12
Ofisi ya Mawasiliano Serikalini inapokea habari za matukio mbalimbali kwa ajili ya News Bullettin hii ya Wizara ya Nishati na Madini Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263 au Fika Ofisi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: [email protected] HABARI ZA NISHATI &MADINI Toleo No. 90 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Oktoba 23 - 29, 2015 Bulletin News http://www.mem.go.tz Soma habari Uk. 2 Serikali kukomesha uchimbaji, uuzaji haramu madini UMEME waongezeka Gridi ya Taifa Mitambo ya kuzalisha umeme Kinyerezi I

MEM 90 Online.pdf

Embed Size (px)

Citation preview

Ofisi ya Mawasiliano Serikalini inapokea habari za matukio mbalimbali kwa ajili ya News Bullettin hii ya Wizara ya Nishati na Madini

Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263 au Fika Ofisi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: [email protected]

Habari za nisHati &madini

Toleo No. 90 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Oktoba 23 - 29, 2015

BulletinNews

Ofisi ya Mawasiliano Serikalini inapokea habari za matukio mbalimbali kwa ajili ya News Bullettin hii na Jarida la Wizara ya Nishati na Madini

Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263 au Fika Ofisi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: [email protected]

http://www.mem.go.tz

HABARI ZA NISHATI &MADINI

Toleo No. 51 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Tarehe - 23-29 Januari , 2015

JWTZ wapongezwa kunusuru mtambo wa Msimbati-Uk4

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, anayeshughulikia Madini Stephen Masele

Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Charles Kitwanga

Mkurugenzi Mtend-aji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Dk. Lutengano Mwakahesya

Wabunge Soma habari Uk. 2

Waimwagia sifa MEM, TANESCO, REA

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AZINDUA RASMI BODI YA TANESCO -Uk2

Soma habari

Uk. 2Serikali kukomesha uchimbaji, uuzaji haramu madini

UMEME waongezeka Gridi ya Taifa

Mitambo ya kuzalisha umeme Kinyerezi I

2 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

Zuena Msuya na Nuru Mwasampeta S

hirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limewasha mtambo mwingine wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa kiasi cha Megawati 35 na

hivyo kufikisha jumla ya Megawati 70 zinazozalishwa kutokana na gesi

asilia inayotoka Madimba hadi kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi I jijini Dar es salaam. Megawati 35 za awali ziliwashwa mnamo tarehe 17 Septemba, 2015.

Akizungumza kituoni hapo Meneja mradi wa Kinyerezi I, Mhandisi John Mageni amesema mtambo huo umewashwa ili kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme nchini kwa kuwa hivi sasa vyanzo vya maji vinavyotegemewa kuzalisha umeme vimeanza kukauka kutokana na ukame.

“Huduma ya umeme itaendelea kuimarika kwani sasa tunawasha mtambo namba 3 baada ya kukamilika kwa kuufanyia majaribio yote na kuridhika nayo kwamba uko tayari kuanza kazi ya uzalishaji wa umeme na hivyo kuongeza kiwango cha umeme unaoingia katika gridi ya taifa,” alisema Mageni

Aliongeza kuwa kwa sasa mkoa

wa Dar es Salaam unapata umeme wa uhakika baada ya kuwasha ule mtambo wa kwanza wa megawati 35, hivyo zoezi la kuwasha mitambo iliyosalia ili kufikisha Megawati 150 litaendelea ili kuimarisha huduma ya upatikanaji wa umeme nchini nzima.

Alisema pindi mitambo yote itakapowashwa katika kituo hicho itakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme kiasi cha megawati 150, ambazo zimeanza kuingizwa katika gridi ya taifa.

Kituo cha Kinyerezi 1 kilizinduliwa tarehe 13 Oktoba, 2015 na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ambaye aliitaka Tanesco kuongeza kasi ya kuzalisha umeme unaotosheleza mahitaji ya Watanzania.

Mitambo miwili kati ya minne inayokamilisha Kinyerezi 1 imewashwa na miwili iliyosalia itaendelea kuwashwa kadri siku zinavyoendelea.

Megawati 35 zaongezwa Kinyerezi I

Mohamed Saif na Clinton Ndyetabula

Imeelezwa kwamba Serikali imejizatiti katika kuhakikisha inakomesha uchimbaji na uuzaji haramu wa rasilimali ya madini yaliyopo nchini kwa manufaa ya

sasa na ya vizazi vijavyo.Hayo yameelezwa hivi karibuni

na Kamishna Msaidizi wa Madini sehemu ya Leseni, Mhandisi John Nayopa kwa niaba ya Kamishna wa Madini wakati wa ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa mpango wa kupambana na uchimbaji haramu wa rasilimali kwa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ujulikanao kama ICGLR Regional Initiative Against Illegal Exploitation of Natural Resources (RINR).

Mhandisi Nayopa alisema lengo la warsha hiyo ni kufafanua hatua ya utekelezaji wa mpango wa RINR kwa kuzingatia mazingira ya Tanzania; kuongeza uelewa wa wadau kuhusu

mpango wa RINR, na kuandaa mpango kazi sahihi ikiwa ni pamoja na mkakati wa utekelezaji wa RINR nchini.

Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi 12 za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ambazo zimeridhia itifaki zenye lengo la kuimarisha amani, utulivu, demokrasia na utawala bora kwenye nchi husika.

Alisema Wakuu wa Nchi 11 za Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) walikutana jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba, 2014 na kukubaliana kwa pamoja kuimarisha maendeleo, usalama na utulivu jambo ambalo anasema linathibitisha dhamira yao ya kubadilisha ukanda wa Maziwa Makuu kuwa na amani endelevu kwa mataifa hayo na kwa wananchi wake, ikiwemo utulivu wa kisiasa na kijamii na ukuaji wa maendeleo ya pamoja.

Mhandisi Nayopa alisema makubaliano hayo yanaitwa Tamko la Dar es Salaam, la Mwaka 2014

ambayo yanajulikana kama The Dar es Salaam Declaration of 2014.

“Ili kufanikisha hili, nchi za ICGLR zilisaini makubaliano ambayo yalizaa itifaki mbalimbali na miongoni mwake ni itifaki ya kupambana na uchimbaji haramu wa madini,” alisema Mhandisi Nayopa.

Alisema kwamba mojawapo ya changamoto kuu kwenye baadhi ya nchi za ICGLR ni kukithiri kwa uchimbaji haramu wa madini jambo ambalo linatumika kuchochea migogoro na pia ni chanzo cha fedha kwa wababe wa kivita.

Mhandisi Nayopa alisema Tanzania imejaaliwa rasilimali nyingi ambazo zinapasa kuleta maendeleo endelevu kwa jamii na Taifa kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi utakaoleta mabadiliko chanya.

“Licha ya mafanikio ambayo Tanzania imekuwa nayo katika kuvutia uwekezaji mkubwa katika Sekta ya Madini na katika kurasimisha idadi

kubwa ya wachimbaji wadogo, bado inakabiliwa na changamoto lukuki,” alisema.

Alisema kupitia Mpango huo wa RINR, Serikali inatarajia matokeo makubwa yenye tija katika kupambana na uchimbaji haramu wa madini yaliyopo nchini. “Lengo letu na matarajio yetu ni kwamba faida zitokanazo na uchimbaji madini zitaongezeka maradufu na hivyo jamii kwa ujumla kunufaika,” alisema Mhandisi Nayopa.

Warsha hiyo ya siku mbili imehudhuriwa na Kamishna Wasaidizi wa Madini kutoka Kanda mbalimbali, watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini hususan kutoka Idara ya Madini, wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani, wawakilishi wa wachimbaji wadogo na washirika wa Maendeleo wa Canada wajulikanao kama Partnership Africa Canada (PAC).

Kamishna Msaidizi wa Madini, Sehemu ya Leseni, Mhandisi John Nayopa katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha. Wa kwanza kushoto waliokaa ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Mrimia Mchomvu na wa kwanza kulia ni Mwakilishi kutoka PAC, Stephen Turyahikayo.

Serikali kukomesha uchimbaji, uuzaji haramu madini

Washiriki wa warsha wakifuatilia uwasilishaji mada kuhusu utekelezaji wa mpango wa kupambana na uchimbaji haramu wa rasilimali kwa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ujulikanao kama ICGLR Regional Initiative Against Illegal Exploitation of Natural Resources (RINR).

3BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

TahaririMEM

Na Badra Masoud

Five Pillars oF reForms

KWa HaBari PiGa simU KitenGo cHa maWasiliano

Bodi ya uhariri

MharIrI Mkuu: Badra MasoudMsaNIfu: Lucas Gordon

WaaNdIshI: Veronica simba, asteria Muhozya, Greyson Mwase Teresia Mhagama, Mohamed saif, rhoda James ,

Nuru Mwasampeta na Zuena Msuya

increase eFFiciencyQUality delivery

oF Goods/service

satisFaction oF tHe client

satisFaction oF BUsiness Partners

satisFaction oF sHareHolders

tel-2110490FaX-2110389

moB-0732999263

Makubwa yamefanyika sekta ya Nishati

tel-2110490FaX-2110389

moB-0732999263

Tuzungumzie Gesi Asilia

Wengi tutakumbuka wakati Rais wa Awamu ya Nne Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete alipoingia madarakani mwishoni mwa mwaka 2005 nchi yetu ilikuwa katika mgawo wa umeme na hadi ilipoingia mwaka 2006 mgawo huo wa umeme uliendelea kuwa mkali.

Mgawo huo ulitokana na kukauka kwa Mabwawa ambayo yanatumika kuzalisha umeme ambayo kwa kipindi hicho ndiyo yalikuwa chanzo kikubwa na pekee cha kuzalisha umeme.

Baadhi ya watafiti na wana mazingira walieleza kwamba kukauka kwa mabwawa hayo kunatokana na sababu kubwa mbili ambazo ni mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kilimo kinachofanywa na baadhi ya watu katika vyanzo vya maji (upstream) ambapo huchepusha maji na kushindwa kufuata mkondo wake.

Kutokana na mgawo huo wa umeme Serikali hiyo ya Awanu ya Nne kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuchukua hatua za makusudi na madhubuti kuanza kukabiliana na hali hiyo ya mgawo na kipaumbele kikiwa ni kujenga mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia nishati mbadala hususan gesi asilia.

Serikali iliruhusu Kampuni binafsi kuchimba gesi na kusafirisha pamoja na kuwauzia Makampuni binafsi, viwanda na TANESCO ili TANESCO nayo iweze kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia.

Ilipofika mwaka 2008 Serikali ilikamilisha ujenzi wa mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Ubungo I wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 102.

Mwaka 2009 mtambo mwingine ulikamilika wa Tegeta wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 45 na mwaka 2012 Serikali ilizundua mtambo wa Ubungo II (Megawati 105). Mitambo yote hiyo inazalisha umeme kwa kutumia gesi asilia na inamilikiwa na Serikali kwa asilimia mia moja.

Serikali pia ilijenga mitambo mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia ya Mtwara (Megawati 18) na Somangafungu mkoani Lindi (Megawati 7.5).

Ili kuwa na umeme wa uhakika katika gridi ya taifa kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa, Serikali ilijenga pia mtambo mwingine wa kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta mazito wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 60 uliopo Nyakato, Mwanza.

Kutokana na gesi asilia kugundulika kwa wingi katika mikoa ya Kusini mwa Tanzania yaani Lindi na Mtwara, Serikali iliamua kujenga bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara na Lindi pamoja na mitambo ya kuchakata ambapo gesi hiyo inazalisha na kusafirishwa hadi kwenye mitambo ya kuzalisha umeme kwani gesi inayozalishwa na kuuzwa na watu binafsi haitoshelezi katika kuzalisha umeme.

Aidha, kutokana na bomba la gesi kujengwa na mitambo yake, Serikali iliona ni busara kujenga mtambo wa Kinyerezi I wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 150.

Mitambo yote ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia iliyojengwa na Serikali tangu mwaka 2008 hadi sasa 2015 imefikia jumla ya Megawati 484.5 ya umeme wote unaozalishwa na mitambo hiyo ya Serikali kupitia TANESCO. Hayo ni mafanikio makubwa katika sekta ya Nishati katika kipindi cha Serikali ya Awanu ya Nne.

Pamoja na kwamba Serikali ya Awanu ya Nne inaondoka madarakani mwishoni mwa mwaka huu lakini imeacha misingi mizuri na jitihada kubwa za kuendelea kuboresha sekta ya nishati hususan katika kuzalisha umeme.

Ni ukweli ulio wazi kwamba kukamilika kwa mtambo wa Kinyerezi I ndiyo mwanzo wa kuanza kwa ujenzi wa mitambo mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia ya Kinyerezi II, Kinyerezi III na Kinyerezi IV kwani zipo kila dalili za kuandaa na kuendelea kwa ujenzi huo kuwapo kwa eneo lenyewe ambapo mitambo hiyo itajengwa na wahusika wameshaanza kazi.

Hivyo tuna kila sababu ya kuipongeza Serikali ya Awanu ya Nne inayoongozwa na Mhe. Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete kwamba imefanya juhudi kubwa katika kuhakikisha kwamba upatikanaji wa umeme unaongezeka ili Taifa la Tanzania litakapofika mwaka 2025 liwe ni taifa la uchumi wa kati na mafaniko hayo yote yatatokana na kuwapo kwa umeme wa kutosha na wa uhakika.

Hii ni dhahiri kwamba maendeleo ya nchi yoyote duniani yanatokana na upatikanaji wa umeme wa uhakika hivyo lazima wote tutambue kwamba bila umeme hakuna maendeleo hivyo, umeme ni maendeleo.

Kurasa hii inakupa fursa ya kuongeza uelewa kuhusu masuala yanayohusu sekta ndogo ya gesi nchini.

Yaliyoandikwa katika kurasa hii ni baadhi tu ya maswali ambayo yamekuwa yakiwatatiza wananchi.

Gesi asilia ni nini?Gesi asilia ni mchanganyiko wa molekuli

nyepesi za Carbon na Hydrogen mfano methane (CH4), Ethane (C2H6). Gesi asilia inatokana na kuoza kwa mata ogania (organic matter) kama vile uozo wa masalia ya mimea na wanyama miaka mingi iliyopita.

Ni kiasi gani cha gesi asilia kimegunduliwa hapa nchini? Kiasi cha gesi asilia kilichogunduliwa hadi

hivi sasa ni futi za ujazo trilioni 55.08 (Gas initially in place- kabla ya kuhakikiwa kiasi kamili kinachoweza kuvunwa). Kati ya hizo, futi za ujazo trilioni 47.08 ni kutoka vitalu vya kina kirefu cha bahari na futi za ujazo trilioni 8 ni kutoka vitalu vya nchi kavu.

Kwanini gesi asilia imepelekwa jijini Dar es Salaam na sio kubaki kwenye Mikoa

ya Lindi na Mtwara?Kwanza kabisa, kujenga miundombinu

hiyo kuliangaliwa uhitaji mkubwa wa gesi asilia ulipo nchini, kama viwanda, kuzalisha umeme na kadhalika.

Pili, uwepo wa miundombinu ya bomba

la gesi kwenda Dar es Salaam, hainyimi fursa kwa Mikoa ya Kusini kutonufaika na gesi asilia. Ikumbukwe kuwa mwaka 2006 kulijengwa Kituo cha kuzalisha umeme kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara ambapo kituo hicho kinatumia gesi inayozalishwa Mnazi Bay, Mkoani Mtwara. Vilevile, miundombinu hiyo kwenda Dar es Salaam imejengwa kitaalam kuruhusu kutoa gesi asilia kwenda kila sehemu soko litakakopatikana. Mfano, ni uwepo wa kiwanda cha Saruji cha Dangote Mkoani Mtwara ambacho kinatarajiwa kutumia gesi asilia.

Je, kuna ukweli gani kwamba makampuni ya mafuta na gesi asilia yaliyogundua gesi katika kina kirefu

cha bahari yameshaanza kuvuna gesi asilia na kusafirisha nchi za nje?

Hapana, makampuni ambayo mpaka sasa yamefanikiwa kufanya ugunduzi wa gesi asilia katika tafiti za mafuta na gesi kwenye kina kirefu cha bahari ni BG, Statoil na washirika wake. Kwa sasa makampuni haya kwa kushirikiana na Serikali yapo kwenye mazungumzo ya kutafuta eneo la kujenga mradi wa kubadili gesi kuwa kimiminika “LNG” (Liquefied Natural Gas). Mradi huu utasaidia upatikanaji wa nishati ya gesi nchini, pamoja na kuuza gesi asilia nchi za nje na kuingizia Serikali fedha za kigeni ili kuchochea ukuaji wa uchumi. Kwa sasa hakuna uuzwaji wowote unaofanywa na Meli kwenda nje ya nchi.

Mitambo ya kuchakata Gesi Asilia, Madimba Mtwara

4 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava (wa tano kulia) na Balozi wa Brazili nchini Fransisco, Carlos Luiz (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na Wanafunzi 15 waliohitimu mafunzo ya lugha ya Kireno. Wanafunzi 7 kati yao walipata ufadhili wa kusoma masuala ya mafuta na gesi katika ngazi za Shahada ya Uzamili na Uzamivu nchini Brazil mwezi Machi, mwaka 2015.

Watanzania waliopata ufadhili wa masomo nchini China mwaka 2014, katika ngazi ya shahada ya uzamili na uzamivu katika fani ya mafuta na gesi wakiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (aliyekaa) na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi (wa nne kutoka kushoto mstari wa nyuma) pamoja na watendaji wengine wa Wizara ya Nishati na Madini mara baada ya kuagwa rasmi katika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini.Wengine katika picha (mstari wa mbele) ni Kamishna Msadizi Nishati anayeshughulikia Umeme, Mhandisi Innocent Luoga (wa kwanza kulia), Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi Utawala – Bi. Caroline Musika (wa kwanza kushoto).

Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene (kushoto) akimkabidhi mmoja wa wanafunzi nyaraka za masomo kwenda nchini China. Anayeshuhudia katikati ni Kamishna Msadizi anayeshughulikia maendeleo ya nishati, James Andilile, Agosti 5, 2015.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi akiwa na wanafunzi waliopata ufadhili wa masomo kupitia Wizara ya Nishati na Madini kusoma Shahada za Uzamili na Uzamivu katika masuala ya mafuta na gesi nchini China.Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu Lusius Mwenda na wa tatu kulia ni Kamishna Msadizi anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile, mwaka 2015.

Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene (kulia) akizungumza na wanafunzi 22 waliopata Ufadhili wa Masomo kupitia Serikali ya Watu wa China kusoma Shahada za Uzamili na Uzamivu kuhusu masuala ya mafuta na gesi nchini China.Hafla ya kuwakabidhi nyaraka za masomo ilifanyika mwezi Agosti, 2015

UFADHILI WA MASOMOTUMEWEZA

5BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda akikabidhi hundi za mikopo kwa wachimbaji wadogo. Mwaka 2013 Serikali ilianza utaratibu wa kutoa mikopo ya masharti nafuu na ruzuku kwa wachimbaji wadogo kupitia Benki ya Maendeleo ya TIB. Hundi za awamu ya kwanza za ruzuku hiyo zenye jumla ya Dola za Marekani 537,000 sawa na shilingi milioni 880.68 zilikabidhiwa mwezi Aprili, 2014 na Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Pinda kwa miradi 11.

Mjasiriamali anayejihusisha na biashara ya vito vya madini kwa kukata, kusanifu na kuuza, Susie Kennedy kutoka Arusha, akipokea mkataba kutoka kwa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene wakati wa mafunzo kwa waliopata ruzuku awamu ya pili ya kuendeleza uchimbaji madini mdogo. Wengine pichani kutoka Kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Sehemu ya Leseni, Mhandisi John Nayopa, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Fedha za Serikali kutoka Benki ya Maendeleo ya TIB, Prisca Chang’a na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA), John Bina. Mafunzo hayo ya siku mbili yalifanyika mjini Dodoma Oktoba 7 na 8, 2015.

Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (wa pili kutoka kulia – waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wachimbaji madini wadogo kutoka Kanda ya Kaskazini waliopata ruzuku awamu ya pili kwa ajili ya kuendeleza uchimbaji madini mdogo.Ruzuku ya awamu ya pili ya kiasi cha shilingi bilioni 7.2 ilitolewa kwa vikundi 111 vya wachimbaji wadogo na watoa huduma mbalimbali katika sekta ya madini.

UTOAJI RUZUKUTUMEWEZA

6 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

Na Veronica Simba

Hivi karibuni, Wizara ya Nishati na Madini iliendesha mafunzo maalum kwa wachimbaji madini ambao miradi yao

ilichaguliwa kupata ruzuku ya Serikali kwa ajili ya kuendeleza uchimbaji mdogo.

Miradi iliyochaguliwa kwa ajili ya kupata ruzuku ilikuwa ya aina mbalimbali na pia ilihusu jinsia zote. Miradi hiyo ni pamoja na ile ya uchimbaji madini, utoaji wa huduma za kiufundi, uchenjuaji madini, usanifu wa vito na pia huduma za mama lishe migodini.

Mafunzo hayo yalilenga kuwawezesha wachimbaji madini wadogo nchini kuendeleza shughuli zao kwa tija na yalihitimishwa kwa utoaji mikataba ya wachimbaji madini wadogo waliopata ruzuku kutoka Serikalini awamu ya pili.

Mambo mbalimbali yalijadiliwa na washiriki wa mafunzo hayo ambapo baadhi ya washiriki waliipongeza Serikali kwa kuwashirikisha wanawake kwa upana zaidi katika uwezeshaji wa shughuli za uchimbaji mdogo.

Kufuatia pongezi hizo, nilitamani pia kupata mtazamo wa washiriki wa semina ikiwa Sera ya Madini ni Mkombozi wa wanawake wachimbaji wa madini kwa kuwa kundi hili ni mhimili wa maendeleo ya jamii yoyote.

Katika kutafuta jibu la swali hilo, nilizungumza na wadau mbalimbali, na hususan wanawake wawili kutoka Merelani, waliojitambulisha kama Pili Hussein na Susie Kennedy.

Nilivutiwa kuzungumza kwa kirefu na Pili Hussein ambae ni mama wa

makamo, na alikuwa na historia ya pekee katika uchimbaji wa madini ya Tanzanite tokea mwaka 1988 katika eneo la Merelani, Mkoani Manyara.

Pili anasema wakati akianza shughuli za uchimbaji, jamii kwa wakati huo iliichukulia shughuli hiyo kuwa ya wanaume pekee hivyo yeye alilazimika kujificha kwa kivuli cha mwanaume akitumia jina la bandia la ‘Mjomba Hussein’.

“Nililazimika kuiaminisha jamii iliyonizunguka katika kazi zangu kuwa mimi ni mwanaume na siyo mwanamke ili niweze kukubalika kufanya kazi hiyo,” anasema mama huyo.

Anasema alilazimika kuchanganyika na wanaume katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuvaa mavazi ya kiume muda wote, kuvuta sigara, na mambo mengine kadhaa ambayo ni aghalabu kwa mwanamke kufanya. “Hata jina la Mjomba Hussein lilianza wakati huo,” anasema Pili.

Pili au ‘Mjomba Hussein’, anawakilisha wanawake katika jamii yetu ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikatishwa tamaa kutokana na mitazamo hasi ya baadhi ya watu hivyo kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo kwa dhana kuwa kazi hizo zinafaa kufanywa na wanaume tu.

Aidha, kutokana na Sera za miaka ya nyuma, hasa wakati wa ukoloni kutotambua rasmi uchimbaji mdogo, suala la ubaguzi wa jinsia lilikuwa na nguvu zaidi kwa kuwa uchimbaji ambao ulionekana kuwa haramu ulihitaji wanaume wenye kuweza kupambana na Serikali ilipobidi.

Ni jambo la kutia faraja kuwa Serikali imekuwa ikipambana na mitazamo na dhana hizo potofu zilizojengeka kwa muda mrefu katika jamii yetu

kwa kuwajengea mazingira wezeshi wanawake ili waweze kufanya kazi mbalimbali za kujiletea maendeleo pasipo kuwa na hofu ya aina yoyote.

Wizara ya Nishati na Madini mathalani, imekuwa ikifanya jitihada za kuwawezesha wanawake kushiriki katika shughuli mbalimbali zinazohusu sekta husika ikiwa ni pamoja na uchimbaji mdogo wa madini.

Katika awamu hii ya pili ya utoaji ruzuku, Serikali imepanua zaidi wigo ambapo imetenga takribani Shilingi za Kitanzania bilioni 7.2 kwa vikundi 111 vya wachimbaji wadogo na watoa huduma mbalimbali katika sekta ya uchimbaji madini mdogo ukilinganisha na Dola za Marekani 500,000 sawa na takribani Shilingi za Kitanzania bilioni moja zilizotolewa kwa waombaji 11 katika awamu ya kwanza.

Kwa mujibu wa Kamishna Msaidizi wa Madini, Sehemu ya Leseni, Mhandisi John Nayopa, utoaji ruzuku katika awamu ya pili umehusisha wachimbaji wadogo pamoja na watoaji huduma

mbalimbali katika sekta husika tofauti na ilivyokuwa katika awamu ya kwanza iliyofanyika katika Mwaka wa Fedha 2013/14 ambapo Wizara iliwalenga wachimbaji madini wadogo pekee.

Mhandisi Nayopa anafafanua zaidi kuwa, watoa huduma katika uchimbaji madini mdogo walionufaika na ruzuku awamu ya pili ni pamoja na vikundi vya wanawake wanaotoa huduma ya chakula, kushona nguo kwa wachimbaji madini na wale wanaojishughulisha na uongezaji thamani madini, hasa ukataji na uchongaji madini ya vito.

Aidha, Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene wakati akifunga mafunzo kwa wachimbaji wadogo mjini Dodoma hivi karibuni aliwapongeza wachimbaji madini wanawake waliopata ruzuku awamu ya kwanza na kueleza kuwa wameonesha mfano mzuri kwa kutumia vizuri fedha walizopatiwa na hivyo kuongeza tija kwenye kazi zao.

Alitoa mfano wa mmoja wa walionufaika na awamu hiyo kuwa ni kampuni ijulikanayo kama Precision Décor inayomilikiwa na mwanamke na inajishughulisha na uchimbaji wa madini ya ujenzi yanayoitwa, Tanga stone.

Simbachawene aliwaasa wanawake wachimbaji kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa mfano wa kuigwa. “Natarajia pia katika awamu hii wanawake wataendelea kuwa mfano wa kuigwa. Dhana ya akina mama wakisaidiwa ni sawa na kusaidia jamii kubwa, inajitokeza hapa,” alisema Waziri.

Wakati huu ambapo Serikali imebainisha kwamba Wizara inaendelea kuweka mikakati mingi ili kuendeleza wachimbaji wadogo, ni fursa nzuri kwa wanawake kujitokeza kwa wingi na kufanya kazi za uchimbaji madini au utoaji huduma katika sekta husika ili waweze kunufaika ipasavyo.

Bila shaka Sera ya Madini ni mkombozi kwa wanawake hawa na wengine ambao watachangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya madini. Shime wanawake wachimbaji, tuendelee kuonyesha mfano kwa kuisaidia Serikali kutimiza azma ya kuhakikisha sekta ya madini inachangia kwa asilimia 10 katika Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025.

Sera ya Madini ni Mkombozi wa Wanawake wachimbaji?>>> “Mjomba Hussein” atoa ushahidi

Mchimbaji madini mdogo, Pili Hussein maarufu kama Mjomba Husein akipokea mkataba kutoka kwa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene wakati wa mafunzo kwa waliopata ruzuku awamu ya pili ya kuendeleza uchimbaji madini mdogo. Wengine pichani kutoka Kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Sehemu ya Leseni, Mhandisi John Nayopa, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Fedha za Serikali kutoka Benki ya Maendeleo ya TIB, Prisca Chang’a na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA), John Bina. Mafunzo hayo ya siku mbili yalifanyika mjini Dodoma Oktoba 7 na 8, 2015.

Baadhi ya akina mama ambao ni wachimbaji wadogo wa madini mkoani Shinyanga wakiwa katika semina kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Kutoka Kushoto ni Amina Mtoro, Hafsa Issa, Halima Mohamed, Khadija Salum na Nusura Juma. Semina hiyo ilifanyika hivi karibuni mjini Shinyanga.

MAKALA

7BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

MIRADI YA GESI ASILIA, 2015TUMEWEZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Kituo cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba. Kulia kwake ni Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu. Kushoto kwake ni Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete. Wengine ni Viongozi mbalimbali wa Kitaifa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete (katikati) akikagua Kituo cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba wakati wa uzinduzi wa mradi wa miundombinu ya kusafirisha na kuchakata gesi asilia. Kushoto kwake ni Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dkt James Mataragio. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu akifuatiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Kikwete akipewa maelezo na Meneja Mitambo ya Kuchakata Gesi Asilia, Mhandisi Sultan Pwaga (aliyenyoosha mikono) kuhusu Mradi wa Kuchakata Gesi Asilia wa Madimba. Wengine katika picha ni viongozi mbalimbali wa Kitaifa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Mradi.

Mtambo wa Kuchakata Gesi Asilia wa Madimba, Mkoani Mtwara

8 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

1. Bomba la gesi katika hatua za awali za ujenzi

2. Mafundi wakifanya kazi ya kuziba maeneo yaliyokuwa na hitilafu katika bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.

3. Baadhi ya nyumba za Wafanyakazi wa Kituo cha Kuchataka Gesi Asilia Madimba, Mtwara.

4. Bomba la gesi likiwekwa chini ya ardhi.

5. Meli ya Discover Americas – 83 ikichoronga visima katika Kitalu N0.2 kwenye kina kirefu cha maji katika Bahari ya Hindi.

Tulipotoka … Tulipofika

1 4

52

3

Kituo cha Kuchakata Gesi cha Madimba, chenye uwezo wa kusafisha Gesi kiasi cha futi za ujazo Milioni 210 kwa siku, Gesi husafirishwa kwenda kituoni hapo kwa njia ya bomba.

9BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

PICHA 1 na 2: Mitambo ya Kufua Umeme ya Kinyerezi I, kutokana na Gesi Asilia kutoka Madimba- Mtwara yenye uwezo wa kuzalisha Megawati 150 za umeme. Mradi wa Kinyerezi I unaomilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), umegharimu kiasi dola za Kimarekani milioni 183 sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 400. Ujenzi wa Miundombinu ya kusafirisha, kusafisha na kuzalisha umeme wa Gesi Asilia ulizinduliwa mwaka 2012 na Rais Jakaya Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa katika eneo lilipo lango la kuingia katika Mitambo ya Kufua umeme ya Kinyerezi I, wakati akikagua mitambo hiyo wakati wa uzinduzi wa mitambo hiyo uliofanyika Oktoba 13, 2015.

PICHA 3 na 4: Mitambo ya kufua umeme eneo la Kinyerezi I, ikiwa katika hatua mbalimbali wakati wa ujenzi wake.

3

4 AWALI

AWALI

MRADI MKUBWA UMEME WA GESI ASILIATUMEWEZA

1

2

10 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

he G

over

nmen

t of

Tan

zani

a, in

cr

eatin

g an

en

ablin

g en

viro

nmen

t fo

r fo

reig

n an

d lo

cal

inve

stm

ents

, form

ulat

ed th

e M

iner

al P

olic

y of

199

7; e

nact

ed t

he M

inin

g Ac

t of

199

8 an

d m

ajor

ref

orm

s in

the

min

ing

�sca

l re

gim

e w

hich

co

ntai

ned

gene

rous

ta

x in

cent

ives

aim

ed a

t at

tract

ing

both

loca

l an

d fo

reig

n in

vest

ors

in

the

min

ing

sect

or.T

he

mea

sure

s re

sulte

d in

to

incr

ease

d la

rge

scal

e ex

plor

atio

n an

d m

inin

g ac

tiviti

es,

inclu

ding

th

e es

tabl

ishm

ent o

f 7 la

rge

scal

e go

ld m

ines

be

twee

n 19

98 an

d 20

09.

How

ever

, th

e Go

vern

men

t co

uld

not

e�ec

tivel

y re

alize

the

exp

ecte

d be

ne�t

s du

e to

in

adeq

uate

ex

perti

se

and

ine�

ectiv

e m

onito

ring

of

min

ing

oper

atio

ns.

In

orde

r to

ad

dres

s th

is sit

uatio

n, t

he G

over

nmen

t, am

ong

othe

r m

easu

res

it re

view

ed t

he m

iner

al p

olic

y, m

inin

g le

gisla

tion

and

stre

ngth

ened

inst

itutio

nal

adm

inist

ratio

n.

As

part

of

inst

itutio

nal

arra

ngem

ents

, th

e Ta

nzan

ia

Min

eral

s Au

dit

Agen

cy

(TM

AA)

was

es

tabl

ished

in

20

09.

The

Agen

cy

is m

anda

ted

to m

onito

r an

d au

dit

larg

e,

med

ium

and

smal

l sca

le m

inin

g op

erat

ions

in

or

der

to

ensu

re

max

imiza

tion

of

Gove

rnm

ent

bene

�ts

from

the

min

ing

indu

stry

, th

ereb

y en

hanc

ing

socio

-eco

nom

ic de

velo

pmen

t.Ke

y fu

nctio

ns o

f th

e Ag

ency

inc

lude

m

onito

ring

and

audi

ting

of q

ualit

y an

d qu

antit

y of

m

iner

als

prod

uced

an

d ex

porte

d by

larg

e, m

ediu

m a

nd sm

all s

cale

m

iner

s in

ord

er t

o fa

cilita

te c

olle

ctio

n of

pa

yabl

e ro

yalty

; au

ditin

g of

re

venu

e ge

nera

ted,

ca

pita

l in

vest

men

t an

d op

erat

ing

expe

nditu

re o

f th

e la

rge

and

med

ium

sca

le m

ines

for

the

pur

pose

of

gath

erin

g ta

xabl

e in

form

atio

n an

d pr

ovid

ing

the

sam

e to

th

e Ta

nzan

ia

Reve

nue

Auth

ority

(T

RA)

and

othe

r

rele

vant

aut

horit

ies;

and

mon

itorin

g an

d au

ditin

g en

viro

nmen

tal

man

agem

ent,

envi

ronm

enta

l bud

get a

nd ex

pend

iture

for

prog

ress

ive

reha

bilit

atio

n an

d m

ine

closu

re.

Sinc

e its

est

ablis

hmen

t TM

AA h

as re

cord

ed

rem

arka

ble

achi

evem

ents

as

a re

sult

of

e�ec

tive

mon

itorin

g an

d au

ditin

g of

m

inin

g op

erat

ions

in

the

coun

try.

Key

achi

evem

ents

inclu

de:

• Pa

ymen

ts o

f Co

rpor

ate

Inco

me

Tax

(CIT

) am

ount

ing

to U

SD 4

19 m

illion

by

m

ajor

m

ines

fo

r th

e pe

riod

cove

ring

year

200

9 to

Sep

tem

ber

2015

. No

CIT

was

pai

d be

fore

TM

AA

esta

blish

men

t. •

Facil

itatio

n of

in

puts

to

di

stric

t co

uncil

s ho

stin

g m

inin

g co

mpa

nies

to

ena

ble

them

with

the

colle

ctio

n of

Lo

cal

Serv

ice

Levy

w

hich

ha

s am

ount

ed to

USD

5.4

milli

on fo

r the

pe

riod

cove

ring

year

20

09

to

Sept

embe

r 201

5.•

Roya

lty

paym

ents

on

bu

ildin

g m

ater

ials

and

indu

stria

l m

iner

als

whe

reby

st

rate

gic

audi

ts

of

such

m

iner

als c

ondu

cted

by t

he A

genc

y in

colla

bora

tion

with

Zo

nal/R

egio

nal

Min

es

O�

ces,

enab

led

the

Gove

rnm

ent t

o co

llect

a to

tal o

f TZS

11

.7 b

illion

from

med

ium

and

sm

all

scal

e m

iner

s fo

r the

per

iod

cove

ring

June

201

1 to

Sep

tem

ber 2

015.

Thes

e au

dits

whi

ch a

re c

ondu

cted

thro

ugh

the

use

of “M

iner

al S

ales

Vou

cher

s” co

ver v

ario

us re

gion

s in

the

coun

try

and

are

expe

cted

to

inclu

de a

lmos

t al

l re

gion

s. Cu

rrent

reg

ions

bei

ng

cove

red

inclu

de A

rush

a, Co

ast.

Dar e

s Sa

laam

, D

odom

a, Ge

ita,

Iring

a, Ka

gera

, Ka

tavi

, Ki

liman

jaro

, Li

ndi,

Man

yara

, M

beya

, M

orog

oro,

M

wan

za,

Mtw

ara,

Rukw

a, Ru

vum

a, Si

miy

u, S

ingi

da an

d Ta

nga.

• Ro

yalty

pay

men

ts o

n go

ld p

rodu

ced

by

min

eral

pr

oces

sors

us

ing

vat

leac

hing

tech

nolo

gy in

Gei

ta, M

beya

an

d M

wan

za re

gion

s. M

onito

ring

of

such

act

iviti

es w

hich

is c

ondu

cted

in

colla

bora

tion

with

Min

es O

�ce

s ha

s en

able

d th

e Go

vern

men

t to

colle

ct a

to

tal o

f TZS

5.9

billi

on fo

r the

per

iod

cove

ring

July

201

2 to

Sep

tem

ber

2015

. Fut

ure

mon

itorin

g w

ill in

volv

e ot

her

regi

ons

like

Shin

yang

a an

d Si

ngid

a w

here

suc

h ac

tiviti

es t

ake

plac

e.

• Th

e Ag

ency

’s sp

ecia

l des

ks a

t maj

or

airp

orts

(Jul

ius

Nyer

ere

Inte

rnat

iona

l Ai

rpor

t, Ki

liman

jaro

In

tern

atio

nal

Airp

ort a

nd M

wan

za A

irpor

t) th

roug

h co

llabo

ratio

n w

ith o

ther

Gov

ernm

ent

enfo

rcin

g in

stitu

tions

, inte

rcep

ted

78

incid

ents

of il

lega

l min

eral

smug

glin

g be

twee

n Ju

ly 2

012

and

Sept

embe

r 20

15.

Thes

e in

ciden

ts

invo

lved

m

iner

als w

orth

USD

10

milli

on. S

ome

of th

e min

eral

s wer

e con

�sca

ted

afte

r co

urt

hear

ings

and

con

vict

s w

ere

�ned

acc

ordi

ng t

o th

e pr

ovisi

ons

unde

r the

Min

ing

Act o

f 201

0.

• Re

gard

ing

envi

ronm

enta

l co

mpl

ianc

e at

m

inin

g sit

es,

envi

ronm

enta

l aud

its c

ondu

cted

by

TMAA

ha

ve

cont

ribut

ed

to

a tre

men

dous

im

prov

emen

t in

en

viro

nmen

tal c

ompl

ianc

e by

larg

e,

med

ium

an

d so

me

smal

l sc

ale

min

ers.

• Th

e Ag

ency

’s la

bora

tory

in

Dar

es

Sala

am, w

hich

is e

quip

ped

with

stat

e of

the

art

equi

pmen

t an

d hi

ghly

tra

ined

pe

rson

nel,

was

ac

cred

ited

with

ISO

/IEC

1702

5: 2

005

in M

arch

20

15

by

SADC

AS,

Bots

wan

a (a

n in

tern

atio

nal a

ccre

dita

tion

body

for

Ea

ster

n an

d So

uthe

rn A

frica

). TM

AA

Labo

rato

ry o

�ers

a w

ide

rang

e of

qu

ality

serv

ices o

f min

eral

anal

yses

at

com

petit

ive

price

s to

all s

take

hold

ers

in th

e m

iner

al se

ctor

.

Des

pite

th

e ab

ove

achi

evem

ents

, th

e Ag

ency

con

tinue

s to

wor

k tir

eles

sly i

n or

der t

o en

sure

that

the

min

ing

indu

stry

in

Tanz

ania

ben

e�ts

bot

h th

e Go

vern

men

t an

d th

e m

inin

g co

mpa

nies

in a

win

-win

sit

uatio

n. In

real

izing

this,

the

Agen

cy w

ill co

ntin

ue to

stre

ngth

en it

s mon

itorin

g an

d au

ditin

g of

min

ing

oper

atio

ns t

o m

eet

Gove

rnm

ent’s

exp

ecta

tions

and

the

publ

ic at

larg

e.

Min

eral

s Aud

iting

in Ta

nzan

ia a

t a G

lanc

e

TMAA

Chi

ef E

xecu

tive o

�ce

r En

gine

er D

omin

ic R

wek

aza

talk

ing

to re

port

ers

at o

ne o

f the

age

ncy'

s pub

lic a

war

enes

s sem

inar

s

Aeria

l vie

w o

f one

of

the

min

ing

area

s in

Tanz

ania

.

11BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

12 BulletinNewshttp://www.mem.go.tzHabari za nisHati/madini

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIAMINISTRY OF ENERGY AND MINERALS

Kwa wadau wa sekta za Nishati na Madini, tembelea kurasa mpya za Wizara kwenye Mitandao ya Kijamii ya Twitter na Facebook kwa anuani ya ‘Nishati na Madini’ Karibu tuhabarishane na

tujadili kuhusu sekta za Nishati na Madini kwa maendeleo ya Watanzania wote.Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini