Upload
iam-muslim
View
848
Download
11
Embed Size (px)
Citation preview
Mimi ni
Mwislamu
Authorship
Muhammed Ashraf Salah
������� ���� � ������ : �� ��������� � ������ ����� �!� "#� $ �%�������&�����'
Mimi ni Mwislamu
Kwa jina la Mungu wa RehemaKwa jina la Mungu wa RehemaKwa jina la Mungu wa RehemaKwa jina la Mungu wa Rehema
(�h�g�f�e�d�c� �b�a� �̀_�h�g�f�e�d�c� �b�a� �̀_�h�g�f�e�d�c� �b�a� �̀_�h�g�f�e�d�c� �b�a� �̀_
k�j�ik�j�ik�j�ik�j�i ) * +�,�- ./ :012
Na mtu anataka dini nyingine zaidi ya
Uislamu wala kukubali kuwa wakati ni
mmoja wa wenye kukhasiri Akhera
Al-Imran: 85
Mimi ni Mwislamu
Copyright, distribution and translation are
reserved for every Muslim
Legal Deposit No. 22274 / 2008
International Serial 977-6157-64-5
For charitable distribution call:
0020101459613
For suggestions e-mail:
WWW.Iam-Muslim.com
Mimi ni Mwislamu
(1) KUMWAMINI MWENYEZI MUNGU
Mimi ni Mwislamu…
• Ninamwamini Mwenyezi Mungu Pekee Asiye na mshirika na hakuna mola mwingine isipokuwa Yeye, Hakuzaa wala Hakuzaliwa, na hakuna kamwe kifano chake.
• Ameumba mbingu na ardhi, Naye Ndiye Anayezimiliki. Anayajua yaliyofichikana na yenye kuonekana. Yu Hai na Hafi, Anayasimamia mambo yote milele na Halali.
• Ana Majina Mazuri Kabisa na Sifa za Juu. Kati yake ni Majina tisini na tisa, mwenye kuyajua na kuyadhibiti vyema na akamwomba Mwenyezi Mungu Kwayo, ataingia peponi.
• Kati yake ni Sifa za Upweke, kwani Yeye Subhaanahu wa Taalaa ni Mmoja wa Dhati, Sifa na Vitendo, Aliyepwekeka, Aliye Pekee, Mkusudiwa, Mmiliki wa ufalme.
Mimi ni Mwislamu
• Na Sifa za Utukufu, kwani Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye habari ya kila jambo, Mwelekezaji wa manufaa, Haki, wa Mwanzo, wa Mwisho, wa Dhahiri, wa Siri, Mrithi, Mwenye Kubakia, Mkwasi, Mtakasifu, Mwenye Kushuhudia, Aliye Karibu, Mbora wa Kupangilia, Mwadilifu, Nuru ya mbingu na ardhi, Mwenye Utukufu na Ukarimu.
• Na Sifa za Uadhama, kwani Yeye ni Mshindi Asiyeshindika, Mwenye Sifa zote Tukufu, Mwenye Uadhama, Mwenye Sifa za Utukuzo, Mwenye Kulazimisha, Mwenye Nguvu, Aliye Imara, Mteza nguvu, Mweza, Mwenye uwezo wa juu, Mwingi wa Kunusuru, Aliye Juu, Aliye Juu ya vyote.
• Na Sifa za Uwezo, kwani Yeye ni Mwingi wa Ujuzi, Mwenye Kusikia, Mwenye kuona, Yu Hai,
Mwenye Kukamata, Mwenye Kukunjua, Mwenye Kushusha, Mwenye Kupandisha, Mwenye Kutukuza, Mwenye Kudhalilisha, Mwenye Kutoa, Mwenye Kuzuia, Mwenye Kunufaisha,
Mimi ni Mwislamu
Mwenye Kudhuru, Mwenye Kuhuisha, Mwenye Kufisha, Mwenye Kutanguliza na Mwenye Kuchelewesha.
• Na Sifa za Uumbaji, kwani Yeye ni Muumbaji, Msanifu wa Maumbile, Mtiaji Sura, Hakimpiti au Kumshinda kitu, Mbunifu, Mwenye Kuanzisha, Mwenye Kurejesha, Mwenye Kufufua, Mwenye Kukusanya, Mpaji Mkuu, Mfunguzi wa kila jambo, Mwingi wa Kuruzuku, Mwenye Kutajirisha, Mdhibiti wa idadi, Mwenye Kudhibiti mambo, Mwenye Kuhifadhi, Mlinzi na Muumbaji wa mbingu na ardhi bila ruwaza.
• Sifa za Rehma, kwani Yeye ni Mwingi wa Rehma, Mwingi wa Kurehemu, Mwingi wa Huruma, Mwenye Kuneemesha neema nzuri, Mwingi wa Penzi, Mtenda Wema, Mwingi wa Kughufiria, Mwenye Kusamehe, Mwingi wa Kukubali toba, Mwenye Amani, Mtoaji amani na imani, Mpole, Mwenye Kulipa vyema, Mkarimu, Mwenye Kuneemesha, Mwingi wa Kutoa, Mwenye Kusaidia, Mwenye Kujibu,
Mimi ni Mwislamu
Mkunjufu, Mwingi wa subira, Mvumilivu kwa Waja Wake, Latifu, Wakili, Mwenye Kutoa Misaada, Mwenye Kuombwa msaada na Mwenye Kukubali toba.
• Amemneemesha mwanadamu neema nyingi zisizo na hesabu. Na hakuna neema yoyote anayoneemeka nayo mja ila hutoka kwa Mwenyezi Mungu Pekee, kwani Yeye Ndiye Aliyemuumba na Akampa uhai, Akamfanya asikie na aone, Akamkirimu, kisha Akamruzuku na Akamfanyia wema.
• Kwa ajili hiyo, ni lazima mja amwabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake – nako ni kufuata amri Yake na kuacha makatazo Yake – kwa kuwa hastahiki yeyote kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake.
• Vile vile, bila shaka Mwenyezi Mungu Anazijua hali zote za mja kati ya utiifu
Mimi ni Mwislamu
na uasi. Hivyo basi, ni wajibu moyo wa mja ujae haiba kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, utukuzo na mapenzi, na aone haya kumwasi na aachane na maasi, kwani Mwenyezi Mungu Humwona wakati akiyafanya.
• Anafurahi kwa amali zake njema zinazomkurubisha kwenye radhi za Muumbaji wake Subhaanahuu wa Taala. Hivyo huzidi kufanya amali hizo hadi kufikia ngazi ya ihsani, kwani imani huzidi kwa matendo mema na hupungua kwa maasi.
• Asivutike kwenye matamanio, hawaa au bid'a, bali avutike kwa Mwenyezi Mungu Pekee huku akifuata maamrisho ya Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam. Asitafute kwa amali yake starehe ndogo ya dunia bali atafute kwayo malipo toka kwa Mwenyezi Mungu tu.
• Aidha, hakika Mwenyezi Mungu Ana huruma mno kwa mwanadamu kuliko huruma ya mama kwa mwanaye. Na rehma Yake imekienea kila kitu.
Mimi ni Mwislamu
Hivyo basi, ni wajibu kwa mja amwombe na anyenyekee Kwake katika haja zake za kidunia na za kiakhera, na wala asimwombe yeyote mwingine.
• Kwa vile hakuna faida yoyote ya kumwomba asiye Mwenyezi Mungu, kwa kuwa hamiliki uwezo ulio kamili isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna asikiaye ya siri na minong'ono ila Mwenyezi Mungu, na hakuna anayemiliki makadirio isipokuwa Mwenyezi Mungu, basi kwa maana hiyo, hakuna wa kujibu dua isipokuwa Mwenyezi Mungu.
• Na kwa ajili hiyo, haijuzu kwa Mwislamu kuliomba kaburi, au kumwomba aliyezikwa humo vyovyote awavyo, kwa kuwa yeye hamsikii. Na kama hamsikii, basi ni vipi atamjibu au kumnufaisha? Hakika Mwenyezi Mungu Pekee Ndiye Mwenye Kunufaisha na Mwenye Kudhuru. Na kwa ajili hiyo, ni wajibu kwa Mwislamu asijenge msikiti juu ya makaburi, kwani Mtume Swalla
Mimi ni Mwislamu
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam amelikataza hilo.
• Kadhalika, ni wajibu kwa mja alinganishe kati ya udhaifu wake na Nguvu za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kati ya umasikini wake na Utajiri wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kati ya ujinga wake na Elimu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kati ya unyonge wake na Utukufu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
• Na ajue kwamba utukufu ni wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na Waumini.
• Hivyo yampasa awe ni miongoni mwa Waumini hawa ambao hawatawakali isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu Pekee, wala hawaombi msaada isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, wala hawaombi kinga na kujilinda isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, wala hawaombi msaada wa dharura ila kwa Mwenyezi Mungu, wala hawamwogopi isipokuwa Mwenyezi Mungu, wala hawataraji isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, wala
Mimi ni Mwislamu
hawamwombi isipokuwa Mwenyezi Mungu, wala hawachinji isipokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wala hawaweki nadhiri isipokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wala hawaapi isipokuwa kwa Jina la Mwenyezi Mungu, wala hawaweki talasimu na hirizi (amali), wala hawasadiki wasemayo makuhani, watabiri (wanajimu) na wachawi, na wala hawawaendei.
• Na wao hawakosi rajua, na huwa na tahadhari ya mponyoko wa ndimi zao ili wasije kutelezea motoni. Hawasemi: "Amependa Mwenyezi Mungu na amependa fulani", "lau si Mwenyezi Mungu na wewe", "nimetawakali kwa Mwenyezi Mungu na kwako". Bali waseme: "Nimetawakali kwa Mwenyezi Mungu Pekee", "Amependa Mwenyezi Mungu kisha amependa fulani".
Maneno haya humsawazisha Mwenyezi Mungu na waja Wake, na ni katika shirki ndogo.
Mimi ni Mwislamu
• Na kama ilivyo wajibu kwetu kumwamini Mwenyezi Mungu, ni wajibu wetu vile vile tuwakatae mataghuti.
• Na kigogo wa mataghuti ni shetani na kila yule aliyeabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu naye akaridhia hilo.
• Na kati ya mataghuti hawa ni yule aliyetunga sheria zinazoharamisha Aliyoyahalalisha Mwenyezi Mungu, au kuhalalisha Aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu.
• Aidha, taghuti ni kila yule aliyelingania hilo, au akawaamuru watu hilo, au akahukumu kwa hilo, kwa vile ametaadi na akavuka mpaka wa kiumbe wa kusikia na kutii.
• Basi Allaah Pekee Ndiye Aliyewaumba wanadamu, na Ndiye Anayejua yanayowafaa, na kwa hivyo, hakuna yeyote awezaye kuwapangia sheria isipokuwa Yeye tu.
Mimi ni Mwislamu
(2) KUWAAMINI MALAIKA
• Ninaamini kuwepo malaika ambao Mwenyezi Mungu Amewaumba kutokana na nuru, na Akawafanya kuwa na mbawa mbili mbili, tatu tatu, na nne nne. Nao hawali, hawanywi, hawalali wala hawaoi. Amewaamuru kufanya kazi na kusimamia majukumu mbalimbali, nao hutekeleza hayo.
• Malaika siku zote humtii Mwenyezi Mungu bila kuchoka. Hawamwasi na humwogopa Mola wao toka juu yao. Kuna kati yao aliyesujudu toka siku Alipoziumba Mwenyezi Mungu mbingu na ardhi hadi siku ya Kiyama. Na atakaponyanyua kichwa chake atasema: "Subhaanak! Hatujakuabudu ukweli wa kukuabudu".
• Wao ni waja wa Mwenyezi Mungu na si wanawake, na wala si wasaidizi Wake, na wao watawaombea shifaa
Mimi ni Mwislamu
Waumini – kwa idhini ya Mwenyezi Mungu – siku ya Kiyama.
Kati ya malaika hawa, wapo:
• Walinzi ambao huwalinda viumbe na madhara.
• Watukufu waandishi ambao huandika matendo ya wanadamu, mema yao na mabaya yao.
• Wenye kumsabihi Mwenyezi Mungu. Hawa humsabihi Mwenyezi Mungu mchana na usiku na hawachoki mpaka siku ya Kiyama.
• Wenye kuvinjari ambao huhudhuria vikao vya dhikri, kisomo cha Qura-aan na vikao vya elimu.
• Wabebaji Arshi ambao idadi yao ni wanane. Ni viumbe wakubwa mno kati ya viumbe wa Mwenyezi Mungu. Ndege huruka toka ncha ya sikio la mmoja wao hadi shingoni kwa muda wa miaka mia tano.
Mimi ni Mwislamu
• Malaika wa mauti anayezitoa roho za viumbe kwa Amri ya Mwenyezi Mungu. Huyu ana wasaidizi wake.
• Israfil atakayelipuliza baragumu, kisha viumbe vyote vitakufa kabla ya kutokea Kiyama. Kisha litapulizwa jingine, na hapo watasimama viumbe wakiangalia.
• Mikaili anayesimamia jukumu la mvua.
• Ridhwaan ambaye ni mlinzi wa Pepo. Yeye ana wasaidizi wake walio mbioni kuwahudumia Waumini Peponi.
• Maalik ambaye ni mlinzi wa moto. Ana wasaidizi wake ambao viongozi wao ni kumi na tisa. Wana marungu ya chuma ya kuwaadhibu makafiri motoni - Mwenyezi Mungu Atuepushe na hayo.
• Mkuu wa Malaika ni Jibril aliyewakilishwa kupeleka wahyi kwa Manabii na Mitume.
Mimi ni Mwislamu
• Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam alimwona katika umbile lake. Kutokana na ukubwa wake, alizifunika peo za mbingu. Ana mbawa mia sita, naye ndiye aliyekikamata kijiji cha Lut kwa ncha ya ubawa wake, akakinyanyua hadi juu mbinguni, kisha akakipindua juu chini.
• Kuna malaika wengineo wengi zaidi ya hawa, na hakuna ajuaye askari wa Mola wako isipokuwa Yeye tu.
(¯̄̄̄�� ��°°°°� � � �� � � �� � � �� � � �±±±±�� ��²²²²�� ��³³³³� � � � � �� � � � � �� � � � � �� � � � � �µ´µµ́´µ´ ) *,34��:562
• Malaika huwapenda Waumini ambao Mwenyezi Mungu Huwapenda na huwaombea maghfira.
• Malaika mbali na nguvu zao hizi hupigana pamoja na Waumini.
Mimi ni Mwislamu
(3) KUVIAMINI VITABU
• Ninaviamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu Alivyoviteremsha kwa Mitume Wake, na kwamba katika asili ya kuteremshwa Kwake, ni Maneno ya Mwenyezi Mungu Aliyowafunulia ili waifikishe sheria na dini Yake. Vitabu vikubwa zaidi ni:
� Quraan Tukufu iliyoteremshwa kwa Mtume wetu Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam.
� Injili iliyoteremshwa kwa Iysa Alayhi Ssalaam.
� Taurat iliyoteremshwa kwa Musa Alayhi Ssalaam.
� Zaburi iliyoteremshwa kwa Daud Alayhi Ssalaam.
� Sahifa zilizoteremshwa kwa Ibrahim Alayhi Ssalaam.
Mimi ni Mwislamu
• Kati ya hivi, kuna vilivyopotolewa na kubadilishwa kabla ya kushuka Qur-aan.
• Na Qur-aan ndiyo iliyo juu ya Vitabu hivi, na ndiyo yenye kuongoza sheria zote na hukumu zake, na yenye kuondosha yale yote yenye kwenda kinyume na hukumu zake baada tu ya kuteremka kwake.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu Hatokubali siku ya Kiyama ila amali kupitia uongofu wa Qur-aan. Hatokubali amali kwa kufuata Vitabu vilivyotangulia baada ya kuteremka Qur-aan kwa Mtume Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam.
• Na kwamba Qur-aan ni Maneno ya Mwenyezi Mungu ya miujiza. Maneno haya yana utukufu wake, na wala hayaingiliwi na batili kabla yake wala baada yake. Mwenye kuyasema, amesema kweli, na mwenye kuhukumia kwayo, amefanya uadilifu, na mwenye kuyafanyia kazi
Mimi ni Mwislamu
basi hakika ameongolewa katika njia iliyonyooka, mwenye kushikamana nayo amefuzu na kuokoka, na mwenye kuyakengeuka atakuwa ni katika wenye kuhiliki.
• Ni kwamba watu wa Qur-aan, hao ndio watu wa Mwenyezi Mungu waliokurubishwa Kwake, na kwamba mbora zaidi wa watu ni yule aliyejifundisha Qur-aan na akawafundisha watu, kwani Qur-aan hii itakuja siku ya Kiyama ikimwombea shifaa kila aliyeisoma, akaihifadhi na akaifanyia kazi, na itawaombea watu wake Pepo.
• Qur-aan huzitwaharisha nyoyo kutokana na shubha na matamanio yanayozichafua, huzikurubisha kwa Muumbaji Wake Subhaanahuu wa Ta'alaa, na huzihimiza kufanya kazi ili kufuzu na kupata neema za kudumu milele.
• Kati ya adabu za kusoma Qur-aan ni:
���� Kuwa twahara na wudhuu.
Mimi ni Mwislamu
���� Kuelekea Kibla.
���� Kukaa kwa adabu na heshima.
���� Kutoisoma kwa haraka.
���� Kuwa na unyenyekevu.
���� Kuonyesha huzuni kwa madhambi na kuvuka mipaka.
���� Kulia kutokana na kumwogopa Mwenyezi Mungu na Utukufu wa Maneno Yake.
���� Kusoma kwa sauti nzuri.
���� Kusoma kwa sauti ya chini ili kutowabughudhi wenye kuswali.
���� Kuzingatia maana ya maneno.
���� Kuhudhurisha moyo.
���� Kutaamuli kwa kina Aayah za Mwenyezi Mungu.
���� Tuwe na yakini kuwa kusimamisha hukumu za Kitabu hiki kwa watu ni moja kati ya sababu za kumakinishwa katika ardhi na kuwashinda maadui.
Mimi ni Mwislamu
Basi harakia ndugu yangu Mwislamu kwenda kwa Mola wako, na kikamate Kitabu hiki kwa hima. Kuwa na shime asikutangulie yeyote kuelekea kwa Mwenyezi Mungu, kwani Mwenyezi Mungu Hufurahi zaidi kwa kurejea kwako Kwake kuliko wanavyofurahi watu kwa kurejea mtu wao aliyekuwa mbali.
Mimi ni Mwislamu
(4) KUWAAMINI MITUME
• Ninawaamini Mitume wa Mwenyezi
Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu
Aliwateua Mitume kati ya wanadamu,
Akawafunulia Sheria Yake kwa njia ya
wahyi, na Akawaamuru kuifikisha kwa
watu, na kwamba mwenye kuwatii
ataingia peponi, na mwenye kuwaasi
ataingia motoni.
• Kisha Akawatilia nguvu kwa miujiza
yenye kuonyesha ukweli wao ili
iwasaidie mbele ya wakadhibishaji, na
ili iwe ni hoja kwao.
• Na kwamba Mtume wa mwanzo ni
Nuhu, na wa mwisho wao ni
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam.
Mimi ni Mwislamu
• Na kuwa Mitume hawa ni watu;
wanakula, wanakunywa,
wanaoa,wanaugua na wanakufa. Wao
ndio viumbe bora kabisa wa Mwenyezi
Mungu na wamehifadhiwa na maasi.
• Mitume wa Mwenyezi Mungu ni wengi.
Mwenyezi Mungu Amewataja baadhi
yao katika Qur-aan. Nao ni Muhammad
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam, Ibrahim Khalili wa Ar-
Rahmaan, Musa aliyesemeshwa na
Allaah, Iysa Neno la Mwenyezi Mungu
na Nuhu. Hawa ndio Mitume wenye
azma ya juu Rehma na Amani ziwe juu
yao. Pia Ismail, Is-haaq, Yakub,
Harun, Ayyub, Yunus, Sulayman,
Daawud, Yahya, Zakariya, Hud, Saleh,
Mimi ni Mwislamu
Yusuf, Shuayb, Ilyaas, Lut, Dhulkifl,
Idris, na wengi wengineo. Kati yao
kuna Aliowahadithia Mwenyezi Mungu
katika Qur-aan na wengineo
Hakuwahadithia.
• Jambo la kwanza walilolilingania
Mitume ni tawhid, na jambo kubwa
zaidi walilolikataza ni shirki, na wote
wamekuja na Uislamu na wito.
• wa tawhid. Lakini sheria zao na
mifumo ya kumwabudu Mwenyezi
Mungu Mtukufu ilitofautiana kutokana
na kutofautiana zama zao na nchi zao.
• Na kwamba Mitume walitoa bishara ya
kuja kwa Nabii Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam na
Mimi ni Mwislamu
wakawaamrisha kaumu zao
kumwamini Muhammad Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam
atakapotumwa kwao.
• Tofauti kati ya Rasuli (Mtume) na
Nabii ni kuwa Rasuli ni yule
aliyefunuliwa sheria mpya na
akaamrishwa kuifikisha kwa watu.
Ama Nabii, ni yule aliyetumwa ili
kuithibitisha na kuipitisha sheria ya
Rasuli aliyemtangulia.
• Ninaamini kuwa mbora wa Mitume
mbele ya Allaah ni Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
toka kwa mwana wa Ismaili bin
Ibrahim Alayhima Ssalaam. Allaah
Amemtuma kwa watu wote,
Mimi ni Mwislamu
Akahitimisha Unabii kwa Unabii wake,
na Utume kwa Utume wake.
• Akamtilia nguvu kwa miujiza,
Akamfanya bora kuliko Mitume wote.
Pia Ameufanya Utume wake kuwa
bora kuliko Utume wote uliotangulia,
na sheria yake kuwa bora kuliko
sheria zinginezo zilizopita, na Kitabu
chake Qur-aan kuwa bora kuliko
Vitabu vyote, na umati wake –
Waislamu – kuwa bora kuliko uma
nyinginezo.
• Na Mola wake Akampa mambo ambayo
Hakumpa yeyote katika Manabii
waliomtangulia. Kati ya mambo hayo
ni:
Mimi ni Mwislamu
(1) Al Wasiylah: Nayo ndiyo daraja ya
juu kabisa Peponi ambayo
Mwenyezi Mungu Amemwandalia
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam.
(2) Al Kawthar: Nao ni mto Peponi
wenye kupita chini ya Arshi ya Ar
Rahman.
(3) Al Hawdh: Ni sehemu ambayo
Waislamu peke yao ndio
watakayokunywa siku ya Kiyama.
Siku ambayo watu watapatwa na
kiu kikali, na jasho litawafika hadi
magotini, viunoni na mabegani –
kila mmoja kwa mujibu wa amali
yake – na Waislamu watakunywa
hapo kwa vikombe atakavyowapa
Mimi ni Mwislamu
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam kwa mikono yake
mitukufu. Baada ya hapo
hawatapatwa na kiu milele.
(4) Shafaa: Ni makamu ya kuhimidiwa
siku ya Kiyama. Hapo Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
ataomba shifaa kwa Mwenyezi
Mungu ili Waislamu waliofanya
maasi watolewe motoni, na
hatobakia ndani ya moto yeyote
anayeshuhudia kwamba hapana
Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu
na Muhammad ni Mtume wa Allaah.
Aliyefanya maasi hatosalia milele
motoni, bali atatoka baada ya
kutakaswa na maasi yake.
Mimi ni Mwislamu
Aliyewaamini Manabii wote na wala
hakumwamini Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam,
basi hatatoka motoni.
(5) Na kwamba Allaah Amemnusuru na
Akawanusuru askari wake na
wafuasi wake hadi siku ya Kiyama
kwa kuzagaza hofu ndani ya nyoyo
za maadui umbali wa mwendo wa
mwezi. Na hakuna Nabii yeyote
aliyepewa hili kabla yake
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam.
(6) Na ardhi imefanywa kwake na
Waislamu kuwa msikiti (sehemu ya
kuswalia) na twahara, na
Mimi ni Mwislamu
haikufanywa hivyo kwa Manabii
waliomtangulia.
(7) Na Allaah Amemtuma kwa watu na
majini wote, lakini Mitume wengine
wametumwa maalumu kwa watu
wao tu.
(8) Na kuwa yeye ndiye wa mwanzo
kaburi lake kufunguka, na ndiye
mwombezi wa kwanza, na ndiye wa
kwanza kupewa shifaa, na ndiye wa
kwanza kugonga mlango wa Pepo.
Atakapougonga, mlinzi
wa Pepo Ridhwaan atamuuliza: "Nani
wewe?" Atajibu: "Muhammad". Ridhwaan
atamwambia: "Kwako nimeamrishwa
nisimfungulie yeyote kabla yako".
Mimi ni Mwislamu
Na kati ya miujiza ya Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam ni:
� Kupasuka mwezi.
� Alilirejesha jicho la Qatada
lilipopofuliwa siku ya Uhud, macho yake
yakarudi yakawa mazima kabisa.
� Aliurejesha muundi wa Ibn Al
Hakam kama ulivyokuwa ulipovunjwa
siku ya Vita vya Badr.
� Aliutaka mti utamke shahada,
nao ukatamka shahada mbili mara tatu
mbele ya kafiri, naye akasilimu.
� Kigogo cha mti alichokuwa
akihutubia juu yake kililia wakati
alipokiacha na hakikunyamaza mpaka
alipoiweka mikono yake juu yake.
Mimi ni Mwislamu
� Alikifanya chakula kidogo kuwa
kingi baina ya mikono yake miwili, na
wakaweza kula na kushiba zaidi ya
watu 80 chakula cha kujaa viganja
viwili.
� Aliyafanya maji kidogo kuwa
mengi siku ya Hudaybiyah wakati jeshi
lilipobakiwa na bakuli moja tu ya maji.
Hapo Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam aliingiza mikono yake
ndani, maji yakaanza kububujika kati ya
vidole vyake kama chemchemu,
wakanywa maji Waislamu wote na
wakatawadhia maji hayo. Walikuwa
kiasi cha watu 1400.
� Alipelekwa usiku hadi Msikiti
wa Al Aqsa, na kisha alipandishwa hadi
Mimi ni Mwislamu
mbingu za juu na kukomea Sidrat Al
Muntahaa.
� Alielezea na kuhadithia habari
za umma zilizotangulia na Manabii wao
nailhali yeye hana kisomo; hajui
kusoma wala kuandika. Pia alielezea
matukio yatakayotokea siku za usoni
kwa kufunguliwa Fursi na Rome,
kusambaratishwa ufalme wa Kisra
aliyechanachana barua ya Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
aliyomtumia, pamoja na miujiza
mingineyo mingi.
� Muujiza mkubwa zaidi wa
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii
wa Sallam ni Qur-aan Tukufu. Ni
Mimi ni Mwislamu
muujiza utakaosalia hadi siku ya
Kiyama.
� Kisha Allaah Ameunyanyua
utajo wake, Akaliandamisha jina la
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii
wa Sallam na Jina Lake Subhaanahuu
wa Taalaa, na Akaifanya shahada ya
kuwa hapana mola isipokuwa Allaah na
kwamba Muhammad ni Mtume wa
Mwenyezi Mungu kuwa ndio jambo la
kwanza analoingia nalo mja katika
Uislamu,na jambo la mwisho analotoka
nalo duniani. Basi yeyote ambaye neno
lake la mwisho litakuwa ni "Laailaaha
illa Allaah", ataingia peponi.
• Ni wajibu wetu kwa upande wa
Mtume wetu Swalla Allaahu Alayhi
Mimi ni Mwislamu
wa Aalihii wa Sallam tusilitangulize
neno la kiumbe yeyote juu ya neno
lake, au rai ya yeyote hata kama ana
sauti kwa watu. Na ikiwa watu
watakutangulia kuhamia kwake, basi
hama wewe kwenda katika sunnah
yake katika kila jambo lako na wala
usimfuate mwingine zaidi yake. Ni
wajibu wetu tushikamane sote
pembezoni mwa amri yake na tumtii,
kwani mwenye kumtii Mtume, basi
huwa amemtii Mwenyezi Mungu.
(AAAA�� ��BBBB�� ��CCCC�� ��DDDD�� ��EEEE�� ��GFGFGFGF ) *7��8��:092:
• Na tusimwiite ila kwa kusema Mtume
wa Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam.
Tusiseme (Muhammad) basi.
Mimi ni Mwislamu
• Tujipambe kwa adabu zake, na
tumwige katika hali zake zote; kulala
kwake, kula kwake, kutembea
kwake, kuswali kwake, kufunga
kwake, kutoa kwake sadaka, na
jihadi yake.
• Na tumpende zaidi kuliko nafsi zetu,
wana wetu, wazazi wetu na watu
wote.
• Na tumpende kila yule anayempenda
Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
na kumfanya kiigizo chake, na
tumchukie kila yule anayemchukia
Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
na wala hawajibiki na sheria yake.
Mimi ni Mwislamu
• Hivyo basi, ni lazima kwa Mwislamu
awapende Waumini, awanusuru,
ajifananishe nao, ashughulikie
mambo yao, asaidiane nao katika
mambo ya kheri, na awafanye kuwa
marafiki zake wa dhati.
• Ni wajibu kwake awabughudhi
makafiri na ukafiri wao, asiwatii,
asiungane nao dhidi ya Waislamu,
wala asisaidiane nao katika ubatilifu
wao, na wala asishiriki katika
sikukuu zao. Ni haramu kwake
kuwadhulumu, na linalotakiwa ni
kuwatendea haki.
• Ni wajibu wetu tuwapende Mama wa
Waumini; Wakeze Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam,
Mimi ni Mwislamu
na tuwapende Maswahaba Wake
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam, kwani wao ndio bora wa
watu baada ya Manabii.
• Pia ni wajibu wetu tuihuishe Sunnah
yake Mtume Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam, tuidhihirishe
sheria yake, na tubalighishe
ulinganio wake kwa watu wote.
Kisha tusubiri maudhi na kero
zinazotupata katika kuyapigania
hayo, kwani hayo hayaepukiki.
• Kwa vile Mwenendo wa Mwenyezi
Mungu uliopita kwa viumbe Vyake
unahukumia kuwa hakuna Nabii au
walii yeyote aliyelingania haki hii ila
alifanyiwa uadui na kuudhiwa.
Mimi ni Mwislamu
• Zindukana ndugu yangu Mwislamu!
Maudhi ya makafiri yasikufanye
ukaiacha dini yako. Kwani Mtume wa
Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam
aliudhiwa wakati Maswahaba
walipokuwa wachache, nao pia
waliudhiwa wakafanya subira.
• Na wala usilegeze azma yako hata
kama watakwambia kuwa
unayoyazungumza ni upuuzi, una
misimamo migumu, au umepitwa na
wakati. Au wakisema: "ashachezewa
akili huyo". Kwani wewe una kiigizo
chema kwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu, yeye ashaambiwa mshairi na
hata mwendawazimu.
Mimi ni Mwislamu
• Wala usisononeke ukiambiwa
mpotevu mwenye siasa kali. Hii ndio
tabia ya makafiri kwa Waumini.
(Ü�Û�Ú�Ù�Ø�×Ü�Û�Ú�Ù�Ø�×Ü�Û�Ú�Ù�Ø�×Ü�Û�Ú�Ù�Ø�× ) *���;��:5<2:
((Na wanapowaona, husema hakika
hawa bila shaka ni wapotevu)).
• Ikiwa watu wako makundi mawili, je
haikutoshi wewe kuwepo katika
kundi aliloko Mtume wako
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam?!
• Achana nao hao mpaka ifike siku
ambayo dhalimu ataviuma vidole
vyake aseme: "Laiti mimi
ningeliifuata njia pamoja na Mtume".
Mimi ni Mwislamu
( \\\\�p�o�n�m����l�k�j��i�h�p�o�n�m����l�k�j��i�h�p�o�n�m����l�k�j��i�h�p�o�n�m����l�k�j��i�hqqqq ) *+�=,���:<>2:
• Wala usibabaike au kuchanganyikiwa
kama watakwambia kuwa wewe ni
gaidi au mwovu, kwani hayo ndio
madai ya madhalimu dhidi ya
Waumini duniani na akhera. Ni kuwa
pale Malaika watakapowaongoza
kwenda Jahannamu wakisunukia,
wataangalia humo kisha waseme:
(J�I�H���G�F�E�D�C�B�AJ�I�H���G�F�E�D�C�B�AJ�I�H���G�F�E�D�C�B�AJ�I�H���G�F�E�D�C�B�A ) *?:@<:2
((Na watasema: Mbona
hatuwaoni watu tuliokuwa
tukiwazingatia kuwa ni katika
waovu?))
Mimi ni Mwislamu
• Na hapa, Waumini (ambao makafiri
wamewaita kuwa ni waovu)
watawaita toka kwenye magorofa ya
juu kabisa ya Firdaws wakiwaambia:
(L�K�J�I�H�G�FL�K�J�I�H�G�FL�K�J�I�H�G�FL�K�J�I�H�G�F�� �� )*A�,-��:BB:2
� و�� ر��� ���(( �٤٤: ا���اف )) أن � و�
(( Hakika sisi tumeyakuta
Aliyotuahidi Mola wetu kuwa ni
kweli))
Mimi ni Mwislamu
(5) KUAMINI SIKU YA MWISHO
• Ninaiamini siku ya mwisho, nayo ni
iku ambayo dunia (nyumba ya amali)
itamalizika, na akhera (nyumba ya
malipo) itasimama, wema wakalipwa
Pepo, na waovu wakalipwa moto.
• Katika siku ya Kiyama, mizani
itawekwa, na kila mja atapewa
kitabu chake. Atakayepokea kitabu
chake kwa mkono wake wa kuume,
basi Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam atakuwa pamoja
naye Peponi. Ama yule atakayepokea
kitabu chake kwa mkono wake wa
kushoto, basi atakuwa pamoja na
Mimi ni Mwislamu
Firauni –laana ziwe juu yake–
motoni.
• Sirati itawekwa, atakayefanikiwa
kuivuka basi atafikia Peponi. Ama
ambaye kulabu zitamnyakua kutokana
na amali zake mbovu, basi
ataangukia motoni.
• Siku ya Kiyama ina dalili, ina alama
ndogo na ina alama kubwa.
• Miongoni mwa alama ndogo ni
kupotea uaminifu, kukithiri mauaji,
madaraka kukamatwa kwa mabavu
na mafasiki, na masuala muhimu
kuzungumziwa na wasiojua kitu.
• Na miongoni mwa alama kubwa ni
kuibuka Al Mahdi, kusimama ukhalifa
Mimi ni Mwislamu
wongofu utakaokwenda juu ya
misingi ya njia ya Utume kabla ya
kutokea Kiyama, na kudhihiri masihi
mwongo.
• Pia kuteremka Iysa Alayhi Ssalaam ili
awaongoze Waislamu, apigane na
makafiri, avunje vunje misalaba, aue
nguruwe, na azikatae dini zote
nyingine ila Uislamu tu.
• Basi haitobakia nyumba yoyote ya
mjini au ya mashambani ila
Mwenyezi Mungu Ataiingiza dini hii,
kwa heshima ya mwenye nguvu, au
kwa udhalili wa mnyonge.
• Vile vile kutoka Yaajuju na Maajuju.
Pia atatoka mnyama
Mimi ni Mwislamu
anayewasemesha watu, na jua
litachomoza toka magharibi, Qur-aan
itaondoshwa na mambo mengineyo.
• Basi yeyote atakayefanya amali ya
uzito wa atomu ikiwa ni ya kheri au
ni ya shari, ataiona siku ya Kiyama
ndani ya kitabu chake.
• Basi harakieni kwenye mambo ya
kheri kabla haujamalizka muda wa
kusajiliwa kwa kufa mja katika muda
ambao haujui yeyote ila Mwenyezi
Mungu Pekee.
• Wakamwosha jamaa zake,
wakamvisha sanda, wakamswalia,
wakamzika. Kisha akajiwa na Malaika
wawili; Munkari na Nakiyr,
Mimi ni Mwislamu
wakamkalisha kitako na kumwuuliza:
"Nani Mola wako? Nini dini yako?
Nani Nabii wako?"
• Ikiwa atajibu kuwa: "Allaah ni Mola
wangu, na Uislamu ndiyo dini yangu,
na Muhammad Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam ndiye Nabii
wangu na Mtume wangu" – na Allaah
Akamwezesha hilo – basi
itafunguliwa katika kaburi lake
harufu ya rayhaan hadi peponi,
akaona mashukio yake huko, na
makasri yake na ufalme wake. Hapo
atashangilia kwa furaha kubwa, na
kaburi lake litapanuliwa upeo wa
macho.
Mimi ni Mwislamu
• Na ikiwa ni katika makafiri, basi
hatoweza kujibu chochote, kwani
majibu wakati huo si kwa akili au
werevu wa mtu.
• Bali Mwenyezi Mungu Huwathibitisha
na kuwaimarisha watu wa imani
wakati huo kwa yale
waliyoyatanguliza kati ya amali
njema zilizosimamia juu ya tawhid,
utekelezaji wa faradhi, kushiriki
jihadi, kutenda mema, kuamrisha
mema, kukataza mabaya, kutoa
sadaka, kusoma Qur-aan, kufunga
siku za joto kali, na kusimama
kuswali muda mrefu usiku wa baridi
kali.
Mimi ni Mwislamu
• Ama akiwa ni katika makafiri, basi
kaburi lake humbana hadi mbavu
zake zikaingiana katika mwili wake,
na kaburi lake huwa ni shimo katika
mashimo ya motoni kwa sababu ya
amali zake mbaya.
• Basi jitahidi ndugu yangu Mwislamu,
kwani leo ni amali na hakuna hisabu,
lakini kesho ni hisabu na hakuna
amali.
• Na siku hiyo, Waislamu watiifu
wataingia Peponi peke yao, kwa vile
Mwenyezi Mungu Hatoikubali dini
yoyote siku ya Kiyama isipokuwa
Uislamu.
Mimi ni Mwislamu
• Ndani ya Pepo kuna neema ambazo
hakuna sikio lililowahi kuzisikia, wala
jicho lililowahi kuziona, wala hata
kuwaziwa katika akili ya
mwanadamu. Neema zake zitasalia
milele wala hazitomalizika, na
waliomo humo hawatakufa milele.
Neema kubwa zaidi ya zote humo, ni
kuuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu
Mola wa walimwengu wote.
• Na waasi, waovu na makafiri
wataingia motoni. Ndani ya moto,
kuna adhabu zisizoweza kuvumilika
Alizoziandaa Mwenyezi Mungu kwa
ajili ya makafiri. Milima mirefu thabiti
haiwezi kuzivumilia adhabu hizi, na
Mimi ni Mwislamu
hao wataadhibiwa humo bila
kupumzishwa.
• Na humo, wafuasi wa mataghuti
wataomba adhabu iongezwe
maradufu kwa wakubwa wao
waliowapoteza. Na hapo Mwenyezi
Mungu Ataamuru adhabu iongezwe
maradufu kwa wote.
• Basi thibiti ndugu yangu Mwislamu
juu ya haki hii, wala usidanganyike
kabisa kuona kuwa wavunjaji sheria
ni wengi zaidi, kwani ikiwa wewe
utawatii na ukawafuata wengi
waliomo ardhini, basi watakupoteza
njia ya Mwenyezi Mungu. Nawe pita
pamoja na wenye kupita kuelekea
kwa Mwenyezi Mungu.
Mimi ni Mwislamu
• Kwani kundi katika umma wa
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam litaendelea kuwa
juu ya haki likiwa na nguvu, hawezi
kuwadhuru yeyote aliyekwenda nao
kinyume au aliyewasaliti mpaka siku
ya Kiyama.
• Basi ni mbinu zipi za kuzijua ngazi
hizo za kupanda juu, na kuokoka na
ngazi hizo za kuporomokea chini? Na
ni mbinu zipi za kuwafikia
waliotangulia wenye kukurubishwa,
na kujiweka mbali na wapingaji
wenye kuangamia? Bila shaka ni toba
ya kweli ya kusahihisha na
kurekebisha yaliyopita, na amali
njema za kuweka sawa umri
Mimi ni Mwislamu
uliosalia, na kuweka nia ya kweli ya
kunyooka na kutokengeuka.
• Basi kuwa pamoja na watu kwa
kiwiliwili chako, ukiuza, ukinunua,
ukioa na ukiiamirisha ardhi kwa yale
Aliyokuhalalishia Mwenyezi Mungu.
• Wala moyo wako usifungamane na
kitu chochote cha kidunia, bali nenda
na moyo wako pale ambapo
unatakikana uwe, huko chini ya Arshi
ya Ar Rahmaan, na sujudu kwa moyo
wako sijdah ambayo utaendelea
kuisujudu hadi siku ya Kiyama.
Mimi ni Mwislamu
(6) KUAMINI QADHAA NA QADARI
• Nako ni kuamini kwamba Mwenyezi
Mungu Anayajua yote yaliyomo
ulimwenguni, yote yanayofanyika na
yatakayotokea hadi siku ya Kiyama.
Hata chembe ndogo mno, Yeye
Hakosi kuijua. Na kwamba Yeye
Anavijua vitendo vya waja, riziki zao,
muda wao wa kuishi, na nani kati yao
atakuwa wa peponi, na nani kati yao
atakuwa wa motoni kabla
Hajawaumba.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu
Ameyaandika makadirio haya katika
Lawh Al Mahfuudh kabla hata
Hajaziumba mbingu na ardhi kwa
miaka elfu hamsini, na kwamba Lawh
Mimi ni Mwislamu
Al Mahfuudh hii hakuna malaika wa
karibu au hata Nabii aliyetumwa
awezaye kuichungulia.
• Hata kijusi kinapokuwa ndani ya
tumbo la uzazi la mama yake,
Mwenyezi Mungu Huwaamrisha
Malaika waandike kama ni cha kike
au kiume, waandike na riziki yake,
amali yake, muda wake wa kuishi na
hatima yake (ima peponi au motoni).
Pia waandike mazuri na mabaya
atakayokabiliana nayo.
• Kisha unapoingia usiku wa cheo
(Laylatul Qadr), huteremka
makadirio ya mwaka mzima toka
Lawh al Mahfuudh kati ya ajali za
watu, riziki zao, nani kati yao atahiji
mwaka huo na mengineyo. Katika
Mimi ni Mwislamu
usiku huo, hukadiriwa mambo ya
mwaka mzima.
• Kisha huteremka makadirio ya kila
siku kwa nyakati zake na watu wake,
hapo Mwenyezi Mungu Huwanyanyua
watu na wengine Huwashusha.
• Na tuamini kuwa Mapendeleo ya
Mwenyezi Mungu ndiyo yawayo,
Alilolitaka huwa na Asilolitaka haliwi.
Mwenyezi Mungu Hana wa
kumshinda, na Yeye Ndiye Mwenye
kuzipindua nyoyo. Humwongoa
Amtakaye kwa fadhila Zake na rehma
Zake, na Humpoteza Amtakaye kwa
Uadilifu Wake na Hekima Yake,
kwani Yeye Ndiye Ajuaye zaidi nani
anastahiki uongofu na nani
anastahiki upotevu.
Mimi ni Mwislamu
• Na Mwenyezi Mungu Haulizwi yale
Ayafanyayo lakini watu huulizwa.
• Na tuamini kuwa Mwenyezi Mungu
Amekiumba kila kitu, na hakuna
chembe yoyote ndogo ulimwenguni
isipokuwa Mwenyezi Mungu
Ameiumba na Akaumba kutikisika
kwake na kutulia kwake.
• `Na kwamba Yeye Amewaumba waja
na vitendo vyao, na kwamba Yeye
Amewaumbia waja uwezo na
mapendeleo yao ili wajichagulie
wenyewe vitendo vyao.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu
Mtukufu Amewaamuru viumbe Wake
wamtii, na Akawaahidi kuwapa Pepo
Yake wakifanya hivyo, na
Amewakataza kumwasi Yeye, na
Mimi ni Mwislamu
Akawapa onyo la kuwaingiza ndani
ya moto Wake wakifanya hivyo, na
wala Hakuwakalifisha kazi isipokuwa
ile ambayo wanaweza kuifanya. Na
hapo wakagawanyika makundi
mawili: Waumini na makafiri; kwa
hiari yao wenyewe, kwa mapendeleo
yao wenyewe na kwa uwezo wao
wenyewe, na yote hayo Mwenyezi
Mungu Amewaumbia.
• Na kwamba thawabu na adhabu
hutokana na kuifuata sheria, si kwa
kutangulia Elimu ya Mwenyezi Mungu
kwao. Basi yeyote atakayefanya amali
yoyote ya kheri ya uzito wa atomu,
atalipwa kwayo. Na yeyote atakayefanya
amali yoyote ya shari ya uzito wa
atomu, basi ataadhibiwa kwayo.
Mimi ni Mwislamu
• Na kwamba kinachozingatiwa ni
mwisho wa matendo, na kwamba kila
mja ni mwenye kuendeshwa katika
lile aliloumbiwa kati ya kufurahika
Peponi au kupata shakawa motoni.
• Na kwa ajili hiyo, ni wajibu kwa mja
aogope mwisho mbaya, na aendelee
daima kumwomba Mwenyezi Mungu
na amhitajie, Amhidi katika njia
iliyonyooka, na adumu kumwomba
Amsaidie katika kumtii, na ajilinde
Kwake na maasia, kwa vile mja hana
hila wala nguvu zozote za kuyafanya
hayo ila kwa Uwezo wa Mwenyezi
Mungu.
• Na kwamba Waumini Huridhia
Qadhaa ya Mwenyezi Mungu na
Qadari Yake; ya kheri yake na ya
Mimi ni Mwislamu
shari yake, katika misukosuko na
katika furaha, na wana yakini kuwa
hawezi yeyote kuwanufaisha
isipokuwa kwa Qadari ya Mwenyezi
Mungu, na wala hawadhuru
isipokuwa liwe lisha andikwa na
Mwenyezi Mungu.
• Na mja hatopata utamu wa imani
mpaka pale atakapojua kwamba
lililompata lisingekuwa la kumkosa,
na lililomkosa lisingekuwa la
kumpata.
Na mwisho naomba nikisema:
"Ninamhimidi Mwenyezi Mungu, na
ninamwomba Aniingize Peponi mimi na
Waislamu wengine, na Anilinde na moto
mimi na Waislamu wengine". Aamiyn.
Mimi ni Mwislamu
� �_�`�a�b��c�d�e�
f�g�h�i�j�k �� �
]٨٥:ل ���ان[
������������٠٠٢٠١٠١٤٥٩٦١٣٠٠٢٠١٠١٤٥٩٦١٣٠٠٢٠١٠١٤٥٩٦١٣٠٠٢٠١٠١٤٥٩٦١٣א���� ��א��א���������� ���[email protected]*(#א)�'�א��������א�& ��א%�$#"! � �
WWW.Iam-Muslim.com
� �
١٤٣١������ J�٢٠١٠�,� �
���W٢٢٢٧٤L٢٠٠٩���א���א� �
� ٠١٢٠١٥٢٩٠٨: א�0123'������������W٠١٠٥٠١٣١٥١٠١٠٥٠١٣١٥١٠١٠٥٠١٣١٥١٠١٠٥٠١٣١٥١א%.א-���
� !" "!# و $%& �&'(% � ,+ ا&*�'ق