Kati ya Wahandisi hao, Wahandisi wahitimu 189 wa kike wanafadhiliwa na Serikali ya Norway. Jumla ya Wahandisi wahitimu 2,224 wameshapitia mpango huu tangu uanzishwe mwaka 2003. Aidha, Wahandisi wahitimu zaidi ya 177 toka
Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali wameshahitimu mafunzo hayo na kusajiliwa na Bodi kama Wahandisi watalaamu.
iv) Kukagua miradi na kuhakiki kama Makandarasi wana Wahandisi wa kutosha na wenye uwezo kutekeleza miradi hiyo.
Katika kipindi cha 2012/13, Bodi ilikagua jumla ya miradi 104. Makandarasi waliobainika kutokuwa na Wahandisi wa kutosha, walielekezwa kuajiri Wahandisi.
60
Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi
86. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/13 lengo la Bodi lilikuwa kusajili Wabunifu Majengo 18, Wakadiriaji Majenzi 25, Wataalamu wenye sifa za kati 31, mafundi Sanifu 7, Warasimu (Draughtsmen) 3 na
Kampuni za Ubunifu Majengo 14 na Ukadiriaji Majenzi 9. Hadi kufikia Aprili, 2013, Bodi ilisajili Wabunifu Majengo 18 na Wakadiriaji Majenzi 25 na hivyo kufanya jumla ya wataalamu wa fani hizo waliosajiliwa na Bodi kuwa 549 (337 ni Wabunifu Majengo, 211 ni Wakadiriaji Majenzi
na “Building Surveyor 1). Aidha, Kampuni 11 za Wabunifu Majengo na Kampuni 9 za Wakadiriaji Majenzi zilisajiliwa na kufanya jumla ya kampuni zilizosajiliwa kuwa 270. Bodi pia iliwasajili wataalamu wa fani za sifa za kati 66. Bodi iliwafutia usajili Wabunifu Majengo 8,
Wakadiriaji Majenzi 7, makampuni 9 na kusitisha usajili wa Mbunifu majengo 1 kwa muda. Bodi pia ilisajili miradi ya ujenzi 774. Usajili wa miradi hiyo unasaidia kupatikana kwa taarifa za ujenzi kwa Serikali na pia wadau wote wa Sekta ya Ujenzi.
87. Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha
kwamba shughuli za majenzi zinasimamiwa na kampuni za Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi waliosajiliwa, Bodi ilikagua miradi ya
61
ujenzi 2,112 katika mikoa 21 ya Tanzania Bara. Tathmini ya ukaguzi huo imeonesha kuwa kuna uelewa mdogo kwa waendelezaji kuhusu umuhimu wa kutumia ushauri wa Wabunifu
Majengo na Wakadiriaji Majenzi katika kuendeleza miradi ya ujenzi. Wengi wanachanganya taaluuma hizi na Wahandisi au Makandarasi. Bodi ilichukua hatua za kuwaelimisha wadau husika umuhimu wa kuwatumia wataalamu hao katika miradi ya
ujenzi wa majengo. Bodi ya Usajili wa Makandarasi 88. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Bodi ya Usajili wa Makandarasi
ilipanga kusajili jumla ya Makandarasi 807 na kutathmini Makandarasi 587 ili kujiridhisha kama wana sifa na uwezo wa kuendelea kuwa katika madaraja waliyopo. Aidha, Bodi ilipanga kukagua miradi ya ujenzi 3,090 nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha kwamba kazi zote
zinafanywa na Makandarasi waliosajiliwa na pia kuwa makandarasi wanafuata sheria na taratibu za usajili wao.
89. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2013 Bodi ilisajili Makandarasi wapya 813, na ilifuta Makandarasi 366 walioshindwa kuzingatia sheria na taratibu za ukandarasi. Hivyo hadi kufikia Aprili, 2013, Bodi ilikuwa na
62
Makandarasi 6,991. Aidha, Bodi ilikagua jumla ya miradi 2,480. Katika miradi iliyokaguliwa miradi 1,672 sawa na asilimia 67.4 ilionekana kutekelezwa kwa kuzingatia sheria na taratibu
za usajili na miradi 808 ambayo ni asilimia 32.6 ilikiuka sheria na taratibu hizo. Makandarasi husika walichukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ya Usajili wa Makandarasi Namba 17 ya mwaka 1997 kama ilivyorekebishwa na Sheria Namba 24 ya mwka 2008.
90. Mheshimiwa Spika, Bodi pia
imeendeleza programu za kuendeleza Makandarasi, kuimarisha mfuko wa kusaidia Makandarasi wadogo na kukuza uwezo wa Makandarasi wazalendo.
Baraza la Taifa la Ujenzi
91. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2012/13 Baraza liliendelea kutekeleza majukumu yake ya kushughulikia maendeleo ya
Sekta ya Ujenzi nchini. Baraza liliendesha mafunzo kwa wadau 163 wa sekta kuhusu shughuli za zabuni, menejimenti ya mikataba, usuluhishi wa migogoro, menejimenti ya madai, gharama za ujenzi wa barabara, shughuli za matengenezo na ukarabati wa majengo. Baraza
liliandaa mafunzo maalum (Tailor Made Course) yaliyofanyikia Mtwara kwa ajili ya Halmashauri ya Mtwara, ambapo wadau 13 walipatiwa
63
mafunzo kuhusu matumizi ya mitambo ya kisasa kwenye upimaji na ramani, usimamizi wa miradi ya ujenzi na usuluhishi wa migogoro ya miradi ya ujenzi. Aidha, Baraza lilifanya tafiti
zifuatazo: i) Upimaji wa tija na ubora wa kazi katika
Sekta ya Ujenzi, ii) Ushindani wa Makandarasi wazalendo
katika kutekeleza miradi ya ujenzi
ikilinganishwa na Makandarasi wa kigeni, iii) Kanuni za mikataba katika utekelezaji wa
miradi ya ujenzi wa miundombinu (barabara, n.k.), na
iv) Usimamizi wa miradi ya ujenzi wa miundombinu kwa njia ya Kusanifu na
kujenga (Design and Build).
92. Mheshimiwa Spika, Baraza katika mwaka 2012/13 liliendelea kutoa ushauri wa kiufundi kwa wadau mbalimbali ikiwa ni
pamoja na Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC), National Ranch Corporation (NARCO), National Audit Office (NAO) na Roads Fund Board (RFB). Aidha, Baraza lilishughulikia usuluhishi wa migogoro ya
miradi ya ujenzi ipatayo 39. Vikosi vya Ujenzi
93. Mheshimiwa Spika, Majukumu ya Vikosi vya Ujenzi ni kufanya kazi za ujenzi na
64
ukarabati wa majengo na shughuli zingine zinazohusiana na ujenzi. Aidha, Vikosi vina jukumu la kubuni na kutekeleza miradi yoyote ya kibiashara yenye mahusiano na kazi za
ujenzi. Makao Makuu ya vikosi yapo Dar es Salaama. Vikosi vina matawi Arusha, Dodoma na Mwanza.
94. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2012/13 Vikosi vimekamilisha ujenzi wa maegesho (Ferry ramps) ya Rugezi kwa ajili ya Kivuko cha Rugezi – Kisorya, Ukerewe Mwanza. Aidha, Vikosi vimekamilisha ukarabati wa Ofisi zake Dar es Salaam na Mwanza na kuanza
ukarabati wa Karakana za useremala (Carpentry workshops) Dar es Salaam na Dodoma. Vikosi vinaendelea na ujenzi wa nyumba za viongozi Dar es Salaam na Mwanza ukiwemo ujenzi wa nyumba za Majaji Dar es Salaam na Mwanza (Phase I).
95. Mheshimiwa Spika, miradi mingine iliyofanywa na Vikosi ni pamoja na ujenzi wa maegesho ya Kivuko cha Msangamkuu-(Mtwara), ukarabati wa Jengo la Hospitali ya
Rufaa Mbeya, ukarabati wa Majengo ya Ofisi na Nyumba za watumishi Siha (Kilimanjaro), ujenzi wa uzio katika Kivuko cha Kigamboni, ujenzi wa uzio katika eneo la kuegesha magari Kimara (Dar es Salaam) na ujenzi wa uzio katika Kiwanja cha Ndege cha Ziwa Manyara.
65
Kituo cha Usambazaji wa Tekinolojia katika Sekta ya Ujenzi na Uchukuzi (Tanzania Transportation Technology Transfer Centre-)
96. Mheshimiwa Spika, madhumuni ya Kituo hiki ni kuimarisha Sekta ya Ujenzi na
Uchukuzi kwa kusambaza tekinologia za kisasa kwa wadau wa sekta hizi.
Katika mwaka 2012/13, Kituo kilisambaza makala na taarifa 82 kwa wadau 94,500 zinazoelezea tekinolojia mbalimbali katika Sekta
ya Ujenzi na Uchukuzi. Kituo kimeendelea na maandalizi ya Mradi unaolenga kuboresha mifumo ya ujenzi, matengenezo na usimamizi wa miundombinu ya barabara na uchukuzi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Morgan State University ya Marekani.
Chuo cha Ujenzi – Morogoro
97. Mheshimiwa Spika, Chuo cha Ujenzi Morogoro katika mwaka 2012/13 kilipanga kuendeleza ujenzi wa jengo jipya la madarasa na karakana ya ufundi, kukarabati majengo 3, pamoja na kununua samani na zana za kufundishia. Aidha, chuo kilipanga kufundisha
jumla ya wanafunzi 780 katika fani za fundi stadi wa kazi za barabara, majengo pamoja na udereva. Hadi kufikia Aprili, 2013, jumla ya wanafunzi wa fani za ujenzi 662 walipata mafunzo kama ifuatavyo: Basic technical course
66
(224), Basic driving course (201), Passenger Service Vehicle (PSV) Driving course (140) na Technician Maintenance Management course (97).
Katika kipindi hiki Chuo kimefanya ukarabati
wa majengo ikiwa ni pamoja na karakana ya umeme wa majumbani na magari. Aidha, ujenzi wa jengo jipya ya karakana na madarasa unaendelea. Chuo kililinunua vifaa mbalimbali vya kufundishia na matumizi ya wanafunzi.
Chuo cha Matumizi Stahiki ya Nguvu Kazi- Mbeya
98. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/13 Chuo cha Mafunzo ya Teknolojia
Stahiki ya Nguvukazi–Mbeya (ATTI) kimetoa mafunzo kwa Wahandisi 18 kutoka Somalia na Mafundi Sanifu 30 kutoka nchini. Aidha, Chuo kimetoa ajira kwa wananchi 150 kupitia mafunzo ya vitendo kuhusu ukarabati na matengenezo ya barabara kwa Teknolojia
Stahiki ya Nguvukazi. Chuo pia kimetoa elimu ya ukarabati na matengenezo ya barabara kwa wanavijiji wapatao 550 waliopo jirani na kukarabati barabara za wanavijiji jumla ya kilometa 11 kwa kujitolea kwa lengo la kuwaelimisha umuhimu wa utunzaji wa
barabara zinazowazunguka. Aidha, Chuo kimefanya matengenezo na ukarabati wa jumla ya kilometa 88.5 kwa barabara za mafunzo.
67
C: MAKADIRIO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2013/2014
Makadirio ya Mapato 2013/2014 99. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Wizara ya Ujenzi inatarajia kukusanya jumla ya Shilingi 45,047,550.00 kutoka Idara zenye vyanzo vya mapato ambazo ni Idara za Utawala na Rasilimali Watu, Huduma za Ufundi
na Idara ya Menejimenti ya Ununuzi. Sehemu kubwa ya mapato hayo itatokana na ada za kusajili magari, pikipiki, bajaji na mitambo ya Serikali kwa namba za Serikali.
Matumizi ya Kawaida 2013/2014
100. Mheshimiwa Spika, bajeti ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara kwa mwaka 2013/14 ni Shilingi 381,205,760,000.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 21,211,514,000.00 ni kwa
ajili ya Mishahara ya Watumishi, Shilingi 6,944,846,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi, na Shilingi 353,049,400,000.00 ni fedha za Mfuko wa Barabara.
Makadirio ya Bajeti ya Maendeleo kwa Mwaka 2013/2014
101. Mheshimiwa Spika, vipaumbele vya
miradi ya maendeleo itakayotekelezwa na
68
Wizara kwa mwaka 2013/14 vimezingatia
miradi inayoendelea kutekelezwa, miradi
inayofadhiliwa na wahisani, utekelezaji wa
miradi iliyo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya
mwaka 2010 na Mpango wa Maendeleo wa
Miaka Mitano (2011/12 – 2015/16).
102. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/2014 Wizara ya Ujenzi imetengewa kiasi
cha Shilingi 845,225,979,000.00 kwa ajili ya
miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi
448,174,599,000.00 ni fedha za ndani na
Shilingi 397,051,380,000.00 ni fedha za nje.
Mgawanyo wa fedha za maendeleo pamoja na
miradi iliyotengewa fedha kwa mwaka
2013/2014 ni kama inavyooneshwa katika
Kiambatisho Na.1. Aidha, maelezo ya kila
mradi ni kama ifuatavyo: -
VIVUKO NA NYUMBA ZA SERIKALI Ujenzi wa Maegesho ya Vivuko Shilingi Milioni 5,990.00 103. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14 Wizara ya Ujenzi kupitia TEMESA
itaendelea kujenga maegesho (Landing Ramps)
69
ya vivuko ili vivuko viweze kuegeshwa kwa urahisi na usalama.
Mradi huu umetengewa Shilingi milioni
5,990.00 kwa ajili ya kazi zifuatazo: ujenzi wa maegesho ya kivuko cha Msanga Mkuu awamu ya II (Shilingi milioni 150.00), Ujenzi wa maegesho ya Kilambo (Shilingi milioni 115.00), kumalizia ujenzi wa maegesho ya Ukara (Shilingi milioni 185.00) na kumalizia ujenzi wa
maegesho Kilombero (upande wa Ulanga) (Shilingi milioni 50.00). Aidha, ujenzi wa maegesho ya Kahunda – Maisome umetengewa Shilingi milioni 854.00, ujenzi wa maegesho Itungi Port (Shilingi milioni
375.00), ujenzi wa maegesho Ilagala Shilingi milioni 250.00, ujenzi wa maegesho mwambao mwa baharí ya Hindi katika maeneo ya Magogoni, Jangwani Beach na Rungwe Oceanic Shilingi milioni 2,500.00 na kumalizia ujenzi wa maegesho ya Bugolora Shilingi milioni 54.00.
Upanuzi wa sehemu ya Maegesho ya Kigamboni umetengewa Shilingi milioni 346.00, upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa maegesho ya usafiri wa majini kati ya Dar es Salaam – Bagamoyo Shilingi milioni 215.00, na ujenzi wa vituo vya kusubiria kivuko kati ya Dar es
Salaam – Bagamoyo katika maeneo ya Govenor Jet (Kivukoni), Jangwani Beach na Rungwe Oceanic Hotel Shilingi milioni 600.00. Upembuzi
70
yakinifu kwa lengo la kuanzisha usafiri wa majini katika mwambao wa Ziwa Victoria ili kupunguza msongamano katika jiji la Mwanza umetengewa Shilingi milioni 200.00. Shilingi
milioni 96 zimetengwa kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hii. Ununuzi wa Vivuko Vipya - Shilingi Milioni 4,484.00
104. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 4,484.00 kwa ajili ya ununuzi wa Kivuko kipya cha Dar es Salaam - Bagamoyo, boti ya uokoaji, mashine za kisasa za kukatia tiketi (ticket vending machines) kwa kivuko cha
Magogoni na vifaa vya karakana za TEMESA. Ukarabati wa Vivuko - Shilingi Milioni 2,102.21
105. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha wa 2013/2014, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,102.21 kwa ajili ya ukarabati wa vivuko mbalimbali nchini.
Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali - Shilingi Milioni 2,245.49) 106. Mheshimiwa Spika, mradi wa kujenga
na kukarabati nyumba kwa ajili ya makazi ya
71
Viongozi na Watumishi wa Serikali utaendelea kwa kutoa kipaumbele katika ujenzi wa nyumba za Majaji pamoja na viongozi wengine wa Serikali wenye stahili ya kupewa nyumba na
Serikali. 107. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 1,010.43 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa nyumba za Majaji katika Mikoa ya
Kilimanjaro (1), Mtwara (1), Kagera (1), Dar es Salaam (1) na Shinyanga (1). Shilingi milioni 250.00 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bariadi Mkoani Simiyu.
108. Mheshimiwa Spika, Wizara imetenga jumla ya Shilingi milioni 220 ajili ya kufanya ukarabati pamoja na kuendelea na ujenzi wa uzio kuzunguka nyumba za viongozi katika nyumba za viongozi wa Serikali zilizopo Mikocheni, Kijitonyama na Msasani Peninsullar.
Shilingi milioni 240.50 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa samani katika nyumba za viongozi wa Serikali wenye stahili hiyo. 109. Mheshimiwa Spika, kiasi cha Shilingi
milioni 150.00 zimetengwa kwa ajili ya
kuendelea na ukarabati wa karakana za TEMESA na Shilingi milioni 40 kwa ajili ya ukarabati wa karakana na ofisi za Vikosi vya
72
Ujenzi Dar es Salaam na Dodoma. Aidha, Shilingi milioni 140.00 zimetengwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Shilingi milioni 113.44 kwa
ajili ya kazi za ushauri na Shilingi milioni 81.12 zimetengwa kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi.
110. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi kwa kupitia Wakala wa Majengo imeanza kutekeleza mradi wa kujenga nyumba 10,000 kwa ajili ya kuishi na kuwauzia wafanyakazi wa Serikali. Wakala umesajili Kikosi cha Ujenzi (Tanzania Building Agency Construction Co.); pamoja na kuwapatia mafunzo maalum
wataalamu wa vikosi vya ujenzi vya Jeshi la Polisi, Magereza, JKT na kikosi cha Wizara ya Ujenzi (CSWS) ambao watashiriki katika mradi huu. Maandalizi na mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa nyumba nyingi kwa muda mfupi.
Aidha, Wakala umepata jumla ya viwanja 2,490 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 10,000 kama ifuatavyo: Arusha (29), Dar es Salaam (627), Dodoma (37), Geita (24), Iringa (54), Kagera (2), Katavi (100), Kigoma (164), Kilimanjaro (63),
Lindi (41), Manyara (32), Mara (267), Mbeya (74), Morogoro (15), Mtwara (90), Mwanza (63), Njombe (102), Rukwa (70), Ruvuma (8), Shinyanga (131), Simiyu (308), Singida (22), Tabora (42), Tanga (123), na Pwani (2). Kati ya
73
viwanja hivyo, jumla ya viwanja 413 vimepata hati miliki kama vifuatavyo: Dar es Salaam (314), Arusha (5), Iringa (53) na Lindi (41). Vile vile Wakala umeanza kazi ya ujenzi wa nyumba
132 kati ya nyumba 2,500. Nyumba 25 Bunju “B” DSM zimefikia hatua ya umaliziaji. Nyumba 87 Bunju “B” DSM; nyumba 20 katika mikoa mipya ya Simiyu (4), Geita (4), Njombe (4), Katavi (4) pamoja na Chalinze, Pwani (4) zitaanza kujengwa katika mwaka 2012/13.
Mradi huu maalum utatumia fedha za Wakala zitokanazo na mauzo ya nyumba na mikopo kutoka Taasisi za Fedha. Baadhi ya Taasisi hizo zimeonesha nia thabiti ya kushirikiana na Wakala.
111. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wakala utakamilisha mazungumzo na Taasisi za fedha ili kuweza kupata mkopo wa ujenzi; utakamilisha ujenzi wa nyumba 25 katika eneo la Bunju “B” na utaandaa upembuzi
yakinifu na usanifu wa majengo kwa ajili ya ujenzi katika mikoa 12 ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Mtwara, Iringa, Lindi, Simiyu, Geita, Njombe na Katavi. Aidha, Wakala utaendelea na ujenzi wa nyumba 2,500 katika mikoa ya DSM (1,400), Arusha
(150), Dodoma (250), Mwanza (150), Mbeya (150), Mtwara (100), Iringa (100), Lindi (50), Bariadi (50), Geita (50), Njombe (50) na Mpanda (50).
74
BARABARA NA MADARAJA
Barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (Expressway) km 200, Sehemu ya Dar es Salaam – Chalinze (km 100) – Shilingi Milioni 100
112. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga barabara ya Dar es Salaam – Chalinze –
Morogoro (km 200) sehemu ya Dar es Salaam – Chalinze (km 100) kwa kiwango cha “Expressway”. Maandalizi ya mradi huu utakaotekelezwa kwa ubia baina ya Serikali na makampuni binafsi yameanza. Baada ya mradi kutangazwa Kampuni 19 zimewasilisha maombi
ya kujenga barabara hii na kuonyesha jinsi ambavyo watatekeleza mradi huu. Uchambuzi wa maombi ya kampuni hizo unaendelea
113. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, kiasi cha Shilingi milioni 100.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa Awamu ya Kwanza itakayohusisha sehemu ya Dar es Salaam – Chalinze (km 100).
Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo – Msata (sehemu ya Bagamoyo – Msata (km 64) - Shilingi milioni 10, 885.24 114. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ya Bagamoyo – Makofia - Msata (km 64). Mkataba
75
wa Ujenzi ulisainiwa tarehe 11 Agosti 2010 kwa gharama ya Shilingi milioni 89,610. Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami inaendelea. Lengo pia ni kuendelea na usanifu
wa barabara ya Bagamoyo – Sadani – Tanga (km 178).
115. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 10,441.10 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Bagamoyo – Msata (km 64) kwa kiwango cha lami. Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 444.14 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na usanifu
wa barabara ya Bagamoyo – Sadani – Tanga (km 178).
Barabara ya Usagara – Geita – Kyamyorwa (km 422) Sehemu ya Uyovu – Biharamulo (km 112) - Shilingi Milioni 10,800.00
116. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kyamyorwa – Buzirayombo – Geita hadi Usagara (km 310) na sehemu ya Uyovu - Biharamulo (km 112). Awamu ya kwanza ilihusisha ujenzi wa Barabara ya Kyamyorwa - Geita (km 220) ambayo ilikamilika Februari,
2008. Awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa barabara ya Geita - Usagara (km 90) ambapo ujenzi wake ulianza Februari, 2008 na umekamilika Januari, 2010. Awamu ya tatu
76
itahusisha ujenzi wa barabara ya Uyovu - Biharamulo kupitia Bwanga (km 112). 117. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Uyovu – Biharamulo (km 112), kiasi cha Shilingi milioni 800.00 kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kyamiyorwa –Buzirayombo (km120)
na kiasi cha Shilingi milioni 2,000.00 kimetengwa kwa ajili ya malipo ya mwisho ya sehemu ya Geita - Usagara (lot 1 na 2) (km 90).
Barabara ya Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 443) – Shilingi Milioni 51,669.34
118. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unalenga kufanya usanifu na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kati ya Kigoma na Tabora (km 443) pamoja na ujenzi wa daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi na barabara za maingilio ya daraja (km 48). Kazi ya ujenzi wa daraja ilianza tarehe 2 Desemba, 2010 na
inatarajiwa kukamilika Desemba, 2013. Ujenzi wa barabara ya Kidahwe - Uvinza (km 76.6) ulianza tarehe 17 Desemba, 2010 na kazi za ujenzi zinaendelea. Ujenzi wa barabara za Tabora-Ndono (km 42) na Ndono-Urambo (km 52) ulianza tarehe 3 Januari, 2011.
77
119. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 2,131.95 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,693.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya
kuendelea na ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Kidahwe-Uvinza (km 76.6). Kiasi cha Shilingi milioni 3,139.53 fedha za ndani na Shilingi milioni 10,130.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Daraja la Kikwete. Kiasi cha Shilingi milioni
6,837.80 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Tabora - Ndono (km 42), Shilingi milioni 7,189.04 kwa ajili ya sehemu ya Ndono -Urambo (km 52) na kiasi cha Shilingi milioni 4,848.02 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Urambo –
Kaliua – Ilunde ( km 146). Barabara za Tabora – Sikonge (km 70) na Uvinza – Malagarasi (km 51) zimetengewa kiasi cha Shilingi milioni 6,700 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.
Barabara ya Marangu – Tarakea – Kamwanga/Bomang’ombe – Sanya Juu (km 173) na Arusha – Moshi – Holili (km 140) – Shilingi Milioni 11,133.63
120. Mheshimiwa Spika, mradi huu unalenga kujenga barabara ya Marangu –
Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 96) kwa kiwango cha lami na kukarabati barabara ya
78
Arusha – Moshi – Holili pamoja na Arusha By-Pass (km 140). Ujenzi wa sehemu ya Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 32) ulikamilika Septemba, 2009 na ujenzi wa sehemu ya
Tarakea – Rombo Mkuu (km 32) ulikamilika Januari, 2011. Kazi za ujenzi wa sehemu ya Marangu – Rombo Mkuu na Kilacha – Mwika (km 32 ) zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika Septemba, 2013. 121. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 488.00
fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipia
sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi wa
Tarakea – Rombo na Shilingi milioni 2,146.00 ni
kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya
Marangu – Rombo Mkuu na Mwika- Kilacha (km
34). Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 5,000.00
kimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya
ujenzi wa sehemu ya Sanya Juu – Kamwanga
(km 75). Jumla ya Shilingi milioni 1,000.00
fedha za ndani zimetengwa kuanza ujenzi wa
barabara ya njia nne katika mradi wa Arusha –
Moshi – Holili/Taveta-Voi sehemu ya Sakina-
Tengeru (km 14.10) na ujenzi wa Arusha Bypass
(km 42.41). Aidha, Shilingi milioni 2,500
zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa
barabara ya KIA-Mererani (km 26).
79
Barabara ya Nangurukuru - Mbwemkulu (km 95) – Shilingi Milioni 2,000.00 122. Mheshimiwa Spika, mradi huu ni
sehemu ya barabara ya Dar es Salaam – Lindi – Mingoyo. Ujenzi wa barabara hii ulikamilika Januari, 2008. Katika mwaka 2013/14, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho kwa Mkandarasi.
Barabara ya Dodoma – Manyoni (km 127) – Shilingi Milioni 1,309.28 123. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara
ya Dodoma - Manyoni (km 127) kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi unagharamiwa na Serikali ya Tanzania na ulikamilika Novemba, 2009. Katika mwaka wa fedha 2013/14, jumla ya Shilingi milioni
1,309.28 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya mchepuo kuingia Manyoni mjini (km 4.8) na kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi.
Barabara ya Mbwemkulu – Mingoyo (km 95) – Shilingi milioni 1,000.00 124. Mheshimiwa Spika, mradi huu
umehusisha kujenga kwa kiwango cha lami
80
barabara ya Mbwemkuru - Mingoyo yenye urefu wa kilomita 95 kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu ni sehemu
ya barabara ya Dar es salaam – Lindi – Mingoyo na ujenzi wake ulikamilika Desemba, 2007. Katika bajeti ya mwaka 2013/2014, barabara hii imetengewa kiasi cha Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya mkandarasi.
Barabara ya Manyoni – Singida: Sehemu ya Manyoni – Isuna (km54) – Shilingi Milioni 1,200 .00 125. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Manyoni - Isuna (km 54) kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga (Design & Build). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Ujenzi ulikamilika tarehe 7 Januari, 2011.
Katika bajeti ya mwaka 2013/2014, barabara hii imetengewa Shilingi milioni 1,200.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya mkandarasi. Barabara ya Port Access (Nelson Mandela - km15.6) Rehabilitation – Shilingi Milioni 1,500.00
126. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu lilikuwa ni kukarabati na kuimarisha
81
barabara ya Nelson Mandela (km15.6) iliyokuwa imeharibika ili kurahisisha kupita kwa magari ya mizigo yanayotoka au kuingia Bandari ya Dar es Salaam na kupunguza msongamano wa
magari kwa jiji la Dar es Salaam. Katika bajeti ya mwaka 2013/2014, barabara hii imetengewa Shilingi milioni 1,500.00 fedha za ndani kwa ajili ya kulipa malipo ya mwisho ya mkandarasi.
Barabara ya Dumila – Kilosa (km 78) – Shilingi Milioni 6,000.00 127. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara Dumila – Kilosa (km 78). Kazi ya ujenzi wa barabara ya Dumila - Rudewa (km 45) ilianza
Februari, 2010 na ujenzi unaendelea. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka 2013/2014 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 6,000.00 fedha za ndani kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.
Barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port (km 112) – Shilingi Milioni 11,241.37 128. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unalenga kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Sumbawanga –Matai-Kasanga Port
(km. 112) kwa kiwango cha lami. Mradi unagharamiwa na Serikali ya Tanzania na unatekelezwa kwa utaratibu wa kusanifu na
82
kujenga. Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 8 Oktoba, 2009 na kazi ilianza Januari, 2010. Mkandarasi anaendelea na kazi za ujenzi. Katika mwaka wa fedha 2013/2014, kiasi cha
Shilingi milioni 11,241.37 fedha za ndani kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi. Ujenzi wa Madaraja Makubwa (Nangoo, Kirumi, Sibiti, Kilombero Maligisu, Kavuu, Mbutu, Ruhuhu, Ruhekei na Momba; na Ununuzi wa Emergency Bridge Parts) – Shilingi Milioni 21,500.00 129. Mheshimiwa Spika, mradi huu ni wa
kujenga/kukarabati madaraja makubwa kwenye barabara kuu. Madaraja hayo ni Daraja la
Nangoo kwenye barabara ya Mingoyo – Masasi – Tunduru, Daraja la Kilombero kwenye barabara ya Mikumi - Ifakara – Mahenge, Daraja la Maligisu (Mwanza) kwenye barabara ya Bukwimba – Kadashi - Maligisu, Daraja la Kavuu kwenye barabara ya Majimoto-Inyonga,
Daraja la Ruhekei katika barabara ya Mbinga-Mbamba Bay, Daraja la Kirumi (Mara), Daraja la Sibiti kwenye barabara ya Ulemo – Gumanga – Sibiti, Daraja la Mbutu kwenye barabara ya Igunga- Manonga, Daraja la Ruhuhu (Ruvuma) na Daraja la Momba kwenye barabara ya
Sitalike-Kilyamatundu/Kamsamba - Mlowo (Rukwa/Mbeya Border). Aidha, mradi
83
unahusisha kununua Madaraja ya Chuma ya dharura (Compact Emergency Bridge).
130. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Daraja la Nangoo limetengewa kiasi cha Shilingi milioni 500.00, Daraja la Maligisu Shilingi milioni 200; Daraja la Sibiti Shilingi milioni 3,000.00, Daraja la Kilombero Shilingi milioni 7,500.00, Daraja la Kavuu Shilingi
milioni 1,000.00, Daraja la Mbutu Shilingi milioni 5,300.00, Daraja la Ruhekei Shilingi milioni 250.00, Daraja la Momba Shilingi 2,000.00. Aidha, Shilingi milioni 50.00 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa madaraja ya chuma ya dharura na mtambo wa kukagua
madaraja (Compact Emergency Bridge na Under Bridge Inspection Lorry) na Shilingi milioni 200.00 kwa ajili ya usanifu wa daraja la Ruhuhu. Ukarabati wa daraja la Kirumi umetengewa Shilingi milioni 1,500.00. Fedha
zote ni fedha za ndani. Barabara ya New Bagamoyo (Kawawa Jct - Tegeta km 17) – Shilingi Milioni 20,500.00 131. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kupanua barabara ya kuanzia makutano ya barabara za Kawawa na Ali Hassan Mwinyi eneo la Morocco hadi Tegeta kutoka njia mbili hadi njia nne ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara hiyo. Mradi huu
84
unafadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia Shirika la Maendeleo la JICA. Mradi huu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza inahusisha mradi wa Mwenge –
Tegeta (km12) na awamu ya pili ni mradi wa Kawawa Jnct – Mwenge (km 4.2)
132. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 jumla ya Shilingi milioni 2,500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 18,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi, kulipa fidia na kuhamisha
miundombinu kwenye eneo la ujenzi (mabomba ya maji, nguzo na nyaya za umeme/simu n.k). Barabara ya Kyaka –Bugene – Kasulo (km 178) – Shilingi Milioni 7,037.53 133. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
kwa mwaka 2013/14 ni kujenga barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo (sehemu ya Kyaka-Bugene) yenye urefu wa kilometa 59.1 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na Serikali kwa asilimia 100. Kazi ya ujenzi ilianza tarehe 15 Desemba, 2010 na kazi za ujenzi
zinaendelea. Katika mwaka wa fedha 2013/2014 jumla ya Shilingi milioni 7,037.53 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.
85
Barabara ya Isaka – Lusahunga (Km 242) na Lusahunga –Rusumo na Nyakasanza - Kobelo (km 150)- Shilingi Milioni 21,520.48 134. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kufanya ukarabati wa sehemu ya Isaka – Lusahunga (km 242) kwa kiwango cha lami kwa fedha za Serikali ya Tanzania. Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili za Isaka – Ushirombo (km 132) na Ushirombo – Lusahunga
(km 110). Mikataba ya ujenzi wa sehemu hizi ilisainiwa tarehe 18/08/2009. Kazi ya ujenzi kwa sehemu zote mbili inaendelea. 135. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/2014, barabara hii imetengewa fedha za
ndani Shilingi milioni 12,512.72 kwa sehemu ya Isaka – Ushirombo na Shilingi milioni 9,007.76 kwa sehemu ya Ushirombo – Lusahunga kwa ajili ya kuendelea na ukarabati. Barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora (km 264) – Shilingi Milioni 22,499.57 136. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Manyoni - Itigi – Tabora kwa kuanzia na sehemu ya Manyoni – Chaya (km 89.35) na
sehemu ya Tabora –Nyahua (km 85) kwa kutumia fedha za ndani. Mikataba ya ujenzi ilisainiwa tarehe 30 Julai, 2010 na kazi ya
86
ujenzi inatarajiwa kukamilika katika mwaka 2013/14 kwa sehemu zote mbili.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha
2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 10,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Tabora – Nyahua na Shilingi milioni 10,299.57 kwa sehemu ya Manyoni – Itigi – Chaya. Kwa barabara ya Nyahua - Chaya (km 90) kiasi cha
Shilingi milioni 2,200.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Barabara ya Korogwe – Handeni (km 65) – Shilingi Milioni 6,356.73
137. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Korogwe – Handeni (km 65). Mradi huu
unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi za ujenzi zinaendelea. Kwa mwaka 2013/2014 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 6,356.73 kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi. Barabara za Mikoa Shilingi Milioni 31,915.27 138. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kuzifanyia ukarabati barabara za Mikoa kwa kiwango cha changarawe, kujenga kwa kiwango cha lami na kujenga madaraja katika
87
mikoa ya Tanzania Bara. Katika mwaka wa fedha 2013/2014 kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ukarabati wa jumla ya kilometa 515.6 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa
35.5 kwa kiwango cha lami. Kazi za ukarabati kwa kiwango cha changarawe zitafanyika katika Mikoa yote. Aidha, ujenzi wa madaraja 17 utafanyika katika Mikoa ya Katavi (1), Morogoro (1), Mbeya (3), Manyara (1), Ruvuma (2), Simiyu (4), Lindi (1), Mtwara (1), Geita (1) na Rukwa (2).
Orodha ya Miradi ya barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Bajeti ya Maendeleo imeoneshwa katika Kiambatisho Na. 2. Barabara ya Mwanza/Shinyanga Border – Mwanza (km 10) Shilingi Milioni 50.00 139. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kuendelea na ukarabati wa sehemu zilizoharibika katika barabara ya Mwanza/Shinyanga Border - Mwanza kwa mwaka 2013/14 jumla ya Shilingi milioni 50.00
za ndani zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.
Barabara ya Handeni – Mkata (km 54) – Shilingi Milioni 4,484.75
140. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Handeni – Mkata (km 54). Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Kazi ya
88
ujenzi ilianza tarehe 28 Desemba, 2010 na umekamilika Novemba, 2012. Barabara hii imetengewa Shilingi milioni 4,484.75 kwa ajili ya kulipia sehemu ya madai ya mkandarasi.
Barabara ya Mwandiga – Manyovu (km 60) – Shilingi Milioni 1,234.35 141. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa
barabara ya kutoka Mwandiga hadi Manyovu
inayounganisha Mkoa wa Kigoma na nchi jirani ya Burundi kwa kiwango cha lami ulikamilika Oktoba 2010. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka 2013/2014 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 1,234.35 kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo
ya mwisho ya mkandarasi.
Miradi ya Kupunguza Msongamano ya Magari Katika Barabara za Dar Es Salaam – Shilingi Milioni 28,634.00
142. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam ulianza katika mwaka wa fedha 2009/10. Barabara hizo ni Ubungo Bus Terminal – Kigogo-Kawawa Roundabout (km 6.4), Kawawa Roundabout-
Msimbazi Valley – Jangwani/Twiga jct (km 2.7), Jet Corner – Vituka-Davis Corner (km 10.3) na ujenzi wa mfereji wa Bungoni unaoanzia
89
barabara ya Nyerere hadi Uhuru (Bungoni). Aidha, mradi wa mabasi yaendayo kasi (Bus Rapid Transit Infrastructure) na vituo vyake unaendelea.
143. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya
mwaka 2013/2014, kiasi cha Shilingi milioni 1,689.00 kimetengwa kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizobakia kwa barabara ya Ubungo Bus Terminal – Kigogo - Kawawa Roundabout,
Shilingi milioni 605.00 kwa barabara ya Kawawa Roundabout - Msimbazi Valley – Jangwani/Twiga Jct na Shilingi milioni 1,290.00 kwa ajili ya barabara ya Jet Corner – Vituka - Devis Corner.
Kiasi cha Shilingi milioni 3,000.00 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Ubungo Maziwa – External na Tabata Dampo – Kigogo, Shilingi milioni 5,000.00 kwa barabara ya Kimara – Kilungule – External, Shilingi milioni 6,000.00
kwa barabara ya Mbezi (Morogoro road) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana, Shilingi milioni 5,000.00 kwa barabara ya Tegeta - Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro road, Shilingi milioni 3,000.00 kwa barabara ya Tangi Bovu – Goba, Shilingi milioni 1,500.00
kwa barabara ya Kimara – Baruti – Msewe – Changanyikeni na Shilingi milioni 1,500.00 kwa barabara ya Kibamba - Kisopwa sehemu ya
90
Kibamba - Mlonganzila (km 4). Shilingi milioni 50.00 zitatumika kufuatilia na kusimamia Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo kasi.
144. Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi
milioni 1,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa
ajili ya maandalizi ya ujenzi wa ‘Fly Over’ ya
TAZARA na Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa
kwa ajili ya maboresho ya makutano ya
Chang'ombe, Ubungo, Magomeni, Mwenge,
Tabata/Mandela na Morocco kwa kutumia
mfumo wa Usanifu na Kujenga (Design and
Build). Aidha, Shilingi milioni 1,000.00
zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya upanuzi
wa sehemu ya Bendera Tatu – Gerezani
(KAMATA) katika barabara ya Dar es Salaam-
Mbagala (Kilwa road).
Barabara ya Ndundu – Somanga (km 60) - Shilingi Milioni 5,287.74 145. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unalenga kujenga barabara sehemu ya Ndundu
hadi Somanga (km 60) kwa kiwango cha lami.
Kazi za ujenzi zinaendelea. Barabara hii
imetengewa Shilingi milioni 5,287.74 fedha za
91
ndani katika mwaka 2013/2014 kwa ajili ya
kukamilisha kazi ya ujenzi.
Kidatu - Ifakara - Lupilo - Malinyi - Londo - Lumecha/Songea (km 396) - Shilingi Milioni 1,600.00 146. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu
wa kina wa barabara ya Kidatu hadi Lumecha/Songea chini ya msaada wa Benki ya Maendeleo ya Afrika na mchango wa Serikali ya Tanzania. Barabara hii imetengewa Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,500.00 fedha za nje kwa ajili ya kuanza
upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Barabara ya Tabora - Ipole - Koga – Mpanda (km 359) - Shilingi Milioni 2,000.00 147. Mheshimiwa Spika, Mkataba wa
kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulisainiwa tarehe 8 Juni, 2009 na kazi zimekamilika. Lengo la mradi ni utayarishaji wa nyaraka za zabuni za ujenzi wa barabara ya Tabora – Ipole – Koga – Mpanda kwa kiwango cha lami.
Katika mwaka wa fedha 2013/2014 jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 fedha za ndani
92
zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Barabara ya Makutano - Natta – Mugumu/ Loliondo – Mto wa Mbu (km 452) – Shilingi Milioni 8,617.63 148. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kufanya usanifu wa kina na kujenga barabara
hii kwa kiwango cha lami. Mradi huu
unagharamiwa na Serikali ya Tanzania.
Mikataba kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina
kwa sehemu ya Natta - Mugumu (km 50) na Mto
wa Mbu – Loliondo (km 213) ilisainiwa tarehe 26
Agosti, 2009. Kazi ya usanifu wa kina
imekamilika mwaka 2011. Katika mwaka wa
fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni
5,617.63 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili
ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa
sehemu ya Makutano -Sanzate (km 50) na
Shilingi milioni 3,000.00 kwa sehemu ya Mto
wa Mbu – Loliondo (km 213).
Barabara ya Ibanda – Itungi/Kiwira Port (km 26) – Shilingi Milioni 1,000.00 149. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kufanya ukarabati wa barabara hii kwa kiwango
93
cha lami. Barabara hii ni kiungo muhimu kwa bandari ya Itungi/Kiwira. Katika mwaka wa fedha 2013/2014 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 1,000.00 fedha za ndani kwa
ajili ya kuendelea na ukarabati ili kuiunganisha bandari mpya ya Kiwira. Barabara ya Nzega – Tabora (Km 115) – Shilingi Milioni 13,392.09 150. Mheshimiwa Spika, mradi unalenga
kujenga barabara ya Nzega – Tabora (km 115) kwa kiwango cha lami. Mradi huu umegawanyika katika sehemu mbili za Nzega-Puge (km 58.8) na Puge-Tabora (km 56.10). Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami
inaendelea kwa sehemu ya Nzega – Puge na sehemu ya Puge-Tabora. 151. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 6,696.05 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na
ujenzi wa sehemu ya Nzega – Puge na Shilingi milioni 6,696.04 kwa sehemu ya Puge – Tabora . Barabara ya Sumbawanga – Mpanda - Nyakanazi (km 829) – Shilingi Milioni 38,858.72
152. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Sumbawanga – Mpanda –
94
Kasulu – Nyakanazi kwa kiwango cha lami. Kazi
za ujenzi kwa sehemu ya Sumbawanga-Kanazi
(km 75) na Kanazi-Kizi-Kibaoni (km 75.6)
zinaendelea.
Katika mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya
Shilingi milioni 8,850.94 fedha za ndani
zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya
ujenzi wa sehemu ya Sumbawanga-Kanazi,
Shilingi milioni 8,850.94 kwa sehemu ya
Kanazi-Kizi-Kibaoni na Shilingi milioni 6,617.63
kwa sehemu ya Kizi-Sitalike-Mpanda. Kiasi cha
Shilingi milioni 4,539.21 kimetengwa kwa ajili
ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Mpanda-
Mishamo (km 100). Sehemu ya Kigoma –
Nyakanazi imetengewa Shilingi milioni
10,000.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa
kilometa 100 kwa kiwango cha lami.
Barabara ya Nyanguge – Musoma (km 183) na Mchepuo wa Usagara - Kisesa (km 17) – Shilingi Milioni 18,235.26
153. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kuikarabati barabara ya Nyanguge-Musoma (km
183) na kujenga kwa kiwango cha lami kilometa
17 za mchepuo wa Usagara - Kisesa. Ujenzi wa
95
sehemu ya Simiyu/Mara Border – Musoma (km
85.5) unaendelea. Maandalizi ya ujenzi kwa
kiwango cha lami kwa barabara ya Nansio -
Kisorya - Bunda sehemu ya Kisorya - Bunda
(km 50) yanaendelea.
154. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014, mradi huu umetengewa
Shilingi milioni 9,735.26 kwa ajili ya kuendelea
na kazi ya ukarabati wa barabara ya Nyanguge -
Musoma. Kiasi cha Shilingi milioni 4,000.00
kimetengwa kwa sehemu ya barabara ya Kisesa
– Usagara Bypass kwa ajili ya kuendelea na kazi
ya ujenzi.
Aidha, kiasi cha Shilingi milioni 4,500.00
kimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa
barabara ya Nansio - Kisorya - Bunda sehemu
ya Kisorya - Bunda (km 50).
Barabara ya Magole - Mziha (Magole-Turiani km 48.8) – Shilingi Milioni 6,266.84 155. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Magole – Mziha kwa kiwango cha lami. Jumla ya Shilingi milioni 6,266.84 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Magole - Turiani katika bajeti ya 2013/2014.
96
Barabara ya Mwigumbi – Maswa – Bariadi – Lamadi (km 171) – Shilingi Milioni 11,965.65 156. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi yenye jumla ya kilometa 171 kwa kiwango cha lami. Kazi zilianza tarehe 8 Julai, 2010 kwa sehemu ya Bariadi – Lamadi na kazi inaendelea. Aidha, maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwigumbi -
Maswa - Bariadi (km 100) yanaendelea.
Katika mwaka wa fedha 2013/2014, kiasi cha Shilingi milioni 6,465.65 kimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi wa barabara ya Bariadi – Lamadi. Aidha, kiasi cha Shilingi
milioni 5,500.00 kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi (km 100). Barabara ya Tabora - Ipole-Rungwa (Ipole-Rungwa – km 95) – Shilingi Milioni 500.00 157. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Tabora – Ipole – Rungwa
kwa kiwango cha lami kwa kuanza na sehemu
ya Ipole – Rungwa yenye urefu wa kilometa 95.
Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya
Tanzania na umetengewa Shilingi milioni 500.00
97
mwaka 2013/14 kwa ajili ya kukamilisha
upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.
Barabara ya Kwenda Uwanja wa Ndege wa Mafia (Mafia Airport Access Road - km 14) – Shilingi Milioni 2,471.17 158. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya kwenda Uwanja wa Ndege
wa Mafia kwa kiwango cha lami. Makubaliano
yaliyofikiwa kati ya Serikali na Shirika la
Misaada la Marekani (MCC) ni kwamba Serikali
itajenga barabara hii na MCC itatoa fedha za
ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mafia. Katika
mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi
milioni 2,471.17 zimetengwa kwa ajili ya kazi ya
ujenzi wa barabara.
Barabara ya Kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma (Dodoma University Road - km 12) – Shilingi Milioni 3,000.00 159. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Chuo Kikuu Dodoma kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa na
Serikali ya Tanzania. Jumla ya Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami katika mwaka 2013/2014.
98
Daraja la Kigamboni – Shilingi Milioni 3,000.00
160. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga daraja litakalounganisha Jiji la Dar es Salaam na mji wa Kigamboni. Katika mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 3,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi ya ujenzi. Mradi unajengwa
kwa ushirikiano kati ya Serikali na NSSF. Barabara ya Sam Nujoma (km 4) – Shilingi Milioni 21.51
161. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi lilikuwa ni kupanua barabara ya Sam Nujoma kutoka njia mbili kuwa njia nne pamoja na njia za waenda kwa miguu kuanzia Mwenge hadi
Ubungo. Mradi huu umegharamiwa na Serikali ya Tanzania na kazi za ujenzi wa barabara zilikamilika Julai, 2009. Shilingi milioni 21.51 fedha za ndani zimetengwa katika mwaka 2013/2014 kwa ajili ya kulipa sehemu ya malipo ya mwisho ya Mkandarasi.
Barabara ya Tunduma - Sumbawanga (km 223) – Shilingi Milioni 57.88 162. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Tunduma – Sumbawanga
yenye urefu wa kilomita 223 kwa kiwango cha lami. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za
99
msaada kutoka Serikali ya Marekani kupitia Millennium Challenge Corporation (MCC) na mchango wa Serikali ya Tanzania. Utekelezaji
wa mradi umegawanywa katika sehemu tatu ambazo ni:-Tunduma – Ikana (km 63.7); Ikana – Laela (km 64.0) na Laela – Sumbawanga (km 95.3).
Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14,
jumla ya Shilingi milioni 17.0 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuhamisha miundombinu katika eneo la ujenzi na usimamizi kwa sehemu ya Tunduma – Ikana, Shilingi milioni 17.0 zimetengwa kwa sehemu ya Ikana-Laela na Shilingi milioni 23.88 kwa
sehemu ya Laela – Sumbawanga. Barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 154) – Shilingi Milioni 14,477.25 163. Mheshimiwa Spika, mradi huu ni
sehemu ya barabara ya Mutukula – Bukoba – Biharamulo – Lusahunga (km 294) iliyofanyiwa usanifu mwaka 1996 chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika. Ujenzi wa sehemu ya barabara ya Mutukula – Muhutwe – Kagoma ulianza Machi, 2001 na ulikamilika Septemba
2004. Awali Benki ya Maendeleo ya Afrika ilitoa mkopo kwa ajili ujenzi wa sehemu ya Kagoma – Lusahunga (km 154) kwa kiwango cha lami. Baada ya Mkandarasi China State Construction
100
Engineering Corporation Ltd (CSCEC) wa China kushindwa kutekeleza mkataba wa awali na kuondolewa, mkataba mpya wa kumalizia ujenzi
wa barabara ya Kagoma – Lusahunga (km154) kwa kiwango cha lami ulisainiwa kwa fedha za Serikali ya Tanzania. Katika mwaka 2013/14 barabara hii imetengewa Shilingi milioni 14,477.25 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.
Barabara ya Arusha – Namanga (km 105) - Shilingi Milioni 3,517.12
164. Mheshimiwa Spika, mradi wa Arusha – Namanga (km 105) ni sehemu ya mradi wa kikanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaojumuisha nchi za Tanzania na Kenya. Kwa
sehemu ya Tanzania, mradi unafadhiliwa na Japan Bank for International Cooperation (JBIC) kwa kushirikiana na Serikali za Tanzania. Kazi za ukarabati wa barabara hii kwa kiwango cha lami zimekamilika Desemba, 2012.
Katika mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 1,228.12 fedha za ndani na Shilingi milioni 2,289.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi.
Barabara ya Singida - Babati – Minjingu - Arusha (km 321) - Shilingi Milioni 26,396.39 165. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ya
101
Singida - Babati -Minjingu yenye urefu wa kilomita 223 na kukarabati kwa kiwango cha lami sehemu ya Minjingu-Arusha yenye urefu wa kilometa 98.
Ujenzi wa barabara ya Singida - Babati - Minjingu umegawanywa katika sehemu tatu za Singida – Katesh (km 65.1), Katesh – Dareda (km 73.8) na Dareda – Babati – Minjingu (km 84.6). Kazi za ujenzi zilianza tarehe 11 Machi,
2009 na zimekamilika Agosti, 2012. Miradi hii inagharamiwa na ADB, JICA na Serikali ya Tanzania. Mkataba wa ukarabati wa sehemu ya Minjingu-Arusha umesainiwa tarehe 12 Mei, 2011 na kazi zinaendelea. Sehemu hii inakarabatiwa kwa kutumia fedha za mkopo
kutoka Benki ya Dunia. 166. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014 kiasi cha Shilingi milioni 240.56 zimetengwa kwa sehemu ya Singida – Katesh, Shilingi milioni 336.00 kwa ajili ya
sehemu ya Katesh – Dareda na Shilingi milioni 375.00 kwa ajili ya sehemu ya Dareda – Babati – Minjingu ili kukamilisha malipo ya Makandarasi wa sehemu zote tatu. Kiasi cha Shilingi milioni 444.83 fedha za ndani na Shilingi milioni 25,000.00 fedha za nje
zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ukarabati wa barabara ya Minjingu hadi Arusha.
102
Barabara ya Msimba – Ruaha/Ikokoto - Mafinga (km 219) – Shilingi Milioni 25,716.53
167. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kufanya ukarabati wa barabara ya lami ya Dar
es Salaam – Tunduma (TANZAM). Mradi huu
unahusisha ukarabati wa sehemu ya Iyovi -
Kitonga Gorge (km 86.3), Ikokoto - Iringa (km
60.9), barabara ya mchepuo kuingia Iringa
mjini (km 2.1) na Iringa-Mafinga (km 68.9).
Mradi huu unagharamiwa kwa mkopo kutoka
Serikali ya Denmark pamoja na mchango wa
Serikali ya Tanzania. Aidha, maandalizi ya
ukarabati kwa kiwango cha lami kwa barabara
ya Mafinga - Igawa (km 146) yanaendelea kwa
mkopo kutoka Benki ya Dunia.
168. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014 jumla ya Shilingi milioni
5,516.53 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili
ya kuendelea na ukarabati wa kilometa 68.9 za
Iringa - Mafinga. Aidha, jumla ya Shilingi milioni
200.00 fedha za ndani na Shilingi milioni
20,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya
ukarabati wa barabara ya Mafinga-Igawa yenye
urefu wa kilometa 146.
103
Barabara ya Korogwe – Mkumbara - Same (km 172)- Shilingi Milioni 53,621.38
169. Mheshimiwa Spika, mradi wa ukarabati wa barabara ya Korogwe - Mkumbara –Same (km 172) ambayo ni sehemu ya barabara
ya Segera – Moshi – Arusha unagharamiwa na Benki ya Dunia pamoja na Serikali ya Tanzania. Katika mwaka 2013/2014 kazi ya ukarabati wa barabara hii zitaendelea kama ifuatavyo:
(i) Korogwe – Mkumbara (km 76):
Katika mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani na
Shilingi milioni 32,671.38 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuendelea na kazi ya ukarabati wa sehemu hii ya barabara.
(ii) Mkumbara – Same (km 96):
Katika mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 100.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 20,750.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuendelea na kazi ya ukarabati wa sehemu hii ya barabara.
Barabara ya Mbeya-Makongolosi (km 115) – Shilingi Milioni 15,691.68 170. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga barabara ya Mbeya hadi Makongolosi
(km 115) kupitia Chunya kwa kiwango cha lami.
104
Ujenzi wa barabara hii umegawanyika katika
sehemu tatu ambazo ni: Mbeya – Lwanjilo (km
36); Lwanjilo-Chunya (km 36) na Chunya-
Makongolosi (km 43). Katika mwaka 2013/2014
barabara hii imetengewa jumla ya Shilingi
milioni 6,528.78 kwa ajili ya kuendelea na
ujenzi wa sehemu ya Mbeya-Lwanjilo, Shilingi
milioni 5,008.00 kwa sehemu ya Lwanjilo-
Chunya na Shilingi milioni 3,847.05 kwa
sehemu ya Chunya – Makongolosi. Aidha,
Shilingi milioni 307.84 zimetengwa kwa ajili ya
kukarabati sehemu ya Makongolosi – Rungwa –
Itigi – Mkiwa kwa kiwango cha changarawe.
Barabara ya Chalinze – Segera - Tanga (km 248) – Shilingi Milioni 7,700.00
171. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kuifanyia ukarabati na upanuzi barabara ya
Chalinze - Segera hadi Tanga. Utekelezaji wa
mradi umegawanyika katika sehemu mbili
ambazo ni: Chalinze-Kitumbi (km 125) na
Kitumbi-Segera-Tanga (km 120). Jumla ya
Shilingi milioni 3,200.00 fedha za ndani na
Shilingi milioni 4,500.00 fedha za nje
zimetengwa katika mwaka wa fedha 2013/14
kwa ajili ya kuendelea na ukarabati wa sehemu
ya Kitumbi-Segera-Tanga.
105
Barabara ya Dodoma – Iringa (km 260) – Shilingi Milioni 86,539.31 172. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Dodoma – Mtera – Iringa (km 260). Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
Ili kuendelea na ujenzi, katika mwaka wa fedha 2013/2014, kiasi cha Shilingi milioni 615.68 fedha za ndani na Shilingi milioni 30,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa sehemu ya Iringa – Migori (km 95.1), Shilingi milioni 538.72 ` fedha za ndani na Shilingi milioni 28,000.00 fedha za
nje kwa ajili ya sehemu ya Migori – Fufu Escarpment (km 93.8) na Shilingi milioni 584.90 fedha za ndani na Shilingi milioni 26,800.00 fedha za nje kwa ajili ya sehemu ya Fufu Escarpment – Dodoma (km 70.9).
Barabara ya Dodoma – Babati (km 261) – Shilingi Milioni 56,992.41 173. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya
Dodoma – Kondoa – Babati (km 261). Utekelezaji wa mradi huu umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni: Dodoma-Mayamaya (km 43.65), Mayamaya-Bonga (km198.15) na Bonga-Babati
106
(km 19.2). Katika mwaka wa fedha 2013/14, kiasi cha Shilingi milioni 6,606.15 zimetengwa kwa ajili ya sehemu ya Dodoma – Mayamaya na Shilingi milioni 2,386.26 kwa sehemu ya Bonga
– Babati. Aidha, ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Mayamaya – Bonga ambayo imegawanywa katika sehemu mbili utaanza katika mwaka 2013/14 kama ifuatavyo: (i) Mayamaya - Mela (km 99.35):
Katika mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 25,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi wa sehemu hii
ya barabara.
(ii) Mela - Bonga (km 98.8):
Katika mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 500.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 22,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili kuanza ujenzi wa sehemu hii ya barabara.
Masasi- Songea – Mbamba Bay (km 659.7) – Shilingi Milioni 136,327.08 174. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni
kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya
107
Masasi- Songea – Mbamba Bay (km 649). Katika mwaka wa fedha 2013/2014, Shilingi milioni 533.88 fedha za ndani na Shilingi milioni 24,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya
kuanza ujenzi wa sehemu ya Mangaka-Nakapanya na Shilingi milioni 532.57 fedha za ndani na Shilingi milioni 23,200.00 fedha za nje kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Nakapanya – Tunduru. Shilingi milioni 532.93 fedha za ndani na Shilingi milioni 24,000.00
fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Mangaka-Mtambaswala na Shilingi milioni 3,567.32 fedha za ndani na Shilingi milioni 16,809.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Tunduru-Matemanga.
175. Mheshimiwa Spika, kwa sehemu ya
Matemanga-Kilimasera, Shilingi milioni
3,679.20 fedha za ndani na Shilingi milioni
14,944.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili
kuendelea na ujenzi. Aidha, Shilingi milioni
3,679.19 fedha za ndani na Shilingi milioni
13,715.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya
sehemu ya Kilimasera – Namtumbo. Fedha
zilizotengwa kwa ajili ya fidia ni Shilingi milioni
17.00 fedha za ndani kwa barabara ya Songea –
Namtumbo na Shilingi milioni 17.00 fedha za
ndani kwa barabara ya Peramiho – Mbinga. Vile
vile Shilingi milioni 4,600.00 fedha za ndani
108
zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa
kiwango cha lami sehemu ya Mbinga-Mbamba
Bay na Shilingi milioni 2,500.00 fedha za ndani
zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa
kiwango cha lami sehemu ya Masasi - Newala –
Mtwara (km 209) .
Ujenzi wa Barabara ya Uongozi Institute Shilingi Milioni 1,500.00 176. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga barabara ya mchepuo kutoka barabara ya Bagamoyo kuingia kwenye Chuo cha Uongozi pamoja na barabara zilizoko ndani
ya chuo hicho. Katika mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni 1,500.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara ya mchepuo kutoka barabara ya
Bagamoyo kuingia Chuo cha Uongozi pamoja na barabara zilizoko ndani ya Chuo hicho. Ujenzi wa Makao Makuu ya Wakala wa Barabara – Shilingi Milioni 1,100.00 177. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga Makao Makuu ya Wakala wa Barabara pamoja na kuanza ujenzi wa Ofisi za mikoa ya Dar es Salaam, Katavi, Geita, Simiyu,
109
Njombe na Lindi. Mradi huu unagharamiwa kwa fedha za ndani. Usanifu wa jengo la Makao Makuu ya Wakala umekamilika. Katika mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya Shilingi milioni
1,100.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi. USALAMA BARABARANI NA MAZINGIRA Usalama Barabarani - Shilingi Milioni 3,387.00 178. Mheshimiwa Spika, mradi huu una
lengo la kuimarisha shughuli za kudhibiti uzito wa magari yanayotumia barabara. Katika mwaka wa fedha 2013/14, kiasi cha Shilingi
milioni 887 fedha za ndani na Shilingi milioni 2,500 fedha za nje zimetengwa. Kazi zitakazofanyika ni zifuatazo:-
(i) Ujenzi wa mizani ya kisasa inayopima uzito wa gari likiwa katika mwendo (Weigh in Motion) katika eneo la Vigwaza ambao umetengewa Shilingi milioni 224 fedha ya ndani;
(ii) Uanzishwaji wa Wakala wa Usalama
Barabarani nchini (National Road Safety Agency) ambao umetengewa Shilingi milioni 293 fedha ya ndani na Shilingi 1000 fedha ya nje;
110
(iii) Utafiti na tathmini wa ajali za barabarani ambao umetengewa Shilingi milioni 230 fedha ya ndani;
(iv) Ukaguzi wa hali ya usalama katika barabara (Road Safety Audit) Shilingi milioni 129 fedha ya ndani;na
(v) Uwekaji Mfumo wa Taarifa za Ajali
Barabarani (Road Accident Information
System) ambao umetengewa Shilingi milioni 11 fedha ya ndani na Shilingi milioni 1500 fedha ya nje.
Usalama Barabarani na Mazingira - Shilingi Milioni 891.98 179. Mheshimiwa Spika, mradi huu una
lengo la kugharamia shughuli za Usalama na Mazingira pamoja na Marekebisho ya Mfumo wa utekelezaji wa shughuli katika maeneo haya. Mradi huu unagharamiwa kwa pamoja kati ya
Serikali ya Tanzania na DANIDA.
Katika mwaka 2013/14 mradi huu umetengewa jumla Shilingi milioni 891.98. Kati ya fedha hizo Shilingi milioni 641.98 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 250 fedha za nje. Aidha, kiasi
cha Shilingi milioni 255 za ndani na Shilingi milioni 100 za nje zimetengwa kwa ajili ya kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa shule
111
za nyanda za juu kusini katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, Rukwa, Katavi na Ruvuma. 180. Mheshimiwa Spika, kiasi cha Shilingi
milioni 349.98 za ndani na Shilingi milioni 150
za nje zimetengwa kwa ajili ya kutoa Elimu ya
Usalama Barabarani kwa umma kupitia vyombo
vya habari, vipeperushi n.k (Road Safety
Awareness Campaign). Aidha, kiasi cha Shilingi
milioni 37 za ndani zimetengwa kwa ajili ya
kuwajengea uwezo watumishi.
Menejimenti na Utunzaji wa Mazingira - Shilingi Milioni 200.00 181. Mheshimiwa Spika, mradi huu una
lengo la kuelimisha na kuwezesha utekelezaji
wa Sheria ya Mazingira katika sekta ya Ujenzi.
Katika mwaka wa fedha 2013/14 kiasi cha
Shilingi milioni 200.00 fedha za ndani
zimetengwa kwa ajili ya kusimamia utekelezaji
wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004
kwa miradi ya ujenzi. Lengo lingine ni kutoa
mafunzo kuhusu tathmini na usimamizi wa
mazingira katika sekta ya ujenzi kwa
Wataalamu wa TANROADS, TEMESA, TBA,
Vikosi vya Ujenzi na wadau mbalimbali katika
sekta ya Ujenzi.
112
Programu ya Kujenga Uwezo (Institutional Support) - Shilingi Milioni 500.131 182. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unalenga kujenga uwezo (capacity building) wa wataalamu wa Wizara ya Ujenzi.
Katika mwaka 2013/14 mradi huu umetengewa Shilingi milioni 200.131 fedha za ndani na Shilingi milioni 300.00 fedha za nje. Fedha hizo
zitatumika kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika fani zao, pamoja na kununua vitendea kazi. Fedha za Mfuko wa Barabara kwa Mwaka 2013/14 183. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Mfuko wa Barabara unatarajiwa kukusanya jumla ya Shilingi 504,306,000,000.00 ikilinganishshwa na
Shilingi 429,664,000,000.00 katika mwaka 2012/13. Hii ni ongezeko la Shilingi 74,642,000,000.00 sawa na asilimia 17.37. Kimsingi, fedha hizi ni kwa ajili ya matengenezo ya barabara na zinagawanywa kwa Wizara ya Ujenzi na TAMISEMI kwa kuzingatia Sheria ya
Tozo za barabara ya mwaka 1998 kama ilivyorekebishwa mwaka 2006. Kati ya fedha hizo, Wizara ya Ujenzi na Taasisi zake
113
imetengewa Shilingi 353,049,400,000.00 ikilinganishwa na Shilingi 300,764,800,000.00 za mwaka 2012/13.
Katika fedha zilizotengwa chini ya Wizara ya Ujenzi, TANROADS imetengewa Shilingi 314,535,652,200.00 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na Wizara ya Ujenzi imetengewa Shilingi 34,948,405,800.00 kwa ajili ya kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa
barabara pamoja na ukarabati na ununuzi wa vivuko, usalama barabarani na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hiyo. Bodi ya Mfuko wa Barabara imetengewa Shilingi 3,565,342,000.00. Kati ya fedha hizo Shilingi 934,245,067.00 ni kwa ajili ya mishahara, Shilingi 2,631,096,933.00 ni kwa ajili ya ukaguzi na ufuatiliaji wa miradi ya Barabara Kuu na za Mikoa katika mikoa yote pamoja na barabara za Halmashauri za Wilaya. Aidha, fedha hizo pia zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Bodi ya Mfuko wa Barabara
Dodoma na kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC) ya Bodi. 184. Mheshimiwa Spika, Fedha za Wizara
ya Ujenzi zitatumika kutekeleza miradi kama inavyoonyeshwa kwenye Kiambatisho Namba 3:-
114
(i) Miradi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara Kuu ambayo imetengewa Shilingi 9,126,610,000.00.
(ii) Miradi ya vivuko imetengewa Shilingi
3,163,730,000.00. Kati ya fedha hizo Shilingi 906,270,000.00 ni kwa ajili ya ununuzi wa Kivuko cha Itungi Port na Shilingi 787,950,000.00 ni kwa ajili ya ununuzi wa Kivuko cha Kahunda - Maisome. Ununuzi wa boti ya uokoaji (Rescue boat) kwa vivuko vya Ukerewe (Rugezi - Kisorya and Buolora-Ukara) umetengewa Shilingi 469,510,000.00. Shilingi 900,000,000.00 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa vipuri vya vivuko na Shilingi 100,000,000.00 ni kwa ajili ya ufuatiliaji wa miradi.
(iii) Shilingi 1,325,370,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa miradi ya barabara, maandalizi ya Kanuni za Sheria ya Barabara, maandalizi na uchapishaji wa taarifa za kaguzi za
miradi ya barabara, uendelezaji wa teknolojia za ujenzi wa barabara, utoaji elimu kwa umma na kushiriki katika shughuli za kikanda (SADC,
115
EAC, COMESA, Central Corridor, nk).
(iv) Usalama Barabarani na Mazingira umetengewa Shilingi 1,140,000,000.00.
(v) Barabara za Mikoa ambazo zimetengewa jumla ya Shilingi
20,192,695,800.00. Mchanganuo wa barabara hizo umeonyeshwa kwenye Kiambatisho Na. 4.
Mpango wa Matengenezo ya Barabara kwa Mwaka 2013/14
185. Mheshimiwa Spika, Mpango wa matengenezo ya Barabara Kuu na Barabara za Mikoa kwa mwaka 2013/14 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni jumla ya Shilingi 314,535,652,200.00 kama
ilivyoonyeshwa katika Kiambatisho Na. 5. Muhtasari wake ni kama ifuatavyo:
(a) Barabara Kuu: Kilomita 11,276.87 na madaraja 1,272 kwa Shilingi 101,315,714,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara.
(b) Barabara za Mikoa: Kilomita 24,489.09 na madaraja 1,305 kwa Shilingi
116
162,103,560,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara.
(c) Matengenezo ya Dharura na Tahadhari: Kiasi cha Shilingi milioni 6,871,541,200.00 zimetengwa kwa kazi hizi kutoka Mfuko wa Barabara.
(d) Mradi wa Majaribio wa Kufanya Matengezo ya Muda Mrefu (PMMR): Kilomita 273 kwa shillingi 2,324,837,000.00
(e) Matengenezo, Ukarabati na Ujenzi wa Mizani. Kiasi cha Shilingi 3,500,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi.
(f) Kazi/Shughuli Zinazohusiana na Matengenezo Zinazofanywa Kutokea Makao Makuu: Kiasi cha Shilingi 4,470,000,000.00 kutoka Mfuko wa Barabara zimetengwa kwa ajili ya kuweka alama za barabarani; na kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Barabara ikiwa ni pamoja na kuweka alama za kuonyesha mipaka ya hifadhi ya barabara. Aidha, fedha hizo pia
zitatumika kuandaa na kusimamia programu za matengenezo ya Barabara Kuu na za Mikoa; kukusanya na
117
kuweka takwimu za barabara na matumizi yake; kufanya kaguzi za hali na uimara wa madaraja; kufuatilia masuala ya usalama barabarani ikiwa
ni pamoja na kubaini maeneo hatarishi (Black Spots) na kuandaa hatua za kuchukua.
(g) Usimamizi wa Kazi na Utawala. Kiasi
cha Shilingi 24,150,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi.
(h) Gharama za Uendeshaji wa Mizani
(Operational Costs): Kiasi cha Shilingi 9,800,000,000.00 kimetengwa kwa kazi hizi.
186. Mheshimiwa Spika, mpango wa
matengenezo ya Barabara Kuu na za Mikoa kwa mwaka 2013/14 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara umeoneshwa katika Viambatisho Na. 5A hadi 5E kama ifuatavyo: (i) Kiambatisho 5(A - 1): Matengenezo ya
Kawaida (Routine Maintenance) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14 – Barabara Kuu: jumla ya shilingi milioni 24,291.040.
(ii) Kiambatisho 5(A - 2): Matengenezo
Kawaida (Routine Maintenance) kwa
118
kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14 – Babaraba za Mikoa: jumla ya shilingi milioni 33,527.835.
(iii) Kiambatisho 5(B - 1): Matengenezo Maalum (Periodic Maintenance) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14 – Barabara Kuu: jumla ya shilingi milioni 64,619.335.
(iv) Kiambatisho 5(B - 2): Matengenezo Maalum (Periodic Maintenance) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14 – Barabara za Mikoa: jumla ya shilingi milioni 90,002.156.
(v) Kiambatisho 5(C - 1): Matengenezo ya
sehemu Korofi (Sport Improvement) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14 – Barabara Kuu lami na Changarawe: jumla ya
shilingi milioni 1,348.720.
(vi) Kiambatisho 5(C - 2): Matengenezo ya sehemu Korofi (Sport Improvement) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara kwa mwaka 2013/14 –
Barabara za Mikoa lami na changarawe: jumla ya shilingi milioni 16,279.01.
119
(vii) Kiambatisho 5(D): Matengenezo ya Kukinga Madaraja (Bridges Preventive Maintenance) kwa Barabara Kuu na Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha
za Mfuko wa Barabara mwaka 2013/14: jumla ya shilingi milioni 3,157.162.
(viii) Kiambatisho 5(E): Matengenezo Makubwa ya Madaraja na Makalvati kwa Barabara Kuu na Barabara za Mikoa kwa kutumia fedha za Mfuko wa
Barabara mwaka 2013/14: jumla ya shilingi milioni 26,388.776.
Mpango Maalum wa Kitaifa wa Kuinua Matumizi ya Teknolojia ya Nguvu Kazi 187. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/201, Chuo cha Matumizi Stahiki ya Nguvu Kazi (Appropriate Technology Training Institute -ATTI) kitaendelea kutoa mafunzo ya ukarabati na matengenezo ya barabara za vijijini kwa wananchi wapatao 2,500 ili kuwa na miundombinu bora na inayopitika kirahisi.
Aidha, mafunzo yatatolewa kwa wahandisi 44 kutoka ndani na nje ya nchi; Makandarasi 100, Wahandisi washauri 10, na Viongozi wa Vikundi 200, ili waweze kutoa huduma bora katika ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara
120
kwa kutumia taaluma na ujuzi wa teknolojia ya nguvu kazi (LBT).
Ushirikishwaji wa Wanawake Katika Kazi za Barabara Nchini 188. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/2014, Wizara itaendelea kuhamasisha wanawake kushiriki katika kazi za barabara kwa kuendesha mafunzo ya ukandarasi kwa
makandarasi wanawake na vikundi vya wanawake 25 kwa kutumia teknolojia ya Nguvu Kazi. Wizara itafanya ufuatiliaji wa maendeleo ya wanawake waliopatiwa mafunzo ya ushiriki katika kazi za barabara. Aidha, Wizara itaendelea kuhamasisha wanawake wengi zaidi
kushiriki katika kazi za barabara kama makandarasi na wafanyakazi katika ngazi mbalimbali za kazi za barabara. Maendeleo ya Watumishi
189. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014, Wizara itaendelea kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma kwa kuwapeleka katika mafunzo ya ndani na nje ya nchi. Mafunzo hayo yatakuwa ni ya muda mrefu na muda mfupi. Aidha, Wizara itaendelea kuajiri
watumishi wapya kukidhi mahitaji yake, kuwathibitisha kazini watumishi wanaostahili Wizara itawapandisha vyeo watumishi wake kwa
121
kadiri ya Ikama itakayotolewa na kutimizwa kwa sifa na masharti ya kupata vyeo kwa mujibu wa kada husika.
Mikakati ya Kupambana na Ukimwi 190. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014 Wizara itaendelea kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI na VVU kwa watumishi pamoja na kuepuka kusambaza
ugonjwa huo kwa kutumia vipeperushi mbalimbali. Pia kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Wizara itaandaa semina na mafunzo kwa watumishi na wataendelea kuhamasishwa kupima afya zao pamoja na kuwapatia huduma ya lishe bora kwa
watakaothibitika kuathirika na ugonjwa huo. Vita Dhidi ya Rushwa 191. Mheshimiwa Spika, Wizara katika
mwaka wa fedha 2013/2014 itaendelea
kuwaelimisha watumishi athari za kutoa na kupokea rushwa pamoja na kuwahimiza kupambana na rushwa katika mazingira yote ya kazi. Elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa itatolewa kupitia vipeperushi, semina na mikutano mbalimbali kwa ushirikiano na
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).
122
Habari, Elimu na Mawasiliano 192. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Wizara itaendeleza mawasiliano na
wadau wote ili kuboresha utoaji wa elimu na taarifa kwa umma. Wizara itaendelea kutoa taarifa za shughuli zinazotekelezwa na Wizara kupitia vipindi vya televisheni, radio, Tovuti (www.mow.go.tz) pamoja na machapisho.
Nachukua fursa hii kuvipongeza vyombo mbalimbali vya habari, kwa ushirikiano wao na jinsi ambavyo vimekuwa vikifuatilia na kutoa taarifa za shughuli zinazohusu sekta ya Ujenzi. Ushirikiano huu utaendelea kudumishwa ili kuhakikisha kuwa umma unapata taarifa za
kutosha zinazohusiana na malengo, sera, sheria na kanuni mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi. MPANGO WA UTEKELEZAJI KAZI KATIKA WAKALA / TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA KWA MWAKA 2013/2014 Wakala wa Barabara 193. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14 Wakala utaendelea kusimamia kazi za
kukarabati, kujenga na kufanya matengenezo ya barabara kuu na barabara za mikoa zenye urefu wa kilometa 35,000.
123
Matengenezo ya barabara kuu na mikoa yatahusisha matengenezo ya kawaida (routine maintenance) kilomita 30,656, matengenezo ya muda maalum na korofi kilomita 5,109.90 na
madaraja 2,577. Mpango huu pia utajumuisha shughuli za utawala na usimamizi wa kazi, udhibiti wa uzito wa magari, kazi za dharura, mradi wa matengenezo ya muda mrefu na kazi zinazosimamiwa toka makao makuu kuhusu mipango, usalama barabarani na hifadhi ya
barabara.
194. Mheshimiwa Spika, Wakala pia utaendelea kusimamia miradi ya ujenzi wa barabara kilomita 495 kwa kiwango cha lami, ukarabati wa kilometa 190 kwa kiwango cha
lami pamoja na ujenzi na ukarabati wa madaraja 11 katika barabara kuu. Kwa upande wa barabara za mikoa, Wakala umepanga kukarabati kilomita 867.60 kwa kiwango cha changarawe, kujenga kilomita 66.1 kwa kiwango cha lami na kujenga/kukarabati madaraja 35.
Wakala umeandaa mpango wa mafunzo kwa watumishi 107. Kati ya watumishi hawa, 12 watahudhuria mafunzo ya muda mfupi nje ya nchi, 20 watahudhuria mafunzo ya muda mrefu (Shahada za Uzamili) na 75 watapatiwa mafunzo
ya muda mfupi katika vyuo mbalimbali ndani ya nchi.
124
Wakala wa Majengo ya Serikali 195. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Wakala umepanga kutekeleza
majukumu yake mbalimbali ikiwemo kukamilisha ujenzi wa miradi inayoendelea, kununua viwanja zaidi mikoani ili kuuwezesha Wakala kujenga nyumba nyingi zaidi za Watumishi Mikoani, kufanya matengenezo ya nyumba za Serikali na kununua samani kwa
nyumba za Viongozi wa umma. Wakala utaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ushauri wa kitaalam kwa miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi na ofisi za Serikali kwa kuzingatia mahitaji ya watu wenye
ulemavu. Wakala wa Ufundi na Umeme
196. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wakala umepanga kuendelea na ununuzi wa vivuko vya Kahunda – Maisome (Geita) na Itungi Port (Kyela – Mbeya); ununuzi wa boti ya uokoaji (rescue boat) na ununuzi wa kivuko cha Dar es Salaam – Bagamoyo;
ukarabati wa vivuko vya MV. Magogoni, MV. Geita, MV. Kome I na MV. Kilombero I; na ujenzi wa maegesho ya vivuko katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha, Wakala utaendelea kukarabati karakana za Dar es Salaam, Arusha,
125
Mwanza na Dodoma na kuzipatia vitendea kazi vya kisasa pamoja na kutengeneza magari ya Serikali katika karakana zote kila mkoa. Wakala pia utaendelea kutoa ushauri wa kihandisi kwa
miradi ya usimikaji wa mifumo ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na majokofu katika nyumba za Serikali pamoja na kukodisha mitambo mbalimbali na magari maalum ya viongozi.
Bodi ya Mfuko ya Barabara 197. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Bodi ya Mfuko wa Barabara itaendelea kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, TANROADS, EWURA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufuatilia na kuweka mikakati ya kuziba mianya ya uvujaji wa mapato kwenye vyanzo vya
mapato ya Mfuko. Aidha, Bodi itaandaa mapendekezo ya kuboresha vipengele katika sheria iliyoanzisha Bodi ili kuboresha ufanisi wa utendaji wa Taasisi za barabara (Road Authorities) na Watendaji wanaosimamia matumizi ya fedha za Mfuko. Bodi itakamilisha
uandaaji wa Taratibu za Sheria ya Mfuko wa Barabara (regulations) na miongozo mbalimbali ili kuboresha usimamizi wa Fedha za Mfuko. Bodi itaimarisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za Mfuko kwa kutumia wataalam
126
washauri na wataalam wa ndani katika kufanya ukaguzi wa kiufundi wa ubora wa kazi (value for Money) kwenye mikoa yote nchini. Bodi ya Usajili wa Wahandisi 198. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Bodi ya Usajili wa Wahandisi imepanga kusajili Wahandisi 800, Mafundi Sanifu 200 na kampuni za ushauri wa kihandisi
25. Aidha, Bodi itasimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo ya vitendo kwa wahandisi wahitimu 1,000. Idadi hii ni pamoja na wahandisi wahitimu 651 wanaoendelea na mafunzo kwa fedha za Serikali na watu binafsi.
Bodi pia itafanya ukaguzi wa shughuli za kihandisi nchini ili shughuli zote za kihandisi zifanywe na wahandisi waliosajiliwa na kwa kufuata maadili ya utendaji kazi za kihandisi. Bodi itatembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa barabara Tanzania Bara, ikiwa ni pamoja na
barabara za Halmashauri ili kutathmini hali ya uhandisi katika halmashauri zote Tanzania bara. Lengo ni kuhakiki kama kazi zote za kihandisi zinafanywa na wahandisi wenye sifa na waliosajiliwa na Bodi. Hii ni pamoja na kupata idadi kamili ya wahandisi walioko katika
shughuli za kihandisi nchini.
127
Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi 199. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi inatarajia kusajili Wabunifu Majengo (362), Wakadiriaji Majenzi (240), Mafundi Sanifu, Warasimu (Draughtmen), pamoja na kampuni za Wabunifu Majengo (200) na kampuni za Wakadiriaji Majenzi (101). Katika
kupanua wigo wa usajili, Bodi itasajili wataalum wenye fani zinazoshabihiana na Kampuni za ushauri (Interior Designers, Landscape Architects, Conservation Architects, Furniture Designers, Naval Architects, Building Surveyors, Building Economists, Project Managers and
Construction Managers). Aidha, Bodi itaendelea kuwawezesha wahitimu kupata mafunzo kwa vitendo, ili kuhakikisha wanapata maarifa na uzoefu unaokidhi haja ya Sekta ya ujenzi kulingana na sheria pamoja na kuwaelimisha watekelezaji wa miradi ya ujenzi katika Mikoa ya
Tanzania Bara kuhusu umuhimu wa kutumia wataalam waliosajiliwa katika miradi yao. Bodi ya Usajili wa Makandarasi 200. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/2014, Bodi ya Usajili wa Makandarasi imepanga kusajili jumla ya makandarasi 813 wa fani za Majengo, Majenzi (Civil works),
128
Umeme, Mitambo, Kazi maalum (Specialists) Makandarasi wa muda (Temporary Contractors na makandarasi wanaofanya kazi kwa ubia. Aidha, bodi itafanya tathmini (Review) ya vigezo
vinavyotumika kusajili makandarasi ili kuendelea kupata makandarasi walio bora zaidi.
Bodi pia itaendesha jumla ya kozi za mafunzo 6 katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na zaidi ya makandarasi 270 wanatarajiwa kuhudhuria
mafunzo haya. Mafunzo yatalenga maeneo ya utawala/udhibiti wa fedha, utawala wa biashara, usimamizi wa mitambo, Matumizi ya Teknohama katika ujenzi, upangaji na udhibiti wa kazi za ujenzi. Ili kuhakikisha kazi zote zinafanywa na makandarasi waliosajiliwa na
makandarasi wanafuata sheria na taratibu za usajili wao, Bodi imepanga kukagua miradi ya ujenzi 3,090 nchini. 201. Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana
na Wizara ya Ujenzi na wadau wengine, Bodi
itaendelea kusimamia mpango maalum wa kukuza uwezo wa makandarasi wazalendo ukiwemo ujenzi wa daraja la Mbutu kwa mfumo wa Kubuni na Kujenga (Design and Build). Mradi huu unatekelezwa kwa ubia na Makandarasi wa kizalendo 13 na Wahandisi
washauri wazalendo wanne kwa lengo la kukuza uwezo wa wazalendo.
129
Baraza la Taifa la Ujenzi 202. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/2014, Baraza la Taifa la Ujenzi limepanga
kukamilisha Kanuni za Utekelezaji wa Sheria iliyoanzisha Baraza (CAP 162 Revised Edition 2008), kufanya ukaguzi wa kiufundi wa miradi ya ujenzi. Aidha, itaratibu na kutoa mafunzo, ushauri wa kiufundi kuhusu utatuzi wa migogoro katika sekta pamoja na kuendelea na
utekelezaji wa miradi ya ujenzi kwa kutumia teknolojia ya nguvu kazi (Labour Based Technology). Bodi pia itaendelea na jitihada za kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Sekta ya Ujenzi (Construction Industry Development Fund (CIDF)), kuratibu mfumo wa kutoa taarifa
muhimu za miradi ya ujenzi ili kukuza uwazi na uwajibikaji (Construction Sector Transparency Initiative (CoST)); ikiwa ni njia mojawapo ya kupambana na rushwa katika sekta. Baraza vilevile, litaendelea kuratibu ukusanyaji, uwekaji na utoaji wa takwimu na taarifa za
Sekta ya Ujenzi na kuandaa majarida ya kiufundi kuhusu sekta ya ujenzi.
Katika mwaka 2013/2014, Bodi kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na mwekezaji binafsi itaendelea na ujenzi
wa jengo la ofisi la ghorofa 22 lililoko Barabara ya Samora, Dar es Salaam.
130
Vikosi vya Ujenzi 203. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/14, Vikosi vya Ujenzi vitaendelea na
ujenzi wa maegesho ya Kivuko cha Msanga Mkuu na maegesho ya Senga ya Kivuko cha Chato, ujenzi wa nyumba za viongozi na watumishi wa Serikali pamoja na kuendeleza viwanja 38 vinavyomilikiwa na Vikosi vya Ujenzi Mjini Dodoma.
Vikosi vitaendelea na maboresho ya kiutendaji kwa kufanya ukarabati wa karakana (Carpentry Workshops) zilizopo Dar es Salaam na Dodoma, ukarabati wa Ofisi zilizopo Dodoma na Arusha pamoja na kuongeza vitendea kazi ili kuongeza
ufanisi katika utekelezaji wa Miradi. Chuo cha Ujenzi – Morogoro 204. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/14, Chuo kimepanga kufundisha
jumla ya wanafunzi 800 katika fani za ufundi stadi wa kazi za barabara, majengo pamoja na udereva. Aidha, chuo kitaendeleza ujenzi wa jengo jipya la madarasa na karakana ya ufundi pamoja na kununua samani na zana ndogo ndogo za kufundishia.
131
Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia Katika Sekta ya Uchukuzi (Tanzania Transportation Technology Transfer Centre) 205. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2013/2014, Kituo kimepanga kuendelea na jukumu la kusambaza teknolojia katika sekta ya barabara na uchukuzi hapa nchini. Kituo kitaandaa warsha na mafunzo yanayolenga kutatua changamoto zinazoikabili
sekta ya barabara na uchukuzi, kusambaza kwa wadau 120,000 jumla ya makala na taarifa 150 zinazohusu teknolojia mbalimbali katika sekta ya barabara na uchukuzi kwa ujumla pamoja na kuendelea kutoa huduma ya Maktaba ya Kituo.
Kituo kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Morgan State University ya Marekani pamoja na wadau wengine kitaanza kutekeleza mradi unaolenga kuboresha mifumo ya ujenzi, matengenezo na usimamizi wa miundombinu ya barabara na uchukuzi hapa
nchini. SHUKURANI 206. Mheshimiwa Spika, napenda nitumie
fursa hii kuwashukuru kwa dhati Wabunge
wote na Kamati ya Bunge ya Miundombinu chini ya uenyekiti wa Mheshimiwa Peter Serukamba, Mbunge wa Kigoma Mjini kwa michango,
132
ushauri na ushirikiano waliotupa katika kuimarisha huduma zitolewazo na Wizara. Wizara inaahidi kufanyia kazi ushauri, na maamuzi ya Bunge lako Tukufu wakati wa
kujadili bajeti hii na katika fursa nyingine. 207. Mheshimiwa Spika, shukurani zetu
ziwaendee Washirika wetu wa Maendeleo waliochangia katika kutekeleza programu na mipango yetu ya sekta. Nchi na Mashirika ya
Kimataifa yaliyochangia kuboresha utoaji huduma na miundombinu ya sekta yetu ni pamoja na Abu Dhabi, Denmark (DANIDA), Japan (JICA), Korea, Marekani (MCC), Uingereza (DFID), Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), Benki ya Dunia (WB), Benki ya Kiarabu ya
Maendeleo ya Afrika (BADEA), Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya Nchi za Ulaya, Kuwait Fund na OPEC Fund. 208. Mheshimiwa Spika, ninawashukuru
kwa dhati viongozi wenzangu katika Wizara kwa
ushirikiano walionipatia katika kipindi chote cha uongozi wa Wizara ya Ujenzi. Viongozi hao ni Mhe. Eng. Gerson H. Lwenge (Mb.), Naibu Waziri; Balozi Herbert E. Mrango, Katibu Mkuu; Eng. Dkt. John S. Ndunguru, Naibu Katibu Mkuu. Wengine ni Wenyeviti na Watendaji Wakuu wa Bodi za Mfuko wa Barabara, Usajili wa Makandarasi, Usajili wa Wahandisi, Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi,
133
Baraza la Taifa la Ujenzi, TANROADS, TEMESA na TBA. Ninawashukuru Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo pamoja na wafanyakazi wote wa Wizara ya Ujenzi na Taasisi zake kwa
ushirikiano wao mkubwa. Nawashukuru sana. 209. Mheshimiwa Spika, napenda pia
niwashukuru kwa dhati wapiga kura wangu wa Jimbo la Chato kwa ushirikiano wao mkubwa wanaonipa katika kuleta maendeleo ya Jimbo
letu pamoja na uvumilivu walionao kwangu wakati nikitekeleza majukumu ya kitaifa. Nawashukuru sana. HITIMISHO Makadirio ya Matumizi ya Kawaida 2013/2014 210. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2013/14, Wizara ya Ujenzi inaomba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi
381,205,760,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo kati ya fedha hizo Shilingi 21,211,514,000.00 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake, Shilingi 353,049,400,000.00 ni fedha za Mfuko wa Barabara na Shilingi 6,944,846,000.00 ni kwa
ajili ya matumizi mengineyo ya Wizara na Taasisi.
134
Bajeti ya Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka 2013/14
211. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara ya Ujenzi inaomba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi
845,225,979,000.00 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 448,174,599,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 397,051,380,000.00 ni fedha za nje.
135
MUHTASARI WA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI KWA MWAKA 2013/2014
A. Matumizi ya Kawaida
MAELEZO KIASI (SHILINGI)
Mishahara 21,211,514,000.00
Mfuko wa Barabara 353,049,400,000.00
Matumizi Mengineyo 6,944,846,000.00
Jumla Fedha za Matumizi ya Kawaida
381,205,760,000.00
B. Fedha za Maendeleo
Fedha za Ndani za Miradi ya Maendeleo
448,174,599,000.00
Fedha za Nje za Miradi ya Maendeleo
397,051,380,000.00
Jumla Fedha za Maendeleo
845,225,979,000.00
JUMLA YA FEDHA ZA MATUMIZI YA KAWAIDA NA MAENDELEO
1,226,431,739,000.00
212. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa
hoja.
137
KIAMBATISHO NA.1
MGAWANYO WA FEDHA ZA BAJETI YA MAENDELEO KWA MWAKA 2013/2014
KASMA JINA LA MRADI UREFU (Km/No)
MAKADIRIO 2013/14 (TSh millions) Chanzo
cha Fedha Fedha za Ndani
Fedha za Nje Jumla
SUB VOTE 1003: POLICY AND PLANNING DIVISION
6267 Institutional Support 200.131 300.000 500.131 GOT/EU
TOTAL 1003 200.131 300.000 500.131
SUBVOTE 2002: TECHNICAL SERVICES DIVISION
4125 Construction of Ferry Ramps
5,990.00 5,990.00 GOT
4139 Procurement of Ferries 4,484.00 4,484.00 GOT
4144 Rehabilitation of Ferries 2,102.21 2,102.21 GOT
6327 Construction of Government Houses
2,245.49 2,245.49 GOT
TOTAL 2002 14,821.700 - 14,821.700
SUB VOTE 2005: ROADS DEVELOPMENT DIVISION
4108 Dar es Salaam - Chalinze - Morogoro Express Way (Dsm- Chalinze Section),
200.00 100.00 - 100.00 GOT/ PPP
138
4109 Wazo Hill - Bagamoyo - Msata
64.00 10,441.10 - 10,441.10 GOT
Bagamoyo - (Makurunge) - Sadani - Tanga and Lower Wami Bridge (DD)
178.00 444.14 - 444.14 GOT/ ADB
Sub total 242.00 10,885.24 - 10,885.24
4110 Usagara - Geita -Buzirayombo - Kyamyorwa (422km)
- -
(i) Kyamyorwa - Buzirayombo
120.00 800.00 - 800.00 GOT
(ii) Buzirayombo - Geita 100.00 - - - GOT
(iii) Geita - Usagara (Lot 1 & Lot 2)
90.00 2,000.00 - 2,000.00 GOT
(iv) Uyovu -Biharamulo 112.00 8,000.00 - 8,000.00 GOT
Sub total 422.00 10,800.00 - 10,800.00
4112 Kigoma - Kidahwe - Uvinza - Kaliua - Tabora
- -
(i) Malagarasi Bridge and Associated approach roads
48.00 3,139.53 10,130.00 13,269.53 S.KOREA/
GOT
(ii) Kigoma - Kidahwe section
36.00 - - - GOT
139
(iii) Kidahwe-Uvinza 76.60 2,131.95 10,693.00 12,824.95 ABU
DHABI/ GOT
(iv) Uvinza - Malagarasi 51.10 2,000.00 2,000.00 ABU
DHABI/ GOT
(v) Tabora - Ndono 42.00 6,837.80 - 6,837.80 GOT
(vi) Ndono - Urambo 52.00 7,189.04 - 7,189.04 GOT
(vii)Urambo - Kaliua - Ilunde -Uvinza, (206.40km) (Kaliua -Kazilambwa Sect)
56.00 4,848.02 - 4,848.02 GOT
(viii) Tabora - Sikonge 70.00 4,700.00 - 4,700.00 GOT Sub total 431.70 30,846.34 20,823.00 51,669.34
4115
Marangu-Tarakea - Rongai - Kamwanga/Bomang'ombe - Sanya Juu
- -
(i) Marangu - Rombo Mkuu incl. Mwika - Kilacha
32.00 2,145.92 - 2,145.92 GOT
(ii) Rombo Mkuu - Tarakea 32.00 487.71 - 487.71 GOT
(iii) Sanya Juu - Kamwanga (Design +Constr)
75.00 5,000.00 - 5,000.00 GOT
(iv) Arusha - Moshi - Himo - Holili & Arusha Bypass incl Himo Weighbridge compensation
140.00 1,000.00 - 1,000.00 GOT / ADB
140
(v) Same - Himo - Marangu & Mombo - Lushoto (FS & DD)
132.00 - - - GOT/WB
(vi) KIA - Mererani 26.00 2,500.00 - 2,500.00 GOT
Sub total 437.00 11,133.63 - 11,133.63
4117 Nangurukuru - Mbwemkulu
95.00 2,000.00
- 2,000.00 GOT
4118 Dodoma - Manyoni (Incl. Manyoni Access Road)
126 1,309.28 - 1,309.28 GOT
4120 Mbwemkulu - Mingoyo 95.00 1,000.00 - 1,000.00 GOT
4121 Singida - Manyoni 54.00 1,200.00 - 1,200.00 GOT
4122 Port Access (Nelson Mandela) Road
15.6 1,500.00 - 1,500.00 GOT/EU
4123 Dumila - Kilosa - Mikumi, km 142) ( Dumila - Rudewa Sect)
45.00 6,000.00 - 6,000.00 GOT
4124 Sumbawanga -Matai - Kasanga Port
112.00 11,241.37 - 11,241.37 GOT
4126 Construction of Bridges - - GOT
(i) Rehabilitation of Kirumi Bridge
1No 1,500.00 - 1,500.00 GOT
(ii) Construction of Nanganga Bridge / Nangoo along Mingoyo - Masasi
2No 500.00 - 500.00 GOT
141
(iii) Construction of Sibiti Bridge along Ulemo - Gumanga - Sibiti road
1No 3,000.00 - 3,000.00 GOT
(iv) Construction of Maligisu Bridge in Mwanza region
1No 200.00 - 200.00 GOT
(v) Construction of Kilombero Bridge Morogoro
1No 7,500.00 - 7,500.00 GOT
(vi) Kavuu Bridge along Majimoto-Inyonga
1No 1,000.00 - 1,000.00 GOT
(vii) Construction of Mbutu Bridge along Igunga-Manonga and Approach Roads
1No 5,300.00 - 5,300.00 GOT
(viii) Purchase of Mabey Bailey Compact Emergency Bridge and Crane Lorry
2No 50.00 - 50.00 GOT
(ix) Ruhekei Bridge along Mbinga-Mbambabay
1No 250.00 - 250.00 GOT
(x) Ruhuhu Bridge cum Dam
1No. 200.00 - 200.00 GOT
(xi) Momba Bridge along Sitalike-Kilyamatundu/ Kamsamba - Mlowo (Rukwa/Mbeya Border)
2,000.00 2,000.00
Sub total 12No 21,500.00 - 21,500.00
142
4127 New Bagamoyo (Kawawa Jct - Tegeta)
17.00 2,500.00 18,000.00 20,500.00 GOT/ JAPAN
4128 Kyaka - Bugene – Kasulo (Constr. & DD)
180.00 7,037.53 - 7,037.53 GOT
4129 Isaka - Lusahunga (Rehabilitaion)
- -
(i) Isaka - Ushirombo (Rehabilitation)
132.00 12,512.72 - 12,512.72 GOT
(ii) Ushirombo- Lusahunga (Rehabilitation)
100.00 9,007.76 - 9,007.76 GOT
(iii) Lusahunga - Rusumo & Nyakasanza - Kobero (FS & DD)
150.00 - - - GOT
Sub total 392.00 21,520.48 - 21,520.48
4130 Manyoni - Itigi - Tabora Road
(i) Tabora - Nyahua Sect. 85.00 10,000.00 - 10,000.00 GOT
(ii) Nyahua - Chaya 90.00 2,200.00 - 2,200.00 GoT
(iii) Manyoni- Itigi - Chaya Sect.
89.35 10,299.57 - 10,299.57 GOT
Sub total 264.35 22,499.57 - 22,499.57 4131 Korogwe - Handeni 65.00 6,356.73 - 6,356.73 GOT
4132 Regional Roads Rehabilitation & upgrading (25 regions)
551.1 31,915.27 - 31,915.27 GOT
143
4133 Mwanza – Shinyanga/ Mwanza Border road Rehabilitation
10.00 50.00 - 50.00 GOT
4134 Handeni - Mkata Road 54.00 4,484.75 - 4,484.75 GOT
4135 Mwandiga - Manyovu (Construction)
60.00 1,234.35 - 1,234.35 GOT
4137 Unity Bridge 1No - - - GOT/MZQ
4138 De-congestion of DSM Roads
- -
(i) Kawawa R/about – Msimbazi – Twiga (Jangwani)
2.70 605.00 - 605.00 GOT
(ii) Ubungo Terminal – Kigogo R/About
6.40 1,689.00 - 1,689.00 GOT
(iii) Jet corner- Vituka-Devis corner
10.30 1,290.00 - 1,290.00 GOT
(iv) Ubungo Maziwa - External & Tabata dampo - Kigogo
2.25 3,000.00 - 3,000.00 GOT
(v) Kimara - Kilungule - External
9.00 5,000.00 - 5,000.00 GOT
(vi) Mbezi - Malambamawili - Kinyerezi - Banana
14.00 6,000.00 - 6,000.00 GOT
(vii)Tegeta - kibaoni - Wazo - Hill - Goba - Mbezi (Moro Rd)
20.00 5,000.00 - 5,000.00 GOT
144
(viii)Tangi Bovu - Goba 9.00 3,000.00 - 3,000.00 GOT
(ix) Kimara Baruti - Msewe - Changanyikeni
2.60 1,500.00 - 1,500.00 GOT
(ix) Bus Rapid Transit Infrastructure (BRT)
21.90 50.00 - 50.00 GOT
(x) Kibamba-Kisopwa (Kibamba-Mlonganzila Section)
4.00 1,500.0 1,500.00 GOT
Sub total 102.15 28,634.00 - 28,634.00
4143 Ndundu - Somanga 60.00 5,287.74 - 5,287.74 GOT/ OPEC
4147
Kidatu - Ifakara - Lupilo - Malinyi - Londo - Lumecha/Songea (FS & DD)
396.00 100.00 1,500.00 1,600.00 GOT/ ADB
4148 Tabora - Ipole - Koga - Mpanda road (Ipole - Koga - Mpanda section)
359.00 2,000.00 - 2,000.00 GOT
4149 Makutano - Natta - Mugumu/ Loliondo - Mto wa Mbu (328km)
- - GOT
(i) Makutano-Natta - Mugumu, (125km) (Makutano -Sanzate Sect)
50 5,617.63 - 5,617.63 GOT
(ii) Mto wa Mbu – Loliondo section
213 3,000.00 - 3,000.00 GOT
Sub total 263 8,617.63 - 8,617.63 Sub total
145
4150 Ibanda - Itungi Port 26.00 1,000.00 - 1,000.00 GOT
4151
Tanga - Horohoro Road (Construction)
65.00 - - - GOT/MCC
4152 Nzega - Tabora
- - GOT
Nzega - Puge 58.60 6,696.05 - 6,696.05 GOT
Puge - Tabora 56.40 6,696.05 - 6,696.05 GOT
Sub total 115 13,392.09 - 13,392.09
4154 Sumbawanga - Mpanda - Nyakanazi Road (DD & Construction)
- -
(i) Sumbawanga-Kanazi 75.00 8,850.94 - 8,850.94 GOT (ii) Kanazi – Kizi - Kibaoni 76.60 8,850.94 - 8,850.94 GOT
(iii) Kizi - Sitalike- Mpanda section
95.00 6,617.63 - 6,617.63 GOT
(iv) Mpanda - Mishamo section
100.00 4,539.21 - 4,539.21 GOT
Sub total 346.60 28,858.72 - 28,858.72
4155 Nyanguge - Musoma & Usagara - Kisesa Bypass
- -
(i) Nyanguge -Mwanza/ Mara Boarder
85.50 2,500.00 - 2,500.00 GOT
146
(ii) Simiyu/ Mara Border - Musoma
80.00 7,235.26 - 7,235.26 GOT
(iii) Makutano - Sirari 83.00 - - GOT
(iv) Kisesa - Usagara Bypass
17.00 4,000.00 - 4,000.00 GOT
(v)Nansio - Kisesa - Bunda (Kisorya - Bunda)
50.00 4,500.00 4,500.00 GOT
Sub total 315.50 18,235.26 - 18,235.26
4160 Magole - Mziha - Handeni Road
- -
(i) Magole - Turiani 48.80 6,156.84 - 6,156.84 GOT
(ii) Turiani- Mziha 40.00 50.00 - 50.00 GOT (iii) Mziha - Handeni 68.00 60.00 - 60.00 GOT
Sub total 156.80 6,266.84 - 6,266.84
4161 DSM Road Flyovers and Approaches
- -
(i) TAZARA 1No. 1,000.00 - 1,000.00 GOT/JICA
(ii) Improvement of Junctions/Intersections at Chang'ombe, Ubungo, Magomeni/Nyerere, Mwenge,Tabata/Mandela and Morocco in Dar es Salaam (Design & Build)
4No. 3,000.00 - 3,000.00 GOT
Sub total 5No 4,000.00 - 4,000.00
147
4162 Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Lamadi
- -
(i) Bariadi - Lamadi 71.80 6,465.65 - 6,465.65 GOT
(ii) Mwigumbi - Maswa - Bariadi
100.00 5,500.00 - 5,500.00 GOT
Sub total 171.8 11,965.65 - 11,965.65
4163 Tabora - Ipole - Rungwa (Ipole - Rungwa section FS & DD)
95.00 500.00 - 500.00 GOT
4164 Kidahwe - Kasulu - Nyakanazi
310.00 10,000.00 - 10,000.00 GOT
4165 Mafia Airport Access Road (Construction)
14.00 2,471.17 - 2,471.17 GOT
4166 Dodoma University Road 12.00 3,000.00 - 3,000.00 GOT
4167 Kigamboni Bridge Construction
1No. 3,000.00 - 3,000.00 GOT / NSSF
4168 Special Road Construction Projects
- - - GOT
4171 Sam Nujoma Road Upgrading
4.00 21.51 - 21.51 GOT
148
4180 Tunduma - Sumbawanga Upgrading (Constr)
- - GOT/IDA/M
CC
(i) Tunduma - Ikana 63.70 17.00 - 17.00 MCC/GOT
(ii) Ikana - Laela 64.20 17.00 - 17.00 MCC/GOT
(iii) Laela - Sumbawanga 95.31 23.88 - 23.88 MCC/GOT
Sub total 223.21 57.88 - 57.88
4181 Kagoma - Lusahunga (Construction)
154.00 14,477.25 - 14,477.25 GOT
4182 (Arusha - Namanga) Rehab.
105.00 1,228.12 2,289.00 3,517.12 GOT/ADB/
JBIC
4183 Singida - Babati - Minjingu (Construction)
- -
(i) Singida - Katesh 65.10 240.56 - 240.56 GOT/ADB
(ii) Katesh - Dareda 73.80 336.00 - 336.00 GOT/ADB
(iii) Dareda - Babati -Minjingu
84.60 375.00 - 375.00 GOT/ADB
(iv) Minjingu - Arusha 98.00 444.83 25,000.00 25,444.83 GOT/ WB
Sub total 321.50 1,396.39 25,000.00 26,396.39
4185 D'Salaam - Mbagala Road Upgrading (Kilwa Road) Lot 3 (1.5km)
1.50 - - - GOT/JICA
Widening of Gerezani Road
1.30 1,000.00 - 1,000.00 GOT / JICA
Sub total 2.80 1,000.00 - 1,000.00
149
4186
Msimba - Ruaha Mbuyuni / Ikokoto - Mafinga (TANZAM) (Rehab.)
- -
(i) Iringa - Mafinga 69.40 5,516.53 - 5,516.53 GOT/
DANIDA (ii) Mafinga - Igawa 146.00 200.00 20,000.00 20,200.00 GOT/WB
(iii) Rujewa - Madibira-Mafinga
152.00 - - GOT
Sub total
367.40 5,716.53 20,000.00 25,716.53
4187 Same - Mkumbara - Korogwe (Rehabilitation)
- -
(i) Korogwe - Mkumbara 76.00 100.00 32,671.38 32,771.38 GOT/WB (ii) Mkumbara - Same 96.00 100.00 20,750.00 20,850.00 GOT/WB
Sub total 172.00 200.00 53,421.38 53,621.38
4188 Mbeya - Makongolosi (Construction)
- -
(i) Mbeya - Lwanjilo 36.00 6,528.78 - 6,528.78 GOT
( ii) Lwanjilo - Chunya Sect.
36.00 5,008.00 - 5,008.00 GOT
(iii) Chunya - Makongolosi section
43.00 3,847.05 - 3,847.05 GOT
(iv) Makongolosi - Rungwa - Itigi - Mkiwa
413.00 307.84 - 307.84 GOT
Sub total 528.00 15,691.68 - 15,691.68
150
4189 Chalinze - Segera - Tanga ( Kitumbi - Segera- Tanga Section)
248.00 3,200.00 4,500.00 7,700.00 GOT/
DANIDA
4192 New Ruvu Bridge 1No. - - - GOT
4195 Dodoma - Iringa - -
(i) Iringa - Migori 95.10 615.68 30,000.00 30,615.68 GOT/ADB
(ii) Migori - Fufu Escarpment
93.80 538.72 28,000.00 28,538.72 GOT/ADB
(iii) Fufu Escarpment - Dodoma
70.90 584.90 26,800.00 27,384.90 GOT/ADB
Sub total 259.80 1,739.31 84,800.00 86,539.31
4196 Dodoma - Babati - -
(i) Dodoma - Mayamaya 43.65 6,606.15 - 6,606.15 GOT (ii) Mayamaya - Mela 99.35 500.00 25,000.00 25,500.00 GOT/ADB
(iii) Mela - Bonga 88.8 500.00 22,000.00 22,500.00 GOT/ADB
(iv) Bonga - Babati incl. Kondoa Access road
19.2 2,386.26 - 2,386.26 GOT
Sub total 251 9,992.41 47,000.00 56,992.41
4197 Masasi - Songea - MbambaBay
- -
(i) Masasi - Mangaka 54.00 - - - GOT/J
ICA
(ii) Mangaka - Nakapanya 70.50 533.88 24,000.00 24,533.88 GOT/ADB/J
BIC
151
(iii) Nakapanya - Tunduru 66.50 532.57 23,200.00 23,732.57 GOT/ ADB/ JBIC
(iv) Mangaka - Mtambaswala
65.50 532.93 24,000.00 24,532.93 GOT/ ADB
(v)Tunduru - Matemanga 59.00 3,567.32 16,809.00 20,376.32 ADB/ GOT
(vi) Matemenga - Kilimasera
68.20 3,679.20 14,944.00 18,623.20 ADB/ GOT
(vii) Kilimasera - Namtumbo
60.00 3,679.19 13,715.00 17,394.19 ADB/GOT
(viii) Namtumbo - Songea 72.00 17.00 - 17.00 MCC/GOT
(ix) Peramiho - Mbinga 78.00 17.00 - 17.00 MCC/ GOT
(x) Mbinga - Mbambabay 66.00 4,600.00
- 4,600.00 GOT
(xi) Makambako - Songea 295.00 - - - GOT/WB
(xii) Mtwara - Mingoyo - Masasi
200.00 - - GOT/WB
(xiii) Masasi - Newala - Mtwara
2,500.00 2,500.00
Sub total 1,154.70 19,659.08 116,668.00 136,327.08
152
6383 Construction of TANROADS HQ (Design & Construction)
- -
(i) Construction of TANROADS HQ (Design & Construction)
1No 500.00 - 500.00 GOT
(ii) Construction of Dar es Salaam Regional Managers' Office
1No 100.00 - 100.00 GOT
(iii) Construction of Katavi Regional Managers' Office
1No 100.00 - 100.00 GOT
(iv) Construction of Geita Regional Managers' Office
1No 100.00 - 100.00 GOT
(v) Construction of Simiyu Regional Managers' Office
1No 100.00 - 100.00 GOT
(vi) Construction of Njombe Regional Managers' Office
1No 100.00
- 100.00 GOT
(vii) Construction of Lindi Regional Managers' Office
1No 100.00 - 100.00 GOT
Sub -total 7No 1,100.00 - 1,100.00
4198 Access Road - Uongozi Institute
8.8 1,500.00 - 1,500.00 GOT
TOTAL 2005 431,423.787 394,001.380 825,425.167
153
SUBVOTE 5002: SAFETY AND ENVIRONMENT DIVISION
4136 Road Safety Activities 887.00 2,500.00 3,387.00 GOT/WB
6221 Institutional Support to Safety and Environment
641.98 250.00 891.98 GOT/
DANIDA
6571 EMA Implementation Support Programme
200.00 - 200.00 GOT
TOTAL 5002 1,728.981 2,750.00 4,478.981
GRAND TOTAL 448,174.599 397,051.380 845,225.979
154
KIAMBATISHO NA.2
MIRADI YA MAENDELEO YA BARABARA ZA MIKOA (KASMA 4132) KWA MWAKA 2013/14
PROJECT NAME
TARGET (in km / No of
Bridges)
APPROVED BUDGET
2012/13 in Tsh mio
Estimated Budget 2013/14
Local Local
REGIONAL ROADS
1
ARUSHA REGION
Upgrading of Mbauda - Losinyai to DSD 27.69km 0.4 150.00 180.00
Rehab.Olokii (T/Packers) - Losinyai road km 22.68 2.0 35.00 65.00
Rehab.Mto wa Mbu - Loliondo road 212.36km 2.0 35.00 70.00
Rehab. Karatu Jnct. - Mangola - Matala ( 150km) 2.0 35.00 70.00
Upgrading to DSD Usa river - Momela - Arusha National Park
0.3 110.00 180.00
Rehab. Noondoto Jnct- Kitumbeine Road (80.6km) 2.0 35.00 70.00
Rehab. Karatu - Arusha/ Manyara boarder towards Mbulu (Karatu - Kilimapunda) 50.77km
2.0 40.00 65.00
FS & DD Kijenge - USA (Nelson Mandela University - 9km)
9.0 40.00 70.00
Sub- total Arusha 19.70 480.00 770.00
155
2
COAST REGION
FS & DD Kisarawe - Maneromango road (54km) 54.0 70.00 84.00
Rehab. Mbuyuni - Saadan road ( 9.5km) 2.5 40.00 50.00
Rehab Kilindoni - Rasmkumbi road - 62km 2.5 40.00 50.00
Rehab. Mkuranga - Kisiju road (45.77km) 2.5 40.00 50.00
Upgrading of TAMCO - Vikawe - Mapinga road
(24km)
0.2 70.00 85.00
FS & DD Makofia - Mlandizi - Maneromango
100km
100.0 40.00 60.00
Rehab.Mbwewe - Lugira road 2.5 40.00 50.00
Upgrading off Msoga - Msolwa road (Otta Seal) 0.4 100.00 123.00
Rehab.Kibiti - Utete road ( 44.73km) 2.5 40.00 50.00
Upgrading to DSD Kwa Mathias - Nyumbu -
Msangani road (9.5km)
3.0 - 1,200.00
Sub- total Coast 170.10 480.00 1,802.00
156
3
DAR ES SALAAM REGION
Upgrading Chanika - Mbande road (Otta seal) 29.6km
0.8 220 300.00
Rehab.Kimbiji - Tundwi Songani road (13km) 2.5 40 50.00
Rehab.Ukonga Mombasa - Msongola road 11 190 235.00
Rehab. Uhuru Road 0.2 70 87.00
Rehab. Shekilango road 0.1 60 75.00
Rehab. Sam Nujoma road 0.1 60 75.00
Rehab. United Nations road 0.2 70 86.00
Upgrading to DSD Mbagala Mission - Kijichi - Zakhem road (6.7km)
2 0 904.00
Sub- total Dar es Salaam 16.90 710.00 1,812.00
4 DODOMA REGION
Rehab. Kolo- Dalai (Mrojochini - Goima section) (118.07km)
2.0 35.00 60.00
Rehab. Mbande - Kongwa - Suguta (Ugogoni - Suguta section) (49.64km)
2.0 35.00 60.00
Rehab. Pandambili - Mlali - Ng'ambi (Mpwapwa - Suguta section) (100.31km)
2.0 35.00 60.00
157
Rehab. Zemahero - Kinyamshindo (Kwamtoro - Kinyamshindo section) - 125.06km
2.0 35.00 60.00
Upgrading to DSD Shabibu- Dodoma/Arusha round about - 6km
0.8 290.00 400.00
Rehab. Mnenia - Itololo - Madege (85km) 2.5 - 69.00
Rehab. Manchali Kongwa - Hogoro Jctn (Kongwa - Hogoro Jctn) - 45.75km
2.0 30.00 60.00
Sub - Total Dodoma 13.30 460.00 769.00
5 GEITA REGION
Rehab. Busisi - Nyang'wale-53.51km 11.0 200.00 210.00
Rehab. Nyang'hwale - Nyanholongo road-56.43km
2.5 40.00 50.00
Rehab. Geita - Nzera -NKome road - 54km 8.0 160.00 160.00
FS & DD : Geita - Bukoli - Kahama(Busoka) Road 139km
139.0 220.00 220.00
Rehab. Ushirombo - Nyikonga - Katoro/ Buseresere road
11.0 220.00 220.00
Upgrading to DSD Geita - Bukombe road 0.5 150.00 200.00
Rehab. Bukombe - Nyikonga road (32km) 3.5 60.000 80.00
158
Upgrading of Chato Port- Chato Ginery to DSD 0.2 50.000 150.00
Rehab. Buseresere - Kibumba - Makurugusi
road(8km)
2.5 40.00 50.00
Rehab. Butengolumasa – Iparamasa –
Masumbwe road
2.5 40.00 50.00
DSD Upgrading.Geita Township roads 1.0 500.00
Construction of Mkolani Bridge along Geita -
Nyang'hwale
1No - 110.00
Sub - Total - Geita 181.70 1,180.00 2,000.00
6 IRINGA REGION
Rehab. Paved section Iringa - Msembe (Ruaha
National Park) (104.6km)
6.5 110.00 135.00
Rehab. Paved section Iringa - Pawaga (64.0km) 0.3 110.00 135.00
DSD Iringa -Msembe (Kalenga Jnct-Ipamba
Hospital)
1 300.00
Rehab. Igowole - Kasanga - Nyigo (54.8km) 1.8 30.00 40.00
159
Rehab. Izazi - Mbolimboli - Pawaga - Mlowa road 83km
7.5 30.00 150.00
FS & DD Izazi - Mbolimboli - Pawaga - Mlowa road 83km
83.0 112.00
Rehab. Iringa - Idete rd (68kms) 4.0 70.00 86.00
Rehab. Mbalamaziwa - Kwatwanga (50km) 5.0 90.00 122.00
Sub - Total - Iringa 109.10 440.00 1,080.00
7 NJOMBE REGION
Rehab. Ndulamo - Nkenja - Kitulo - Mfumbi 95km 2.5 30.00 50.00
Upgrading of Njombe - Ndulamo - Makete (109.4km) to DSD
3.0 1,610.00 1,610.00
Opening up Lupembe - Madeke - Taweta road(53km) along Kibena - Lupembe rd
4.0 30.00 50.00
Rehab. Mkiu - Madaba (79.8km) 2.0 30.00 50.00
Upgrading to DSD Njombe township roads(CCM and Kongo Streets - 4km)
0.3 110.00 250.00
Rehab. Mlevela-Mhaji -Ibumila (15km) 2.5 40.00 50.00
Sub - Total - Njombe 14.30 1,850.00 2,060.00
160
8 KAGERA REGION
Rehab. Muhutwe - Kamachumu - Muleba rd (6km)
3.5 40.00 70.00
Rehab. Katoma - Kanyigo to gravel standard(6km)
3.5 40.00 80.00
Otta Seal. Bugene - Kaisho - Murongo road (Rwabunuka Escarpment) Sect.) (109km)
0.8 110.00 170.00
Rehab. Bukoba - Kabango bay ( 42 km) 5.0 75.00 110.00
FD & DD Murugarama - Rulenge - Nyakahura 86km
86.0 140.00 180.00
Rehab. Kashalunga - Ngote - Kasindaga (37km) 6.0 126.00
Rehab. Kyakailabwa - Nyakato (54km) 5.0 100.00
Sub - Total - Kagera 109.80 405.00 836.00
9
KATAVI REGION
Rehab. Kagwira - Karema (112km) 2.5 40.0 60.00
Rehab. Mamba - Kasansa(18km) Mamba - Kibaoni section
2.5 40.0 60.00
Rehab. Mwese - Kibo road(60Km) 3.0 50.0 70.00
Rehab. Mpanda (Kawajense) - Ugalla road(74Km)
18.0 290.0 360.00
Ugalla Bridge (Construction) 1No 150.0 286.00
161
Rehab Majimoto-Inyonga 12.0 150.0 240.00
Rehab of Kibaoni-Mamba 3.0 50.0 70.00
Sub - Total - Katavi 41.00 770.00 1,146.00
10 KIGOMA REGION
Rehab. Simbo - Ilagala - Kalya (Upgrading to gravel std from Rugufu bridge)
9.0 150.00 200.00
Upgrading of Katonga - Ujiji road to DSD 0.6 180.00 250.00
Upgrading of Gungu - Kibirizi to DSD 0.6 180.00 226.00
Rehab.Mugunzu - Bukililo - Kinonko 56km 4.0 84.40
Sub - Total - Kigoma
14.20 510.00 760.40
11 KILIMANJARO REGION
Upgrading to Otta Seals Mwanga - Kikweni road (22.5km)
1.0 110.00 135.00
Rehab. Holili - Tarakea ( 55 km) 2.0 30.00 41.00
Rehab. Kibosho Shine - Mto Sere 2.0 30.00 41.00
Rehab.Sanya juu - Rongai – 80 km 2.0 30.00 40.00
Upgrading to DSD of Kawawa - Pakula - Nduoni, Nduoni - Marangu Mtoni road (15km)
0.5 220.00 270.00
162
Upgrading to DSSD of Kibosho Shine- Kwa Raphael - International School road (12km)
0.4 180.00 222.00
Upgrading to DSSD Kwasadala - Masama 12.5km
0.3 150.00 185.00
Upgrading to DSD of Uru Njari - Rau Madukani (9.5km)
0.5 90.00 110.00
Construction to DSD of Same - Kisiwani - Mkomazi road(96.7Km).
1.0 220.00 500.00
Sub - Total - Kilimanjaro 9.70 1,060.00 1,544.00
12 LINDI REGION
Rehab. Ngongo - Mandawa - Ruangwa Road ( 45Km) (Ngongo - Mlola Sect)
10.00 40.00 250.00
Rehab. Lukuledi II Bridge along Mtama - Nyangamala road
1No. 140.00 157.00
Rehab. Nangurukuru - Liwale road 2.5 40.00 50.00
Rehab. Tingi - Kipatimu(50Km) 2.5 40.00 50.00
Rehab. Nanganga - Mandawa(60Km) 2.0 30.00 40.00
Rehab. Nachingwea - Liwale(30Km) 2.5 40.00 50.00
163
Rehab. Mtupwa VillageAaccess Road 2.5 40.00 50.00
Rehab. Nachingwea - Kilimarondo(60Km) 2.5 30.00 50.00
FS & DD Masasi -Nachingwea - Nanganga road. 112.0 75.00 169.00
Sub - Total - Lindi 136.50 475.00 866.00
13
MOROGORO REGION
Rehab. Lusanga - Kibati road 2.5 30.00 60.00
Bridge Construction along Mvomelo - Ndole - Kibati (80km)
3.0 40.00 60.00
Upgrading to Otta seal Liwambanjuki hills(5km) along Lupiro - Malinyi road
4.5 70.00 90.00
FS & DD Ifakara - Kihansi road 130km 130.0 40.00 60.00
Rehab.Ubena Zamozi - Ngerengere road 52km ( Sect. 26+00 - 31+00)
3.0 45.00 60.00
Opening up of Kilosa kwa Mpepo - Londo road (Morogoro/ Ruvuma boarder) -121km
15.0 70.00 100.00
Rehab. Miyombo-Lumuma - Kidete (Moro/Dodoma Boarder) - km 73
2.0 30.00 70.00
164
Construction of Mtibwa Bridge across Wami river along Dakawa/ Wami Mbiki game reserve - Lukenge/ Songambele road
1No. 75.00 100.00
FS & DD Morogoro (Bigwa)-Mvuha road (78km) 78 50.00 74.00
Rehab of Ngiloli - Iyongwe-Gairo road -48km. 3.0 30.00 70.00
Sub - Total - Morogoro 241.00 480.00 744.00
14
MBEYA REGION
Start of Constr. of Mpona Bridge along Galula - Namkukwe road 57km
1No. 90.00 110.00
Rehab. Mbalizi - Shigamba - Isongole 87km ( Mbalizi - Shigamba Sect 52km ) road
5.0 90.00 110.00
Rehab. Saza - Kapalala-63km 2.5 35.00 50.00
Rehab. Ilongo - Usangu road-36.846km 2.5 35.00 50.00
Rehab. Mlowo - Kamsamba road -130.141km (Itumba - Kamsamba Sect - 25km)
2.5 30.00 50.00
Construction of Mbaka & Mwalisi Bridge along Katumba - Tukuyu road (83km)
2No 90.00 110.00
Rehab. Matema - Ikombe (5.8km) 2.0 30.00 37.00
Rehab. Katumbasongwe- Njisi (Ipyana - Katumba Songwe section ) 19.8km
2.5 40.00 50.00
165
Upgrading to DSD of Kikusya - Ipinda - Matema (Kyela-Matema) road -39.5 km.
3.0 220.00 1,500.00
Upgrading to DSD of Katumba-Lwangwa - Mbambo - Tukuyu road (83km).
2.5 220.00 1,270.00
Sub - Total - Mbeya 22.50 880.00 3,337.00
15 MANYARA REGION
Rehab. Losinyai - Njoro (306km) 2.5 35.00 134.00
Rehab. Kilimapunda - Kidarafa 2.5 35.00 100.00
Start Construction of Magara Bridge along Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu road
1No. 75.00 135.00
Upgrading to DSD KIA - Mererani Road 4.3 2,205.00 -
Constr. Concrete slab Along Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu (Rift Valley Section)
0.5 70.00 86.00
Rehab. Arusha/ Manyara boarder - Mbulu road 2.5 30.00 100.00
Rehab. Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu 2.5 30.00 100.00
Sub - Total - Manyara 14.80 2,480.00 655.00
166
16 MARA REGION
Rehab. Nyamwaga - Mriba - Itiryo - Kegonda road
2.0 30.00 50.00
Rehab. Muriba - Kegonga 2.0 30.00 50.00
Rehab. Murangi - Bugwema(15km) 2.0 30.00 50.00
Reh. Guta - Kisorya road section (50km) along Bunda - Kisorya road -64km
2.0 30.00 50.00
Rehab. Manyamanyama - Nyambui (37km) 2.0 30.00 40.00
Feasibility study of Nyamuswa - Bunda - Kisorya (Bunda - Kisorya - Nansio) -118.5km
118.5 1,690.00 200.00
Rehab.Nyankanga - Rung'abure road (89km) 2.0 30.00 40.00
Rehab of Mugumu - Fort Ikoma(Km 31) 2.0 30.00 40.00
Rehab of Balili-Mugeta-Manchimwelu(Km 57) 2.0 30.00 40.00
Rehab of Tarime -Mugumu(Km 87) 10.0 180.00 200.00
Upgrading to DSD Tarime - Nyamwaga road - 25km (Tarime - Nyamigura Sect. ) Otta Seal
0.5 201.50
Upgrading to DSD of Mika Utegi - Shirati road-44Km
0.5 150.00 183.37
Sub - Total - Mara 145.50 2,260.00 1,144.87
167
17 MTWARA REGION
Rehab. Mnongodi - Mdenganamadi - Kilimahewa - Michenjele (boarder road)
2.5 45.00 60.00
Construction of Lukwamba bridge along Mnongodi -Mdenganamadi - Kilimahewa - Michenjele (boarder road)
1No 50.00 200.00
DD and Rehab. Magamba - Mitema - Upinde Rd.297km)
7.0 110.00 140.00
Rehab. Newala - Mkwiti - Mtama road ( Amkeni - Mkwiti Section)
7.0 110.00 140.00
Rehab. Mangamba - Mnazi bay 3.0 50.00 62.00
Upgrading to DSD Kinorombedo escarpment along Newala - Mkwiti Road
0.1 75.00 60.00
Rehab of Mbuyuni - Makong'onda - Newala rd 8.0 - 157.00
Upgrading to SDS Kitangali Hill along Mtama- Kinorombedo - Mkwiti road
0.4 150.00
Sub - Total - Mtwara 27.60 440.00 969.00
168
18
MWANZA REGION
Rehab. Bukongo - Rubya - Bukongo - Masonga road-60.18km
3.0 30.00 70.00
Construction of By- Pass Mwanza Airport - Kayenze road (17km)
0.0 70.00 -
Rehab. Nyakato - Bushwelu - Mhonze road 18km 4.0 80.00
Upgrading to DSD Mwanza Urban roads 0.3 125.00 200.00
Rehab of Bukwimba-Kadashi-Maligisu 3.0 30.00 60.00
FS & DD and Rehab. of 5km Mwanangwa - Misasi - Salawe (49.7km)
49.7 150.00 200.00
Rehab. Ngudu - Nyamilama - Hungumalwa (26km)
2.0 35.00 60.00
Rehab of Misasi Jct - Ihelele (57km) to Mza - Shy Water project
4.5 35.00 90.00
Sub - Total - Mwanza 66.50 475.00 760.00
19 RUKWA REGION
Rehabilitation Kasansa - Mamba - Muze (32Km) 2.0 40.00 60.00
Rehab. Laela - Mwimbi - Kizombwe-92.14Km 2.0 40.00 60.00
Rehab. of Kalepula Junction - Mambwenkoswe-59.9km
2.0 40.00 60.00
169
Rehab Nkundi - Kate - Namanyere-74.14Km 2.0 40.00 60.00
Rehab Kaengesa - Mwimbi (51.11Km) 2.0 40.00 60.00
DD Mtowisa - Ilemba for Realignment and Construction of wash out section (61.37 Km)
2.5 70.00 86.00
Construction of Momba Bridge along Stalike - Kilyamatundu - Kamsamba Mby/Rukwa Boarder
1No 180.00 294.00
Construction of Sakalilo bridge along Mtowisa - Ilemba road
1No 150.00
Sub - Total - Rukwa 12.50 450.00 830.00
20 RUVUMA REGION
Construction of Box Culverts at Londo and its Approach Roads (Lumecha - Kitanda - Londo Rd)
1No. 70.00 80.00
Upgrading to Ottta Seal.Unyoni - Kipapa -Chamani-Mkoha (Mawono Escarpment) 15km
1.0 30.00 190.00
Rehab of Wino - Ifinga road 10km 3.0 50.00 60.00
Rehab. Lumecha - Kitanda - Londo road (Kitanda - Londo Section.) Ruvuma/ Morogoro Boarder 10km
3.0 50.00 60.00
Upgrading Hanga - Kitanda (Mhangazi sect.) ( Otta Seal)
1.0 150.00 193.00
170
Upgrading to otta seal Mbinga - Mbuji - Litembo - Mkili road (Myangayanga escarpment.
1.1 160.00 190.00
Rehab. Nangombo - Chiwindi road (Ng'ombo - Chiwindi Sect )
3.0 50.00 60.00
Rehab. of Songea (Likuyufusi) - Mitomoni road 3.0 50.00 60.00
Rehab. and Realignment chainage 50+000 - 75+000 along Mbababay - Lituhi road
2.5 40.00 50.00
Rehab. Liuli - Lituhi Road 2.5 40.00 50.00
Upgrading of Lumecha - Kitanda - Londo Road (Hanga Section) to Otta Seal
0.5 70.00 80.00
Opening up of Kingosera -Kilindi - Hinga (Kilindi Hinga Sect)
20.0 90.00
DD and Construction of Box Culvert at Mbesa along Tunduru - Nalasi road
1No 30.00 150.00
FS&DD of Kitai - Lituhi - Ndumbi (New Port) rd 120.0 - 170.00
Sub - Total - Ruvuma 160.60 790.00 1,483.00
171
21 SIMIYU REGION
Rehab. Sola - Bushashi - Sakasaka 78.31 km road
10.0 50.00 220.00
Construction of Gamaloha Bridge 0.0 330.00 -
Construction of Bukingwaminzi Bridge 0.0 290.00 -
Rehab of Bariadi-Budalabujiga-Gambasingu Bariadi/Meatu Boarder(Km 40)
7.5 70.00 150.00
Rehab of Lugulu-Kadoto-Malya (56.92 km) 4.5 70.00 100.00
Rehab. Bariadi - Kasoli - Salama (49.01 km) 4.5 70.00 100.00
Construction of 4Nos Box Culverts along Mwanuzi - Sibiti (54.73 km) road
4No. 130.00 160.00
Rehab Sisiyu - Maligisu road (18.48 km) 7.5 150.00
Rehab Mwandete - Mwamanoni road (50.88 km) 7.5 150.00
Rehab Malya - Malampaka - Ikungu road (31.34 km)
7.5 158.00
Rehab. Maswa - Lalago 34km 12.0 250.00
Sub - Total Simiyu 26.50 1,010.00 1,438.00
172
22 SINGIDA REGION
Rehab.Manyoni - Ikasi - Chaligongo 4.0 60.00 80.00
Rehab.Ulemo - Gumanga - Sibiti 3.0 40.00 80.00
Rehab. Senkenke - Shelui 4.0 60.00 80.00
Rehab.Ikungi - Kilimatinde 3.0 40.00 60.00
Rehab. Iguguno - Nduguti - Gumanga 70km 4.0 60.00 80.00
Rehab. Ulemo - Gumanga - Chemchem - Sibiti (Chemchem - Sibiti sect)
3.0 40.00 70.00
Rehab.Mkalama - Mwangaza -Kidarafa road 4.0 60.00 80.00
Rehab. Kititimo - Kinyamshindo road 7.0 70.00 140.00
Rehab. Kisaga - Sepuka - Mlandala (Sepuka - Mlandala Sect.)
4.0 60.00 80.00
Sub - Total - Singida 36.00 490.00 750.00
23 SHINYANGA REGION
Rehab Kahama - Chambo road (Km 45) 7.5 110.00 180.00
Upgrading to DSD Kahama township roads (5.5km)
0.5 220.00 290.00
Rehab. Old Shinyanga - Salawe road 9.0 110.00 176.00
Rehab. Nyandekwa - Uyogo - Sunga 60km 7.5 160.00
Sub - Total - Shinyanga 24.50 440.00 806.00
173
24 TABORA REGION
Rehab Puge - Ziba 5.0 45.00 100.00
Rehab. Usagali - Fuluma - Ndono road (38km) 5.0 45.00 100.00
FS & DD for a Bridge along Lusu - Nzega road 0.0 45.00 -
Rehab. Kaliua - Uyowa - Makazi road 5.0 45.00 100.00
Rehab. Mambali - Bukene 5.0 45.00 100.00
Rehab. Ibologero - Igurubi (Regravelling and 1 Bridge)
0.0 140.00 -
Rehab. Sikonge - Usoke road (Tutuo - Usoke) 5.0 45.00 100.00
Opening up of Tura - Iyumbu (upgraded rd) 4.0 40.00 100.00
Rehab. Sikonge - Mibono - Kipili - 165km 9.0 180.00
Sub - Total - Tabora 38.00 450.00 780.00
25 TANGA REGION
Rehab. Lushoto - Mlalo 2.5 40.00 60.00
Upgrading to DSD Mombo -Lushoto - Magamba road(Lushoto - Magamba Sect. Km 5.1)
0.3 120.00 199.00
Rehab of Mbuyuni-Kasera(Mkinga districts)-Km 9 3.0 45.00 70.00
Rehab. Handeni – Kiberashi - Songe 3.0 45.00 60.00
174
Rehab of Songe-Vyadigwa-Mziha road(Km 103) (Kwaluguru - Songe)
3.5 60.00 75.00
Rehab. Kwekivu - Kwalugalu Road (Kwekivu - Iyogwe)
2.5 40.00 60.00
FS and DD of Muheza - Amani road 0.0 40.00 -
Resealing of Tanga - Pangani rd (Mabanda ya Papa - Boza jctn)
0.2 70.00 70.00
Upgrading of Muheza - Amani to DSD 1.0 500.00
Sub - Total - Tanga 16.00 460.00 1,094.00
WORKS/TANROADS 1,668.30 19,925.00 30,236.27
26 Consultancy Services for Identification and classification of Urban Roads.
0.00 500.00
27 ERB - SEAP Programme 0.00 500.00
28 MONITORING (MoW) 485.00 679.000
TOTAL CONSOLIDATED
1,668.30 20,410.000 31,915.270
& 17 Bridges
175
KIAMBATISHO NA. 3 MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14
Kasma Jina la Mradi Urefu/Km
Makadirio ya Bajeti kwa Mwaka 2013/2014
Miradi ya Barabara
2326 Bagamoyo - Saadani - Tanga ( FS & DD) 178 50,000,000.00
2326 Sumbawanga - Matai - Kasanga Port/Matai-Kasesya Border(DD)
50 100,000,000.00
2326 Training & Technical Assistance TANROADS 300,000,000.00
2326 Ifakara - Mahenge (FS & DD) 67 200,000,000.00
2326 Kibondo - Mabamba (FS & DD) 35 200,000,000.00
2326 Mpemba - Isongole (Tanzania/ Malawi) (FS & DD) 49 200,000,000.00
2326 Omugakorongo - Kigarama - Murongo (FS & DD) 105 400,000,000.00
2326 Review and preparation of Standards and Specifications
300,000,000.00
2326 Kyaka - Bugene - Kasulo/Benako -Bugene - Kasulo Section (FS & DD)
124 400,000,000.00
2326 Handeni-Kiberashi- Kijungu - Kibaya - Njoro - Olboloti - Mrijo Chini - Dalai - Bicha - Chambalo - Chemba - Kwa Mtoro - Singida (FS & DD)
460 900,000,000.00
2326 Upgrading to DSD Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi road.
17 1,000,000,000.00
176
2326 New Wami Bridge (FS&DD) 1No. 300,000,000.00
2326 Kidatu - Ifakara - Lupilo - Malinyi - Londo - Lumecha/Songea (FS & DD)
396 50,000,000.00
2326 Road Flyovers Compensation for TAZARA and Ubungo 1No. 100,000,000.00
2326 Mtwara - Newala - Masasi Including Mwiti Bridge (FS & DD) 209 600,000,000.00
2326 Kolandoto - Lalago - Mwanhuzi - Matala - Oldeani Junction (FS & DD)
328 500,000,000.00
2326 Environmental Impact Assesment (EIA) Rusumo Bridge in Kagera Region
1No. 50,000,000.00
2326 Central Materials Laboratory (CML) 1No. 500,000,000.00
2326 Preparation of Strategic Plan - TANROADS 100,000,000.00
2326 Monitoring and Evaluation of Strategic Plan, Development & Maintenance Projects – TANROADS
M&E 400,000,000.00
2326 Monitoring and Other Related Activities (MOW) 860,000,000.00
2326 Mwanangwa - Misasi - Salawe - Kahama (FS & DD) 149 500,000,000.00
2326 Itoni - Ludewa - Manda (FS & DD) 211 346,610,000.00
2326 Arusha-Kibaya-Kongwa (FS & DD) 430 500,000,000.00
2326 Provision of Escape Ramps for Long Steep Grades and Climbing Lanes along Major Trunk Roads - FS & DD
270,000,000.00
Jumla ndogo 9,126,610,000.00
Barabara za Mikoa 20,192,695,800.00
Miradi ya Vivuko
177
2326 Procurement of New ferry for Kahunda-Maisome 787,950,000.00
2326 Procurement of New ferry for Itungi Port 906,270,000.00
2326 Procurement of ferry spare parts 900,000,000.00
2326 Procurement of Rescue boat for Ukerewe ferries (Rugezi- Kisorya and Buolora-Ukara).
469,510,000.00
2326 Monitoring, Evaluation and Other Related Activities 100,000,000.00
Jumla Ndogo 3,163,730,000.00
Road Related Activities
2326 Support to Roads Monitoring and Evaluation activities, Preparation of Roads Sector Performance Indicators and Roads Sector statistics
202,870,000.00
2326 Participation in East African Cooperation Road Network meetings, SADC Roads Related Programmes, COMESA-EAC-SADC Tripartite Free Trade Area and Sub Saharan Africa Transport Policy – SSATP meetings
185,000,000.00
2326 Co-ordination of Corridor Development Issues (Mtwara, Central and Dar es Salaam Corridors)
150,000,000.00
2326 Co-ordination of Ministry’s Budget and Action Plan Preparations and Roads Sector Concept Papers and Write- ups.
370,000,000.00
2326 Preparations of Roads Act Regulations 40,000,000.00
178
2326 Preparations of Audit Reports for Roads Fund Accounts, Roads Fund Operational Plans and Roads Fund Progress Reports
107,500,000.00
2326 Contribution to Roads Associations and Participation in Roads and Transport Professional Bodies Meetings
70,000,000.00
2326 Facilitation to Technology Transfer Center (T2 Centre ) 100,000,000.00
2326 Expenses on television broadcasting on implementation of roads, bridges and ferries projects and advertisement of Ministry’s Budget Speech
100,000,000.00
Jumla Ndogo 1,325,370,000.00
Usalama Barabarani na Mazingira
2326 EAC Vehicle Load Control Bill 2012 and conduct optimal number of weighbridges
300,000,000.00
2326 Purchasing and installation of CCTV cameras to 26 weighbridge stations
200,000,000.00
2326 Construct Prototype resting station 200,000,000.00
2326 Support to Environmental Management in the Road Sector 132,000,000.00
2326 Skills development on road safety profession 50,000,000.00
2326 Promote through pilot projects and conduct training for weigh in motion weighbridges and road damage control sensors
200,000,000.00
2326 Monitoring and evaluation of Road and vehicle Safety 58,000,000.00
Jumla Ndogo 1,140,000,000.00
JUMLA KUU 34,948,405,800.00
179
KIAMBATISHO NA.4 MCHANGANUO WA BARABARA ZA MIKOA INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA 2013/14
S/N PROJECT NAME
TARGET (in km / No of bridges) 2013/14
APPROVED BUDGET
2012/13 in Tsh mio
BUDGET ESTIMATES
2013/14 in Tsh. Mio
Local Local
REGIONAL ROADS
1 ARUSHA REGION
Rehab. Longido - Kitumbeine - Lengai (Kitumbeine - Lengai Sect.) km 102.4
10.5 200.00 210.00
Rehab. KIA - Majengo along KIA - Mererani road km 25
7.5 150.00 150.00
Rehab. Tengeru Jct - Cairo 7.0 140.00
Sub- total Arusha 25.0 350.00 500.00
2 COAST REGION
Rehab. Kisarawe - Masaki - Msanga - Chole - Vikumburu Road
5.0 100.00 100.00
Rehab. Kiparang'anda-Nyamalile-Kibululu-Magonza Road
2.5 60.00 50.00
Purchase of Excavator/Roller/back hoe for Mafia roads
0.0 70.00 -
180
FS & DD Mlandizi - Mweneromango road 137.0 90.00 120.00
Upgrading of TAMCO - Vikawe - Mapinga to DSD (24km)
0.7 65.00 310.00
Rehab of Ikwiriri - Mloka - Vikumburu 4.0 75.00 80.00
Rehab. Utete - Nyamwage (km 32) 2.0 40.00
Sub- total Coast 151.2 460.00 700.00
3
DAR ES SALAAM REGION
Rehab. Uhuru Road -1km 0.4 550.00 340.00
Upgrading Chanika - Mbande road DSD 29.6km
0.3 120.00 130.00
Upgrading to DSD Feri - Tungi Kibada road 0.3 120.00 130.00
Upgrading of Mzinga - Way to DSD 0.0 120.00 -
Upgrading Boko - Mbweni road to DSD (6.9km) 0.5 290.00 220.00
Sub- total Dar es Salaam 1.5 1,200.00 820.00
4
DODOMA REGION
Rehab. Izava - Dosidosi road (15km) 5.0 120.00 100.00
Upgrading of Mbande-Kongwa Junction-Mpwapwa(50Km) to Paved standard
0.1 110.00 200.00
Start Construction of Gulwe Bridge along Mpwapwa - Gulwe - Kibakwe - Chipogoro road
1N0 200.00 200.00
Sub - Total Dodoma 5.1 430.00 500.00
181
5 GEITA REGION
Rehab. Chibingo - Bukondo road - 37km 4.0 100.00 80.00
Rehab. of Geita - Nkome - Mchangani-13km 4.0 80.00 80.00
Rehab. of Geita - Nyarugusu - Bukoli-52.85km 4.5 80.00 90.00
Design and Construction of Bugoyo Bridge along Ngw'amhaya-Itongoitale road
0.0 110.00 -
Upgrading to DSD Chato-Mkuyuni-Rubambangwe
1.0 70.00 350.00
Rehab. Muganza-Kasenda 4.0 70.00 80.00
Rehab. Kibehe-Kikumbaitale 4.0 100.00 80.00
DSD Upgrading.Geita Township roads 0.7 300.00
Rehab.Chato Ginnery - Bwina 5km 2.5 0.00 50.00
Sub - Total - Geita 24.7 610.00 1,110.00
6
IRINGA REGION
FS and DD Iringa - Msembe road 104.0 65.00 60.00
FS & DD Izazi - Mbolimboli - Pawaga - Mlowa road(83km)
0.0 70.00 -
FS & DD Nyololo-Igowole-Kibao km 40.4 40.4 65.00 70.00
DSD Iringa -Msembe (Kalenga Jnct-Ipamba Hospital)
0.5 230.00
Rehab. Nyololo - Kibao km 40.4 4.5 100.00 90.00
Rehab. Ilula - Kilolo km 87.6 6.0 130.00 120.00
Sub - Total - Iringa 155.4 430.00 570.00
182
7 KAGERA REGION
Rehab. Kajai -Swap along Katoma - Bukwali road (9km)
2.0 180.00 200.00
Rehab. Muhutwe - Kamachumu - Muleba road Km 53.2
15.0 170.00 300.00
Sub - Total - Kagera 17.0 350.00 500.00
8 KATAVI REGION
Rehab. Mamba - Kasansa(18Km) 5.0 100.00 110.00
Rehab. Mpanda - Ugala road(74Km) 6.0 100.00 120.00
Rehab. Mnyamasi - Ugallla km 29.2 6.0 95.00 120.00
Rehab. Inyonga - Majimoto (135km) 7.0 145.00 150.00
Sub - Total - Katavi 24.0 440.00 500.00
9 KIGOMA REGION
Construction of Kangwena bridge along Simbo - Ilagala - Kalya road
1No 275.00 210.00
Construction of 9 bridges along Simbo - Ilagala - Kalya road
9Nos 100.00 340.00
Rehab. Kakonko - Nyaronga - Ngara Boarder 6.0 125.00 120.00
Sub - Total - Kigoma
6.0 500.00 670.00
183
10
KILIMANJARO REGION
Const. of Kikuletwa Bridge along TPC Road 1No 100.00 120.00
Rehab of Mwembe - Myamba - Ndungu 7.0 110.00 150.00
Upgrading of Same - Kisiwani - Mkomazi incl Mamba bridge
1.5 380.00 700.00
Sub - Total - Kilimanjaro 8.5 590.00 970.00
11 LINDI REGION
Mbwemkuru - Nanjilinji - Kiranjeranje (134km) 5.0 110.00 110.00
Rehab. Nangurukuru - Liwale road 6.0 150.00 120.00
Rehab. Nachingwea - Masasi road 5.0 0.00 110.00
Upgrading of Kinolombedo escarpment to DSD along Makao - Mtama road Sectn
110.00 -
Upgrading to DSD Ruangwa township roads 1.7 700.00
DD Lukuledi Bridge along Luchelegwa - Ndanda road
1NO 50.00
Sub - Total - Lindi 17.7 370.00 1,090.00
12 MANYARA REGION
Construction of Babati - Orkesumet/Kibaya New Acess Rd- 250km
7.0 130.00 140.00
Rehab Kibaya - Kibereshi road 92 km 4.5 80.00 90.00
Rehab. Nangwa - Gisambang - Kondoa Brd. 4.5 80.00 90.00
184
Rehab Mogitu - Haydom 68 Km 4.5 80.00 90.00
Rehab. Magara Escarpment (concrete pavement)
1.0 270.00 270.00
Sub - Total - Manyara 21.5 640.00 680.00
13
MARA REGION
Rehab. Musoma - Makojo road(7km) 4.5 80.00 90.00
Rehab. Balili - Mgeta - Manchimweli - Rimwani road(57km)
4.5 80.00 90.00
Upgrading to DSD Bunda - Kisorya - Nansio road (Nansio - Kisorya sect.) -118.5km
0.3 110.00 120.00
Upgrading to DSD Mika - Utegi - Shirati road (60km)
0.3 130.00 140.00
Upgrading to DSD Tarime - Nyamwaga road - 25km (Tarime - Nyamigura Sect. ) Otta Seal
0.9 240.00 410.00
Rehab Makutano ya Kinesi - Kinesi (11km) 3.0 50.00
Rehab Nyamwigura-Gwitiryo 5.0 90.00 100.00
Sub - Total - Mara 18.5 730.00 1,000.00
14 MBEYA REGION
Rehab. of Gagula - Namkukwe road (57km) Construction of 3 No. structures
3.0 65.00 70.00
Rehab. Mbalizi - Shigamba - Isongole (Ibaba - Shigamba Sect 9km road
6.0 110.00 120.00
Upgrading to DSD Igawa - Rujewa - Ubaruku 0.3 150.00 160.00
185
Construction of Mbalizi - Makongorosi ( Mbalizi - Utengule 8km) Otta Seal
0.4 150.00 180.00
Rehab. Ilongo - Usangu road( 36.846km) 4.0 70.00 80.00
Raising Embakment Msangano - Tindingoma (6km section) road
4.0 60.00 70.00
Upgrading to DSD of Kikusya - Ipinda - Matema (Kyela-Matema) road -39.5 km.
0.0 200.00 -
Sub - Total - Mbeya 17.7 805.00 680.00
15 MOROGORO REGION
Rehab. Mahenge - Mwaya-Ilonga road ( 40km) 2.5 50.00 60.00
Upgrading "Mlima Simba hills 6km" (Otta Seal) along Mahenge - Mwaya Road
0.5 180.00 180.00
Rehab Ifakara - Taweta-Madeke road (246km) 3.5 70.00 80.00
Feasibility study and Preliminary Engineering Design for Duthumi II bridge.
1No 80.00 80.00
Rehab. Gairo-Nongwe (74km) 15.0 700.00 300.00
Upgrading of Mahenge township roads 0.8 400.00
Sub - Total - Morogoro 22.23 1,080.00 1,100
186
16 MTWARA REGION
Upgrading to DSD Newala Township Roads (5km)
1.0 460.00 340.00
Rehab.Tandahimba - Litehu Mkwiti Road 5.0 90.00 100.00
DD of Mwiti bridge along Mtwara -Newala -Masasi road (209km)
0.0 90.00 -
Constructioin of Lukwamba Bridge 1No 190.00 200.00
Upgrading to DSD Kinorombedo escarpment along Newala - Mwiti road
0.5 120.00
Sub - Total - Mtwara 6.5 830.00 760.00
17 MWANZA REGION
Rehab. Kayanze - Nyanguge road -20.24km 4.0 80.00 80.00
Rehab. Kabaganga Ferry - Mugogo - Nyakabanga (5km)
3.5 80.00 80.00
Rehab. Magu - Bukwimba Ngudu - Jojiro road (64km)
4.0 80.00 80.00
Rehab. of Lumaji - Nyanshana (14km) 4.0 80.00 80.00
Construction of Sukuma (Simiyu II) bridge along Magu - Mahaha road
1No. 90.00 100.00
Rehab Inonelwa - Kawekamo-(29km) 4.0 90.00 80.00
187
Rehab Mwamhaya - Itongoitale-(51km) 3.5 70.00 70.00
Rehab.Nyambiti - Fulo road-(46.97km) 3.5 70.00 80.00
Rehab. Mwanangwa-Misasi-Buhingo-Ihelele 4.0 110.00 80.00
Purchase of Motor Grader for Ukerewe roads 1No 300.00
Sub - Total - Mwanza 30.5 750.00 1,030.00
18 NJOMBE REGION
Rehab. Ndulamo - Nkenja - Kitulo - Mfumbi 95km
5.0 100.00 100.00
Rehab Njombe - Ndulamo - Makete (109.4) 5.0 90.00 100.00
FS & DD of Kibena - Lupembe - Mfuji (Moro/Iringa Brd) 125.2km
125.0 150.00 140.00
FS & DD of Njombe - Iyayi 74km 74.0 100.00 240.00
Rehab of Ikonda - Lupila - Mlangali Rd (Lupila - Mlangali section)
5.0 110.00 110.00
Upgrading to DSD Igwachanya township roads 1.0 400.00
Sub - Total - Njombe 215.0 550.00 1,090.00
19 RUKWA REGION
Rehab. Ntendo - Muze (39km) Kizungu hill section to DSD
6.0 120.00 120.00
Rehab. Kasansa - Muze (32Km) 6.0 100.00 120.00
Rehab. Miangalua - Kipeta road (Miangalua - Chombe Section :19km)
7.5 90.00 150.00
Rehab Kalambanzite - Ilemba road 5.5 90.00 110.00
Sub - Total - Rukwa 25.0 400.00 500.00
188
20 RUVUMA REGION
Rehab. Azimio - Lukumbule-Tulingane (Lukumbule-Tulingane section 16.3km) road
3.5 60.00 70.00
Rehab.of Lilondo Quarry Plants. set 60.00 50.00
Opening up Londo - Kilosa Kwa Mpepo road Section (40km)
15.0 110.00 150.00
F.S and DD of Songea - Mitomoni - Mkenda road (124km)
124.0 65.00 80.00
Rehab. Chamani - Matuta - Mango - Kihagara road 10km
3.0 65.00 60.00
Upgrading to DSD Kilimo Mseto - Makambi road (2km)
0.2 110.00 200.00
Upgrading to Otta Seal Hilly setions along Mtwara Pachani - Mkongo - Sasawala - Nalasi road 232km - (2km long streach)
0.5 90.00 100.00
Construction of Londo bridge approach road - Otta Seal ( 1km ) along Kitanda - Londo (Ruvuma/ Morogoro Brd)
0.5 110.00 100.00
Rehab of Kitai - Lituhi 4.0 70.00 80.00
Rehab. Matimira - Mkongo (11.8km) 4.0 110.00 80.00
Rehab. Mpitimbi - Ndongosi - Nambendo (63km)
4.0 110.00 90.00
Upgrading to Ottta Seal.Unyoni - Kipapa -Chamani-Mkoha (Mawono Escarpment) 15km
0.8 200.00
Sub - Total - Ruvuma 159.5 960.00 1,260.00
189
21 SHINYANGA REGION
Upgrading to DSD Shinyanga - Old Shinyanga road
0.9 160.00 400.00
Constr. Of Vented Drift along . Isagenye - Budekwa - Mabaraturu road
1No 120.00 340.00
Kahama - Bulige - Mwakitolyo - Solwa 2.5 80.00 50.00
Rehab. Nyandekwa - Uyogo - Mwande (Shy/Tbr brd)
3.0 80.00 80.00
Rehab. Nyandekwa -Butigu road (20 km) 2.5 50.00
Sub - Total - Shinyanga 8.9 440.00 920.00
22 SIMIYU REGION
Rehab. Luguru - Kadoto - Malya road 7.5 75.00 150.00
Rehab. Maswa - Kadoto - Shishiyu - Jija - Maligisu road
7.5 75.00 150.00
Rehab. Mkoma - Makao road 10.0 70.00 200.00
Construction of Gamaloha Bridge 0.0 380.00 -
Sub - Total - Simiyu 25.0 600.00 500.00
23 SINGIDA REGION
Rehab. Soweto(Kiomboi)-Kisiriri-Chemchem 9.0 150.00 180.00
Rehab. Mkalama-Mwangeza-Kidarafa 8.5 135.00 170.00
190
Construction of Msosi Box culvert and approaches along Iyumbu (Tabora brd) - Mgungira - Mtunduru - Magereza rd
1No. 105.00 150.00
Sub - Total - Singida 17.5 390.00 500.00
24 TABORA REGION
Rehab. Tutuo - Izimbili - Usoke (70km) 7.5 120.00 150.00
Rehab. Nzega - Itobo - Bukooba (54.5km) 8.5 120.00 170.00
Rehab. Sikonge - Mibono - Kipili road 9.0 115.00 180.00
Sub - Total - Tabora 25.0 355.00 500.00
25 TANGA REGION
Rehab Mlalo - Mng'aro road (25km) 4.5 125.00 90.00
Rehab.Muheza - Maramba (41km) 4.5 120.00 90.00
Rehab Mbaramo - Misozwe - Maramba - Kasera road (90km)
4.5 70.00 80.00
Rehab of Magamba - Mlola Km 35.7 4.5 70.00 90.00
FS & DD of Amani - Muheza 34km 34.0 150.00
Sub - Total - Tanga 52.0 385.00 500.00
191
26
MoW ( Monitoring and Road Related Activities Including Purchase of one (1 ) Vehicle for Monitoring)
0.0 500.00 700.00
27 Road Classification Activities 0.0 120.00
28 SPECIFIC ROAD RELATED PROJECTS:
ATTI (Taking Labour Based Technology to Scale)
0.0 140.00 160.00
MWTI 0.0 160.00 180.00
WPU 0.0 79.90 82.696
TOTAL ROAD FUND 1,081.00 15,524.90 20,192.6958
18 bridges
192
KIAMBATISHO 5 (A) – (E)
MPANGO WA MATENGENEZO YA BARABARA 2013/14
193
KIAMBATISHO 5
MUHTASARI WA MPANGO WA MATENGENEZO YA BARABARA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA MWAKA 2013/14
(i) Barabara za Kuu
S/NO MAINTENANCE ACTIVITY ANNUAL PLAN
PHYSICAL FINANCIAL (Tshs. mio.)
UNIT QTY ROAD FUND FOREIGN TOTAL
1.0 Routine & Recurrent - Paved km 5,798.11 15,301.389 - 15,301.389
2.0 Routine & Recurrent - Unpaved
km 4,386.73 8,989.651 - 8,989.651
3.0 Periodic Maintenance - Paved
km 258.80 49,576.594 - 49,576.594
4.0 Periodic Maintenance - Unpaved
km 741.59 15,042.745 - 15,042.745
5.0 Spot Improvement - Paved km 26.20 2,866.202 - 2,866.202
6.0 Spot Improvement - Unpaved km 65.44 1,348.720 - 1,348.720 7.0 Bridges Preventive Mtce Nos. 1,187 1,482.187 - 1,482.187
8.0 Bridges Major Repairs Nos. 85 6,708.226 - 6,708.226
SUB-TOTAL Routine & Recurrent
Km 10,184.84 24,291.040 - 24,291.040
SUB-TOTAL Periodic & Spot Maintenance
Km 1,092.03 68,834.261 - 68,834.261
SUB-TOTAL Bridges Nos. 1,272 8,190.413 - 8,190.413
TOTAL TRUNK ROAD BUDGET 101,315.714 - 101,315.714
194
(ii) Barabara za Mkoa
S/NO MAINTENANCE ACTIVITY
ANNUAL PLAN PHYSICAL FINANCIAL (Tshs. mio.)
UNIT QTY ROAD FUND FOREIGN TOTAL
1.0 Routine & Recurrent - Paved km 972.63 2,530.780 - 2,530.780
2.0 Routine & Recurrent - Unpaved
km 19,498.59 30,997.055 - 30,997.055
3.0 Periodic Maintenance - Paved
km 131.82 36,654.144 - 36,654.144
4.0 Periodic Maintenance - Unpaved
km 2,888.64 53,348.012 - 53,348.012
5.0 Spot Improvement - Paved km 5.18 939.030 - 939.030
6.0 Spot Improvement - Unpaved km 992.23 16,279.015 - 16,279.015 7.0 Bridges Preventive Mtce Nos. 1,141 1,674.975 - 1,674.975
8.0 Bridges Major Repairs Nos. 164 19,680.550 - 19,680.550
SUB-TOTAL Routine & Recurrent
km 20,471.22 33,527.835 - 33,527.835
SUB-TOTAL Periodic & Spot Maintenance
km 4,017.87 107,220.200 - 107,220.200
SUB-TOTAL Bridges Nos. 1,305 21,355.525 - 21,355.525
TOTAL REGIONAL ROAD BUDGET 162,103.560 - 162,103.560
GRAND TOTAL TRUNK & REGIONAL ROADS(Works)
Routine & Recurrent
km 30,656.06
263,419.274 - 263,419.274 Periodic & Spot km 5,109.90
Bridges Bridges 2,577
195
(iii) Dharura na Tahadhari
1.0 Emergency & Urgent Works 6,871.541 - 6,871.541 (iv) Mradi wa PMMR
1.0 Works & Supervision Consultancy
km 273.0 2,324.837 - 2,324.837
(v) Matengenezo, Ukarabati na Ujenzi wa Mizani
1.0 Improvements & Major Repairs
1,200.000 - 1,200.000
2.0 Installation of missing W/bridge
2,300.000 - 2,300.000
SUB-TOTAL 3,500.000 - 3,500.000
(vi) HQ BASED MAINTENANCE ACTIVITIES 1.0 RMMS Systems 680.000 - 680.000
2.0 Road Data Collection 720.000 - 720.000
3.0 Bridge Management System
400.000 - 400.000
4.0 Road Safety 1,870.000 - 1,870.000 5.0 Road Act Enforcement 800.000 - 800.000
SUB-TOTAL 4,470.000 - 4,470.000
196
(vii) ADMINISTRATION AND SUPERVISION (Non Works)
1.0 Administration Cost 10,650.000 - 10,650.000
2.0 Supervision Cost 13,500.000 - 13,500.000
SUB-TOTAL 24,150.000 - 24,150.000 (viii) WEIGHBRIDGE OPERATIONS (Non Works)
1.0 Weighbridge Operations
9,800.000 - 9,800.000
SUB-TOTAL 9,800.000 - 9,800.000 TOTAL ROADS FUND BUDGET 314,535.652 - 314,535.652
197
KIAMBATISHO NA. 5(A - 1)
MATENGENEZO YA KAWAIDA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA MWAKA 2013/14 BARABARA KUU
(a) Barabara Kuu za Lami Estimated Expenditure in Tshs mio. Target (km) FY 2013/14
Mkoa Roads Fund Foreign Total Estimate
Arusha 253.05 909.997 - 909.997
Coast 396.29 1,021.449 - 1,021.449 Dar es Salaam 86.70 470.997 - 470.997 Dodoma 200.52 388.080 - 388.080 Geita 201.83 319.067 - 319.067
Iringa 270.00 909.995 - 909.995 Kagera 282.36 677.110 - 677.110 Katavi 1.30 5.620 - 5.620 Kigoma 172.58 391.764 - 391.764 Kilimanjaro 223.60 651.798 - 651.798
Lindi 335.48 546.834 - 546.834 Manyara 173.91 238.786 - 238.786
Mara 185.20 720.982 - 720.982 Mbeya 357.28 1,138.249 - 1,138.249 Morogoro 445.13 1,393.772 - 1,393.772
Mtwara 170.27 499.355 - 499.355 Mwanza 230.92 515.138 - 515.138 Njombe 194.06 493.320 493.320 Rukwa 242.68 439.936 - 439.936 Ruvuma 385.95 912.872 - 912.872 Shinyanga 209.20 526.131 - 526.131 Simiyu 66.72 249.979 249.979
Singida 340.60 874.900 - 874.900
Tabora 145.27 325.998 - 325.998 Tanga 227.21 679.260 - 679.260
Sub-Total 5,798.11 15,301.389 - 15,301.389
198
(b) Barabara za Kuu za Changarawe/Udongo
Estimated Expenditure in Tshs mio.
Target (km) FY 2013/14
Mkoa Roads Fund Foreign Total Estimate
Arusha 125.62 74.981 - 74.981
Coast 3.00 5.790 - 5.790
Dar es Salaam 22.00 22.000 - 22.000 Dodoma 186.91 542.450 - 542.450 Iringa 66.40 168.347 - 168.347 Kagera 208.79 374.840 - 374.840 Katavi 327.80 869.000 869.000 Kigoma 641.49 1,422.140 - 1,422.140 Manyara 31.04 57.546 - 57.546 Mara 261.55 444.996 - 444.996 Mbeya 278.43 589.986 - 589.986
Morogoro 317.70 596.455 - 596.455
Njombe 209.00 353.134 353.134 Rukwa 203.00 424.650 - 424.650
Ruvuma 470.64 776.299 - 776.299 Shinyanga 69.13 168.373 - 168.373
Simiyu 196.09 418.978 418.978
Singida 224.40 504.486 - 504.486 Tabora 543.74 1,175.200 - 1,175.200
Sub-Total 4,386.73 8,989.651 - 8,989.651
Total Trunk Roads Routine/Recurrent Maintenance (TShs. Mio.)
Target Roads Fund Foreign Total
10,184.84 24,291.040 - 24,291.040
199
KIAMBATISHO NA. 5(A - 2) MATENGENEZO YA KAWAIDA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14 BARABARA ZA MIKOA
(a) Barabara za Mikoa za Lami Estimated Expenditure in Tshs mio. Target (km) FY 2013/14
Roads Fund Foreign Total Estimate
Arusha 33.00 51.000 - 51.000
Coast 18.10 22.999 - 22.999 Dar es Salaam 171.85 628.668 - 628.668 Dodoma 12.95 32.730 - 32.730
Geita 72.00 197.629 - 197.629 Iringa 20.40 132.436 - 132.436
Kagera 68.58 89.550 - 89.550 Kilimanjaro 131.02 350.817 - 350.817
Lindi 37.49 43.750 - 43.750
Manyara 10.62 26.597 - 26.597 Mara 44.10 234.994 - 234.994 Mbeya 28.44 72.768 - 72.768
Morogoro 52.95 223.361 - 223.361 Mtwara 50.40 86.309 - 86.309
Mwanza 15.54 33.120 33.120 Njombe 12.50 23.805 23.805
Rukwa 5.00 12.50 - 12.500
Ruvuma 12.27 45.960 - 45.960 Shinyanga 13.57 41.817 - 41.817
Singida 27.20 24.549 - 24.549
Tabora 6.30 11.997 - 11.997 Tanga 128.35 143.424 - 143.424
Sub-Total 972.63 2,530.780 - 2,530.780
200
(b) Barabara za Mikoa za Changarawe/Udongo Estimated Expenditure in Tshs mio.
Target (km) FY 2013/14
Roads Fund Foreign Total Estimate Arusha 439.80 898.181 - 898.181
Coast 879.90 1,027.999 - 1,027.999 Dar es Salaam 226.40 410.594 - 410.594 Dodoma 1,113.18 1,659.970 - 1,659.970 Geita 373.62 689.740 689.740 Iringa 639.40 1,230.166 - 1,230.166 Kagera 864.28 1,258.000 - 1,258.000
Katavi 465.46 674.087 674.087
Kigoma 414.85 1,343.780 - 1,343.780 Kilimanjaro 541.01 778.607 - 778.607 Lindi 905.35 1,425.688 - 1,425.688 Manyara 1,437.33 1,682.650 - 1,682.650 Mara 896.12 1,914.405 - 1,914.405 Mbeya 1,414.99 1,548.552 - 1,548.552
Morogoro 988.36 1,489.287 - 1,489.287 Mtwara 716.80 1,020.042 - 1,020.042 Mwanza 685.63 1,198.137 - 1,198.137 Njombe 589.63 899.145 899.145 Rukwa 841.48 1,961.761 - 1,961.761 Ruvuma 1,062.70 2,154.660 - 2,154.660 Shinyanga 659.24 1,178.000 - 1,178.000
Simiyu 579.04 1,075.393 1,075.393 Singida 985.90 1,239.400 - 1,239.400 Tabora 691.28 965.001 - 965.001 Tanga 1,086.84 1,273.810 - 1,273.810 Sub-Total 19,498.59 30,997.055 - 30,997.055
Total Regional Roads Routine/Recurrent Maintenance (Tshs mio.):
Target Roads Fund Foreign Total
20,471.22 33,527.835 - 33,527.835
201
KIAMBATISHO NA. 5 (B - 1)
MATENGENEZO MAALUMU (PERIODIC MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14 BARABARA KUU
(a) Barabara Kuu za Lami
Region Road name Length (km) Estimate (mio Tshs) ARUSHA
KIA JCT - TCA JCT - Namanga 5.50 1,298.182
TCA Junction - Mijingu 1.71 544.100 Makuyuni - Ngorongoro Gate 1.40 354.430
Subtotal 8.61 2,196.712 COAST Kibaha - Mlandizi - Ngerengere 9.50 2,555.440
Kongowe - Kibiti - Nyamwage 9.00 864.080
Bunju - Bagamoyo 2.00 130.000 Subtotal 20.50 3,549.520
DAR ES SALAAM
Morogoro Road 2.00 570.000 Kilwa Road 5.00 2,300.000
New Bagamoyo Road 1.00 500.000 Nyerere Road (Shoulders, Service roads, walk way, cyclists path)
5.00 1,460.333
Improvement of TR Junctions 1.50 2,000.000 Climbing lane Morogoro Road (Kibamba)
1.20 1,800.000
202
Road Safety Measures
Installation of Solar Traffic Lights at Sokota Jct (Mandela road)
1.00 200.000
Installation of pedestrian overhead bridge at Mbezi Mwisho along Morogoro Rd
2.00 200.000
Road Markings and signs along Trunk roads
500.000
Subtotal 18.70 9,530.333 DODOMA
Gairo - Dodoma - Kintinku 4.00 1,034.150
Installation of Traffic lights Dodoma Urban
400.000
Mtera - Dodoma 2.94 1,067.860
Dodoma – Bereko (Dom/Manyara Bdr) 3.88 458.150 Subtotal 10.82 2,960.160
IRINGA
Tanzam Highway 4.00 978.480
Mafinga - Mgololo 3.00 312.000
Subtotal 7.00 1,290.480
KAGERA
Mutukula - Bukoba - Kagoma - Kalebezo
1.35 510.000
Bukoba - Bukoba Port 1.00 300.260
Rusumo - Lusahunga 1.20 500.000
Kobero - Ngara - Nyakasanza 3.59 260.630
Subtotal 7.14 1,570.890 KIGOMA
Kasulu - Kigoma (Mwanga) - Kigoma 29.37 594.115
Subtotal 29.37 594.115
203
KILIMANJARO
Same - Himo Jct - KIA Jct 6.20 1,604.923
KIA Jct - KIA 0.50 126.545
Subtotal 6.70 1,731.468
LINDI Mtegu - Mingoyo - Mkungu 19.50 2,007.422
Malendegu - Nangurukuru - Mingoyo 8.50 972.478
Subtotal 28.00 2,979.900
MARA
Sirari Jct - Sirari (Overlay & embankment reinstatement)
12.50 3,112.000
Subtotal 12.50 3,112.000
MBEYA
TANZAM (Iyayi (Iringa/Mbeya Border) - Tunduma (Tanz/Zambia brd))
3.30 1,023.302
Ibanda - Kiwira Port 4.90 1,242.100
Subtotal 8.20 2,265.402
MOROGORO
Tanzam Highway 10.90 1,100.000
Morogoro - Dodoma(Gairo) 14.40 1,605.640
Mikumi - Kidatu - Mahenge - K/mpepo - Londo
3.00 300.000
Subtotal 28.30 3,005.640
MTWARA
Mtwara - Mtegu 4.53 647.920
Mkungu - Masasi 18.00 1,470.883
Masasi-Mangaka (Lined Ditches) 200.000
Subtotal 22.53 2,318.803
MWANZA
Geita brd - Usagara - Mwanza - Simiyu bdr
8.00 1,799.630
Mwanza - Simiyu brd (Urgent repairs) 1.00 600.000
Mwanza - Shinyanga bdr 6.30 1,200.000
Subtotal 15.30 3,599.630
204
NJOMBE
TANZAM 5.07 600.000
Lukumburu-Makambako 5.00 1,100.000
Itoni-Ludewa-Manda (DSD) 1.75 1,050.000
Subtotal 11.82 2,750.000
RUVUMA
Songea -Lukumbulu 2.00 1,122.000
Lumecha - Kitanda (Hanga & Kitanda sections)
2.00 450.000
Songea - Mbinga - Mbambabay 9.00 1,581.276
Subtotal 13.00 3,153.276
SIMIYU
Masanza (Mwz/Simiyu brd) - Simiyu/Mara brd
3.00 450.290
Subtotal 3.00 450.290
SINGIDA
Dodoma Brd - Singida - Tabora Brd 2.00 467.627
Subtotal 2.00 467.627
TABORA
Ipole - Tabora (Isike NBC) 1.00 734.088
Tabora (Isike NBC) - Nzega 0.96 302.860
SGD/Tabora bdr - Nzega 2.40 795.690
Tabora (Isike NBC) - Urambo 0.95 217.710
Subtotal 5.31 2,050.348
Grand total 258.80 49,576.59
205
(b) Barabara Kuu za Changarawe/Udongo
Region Road name Length (km) Estimate (mio Tshs)
ARUSHA
Singida/Arusha brd (Matala) - Njia Panda 42.50 437.520
Subtotal 42.50 437.520
COAST
Bagamoyo - Msata 1.90 65.430
Subtotal 1.90 65.430
DAR ES SALAAM
Morogoro road (Unpaved service road) 1.50 150.000
New Bagamoyo road (Unpaved service road)
1.50 150.000
Nyerere road (Unpaved service road) 2.00 200.000
Subtotal 5.00 500.00
DODOMA
Dodoma - Bereko(Dom/Many Bdr) 28.37 663.090
Subtotal 28.37 663.090
IRINGA
Mafinga - Mgololo 19.00 436.970
Subtotal 19.00 436.970
KAGERA
Nyakanazi - Kagera/Kigoma Border 10.00 203.000
Bugene - Kasulo 25.00 501.160
Omugakarongo - Murongo 13.00 272.000
Subtotal 48.00 976.160
206
KATAVI
Mpanda - Koga(Tabora Bdr) 39.00 925.000
Lyambalyamfipa - Mpanda 20.00 500.000
Mpanda-Kigoma Bdr 39.00 973.695
Subtotal 98.00 2,398.695
KIGOMA
Katavi/Kigoma border - Kasulu 10.00 200.700
Kidahwe - Kasulu 8.00 160.000
Kasulu - Kibondo 42.00 850.000
Kibondo - Kigoma/ Kagera brd 20.00 400.000
Subtotal 80.00 1,610.700
MANYARA
Bereko - Babati - Minjingu 9.04 101.500
Subtotal 9.04 101.500
MARA
Makutano Juu - Nabi Hill Gate 32.00 596.700
Subtotal 32.00 596.700
MBEYA
Mpemba - Isongole 14.00 286.960
Mbeya - Rungwa 10.00 200.000
Subtotal 24.00 486.960
MOROGORO
Kidatu - Ifakara-Mahenge/Lupiro-Kmpepo-Londo
37.00 750.000
Subtotal 37.00 750.000
NJOMBE
Itoni-Ludewa-Manda 46.50 950.000
Subtotal 46.50 950.000
207
RUKWA
Sumbawanga - Lyambalyamfipa 32.00 628.990
Subtotal 32.00 628.990
RUVUMA
Songea -Mbinga-Mbambabay 20.44 409.670
Londo-Kitanda-Lumecha 7.18 343.770 Likuyufusi-Mkenda 31.50 695.000
Subtotal 59.12 1,448.440 SHINYANGA
Kolandoto -Mwangongo (Simiyu brd) 20.00 400.000
Subtotal 20.00 400.000
SIMIYU
Lamadi-Wigelekelo(Simiyu/Shy Bdr) 20.00 398.600 Mwangongo-Mwanhuzi-Sibiti 20.00 431.560
Subtotal 40.00 830.160
SINGIDA
Rungwa - Itigi - Mkiwa 20.00 381.190
Rungwa (Mby/Sgd bdr) - Rungwa (Sgd/-Tbr bdr)
2.40 36.000
Subtotal 22.40 417.190
TABORA
Ipole - Rungwa (Mbeya Brd) 10.00 108.000
Ipole - Tabora (Isike NBC) 39.36 391.580
Koga (Katavi Brd) - Ipole 16.00 172.800
Chaya - Kigwa - Tabora 18.30 300.780
Urambo-Kaliua-Chagu(Tbr/Kig Bdr) 33.10 371.080
Subtotal 116.76 1,344.240
TOTAL 741.59 15,042.745
GRAND TOTAL 64,619.335
208
KIAMBATISHO NA. 5 (B - 2)
MATENGENEZO MAALUMU (PERIODIC MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14 BARABARA ZA MIKOA (b) Barabara za Mikoa za Lami
Region Road name Length (km) Estimate (Mio Tshs)
ARUSHA
Mbauda - Losinyai 3.00 500.000
Kilala - Nkoaranga 1.00 250.000
Monduri - Engaruka Jct 1.00 100.000
Usa -Oldonyo - Sambu 1.00 200.000
Kijenge - Usa River 2.00 300.000
Subtotal 8.00 1,350.000
COAST
Pugu-Vikumburu 0.80 33.610
Kibiti - Utete - Nyamwage 0.30 100.000
TAMCO - Vikawe - Mapinga 1.00 500.000
Subtotal 2.10 633.610
209
DAR ES SALAAM
Tabata Jct (Mandela rd) - Kinyerezi - Banana 2.40 1,000.000
Ukonga jct - G/Mboto - Chanika (widening) 7.50 1,000.000
Buyuni - Ununio - Boko to bitumen std 2.50 1,250.000
Kigamboni - Kibada - Dsm/Co bdr 1.00 750.000
Goba - Wazo Hill - Tegeta Kibaoni 1.90 632.030
Mbande - Mbagala rangi tatu 1.00 750.000
Mjimwema - Pembamnazi (DSD) 2.00 700.000
Kawe - Lugalo 1.00 300.000
Bunju A - Mbweni - Bunju 2.00 1,400.000
Kongowe-Mjimwema-Kivukoni 5.20 1,000.000
Subtotal 26.50 8,782.030
DODOMA
Chamwino Ikulu Jct - Chamwino Ikulu - Dabalo - Itiso
1.82 119.070
Jamatini R/About - CBE Jct 1.39 437.600
Bahi Road Jct - Dodoma Airport R/About 0.67 168.940
Subtotal 3.88 725.610
GEITA
Nyamirembe - Bwanga 3.60 500.000
Nyankumbu (Geita) - Nyang'hwale (Urban section)
2.00 500.000
Chato Jct - Chato Ginnery 3.60 500.000
Subtotal 9.20 1,500.000
210
IRINGA
Iringa - Idete 1.50 882.040
Iringa - Pagawa 0.50 375.000
Subtotal 2.00 1,257.040
KAGERA
Bukoba CRDB - Kabangobay 1.50 358.200
Kyaka 2 - Kanazi - Kyetema 0.13 30.000
Murugarama - Nyakahura 1.00 401.230
Bugene - Nkwenda - Murongo 2 1.00 369.920
Muhutwe - Kamachumu - Muleba 1.35 449.824
Magoti - Makonge - Kanyangereko 0.13 30.000
Subtotal 5.11 1,639.174
KILIMANJARO
Bomang'ombe - Sanyajuu - Kamwanga - Tarakea
6.19 1,230.880
Mwanga - Kikweni - Vuchama 3.00 900.000
KMT - Machame 6.56 1,050.250
Subtotal 15.75 3,181.130
LINDI
Kilwa Masoko - Nangurukuru - Liwale 2.88 216.440
Liwale - Nachingwea - Lukuledi (Lindi/Mtwara Bdr)
2.55 184.450
Subtotal 5.43 400.890
MANYARA
Singe - Sukuro Jct 1.00 900.000
Kiru Jct - Mbulu 1.00 900.000
Subtotal 2.00 1,800.000
211
MARA
Tarime - Nyamwaga (Rebu - Kibumayi) 0.48 390.000
Buhemba Jct - Tarime Hill 0.70 535.300
Musoma - Makojo 0.90 683.800
Mika - Ruari Port 0.10 86.000
Musoma Urban Roads (Makoko) 0.80 570.000
Subtotal 2.98 2,265.100
MBEYA
Mbalizi - Makongolosi 1.51 289.670
Igawa - Mbarali 0.34 150.000
Kyimo - Ibungu 0.45 200.000
Subtotal 2.30 639.670
MOROGORO
Mahenge - Mwaya - Ilonga 1.70 381.150
Bigwa - Kisaki 3.10 693.000
Subtotal 4.80 1,074.150
MTWARA
Lukuledi - Masasi - Newala 4.00 300.000
Mtama - Mkwiti - Newala 2.00 600.000
Mangamba - Msimbati (Mtawanya Hill) 1.00 400.000
Msangamkuu Ferry Acess road 0.60 300.000
Newala Urban section 1.00 500.000
Mbuyuni - Newala 1.00 100.000
Newala - Mtwara 2.50 403.810
Subtotal 12.10 2,603.810
212
MWANZA
Rugezi-Nansio-Bukongo-Masonga 1.50 176.040
Magu - Ndagalu(Magu Town) 1.80 1,000.000
Misungwi Town( Divesion) 0.32 250.000
Subtotal 3.62 1,426.04
NJOMBE
Njombe - Iyayi 2.00 1,200.000
Subtotal 2.00 1,200.000
SHINYANGA
Shinyanga - Bubiki 6.00 995.610
Subtotal 6.00 995.610
SIMIYU
Bariadi - Kisesa (Urban section) 1.00 400.000
Bariadi - Salama (Urban section) 1.00 400.000
Subtotal 2.00 800.000
SINGIDA
Misigiri - Kiomboi DBST 2.00 500.000
Njuki - Ilongero - Ngamu 3.71 900.000
Gumanga - Sibiti 2.00 600.000
Iyumbu-Mgungira-Mtunduru-Magereza 3.00 900.000
Subtotal 10.71 2,900.000
TABORA
Tabora - Mambali 2.00 610.140
Tabora - Ulyankulu 2.00 550.140
Kasu - Airport 1.34 320.000
Subtotal 5.34 1,480.280
TOTAL 131.82 36,654.144
213
(c) Barabara za Mikoa za Changarawe/Udongo
Region Road name Length (km) Estimate (mio Tshs)
ARUSHA
Monduli - Engaruka Jct 16.00 300.850
Mto wa Mbu - Loliondo 40.00 704.000 T/Packers - Losinyai 19.50 353.640
Mbauda - Losinyai 16.50 303.850 Tengeru - Mererani 11.00 200.000
Kijenge - Usa River 11.00 200.000
Longindo - Oldonyolengai Jnct 5.50 150.000 KIA-Majengo 8.00 47.500
Usa river - Oldonyosambu 16.50 300.000 Longido - Siha 42.00 490.000
Engusero - Kitumbeine Jct 8.00 100.000
Karatu - Kilimapunda 16.50 300.000
Monduli Jct - Lolkisale 8.00 150.000
Subtotal 218.50 3,599.840 COAST
Mbwewe - Lukigura bridge 7.00 150.000
Mbuyuni-Saadani-Makurunge 7.00 150.000
Mandera-Saadani 11.00 224.570
Chalinze - Magindu 3.50 71.705
Makofia - Mlandizi - Maneromango
20.00 352.220
Kiluvya - Mpuyani 4.00 80.000
Pugu - Vikumburu 14.00 288.665
214
Mkuranga - Kisiju 18.00 271.590
Bungu - Nyamisati 3.00 80.000
Kibiti - Utete - Nyamwage 8.00 160.000
Kilindoni - Utende - Rasmkumbi 6.00 100.000
Kilindoni - Utende 1.10 6.600
Vikumburu - Mloka - Mkongo - Ikwiriri
- 100.000
Ubena Jct - Lugoba 1.00 35.000
Tamco - Vikawe - Mapinga 2.00 80.000
Subtotal 105.60 2,150.350
DSM
Kibamba - Kwembe - Makondeko 2.22 63.330
Victoria - Magoe Mpiji - Bunju 10.00 270.000
Mbezi -M/Mawili - Kinyerezi 10.23 291.770
Makabe Jct - M/Msakuzi 2.00 57.020
Goba - Wazo hill - Tegeta kibaoni 5.00 142.500
Mbezi Mwisho - Samaki wabichi 2.67 76.130
Temboni - Matosa - Goba 2.00 57.020
Chanika - Mbagala rangi tatu 7.20 220.370
Mjimwema - Pembamnazi 7.25 206.480
Kibada - T/Songani - C/Boarder 20.92 293.710
Pugu - Kajiungeni - Kiltex 6.72 146.620
Kimbiji Mwasonga jct - Kimbiji 1.00 28.000
Tundwi Songani - Buyuni II 4.00 73.970 Kibamba-Magoe-Mpiji 8.83 161.720
Kimara Baruti - Changanyikeni Jct 4.40 80.000
Subtotal 94.44 2,168.640
215
DODOMA
Mtiriangwi-Gisambalan-Kondoa 15.95 348.000
Hogoro Jct- Dosidosi 15.00 327.000
Mpwapwa-Gulwe-Kibakwe-
Chipogoro
20.13 390.395
Ihumwa - Hombolo - Mayamaya 15.57 340.395
Kibaigwa-Ngomai-Njoge - Dongo 14.57 318.000
Mpwapwa-Makutano Jct-Lumuma 14.57 318.000
Chali Igongo (Sgd/Dom Bdr) -
Chidilo Jct - Bihawana Jct
5.00 109.000
Subtotal 100.79 2,150.790
GEITA
Nyankanga (Kagera/Geita Bdr) -
Nyamirembe Port
18.00 354.000
Mtakuja - Bukoli - Buyange
(Geita/Shy Bdr)
17.00 354.000
Wingi 3 (Mwz/Geita Bdr) -
Nyang'holongo (Geita/Shy Bdr)
21.00 421.000
Chato - Chato Ginery - Bwina 5.00 100.000
Nyankumbu - Nyang'hwale 19.00 398.000
Geita (Nzera Jct) - Nzera 8.00 176.000
Chibingo-Bukondo Port 6.00 111.000
Katoro - Ushirombo 23.00 453.500
Subtotal 117.00 2,367.500
216
IRINGA
Iringa - Msembe 8.00 176.000
Iringa - Pawaga 8.00 176.000
Ilula-Kilolo 10.00 216.000
Iringa - Idete 10.00 220.000
Nyololo - Kibaoni 7.00 150.000
Igowole - Kasanga - Nyigo 6.00 132.000
Ihemi - Ihimbo 2.00 44.000
Ihawaga - Mgololo 8.00 172.000
Kinyanambo - Sadani - Mbeya BRD
5.00 110.000
Mbalamaziwa - Kwatwangwa 5.00 110.000
Kinyanambo C - Kisusa 10.00 216.000
Subtotal 79.00 1,722.000
KAGERA
Bugene - Nkwenda - Kaisho - Murongo 2
33.10 350.000
Kakunyu - Kagera Sugar Jct 2.00 40.600
Kyaka - 2 - Kanazi - Kyetema 4.90 100.000
Kamkumbwa - Nagetageta 1.50 30.000
Rusumo Custom-Ngara 3.40 70.000
Busimbe - Kagemu Kituoni 0.50 10.000
Kasharunga - Ngote - Kasindaga 4.90 100.000
Amushenye - Ruzinga 10.00 200.000
Muhutwe-Kamachumu-Muleba 13.30 269.180
Magoti - Makonge - Kanyangereko
1.90 38.670
Rutenge - Rubale - Kishoju 4.90 100.000
Mwogo-Makonge-Ruhija 1.00 20.300
Murugarama-Rulenge-Nyakahura 15.00 204.500
217
Kabindi - Nyankatara 7.40 150.000
Katoma - Bukwari 2.50 50.000
Rulenge - Murusagamba - Kumubuga 4.90 100.000
Subtotal 111.20 1,833.250
KATAVI
Sitalike - Kibaoni - Kasansa 23.00 417.658
Majimoto - Inyonga 14.50 270.000
Kagwira-Karema 18.50 370.000
Subtotal 56.00 1,057.658
KIGOMA
Biharamuro Bdr - Nyaronga 3.17 48.534
Mabamba Jct - Mabamba 3.97 58.700
Simbo - Ilagala - Kalya 38.00 778.356
Kasulu - Manyovu 7.98 153.500
Kisili-Mahembe-Buhigwe 5.00 150.440
Subtotal 58.12 1,189.530
KILIMANJARO
Sanya juu - Kamwanga 10.73 86.360
Mwanga-Kikweni-Vuchama 12.00 269.520
Mwembe-Ndungu 12.00 246.262
Gunge Bridge - Hedaru 6.17 117.870
Same - Kisiwani- Mkomazi 8.00 173.760
Kwa Sadala - Kware - Lemira 4.00 66.237 Kibosho Road Jct - Mto Sere 2.00 33.119
Kawawa - Nduoni 5.00 112.300
Kifaru - Butu - Kichwa cha Ng'ombe 7.77 128.410
Kisangara - Nyumba ya Mungu 5.00 112.300
Bangalala - Ndolwa 8.00 141.158 Kikweni - Lomwe 8.72 195.810
Subtotal 89.39 1,683.106
218
LINDI
Tingi - Chumo - Kipatimu 5.79 98.380
Kilwa - Nangurukuru - Liwale 73.22 1,126.960
Nachingwea - Nanganga 10.00 224.640
Nachingwea - Mtua - Kilimarondo 14.00 169.820
Liwale - Nachingwea - Lukuledi 53.80 927.630
Matangini - Chiola - Likunja 2.00 33.080
Ngongo - Ruangwa 27.02 371.580
Mikao - Nyangamara - Mtama 10.79 51.300
Chekereni - Likwachu 0.17 2.810
Kiranjeranje - Nanjirinji - Namichiga 19.40 300.000
Subtotal 216.19 3,306.200
MANYARA
Kilimapunda - Kidarafa 4.00 89.860
Singe - Kimotorok - Sukuro Jct 25.00 500.000
Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu 9.50 214.500
Kiru Jct - Mahakamani 42.43 290.276
Mirerani - Landanai - Orkesumet 42.05 377.039
Kibaya - Olboloti 9.51 213.610
Losinyai-Njoro 17.60 400.000
Dareda - Dongobesh 15.82 355.270
Mogitu - Haydom 20.25 449.174 Subtotal 186.16 2,889.729
MARA Shirati - Kubiterere 6.00 54.000
Mika - Ruari port 3.00 114.680
Tarime - Nata (Mbise) 20.00 369.020
Sirori Simba - Majimoto- Mto Mara 5.00 90.000 Nyankanga - Rung'abure 12.00 254.000
219
Musoma - Makojo 39.80 718.956
Manyamanyama - Nyambui 3.00 54.000
Nyamuswa - Kisorya 6.00 134.780
Kuruya - Utegi 3.00 54.000
Muriba Jct - Kegonga 5.00 90.000
Mugumu - Fort Ikoma 3.00 67.390
Balili - Manchimwelu 6.00 82.000
Subtotal 111.80 2,082.826
MBEYA
Katumba - Lutengano - Kyimbila 7.03 145.670
Ipyana-Katumba Songwe 6.12 137.480
Igamba - Msangano - Utambalila 8.91 192.760
Kyimo - Ibungu 5.00 112.320
Tukuyu Mbambo-Ipinda 9.04 202.960
Shigamba - Ibaba 9.40 201.330
Muungano - Lubele (Kasumulu) 14.93 246.950
Isyonje-Kikondo 4.27 95.990
Mlowo-Kamsamba 13.00 262.320
Mbalizi - Makongorosi 10.00 200.000
Galula - Namkukwe 6.00 120.000
Igurusi - Utengule - Luhanga 2.00 40.000 Zelazela-Isansa-Itaka 5.00 112.320
Ndembo - Ngana - Kasumulu 3.00 60.000
Katumba-Lwangwa-Mbambo 4.45 100.050
Mahenje - Hansamba - Vwawa 5.00 112.320
Vensi - Maseshe - Mswiswi 31.00 238.850 Kikusya - Ipinda - Matema 11.48 245.610
Hasamba - Izilya - Itumba 15.04 322.960 Subtotal 170.67 3,149.890
220
MOROGORO
Miyombo - Lumuma - Kidete 7.70 158.204
Mvomero-Kibati-Lusanga 17.00 350.950
Chazuru Jct-Melela 14.50 313.030
Bigwa-Kisaki 16.00 350.976
Ifakara-Taweta - Madeke 11.00 250.000
Subtotal 66.20 1,423.160
MTWARA
Lukuledi - Masasi - Newala 18.00 404.360
Newala - Mtwara 30.00 684.590
Madimba - Tangazo - Kilambo 20.00 400.000
Mpapura - Makao 15.00 300.000
Mangamba - Msimbati 2.40 61.050
Subtotal 85.40 1,850.000
MWANZA
Rugezi - Nansio - Bukongo - Masonga 3.00 63.504
Bukonyo - M/tunguru - Bulamba -Bukongo 3.00 63.504
Nyang'hwale Jct- Wingi 3 (Mwanza/Geita Bdr)
4.00 84.672
Magu - Ndagalu (Mwanza/Simiyu Bdr) 6.00 127.000
Fulo - Nyambiti 4.00 84.672
Nyakato - Buswelu 18.00 450.000
Bukwimba - Kadashi - Maligisu (Mwanza/Simiyu Bdr)
2.95 63.504
Ng'hwamhaya - Kawekamo - Itongoitale (Mz/Shy Bdr)
3.00 63.504
Ngudu - Malya (Mwanza/Shinyanga border)
3.00 72.960
Mwanangwa - Misasi - Salawe (Mwanza/Shy bdr)
10.00 211.680
Subtotal 56.95 1,285.000
221
NJOMBE
Kikondo-Makete 14.00 325.000
Makete-Njombe 13.50 325.000
Ndulamo-Nkenja-Kitulo 7.50 150.000
Njombe(Ramadhan)-Iyayi 15.00 300.000
Kibena-Lupembe 18.70 187.000
Mkiwu-Lugarawa-Madaba 6.20 124.144
Ikonda-Lupila-Malangali 19.00 450.000
Subtotal 93.90 1,861.144
RUKWA
Kizwite - Mkima 37.24 618.080
Mtowisa - Ilemba 18.00 521.160
Kaengesa - Mwimbi 4.12 39.010
Laela - Mwimbi - Kizombwe 2.00 28.940
Lyazumbi - Kabwe 50.74 482.190
Chala - Nanyere - Kirando 2.80 259.400
Mtimbwa - Ntalamila 7.00 49.740
Kaoze - Kilyamatundu 5.00 72.350
Subtotal 126.90 2,070.870
RUVUMA
Mbambabay - Liuli - Lituhi 27.60 605.912
Tunduru - Nalasi/Chamba 7.00 158.760
Peramiho - Litumbandyosi - Kingole
23.00 403.652
Namtumbo - Likuyu road 8.00 181.440
Azimio - Tulingane 9.20 201.462 Nangombo - Chiwindi 5.50 115.890
Mbinga - Tangapachani - Mkiri 7.50 713.400
Unyoni - Liparamba - Mkenda 22.00 400.560
Mindu - Nachingwea 34.00 163.200
Naikesi - Mtonya 36.00 384.040 Subtotal 179.80 3,328.316
222
SHINYANGA
Buyange - Busoka 20.00 423.468
Shinyanga-Bubiki 9.34 191.827
Kahama-Bulige-Solwa 2.99 13.392
Nyandekwa jct - Nyandekwa - Butibu 10.00 171.543
Salawe (Mza/Shy bdr) - Old Shinyanga 8.00 172.751
Kishapu-Businza 6.00 116.164
Kahama-Chambo 5.00 105.840
Kanawa - Mihama 0.87 18.501
Kagongwa - Bukooba (Shy/Tbr bdr) 10.00 211.680
Itongoitale(Mz brd) - Mwapalalu 1.50 30.000
Masabi - Mega 6.08 128.680
Kanawa jct - Manonga river (Tbr/Shy bdr) 5.07 79.063
Subtotal 84.85 1,662.909
SIMIYU
Bariadi (Butiama) - Kisesa (Bariadi/Meatu
Bdr)
12.76 275.510
Maswa - Lalago 10.00 210.590
Bariadi - Salama (Bariadi/Magu Bdr) 9.56 128.850
Malya - Malampaka - Ikungu 22.56 437.190
Subtotal 54.88 1,052.140
223
SINGIDA
Kizaga - Sepuka - Mlandala - Mgungira 17.00 194.240
Iguguno Shamba - Nduguti - Gumanga 6.00 106.290
Ikungi - Londoni - Kilimatinde 10.00 160.000
Heka - Sasilo - Iluma 5.00 71.680
Manyoni - Heka - Sanza - Chali Igongo 15.00 270.000
Ulemo - Gumanga - Sibiti 4.00 60.000
Soweto - Kisiriri - Chemchem 5.00 80.000
Shelui - Sekenke 15.00 300.000
Ilongero - Mtinko - Ndunguti 13.00 150.000
Njuki - Ilongero - Ngamu 15.00 315.000
Kinyamshindo - Kititimo 10.00 160.000
Iyumbu - Mgungira - Mtunduru - Magereza 5.00 81.350
Mkalama - Mwangeza - Kidarafa 5.00 80.000
Subtotal 125.00 2,028.560
TABORA
Tabora - Ulyankulu 11.00 137.600
Mambali-Bukumbi 9.00 100.000
Tabora-Mambali 18.52 200.040
Mambali-Bukene 17.96 329.150
Sikonge - Mibono 10.00 200.000
Ugala - Kaliua 10.00 200.000 Igurubi-Iborogero 14.26 167.700
Puge-Ziba 28.94 273.360
Kahama border - Nzega 12.00 140.400
Subtotal 131.68 1,748.250
224
TANGA
Malindi - Mtae 3.00 67.847
Boza jct - Muheza 14.26 322.411
Silabu - Dindira 17.00 407.295
Tanga - Pangani - Buyuni 9.98 225.796
Mkalamo Jct - Mkata 25.00 510.096
Nyasa - Magamba 10.00 197.728
Pangani - Mkalamo Jct 4.00 89.085
Muheza - Amani 10.00 170.364
Lushoto - Umba Jct 7.87 177.986
Nkelei - Lukozi 6.00 135.695
Muheza-Kwa Mkoro 14.11 319.109
Kiberashi(Manyara/Tanga Bdr)-Handeni 20.00 452.316
Vibaoni-Mziha 7.00 158.311
Umba jct - Mkomazi jct 10.00 226.158
Mbaramo-Maramba-Kwasongoro 10.00 226.158
Subtotal 168.22 3,686.354
TOTAL 2,888.64 53,348.012
GRAND TOTAL 90,002.156
225
KIAMBATISHO NA.5 (C - 1)
MATENGENEZO YA SEHEMU KOROFI (SPOT IMPROVEMENT) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA
BARABARA KWA MWAKA 2013/14 5 - BARABARA KUU
Barabara Kuu za Lami na Changarawe/Udongo
REGION PAVED UNPAVED Road Name Target
Length (Km) Amount (TShs mio.)
Road Name Target Length (Km)
Amount (TShs mio.)
Coast
Kongowe - Kibiti - Nyamwage
1.00 349.690
Chalinze - Manga 1.00 750.000
Sub total 2.00 1,099.690
DSM
New Bagamoyo 1.00 150.000
Mandela 0.20 97.610 Sam Nijoma 0.30 21.200
Sub total 1.50 268.810 - -
Dodoma
- - Dodoma - Bereko
1.81 32.550
Sub total - - 1.81 32.550 Geita
Bwanga - Katoro - Ibanda (Mz brd)
2.00 256.000
Sub total 2.00 256.000 Katavi
Mpanda - Tabora Border
0.50 8.500
Mpanda - Kigoma border
0.50 8.500
Sub total - - 1.00 17.000
226
Kigoma
Katavi brd - Kasulu
2.70 50.020
Kasulu - Kibondo
2.79 51.540
Kibondo - Kagera brd
2.48 43.800
Kasulu - Mwanga - Kigoma
5.61 145.890
Sub total - - 3.58 291.250
Lindi
Mtengu - Mingoyo - Mkungu
1.63 141.620
Malendegu - Nangurukuru
0.62 53.050
Sub total 2.25 194.670 - - Manyara
Bereko - Babati - Minjigu
3.60 53.500
Sub total - - 3.60 53.500 Mara
- - Makutano Juu - Nabi Hill
0.93 193.000
Sub total - - 0.93 193.000 Mbeya
Mbeya - Rungwa (Singida Border)
0.90 12.750
Mpemba - Isongole
0.02 0.200
Sub total - - 0.92 12.950
227
Mtwara
Mtwara-Mtegu 6.00 395.645
Sub total 6.00 395.645 - -
Mwanza
Mwanza - Shinyanga border
0.65 67.820
Sub total 0.65 67.820 - -
Rukwa Sumbawanga - Kasesya
2.80 41.000
Sumbawanga - Lyamba Lya Mfipa
0.10 1.000
Sub total - - 2.90 42.000 Ruvuma
Lumesule - Songea 11.80 183.567 Songea - Mbinga - Mbamba Bay
19.78 313.120
Likuyufusi - Mkenda
0.06 51.240
Sub total 11.80 183.567 19.84 364.360 Singida
Dodoma Brd - Singida - Tbr Brd
2.00 400.000 Rungwa - Rungwa (Sgd/ tbr bdr)
0.30 4.500
Rungwa - Itigi - Mkiwa
6.60 118.030
Sub total 2.00 400.000 6.90 122.530
228
Tabora
Tabora - Nzega 4.83 79.480
Ipole - Tabora (Isike NBC)
1.53 26.400
Koga - Ipole 5.93 87.750
Urambo - Kaliua - Chagu
1.67 25.950
Sub total - - 13.96 219.580
TOTAL 26.20 2,866.200 65.44 1,348.720
TOTAL (PAVED + UNPAVED) 4,214.920
229
KIAMBATISHO NA. 5 (C - 2)
MATENGENEZO YA SEHEMU KOROFI (SPOT IMPROVEMENT) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14 BARABARA ZA MIKOA Barabara za Mkoa za Lami na Changarawe/Udongo
REGION PAVED UNPAVED
Road Name Target Length (Km)
Amount (TShs mio.)
Road Name Target Length (Km)
Amount (TShs mio.)
Arusha
Majengo (Mererani) - KIA 2.00 44.967
Engusero - Kitumbeine 2.40 44.980
Sub Total - - 4.40 89.947
Coast
Mbuyuni - Saadani - Makurunge
2.20 53.200
Makofia - Mlandizi - Maneromango
2.10 28.730
Kiluvya - Mpuyani 0.40 6.880 Pugu - Vikumburu 1.00 15.570
Mkuranga - Kisiju 1.00 14.250
Mbwewe - Lukigura Bridge 1.90 28.750
Kilindoni - Utende - Rasmkumbi
0.80 8.720
Bungu - Nyamisati 0.70 8.500
Ubena Jct - Lugoba 1.30 17.640
Mwanambaya - Hoyoyo 0.20 2.250
Kilindoni - Utende 0.20 4.000
Kibiti -Uutete - Nyamwage 0.80 11.560
Sub Total - - 12.60 200.050
230
DSM
Chanika - Mbagala Rangi Tatu
2.00 300.000 Makabe Jct - Mbezi Msakuzi
2.07 38.600
Boko - Kunduchi - Mbuyuni
0.50 250.000 Mbezi Victoria - Bunju Sport Motel
1.40 26.280
Morocco - Mlalakuwa - Africana
1.00 150.000 Kibamba - Kwembe - Makondeko
1.10 21.220
Veta/Changombe - Morrocco
0.50 150.000 Goba - Tegeta Kibaoni 1.00 20.000
Mbezi Mwisho - S/Wabichi 0.20 20.000
Mbezi Mwisho - Kinyerezi 2.00 50.000
Temboni - Goba 1.00 20.000
Chanika - Mbagala Rangi Tatu
2.50 43.500
Mji Mwema - Pemba Mnazi 2.56 38.400
Kigamboni - Kibada -T/Songani
1.58 29.160
Kimbiji Mwasonga Jct - Kimbiji
0.45 10.000
Buyuni II - Tundimwisongani 0.50 10.000
231
Kimara Baruti Jct - Changanyikeni Jct
1.00 20.000
Kimbiji/Songani Jct - K/Mwasonga Jct
0.70 12.500
Kifuru - Pugu Station (Mnadani)
6.00 18.000
Kimara Mwisho - Kinyerezi 6.80 30.000
Kawe - TPDF Firing Range - Jangwani
5.20 15.600
Korogwe - Kilungule - External
8.80 26.400
Mlimani City - Ardhi - Makongo - Goba
7.00 21.000
Kigogo Round about - Jangwani
1.90 40.000
Ununio - Mpigi Bridge 15.70 47.130
Tabata Dampo - Kigogo 1.70 35.000
Temeke - Mtoni Mtongani 3.40 30.000
Buza - Kilungule - Nzasa 9.00 27.000
Kawawa/Nyerere Jct - Changombe Police (Chang'ombe Road)
3.00 10.000
Taifa Road 1.20 10.000
232
Mgulani Road (DUCE - Mgulani JKT
1.40 10.000
Kinondoni Road (Kinondoni - Ally Hassanimwinyi Jct)
1.50 10.000
Shaurimoyo Road (Karume - Bohari)
0.70 10.000
DSM - Buguruni (Uhuru Road )
5.30 750.000
Sub Total 4.00 850.000 96.66 1,449.79
Dodoma
Pandambili - Mlali - Suguta - Mpwapwa
4.87 93.300
Hogoro Jct - Dosidosi 2.52 48.300
Ihumwa - Hombolo - Mayamaya
0.65 9.800
Mpwapwa - Gulwe - Kibakwe
6.38 116.400
Mpwapwa - Makutano Jct - Pwaga Ict - Lumuma
5.05 98.800
Olbolot - Dalai - Kolo 12.52 226.250
Chenene - Izava 0.33 4.550
Zamahero - Kinyamshindo 7.99 131.450
Chali Igongo - Chidilio - Bihawana Jct
1.54 31.450
Chamwino - Ikulu - Dabilo - Itiso
0.10 2.000
Sub Total - - 41.95 762.300
233
Geita
Nyamirembe - Bwanga
1.00 74.000 Mtakuja - Bukoli - Bunyange 8.00 130.000
Wingi 3 (Mwz brd - Nhang'holongo(Shy brd)
10.00 220.000
Nyankumbu - Nyang'hwale 4.00 80.000
Katoro - Ushirombo 8.00 130.000
Sub Total 1.00 74.000 30.00 560.000
Iringa
Ihawaga - Mgololo 5.00 110.000
Iringa - Msembe 1.00 500.000
Kinyanambo c - Kisusa 5.00 110.000
Ilula - Kilolo 5.00 110.000
Sub Total - - 16.00 830.000
Katavi
Magamba - Mtisi 0.30 4.500
Ifukutwa - Lugonesi 1.73 29.450
Kawajense - Mnyamasi Jct 9.70 130.500
Majimoto - Inyonga 2.10 44.500
Sub Total - - 13.83 208.950
Kigoma
Kisili - Mahembe - Buhigwe 3.38 53.500
Ngara brd - Nyaronga - Kakonko
1.65 24.000
Rusesa - Kazuramimba 25.18 75.540
Mugunzu - Kakonko 56.23 168.690
234
Kasulu - Manyovu 5.30 90.100
Nyaronga - Biharamulo Brd 1.41 26.100
Simbo - Ilagala - Kalya 7.93 129.790
Sub Total - - 101.08 567.720
Kilimanjaro
Sanyajuu - Kamwanga 1.50 33.750
Tingatinga - Nyumbamoja 15.34 46.020
Kawawa - Nduoni 0.30 12.000
Sub Total 17.14 91.770
Lindi
Kilwa Masoko - Nangurukuru - Liwale
0.10 1.200
Liwale - Nachingwea 0.40 5.500
Nachingwea - Nanganga 0.30 4.500
Ngongo - Ruangwa - Ruangwa
0.40 6.000
Sub Total - - 1.20 17.200
Manyara
Kilimapunda - Kidarafa 11.48 136.600
Losinyai - Njoro 22.25 351.784
Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu
2.55 34.000
Lolkisale - Sukuro 4.26 91.850
Dareda - Dongobesh 4.85 63.330
235
Magidu - Haydom 2.83 36.200
Kiru Jct - Mbulu
Mahakamani
0.49 7.200
Singe - Sukuro Jct 6.72 84.020
Mirerani - Landanai -
Orkesumet
2.50 39.730
Kibaya - Dosidosi 3.20 50.250
Kibaya - Kibirashi 6.39 101.700
Orkusmet - Gunge 20.07 300.700
Cairo - Mererani 0.05 0.500
Kimotorok - Ngopito 1.94 24.800
Kijungu - Sunya - Dongo 15.08 230.800
Kibaya - Olboloti 1.33 20.550
Sub Total - 105.99 1,574.014
Mara
Nyamuswa - Bunda -
Kisorya
5.00 106.640
Sub Total - - 5.00 106.640
236
Mbeya
Mbalizi - Makongolosi 10.99 139.510
Igawa - Mbarali 0.50 5.860
Mlowo - Kamsamba (Rukwa bdr)
0.65 9.000
Mbalizi - Shigamba - Isongole
0.74 3.000
Mahenje - Hansamba - Vwawa
1.15 12.250
Kikusya - Ipinda - Matema 2.75 32.000
Masebe - Kyejo 1.05 15.250
Zelezeta - Isansa - Itaka 2.88 35.800
Bujesi - Itete 0.10 1.000
Iseche - Ikonya 0.55 5.750
Isansa - Itumpi 0.30 4.000
Ruanda - Nyimbili 0.10 1.000
Majombe(Madibira Jct) - Mbarali/Mufindi Brd
0.60 18.750
Isongole II - Isoko 0.10 1.500
Malenje - Lungwa 0.05 0.500
Isonje - Kikondo 0.28 3.850
Sub Total - - 22.79 289.020
237
Morogoro
Mziha - Magole 3.30 61.750
Mvomero - Ndole - Kibati - Lusanga
8.60 167.750
Dumila - Kilosa - Mikumi 10.60 222.140
Chanzuru Jct - Melela 6.00 115.000
Miyombo - Lumuma - Kidete 5.50 108.020
Ifakara - Taweta - Madeke 6.60 113.700
Kiswira - Tawa 0.30 4.950
Mtombozi - Lugenzi - Dutumi
5.00 100.000
Mahenge - Mwaya - Ilonga 3.60 57.750
Madamu - Kinole 0.20 3.000
Sub Total - - 49.70 954.060
Mtwara
Newala - Tandahimba - Mtwara
3.38 50.700
Mbuyuni - Newala 0.80 14.500
Mkwiti - Kitangari - Amkeni 8.65 173.500
Matipa - Kitama 4.20 73.000
Mpapura - Mikao - Kinolombedo
5.70 99.000
Msijute - Nanyamba 5.10 98.000
238
Lukuledi - Masasi - Newala 5.86 90.340
Madimba - Tangazo - Namikupa
0.90 15.550
Magamba - Msimbati 1.40 21.000
Sub Total - - 35.99 635.590
Mwanza
Mwanza - Airport
0.18 15.030 Ngudu - Nyamilama - Hungumalwa
10.00 196.920
Sub Total 0.18 15.030 10.00 196.920
Njombe
Kitulo - Matamba - Mfumbi 8.01 111.400
Kandamija - Kipingu 0.50 6.030
Kikondo - Njombe 14.30 252.450
Madeke - Lupembe( Morogoro border)
14.50 290.000
Ludewa - Lupingu 20.00 400.000
Njombe (Ramadhan) - Iyayi 4.69 94.650
Kibena - Lupembe 3.24 46.250
Mkiwu - Lugarawa - Madaba(Songea brd)
4.49 61.350
Ibumila - Mlevela 0.63 10.400
Ilunda - Igongolo 1.00 15.250
Chalowe - Igwachanya 0.65 13.000
Mlangali - Ikonda 4.30 92.650
Ndulamo - Kitulo 6.24 129.900
Sub Total - - 82.55 1,523.330
239
Rukwa
Mtowisa - Ilemba 3.65 64.700
Ilemba - Kaoze 1.07 5.550
Kaoze - Kilyamatundu 0.05 0.500
Lyazumbi - Kabwe 2.25 38.250
Chala - Nanyere - Kirando 2.80 60.500
Ntendo - Muze 0.35 3.500
Mtimbwa - Ntalamila 0.80 12.000
Sub Total - - 10.97 185.000
Ruvuma
Mtwarapachani-Lingusenguse-Nalasi.
16.13 264.940
Tunduru-Nalasi-Chamba 0.20 3.000
Azimio-Tulingane 0.20 4.000
Sub Total - - 16.53 271.940
Shinyanga
Shinyanga - Bubiki 0.40 7.500
Buyange [Mza/Shy Border - Busoka
3.23 51.500
Nyandekwa Jct - Nyandekwa - Butibu
0.70 10.500
Kanawa Jct - Manonga River [Tbr Bdr]
0.43 7.750
Bulyanhulu Jct - Bulyanhulu Mine
0.95 11.750
Kagongwa-Bukooba [Shy/Tbr Bdr]
0.30 4.500
240
Kahama - Chambo 6.00 150.000
Kahama - Bulige - Solwa 20.00 500.000
Nyandekwa - Uyogo - Ng'hwande
20.00 500.000
Nyambula - Nyang'holongo 7.40 185.000
Sub Total - - 59.41 1,428.50
Simiyu
Nyashimo - Ngasamo - Dutwa
6.46 99.550
Bariadi - Salama 9.14 190.940
Sola Jct - Mwandoya - Sakasaka
8.36 122.960
Malya - Malampaka - Ikungu
2.13 27.390
Mwandete - Kabondo - Mwamanoni
8.17 146.500
Ndagalu (Sukuma) - Kabila - Mahaha
4.00 42.500
Sub Total - - 38.26 629.840
Singida
Kidarafa (Mny/Sgd Brd) - Nkungi
2.00 40.000
Kizaga - Sepuka - Mlandala - Mgungira
2.00 30.000
Iguguno Shamba - Nduguti - Gumanga
2.00 15.000
241
Ilongero -Mtinko - Ndunguti 5.60 80.000
Njuki - Ilongero - Ngamu 6.70 134.000
Sabasaba - Sepuka 2.00 32.750
Iyumbu (Tbr Brd) - Mgungira - Magereza (Sgd)
1.50 15.130
Ikungi - Londoni - Kilimatinde (Solya)
3.00 45.000
Manyoni East - Heka - Sanza - Chali Igongo
3.70 52.810
Sub Total - - 28.50 444.690
Tabora
Tabora - Ulyankulu 11.01 195.950
Mambali - Bukumbi 4.46 68.900
Tabora - Mambali 2.37 41.360
Mambali - Bukene 2.59 45.830
Kaliua - Ulyankulu - Ng'wande
21.62 364.150
Kaliua - Ugala 25.00 500.000
Ziba - Choma 1.04 16.320
Kahama Border - Nzega 5.84 89.280
Sub Total - - 73.93 1,321.790
242
Tanga
Lushoto - Umba Jct 8.58 127.950
Tanga-Mabanda ya Papa-Boza - Buyuni
17.85 278.090
Nkelei - Lukozi 6.47 97.050
Malindi - Mtae 6.81 109.135
Magamba - Mlola 8.20 124.670
Vuga - Vuga Mission 1.70 27.500
Maramba - Kasera 0.10 129.954
Boza Jct - Muheza 1 7.80 124.440
Mlingano Jct - Kiomoni Jct 3.17 43.300
Mkalamo Jct - Mkata 1 2.60 39.000
Bombani - Kimbe 1.35 19.580
Manyara Brd - Handeni - Kilole Jct
16.65 259.795
Umba Jct - Mkomazi Jct 16.73 250.450
Muheza - Bombani - Kwamkoro
4.79 82.970
Vibaoni - Mziha 10.95 163.750
Kwekivu Jct - Iyongwe 4.00 62.320
Sub Total - - 117.75 1,939.954
TOTAL 5.18 939.030 992.23 16,279.010
TOTAL (PAVED + UNPAVED) 17,218.040
243
KIAMBATISHO NA. 5 (D) MATENGENEZO YA KUKINGA MADARAJA (PREVENTIVE MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2013/14 Barabara Kuu (TR) na Barabara za Mikoa (RR)
Estimated Expenditure TShs. ''mio.'' S/N REGION BRIDGES TO GET PREVENTIVE
MTCE ESTIMATED AMOUNT (TShs.) (ROAD FUND)
TOTAL AMOUNT (TShs.)
TR RR TOTAL TR RR
1 Arusha 68 32 100 25.923 57.765 83.688
2 Coast 13 30 43 14.663 21.522 36.185
3 DSM 15 30 45 28.125 17.000 45.125
4 Dodoma 102 168 270 209.147 278.701 487.848
5 Geita 7 35 42 15.090 67.120 82.210
6 Iringa 39 65 104 19.500 38.500 58.000
7 Kagera 155 42 197 71.200 18.220 89.420
8 Katavi 17 34 51 17.000 27.200 44.200
9 Kigoma 88 48 136 85.318 82.412 167.730
10 K’manjaro 25 35 60 90.000 120.000 210.000
11 Lindi 80 30 110 150.000 100.000 250.000
12 Manyara 2 28 30 4.000 56.000 60.000
13 Mara 20 35 55 154.630 144.558 299.188
14 Mbeya 186 190 376 102.300 52.250 154.550
15 Morogoro 75 91 166 75.000 91.000 166.000
16 Mtwara 50 9 59 50.000 30.000 80.000
244
17 Mwanza 4 5 9 30.675 40.150 70.825
18 Njombe 35 35 70 17.500 31.000 48.500
19 Rukwa 11 43 54 11.000 34.400 45.400
20 Ruvuma 30 42 72 27.455 104.950 132.405
21 Shinyanga 8 7 15 37.524 59.027 96.551
22 Simiyu 4 3 7 64.949 45.000 109.949
23 Singida 23 12 35 106.188 27.500 133.688
24 Tabora 125 75 200 60.000 24.000 84.000
25 Tanga 5 17 22 15.000 106.700 121.700
TOTAL 1,187 1,141 2,328 1,482.187 1,674.975 3,157.162
NOTE:- TR – Trunk Road
RR – Regional Roads
245
KIAMBATISHO NA. 5 (E)
MATENGENEZO MAKUBWA YA MADARAJA NA MAKALVATI (BRIDGE MAJOR REPAIR) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA MWAKA WA FEDHA 2013/14 – BARABARA KUU NA ZA MIKOA (d) Barabara Kuu
Estimated Expenditure in TShs. ''mio.''
FY 2013/14 Total Total RF for Region Region Name of Bridge No. of
bridges Roads Fund
Foreign Estimate
Arusha Matala - Njia Panda 2 324.095 - 324.095 324.095
Coast Kibaha - Mlandizi - Ngerengere
1 218.098 218.098 787.098
Kibiti - Ikwiriri - Malendego 1 569.000 - 569.000
DSM Morogoro Road 5 160.000 - 160.000 330.000
Kilwa Road 3 40.000 - 40.000
Nyerere Road 1 10.000 10.000
New Bagamoyo Road 4 80.000 80.000
Mandela Road 3 40.000 - 40.000
Dodoma
Gairo (Morogoro/Ddm Brd) - Dodoma - Kintinku
2 389.712 - 389.712
Dodoma - Bereko ( Dodoma/Manyara Border)
1 80.000 80.000 469.712
Iringa
TANZAM 1 11.050 - 11.050
Mafinga - Mgololo ( Paved) 1 17.100 17.100
Mafinga - Mgololo (Unpaved) 1 50.000 - 50.000 78.150
Kagera Bukoba - Bukoba Port 1 399.250 - 399.250 399.250
246
Katavi Mpanda - Koga (Katavi/Tabora Border)
1 60.000 - 60.000 60.000
Kilimanjaro Same - Himo Jct - KIA Jct 4 350.000 - 350.000 350.000
Mara Sirari Jct-Sirari 1 400.000 - 400.000 400.000
Mbeya Uyole - Ibanda - Kasumullu ( Tz/Malawi Border)
1 103.000 - 103.000 103.000
Morogoro
Tanzam Highway ( Coast/Moro /Iringa Brd
10 156.000 - 156.000 601.000
Morogoro - Gairo(Moro/Dodoma Brd)
10 185.000 - 185.000
Mikumi - Mahenge /Lupiro K/k Mpepo - Londo
6 260.000 - 260.000
Mtwara Mtwara - Mtegu 3 586.744 - 586.744 1,264.004
Mkungu - Masasi 2 377.260 - 377.260
Mangaka - Mtambaswala 1 300.000 - 300.000
Mwanza Mwanza - Simiyu brd (Mabatini pedestrian bridge)
1 300.000 - 300.000
Ibanda (Geita brd)- Usagara - Mwanza - Simiyu Brd
2 78.665 - 78.665 378.665
Njombe Lukumburu-Makambako 2 20.000 - 20.000 122.550
Itoni-Ludewa-Manda 4 102.550 - 102.550
247
Ruvuma
Lumesule-Songea - Lukumburu
5 40.000 - 40.000 50.280
Lukufusi-Mkenda 1 10.280 - 10.280
Simiyu Mwangongo(Shy/Simiyu Border)-Lalago-Mwanhuzi
2 425.500 - 425.500 425.500
Singida Kintinku - (Dod/Sgd brd) - Sdg /Tbr Brd
1 400.000 - 400.000 400.000
Tabora Rungwa (Mbeya Border) - Ipole
1 164.922 - 164.922 164.922
Total 85 6,708.226 - 6,708.226 6,708.226
(b) Barabara za Mikoa
Estimated Expenditure in TShs. ''mio.''
Region Name of Bridge No. of bridges
FY 2013/14 Total Estimate
Total RF for Region Roads
Fund Foreign
Arusha
Usa river - Oldonyo Sambu 1 97.780 - 97.780
393.334
Olkoi II 1 100.000 - 100.000
T/Packers Losinyai 1 97.780 - 97.780
Karatu - Kilimapunda 1 97.774 - 97.774
Coast
Mbuyuni - Saadani - Makurunge
1 150.000 - 150.000
587.951 Kiluvya - Mpuyani 1 200.000 - 200.000
Makofia - Mlandizi - Maneromango
1 237.951 - 237.951
248
DSM Kinyerezi -Majumba Sita Ukonga
1 2,100.000 - 2,100.000 2100.000
Dodoma
Olbolot - Dalai - Kolo 1 80.000 - 80.000
880.000
Pandambili-Mpwapwa-Ngambi
1 80.000 - 80.000
Zamahero - Kwamtoro - Kinyamshindo
1 80.000 - 80.000
Ihumwa - Hombolo - Mayamaya
1 80.000 - 80.000
Mpwapwa - Gulwe-Kibakwe-Chipogolo
1 80.000 - 80.000
Mpwapwa-Makutano Jct-Pwaga Jct-Lumuma
1 80.000 - 80.000
Chamwino Jct-Ikulu Jct - Chamwino - Dabalo -Itiso
1 80.000 - 80.000
Chali Igongo (D/Sg Bd) Chidilo Jct - Bihawana Jct
2 160.000 - 160.000
Kibaigwa-Manyata Jct-Ngomai-Njoge-Dongo (Dodoma Manyara Border)
1 80.000 - 80.000
Mtiriangwi/Gisambalang-Kondoa
1 80.000 - 80.000
249
Geita
Wingi 3 ( Mz/Gt Brd) Nyang'olongo ( Gt/Shy Bdr)
1 70.000 - 70.000 520.000
Nyankumbu - Nyang'hwale 2 170.000 - 170.000
Mtakuja - Bukoli Buyange( Kagera/Geita Border)
2 180.000 180.000
Katoro - Ushirombo 1 100.000 - 100.000
Iringa
Kinyanambo - Sadani - Mbeya Brd
2 23.675 - 23.675
394.250
Iringa - Msembe 1 21.675 21.675
Iringa - Pawaga 3 25.000 - 25.000
Kinyanambo C - Kisusa 1 82.000 - 82.000
Iringa - Idete 1 100.000 100.000
Ihemi - Ihimbo 1 50.000 - 50.000
Mbalamaziwa - Kwatwanga 2 41.900 - 41.900
Ilula - Kilolo 2 50.000 - 50.000
Kagera
Murugarama - Rulenge -Nyakahura
1 35.000 - 35.000 111.550
Rutenge - Rubale - Kishoju 2 76.550 - 76.550
Katavi
Majimoto - Inyonga 13 648.000 - 648.000
953.375
Sitalike - Kibaoni - Kasansa 1 50.375 50.375
Kagwira - Karema 5 175.000 - 175.000
Ugalla-Myamasi 1 80.000 - 80.000
Kigoma Simbo - Ilagala - Kalya 8 1,140.000 - 1,140.000 1140.000
250
Kilimanjaro
Same kwa Mgonja-Makanya
1 250.000 - 250.000
1225.000 Kifaru-Butu-Kichwa cha ng'ombe
1 225.000 225.000
Tarakea Jct - Tarakea Nayemi
1 250.000 - 250.000
Same - Kisiwani - Mkomazi 3 500.000 - 500.000
Lindi Kilwa Masoko - Nangurukuru - Liwale Road
2 149.260 - 149.260 1344.450
Liwale - Nachingwea - Lukuledi ( Lindi /Mtr Brd)
1 90.500 - 90.500
Mtama - Mikao (Lukuledi II bridge)
1 700.000 - 700.000
Ngongo - Ruangwa - Ruangwa Jct
1 70.000 - 70.000
Kiranjeranje - Nanjirinji - Namichiga
1 334.690 - 334.690
Manyara
Kilimapunda - Kidarafa 1 571.000 - 571.000
903.000 Losinyai - Njiro 2 182.000 - 182.000
Kiru Jct - Mahakamani 1 150.000 - 150.000
Mara Mika - Ruari Port 1 100.000 - 100.000 400.000
Sirori Simba - Majimoto - Mto Mara
1 100.000 - 100.000
Nyankanga - Rung'abure 1 100.000 - 100.000
Musoma - Makojo 1 100.000 - 100.000
251
Mbeya
Mbalizi-Makongolosi 1 100.000 - 100.000
Isongole II - Isoko 1 100.000 100.000
Mbalizi-Shigamba-Isongole 1 100.000 - 100.000 300.000
Morogoro
Mvomero - Lusanga 2 40.000 - 40.000 851.000
Kimamba - Rudewa 2 300.000 - 300.000
Sangasanga - Langali 7 210.000 - 210.000
Msomvizi - Mikese 7 301.000 - 301.000
Mtwara
Mkwiti - Kitangari - Amkeni 1 183.325 - 183.325 483.325 Magamba - Mitemaupinde
(Likwamba ) 1 300.000 - 300.000
Mwanagwa -Misasi - Salawe(Mz /Shy Brd)
1 55.257 55.257
Mwanza Ngudu - Malya ( Mz / Shy Brd)
1 140.000 - 140.000 195.257
Njombe Kikondo-Njombe 3 30.327 - 30.327 272.661 Kibena-Lupembe 1 19.514 - 19.514
Mlangali-Ikonda 2 222.820 - 222.820
Rukwa Mtowisa - Ilemba 12 1,670.000 - 1,670.000 1670.000
Ruvuma
Mbambabay -- Lituhi 3 284.000 - 284.000
409.000
Kigonsera - Mbaha 2 10.000 10.000
Namtumbo-Likuyu 1 10.000 10.000
Mtwarapachani - Lingusenguse-Nalasi
4 75.000 75.000
Paradiso - Kingole 1 30.000 - 30.000
252
Shinyanga
Shinyanga - Bubiki 2 475.147 - 475.147 902.816
Kishapu - Buzinza 1 110.000 110.000
Kanawa Jct – ManongaRiver ( Tbr/Shy Brd)
2 317.669 317.669
Simiyu Mwandete-Mwamanoni 1 275.000 275.000 275.000
Singida
Ilongero - Mtinko - Nduguti 1 160.000 - 160.000 1131.189
Kidarafa ( Mnyr/Sgd Brd)- Nkungi
2 350.000 - 350.000
Iguguno - Shamba - Nduguti - Gumanga
1 168.791 - 168.791
Iyumbi (Tbr brd) - Mgungira - Magereza (Sdg )
1 120.000 - 120.000
Njuki - Ilongero - Ngamu 1 60.000 - 60.000
Soweto - Kiomboi - Kisiriri - Chemchem
1 45.000 - 45.000
Ulemo-Gumanga-Sibiti 1 50.000 - 50.000
Kinyamshindo-Kititimo 1 177.398 - 177.398
Tabora
Ugala-Kaliua-Ulyankulu-Ng'wande
2 712.492 - 712.492 982.492
Manonga River (Shinyanga Tabora Border)-Igurubi
1 270.000 270.000
Tanga Kwekivu Jct - Iyongwe 3 1,254.900 - 1,254.910 1254.910
Total 164 19,680.550 - 19,680.550 19,680.560
TRUNK & REGIONAL ROADS BRIDGES: Major repairs FY 2013/14
Target Roads Fund Foreign Total
249.00 26,388.786 - 26,388.786
253
KIAMBATISHO NA. 6
RAMANI ZA MIKOA ZINAZOONYESHA MTANDAO WA BARABARA KUU NA ZA MIKOA