16
!"#2 AGOSTI 2015 Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

  • Upload
    others

  • View
    5

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

!"#2 AGOSTI 2015

Chembe ZakoMAKTABA ILIYO HAI!

Page 2: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Je, ungependa kupata habari zaidi aukujifunza Biblia nyumbani kwako bila malipo?Tembelea www.jw.org/sw au utume ombi lakoukitumia mojawapo ya anwani zilizo hapa chini.JEHOVAH’S WITNESSES: SOUTH AFRICA: Private Bag X2067,Krugersdorp, 1740. KENYA: International Bible Students Association,PO BOX 21290, 00505 Nairobi. Ili upate orodha kamili ya anwanizetu ulimwenguni pote, tazama www.jw.org/sw/mawasiliano.

Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango yahiari. Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko yamenukuliwa kutoka katika Biblia Takatifu—Tafsiriya Ulimwengu Mpya.Awake! (ISSN 0005-237X) is published monthly by Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.;L. Weaver, Jr., President; G. F. Simonis, Secretary-Treasurer; 25 Columbia Heights, Brooklyn, NY 11201-2483,and printed by Watch Tower Bible and Tract Society of South Africa NPC, 1 Robert Broom Drive East, Rangeview,Krugersdorp, 1739. � 2015 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Printed in South Africa.

!"#2

KATIKA TOLEO HIL I

3 HABARI KUUChembe Zako—MaktabaIliyo Hai!

8 MSAADA KWA AJILI YA FAMILIAKuwafundisha WatotoSifa ya Kujizuia

10 Elimu ya Biblia HusaidiaWatu Kujua Kusoma naKuandika

12 MAONI YA BIBLIAUvumilivu

14 Alishikamana na ImaniYake

16 JE, NI KAZI YA UBUNI?Mfumo wa Gia wa PanziAnayeitwa Issus

s HABARI ZAIDI KWENYE INTANETI

MATINEJAVIJANA WENZAKO WANASEMA NINI?

Kutunza AfyaKutunza afya kunahusisha nini?Tazama video Kutunza Afya.Unaweza pia kupata majibu ya maswaliya Biblia ambayo huenda ukaulizwashuleni kama vile: “Uumbaji auMageuzi?”(Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA ˛ MATINEJA)

WATOTOUWE RAFIKI YA YEHOVA

Watii Wazazi WakoTazama video zenye masomo muhimu,kama vile Watii Wazazi Wako.(Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA ˛ WATOTO)

Vol. 96, No. 8 / Monthly / SWAHILIKila Toleo Linalochapishwa: 51,788,000 Katika Lugha 103

w

r

w

r

Page 3: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 3

KATIKA mwaka wa 1953, wanabiolojia wa molekuli James Watson naFrancis Crick walichapisha ugunduzi wao ulio muhimu sana katika ue-lewaji wetu wa kisayansi kuhusu uhai. Waligundua umbo la DNA lina-lofanana na kamba yenye matita mawili.� Mara nyingi kamba hizo zi-nazopatikana ndani ya kiini cha kila chembe huwa na programu,“maandishi” au habari zinazofanya chembe hizo kuwa kama makta-ba zilizo hai. Ugunduzi huo wenye kustaajabisha ulikuwa wa muhimusana katika elimu ya biolojia! “Maandishi” yaliyo kwenye chembeyana umuhimu gani? Yalitokeaje?

�Watson na Crick walifanya utafiti wao wakitegemea uchunguzi uliofanywa awali kuhusuDNA, au deoksiribonyukilia asidi.—Ona sanduku “Historia ya Ugunduzi wa DNA.”

HABARI KUU

Chembe ZakoMAKTABA ILIYO HAI!

Page 4: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

KWA NINI CHEMBE ZINAHITAJI HABARI?Je, umewahi kujiuliza ni kwa nini mbegu

inapopandwa hatimaye huwa mti au ni jinsigani yai lililotungishwa mimba hatimayehuwa mwanadamu? Je, umewahi kufikiria ji-nsi ulivyorithi tabia? Majibu ya maswali hayoyanategemea habari zinazopatikana kwenyeDNA.

Karibu chembe zote zina DNA ambayo nimolekuli tata zaidi inayofanana na ngazi ili-yopindika. Katika genome ya mwanadamuau safu kamili ya DNA, ngazi hizo zinakadiri-wa kuwa na “vipande” bilioni tatu vya kemi-kali. Wanasayansi huviita vipande hivyo joziza msingi kwa sababu kila kipande kimeu-ndwa kwa kemikali za aina mbili ambazokwa pamoja ziko nne. Chembe hizo huandi-kwa kwa kifupi kwa kutumia herufi nne rahi-si ambazo ni A, C, G, naT.� Katika mwaka wa1957, Crick alieleza pia kwamba kuna mi-stari yenye mpangilio katika vipande vya ke-mikali ambayo hutokeza maagizo yaliyoandi-kwa. Jambo hilo lilianza kueleweka vizurikatika miaka ya 1960.

Habari yoyote iwe ni picha, sauti, au maa-ndishi, inaweza kuhifadhiwa na kushughuliki-wa kwa njia nyingi. Kwa mfano, kompyutahufanya hivyo kielektroniki. Kwa kutumiaDNA, chembe hai huhifadhi na kushughulikiahabari kwa njia ya kikemikali. DNA hupiti-shwa wakati chembe zinapogawanyika naviumbe vinapozaliana—uwezo unaoaminikakwamba ndiyo unaofafanua maana ya uhai.

Chembe hutumia habari jinsi gani? Hebuwazia kwamba DNA ni kama kitabu cha ma-pishi chenye maelekezo na hatua mbali-mbali, na kila hatua imeandikwa kwa umaki-ni na utaratibu maalumu. Hata hivyo, badala

� Herufi hizo humaanisha kemikali ya adenine, cytosine,guanine, na thymine.

Historia yaUgunduzi waDNA1869 Mtaalamu wa kemiaFriedrich Miescher, alie-leza kuhusu kile amba-cho kwa sasa hujulikanakuwa deoksiribonyukiliaasidi, au DNA.

Mapema katika miakaya 1900 MwanabiolojiaPhoebus Levene aligu-ndua utaratibu wa miu-ndo ya kemikali fulani zaDNA na jinsi zinavyou-ngana kutokeza molekuliinayofanana na mnyo-roro.

1950 Mtaalamu wabiokemia Erwin Chargaffaligundua kwamba muu-ndo wa DNA hutofautia-na kati ya kiumbe kimojana kiumbe kingine.

1953 WanasayansiJames Watson na Fran-cis Crick walifafanuakwamba umbo la DNA li-nafanana na ngazi.

Page 5: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 5

ya maelekezo hayo kutokeza keki au biskutiyanatokeza kabichi au ng’ombe. Hata hivyo,hatua hizo hujiendesha zenyewe katika che-mbe hai na hivyo hufanya iwe vigumu kuzie-lewa.

Habari zilizo kwenye chembe ya urithi hu-hifadhiwa mpaka zitakapohitajiwa, labda ilikubadili chembe zilizochakaa au zilizo naugonjwa kwa kutokeza chembe mpya au ku-pitisha tabia kwa mtoto. DNA ina habari nyi-ngi kadiri gani? Fikiria bakteria, mmoja katiya viumbe wadogo zaidi. Mwanasayansi Mje-rumani Bernd-Olaf Kuppers alisema hivi:“Tukilinganisha na lugha, ujumbe ulio katikamolekuli unaofafanua muundo wa chembeya bakteria unaweza kutoshea kitabu che-nye kurasa elfu kadhaa.” Kwa sababu hiyo,profesa wa kemia David Deamer aliandikahivi: “Mtu anaweza kupendezwa na mambotata kuhusu uhai hata ule unaonekana kuwawa hali ya chini.” Genome ya mwanadamuinaweza kulinganishwa na nini? Kuppers ana-sema hivi: “Habari zilizo katika [Genome] zi-naweza kujaza maelfu ya vitabu katika mak-taba.”

“ZIMEANDIKWA KWA NJIA AMBAYOTUNAWEZA KUELEWA”

Kufafanua habari zilizo katika DNA kama“lugha ya molekuli ya chembe za urithi haku-toshi,” anasema Kuppers. Anaendelea kuse-ma hivi: “Kama tu ilivyo katika lugha za wa-nadamu, lugha ya molekuli ya chembe zaurithi ina utaratibu maalumu.” Kwa ufupi,DNA ina “sarufi,” au kanuni, zinazoongoza ki-kamili jinsi maagizo yanavyotolewa na kute-kelezwa.

“Maneno” na “sentensi” katika DNA huu-nda “maagizo” mbalimbali ambayo huongo-za kutokezwa kwa protini na viini vingine vi-navyojenga chembe mbalimbali zinazoundamwili. Kwa mfano, “maagizo” hayo yanawe-za kuongoza kufanyizwa kwa chembe za mi-fupa, misuli, neva, au chembe za ngozi. Mwa-nabiolojia wa mageuzi, Richard Dawkinaliandika hivi: “Uzi wa DNA una habari auujumbe ulioandikwa kikemikali, na kila heru-fi moja inawakilisha kemikali moja.” Akao-ngezea hivi: “Ni jambo la kushangaza kwa-mba alama hizo au utaratibu huo hubadilikana kuwa maandishi tunayoweza kuelewa.”

Habari zilizo katika chembe ya bakteria zinaweza kujaza kurasa 1,000 za kitabu

Mtoto hurithitabia za wazaziwake jinsi gani?

Page 6: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Mwandikaji wa Biblia Daudi alisali kwa Mu-ngu hivi: “Macho yako yalikiona kiini-tetechangu, na katika kitabu chako sehemu zakezote zilikuwa zimeandikwa.” (Zaburi 139:16)Daudi alitumia lugha ya kishairi. Hata hivyo,kulingana na kanuni, alikuwa sahihi kabisaakiwa mwandishi wa Biblia. Hakuna mwandi-shi yeyote wa Biblia aliyeathiriwa hata kido-go na hekaya au mapokeo ya watu wa kale.—2 Samweli 23:1, 2; 2 Timotheo 3:16.

MAANDISHI HAYO HUANDIKWAJE?Kama ilivyo katika visa vingi, wanasaya-

nsi wanapofafanua jambo moja maswali me-ngi hujitokeza yanayohitaji ufafanuzi mwingi-ne. Hivyo ndivyo ilivyokuwa walipogunduaDNA. Ilipojulikana kwamba DNA ina habarizilizoandikwa, watafiti waliuliza hivi: ‘Maandi-shi hayo huandikwaje?’ Bila shaka, hakunamwanadamu aliyeona molekuli ya kwanza yaDNA ilipoumbwa. Hivyo, tunaweza kuwa namaoni mbalimbali. Hata hivyo, maoni hayohayapaswi kukisiwa-kisiwa. Fikiria ulinganifuufuatao.

˙ Katika mwaka 1999, vipande vya vigaevya kale vilivyo na alama au michoro isiyoya kawaida vilichimbuliwa nchini Pakistan.Alama hizo bado hazijaweza kufafanuliwa.Hata hivyo, inadhaniwa kwamba alamahizo ziliandikwa na binadamu.

˙ Miaka michache baada ya Watson na Crickkugundua muundo wa DNA, wanafizikiawawili walianza kuchunguza mawimbi yaredio kutoka angani. Huo ukawa mwanzo

wa uchunguzi unaoendelea wa ikiwa kunaviumbe hai katika sayari nyingine.

Jambo kuu ni nini? Watu huhusianisha ha-bari na ujuzi iwe habari hiyo iko kwenye mi-choro ya kigae au ishara kutoka angani. Ha-wahitaji kuona jinsi habari hiyo ilivyojitokezaili kufikia mkataa huo. Hata hivyo, wakatimfumo tata wenye habari ulipogunduliwa,yaani, kemikali yenye habari kuhusu uhai,wengi huona utendaji wa DNA kuwa jambo li-silo na maana yoyote. Je, ni jambo linalofaakuwa na maoni hayo? Je, linapatana naakili? Je, hilo ni jambo la wanasayansi pe-kee? Wanasayansi wengi mashuhuri husemahaipaswi kuwa hivyo. Baadhi ya wanasayansihao ni Dakt. Gene Hwang na ProfesaYan-DerHsuuw.� Fikiria yale waliyosema.

Dakt. Gene Hwang amefanya utafiti wamsingi wa mpangilio wa chembe za urithi.Wakati fulani aliamini mageuzi, lakini utafitialiofanya ulibadili maoni yake. Aliliambia ga-zeti la Amkeni! hivi: “Kujifunza kuhusu che-mbe za urithi kunaongeza ujuzi kuhusu mfu-mo wa uhai, ujuzi unaonifanya niheshimusana hekima ya Muumba.”

ProfesaYan-Der Hsuuw ni kiongozi wa uta-fiti wa viini-tete katika Chuo kikuu chaTaiwancha National Pingtung University of Scienceand Technology. Yeye pia aliamini mageuzimpaka baada ya kufanya utafiti uliomwongo-za kufikia mkataa tofauti. Alisema hivi kuhu-

� Mahojiano zaidi pamoja na wanasayansi mashuhuri yana-weza kupatikana kwenye tovuti yetu, jw.org/sw. Bonyeza kitu-fe cha Tafuta, kisha ingiza “mahojiano na wanasayansi.”

Gene Hwang (kushoto)na Yan-Der Hsuuw

Page 7: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

su mgawanyiko wa chembe na utendaji wakewa pekee: “Chembe zinazofaa lazima zitoke-zwe kwa utaratibu na sehemu zinazofaa.Kwanza chembe hizo huungana na kuwa ti-shu ambazo pia huungana na kuwa viungo.Ni injinia gani anayeweza kuandika maagizoyanayojiendesha yenyewe? Hata hivyo, maa-gizo ya ukuzi wa viini-tete yameandikwa kwanjia ya pekee katika DNA. Ninapofikiria uta-ratibu huo mzuri ninaamini kwamba uhai uli-buniwa na Mungu.”

JE, JAMBO HILO NI MUHIMU?Bila shaka! Ikiwa Mungu ndiye aliyeumba

uhai, basi Mungu ndiye anayestahili kusifiwawala si mageuzi. (Ufunuo 4:11) Pia, ikiwa sisitumeumbwa na Muumba mwenye hekima,basi tupo hapa kwa kusudi fulani. Hali isinge-kuwa hivyo ikiwa uhai ulijitokeza wenyewe.�

Kwa kweli, watu wanaotafakari hutafutamajibu yenye kuridhisha. “Ni jambo la msi-ngi kwa wanadamu kutafuta kusudi la uhai,”akasemaViktor Frankl, aliyekuwa profesa wamfumo wa neva na magonjwa ya akili. Kwaupande mwingine, tuna njaa ya kiroho amba-yo tunatamani kuitosheleza, yaani, njaa ina-yowapata wanadamu kwa sababu wao niviumbe wa pekee. Hata hivyo, ikiwa tumeu-mbwa na Mungu, je, ametupatia njia ya kuto-sheleza uhitaji wetu wa kiroho?

Yesu Kristo alijibu swali hilo aliposemakwamba: “Mwanadamu ataishi, si kwa mkatetu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywacha Yehova [au Mungu].” (Mathayo 4:4) Ma-neno yaYehova yaliyoandikwa kwenye Biblia,yametosheleza njaa ya kiroho ya mamilioniya watu, na yamewapa kusudi la uhai na tu-maini zuri la wakati ujao. (1 Wathesalonike 2:13) Biblia inaweza kukusaidia. Kwa kweli, ita-faa pia ukisoma kitabu hicho cha pekee. ˛

� Maswali kuhusu uumbaji na mageuzi yamezungumziwakwa kina katika broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? na Ma-swali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai zinazopatika-na kwenye www.jw.org/sw.

Je, Mageuzi niNadharia yaKisayansi?Ni nini kinachofanya nadharia iwe nadhariaya kisayansi? Kulingana na kitabu Encyclo-pedia of Scientific Principles, Laws, andTheories, nadharia ya kisayansi, kama vilenadharia ya Albert Einstein ya nguvu yauvutano, lazima iweze

1. Kuonekana

2. Kutokezwa kupitiamajaribio

3. Kukisia kwa usahihi

Kwa sababu hiyo, nadharia ya mageuziina msingi gani?� Utendaji wake hauwezikuonekana. Hauwezi kutokezwa. Na hauwe-zi kufanya makisio sahihi. Je, mageuzi ya-naweza kuonwa kuwa dhana ya kisayansi?Kitabu hicho cha encyclopedia kinaelezakuwa dhana ni “uchunguzi usio na uhakikawa mambo [zaidi ya nadharia],” unaokubali“kufanyiwa majaribio.”

� Tunaposema “mageuzi,” tunamaanisha “mageuzi makubwa,”kwa mfano, sokwe kubadilika na kuwa binadamu. “Mageuzimadogo” hurejelea mabadiliko madogo yanayotukia kwa wa-nyama na mimea labda kupitia kutokezwa kwa viumbe bora.

Amkeni! Agosti 2015 7

Page 8: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

KIKWAZOInaonekana kwamba mwanawako mwenye umri wa miaka sitahana sifa ya kujizuia. Anapoonakitu anachopenda, anataka ape-we wakati huohuo! Anapokasiri-ka mara nyingi yeye hukupiga-piga. Unajiuliza: ‘Je, ni kawaidakwa mtoto kutenda hivi?’ ‘Je, nihali tu ya muda, au ninapaswakumfundisha sifa ya kujizuia?’�

� Ingawa tunamzungumzia mtoto wa kiume,kanuni zinazotajwa katika makala hii zinawa-faa pia watoto wa kike.

MAMBO UNAYOHITAJI KUJUAMtazamo wa watu leo huathiri sifa ya kujizuia. Dakt. DavidWalsh anasema hivi: “Katika tamaduni nyingi zilizokubaliwa,watu wazima na watoto husikia kwa ukawaida ujumbe unaose-ma kwamba tunapaswa kufanya jambo lolote tunalotaka. Uju-mbe huo unaochochea watu kufanya lolote wanalotaka, huto-lewa na watu wenye nia njema ya kusaidia kuboresha maishaya watu na pia watu wenye nia ya kupata pesa tu.”�Ni muhimu kumfundisha mtoto mapema sifa ya kujizuia.Katika uchunguzi uliofanywa kwa muda mrefu, watafiti waliwa-pa watoto wenye umri wa miaka minne pipi moja-moja na ku-waambia kwamba wanaweza kuamua ama kula pipi hizomara moja au kusubiri kwa kipindi fulani kifupi ili wapewe pipinyingine ikiwa zawadi kwa sababu ya kuonyesha sifa ya subi-ra. Baadaye maishani, walipohitimu shule za sekondari, wato-to walioonyesha sifa ya kujizuia, walikuwa na hali nzuri kihisia,walikuwa na mahusiano mazuri na watu, na walifanya vizurikatika masomo kuliko wale waliokosa sifa hiyo.Kuna madhara makubwa ya kutowafundisha watoto sifaya kujizuia.Watafiti wanaamini kwamba ubongo wa mtotounaweza kuathiriwa na hali anazopitia. Dakt. Dan Kindlon,anafafanua jambo hilo hivi: “Tukiendekeza watoto wetu, tusi-poacha wajifunze kuwa na subira, tusipochelewa kuwapa wa-nachohitaji na kuwafundisha jinsi ya kupinga vishawishi, ma-badiliko ya mfumo wa neva unaohusianishwa kwa ukaribu naukuzi wa utu hayawezi kutokea.”�

� Kutoka kwenye kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Pa-rents Can Say It.� Kutoka kwenye kitabu Much of a Good Thing—Raising Children of Character inan Indulgent Age.

MSAADA KWA AJ I L I YA FAM I L IA � KULEA WATOTO

KuwafundishaWatoto Sifa yaKujizuia

r Pata msaada zaidi kwa ajili ya familia kwenye www.jw.org/sw

Page 9: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 9

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYAWeka mfano. Je, wewe hujitahidi kuwa na sifa ya kujizuia? Je,watoto wako hukuona ukiwa umekasirika kunapokuwa na fole-ni ya magari, ukishindwa kufuata utaratibu wa kusimama kati-ka foleni unapokuwa dukani, au ukiwakatiza wengine wanapo-zungumza? “Njia nzuri zaidi ya kuwasaidia watoto wetu kuwana sifa ya kujizuia ni kwa sisi wenyewe kwanza kujitahidi kuio-nyesha,” anaandika Kindlon.—Kanuni ya Biblia: Waroma 12:9.Wafundishe watoto kuhusu matokeo ya kutojizuia. Ikitege-mea umri wa mtoto, msaidie kuona kwamba kuna faida ana-pojizuia na hasara ya kutofanya hivyo. Kwa mfano, ikiwa mto-to wako amekasirika kwa sababu ya kutendewa isivyo haki namtu, msaidie atulie na ajiulize hivi: ‘Je, kulipiza kisasi kutani-saidia au kutaongeza tatizo? Je, kuna njia yoyote nzuri ya ku-shughulikia hali hii—labda kwa kuhesabu moja mpaka kumi nahivyo kuruhusu hasira ipungue? Je, huenda ikafaa zaidi nikio-ndoka?’—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:7.Mpongeze mtoto wako. Mpongeze mtoto wako anapoonye-sha sifa ya kujizuia. Mweleze kwamba huenda isiwe rahisi siku-zote kuonyesha sifa hiyo, hata hivyo anafanya vema kila maraanapoionyesha. Biblia inasema hivi: “Mtu asiyezuia roho yakeni kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta.” (Methali 25:28) Ki-nyume na hilo, “asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwa-namume mwenye nguvu.”—Methali 16:32.Tenda. Unaweza kumfundisha mtoto wako kwa kuwa na kipi-ndi cha maigizo chenye maswali kama vile: “Ungefanya Nini?”au “Maamuzi Mazuri, Maamuzi Mabaya” au jambo linginekama hilo. Zungumzieni hali mbalimbali zinazohusiana na ma-mbo hayo na jinsi ya kukabiliana nazo, kisha kuonyesha ikiwani “nzuri” au “mbaya.” Uwe mbunifu: Ukipenda, unaweza kutu-mia vikaragosi, michoro, au mbinu yoyote ili kufanya zoezi hiloliwe lenye kufurahisha na pia kufundisha. Lengo lako liwe ku-msaidia mtoto kutambua kwamba kujizuia ni bora kuliko kufa-nya mambo haraka-haraka.—Kanuni ya Biblia: Methali 29:11.Uwe na subira. Biblia inasema hivi: “Ujinga umefungwa pa-moja na moyo wa mvulana.” (Methali 22:15) Hivyo, usitarajiekwamba mtoto wako atasitawisha sifa ya kujizuia mara moja.“Hilo huchukua muda mrefu na maendeleo hufanyika polepo-le, makosa hujitokeza, na hatimaye mafanikio,” kinasema kita-bu Teach Your Children Well. Hata hivyo, jitihada hizo si zabure. Kitabu hicho kinaendelea kusema hivi: “Mtoto anayewe-za kujizuia, atakuwa na uwezo mkubwa wa kujiepusha nadawa za kulevya atakapokuwa na umri wa miaka kumi na mbiliau kujiepusha na ngono atakapokuwa na umri wa miaka kumina nne.” ˛

MAAND IKO MUH IMU

“Upendo wenu na uwe bila unafiki.”—Waroma 12:9.

“Lolote lile analopanda mtu,atavuna hilo pia.”—Wagalatia 6:7.

“Mtu mjinga huiachilia roho yakeyote, lakini mwenye hekimahuituliza mpaka mwisho.”—Methali 29:11.

MPONGEZE MTOTO KWAJITIHADA ZAKE

Watoto wadogo wanaweza kujifu-nza jinsi ya kujizuia. Kitabu Gener-ation Me kinasema hivi: “Ikiwamtoto analilia pipi dukani na ukaa-mua kumpatia, elewa kwambaunamfundisha kuwa kulia ni njiainayofaa ili kupata kile anachota-ka. Pindi nyingine atakapotaka kitufulani, atalia na kupiga kelele kwasababu kufanya hivyo kulimsaidiawakati uliopita. Badala yake, mpo-ngeze mtoto wako kila mara ana-poonyesha tabia nzuri. Wazaziwengi hushindwa kumvumilia mto-to anapolia kwa sababu wanagu-swa hisia haraka au wanashindwakumnyima mtoto anachotaka.Hata hivyo, haumsaidii mtotowako kwa kumtimizia madai yake.Unapompongeza mtoto anayeo-mba kitu kwa njia nzuri, unamsai-dia kuwa na uhusiano mzuri nawengine na pia kuonyesha sifa yakujizuia.”

Page 10: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

“Mwanadamu ana haki ya kujua kusoma na kuandika, hilo ni muhimu kwamaendeleo yake na ya jamii.”—UNESCO.�

RIPOTI zinaonyesha kwamba ulimwenguni pote watu zaidi ya milioni 700 walio na umriwa miaka 15 na zaidi hawajui kusoma na kuandika. Hivyo, hawawezi kujifunza mambo mengikama vile mwenendo unaofaa na mafundisho ya kiroho yaliyo katika Biblia ‘yaliyoandikwa ilikutufundisha sisi.’ (Waroma 15:4) Hivyo, katika nchi nyingi Mashahidi wa Yehova wanawafu-ndisha watu kusoma na kuandika kupitia programu yao ya kufundisha Biblia—bila malipo yo-yote. Je, programu hiyo imekuwa na mafanikio?

Fikiria kazi ya Mashahidi waYehova nchini Mexico, ambako lugha yao ya taifa ni Kihispa-nia. Tangu mwaka wa 1946, Mashahidi wamewafundisha watu zaidi ya 152,000 kusoma nakuandika, na baadaye wanafunzi hao walikuwa walimu. Kwa kutambua mchango wa kazi yao,Mashahidi wamepokea barua nyingi kutoka serikalini. Barua moja inasema hivi: “Bodi Kuuya Elimu inatambua na kuwapongeza kwa ushirikiano wenu mnaoonyesha katika kuendelezaProgramu ya Elimu ya Watu Wazima.”

� Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni.

Elimu ya Biblia Husaidia Watu KujuaKusoma na Kuandika

Page 11: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 11

Vijana kwa wazee wamenufaika kutokana na programu ya kuji-funza kusoma na kuandika. Kwa mfano, Josefina alikuwa na umri wamiaka 101 alipojiunga na programu hiyo na alifanikiwa kumaliza ma-somo yake baada ya miaka miwili!

Ijapokuwa lugha ya taifa nchini Mexico ni Kihispania, madarasa yakusoma na kuandika hayafanywi katika lugha hiyo peke yake. Katikamwaka wa 2013, vikundi nane vya watu wanaozungumza lugha zaoza asili, walijifunza kusoma na kuandika katika lugha hizo.

Kujua kusoma na kuandika kunaweza kukusaidia kujifunza ma-mbo mengi. Zaidi ya yote, ujuzi huo huwawezesha watu wa namnazote kuisoma Biblia—kitabu kilichoongozwa na roho ya Mungu ki-nachoweza kuwaweka watu huru kutokana na utumwa wa ushirikina,mafundisho ya kidini yasiyo ya kweli, na mwenendo usiofaa.—Yoha-na 8:32. ˛

%Mamilioni ya nakala za chapisho linalosaidiakujifunza kusoma na kuandika lenye kichwaJitahidi Kusoma na Kuandika zimechapishwakatika lugha zaidi ya 100

Daniel alijifunza Lugha ya Isharaya Mexico kupitia DVD

Daniel alikuwa kiziwi na haku-weza kuwasiliana vizuri. Maranyingi hali hiyo ilimfanya awemwenye hasira hata kuelekeafamilia yake. Daniel alipokuwana umri wa miaka 23 hivi, Sha-hidi kiziwi anayeitwa Josuealianza kujifunza Biblia pamo-ja naye, mwanzoni wakifanyahivyo kupitia ishara zisizo ras-mi, au ishara za mwili pamojana michoro. Baadaye, Danielalijifunza Lugha ya Ishara yaMexico kwa kutumia DVD.�

Kadiri Daniel alivyozidi kui-shi kulingana na mafundishoya Biblia, alivaa kile ambachoBiblia hukiita “utu mpya,”unaoonekana wazi kupitia sifakama vile, “fadhili, unyenyeke-vu wa akili, upole, na ustahi-milivu.” (Wakolosai 3:10, 12)Daniel alitii pia himizo la Bibliala kutii na kuheshimu wazazi.(Waefeso 6:1, 2) Familia yakeilishangazwa sana! Mama yaDaniel huku akitokwa na ma-chozi, alimshukuru Josue kwakumsaidia kiroho mtoto wake.Daniel alibatizwa na kuwaShahidi waYehova mwakawa 2007.

� Nchini Mexico, machapisho 46ya Mashahidi wa Yehova yanapatika-na kwenye DVD katika Lugha ya Isha-ra ya Mexico. Tovuti yetu ya jw.org,ina habari zinazopatikana katika lughaza ishara zaidi ya 80. Pia, kuna ma-chapisho yaliyo katika maandishi yavipofu.

ALIISHANGAZAFAMILIA YAKE(

Page 12: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

MAON I YA B IBL IA � UVUM I L IVU

U V U M I L I V UKukubali, kusamehe, na kuvumilia huleta amani. Hata hivyo, je, uvumilivuunapaswa kuwa na mipaka?

Ni nini siri ya kuwa mvumilivu?HALI ILIVYO LEO Ulimwenguni pote watu wa-nazidi kukosa sifa ya uvumilivu kwa sababuya ubaguzi wa rangi au jamii, taifa, kabila, nadini zenye imani kali.BIBLIA INASEMA NINI? Wakati wa hudumayake, Yesu Kristo aliishi miongoni mwa watuwaliokosa sifa ya uvumilivu.Wayahudi na Wa-samaria walichukiana. (Yohana 4:9) Wana-wake walidharauliwa na wanaume. Na vio-ngozi wa kidini Wayahudi waliwadharau watuwa kawaida. (Yohana 7:49) Hata hivyo, YesuKristo alikuwa na mtazamo tofauti sana.Wa-pinzani wake walisema hivi: “Mtu huyu huka-ribisha watenda-dhambi na hula pamojanao.” (Luka 15:2) Yesu alikuwa mwenye fadhi-li, subira, na mvumilivu kwa kuwa alikuja, sikuhukumu watu, bali kuwaponya kiroho. Upe-

ndo ndiyo sifa kuu iliyomchochea kufanyahayo yote.—Yohana 3:17; 13:34.

Upendo, sifa muhimu ili kuwa na uvumilivu,hutufanya tuwapende wengine kutoka moyo-ni licha ya kutokamilika au kasoro zao. Andi-ko la Wakolosai 3:13 linasema hivi: “Endeleenikuvumiliana na kusameheana kwa hiari ikiwayeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwi-ngine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ni-nyi kwa hiari, nanyi fanyeni vivyo hivyo pia.”

“Zaidi ya mambo yote, iweni na upendomkubwa ninyi kwa ninyi, kwa sababuupendo hufunika dhambi nyingi.”—1 Petro 4:8.

Yesu ni mfano mzuri wamtu mwenye uvumilivukwa kuwa alikuja, sikuhukumu watu, balikuwaponya kiroho

r Pata majibu ya maswali mengine ya Biblia kwenye www.jw.org/sw

Page 13: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 13

Kwa nini uvumilivu una mipaka?HALI HALISI Jamii nyingi zinajaribu kudumishasheria na utaratibu. Hivyo, huwawekea watuviwango vyenye usawaziko vya jinsi ya kujie-ndesha.BIBLIA INASEMA NINI? “[Upendo] haujiendeshibila adabu.” (1 Wakorintho 13:5) IjapokuwaYesu aliweka mfano mzuri katika kuvumilia,hakuunga mkono ukosefu wa adabu, unafiki,wala uovu wowote. Badala yake, alishutumukwa ujasiri mambo hayo. (Mathayo 23:13) Ali-sema hivi: “Kwa maana yule ambaye huzoeakufanya mambo maovu huchukia nuru [yakweli].”—Yohana 3:20.

Mtume Mkristo Paulo aliandika hivi: “Chu-kieni maovu, shikamaneni na mema.” (Wa-roma 12:9) Aliishi kulingana na maneno hayo.Kwa mfano, Wakristo fulani Wayahudi wali-pojitenga na waamini wasio Wayahudi, Pau-lo aliyekuwa Myahudi, kwa ujasiri na fadhili

alizungumzia hali hiyo. (Wagalatia 2:11-14)Alijua kwamba Mungu ambaye “hana uba-guzi,” hangevumilia kuona ubaguzi wa kijamiimiongoni mwa watu Wake.—Matendo 10:34.

Kwa kuwa ni Wakristo, Mashahidi wa Ye-hova hufuata mwongozo wa maadili unaopa-tikana katika Biblia. (Isaya 33:22) Hata hivyo,hawavumilii uovu miongoni mwao. Kutanikosafi la Kikristo linapaswa kutochafuliwa nawatu wasiofuata viwango vya Mungu. Kwasababu hiyo, Mashahidi wanatii mwongozohuu ulio wazi wa Biblia: “Ondoeni yule mtumwovu kati yenu.”—1 Wakorintho 5:11-13.

“Enyi mnaompenda Yehova, chukieniyaliyo mabaya.”—Zaburi 97:10.

Je, Mungu ataendelea kuvumilia uovu milele?MAONI YAWATUWENGI Uovu utaendelea ku-wapo kwa kuwa ni asili ya mwanadamu.BIBLIA INASEMA NINI Nabii Habakuki alisalihivi kwaYehova Mungu: ‘Kwa nini unaendeleakutazama taabu tupu? Na kwa nini kuna upo-raji na jeuri mbele yangu, kwa nini kugomba-na hutokea, kwa nini mzozo huendelezwa?’(Habakuki 1:3) Mungu alimhakikishia nabiiwake aliyekuwa na wasiwasi kwamba ange-waadhibu waovu. Mungu alisema hivi kuhu-siana na ahadi hiyo: ‘Bila shaka itatimia. Hai-tachelewa.’—Habakuki 2:3.

Hata hivyo, watenda maovu bado wananafasi ya kuacha mwenendo wao mbaya.“‘Je, ninapendezwa hata kidogo na kifo chamtu mwovu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu

Yehova, ‘bali kwamba ageuke na kuziachanjia zake, naye kwa kweli aendelee kuishi?’ ”(Ezekieli 18:23) Wale wanaomtafuta Yehovakwa kuacha njia zao mbaya wanaweza kuwana tumaini zuri la wakati ujao. Methali 1:33inasema hivi: “Mtu anayenisikiliza, yeye ata-kaa salama wala hatasumbuliwa na hofu yamsiba.” ˛

“Na bado muda kidogo tu, na mtumwovu hatakuwako tena. . Wapolewataimiliki dunia, nao watapatafuraha yao tele katika wingiwa amani.”—Zaburi 37:10, 11.

Page 14: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Je, madaktari waliwezakukusaidia ulipogunduliwana ugonjwa huo?Ijapokuwa kwa miaka mitatu hivi,nilikuwa chini ya uangalizi wa ma-daktari wawili, bado uti wangu wamgongo ulizidi kupinda. Hali iliku-wa mbaya sana kiasi cha kwa-mba uti wa mgongo ukaanza ku-songa moyo na mapafu yangu nakufanya iwe vigumu kupumua. Ni-lihitaji kufanyiwa upasuaji.

Je, ulikubali kufanyiwaupasuaji?Ndiyo. Hata hivyo, niliambiwakwamba upasuaji huo haungeku-wa rahisi. Kufikia wakati huo, utiwangu wa mgongo ulipinda kufi-kia nyuzi 116, kiwango ambachoni hatari sana kwa afya. Pia, kufa-nyiwa upasuaji kulitokeza changa-moto moja ya pekee. Kwa sababuya imani yangu inayotegemea

Biblia, mimi nisingekubali kutiwadamu mishipani.1

Je, ulipata daktari aliyekuwatayari kukutibu?Mimi na mama yangu tulimpatadaktari mmoja katika jimbo tulioi-shi la Florida, Marekani. Hata hi-vyo, nilipomwambia kwamba ni-ngependa kufanyiwa upasuaji bilakutiwa damu, alisema kwambahakuna daktari mpasuaji ambayeangekubali kufanya upasuaji huomgumu bila kunitia damu. Pia, ali-niambia kwamba huenda ninge-kufa kabla ya kufikisha umri wamiaka 20 ikiwa sitafanyiwa upa-suaji.Wakati huo nilikuwa na umriwa miaka 14.

Je, ulimwambia msingi waimani yako?Ndiyo. Nilimwambia kwamba ima-ni yangu inategemea Biblia, nakwamba Mungu anaiona damu

kuwa takatifu iwe ya mwanadamuau mnyama.2 Mwisraeli angeuawaikiwa angekula damu!3 Nilimwo-nyesha pia andiko la Matendo 15:19, 20. Kwa sehemu, andiko hilo li-nawaagiza hivi Wakristo: ‘Jiepu-sheni . . . na damu.’ Hilo linamaa-nisha kwamba damu haipaswikuwekwa katika mwili wa mtu kwanjia yoyote ile, iwe kwa kutiwa mi-shipani au kuliwa.

Daktari mpasuaji alisemaje?Aliendelea kusisitiza kwambabado angehitaji kunitia damu mi-shipani. Nilishangazwa pia kwa-mba hospitali ilisema, ikiwa ninge-kubali kutiwa damu, nisingelipiagharama za upasuaji.

Hiyo ilikuwa nafasi nzuri!Wewe na mama yako mlifanyanini?Ingawa hakuna mtu aliyekuwa ta-yari kufanya upasuaji bila damu,

Alishikamana na Imani YakeMahojiano na Song Hee Kang

Song Hee alipokuwa na umri wa miaka 11, mama yakealigundua kwamba mgongo wa binti yake umepinda.Daktari aligundua kwamba ana ugonjwa wa mgongouliopinda, yaani uti wake wa mgongo umepinda kamaherufi “C” au “S.” Hali ya Song Hee ilizidi kuwa mbayakiasi cha kwamba alihitaji kufanyiwa upasuaji. Hata hi-vyo, Song Hee alikataa kutiwa damu mishipani. Gazetila “Amkeni” lilimhoji Song Hee.

Page 15: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

Amkeni! Agosti 2015 15

tuliazimia kushikamana na imaniyetu. Mambo yakawa magumuhata zaidi. Kulingana na sheria,nilikuwa bado mtoto. Kwa kuwahali ya afya yangu ilizidi kuwambaya, kesi yangu ilipelekwa ma-hakamani. Hata hivyo, tulishukurusana wakili wa jimbo la Florida ali-potupatia siku 30 za kutafutadaktari mpasuaji atakayekubalikufanya upasuaji bila damu.

Je, mlipata daktari?Ndiyo! Kwa fadhili, Halmashauriya Uhusiano na Hospitali (HLC)ya Mashahidi waYehova iliyo kati-ka jimbo letu iliwasiliana na mtaa-lamu wa kutibu ugonjwa wa mgo-ngo uliopinda katika jimbo la NewYork aliyekuwa mtazamo tofautina aliyekubali kuniona. Hivyo, tuli-weza kutii amri ya mahakama.4

Matokeo yalikuwaje baada yakufanyiwa upasuaji?Upasuaji ulifanikiwa! Ili kunyooshauti wa mgongo wangu, Daktari

Robert M. Bernstein, aliingiza ka-tika mgongo wangu vyuma vidogovinavyoweza kurekebishwa. Alini-fanyia upasuaji mara mbili katikakipindi cha majuma manne.

Kwa nini alifanya upasuaji kwahatua mbili?Ikiwa kwa sababu ya upasuajiwa mara ya kwanza ningepotezadamu nyingi sana, kipindi cha ma-juma mawili kingefaa kuupa mwiliwangu muda wa kuzalisha che-mbe nyekundu za damu kabla yakufanyiwa upasuaji wa pili. Hatahivyo, katika upasuaji wote huo,nilipoteza damu kidogo. Ninaishu-kuru timu ya madaktari wapasua-ji waliokuwa na mipango mizuri,ustadi, na uangalifu mkubwa. Nili-pona vizuri bila kuwa na matatizoyoyote ambayo huenda ningepataikiwa ningetiwa damu mishipani.5

Daktari aliyekufanyia upasuajialihisije baada ya kuona haliyako?Alifurahi sana! Alisema hivi: “Ma-tibabu si kufanya upasuaji tu.”Aliendelea kusema kwamba ana-hisi kwamba madaktari wanapa-swa kufikiria kikamili hali ya mgo-njwa kutia ndani imani naviwango vyake. Watu wengineambao si Mashahidi wa Yehova,wanakubaliana na maoni hayo. ˛

1. Mama ya Song Hee ni Shahidi waYehova. SongHee pia ni Shahidi waYehova na alibatizwa mwa-ka wa 2012, akiwa na umri wa miaka 16.2. Mwanzo 9:3-5.3. Mambo yaWalawi 17:10-14.4. Halmashauri ya Uhusiano na Hospitali huwa-saidia Mashahidi walio wagonjwa kutafuta mada-ktari walio tayari kuwatibu bila kutumia damu.5. Katika makala yake kuhusu madhara ya kutiwadamu mishipani, Clinical Excellence CommissionNew South Wales (Australia) Health, inasemahivi: “Kutiwa damu mishipani ni sawa na kupandi-kiza tishu iliyo hai katika mwili. Kwa asili, mwili wabinadamu hukataa kitu chochote kipya kinacho-wekwa katika mwili. Ni muhimu sana kulinda halinjema ya mwili.”

Madaktari wanapaswa kufikiria kikamili hali ya mgonjwa

˙ Ugonjwa wa uti wa mgongo uliopinda� hausababishwi na mkaombaya au ukosefu wa madini ya kalisi

˙ Ugonjwa wa uti wa mgongo hauambukizwi˙ Vifaa vya kutegemeza uti wa mgongo haviwezi kuunyoosha lakini

vinaweza kuzuia uti wa mgongo usiendelee kupinda˙ Upasuaji wa uti wa mgongo uliopinda haudhuru uwezo wa kupata

mtoto˙ Hakuna kinga inayojulikana ya magonjwa ya uti wa mgongo˙ Uvutaji wa sigara huzuia kupona kwa mifupa

� Vyanzo: Spinal Deformity: Scoliosis and Kyphosis—A Handbook for Patients; “Diseasesand Conditions—Scoliosis,” kilichochapishwa na Mayo Clinic Staff, Mayo Clinic, U.S.A.

UKWELI WA MAMBO KUHUSUUTI WA MGONGO ULIOPINDA

UTI WA MGONGO WA KAWAIDA

UTI WA MGONGO ULIOPINDA

Page 16: Chembe Zako MAKTABA ILIYO HAI!

g1

5 0

8-S

W1

50

81

2sPakua gazetihili na matoleoyaliyotanguliabila malipo

Biblia inapatikanakwenye Intaneti katikalugha zaidi ya 100

Tumia alama hiikufungua Tovutiyetu au utembeleewww.jw.org/sw

no

p

KWA MUDA mrefu, imedhaniwa kwambawanadamu ndio waliogundua mfumo wa

gia. Hata hivyo, mawazo hayo yamethibiti-shwa kuwa si ya kweli! Hivi karibuni, mfumowa gia zinazofanya kazi kwa pamoja umegu-nduliwa katika mdudu mchanga anayeitwaIssus, anayepatikana katika bustani nyingibarani Ulaya.�

Panzi huyo anapokuwa mchanga anawezakuruka kwa mwendo kasi wa mita 3.9 kwa se-kunde chache tu, na kujirusha karibu mara200 zaidi ya nguvu za uvutano! Anaweza ku-toroka kwenye upeo wa macho ukipepesa ji-cho tu. Ili aweze kuruka, miguu miwili yanyuma ya mdudu huyo inahitaji kutoke-za msukumo uleule sahihi na kwa wakatimmoja. Ni nini siri ya usahihi huo?

Fikiria hili: Wanasayansi wamegundua mi-fumo miwili ya gia zinazoungana chini ya mi-guu ya nyuma ya kiumbe huyo. Panzi huyoanaporuka, gia hizo husaidia miguu yake mi-wili ifanye kazi kwa usahihi na upatano. Isi-ngekuwa hivyo, asingeweza kuruka kwa njianzuri!

� Gia hizo huacha kufanya kazi anapokomaa.

Viumbe wakubwa wanaporuka hutegemeamfumo wa neva kupatanisha miguu yao. La-kini, kwa panzi huyo, msukumo huo wa nevaungekuwa na kasi ndogo sana. Hivyo ndiosababu mdudu huyo ana mfumo wa gia.“Kwa kawaida sisi tunafikiria gia kuwa kitu fu-lani tunachokiona katika mashine ambazomwanadamu ameunda,” alisema mtunzi namtafiti Gregory Sutton. Kisha akaongezeasababu kwa kusema hivi: “Hatukuwa tume-chunguza [kila mahali] kwa ukamili.”

Una maoni gani? Je, mfumo wa gia wa pa-nzi anayeitwa Issus ulitokana na mageuzi?Au ulibuniwa? ˛

J E , N I KAZ I YA UBUN I?

Mfumo wa Gia wa PanziAnayeitwa Issus

Leafhopper photo: Image � Sue Robinson/Shutterstock; gears: Courtesy Burrows and Sutton, University of Cambridge, UK