Upload
muhidin-issa-michuzi
View
297
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
1/14
TANZANIA KUKUZA SOKO LA MADINI YA VITO NCHINI KWA
KUFUATA NYAYO ZA THAILAND
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
2/14
SOKO LA MADINI YA VITO NCHINI THAILAND
Thailand ni nchi iliyoendelea ikilinganishwa na nchi nyingine
zinazoizunguka.Sababu kadha wa kadha huzungumzwa ikiwa ni pamoja na
sera ya ubepari iliyosababisha mataifa ya magharibi kuwekeza nchini humo
katika miaka ya awali ya Uhuru pamoja na Marekani kujenge miundo mbinu
mingi ili kuitumia nchi hiyo kama kituo katika vita ya Vietnum.
Aidha ugunduzi wa Gesi uliongeza kwa kiasi kikubwa sana maendeleo ya
Thailand kwa kuwa na staha ya kusubiri mabadiliko ya sera ya uwekezaji
katika nyaja hiyo na mwishowe kuweza kupata sera nzuri iliyowanufaisha
kama taifa.
Baada ya kuwa na uhakika wa miundo mbinu na nishati ya kutosha, Thailand
iliazimia kuanzisha uchumi imara wa viwanda vidogo,vya kati na vikubwa.
Viwanda vya nguo na viatu ilikuwa ndiyo chaguo lao la kwanza pamoja na
uanzishwaji wa vyuo vya kati (Polytechnic/Vocational Colleges ).Hatua ya pili ,
walitangaza vivutio vilivyopo nchini humo na kuruhusu nchi zinazopeleka
watalii wengi zaidi kupata pasi ya kusafiria mara wafikapo nchini Thailand( on
arrival VISA).
Baada ya uchumi kuimarika, Serikali ya Thailand ilitunga sheria; shughuli
zote za uchimbaji na biashara ya madini vito itakuwa chini ya wazawa nakupiga marufuku usafirishaji wa madini vito ghafi nje ya Thailand bali ina
ruhusu uingizwaji wa madini ghafi ya aina yoyote ndani ya Thailand bila
kibali.Hatua iliyofuata ni kutengwa kwa mji wa CHANTHABURI kama kitovu
cha biashara ya madini hususan madini ya Vito.
Serikali ya Thailand kwa kushirikiana na taasisi za elimu walianzisha mafunzo
ya utengenezaji na uvumbuzi wa mashine za bei nafuu zitakazotumika kukata,
kuchonga na kung’arisha madini vito ili kuyaongeza thamani.Zoezi hili lilianza
kwa kuwatumia Wahunzi wa Jadi.Kwa kuwatumia hao, ilikuwa rahisi kuweza
kutengeneza mashine kwa kutumia tekinolojia ya ndani.Zoezi hilo lilipata
mwitikio mkubwa na mashine mbalimbali na ujuzi tofauti wa kukata madini
ya vito vilivumbuliwa zaidi.
Nchi ya India pia ilifuata mfano huu kwa kuwachukua baadhi ya Wahunzi wa
mashine za kutengeneza nguo na kuwapeleka nchini Thailand kujifunza
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
3/14
namna ya kutengeneza mashine za kuchonga na kung’arisha madini ya vito
ikiwa ni pamoja na kujifunza kukata.
Baada ya mafunzo husika walirudi na serikali ya India ikatenga mji wa Jaipur
kuwa eneo la kuanzia shughuli husika.Ndani ya muda mfupi Jaipur ukawa mji
maarufu kwa uuzaji na ukataji wa madini ya vito.Itakumbukwa madini ya Tanzanite hukatwa kwa wingi na kuuzwa katika mji huu sababu kuu ikiwa ni
hizo zilizotajwa – Manguli wa Kukata,kuchonga na kung’arisha Madini ya Vito
kwa ustadi wa hali ya juu pamoja na Gharama nafuu.
Thailand imeendelea kuboresha biashara ya madini ya vito kwa kuanzisha
huduma fungamano; vyuo vinavyotoa elimu ya Madini ya vito, viwanda
vinavyotengeneza bidhaa (mapambo) zinazotumia madini ya vito, uanzishwaji
wa maeneo rasmi ya uuzaji na ununuzi wa madini (Minerals Bourses),
maonesho ya biashara ya madini ya vito mwaka mzima katika vipindi tofauti.
Katika nchi zote zinazo jishughulisha na madini ya vito, ‘ Bourses ’ imekuwa
ndiyo suluhisho la makusanyo badala ya ‘ Individual Broker and Delears’ .
Masharti yamewekwa ya kuongeza kodi zaidi kwa ‘ Individual Broker and
Delears’ na kuondoa au kupunguza kodi kwa wafanyabiashara katika
‘ Bourses ’ .
Bourses ni eneo linalotengwa na kujengwa na serikali na kuandaa meza
ambazo wafanyabiashara huruhusiwa kufanya mauzo na manunuzi ya madini
na watumishi wa serikali kutoza kodi na kutoa vibali vyote katika eneo hilo.Piawafanyabiashara hupata fursa ya kujua bei halisi na masoko ya nje.Taarifa
hizi hutolewa na watumishi wa serikali katika eneo hilo.Falsafa ya uanzishwaji
wa bourse ulianzia katika nchi ya Ubeligiji na mantiki kuu ikiwa ni kufifisha
biashara ya mtu mmoja mmoja katika maeneo mbalimbali na kuweka motisha
ya wafanyabiashara kufanya biashara ya madini ya vito sehemu moja na pia
kwa kutumia minada.1
1My personal point of view is that : ‘ Dealing with individual, means dealing with
his/her mind set but dealing with organization means dealing with underlined formal
procedures’ which are easy to control, improve and benefits the country in a multi -
effects. Therefore always let’s encourage economic groups’.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
4/14
SOKO LA MADINI YA VITO NCHINI TANZANIA
Samaruga Inc: Madini aina ya Rhodolite garnet
Tanzania licha ya kuwa na wingi wa Madini ya Metali, pia imejaliwa kuwa na
mashapo ya kutosha ya Madini ya vito.Uelewa wa wananchi katika
kujishughulisha na biashara ya Madini, umejikita zaidi katika aina moja ya
Madini.Watanzania wanauelewa mkubwa wa Madini ya metali kama dhahabu,Shaba na fedha.
Hii imetokana na uhitaji wa Madini hayo kuwa wa kiasi kikubwa sababu
Madini hayo mbali ya kutumika kama mapambo, hutumika pia katika nyanja
ya viwanda na matumizi mengine ya vifaa vya kielektroniki.Uhitaji huu
umesababisha Madini hayo kupata wawekezaji na wanunuzi wakubwa kwa
urahisi.
Madini ya vito hayafahamiki sana miongoni mwa wa Tanzania ikilinganishwa
na Madini ya Metali (Precious metal).Sababu kubwa ni kutokana na uhitajiwake kuwa mdogo ikilinganishwa na Madini mengine kwa sababu Madini ya
vito hutumika kwa mapambo tu ukiachilia mbali kwa sasa ambapo kutokana
na ukuwaji wa teknolojia, Madini ya Vito nayo yameanza kutumika katika vifaa
vya viwandani.Hali hii imeongeza uhitaji wa Madini ya vito na hivyo soko lake
kuimarika kama la Madini ya metali.Ni wakati sasa watanzania kujikita kwa
dhati katika biashara ya Madini ya vito yapatikanayo Tanzania kwa wingi
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
5/14
kama yalivyo ainishwa katika vitabu na majarida mbalimbali ikiwamo
GEMSTONES OF TANZANIA( Google Gemstones of Tanzania by Gilay Shamika)
Faida moja wapo kubwa ya Madini ya Vito ni kwamba mara baada ya
kuchimbwa unaweza uza moja kwa moja (direct to the market like harvested
crops ).Huitaji hatua nyingine kama dhahabu kuichakata na kuichoma ili upatezao la mwisho kwaajili ya kuuza.Kwa mantiki hii, uwekezaji katika shughuli ya
biashara ya Madini ya vito ni rahisi sana ikilinganishwa na Madini ya metali.
Mbali ya faida hiyo, pia kuna faida nyingine ambayo Madini ya vito
inayo.Madini ya vito mengi yana bei kubwa sana zaidi ya Madini ya metali.Kwa
ujumla, uwekezaji katika Madini ya vito ni njia mahususi katika kuondoa
umaskini kwa wananchi na kuongeza mapato kwa serikali.
Aidha suala la uharibifu wa mazingira hasa vyanzo vya maji, ni mdogo kwa
sababu madini ya vito hayahitaji kemikali maana haya chakatwi kama madini ya metali.
JITIHADA ZA SERIKALI ILI KUKUZA SOKO NA BIASHARA YA MADINI YA VITO NCHINI
Samaruga Inc: Tanzanite the Uniqueness of Tanzania, the stones on the foot of Mount Kilimanjaro
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
6/14
Kitendo cha nchi nyingine kuwa na mauzo ya Madini yaliyo juu zaidi ya
Tanzania na wakati huohuo Madini husika yanapatikana ama Tanzania tu au
ndipo yalipo kwa wingi, imekuwa ni kitendawili cha muda mrefu.
Wafanyabiashara pamoja na wataalamu wa Serikali wamekuwa wakijadili
kuona namna ya kuboresha hali ya soko na mifumo nchini ili kuondokana na
kitendawili hicho.Hivyo jitihada na udhati wa pande hizo mbili ni wa muhimu
ili kufikia lengo la kupata jibu la kitendawili husika.
Kwa kufuatilia Taarifa zinazotolewa na Serikali katika vyombo vya habari ni
wazi kuwa jitihada za Serikali zinazoendelea kuhusu kukuza soko la ndani na
nje la Madini ya Vito ni kama ilivyo ainishwa.
SHERIA YA MADINI YA MWAKA 2010
Katika sheria hii mpya ya Madini, Serikali kwa makusudi kabisa ya kusaidia
wananchi kiuchumi imeeleza wazi shughuli za Madini ya Vito kuwa chini ya
Watanzania.Aidha sheria imetoa mwanya kwa wageni kujihusisha na shughuli
za Madini ya Vito kwa shariti la kuingia ubia na wazawa.Sheria imezuia
mwanya wa Wawekezaji wa nje kumiliki shughuli za uzalishaji na biashara ya
Madini ya Vito kwa asilimia mia moja.
Kuna mantiki mbili katika kipengele hiki cha sheria ya Madini.Kwanza ni
kuinua wazawa kiuchumi kwa kuwapa fursa pana ya kuwekeza katika Madini
ya vito bila kuingiliwa na wawekezaji wa nje mpaka pale wazawa wanapo amua
kuingia ubia kwa utashi wao.
Pili ni kutatua kitendawili husika cha utoroshwaji wa Madini ya Vito. Kwakuwa
Madini ya Vito yapo katika miliki ya Wazawa ama kwa asilimia miamoja au
kwa ubia, hakuna uwezekano wa wawekezaji kutorosha au kukiuka sheria bila
wazawa kujua au kushiriki maana wao ndiyo wamiliki.Hivyo ikitokea kuna
utoroshaji maana yake wazawa wameridhia kufanya hivyo na kuhujumu Taifa.
Kero ya nchi nyingine kusafirisha Tanzanite zaidi ya Tanzania, kwa muhtadha
wa hapo juu, ni juhudi zinazofanywa na watanzania wenyewe.Ni muda
muafaka tutumie fursa tuliyopewa na Serikali ya kumiliki Madini ya Vito na
kuiletea nchi manufaa na si kinyume chake.
Sheria hii pia ndiyo iliyopo nchini Thailand ya Wazawa kumiliki Madini ya Vito
na kuhusika kudhibiti utoroshwaji kinyume cha sheria.Wamiliki wote ndiyo
waangalizi kwa niaba ya Serikali na anaekiuka hufutiwa Umiliki na
kuadhibiwa.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
7/14
MAONESHO YA MADINI YA VITO JIJINI ARUSHA KILA MWAKA
Kwa bahati mbaya au mazoea ni sekta moja tu ambayo inamaeneo rasmi ya
Masoko kwa ajili ya bidhaa zao: Sekta ya Kilimo na Mifugo wana maeneo rasmi
(minada na maghala ya Serikali) ya kuuza mazao na mifugo na serikalikusimamia kutoa Vibali pamoja na kutoza ushuru wa shughuli husika.
Samaruga Inc: Madini ya Vito katika moja ya banda kwenye maonesho ya Madini ya Vito
yaliyofanyika Mwaka huu jijini Arusha katika hoteli ya Mt.Meru.
Sekta nyeti ya Madini kwa muda mrefu haina ama sehemu maalumu ya kuuza
na kununua na vilevile hakuna minada kwa ajili ya Madini.
Watu binafsi (dealers,brokers and jewellers) wanavibali kwaajili ya shughuli
hiyo ya kununua na kuuza Madini.Ni vema, lakini bado kuna uhitaji wa eneo
maalumu kwa yeyote mwenye Madini kuuza na kununua (minerals bourses)
kwa uwazi ili kuzuia utapeli unaojitokeza kwa baadhi ya watu binafsi
wanaoendesha shughuli hizo.
Kwa kulijua hilo Serikali imeanzisha Maonesho ya Madini ya Vito kila mwaka
jijini Aruha ili kukuza soko la Madini ya Vito. Wauzaji na wanunuzi wa ndani
hufanya biashara zao kwa mujibu wa taratibu husika.Aidha maonesho hayo
yamekuwa ni kiunganishi muhimu kati ya wafanyabiashara wa ndani na nje
pamoja na kutangaza Madini ya Vito kwa wageni.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
8/14
Jitihada hii ya kuanzishwa kwa Maonesho ya Madini ya Vito yamekuza mauzo
ya Madini ya Vito kadri maonesho yanavyoendelea.Mwakani maonesha hayo
yatafanyika kuanzia tarehe 19-21/04/2016. Ni vema watanzania
kuchangamkia fursa hii kwa kupata Taarifa zaidi Wizarani pamoja na Ofisi za
Kanda za Madini.Aidha waweza tembelea tovuti ya www.arushagemshow.com
kwa Taarifa zaidi.
Nchini Thailand, maonesho ya Madini ya Vito hufanyika mara tatu kwa
mwaka.Aidha Thailand imetenga mji wa Chanthaburi kuwa eneo maalumu
kwaajili ya kuuza na kununua Madini ya Vito.Vilevile katika jiji la Bangkok
kuna maeneo Maalumu ya kuuza na kununua Madini ( Minerals bourses).
Nchi za Asia,Ulaya na Marekani zinamaeneo hayo pamoja na Minada ya Madini
kila baada ya muda kadhaa mara nyingi baada ya miezi 3.Minada ya Madini
huvuta wanunuzi kutoka sehemu mbali mbali ikiwa ni pamoja na Madini
kuuzwa kwa bei ya juu kutokana na ushindani katika Mnada.
Niwazi kuwa Serikali ipo mbioni kuanzisha maeneo hayo ya kuuzia na
kununulia Madini pamoja na Minada ya Madini nchini kutokana na maelezo
yaliyotolewa na Kamishna wa Madini Eng.Paul Masanja wakati wa ufunguzi wa
Maonesho ya Madini ya Vito Arusha kwa kuanzisha Jengo maalumu
kuendeshea shughuli hizo. Maofisa wa Serikali watakuwepo ili baada ya
kununua au kuuza wahusika wapate vibali husika (Madini and TRA Officials).
Pamoja na mpango huo Kamishina wa Madini Eng.Paul Masanja ameanzisha
pia utaratibu wa kisasa wa kuomba Leseni za Madini kwa njia yamtandao.Jambo hili nila kupongezwa kwa kwenda na wakati pamoja na kuwa
mbunifu.
WAKALA WA UKAGUZI WA MADINI TANZANIA (TMAA)
Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), kwa kuzingatia sababu tajwa,
umekuwa ukitoa elimu ya Madini ya Vito kwa wananchi, kuanzisha Maabara
za kisasa kwaajili ya kutambua Madini ya Vito kwa Gharama nafuu,kutoa bei
elekezi kwa wananchi ili wauze kwa mujibu wa thamani halisi badala ya
kutapeliwa na wafanyabiashara wasio waaminifu.
http://www.arushagemshow.com/http://www.arushagemshow.com/http://www.arushagemshow.com/
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
9/14
Samaruga Inc : Mitambo yakisasa ya kupimia madini katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)
Maabara za Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania zinapatikana Dar es
Salaam,Arusha,Mwanza na Mbeya.Kwa habari zaidi kuhusu huduma za
Maabara ya Madini ya Vito na Metali zitolewazo na Wakala wa Ukaguzi wa
Madini Tanzania (TMAA) tembelea Ofisi Kuu jijini Dar es Salaam Chole
Road,Masaki (+255 22 2601819 ) pamoja na Ofisi za Kanda za Wakala kama
zilivyotajwa hapo juu.Tovuti ya Wakala ni www.tmaa.go.tz.
Aidha mbali ya jitihada husika hapo juu, Wakala pia umesomesha wataalamu
katika Nyanja hiyo ambao hushiriki katika maonesho ya Madini ya Vito jijini
Arusha na kutoa elimu ya masoko na utambuzi wa Madini kwa kutumia Vifaa
vya kisasa pamoja na kuhudumu Maabara tajwa.Jitihada hizo zimeongeza
uelewa kwa wananchi na pia makusanyo ya maduhuli ya Serikali.
Ni jukumu la watanzania kutumia taasisi za serikali kupata huduma
mahususi.Baadhi ya Maabara nyingine ni ile ya Madini Dodoma, GST na
SEAMIC.
http://www.tmaa.go.tz/http://www.tmaa.go.tz/http://www.tmaa.go.tz/
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
10/14
Samaruga Inc : Mitambo yakisasa ya kupimia madini katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)
Huduma fungamano: Mbali ya kuwa na soko au eneo maalumu kwa ajili ya
biashara ya Madini,huduma pia hazina budi kupatikana hapo, Gem-min
Lab,Gem-treatment,Gem-valuation and Pricing .Huduma hizi hurahisisha na
kuvutia wafanyabiashara wengi na ni mnyumbuliko wa 4Ps ( Place, Product,
Price and Promotion).Huduma fungamano husaidia mtu kununua Madini
akiwa na uhakika wa anachonunua pamoja na thamani halisi.Huduma za
kupima na kuthaminisha Madini kutolewa kwa bei nafuu.
Nchini Thailand huduma fungamano za Madini ya Vito zipo kila mtaa na
wanausemi kuwa huwezi nunua nguo bila kupima kama inakuenea na vivyo
hivyo si busara kununua Madini bila kupima thamani yake kwa kuthibitisha
na kujua ubora wake.
Kwa minajili hiyo, upatikanaji wa huduma fungamano za kupima Madini
sehemu yanapouzwa au kununuliwa ni wazi ule msemo wa Tanzania wa aliye
uziwa cheni feki nae katoa fedha feki hauta dhihirika maeneo hayo
(Minerals bourses) maana cheni feki hazitaletwa kwasababu Madini
yanapimwa kuthibitishwa.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
11/14
Samaruga Inc : Mitambo yakisasa ya kupimia madini katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)
TANSORT
Tanzania Sorters (Tansort) kwa tafasiri ya moja kwa moja ni Wachambuzi wa
Madini ya Vito Tanzania. Sort: ni kitendo cha kuchambua Madini ya Vito na
kuyatenga kwa mujibu wa madaraja ya ubora wakwanza, wapili, watatu,wanne
na mwisho makapi.
Mara baada ya kuanzishwa kwa STAMICO ili kusimamia shughuli za
uendeshaji migodi na biashara ya Madini nchini, Serikali iliona umuhimu wa
kuwa na kitengo hicho ili kuisaidia kuthaminisha Madini ya Vito na kujua
thamani halisi kwa ajili ya kodi.
Baada ya muda Serikali iliona umuhimu wa kuongeza thamani ya Madini ya
Vito kwa kuyakata na kung’arisha, hivyo ilianzishwa pia Tanzania Cutters –
Almasi (Tancut-Almasi).Mlio wengi mtakumbuka pia Band ya Music ya shirika
hilo ikiitwa Tancut Almasi Band – Wazee wa kukata na kung’arisha.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
12/14
Vitengo hivi viwili vilifanyakazi na mwishowe TANSORT shughuli zake
mahususi kwa ajili ya kuthaminisha Almasi za Mgodi wa Mwadui zilihamia
Uingereza ambapo mauzo yalikuwa yakifanyika mpaka hivi karibuni kitengo
kilipo rejea na utaratibu wa sasa ni mtumishi kuongozana na Mzigo mpaka
sokoni nchi ambayo itauzwa ili kudhibiti Mapato ya Serikali.
Kitengo hiki kinafanyakazi nzuri sana kwa mujibu wa Taarifa ambazo
zimekuwa zikitolewa katika vyombo vya habari hususan kipindi Wizara ya
Madini inapotoa Taarifa ya utendaji kwa kila idara.
Tancut Almasi ilikufa ila uhitaji wa kukata,kuchonga na kung’arisha Madini ya
Vito ni mkubwa sana.Jijini Arusha ambapo ndiyo soko kuu la Madini ya Vito,
uhitaji huo unaonekana dhahiri.Ni fursa kwa sekta binafsi kuchangamkia eneo
hili na kuwekeza kwa kutumia mashine za bei ndogo wanazotumia Jaipur
zinazo gharimu takriba dola 800 kwa mashine moja.
Hivyo tutumie kitengo cha TANSORT, TMAA na Ofisi za Madini Kanda katika
kutambua thamani za Madini ya Vito.Itategemea na taasisi ipi kati ya hizo ipo
karibu na eneo lako. Hizi ni jitihada za Serikali kuleta huduma karibu na
wananchi katika kukuza biashara ya Madini ya Vito.
Ukipata jiwe lenye rangi yeyote, peleka katika taasisi hizo kwa uchunguzi
huenda una mali ya thamani mikononi mwako.
STAMICO
STAMICO ni moja kati ya taasisi kongwe nchini zilizo anzishwa mara baada ya
uhuru kuisaidia Serikali kuu katika jitihada za kumiliki na kukuza uchumi wa
nchi.Baada ya sheria mpya ya Madini ya mwaka 2010, STAMICO ilihuishwa
kuwa msimamizi wa Hisa za serikali katika migodi mikubwa itakayo anzishwa
au kuhuishwa Leseni zao mara baada ya sheria husika.Tumeshuhudia mpaka
sasa STAMICO ikimiliki hisa katika Mgodi wa TanzaniteOne Mkoani Manyara
Mererani.Pia ikimiliki kwa asilimia miamoja Mgodi wa STAMIGOLD uliopo
Biharamuro.
Katika kukuza Soko la Madini ya Vito, STAMICO imeamua kumiliki asilimia
hamsini ya Mgodi wa TanzaniteOne katika kuendesha shughuli za uchimbaji
na biashara ya Tanzanite kwa kushirikiana na Wazawa wanaomiliki asilimia
hamsini pia.Juhudi zinaonekana katika kusimamia soko la Tanzanite
zitokanazo na mgodi husika.
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
13/14
CHUO CHA JIMOLOJIA JIJINI ARUSHA – TANZANIA GEMOLOGICAL CENTRE
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeanzisha chuo cha kisasa
kinachotoa mafunzo yahusuyo elimu ya Madini ya Vito. Wahitimu katika chuo
hicho wanapata ujuzi wa kutambua,kupanga madaraja ya Madini vito,kuthaminisha Madini ya vito pamoja na uwezo wa kutumia mashine za
kukata,kuchonga na kung’arisha Madini ya Vito. Hii ni hatua kubwa
inayopaswa kupongezwa. Aidha ni wajibu wa Sekta binafsi kuwatumia
Wahitimu katika kuwekeza kwenye fursa hii ya Madini ya Vito.Chuo husika
pia kinatoa huduma za Kimaabara kwa wananchi wanaohitaji kutambua
Madini yao ya Vito.
Samaruga Inc: Wanafunzi wakijifunza aina ya Madini ya Vito
Kwa maelezo yote hapo juu, inaonesha ni kwa namna gani Serikali
imedhamilia kukuza shughuli na biashara ya Madini ya Vito
nchini.Kilichobakia ni utayari wa sisi wananchi kutumia huduma za taasisi za
serikali tajwa hapo juu na pia kuanza kujikita katika biashara ya Madini ya
Vito ambayo haijakuwa nchini.
Pia fursa katika uwekezaji wa kukata na kung’arisha Madini ya Vito,
unahitajika kupewa mkazo kwa kutoa elimu kwa wananchi ili watambue na
kuwekeza.
CHUO CHA MADINI DODOMA
Miongoni mwa taasisi za Serikali zilizotoa mchango mkubwa katika kuimarisha
Wizara ya Nishati na Madini ni chuo cha Madini Dodoma.Chuo hiki ndicho
chuo cha mwanzo kabisa nchini kutoa mafunzo ya Madini pamoja na Maabara
8/20/2019 Tz Kukuza Soko La Madini Ya Vito Kwa Kufuata Nyayo Za Thailand Makala
14/14
ya kupima Madini na Sampuli za udongo pamoja na miamba.Mpaka leo hii
chuo hicho bado kinatoa huduma hizo na kwasasa zimeboreshwa zaidi.
Serikali imeongeza kozi za Madini zinazotolewa chuoni hapo na ufanisi wake
unaonekana kwa kutoa wahitimu walio bobea wa ngazi ya kati.Migodi mingi
nchini inapendelea kuchukua wafanyakazi waliohitimu chuo cha MadiniDodoma (MRI) pamoja na wanao hitimu VETA kwaajili ya nafasi za ngazi ya
operators.
Aidha huduma za Maabara ambazo zimekuwa zikitolewa tangu miaka ya
1970’s zinaendelea katika jitihada za kuimarisha huduma za Madini kwa
wananchi.
GST
Geological Survey of Tanzania (GST) ni muhimili muhimu sana katika kukuzabiashara na shughuli za Madini nchini.
Huduma ya uhakiki wa mashapo ya Madini nchini kote ni muhimu ili
kutambua maeneo yenye Madini na kiasi husika kwa ajili ya uendelezaji na
uwekezaji wa uhakika badala ya kubahatisha.
Uhakiki na Upimaji wa maeneo yenye Madini unaoendelea kufanywa na GST
nchini, unaongeza kasi ya uwekezaji na mipango ya serikali kuhusu sekta ya
Madini.
Wananchi tutumie huduma za GST kujua kiasi kilichopo kwenye maeneo yetu
yenye Madini.
Fanya sasa biashara ya Madini ya Vito ambayo ni changa nchini (niche market)
na kuepuka ushindani uliopo katika biashara nyingine .
Kwa jitihada hizi za Serikali, ni wazi kuwa mwisho wa ule usemi wa
ALIEUZIWA ‘CHENI FEKI’ KATOA ‘FEDHA FEKI’ utafikia ukomo kutokana na
huduma fungamano za kutambua na kupima ubora wa madini zitolewazo na
taasisi za serikali.
Mwandishi wa Makala;
Eng.Gilay Charles Shamika [email protected]
Mhandisi Mwandamizi Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)
mailto:[email protected]:[email protected]